STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, February 4, 2015

Bayern Munich wang'ang'aniwa nyumbani Bundesliga

http://i1.eurosport.com/2015/02/03/1408140-30159502-1600-900.jpg
Thomas Mullier akipambana dhidi ya wachezaji wa Schalke 04
http://b.smimg.net/15/06/640x480/bayern-munich-arjen-robben.jpg
Mfungaji wa bao la Bayern Munich, Arjen Robbin akishangilia
MABINGWA watetezi wa Bundesliga, Bayern Munich wameshindwa kutamba nyumbani baada ya kung'ang'aniwa na Schalke 04 na kulazimishwa sare ya bao 1-1 katika mfululizo wa ligi hiyo nchini Ujerumani.
Bayern wakiwa kwenye uwanja wao wa Allianz Arena, walijikuta wakishindwa kufurukuta mbele ya wageni wao ambao walionekana kudhamiria kuendeleza aibu kwa mabingwa hao ambao walikuwa wametoka kupokea kipigo chao cha kwanza katika ligi hiyo wakiwa ugenini dhidi ya Wolfsburg waliowachapa mabao 4-1.
Baada ya kumaliza dakika 45 za awali wakiwa nguvu sawa, wenyeji walianza kuandikisha bao la kuongoza dakika ya 67 kupitia kwa Arjen Robben akimalizia kazi nzuri ya Xabi Alonso.
Hata hivyo bao hilo lilidumu kwa dakika tano tu kwani Schalke walisawazisha kupitia kwa Benedikt Howedes na kuwafanya wenyeji waliocheza pungufu kwa muda mrefu baada ya beki wake tegemeo Jeremy Boateng kulimwa kadi nyekundu dakika ya 17 tu ya mchezao kuhaha kusaka bao la ushindi bila mafanikio.
Kwa matokeo hayo Bayern wameendelea kukalia kiti cha uongozi wa Bundesliga wakiwa na pointi 46 baada ya mechi 19 huku wapinzani wao wakipanda hadi nafasi ya nne wakiwa na pointi 31.
Katika michezo mingine ya ligi hiyo iliyochezwa juzi, Borussia Monchengladbach walipata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Freiburg uliowapeleka hadi nafasi ya tatu wakifikisha pointi33, huku Hannover 96 na Mainz 05 wakishindwa kutambiana kwa kutoka sare ya 1-1 kama ilivyokuwa katika mchezo wa timu za Eintracht Frankfurt na 'wababe' wa Bayern Munich Wolfsburg

Ivory Coast iliyokamilika kuvaana na DR Congo leo Afcon

http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/8/8a/Cheick_Ismael_Tiote_9030.JPG
Cheikh Tiote
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiW4t072rDsv7i065sgWdPt51mT1c0i-lbQg5kDT8bcTMgvICAFJ60KLvXsHnqWGDAQuuaknHY-9zn2a2NQntbalajJRXyMoLk2UvQJpJ2JWD4e_ihAo2feQ84Jv6kUFeZT8wKM4xMN2T0/s1600/IMG_9994.JPG
Kikosi cha Ivory Coast kitakachokabuiliana na DR Congo leo kwenye nusu fainali ya kwanza ya AFCON 2015
TIMU ya taifa ya Ivory Coast imemkaribisha kwa mikono miwili katika mazoezi ya timu hiyo mchezaji wake Cheick Tiote kabla timu hiyo leo haijashuka dimbani kucheza  mchezo wao wa nusu fainali wa Mataifa ya Afrika.
Ivory Cioast baada ya kuitoa  Tunisia katika hatua ya robo fainali, inapewa nafasi kubwa ya kutwaa ubingwa wa mashindano hayo makubwa kwa nchi barani Afrika.
Cheick Tiote huenda leo Jumatano akawemo katika kikosi cha Ivory Coast cha nusu fainali dhidi ya Jamhuri ya Watu wa Kongo.
Kiungo huyo mahiri wa Newcastle United hajapangwa katika kikosi cha kocha wake Herve Renard  tangu alipoichezea timu hiyo kwa mara ya mwisho wakati ilipocheza na Mali katika mchezo wa  Januari 24 kutokaana na maumivu ya kifundo cha mguu.
Hatahivyo, kocha wa timu hiyo Renard ana matumaini makubwa kuwa, mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28, atarejea uwanjani na wanafuzu kwa fainali zao za sita ndani ya miaka sita katika mashindano hayo.
"Tiote alianza mazoezi mepesi na yumo katika orodha ya kikosi cha leo Jumatano kitakachoshuka dimbani.
"Kwa kweli ni vigumu kwake kuanza mchezo huo, lakini yumo katika kikosi hicho.
Ivory Coast wanaangalia kutwaa taji lao la kwanza la AFCON tangu mwaka 1992 huko Equatorial Guinea, huku kocha Renard akiwa na matumaini kibao ya kujaribu bahati ya kulitwaa taji hilo tena baada ya kufanikiwa kufanya hivyo alipokuwa akiifundisha Zanzibar mwaka 2012.
Kesho Alhamisi kutakuwa na nusu fainali ya pili itakayozikutanisha Ghana na wenyeji Equatorial Guinea ambao watakuwa wakicheza mbele ya wapenzi wao.

Tuesday, February 3, 2015

Kocha Redknapp abwaga manyanga QPR

http://static.guim.co.uk/sys-images/Football/Pix/pictures/2012/11/24/1353767357535/Harry-Redknapp-new-QPR-ma-008.jpg
Kocha Harry Redknapp aliyebwaga manyanga QPR
KOCHA wa timu ya Ligi Kuu ya England ya  Queen Park Rangers, Harry Redknapp ametangaza kujiuzulu kuwa kocha wa timu hiyo.
Redknapp huyo  mwenye umri wa miaka 67 amedumu na klabu hiyo kwa takribani miaka miwili ameamua kuachana na klabu hiyo kwa hiari yake baada ya kushindwa kuopa mafanikio.
Taarifa kutoka kwa Tony Fernandes inasomeka hivi; "Tunashukuru kwa kila alichofanya Redknapp hapa klabuni wakati wote wa utawala wake kama kocha."
Taarifa hiyo ya kujiuzulu kwa kocha huyo haijaeleza wazi chanzo cha kujiuzulu kwa kocha huyo ambaye pia aliwahi kuifundisha Tottenham Hotspurs na kuipa mafanikio akisi cha kupigiwa debe kuchukua mikoba ya kuifundisha timu ya taifa ya England.
Hata hivyo inaelezwa tatizo la kiafya alilonalo kocha huyo ndilo lililomfanya achukue uamuzi huo wa kutekma kibarua hicho.
Redknapp amekunuliwa akisema kuwa maumivu ya magoti yanayomsumbua kwa muda mrefu kiasi cha kuweza kusimama kwa muda mrefu ndicho sababu ya kuacha kibarua hicho na kumpigia simu bosi wake Tony Fernandes ili atafute mtu wa kuisimamia timu hiyo iliyopo nafasi ya pili mkiani mwa msimamo wa Ligi.

