STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, February 22, 2015

Liverpool yaua, Spurs, Everton zabanwa nyumbani

Hivi ndivyo vita vya Liverpool na wenyeji wao Soputhmapton ilivyokuwa Victor Wanyama akichuana na Jordan Hendeson

WAKATI klabu ya Tottenham Hotspur ikilamizika kupigana kiume kurejesha mabao mawili ili wasife nyumbani mbele ya West Ham Utd, Liverpool wameendelea kutoa dozi kwa kuicharaza Southampton kwa mabao 2-0 katika mfululzii wa Ligi Kuu ya England.
Spurs ikiwa nyumbani ilitanguliwa kufungwa mabao 2-0 kabla ya kuyarejesha baadaye na kuambulia sare ya mabao 2-2, shukrani za pekee zieende kwa Harry Kane aliyefunga bao la kusawazisha baada ya awali kukosa penati na mpira kumrudia na kuutumbukiza wavuni.
Katika mchezo mwingine timu ya mkiani ya Leicester City ilijitutumua na kulazimisha sare ya ugenini ya mabao 2-2 dhidi ya Everton kabla ya hivi punde Liverpool kuandikisha ushindi wa mabao 2-0 ugenini dhidi ya Southampton.
Mabao ya Phillipe Coutinho katika dakika ya tatu na jingine la kipindi cha pili lililofungwa na Raheem Sterling liliwapa vijogoo hao wa Anfield kupata ushindi huo uliowafanya wafikishe jumla ya pointi 45 na kulingana Spurs ingawa wameshindwa kuiengua Southampton katika nafasi ya tano wakati ligi ikiwa ipo raundi ya 26.
Katika pambano hilo wenyeji walilalamika kunyimwa penati mbili za wazi baada ya wachezaji wao kufanyiwa madhambi langoni mwa Liverpool.

Mwadui Fc ndiyo mabingwa wa FDL2014-2015

Kocha wa Mwadui, Jamhuri Kihwelu 'Julio
http://shaffihdauda.co.tz/wp-content/uploads/2015/01/DSC_4165.jpg
Mabingwa wa FDL,. Mwadui Shinyanga walioizabua Wana Kimanumanu kwa bao 1-0
'KOCHA Jamhuri Kihwelu 'Julio'amedhihirisha kweli yeye ni bab'Kubwa baada ya kuiongoza timu yake ya Mwadui Shinyanga kupata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Africans Sports ya Tanga na kunyakua ubingwa wa Ligi Daraja la Kwanza Tanzania Bara (FDL).
Mwadui imeibuka na ushindi huo katika mechi iliyochezwa kwenye uwanja wa Azam Complex, Chamazi na kuzima ngebe za wapinzani wao waliotamba awali kushinda pambano hilo kudhihirisha kuwa Mwadui ni 'vibabu'.
Hata hivyo tambo hizo za Wana Kimanumanu zilizimwa kwa bao tamu la kichwa lililofungwa na Kelvin Sabato 'Kiduku' na kuwapa taji Mwadui ambao waliongoza katika kundi lao la ligi daraja la kwanza na kupanda Ligi Kuu msimu wa 2015-2016 mwaka mmoja baada ya kubaniwa na TFF msimu uliopita.
Mbali na Mwadui, nyingine zilizopanda ligi hiyo msimu ujao kuchukua nafasi ya timu nne zitgakazoshuka katika Ligi ya msimu huu inayozidi kushika kasi ni Africans Sports, Toto Africans na Majimaji-Songea.

Mnyama afa Shinyanga, Stand Utd yaifanyizia

Kikosi cha Simba
BAADA ya kufanikiwa kuondoa 'gundu' kwa Polisi Moro na kudai walikuwa wameianza rasmia Ligi Kuu, klabu ya Simba leo ametolewa nishai ugenini mjini Shinyanga kwa kukubali kipigo cha bao 1-0.
Kipigo hicho kimetolewa kwa Simba na timu ya Stand United katika pambano tamu lililochezwa kwenyue uwanja wa Kambarage na kuzima mbwembwe za vijana wa Msimbazi huku mashabiki wao wakiibua zogo.
Zogo hilo lililosababisha pambano hilo kusimama kwa muda ilitokana na imani kwamba lango la wapinzani wao lilikuwa limefukiwa 'vitu' ambavyo vilikuwa vikiwafanya vijana wao kushindwa kufunga mabao.
Bao pekee lililowaua Simba ya kocha Goran Kopunovic, liliwekwa kimiani na Mnigeria Absalim Chiibibele likiwa ni bao lake la tano msimu huu katika dakika ya 11 na kuwafanya Simba kuhaha kurirejesha bila mafanikio.
Kwa kipigo hicho Simba imesaliwa na pointi pointi 20 baada ya mechi 16 wakati Stand imefikisha pointi 18 baada ya mechi 16 pia na itavaana na Kagera Sugar katika mechi yao ijayo mjini Shinyanga.