Copy and WIN : http://bit.ly/copy_win

Viporo FA: Manchester Utd kutoka vipi leo?! Liverpool kesho

http://mufclatest.com/wp-content/uploads/2015/02/Cambridge-United-FA-Cup-Replay-750x360.png
http://i3.mirror.co.uk/incoming/article5032437.ece/alternates/s615/Cambridge-United-v-Manchester-United-FA-Cup-Fourth-Round.jpg
Man United walivyohenyaka mechi ya kwanza kwa Cambridge United, leo watatokaje
BAADA ya kushukizwa ugenini kwa kulazimishwa suluhu isiyo na magoli dhidi ya timu ya daraja la pili ya Cambridge United, leo watakuwa uwanja wa nyumbani wa Old Trafford kurudiana na timu hiyo katika mechi ya Raundi ya Nne ya Kombe la FA.
Katika michuano ya kombe hilo, leo kutakuwa na mechi nyingine mbili zitakazowakutanisha timu za Fulham  na Sunderland ambazo zilishindwa kutambiana katika mechi yao ya kwanza kwa kutoka sare ya 0-0, huku timu zilizofungana bao 1-1 katika mechi iliyopita Sheffield United na  Preston North End nao wataonyeshana kazi.
Bolton Wanderers waliowasimamisha Livepool nyumbani kwao Anfield watakuwa wenyeji wa Liverpool katika mechi nyingine itakaypogwa kesho kukamilisha mechi za viporo vya michuano hiyo kabla ya kuanza mechi za raundi ya tano.
Manchester Utd ambayo imetoka kupata ushindi mnono wa mabao 3-1 nyumbani katika Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya vibonde wa ligi hiyo Leicester City italazimika kugangamala ili wasije wakaenda na maji kama ilivyowakuta timu za Manchester City na Chelsea waliotolewa nishai na timu za madaraja ya chini katika michuano hiyo.
Kocha Luis Van Gaal anatarajiwa kuchezesha kikosi kamili katika pambano hilo ili kuweza kuvuka hatua hiyo na kujiweka katika nafssi nzuri ya kunyakua angalau kombe moja kati ya mawili ambayo wana nafasi ya kuyatwaa wakigangamala lingine likiwa la Ligi Kuu japo ana nafasi finyu.
Mabingwa hao wa zamani na wenye historia kubwa katika FA kwa kunyakua mara nyingi, imeshaondoshwa kwenye Kombe la Ligi (Capital One) na pia haishiriki michuano yoyote ya kikmataifa baada ya msimu uliopita kuwa na wakati mgumu chini ya kocha David Moyes.

HII NDIYO NGOMA MPYA YA AY- ZIGO


Chelsea nouma, yafanya kufuru usajili dirisha dogo

http://cdn.caughtoffside.com/wp-content/uploads/2015/02/Chelsea-Juan-Cuadrado.jpg
Kifaa kipya kilichotua Chelsea
DIRISHA dogo la usajili nchini Uingereza limefungwa usiku wa jana huku klabu ya Chelsea ikiwa ndiyo timu inayoongoza kwa kutumia fungu kubwa la fedha katika usajili huo kwa kumchukua winga wa kimataifa wa Colombia Juan Cuadrado kwa kitita cha paundi milioni 23.3.
Kwa ujumla klabu za Ligi Kuu zimetumia kiasi cha paundi milioni 130 katika usajili huu hivyo kufikia kiwango kama walichotumia mwaka jana.
Klabu ya Crystal Palace ndio iliyokuwa na harakati nyingi katika siku ya mwisho ya usajili kwa kuwachukua wachezaji wanne akiwemo Wilfried Zaha.
Klabu ya Hull City ndio iliyofunga dirisha hilo kwa kutangaza usajili wa kumchukua mshambuliaji wa Lokomotiv Moscow Dame N’Doye katika muda wa mwisho.
Jumla ya wachezaji 13 wamesajiliwa katika siku ya mwisho ya usajili huku 35 zaidi wakisajiliwa katika kipindi chote toka dirisha lilipofunguliwa Januari mosi mwaka huu.

Vita vya Nusu Fainali Afcon kuanza kesho, DRC, Ivory Coast balaa!

http://2.bp.blogspot.com/-SB-d541z6sc/VL4AkhGjdBI/AAAAAAAAxDQ/t-i41NY82rw/s1600/ivory-coast%2Bnational%2Bteam%2B2015.jpg
Kikosi cha Tembo wa Afrika, Ivory Coast watakaoanza kuvaana na DR Congo kesho mjini Bata
Kikosi cha DR Congo
http://sportsworldghana.com/wp-content/uploads/2014/12/ghana-black-stars-2.jpg
Kikosi cha Black Stars kitakachovaana na wenyeji Guinea ya Ikweta
http://en.starafrica.com/football/files/2013/03/615_340_SA_EQUATORIAL-GUINEA.jpg
Wenyeji Guinea ya Ikweta kuendeleza maajabu yao AFCON 2015
MBIVU na mbichi za timu zipi zitakazotinga Fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) itafahamika kesho wakati mechi za Nusu Fainali zitakapochezwa.
Pazia la hatua hiyo litaanza kesho kwa mchezo wa kukata na mundu kati ya Ivory Coast iliyowaduwaza Algeria dhidi ya wapiganaji wa DR Congo.
Pambano hilo linatarajiwa kuchezwa kwenye uwanja wa Bata, mjini Bata.
DR Congo ambayo haikuwa ikipewa nafasi ya kufika kokote kwenye michuano hiyo ilipenya hatua hiyo baada ya kuwatoa nishai watani zao wa jadi Congo Brazzaville kwa kuwanyuka mabao 4-2.
Vijana hao wa Kabila walitoka nyuma ya mabao 2-0 na kuwaduwaza wakongo wenzao ambao hata hivyo licha ya kuondoka wameweka rekodi baada ya miaka mingi.
Wakongo hao watakuwa na kibarua kigumu mbele ya Tembo wa Ivory Coast ambao waliwanyuka Algeria mabao 3-1 na kutinga hatua hiyo bila kutarajiwa.
Nusu fainali ya pili itakuwa keshokutwa kwenye uwanja wa Malabo, kwa pambano kali kati ya wenyeji Guinea ya Ikweta dhidi ya Black Stars ya Ghana ambayo waliwachapa Guinea mabao 3-0 katika mechi ya robo fainali.
Wenyeji ambao hakuna aliyetarajia kama ingefika hatua hiyo kutokana na maandalizi yake, iliwatoa nishai kitatanishi Tunisia baada ya 'kupewa' penati dakika za lala salama kabla ya kupata bao la ushindi dakika ya nyongeza zilizowafanya waweke rekodi.
Hata hivyo hakuna anayetarajia Guinea ya Ikweta ifanye maajabu mengine mbele ya Ghana ambao kikosi chake kimekuwa kikizid kuimarika tangu walipoanza michuano hiyo ya kipigo toka Senegal.
Mashabiki wa soka wana hamu kubwa ya kujua ni timu zipi zitakazofuzu kwa Fainali itakayopigwa Jumapili ili kupata bingwa mpya wa Afrika.
Taji la michuano hiyo ya mwaka huu halina mwenyewe baada ya waliokuwa watetezi, Nigeria kushindwa kupata nafasi ya kwenda Guinea ya Ikweta baada ya kung'oka kwenye mechi za makundi za mchujo.
Timu mbili kati ya tano zilizokuwa zikipigiwa chapuo na kutajwa huenda zingewarithi Nigeria ndizo zilizobakia kwenye michuano hiyo ambazo ni Ghana na Ivory Coast, huku Cameroon, Afrika Kusini na Algeria zikiwa zimesharejea makwao mapema.