Yanga 'watamu' kama Mcharo! Yaifumua Mbeya City

Simon Msuva aliyeanza kufungua neema ya mabao Mbeya leo
Mrisho Ngassa  akadhihrisha amerejea upya Jangwani
Amissi Tambwe akamaliza udhia kwa kufunga bao la tatu
MABAO matatu kutoka kwa Simon Msuva, Mrisho Ngassa na Amissi Tambwe yameiwezesha Yanga kupata ushindi wa pili mfululizo jijini Mbeya baada ya kuicharaza Mbeya City kwa mabao 3-1.
Mchezo huo wa Ligi Kuu Tanzania Bara ulichezwa kwenye uwanja wa Sokoine na kuiwezesha Yanga kuibuka na ushindi huo mnono ulioifanya izidi kujizatiti kileleni ikiwa na pointi 31 baada ya mechi 15.
Simon Msuva alianza kufunga katika kipindi kwanza kabla ya Ngassa 'kuzawadiwa' bao mara baada ya kipindi cha pili kutokana na mbwembwe za kipa David Burhan wa Mbeya City kumpoza.
Kipa huyo Bora wa msimu wa 2012-2013, alirudishiwa mpira na Steven Mazanda na badala ya kuupiga mbele alijaribu kumpiga chenga Ngassa aliyeunasa kilaini na kutumbukiza wavuni kaundika bao la pili la Yanga.
Amissi Tambwe aliunganisha kwa kichwa mpira wa kona uliopigwa na Haruna Niyonzima na kuiandikia bao la tatu, wakati huo tayari wenyeji alishapata bao la kufutia machozi kupitia kwa Peter Mapunda.
Bao hilo la Mapunda limeitibua rekodi ya kipa Ally Mustafa 'Barthez'ambaye alikuwa amecheza muda wa dakika 704 bila kuruhusu wavu wake kutikiswa. Dakika hizo ni 630 za mechi sita na 74 za leo kabla ya Mapunda kumtungua kufuatia mabeki wake kushindwa kuokoa.
Kwa ushindi huo Yanga imejikita kileleni ikiwa na pointi 31 baada ya mechi 15 ikijiandaa kuondoka nchini kwenda Botswana kurudiana na BDF XI katika mechi ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Simanzi! Christopher Alex hatunaye duniani!

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgTo5gnxm0hxL2vl32ZTdKTWURp8bI9AhqxaS4u79wBsu7mcRP0Bn9ulEdWLFZaFH-QzfMXd4561SJIzpTRzFR-0cOFzLUd4bEqUojYVciaPBRvmiskU_my2Mc8MEQgDkCBkGg0-aT8C85u/s1600/426453_235934163168144_100002546855024_482737_173110702_n.jpg
Christopher Alex (wa tatu toka kulia) enzi za uhai wake akiwa na kikosi kilichoing'oa Zamalek mwaka 2003
KIUNGO nyota wa zamani wa klabu ya Simba na timu ya taifa, Taifa Stars, Christopher Alex Massawe amefariki dunia asubuhi ya leo.
Kwa mujibu wa taarifa ambazo MICHARAZO imezipata mapema zinasema kuwa, kiungo huyo aliyekuwa akiugua kwa muda mrefu amefariki akiwa kalazwa katika Hospitali ya Milembe, iliyopo mkoani Morogoro.
Alex, anayekumbukwa kwa kupiga penati ya mwisho ya Simba iliyowavua ubingwa Zamalek ya Misri katika pambano la Ligi ya Mabingwa kati yao iliyochezwa mwaka 2013, alikuwa akisumbuliwa na maradhi ya kifua.
Mama mzazi wa Alex amethibitisha kutokea kwa kifo hicho ambaye alikuwa akiishi naye na kumuuguza kwa msaada wa wasamaria wema wakiwamo wadau wa soka.
Wakati klabu yake ya zamani ikiwa 'ímemsusa', mashabiki wa klabu hiyo na wengine wa soka walikuwa bega kwa bega na mama huyo kwa kuchangia fedha za matibabu, harambe kubwa ikiendeshwa na kituo cha Cloud's FM
Marehemu Christopher Alex, alizaliwa Septemba 12, 1975, na kupata elimu yake ya msingi katika shule ya msingi Uhuru na kumaliza katika shule ya Chamwino huko Dodoma mwaka 1993.
Alianza kucheza mpira kwenye timu ya daraja la nne ya Chamwino Utd na baadaye daraja la tatu akiwa na kikosi cha Aston Villa nayo ya Dodoma.

Mwaka 1999-2001, aliitumikia klabu ya CDA ya Dodoma, kabla ya kutimkia klabu ya Reli ya Morogoro mwaka 2002, na baadaye kujiunga na Wekundu wa Msimbazi Simba.
Marehemu ameacha mtoto mmoja aitwaye Alex.
MICHARAZO inatoa pole kwa ndugu, jamaa na familia nzima ya marehemu Alex kwa msiba huo na kuwaombea Subira kwa Mungu kwa kukumbuka kuwa 'Kila Nafsi Itaonja Mauti'
Mungu aiweke roho ya marehemu Alex Mahali Pema Ameen!

Bingwa wa FDL kujulikana leo Chamazi

http://shaffihdauda.co.tz/wp-content/uploads/2015/01/DSC_4165.jpg
Mwadui Shinyanga
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhX4CPi_gLzDiNDFJxODqQK-bun_Lz_-fqogmOSBafonpNyQztxKsciMrA9kx7T2CAkfa14juJT5WVK1BxZPxkqTuD40uPWHMTtpatpKUHMvQpdWau2Aw3yYJfbYrgwYFAnwHWaIEFpT7c/s1600/sports.JPG
Africans Sports 'Wana Kimanumanu'
FAINALI za kusaka Bingwa wa Ligi Daraja la Kwanza Tanzania Bara (FDL), zinafanyika leo kwa pambano kati ya Mwadui Shinyanga dhidi ya Africans Sports mchezo utakaochezwa kwenye Uwanja wa Azam Complex Chamazi kuanzia majira ya saa 10 kamili jioni kwa saa za Afrika Mashariki.
Awali mchezo huo wa fainali ulikuwa umepangwa kufanyika kwenye dimba la Uwanja wa Taifa, lakini kutokana na sababu zilizopo nje ya uwezo wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini TFF imepelekea mchezo huo kuhamishiwa Chamazi.
Mchezo huo wa fainali utaanza saa 10 kamili jioni, na utaonyeshwa moja kwa moja na kituo cha Azam TV ili kuwapa nafasi wapenzi na wadau wa soka waliopo mbali na hasa mikoani kuweza kushuhudia mchezo huo.
Bingwa wa Fainali ya Ligi Daraja la Kwanza atazawadiwa Kombe pamoja na medali, huku mshindi wa pili akipata kikombe na medali pia.
Viingilio vya mchezo huo ni tsh.5,000 kwa jukwaa kuu na tsh. 3,000 kwa majukwaa ya mzunguko.

Mo Farah aweka rekodi ya dunia

http://e0.365dm.com/15/02/660x350/mo-farah-birmingham-indoor-two-mile-record_3267495.jpg?20150221163812
Mwanariadha Mo Farah akimaliza mbio na kuweka rekodi mpya Birmingham
LONDON, England
MWANARIADHA Muingereza Mo Farah amevunja rekodi ya dunia ya mbio za ndani za Maili Mbili katika mbio za Birmingham Indoor Grand Prix.
Farah, 31, aliondoka uwanjani baada ya kumaliza mbio hizo kwa kutumia dakika 3.40 akiivunja rekodi iliyotanguliwa iliyowekwa na Muethiopia Kenenisa Bekele.
Hiyo ni rekodi ya kwanza kuwekwa na mwanariadha huyo bingwa mara mbili wa Olimpiki.
"Hii ina maana kubwa kwangu, " alisema Farah. "Napenda kuliwakilisha taifa langu, kutoa kitu fulani kwa watu wote. Siamini. "
Maandalizi ya kabla ya kuanza kwa mbio hizo za Jumamosi yalitawaliwa na malumbano dhidi ya mchezaji mwenzake Muingereza Andy Vernon.
Farah alidai kuwa Vernon alihoji uraia wake baada ya bingwa huyo mara mbili wa Olimpiki kushinda mbio za Ulaya za mita 10,000 mwaka 2014, huku Vernon akielezea kuwa huo ulikuwa ni upotoshaji mkubwa.
Pamoja na suala hilo lakini Farah hakutetereka kwani alitawala mbio hizo zilizofanyika jijini Birmingham, na kuwaacha Mkenya Paul Koech na Mmarekani Bernard Lagat na kushinda mbio hizo.
"Ni (malumbano na Vernon) ndio yaliyonihamasisha mimi, nilitaka kufanya hivyo, " alisema Farah.