Hatem Ben Arfa kustaafu soka mapema?!

http://talksport.com/sites/default/files/tscouk_old_image/benarfa_2.jpg
Hatem Ben Arfa anayedaiwa huenda akastaafu?
WAKILI wa Hatem Ben Arfa amedokeza kiungo huyo anaweza kustaafu soka baada ya Ligi ya Soka ya Ufaransa-LFP kumfungia kucheza mechi za mashindano na klabu ya Nice.
Nyota huyo wa kimataifa wa Ufaransa mwenye umri wa miaka 27 alijiunga na Nice akitokea Newcastle United mapema mwezi huu baada ya mkopo wake katika klabu ya Hull City kusitishwa.
Kwa mujibu wa taratibu za Shirikisho la Soa Dunia-FIFA, wacheza wanaweza kuruhusiwa kucheza mechi za mashindano katika vilabu viwili pekee kwa msimu.
Wakili Jean-Jacques Bertrand amesema ni wazi kuwa uwepo wa Ben Arfa katika timu hiyo utamalizika leo na kuhofu kuwa mchezaji huyo anaweza kuwa anafikiria kustaafu.
Ben Arfa aliifungiwa Newcastle katika ushindi wa mabao 5-2 dhidi ya Readings kwa timu za vijana chini ya umri wa miaka 25 Agosti mwaka jana kabla ya kwenda Hull kwa mkopo ambako nako alicheza mechi tisa.

West Ham Utd hatarini kuenguliwa FA Cup

http://www.africatopsports.com/wp-content/uploads/2014/10/diafra-sakho.jpg
Diafra Sakho
KLABU ya West Ham United inakabiliwa na adhabu ya kuenguliwa katika michuano ya Kombe la FA kama Shirikisho la Soka Duniani-FIFA litawakuta na kosa kwa kumtumia mshambuliaji Diafra Sakho.
Sakho mwenye umri wa miaka 25 alijitoa katika kikosi cha Senegal kilichoshiriki michuano ya Mataifa ya Afrika kutokana na maumivu ya mgongo lakini aliifungia West Ham bao siku 18 baadae katika ushindi wa bao 1-0 waliopata dhidi ya Bristol City.
Sheria za FIFA hazimruhusu mchezaji kuichezea klabu yake kama anatakiwa kuwa na majukumu ya kimataifa. FIFA tayari imeshaanza kuchunguza suala hilo huku West Ham wenyewe wakikanusha kufanya lolote baya kwa kumtumia mchezaji huyo.
Kama West Ham watakutwa na kosa, FIFA inaweza kuliamuru Shirikisho la Soka la Uingereza-FA kubadilisha matokeo waliyopata dhidi ya Bristol City.

Copy and WIN : http://bit.ly/copy_win
KLABU ya West Ham United inaweza kukabiliwa na adhabu ya kuenguliwa katika michuano ya Kombe la FA kama Shirikisho la Soka Duniani-FIFA litawakuta na kosa kwa kumtumia mshambuliaji Diafra Sakho. Sakho mwenye umri wa miaka 25 alijitoa katika kikosi cha Senegal kilichoshiriki michuano ya Mataifa ya Afrika kutokana na maumivu ya mgongo lakini aliifungia West Ham bao siku 18 baadae katika ushindi wa bao 1-0 waliopata dhidi ya Bristol City. Sheria za FIFA hazimruhusu mchezaji kuichezea klabu yake kama anatakiwa kuwa na majukumu ya kimataifa. FIFA tayari imeshaanza kuchunguza suala hilo huku West Ham wenyewe wakikanusha kufanya lolote baya kwa kumtumia mchezaji huyo. Kama West Ham watakutwa na kosa, FIFA inaweza kuliamuru Shirikisho la Soka la Uingereza-FA kubadilis

Hii ndiyo bei halisi atakayouzwa Cristiano Ronaldo

http://www.independent.co.uk/incoming/article9760507.ece/binary/original/cristiano-ronaldo-5.jpg
Nyota wa Real Madrid Cristiano Ronaldo
CRISTIANO Ronaldo atauzwa kwa kiasi cha pauni Milioni 300 endapo klabu ya Real Madrid itaamua hata kesho kumuchia mchezaji huyo kuondoka.
Hayo yalisemwa na wakala wa mchezaji huyo nyota wa Ureno alipozungumza leo na BBC Sport.
Wakala huyo Jorge Mendes alisema nahodha huyo wa timu ya taifa ya Ureno ni mchezaji bora wa muda wote.
"Ni mchezaji bora wa muda wote duniani. Kamwe huwezi kumfananisha na mchezaji mwingine yeyote, alisema Mendes alipozungumza na muhariri wa michezo Dan Roan.
Ronaldo, mwenye umri wa miaka 29, mwezi uliopita alichaguliwa kwa mara ya tatu kuwa mchezaji bora wa dunia, akimbwaga Lionel Messi wa Barcelona katika tuzo hiyo.
Alipoulizwa mchezaji huyo ana thamani kiasi gani, Mendes alisema: 
"Cristano Ronaldo? Bilioni moja. Anakaribia Bilioni moja, hivyo ni bilioni moja. Kwa kweli haiwezekani kumpata mwingine anayefanana nay eye.
"Endapo kwa sabbau zozote zile klabu itaamua kumuuza hata kesho kwa Milioni 300, mtu atalazimika kulipa kiasi hicho cha pesa. "
Hata hivyo, Mendes alisisitiza kuwa raia huyo mwenzake wa Ureno ambaye alinunuliwa na Real Madrid kwa rekodi ya dunia ya ada ya dola za Marekani Milioni 80 mwaka 2009, ataendelea kubaki Bernabeu, licha ya mapenzi yake" kwa klabu yake ya zaman ya Manchester United.
Alipoulizwa kama atamalizia soka lake Real Madrid, Mendes alisema "na uhakika". "Hataondoka Real Madrid," aliongeza.
Mendes, aliyeripotiwa kuwa alipata zaidi na pauni bilioni 1 kwa ajili ya uhamisho tu, akielezewa kuwa ni mmoja wa watu wenye nguvu sana katika mchezo huo.
"Watu wana mtazamo tofauti kuhusu mawakala. Kuwa wakala kuna maana tofauti. Mimi ni mtu wa kawaida kabisa. Ninafanya kazi kwa bidii kila siku. Nina malengo na kusema ukweli ninatenda haki na hilo ndio muhimu zaidi.
Alielezea kuwa soka ni mchezo muhimu sana duniani na alitetea mishahara ya wachezaji, akisema wanastahili kiasi kikubwa kama inawezekana".
Mendes alifananisha kufanyakazi na wachezaji kwa mikataba ni sawa na familia.
"Ni kama vile unavyozungumza na mtoto wako, au familia yako wakati wote unajaribu kutafuta njia bora ya kuwasaidia."
Mendes, DJ wazamani na mmiliki wa klabu ya usiku, pia ni wakala wa Jose Mourinho, Luiz Felipe Scolari, Radamel Falcao, Angel Di Maria, James Rodriguez, David De Gea, Victor Valdes na Diego Costa.

TFF kusaka mdhamini Ligi Daraja la Kwanza

http://api.ning.com/files/XCoElX7q3j2IeT5tiuUefPUOAr*u*C4UA*eK*naDvxjwjW3u89dAVaxJeE-HBCAXGvMt6yoAQJAritE0jIquj2X1*yXj0FNz/tff.jpg

SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) liko mbioni kupata mdhamini wa Ligi Daraja la Kwanza (FDL).
Tunatarajia mdhamini huyo atakuwa tayari kwa ajili ya msimu wa 2015/2016.
Ligi Daraja la Kwanza inashirikisha timu 24 zinazocheza katika makundi mawili ya timu 12 kila moja kwa mtindo wa nyumbani na ugenini.
Timu zinazocheza FDL msimu huu ni African Lyon (Dar es Salaam), African Sports (Tanga), Ashanti United (Dar es Salaam), Burkina Faso (Morogoro), Friends Rangers (Dar es Salaam), Geita Gold (Geita), Green Warriors (Dar es Salaam), JKT Kanembwa (Kigoma), JKT Mlale (Ruvuma) na JKT Oljoro (Arusha).
Nyingine ni Kimondo (Mbeya), Kinondoni Municipal Council (Dar es Salaam), Kurugenzi (Iringa), Lipuli (Iringa), Majimaji (Ruvuma), Mwadui (Shinyanga), Panone FC (Kilimanjaro), Polisi Dar es Salaam, Polisi Dodoma, Polisi Mara, Polisi Tabora, Rhino Rangers (Tabora), Toto Africans (Mwanza), na Villa Squad (Dar es Salaam).

Yanga yafanya kufuru yatenga fedha Ebola Cup

http://shaffihdauda.co.tz/wp-content/uploads/2014/05/SAM_1702.jpg
Mwwenyekiti wa Yanga, Yusuf Manji
MWENYEKITI wa Yanga, Yusuf Manji ametenga kiasi cha dola 500,000 kwa ajili ya michuano ya Ebola  Cup itakayoshirikisha timu 108 za Afrika.
Katika michuano hiyo Tanzania itawakilishwa na Yanga pamoja na mabingwa watetezi wa ligi kuu Tanzania Bara, Azam.
Akizungumza Dar es Salaam jana, kwa niaba ya Mwenyekiti wa Yanga, Katibu Mkuu wa klabu hiyo Jonas Tibohora  alisema hatua za kuanza michuano hizo zipo kwenye hatua nzuri.
Alisema michuano hiyo imeandaliwa kwa ajili ya  kuchangisha fedha  zitakazowasaidia waafrika walioathirika na ugonjwa wa Ebola.
Alisema michuano hiyo itasimamiwa na Chama cha Soka Afrika (CAF), na kwamba kwa sasa kamati ya michuano hiyo yenye wajumbe mchanganyiko kutoka nchi wanachama wa CAF itakaa na kupanga tarehe ya michuano hiyo.
Alisema michuano hiyo itachezwa kwa mtindo wa makundi ambapo kutakuwa na makundi 16 na kila kundi litakuwa na timu kati ya nne na saba.
Alisema michuano hiyo itashirikisha timu zote kutoka Afrika ambazo ni mwanachama wa CAF ambapo kila nchi itatoa timu mbili na michuano itachezwa nyumbani na ugenini.
Alisema  kila timu zitachangia kiasi cha dola 100,000 kama ada ya ushiriki ambazo zitaingizwa moja kwa moja katika mfuko wa kusaidia waathirika hao.
"Mpango huu yatari umepitishwa na kinachofuata ni kupangwa kwa tarehe ya michuano ambapo kamati ya mashindano inayoongozwa na Mwenyekiti wake Machache Shipanda kutoka Zambia itakutana na kutoa ratiba,"alisema Tibohora.
Alisema pia mpango huo umeungwa mkona na umoja wa Afrika (AU) ambao watashirikiana kwa pamoja kuhakikisha michuano hiyo inafanyika kwa manufaa makubwa.


HUU NDIYO USAJILI WA DIRISHA DOGO ENGLAND

http://i.dailymail.co.uk/i/pix/2015/01/28/252596E800000578-2930164-Gabriel_Paulista_poses_with_an_Arsenal_shirt_as_the_club_unveil_-a-46_1422466068639.jpg
Paulista aliyenyakuliwa na Arsenal

http://resources2.news.com.au/images/2015/01/27/1227198/061530-6ca4ddec-a5bb-11e4-a11e-9d15a37a8504.jpg
Huyu kasajiliwa Chelsea
http://a.espncdn.com/combiner/i/?img=/media/motion/ESPNi/2015/0107/int_150107_FC_VALDES_united_DISC/int_150107_FC_VALDES_united_DISC.jpg&w=738&site=espnfc
Kipa Victor Valdes aliyetua Manchester United
Wolfsburg and Chelsea have agreed terms over £24million switch for Andre Schurrle
Andre Schurrle aliyeondoka Chelsea kutua Wolfsburg
JANA ilikuwa siku ya mwisho wa dirisha dogo la usajili barani Ulaya hususani katika nchi ya England na baadhi ya timu zimechangamsha za kutosha kuimarisha vikosi vyao, japo safari hii haikusisimua kama katika dirisha kubwa au dogo la msimu uliopoita.
Klabu kubwa kama Arsenal iliwanyakua kiungo mkabaji kinda wa miaka 17,  Krystian Bielik na beki wa kati, Gabriel Paulista, wakati Manchester United ilimsajili kipa Victor Valdes, huku Sunderland ikimnyakua Jermain Defoe.
Liverpool haijafanya usajili wowote wa dirisha dogo, huku West Brom yamnyakua Callum McManaman kutoka WiganYaya Sanogo ajiunga na Crystal Palace
Chini ni usajili kamili wa klabu 20 za Ligi Kuu ya England kujua walioingia na kutoka;
ARSENAL
WALIOSAJILIWA

Gabriel Paulista (Villarreal, £11.2m)
Krystian Bielik (Legia Warsaw, £2.5m) 
WALIOONDOKA
Benik Afobe (Wolves, ada haikutajwa)
Lukas Podolski (Inter Milan, mkopo)
Yaya Sanogo (Crystal Palace, mkopo)
Joel Campbell (Villarreal, mkopo) 

ASTON VILLA
WALIOSAJILIWA

Carles Gil (Valencia, £3.25m)
Scott Sinclair (Manchester City, mkopo)
WALIOONDOKA
Darren Bent (Derby, mkopo)
Gary Gardner (Nottingham Forest, mkopo)
Chris Herd (Wigan, mkopo)
Callum Robinson (Preston, mkopo)

BURNLEY
WAlIOSAJILIWA

Michael Keane (Manchester United, ada haikutajwa)
WALIOONDOKA
Hakuna

CHELSEA
WALIOSAJILIWA

Juan Cuadrado (Fiorentina, £27m)
WALIOONDOKA
Andre Schurrle (Wolfsburg, £24m)
Ryan Bertrand (Southampton, £10m)
Mark Schwarzer (Leicester, huru)
Thomas Kalas (Middlesbrough, mkopo)
John Swift (Swindon, mkopo)
Lewis Baker (Sheffield Wednesday, mkopo)
Marko Marin (Anderlecht, mkopo)
Mohamed Salah (Fiorentina, mkopo)