Simba, Yanga Azam katika vita nyingine VPL

Kikosi cha Simba kitakachokuwa mjini Shinyanga,

Azam watakuwa uwanja wa nyumbani wa Chamazi
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhErXyx1Zkj3OCoFFiXSN67k52f3gi-xri1jU6EVAQNSzUHaLOE-aGYio6UwnJav0_qsoTFjW-lII6MoCyTEDN6NO6aDEosezFiW3YLR8VtXdxto3puBagAfzT7oBKaY4iLz98CetK57ihU/s1600/IMG_0916.JPG
Kikosi cha Yanga kilichopo ugenini jijini Mbeya kuvaana na Mbeya City
VIGOGO vya Ligi Kuu Tanzania Bara, Simba, Yanga na Azam zitakuwa kwenye viwanja tofauti kwa ajili ya kusaka pointi tatu muhimu katika mbio za kuwania ubingwa wa ligi hiyo.
Vinara Yanga wenyewe watakuwa kwenye uwanja wa Sokoine kwa mara nyingine tena kupepetana na wenyeji wao Mbeya City, ikiwa ni siku chache baada ya kugawa dozi ya mabao 3-0 dhidi ya Prisons.
Simba walioanza kushika kasi katika ligi hiyo baada ya kuchechemea kwa muda mrefu, pia ipo ugenini mkoani Shinyanga kwa ajili ya kupepetana na Stand United  kwenye uwanja wa Kambarage.
Mabingwa watetezi Azam watakuwa uwanja wa nyumbani wa Azam Complex, Chamazi kuikaribisha Prisons-Mbeya baada ya katikati ya wiki kubanwa mbavu na Ruvu Shooting na kutoka suluhu ya 0-0.
Yanga watakuwa na hamu ya kuendeleza rekodi yao ya kushinda mfululizo, ingawa Mbeya City ambayo imekuwa haina msimu mzuri safari hii ikiwa imeapa kumaliza uteja kwa wapinzani wao hao.
Mbeya City iliyopanda ligi kuu msimu uliopita, haijawahi kuifunga Yanga zaidi ya kulazimisha sare au kuambulia vipigo, kitu ambacho Kocha wake, Juma Mwambusi anaamini leo watavunja mwiko.
Hata hivyo Yanga imetamba kutaka kutoa dozi kwa lengo la kuongeza morali kabla ya kuondoka nchini kwenda Botswana kwa ajili ya mechi ya marudiano ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya BDF XI.
Yanga inayoongoza msimamo wa ligi ikiwa na pointi 28, mbili zaidi ya Azam yenye 26 itarudiana na BDF wiki ijayo mjini Gaborone baada ya wiki iliyopita kuwacharaza mabao 2-0.
Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa Yanga, Jerry Muro alisema hawaoni cha kuwazuia kuvuna pointi nyingine tatu jijini Mbeya wakati kikosi chao kimeandaliwa vema na kina morali mkubwa.
Muro alisema anafahamu Mbeya City ni timu ngumu na itataka kutumia vema uwanja wa nyumbani, lakini Yanga imejipanga kutoka na pointi zote ili kujikita zaidi kileleni kabla ya kwenda Botswana.
Wakati Yanga na Mbeya wakiwindana hivyo, Simba wenyewe wakiwa na furaha ya ushindi wa mabao 2-0 iliyopata ugenini mjini Morogoro dhidi ya Polisi wataivaa Stand United wakiwa na tahadhari kubwa.
Stand Utd imetoka kuwatoa nishai Mgambo JKT kwa kuicharaza mabao 4-1, kitu ambacho kinaonyesha namna gani wameanza kuizoea ligi hiyo wanayoicheza kwa msimu wao wa kwanza.
Katika pambano hilo kila timu itakuwa ikitegemea nyota wake, Simba ikitambia akina Emmanuel Okwi, Dan Sserunkuma, Eliasi Maguri na wengine huku Stand ikimtegemea Mnigeria Abasalim Chiibibele na Heri Mohammed wenye mabao manne kila mmoja katika ligi hiyo.
Katika mchezo wa kwanza uliochezwa Oktoba 4, mwaka jana timu hizo zilizoshindwa kutambiana baada ya kutoka sare ya bao 1-1 kwenye uwanja wa Taifa.
Angalia msimamo wa Ligi Kuu ulivyo:

                                P   W    D    L    F    A   GD Pts
01. Yanga               14  08   04  02  18  07  11  28
02. Azam                14  07   05  02  22  12  10  26
03. Kagera Sugar    16  06   06  04  13  11  02  24
04. Simba               14  04   08  02  15  11  04  20
05. Ruvu Shooting  15  05   05  05  10  11  -1   20
06. Mtibwa Sugar    15  04   07  04  15  15  00  19
07. Coastal Union   16   04  07   05  11  11  00  19
08. Polisi Moro        16  04   07   05  12  14  -2  19
09. JKT Ruvu          15  05  04  06   14   15  -1  19
10. Ndanda Fc        16  05  04   07  14   18  -4  19
11. Mbeya City       14  04  05  05   09   11  -2   17
12. Mgambo JKT    14  05  02  07   08    15  -7  17
13.Stand Utd         15  03  06   06   13   18  -5  15
14. Prisons            14  01  08   05   10   15  -5   11
Wafungaji:
8-
Didier Kavumbagu(Azam)

7- Rashid Mandawa (Kagera Sugar)
6-
Samuel Kamuntu (JKT Ruvu), Ame Ali (Mtibwa), Simon Msuva (Yanga),
5-
Danny Mrwanda (Yanga), Kipre Tchetche (Azam)
4- Rama Salim (Coastal),  Emmanuel Okwi (Simba), Nassor Kapama, Jacob Massawe (Ndanda), Heri Mohammed, Abasalim Chiibibele (Stand Utd) , Malimi Busungu (Mgambo)
3- Ally Shomari (Mtibwa), Frank Domayo (Azam), Atupele Green (Kagera)
2-
Shaaban Kisiga, Dan Sserunkuma, Elias Maguli (Simba), Salum Kanoni, (Kagera Sugar) Aggrey Morris (Azam),  Najim Magulu, Jabir Aziz (JKT Ruvu), Amissi Tambwe, Jerry Tegete, Mrisho Ngassa, Andrey Coutinho (Yanga), Ibrahim Kihaka (Prisons), Mussa Mgosi (Mtibwa), Mussa Said (Stand Utd), Ally Nassor (Mgambo), Nicolaus Kabipe (Polisi),Yahya Tumbo (Ruvu Shooting)