CRYSTAL PALACE
WALIOSAJILIWA

Wilfried Zaha (Manchester United £6m)
Jordon Mutch (QPR, £5.75m)
Lee Chung-yong (Bolton, ada haikutajwa)
Keshi Anderson (Barton Rovers, £35,000)
Shola Ameobi (Gaziantep, huru)
Pape Souare (Lille, ada haikutajwa)
Yaya Sanogo (Arsenal, mkopo)
WALIOONDOKA
Stuart O'Keefe (Cardiff, ada haikutajwa)
Alex Wynter (Colchester, ada haikutajwa)
Zeki Fryers (Rotherham, mkopo)
Lewis Price (Crawley, mkopo)
Jake Gray (Cheltenham, mkopo) 
Barry Bannan (Bolton, mkopo)
Jimmy Kebe (huru)

EVERTON
WALIOSAJILIWA

Aaron Lennon (Tottenham, mkopo)
WALIOONDOKA
Samuel Eto'o (Sampdoria, huru)
Chris Long (Brentford, mkopo) 
Conor McAleny (Cardiff, mkopo)

HULL CITY
WALIOSAJILIWA

Dame N'Doye (Lokomotov Moscow, £3m)
WALIOONDOKA
Tom Ince (Derby County, mkopo)

LEICESTER CITY
WALIOSAJILIWA

Andrej Kramaric (Rijeka, £9.5m)
Mark Schwarzer (Chelsea, huru)
Robert Huth (Stoke City, mkopo)
WALIOONDOKA
Tom Hopper (Scunthorpe, mkopo)

LIVERPOOL
WALIOSAJILIWA

Hakuna
WALIOONDOKA
Oussama Assaidi (Al Ahli, £4.7m)
Suso (AC Milan, £1m) 

MANCHESTER CITY
WALIOSAJILIWA
 
Wilfried Bony (Swansea, £28m)
WALIOONDOKA
Matija Nastasic (Schalke, mkopo)
Scott Sinclair (Aston Villa, mkopo) 

MANCHESTER UNITED
WALIOSAJILIWA

Victor Valdes ( huru)
Sadiq El Fitouri (Salford City, huru)
Andy Kellett (Bolton, mkopo)
WALIOONDOKA
Wilfried Zaha (Manchester United, £6m)
Michael Keane (Burnley, £3m)
Darren Fletcher (West Brom, huru)
Will Keane (Sheffield Wednesday, mkopo)
Ben Amos (Bolton, mkopo)
Jesse Lingard (Derby County, mkopo)

NEWCASTLE UNITED
WALIOSAJILIWA

Hakuna
WALIOONDOKA
Mapou Yanga-Mbiwa (Roma, £5.2m)
Hatem Ben Arfa (huru)
Gael Bigirimana (Rangers, mkopo)
Haris Vuckic (Rangers, mkopo)
Shane Ferguson (Rangers, mkopo)
Davide Santon (Inter Milan, mkopo)

QUEENS PARK RANGERS
WALIOSAJILIWA
 
Mauro Zarate (West Ham, mkopo)
Ryan Manning (Galway United, huru)
WALIOONDOKA
Jordon Mutch (Crystal Palace, £5.75m)
Bruno Andrade (Stevenage, mkopo)

SOUTHAMPTON
WALIOSAJILIWA

Ryan Bertrand (Chelsea, £10m)
Eljero Elia (Werder Bremen, mkopo)
Filip Djuricic (Benfica, mkopo)
WALIOONDOKA
Jack Cork (Swansea, £3m)
Jos Hooiveld (Millwall, mkopo)
Artur Boruc (Bournemouth, mkopo)

STOKE CITY
WALIOSAJILIWA

Philipp Wollscheid (Bayer Leverkusen, mkopo)
WALIOONDOKA
Ryan Shotton (Derby, ada haikutajwa)
Maurice Edu (Philadelphia Union, ada haikutajwa)
Robert Huth (Leicester City, mkopo)

SUNDERLAND
WALIOSAJILIWA

Jermain Defoe (Toronto, ada haikutajwa)
WALIOONDOKA
Jozy Altidore (Toronto, ada haikutajwa)
Mikael Mandron (Shrewsbury, mkopo)
Charis Mavrias (Panathinaikos, mkopo)
Cabral (huru)

SWANSEA CITY
WALIOSAJILIWA
 
Kyle Naughton (Tottenham, £5m)
Jack Cork (Southampton, £3m)
Matt Grimes (Exeter City, £1.75m)
Nelson Oliveira (Benfica, mkopo) 
WALIOONDOKA
Wilfried Bony (Manchester City, £28m)
Rory Donnelly (Tranmere, mkopo)
Jazz Richards (Fulham, mkopo)

TOTTENHAM HOTSPUR 
WALIOSAJILIWA

Dele Alli (MK Dons, £5m)
WALIOONDOKA
Kyle Naughton (Swansea, £5m)
Aaron Lennon (Everton, mkopo)
Milos Veljkovic (Charlton, mkopo)
Benoit Assou-Ekotto (huru)
Dele Alli (MK Dons, mkopo)

WEST BROMWICH ALBION
WALIOSAJILIWA 

Callum McManaman (Wigan, £4.75m)
Darren Fletcher (Manchester United, huru)
WALIOONDOKA
Luke Daniels (Scunthorpe, ada haikutajwa)

WEST HAM UNITED
WALIOSAJILIWA

Doneil Henry (Apollon Limassol, ada haikutajwa)
WALIOONDOKA
Mauro Zarate (QPR, mkopo)
Ricardo Vaz Te (huru)


Wateja wa Airtel kuzoa magari kila siku kupitia Yatosha

Sehemu ya magari yatakayoshindaniwa  na wateja wa Airtel
KAMPUNI ya mtandao wa simu za mkononi ya Airtel Tanzania imezindua promosheni  kabambe ijulikanayo kama Airtel Yatosha Zaidi kwa wateja wanaotumia vifurushi vya Airtel Yatosha kuweza kujishindia gari Aina ya Toyota IST kila siku.
Akiongea wakati wa uzinduzi wa promosheni hiyo Mkurugenzi wa Masoko ya Airtel Bwana Levi Nyakundi alisema;
"Promosheni hii ni nafasi ya peeke wa wateja wetu wanaojiunga na vifurshi vya Airtel yatosha vya siku, wiki na mwezi kupata faida zaidi kutokana pesa wanazozitumia. Nia yetu kuhakikisha tunatoa huduma na bidhaa bora kwa kupitia huduma yetu ya Airtel Yatosha huku tukiwazawadia wateja wetu zawadi nono.
Tunaamini promosheni hii itawapatia wateja wetu uzoefu tofauti wakati wote wakitumia huduma zetu za Airtel Yatosha. Zaidi ya wateja wetu kijishindia magari promosheni hii ya Airtel Yatosha Zaidi itawapatia wateja wetu vifurushi zaidi"Aliongeza Nyakundi.

Akiongea kuhusu namna ya kushiriki Mkurugenzi wa mawasiliano wa Airtel, Bi. Beatrice Singano Mallya alisema” ili kushiriki kwenye promosheni hii wateja wanatakiwa kuendelea kununua vifurushi vyao vya Yatosha vya siku, wiki na mwezi. Hakuna gharama ya ziada, kwa kununua vifurushi vya yatosha tayari utakuwa umeunganishwa kwenye droo ya yatosha zaidi na kupata nafasi ya kujishinidia Toyota IST moja kila siku.

Hii ni promosheni ya aina yake ambapo wateja wetu wanazawadiwa kutokana na matumizi yao ya kawaida ya vifurushi vya Yatosha.  Tunatoa wito kwa wale ambao hawajajiunga na vifurushi vya Airtel yatosha kufanya hivi na kupata nafasi ya kushinda gari moja kila siku”, aliongeza  Mallya.

Kununua vifurushi vya yatosha wateja wanaweza au  kupiga *149*99#, kunua kwa kupitia huduma ya Airtel Money au kwa kununua vocha ya Airtel yatosha inayopatikana katika maduka yetu nchi nzima.

Mwaka Jana Airtel ilizindua huduma ya kisasa ya kibunifu na yenye vifurushi vya gharama nafuu sokoni. Kuzinduliwa kwa promosheni hii ya Airtel yatosha Zaidi ni mwendelezo wa dhamira ya Airtel ya kutoa huduma bora huku ikiwazawadia wateja wake kwa kutumia huduma zake.

Monday, February 2, 2015

Wife wa Ali Kiba avuja mtandaoni, msikilize hapa


Maradhi ya Moyo ya Diamond hadharani usikilize hapa


Newz Alert! Francis Cheka ahukumiwa miaka mi3 jela

Cheka (kulia) katika mikutano ya mapambano yake pembeni yake ni promota Omar Kimbau
BONDIA nyota wa ngumi za kulipwa nchini aliyewahi kuwa Bingwa wa Dunia wa WBF, Francis Cheka 'SMG' mwenye maskani yake mjini Morogoro amehukumiwa kifungo cha miaka mitatu jela.
Kwa mujibu wa kituo cha redio cha EFM kipindi cha Sports Headquarter, Cheka amehukumiwa adhabu hiyo baada ya kukutwa na hatia ya kumpiga meneja wake katika shughuli zake za biashara ya ukumbi wa Vijana Social mjini Morogoro anayedaiwa kumuingiza mjini kiasi kikubwa cha fedha kiasi cha kufikia kuchapana naye.
Akizungumza na kituo hicho baba mzazi wa Francis Cheka amesema haikuwa sahihi kwa mwanae kupewa hukumu hiyo na badala yake wangekaa na kuzungumza ili kuyamaliza matatizo hayo.
Mzee huyo alienda mbali zaidi na kusema kuwa kuna watu wenye chuki na mwanae wameitumia kesi hiyo ya muda mrefu kutimiza malengo yao lakini pia mzee huyo ameelezea hisia zake kwa wakazi wa Morogoro kutoa sapoti ndogo kwa mwanae.
Taarifa zinasema kuwa Cheka amehukumiwa adhabu hiyo leo JUmatatu Februari 2, katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Morogoro.
EFM.

Shaa kutoa mpya, video ya Subira bado yakwama

WAKATI video ya wimbo wake wa 'Subira' ikiwa inaendelea kupigwa danadana bila kuachiwa tangu itengenezwe, msanii Sarah Kais 'Shaa' yupo njiani kuachia kazi mpya.
Akizungumza na MICHARAZO mapema leo, Meneja wa msanii huyo Said Fella 'Mkubwa' alisema kuwa katikati ya mwezi huu Shaa ataachia kazi mpya kulingana na utaratibu waliojiwekea.
Akiwa chini ya Mkubwa na Wanae, Shaa ameshaachia nyimbo mbili za 'Sugua Gaga' na 'Subira' na hivi karibuni akiwa Kenya kikazi alitoa wimbo mpya uitwao 'Njoo' akishirikiana na mkenya Redsan.
"Tupo katika maandalizi ya mwisho kabla ya Shaa kuingia studio kutengeneza kazi mpya," alisema Fella na kufafanua juu ya video ya wimbo wa 'Subira' ambao ina muda mrefu tangu itangazwe itaachiwa hadharani bila mafanikio.
"Video hiyo imeshakamilika kitambo ila bado ipo mikononi mwa Adam Juma aliyeitengeneza, tukikabidhiwa tutaiachia mara moja," alisema Fella.
Alipoulizwa sababu ya kucheleweshwa kwa video hiyo alisema kuna mambo ambayo hawajaridhishana katika video hiyo ya 'Subira' ambayo ilitengenezwa mwishoni mwa mwaka jana kabla ya Shaa hajaenda Kenya.

Chegge, Mhe Temba, Madee kuzindua video zao Escape One

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhRcuFMHdCOMH-6MJo0M0ke2rBniv8pPETU5_l3lk5chotAEkEwbjahckMWz6qtRuRnbCvvvfPLQcoQci2-PeTusKm9ik3rwx6oDiF6JkqNCZ27dc2yH8EhHF2u85Rr1GwBubQzST4gDeI/s1600/Madee+-+Vuvula.jpgWASANII nyota nchini Mhe Temba, Chegge na Madee wanatarajiwa kuzindua rasmi video ya nyimbo zao mpya walizorekodiwa nchini Afrika Kusini wakimshirikisha Dj Maphorisa wa Uhuru.
Meneja wa wasanii hao, Said Fella aliliambia MICHARAZO kuwa, uzinduzi wa video hizo utafanyika siku ya Jumamosi  kwenye ukumbi wa Escape One, Mikocheni.
Fella alisema Madee atazindua video ya wimbo wake uitwao 'Vuvula' wakati Chegge na Mhe Temba watazindua 'Kaunyaka' ambazo zinafanya vema kwenye vituo vya radio na televisheni.
Meneja huyo alisema uzinduzi huo utapambwa na burudani za wasanii kadhaa nyota watakaousindikiza akiwataja baadhi kuwa ni Diamond, Yamoto Band, Jux, Vanessa Mdee, Shaa na wengine.
"Madee, Chegge na Mheshimiwa Temba wanatarajia kuzindua video za nyimbo zao zinazoendelea kutamba hewani kwa sasa, uzinduzi utafanyika Escape One na utasindikizwa na wasanii kadhaa nyota akiwamo Diamond, Shaa, Vee Money na wengine," alisema Fella.

Costa ajitetea, adai hakukanyaga kwa makusudi

http://i.telegraph.co.uk/multimedia/archive/03178/CostaButt_3178918b.jpg
Diego Costa akizinguana na Martin Skrtel
MSHAMBULIAJI wa Chelsea, Diego Costa amesema hakuwa na nia yeyote ya makusudi kumkanyaga mchezaji wa Liverpool Emre Can.
Chama cha Soka Uingereza-FA kilimtwanga adhabu kwa vurugu kutokana na tukio hilo lililotokea katika mchezo wa nusu fainali ya mkondo wa pili wa Kombe la Ligi Jumanne iliyopita jambo ambalo Costa amelipinga.
Costa mwenye umri wa miaka 26 amesema jambo kubwa ni wakati akienda nyumbani kwake kulala na kujua kuwa hakufanya jambo lolote baya.
Strika huyo wa kimataifa wa Hispania amesema hakuwa na nia ya makusudi kutenda kitendo kile kwani ilikuwa bahati mbaya.
Hata hivyo Costa amesema amekubali na kuheshimu adhabu aliyopewa, japo  amesisitiza hakufanya vile kwa makusudi.