Chungulia video mpya ya Vanessa Mdee ft Barnaba-SIRI

Saturday, February 21, 2015

Chelsea wabanwa, Man Utd yafa, Arsenal raha

Ben Mee rises above the Chelsea defence to equalise for Burnley against Premier League leaders Chelsea at Stamford Bridge
Ben Mee akiisawazishia Burnley bao kwa kichwa
Mee wheels away in celebration after finding the target with a header to level proceedings at Stamford bridge with 10 minutes left
Oyooooooooooo!
Manchester United must get used to their new style of play under Louis van Gaal, according to Gary Neville
hoi
Cazorla is congratulated by his team-mates as Arsenal looked to pick up an eighth win in nine games
Arsenal kwa raha zao
Wilfried Zaha skips past Nacho Monreal in the opening moments, and the England winger caused his full back plenty of problems
ilikuwa vita
QPR walip[okuwa wakizamishwa ugenini
WAKATI vinara wa Ligi Kuu ya England, Chelsea wakingángániwa nyumbani kwa kulazimishwa sare ya bao 1-1, Mashetani Wekundu, Manchester United wamenyukwa mabao 2-1 na Swansea City, huku Arsenal ikingára ugenini kwa kupata ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Crystal Palace.
Chelsea wakiwa kwenye uwanja wao wa Stanford Bridge walitangulia kuandika bao la kuongoza lililofungwa na beki wake Branslav Ivanovic katika ya 14 na wageni Burnley kuchomoa bao hilo dakika tisa kabla ya mchezo kumalizika kupitia kwa Ben Mee.
Chelsea itajilaulumu kwa kushindwa kuibuka na ushindi nyumbani kutokana na kutawala mchezo huo na washambuliaji wake Eden Hazard na Diego Costa wakikosa mabao ya wazi.
Sare hiyo imeifanya Chelsea kufikisha pointi 60 na kutoa fursa kwa wapinzani wao mabingwa watetezi Manchester City kupunguza pointi zilizokuwapo kwani mpaka muda huu wa mapumziko City wanaoongozxa mabao 3-0 dhidi ya Newcastle United.
Katika mechi nyingine za ligi hiyo Arsenal ikiwa ugenini imeshinda mabao 2-1, Manchester Utd ikipigwa 2-1 na Swansea City, wakati Aston Villa wameendelea kutetepa kwa kukubali kichapo cha 2-1 wakiwa nyumbani toka kwa Stoke City huku QPR wakilala ugenini 2-1 mbele ya Hully City na timu za Sunderland na West Bromwich wakitoka suluhu ya kutofungana.

Barcelona yazamishwa nyumbani na Malaga

Barcelona 0-1t Bat BA Malaga
Juanmi akiitungua Barcelona leo
Barcelona forward Lionel Messi (left) vies with Malaga's forward Samuel Castillejo (right) on Saturday
Messi hakufua dafu leo kwa Malaga siku chache kabla ya Barcelona kuvaana na Manchester City kwenye mechi ya Ligi ya Mabingwa Ulaya
KLABU ya Barcelona ikiwa dimba la nyumbani la Camp Nou imekubali kipigo cha bao 1-0 mbele ya Malaga katika mfululizo wa Ligi ya Hispania, La Liga.
Kipigo hicho cha nne kwa Barcelona msimu huu katika ligi hiyo kimezidi kuongeza ushindani wa mbio za ubingwa dhidi ya watetezi Real Madrid ambayo watashuka dimbani kesho wakiwa ugenini.
Bao pekee la wageni Malaga mbele ya Barcelona liliwekwa kimiani na  Juanmi katika dakika ya saba ya mchezo huo na kungángánia hadi mwisho na kuwaacha Barcelona wakiwa hoi nyumbani.
Mechi nyingine inayochezwa hivi sasa Valencia wakiwa ugenini waongoza bao 1-0 dhidi ya wenyeji wao Cardoba.

Jahazi la Mtibwa lazidi kuzama, Coastal hoi, Kagera yaua

Mtibwa Sugar iliyoipokea kichapo cha nne mfululizo leo kwa Mgambo JKT
http://api.ning.com/files/cPakA0chAEyfyqjZRP3k2djpZ9GyxNW23W69D7FY4fYhsuNz2vmH6gr7yEITcci18IdnTvIgOej4xydmYu8LtJiXW0uQDhCL/16.jpg
Kagera Sugar waliongára Kambarage kwa kuilaza Polisi Moro
Polisi Moro wliopoteza mchezo wa pili leo mbele ya Kagera Sugar baada ya wiki iliyopita kulala kwa Simba 2-0
Ndanda iliyotakata nyumbani Mtwara kwa kuilaza Coastal Union 1-0
JAHAZI la Mtibwa Sugar linazidi kuzama baada ya kufungwa 1-0 na Mgambo JKT ikiwa ni mechi ya nne mfululizo kupoteza katika Ligi kuu Tanzania Bara.
Kipigo hicho cha Mtibwa kimeifanya timu hiyo kuzidi kuporomoka kwenye msimamo wa ligi hiyo wakisaliwa na pointi zao 19 baad ya mechi 15.
Bao lililoizamisha Mtibwa katika pambano hilo lililochezwa katika uwanja wa Mkwakwani Tanga, liliwekwa kimiani na Malimi Busungu katika dakika ya 36 na kuifanya timu yao kufikisha pointi 17.
Katika mchezo mwingine ul;iochezwa Nangwanda Sijaona, wenyeji Ndanda waliinyuka Coastal Union kwa bao 1-0 lililowekwa kimiani na Jacob Massawe katika dakika ya 79.
Aidha Kagera Sugar wakwia uwanja wa Kambarage Shinyanga wanaoutumia kama uwanja wao wa nyumbani, iliendelea kutakata baada ya kupata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Polisi Moro.
Bao hilo pekee lililowapa ushindi Kagera na kuzidi kujikita nafasi ya tatu ikifikisha pointi 24 liliwekwa kimiani na Rashid Mandawa ambaye anafikisha bao lake la saba katika ligi hiyo, bao moja nyuma dhidi ya kinara wa mabao kwa sasa wa ligi hiyo Didier Kavumbagu wa Azam.
Ligi hiyo itaendelea kesho kwa michezo mitatu, Yanga wakiwa uwanja wa Sokoine Mbeya kupapetana na Mbeya City, Simba watakuwa wageni wa Stand Utd mjini Shinyanga na Azam watauamana na Prisons Mbeya uwanja wa Chamazi.
Mechi hiyo ya Azam na maafande itachezwa saa 2 usiku na kila timu imetamba kujiandikishia ushindi katika pambano hilo.