Baada ya kuwakosa Ndanda, Yanga kumalizia hasira Mkwakwani

Yanga
BAADA ya jana kushindwa kupata ushindi kama walivyoahidi mbele ya Ndanda Fc ya Mtwara, Yanga itaifuata Coastal Unioni nyumbani kwa Mkwakwani Tanga wakiwa na dhamira moja tu ya kupata pointi tatu.
Yanga ililazimishwa suluhu na Ndanda jana katika mfululizo wa Ligi Kuu Tanzania Bara iliyochezwa jkwenye uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kuwafanya washindwe kukalia kiti cha uongozi wa ligi hiyo unaoshikiliwa na Azam waliopo DR Congo, japo imerejea katika nafasi ya pili walioshushwa Jumamosi na Mtibwa Sugar.
Sare hiyo ya jana imeifanya Yanga kufikisha pointi 19 baada ya mechi 11, mbili nyuma ya Azam waliolingana nao kimichezo ambao kesho wanatarajiwa kumalizia mechi zao nchini Congo baada ya juzi kulazimisha sare ya 2-2 dhidi ya wenyeji wao TP Mazembe.
Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa Yanga, Jerry Muro alisema wanatarajia kwenda Tanga kwa mechi tyao ya Jumatano wakiwa na nia mopja ya kuhakikisha wanapata ushindi kama ilivyofanya wiki iliyopita mjini Morogoro walipowafunga maafande wa Polisi kwa bao 1-0.
Muro alisema wanatambua pambano hilo litakuwa gumu kutokana na ukweli Coastal Union watakuwa nyumbani na hawajafanya vema katika mechi zao za karibuni, lakini wao hawatajali hilo zaidi ya kupata ushindi ili kujiweka katika nafasio nzuri ya kunyakua taji hilo.
"Matokeo dhidi ya Ndanda ni ya kawaioda katika mchezo na sasa tunajipanga kwa mechi ijayo dhidi ya Coastal Union tutakaowafuata Mkwakwani kwa dhamira moja ya kuvuna pointi," alisema Muro.
Tangu ligi iendelee tena baada ya mapumziko ya Novemba 9, Yanga imevuna pointi  sita tu katika mechi nne ilizocheza mpaka sasa baada ya kutoka sare ya 2-2 na Azam kisha kulazimishwa suluhu na Ruvui Shooting kabla ya kuwazabua Polisi Moro na kubanwa na Ndanda.

Renard awasifu Algeria licha ya kuwang'oa AFCON

http://zambianintelligencenews.com/wp-content/uploads/2013/08/Renard.jpg
Kocha wa Ivory Coast
KOCHA wa timu ya taifa ya Ivory Coast Herve Renard amedai kuwa, wapinzani wao Algeria walikuwa wazuri zaidi yao licha ya kuwafunga bao 3-1 katika mchezo wa robo fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika.
Renard ambaye aliwahi kuipa Zambia ubingwa wa michuano hiyo alisema kuwa, kikosi chake jana usiku kilikuwa dhaifu licha ya ushindi huo ulioiwezesha kutinga hatua ya nusu fainali ya mashindano hayo.
Washindi wa mchezo huo ndio walikuwa wa kwanza kupata bao lililowekwa kimiani na mchezaji mpya wa Manchester City Wilfried Bony, ambaye pia ndiye aliyefunga la pili baada ya Mualgeria El Arbi Hillel Soudani kusawazisha.
Gervinho aliihakikishia Ivory Coast ushindi baada ya kufunga bao la tatu katika dakika za majeruhi katika mchezo huo uliofanyika jijini hapa na kuihakikishia timu hiyo nafasi ya kusonga mbele.
Renard alisema kuwa wapinzani wao hao kutoka Afrika ya Kaskazini walikuwa wazuri, lakini walishindwa kutumia nafasi zao vizuri.
"Kwa upande wa soka, mbinu, Algeria walikuwa bora zaidi yetu, " alisema Renard alipozungumza na waandishi wa habari mara baada ya mchezo huo.
Timu hiyo sasa itavaana na DR Congo walioiondosha Congo kwa mabao 4-2, timu nyingine iliyofuzu nusu fainali ni Ghana iliyoicharaza Guinea kwa mabao 3-0 na sasa watacheza na wenyeji Guinea ya Ikweta keshokutwa.
Naye Kocha Mkuu wa timu ya taifa ya Algeria Christian Gourcuff aliunga mkono maneno ya mwenzake, ambapo alisisitiza kuwa timu iliyoshinda haikuwa bora.
"Hii sio timu bora iliyoshinda. Kwa upande wa mchezo, tulicheza vizuri lakini bahati haikuwa yetu, " alibainisha Gourcuff.
"Wachezaji wa Ivory Coast hawakupata nafasi nyingi. Hawakustahili kushinda."
Gourcuff pia alitupia lawama ubora wa kiwanja, na kusema kuwa lilikuwa kosa lao kukubali kufungwa na Ghana baada ya kukubali bao la dakika za mwisho na kumaliza wa pili katika Kundi C kwani wangeshinda wangekuwa wa kwanza na wangeikwepa Ivory Coast katika robo fainali.
"Lakini ikiwa tumecheza mechi 10, lakini haujafungwa mara 10, ni wazi sisi ni timu bora…”

Sunday, February 1, 2015

Real Madrid yamtoa nishai David Moyes

Bale (centre) takes Real Sociedad's Yuri Berchiche at Bernabeu stadium in Madrid
Bale akipambana mbele ya vijana wa Real Sociedad
KOCHA wa zamani wa Manchester United, David Moyes anayeinoa kwa sasa Real Sociaded hana hamu na vinara wa La Liga, Real Madrid baada ya kuwashuhudia vijana hao wa Santiago Bernabeu wakiitoa nishai timu yake kwa kuicharaza mabao 4-1 katika pambano la Ligi Kuu ya Hispania usiku wa jana.
Moyes aliyeiongoza Sociaded kuilaza Barcelona bila kutarajiwa hivi karibuni alishuhudia vijana wake wakipotea Bernabeu licha ya kutangulia kufunga la mapema dakika ya kwanza tu tangu kuanza kwa mchezo huo.
Aritz Elustondo aliiandikia wageni bao dakika ya kwanza akimalizia kazi nzuri ya Rubén Pardo kabla ya James 'Bond' Rodríguez kulisawazisha dakika mbili baadaye akimlazia kazi ya Marcelo.
Beki mfungaji wa Real Madrid, Sergio Ramos aliionmgeza timu yake bao la pili dakika ya 37 na kudumu hadi mapumziko wenyeji wakiwa mbele kwa mabaoi 2-1.
Mshambuliaji wa kimataifa wa Ufaransa, Karim Benzema aliwapa furaha mashabiki wa Real Madrid ambao walimkosa nahidha wao, Cristiano Ronaldo anayetumikia adhabu ya kandi nyekundu aliyopata katika mechi hiyo iliyopita kufanya undava uwanjani aliingozea timu hiyo bao la tatu dakika ya 52 akiunganisha krosi ya Gareth Bale.
Benzema alirudi tena kambani dakika ya 76 akifunga bao la nne na kuifanya Real Madrid kuzidi kujikuta kileleni mwa msimamo wa ligi hiyo wakiwa na pointi 51 baada ya kucheza mechi 20, pointi nne zaidi ya wanaowafukuzia Barcelona wanaocheza leo na Atletico Madrid walioshinda jana ugenini kwa mabao 3-1.
Matokeo mengine ya mechi hiyo, Rayo Vallecano ilikubali kichapo nyumbani cha mabao 2-1 mbele ya wageni wa Deportivo La Coruna, Atletico Madrid wakishinda ugenini mabao 3-1 dhidi ya Eibar, Granada wakishinda nyumbani bao 1-0 dhidi ya Elche na Celta Vigo wakiilaza Cordoba kwa bao 1-0.
Ligi hiyo itaendelea tena leo kwa michezo ifuatayo;
Levante vs  Athletic Bilbao (saa 8 mchana)
Almería vs Getafe (saa 1 usiku)
Sevilla vs Espanyol (saa 3 usiku)
Barcelona vs Villarreal (saa 5 usiku)

Yanga, Ndanda hapatoshi leo Taifa

Yanga
Ndanda FC
KLABU ya soka ya Yanga leo watakuwa na kibarua kigumu mbele ya Ndanda Fc ya Mtwara katika mfululizo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.
Yanga ambayo imetoka kupata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Polisi Moro itawakaribisha Ndanda kwenye dimba la Taifa, jijini Dar es Salaam huku wageni hao wa ligi ambao walitoka kuwatoa nishai Kagera Sugar.
Vijana wa Jangwani ambao walikuwa nafasi ya pili katika msimamo kabla ya mechi zilizochezwa jana, wametamba kushinda mchezo huo wakiwa na nia ya kujiweka pazuri kwenye mbio zao za kurejesha taji hilo.
Yanga inayonolewa na kocha Hans van der Pluijm ina pointi 18 baada ya mechi 10 wakati wapinzani wao wakikamata nafasi ya 12 wakiwa na pointi 13 wakianza kuchanganya kasi tofauti na walipoianza ligi hiyo.
Kocha wa Ndanda, Meja Abdul Mingange alinukuliwa kuwa anatarajiwa upinzani mkali toka kwa Yanga, lakini vijana wake wapo tayari kupigana ili kuendeleza wimbi lao la ushindi baada ya kushinda mechi iliyopita.
Yanga itakayoiwakilisha Tanzania kwenye Kombe la Shirikisho, inakabiliwa na mechi nyingine ngumu katikati ya wiki dhidi ya Coastal Union.
Mechi hiyo ya Yanga na Coastal Union itachezwa siku ya Jumatano  kwenye uwanja wa Mkwakwani, ikiwa ni mechi ya kiporo baina ya timu hizo baada ya mechi ya awali kuahirishwa ili Yanga ishiriki Mapinduzi Cup.
Wanayanga wanahamu ya kutaka kuona timu yao ikipata matokeo mazuri leo na mechi ya Jumatano baada ya awali kuzinguliwa na sare mbili mfululizo dhidi ya Azam na Ruvu Shooting kabla ya kuilaza Polisi.
Pambano jingine litakalochezwa leo katika mfululizo wa ligi hiyo ni lile la Ruvu Shooting watakaoikaribisha Stand United ya Shinyanga kwenye uwanja wa Mabatini, Mlandizi Pwani.
Msemaji wa Ruvu, Masau Bwire ametamba kuwa vijana wao wanaonolewa na kocha Tom Olaba wapo tayari kuvuna pointi tatu baada ya kuwatioa nishai na kuvunja mwiko wa Mtibwa wa kutofungwa katika ligi walipowazabua mabao 2-1 wiki iliyopita ikiwa ni siku chache walipong'ang'ania Yanga na kutoka 0-0.

DR Congo, wenyeji watangulia Nusu Fainali Afrika

Javier Balboa akishangilia moja ya mabao ya wenyeji Guinea ya Ikweta
Referee Rajindraparsad Seechurn is shielded from angry Tunisia players by security personal
Polisi wakimuokoa refa baada ya wachezaji wa Tunisia kuchukizwa na penati waliopewa wenyeji dakika za jioni
Guinea's midfielder Javier Balboa (bottom-R) celebrates with teammates after scoring their second goal
Wenyeji Guinea ya Ikweta wakishangilia ushindi wao dhidi ya Tunisia
Democratic Republic of the Congo's forward Jeremy Bokila (C) celebrates his goal in Bata
DR Congo wakipongezana walipowaduwaza majirani zao Congo-Brazzaville
Mbokani and Sagesse Babele go flying as they compete for the ball in a hotly contested game
Ilikuwa kama Vita baina ya Congo-Brazzaville na DR Congo
TIMU za DR Congo na wenyeji Guinea ya Ikweta zimekuwa timu za kwanza kufuzu Nusu Fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika baada ya kushinda mechi zao za Robo Fainali bila kutarajiwa.
DR Congo walityoka nyuma ya mabao 2-0 na kuibuka na ushindi wa mabao 4-2 dhidi ya wapinzani wao wa jadi Congo-Brazzaville katika mchezo uliochezwa mapema kabla ya wenyeji kuwang'oa kwenye muda wa ziada mabingwa wa zamani wa Afrika Tunisia kwa mabao 2-1.
Congo-Brazzaville walianza kuwashtua majirani zao dakika 10 baada ya kuanza kwa kipindi cha pili pale Ferebory Dore alipofunga bao la kuongoza kabla ya Thievy Bifouma kuongeza la pili dakika ya 62 baada ya kutokea piga nikupige langoni mwa DR Congo.
Hata hivyo DR Congo hawakukata tamaa baada ya kufungwa mabao hayo mawili na badala ake kucharuka na kurejesha bao moja baada ya jingine kupitia wachezaji wake nyota, Dieumerci Mbokani aliyefunga mabao mawili katika dakika ya 65 na 90, Jeremy Bokila dakika ya 75, na   Joel KImwaki aliyefunga bao la tatu dakika ya 81 na kuivusha timu yao nusu fainali tangu 1988.
Katika meechi ya pili iliyochezwa pia kwenye uwanja huo wa Bata usiku wenyeji waliwaduwaza Tunisia kwa kuwalaza mabao 2-1 wakichomoa bao dakika ya jioni na kumaliza dakika 90 kwa sare ya 1-1 kabla ya kufunga bao la ushindi kwenye muda wa nyongeza wa dakika 30.
Tunisia walianza kuandika bao lililokuwa likionekana kama limewavusha hatua ya nusu fainali kupitia kwa Ahmed Akaichi katika dakika ya 70, lakini Guinea ya Ikweta ilichomo dakika za ziada za pambano hilo kabla ya halijamalizika kupitia kwa Javier Balboa aliyefunga kwa penati, iliyozua zogo kwa wachezaji wa Tunisia kumlalamikia mwamuzi kiasi cha Polisi kuamua kuingilia kati kumuokoa mwamuzi huyo.
Dakika ya 102 Balboa tena aliwatoa kimasomaso wenyeji wa kufunga bao la pili ambalo lilidumu hadi mwisho wa mchezo na kuifanya Guinea ya Ikweta kufuzu kwa mara ya kwanza hatua hiyo na sasa wanasubiri mshindi kati ya Ghana na Guinea wanaocheza leo kwenye robo fainali nyingine wa michuano hiyo.
DR Congo wenyewe watasubiri kujua watacheza nani hatua ya nusu fainali kati ya Ivory Coast na Algeria ambazo zitakamilisha mechi za robo fainali usiku wa leo kwenye uwanja wa Malabo.