Friday, February 20, 2015

Yamoto Band watua UK tayari kwa shoo wa kesho


Kikosi kizima cha Yamoto Band ndani ya jiji la London tayari kwa makamuzi ya jumamosi hii ndani ya ukumbi wa Royal Regency Monor Park London

Yamoto Band Touchdown London this morning., safe and sound.Now let's Get it...Let's Goooo. ..Made in East Africa 2015 ,Yamoto band Live in London Royal Regency Banquite .



Wakijiachia na mmoja wa mabosi wake







Enock Bella akiosha maji

Wacheza filamu nchini waonywa

Mlela akipeana mkono na Katibu Mtendani wa Bodi ya Filamu nchini, Joyce Fisoo
Na Genofeva Matemu, Maelezo
WASANII wa filamu nchini wameshauriwa kutumia taaluma waliyonayo kupanua wigo wa filamu nchini na kuitangaza Tanzania duniani kote kwa kuzingatia matumizi mazuri ya lugha ya Kiswahili katika filamu wanazozitengeneza.
Rai hiyo imetolewa na Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu, Joyce Fisoo, juzi alipokutana na wasanii waliotarajia kuondoka jana kwenda Uingereza kurekodi filamu ya 'Sabasi' na Kampuni ya Didas Entertainment iliyopo nchini humo.
Fisoo alisema kuwa baadhi ya wasanii nchini wamekuwa makontena yanayopitisha biashara haramu kutoka nchi moja kwenda nchi nyingine hivyo kuwaomba wasanii wanaokwenda Uingereza kuachana na tabia hiyo bali watumie fursa waliyoipata kuiwakilisha Tanzania vizuri na kutengeneza filamu bora itakayowawezesha kujulikana na kufungua fursa za kushirikishwa katika filamu na nchi nyingine duniani.
Aidha, Fisoo aliwataka wasanii hao kuheshimu sheria, kanuni na taratibu za Uingereza kwani kwa kufanya hivyo watakuwa mabalozi bora na kutoa nafasi kwa wasanii wengine kupata fursa hizo.
Naye Mama wa Didas Entertainment, Nuru Idrisa, aliwataka wasanii wa Bongo Movie waliopata nafasi ya kurekodi filamu na Didas Entertainment kujiheshimu na kuvaa mavazi ya staha yatakayostiri miili yao muda wote watakaokuwa nchini Uingereza kwani kwa kufanya hivyo watakuwa wamelinda heshima ya nchi.
Akitoa neno la shukrani, msanii wa Bongo Movie, Yusuph Mlela, aliishukuru Bodi ya Filamu kwa kuwa bega kwa bega na wasanii na kuwaahidi wadau wa filamu nchini kazi bora na yenye tija katika jamii.
Filamu ya 'Sabasi' inatarajiwa kurekodiwa hivi karibuni nchini Uingereza na Kampuni ya Didas Entertainment na kuwashirikisha wasanii Mlela, Esha Buhet na Husna Athumani, na ni filamu ya pili kurekodiwa na kampuni hiyo na kuwashirikisha wasanii kutoka Tanzania. Filamu ya kwanza kurekodiwa na kampuni hiyo iliyowashirikisha wasanii kutoka Tanzania ni ile ijulikanayo kwa jina la 'Mateso Yangu Ughaibuni'.

Balotelli alianzisha tena Liverpool

3f
Muunganiko wa picha zilizochapishwa na Daily Mail zinazomuonyesha Balotelli na nahodha wake, Steven Gerrard
Balotelli akifunga penati yake
Balotelli took the ball off Liverpool captain Jordan Henderson and fellow striker Daniel Sturridge to take the penaltyMARIO Balotelli, aliifungia Liverpool mkwaju wa penati dakika tano kabla ya kumalizika kwa pambano lao dhidi ya Besiktas ya Uturuki, lakini ameibua mambo.
Kitendo chake cha kulazimisha kuipiga penati hiyo kimemtibua nahodha wa timu ya Liverpool Steven Gerrard anayemshutumu kwa utovu wa nidhamu.
Balotelli alifunga penalti hiyo na kuiwezesha Liverpool kuibuka washindi wa bao 1-0 katika mchezo wa Ligi Ndogo ya Ulaya, katika uwanja wa Anfield.Hali hiyo ilijitokeza baada ya kushindwa kuelewana na nahodha wa mchezo huo Henderson na Daniel Sturridge juu ya nani abebe jukumu la kupiga penalti hiyo.
Gerrard amesema: "Henderson ni nahodha na Balotelli kwa kiasi fulani alionyesha kumkosea adabu katika hali hiyo."
Gerrard ambaye kwa sasa ni majeruhi, alikuwa mchambuzi katika matangazo ya mchezo huo kwenye televisheni ya ITV ya nchini Uingereza.
Katika mechi nyingine timu ya Tottenham Hotspur ililazimishwa sare ya 1-1 dhidi ya Fiorentina wakati Everton wakipata ushindi mnono wa mabao 4-1 ugenini dhidi ya Young Boys ya Uswisi.

NASAHA ZA IJUMAA-SIRI SIRINI

Thursday, February 19, 2015

Ally Mustafa 'Barthez' ni Nouma sana!

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi2gWCT-X80QbEFaBLH3ow-j-DUBUoiESu7HybsUaOTaiK29nZu8xGcFRQwETVHpw-nbY11UkU2DDjhKczuGFnfxgBd_5QO8ZU6Kvpo1vd4IHZkFNaX3sIoyhhtPOFOXUbpjMPWPETf4lkv/s1600/35.jpg
Barthez mbele kushoto akiwaongoza wachezaji wenzakle wa Yanga
PAMBANO la Yanga dhidi ya Prisons-Mbeya lililochezwa uwanja wa Sokoine, jijini Mbeya kwa vijana wa Jangwani wakiibuka na ushindi wa mabao 3-0 umezidi kumpandisha chati kipa Ally Mustafa 'Barthez' ambaye amedaka mechi sita mfululizo za Ligi Kuu Tanzania Bara bila kuruhusu bao lolote.
Kipa huyo aliyekuwa na wakati mgumu mbele ya kikosi cha Jangwani tangu Yanga ilipolazimishwa sare ya mabao 3-3 na Simba Oktoba mwaka juzi, hajafungwa bao lolote katika muda wa dakika 540 huku kwenye uwanja wa Sokoine akigeuka kuwa shujaa kwa kuokoa michomo mingi ya wachezaji wa Prisons.
Hizo ni mbali na dakika 90 za pambano la kimataifa la Kombe la Shirikisho Afrika ambapo Yanga ilishinda mabao 2-0 na yeye akiwa kwenye milingoni mitatu ya lango ya vijana wa Jangwani.
Barthez aliyesajiliwa na Yanga akitokea Simba, rekodi zake zinaonyesha kuwa ameshuka dimba katika mechi hizo kama ifuatavyo na kuwafunika makipa wote wa timu nyingine 13 zinazoshiriki ligi hiyo.
Jan 17, 2015Yanga vs Ruvu Shooting (0-0)
Jan 24, 2015Polisi Moro vs Yanga (1-0)
Feb 01, 2015Yanga vs Ndanda (0-0)
Feb 4, 2018Coastal Union vs Yanga (0-1)
Feb 08, 2015Yanga vs Mtibwa Sugar (2-0)
 Feb 14, 2015-Kimataifa
Yanga vs BDF XI (2-0)
Feb 19, 2015
Prisons vs Yanga (0-3)

FAINALI ZA DUNIA 2022 KUFANYIKA DESEMBA?

http://www.shalomlife.com/img/2014/12/27573/qatar_.jpg
MTANDAO mmoja barani Ulaya umetoa taarifa kuwa tayari muafaka umeshafikiwa kwa michuano ya Kombe la Dunia itakayofanyika nchini Qatar mwaka 2022 kufanyika katika kipindi cha Novemba na Desemba ili kuwepa joto kali katika kipindi cha kiangazi.
Wakiorodhesha vyanzo mbalimbali mtandao huo umedai kuwa uamuzi umeshafanyika kwani kikosi kazi kilichoteuliwa na Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) kinatarajia kuwasilisha miezi hiyo katika kikao chao kitakachofanyika wiki ijayo jijini Doha kabla ya kamati ya utendaji haijakamilisha mpango huo wakati wa kikao cha mwezi ujao jijini Zurich.
Wiki tatu zilizopita, Katibu Mkuu wa FIFA Jerome Valcke katika mahojiano yake na radio moja nchini Ufaransa alisema Kombe la Dunia nchini Qatar linatakiwa kuandaliwa wakati wa majira ya baridi lakini kugongana na michuano ya Olimpiki ya kwenye baridi Februari mwaka 2022 pia ni hatihati.
Hata hivyo mpango huo haujafafanua kwa undani zaidi kuwa michuano ya Kombe la Shirikisho ambayo huchezwa mwaka mmoja kabla ya Kombe la Dunia kama nayo itasogezwa mbele kuepuka majira ya kiangazi.
Desemba mwaka jana Chama cha Vilabu barani Ulaya na Muungano wa Ligi za Soka barani humo vilipendekeza michuano hiyo ya Qatar kuchezwa kati ya May na Juni ili kutovuruga ratiba zingine za kawaida za msimu.
Uteuzi wa Qatar kuandaa fainali hizo na zile za mwaka 2018 nchini Russia zimeghubikwa na mizengwe na kuelezwa kujaa vitendo vya rushwa, ingawa FIFA imekuwa ikijitetea.

BAHANUZI, MAHUNDI WANG'ARA VPL

http://2.bp.blogspot.com/-ORUnNfNV-xE/VM0wOPMp6vI/AAAAAAABdBc/1sAbma_8dB4/s1600/BAHANUZI.jpg
Said Bahanuzi
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh2NUIe7-6s8hh3LAnWZphC1Sfmct-j1gnFK6vBlYl6-vWAkEms7KvbsXk8lsXx7as54qc9WOVhCaehk3-wlIYA3DXm_G5D2mryGl3IxaJ0IKhGMNNPLYmPUTtm0N9aOnG0wHywciFMsGQ/s1600/IMG_1197.jpg
Mahundi (kulia) akichuana na Niyonzima katika moja ya mechi ya Ligi Kuu
KIUNGO wa timu ya Coastal Union ya Tanga, John Mahundi amechaguliwa kuwa mchezaji bora wa mwezi Desemba 2014 wa Ligi Kuu Tanzania Bara.
Mahundi alitoa mchango mkubwa kwa timu yake ya Coastal Union mwezi huo na kuchaguliwa na jopo la makocha linalofanya kazi ya kuchagua mchezaji bora wa kila mwezi.
Aidha mshambuliaji wa timu ya Polisi Morogoro, Said Bahanuzi 'Spider Man' amechaguliwa kuwa mchezaji bora mwezi Januari 2015.
Bahanuzi anayechezea timu ya Polisi Moro kwa mkopo akitokea timu ya Young Africans amekua na mchango mkubwa kwa timu yake tangu kujiunga nayo mzunguko wa pili wa Ligi Kuu ya Vodacom nchini.
Kwa kuibuka wachezaji bora, Mahundi na Bahanuzi watazawadiwa fedha taslimu Sh. Mil. 1/ kwa kila mmoja kutoka kwa wadhamini wa ligi hiyo kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom.
Jopo maalum la makocha waliopo katika viwanja vyote vinavyotumika kwa mechi za Ligi Kuu ndiyo wanaofanya kazi ya kuchagua mchezaji bora kwa kila mechi kwa kuzingatia vigezo vilivyowekwa.
Baadaye alama zao kujumlishwa ili kumpata mshindi wa mwezi.

Yanga wafanya mauaji Mbeya, Azam yabanwa

Yanga
Msuva na Coutinho walipokuwa wakijiandaa kuiangamiza Prisons-Mbeya

Azam
Azam walishindwa kushangilia kama hivi leo kwa Ruvu Shooting
KLABU ya Yanga imeendeleza rekodi yake ya kugawa dozi kwa wapinzani wao katika Ligi Kuu Tanzania Bara, baada ya kuilaza Prisons-Mbeya kwa mabao 3-0 na kukwea kileleni mwa msimamo wakiiengua Azam.
Azam waliokuwa uwanja wa Mabatini-Mlandizi wameshindwa kutamba kwa kulazimishwa suluhu mbele ya maafande wa Ruvu Shooting na kutoa nafasi kwa Yanga kuwaacha kwa pointi mbili kileleni.
Kwa suluhu iliyopata kwa Ruvu, imeifanya mabingwa watetezi Azam kufikisha pointi 26 na kushuka hadi nafasi ya pili licha ya timu zote mbili kulingana mechi zote zikicheza michezo 14 kila moja.
Yanga ikicheza kwenye uwanja wa Sokoine, Mbeya walipata ushindi huo murua na uliowafanya kufikisha pointi 28 baada ya kupata mabao yake mawili katika kipindi cha kwanza na jingine kipindi cha pili.
Mabao hayo yaliwekwa kimiani na Simon Msuva aliyefunga dakika ya tatu tu ya mchezo kabla ya Coutinho kuongeza la pili.
Msuva alirudi tena kambani kwa kufunga bao la tatu kipindi cha pili na kumfanya afikishe jumla ya mabao sita akibakisha mabao mawili kumkuta Didier Kavumbagu wa Azam mwenye mabao nane.
Yanga wataendelea kusalia jijini humo kwa ajili yua kusubiri pambano lake la Jumapili dhidi ya Mbeya City kabla ya kutimka zao Botswana kuwafuata BDF XI kwa ajili ya mechi ya marudiano ya Kombe la Shirikisho Afrika.
Katika mchezo wao wa kwanza uliochezwa mwishoni mwa wiki, Yanga iliitambia BDF kwa kuilaza mabao mawili yote yakiwekwa kimiani na Mrundi, Amissi Tambwe.