STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, January 13, 2017

Maafande wa Ruvu washindwa kutambiana Mabatini

JKT Ruvu
Ruvu Shooting
Na Rahim Junior
MAAFANDE wa JKT Ruvu na Ruvu Shooting zimeshindwa kutambiana jioni ya leo baada ya kutoka sare ya bao 1-1 katika muendelezo wa Ligi Kuu Bara iliyoanza tena baada ya kusimama kwa wiki mbili.
Timu hizo zimevaana kwenye Uwanja wa Mabatini, Mlandizi na JKT imeshindwa kulipa kisasi cha kipigo cha bao 1-0 ilichopewa na ndugu zao hao kwenye mchezo wa duru la kwanza.
JKT ndio waliojkuwa wa kwanza kuandika bao la kuongoza lililopatikana mapema dakika ya tatu tu, kupitia Renatus Morris, lakini Ruvu Shooting ilichomoa dakika sita baadaye kupitia mfumania nyavu wao mahiri, Abdulrahman Mussa.
Bao la Mussa limemfanya kufikisha jumla ya mabao nane na kubakisha moja tu kuwanasa vinara wa magoli, Shiza Kichuya wa Simba, Amissi Tambwe na Simon Msuva wa Yanga wenye mabao tisa kila mmoja.
Sare hiyo haijabadilisha lolote katika nafasi kwa timu hizo, kwani Ruvu imeongeza pointi na kufikisha 24, lakini imesalia nafasi iliyokuwapo sawa na JKT ambayo inasalia mkiani ikiwa na pointi 15 tu,  ikiwa imecheza mechi 19.
Ligi hiyo itaendelea tena kesho Jumamosi kwa mechi mbili ambapo mjinio Shinyanga, Chama la Wana, Stand United itavaana na Mwadui kwenye Uwanja wa Kambarage, huku Ndanda itakaribishwa na Kagera Sugar kwenye Uwanja wa Kaitaba, mjini Bukoba mkoani Kagera.
Msimamo wa Ligi Kuu Bara
                               P  W   D  L   F   A  Pts

1. Simba                 18 14  2   2  30  6  44
2. Yanga                 18  12  4   2  39  9  40
3. Azam                  18  8   6   4  23  15 30
4. Mtibwa Sugar      18  8    6   4  22  19 30
5. Kagera Sugar      18  8   4   6   19  18 28
6. Mbeya City          18  6   6   6   16  16 24
7. Ruvu                   19  5   9   5   18  20  24
8. Stand Utd            18  5   7   6   16  16  22
9. Prisons                18  5   7   6   10  13  22
10.Mwadui               18  6   4   8   16  22 22
11.African Lyon        18  4   8   6   11   16  20
12.Mbao                  18  5   4   9   17  24  19
13.Ndanda               18  5   4   9   15  24  19
14.Majimaji              18  5   2  11  13  26  17
15.Toto Africans        18  4   4  10  11  20  16
16.JKT Ruvu            19   3   9   7    7  17   15

Wafungaji:   

9- Shiza Kichuya                           (Simba)
     Simon Msuva                            (Yanga)   
     Amissi Tambwe                         (Yanga)
8- Abdulrahman Mussa      (Ruvu Shooting)
7- Rashid Mandawa             (Mtibwa Sugar)
    Donald Ngoma                           (Yanga)
    John Bocco                                 (Azam)
6- Mzamiru Yasin                           (Simba)
    Haruna Chanongo            (Mtibwa Sugar)
5- Omar Mponda                          (Ndanda)
    Obrey Chirwa                             (Yanga)
    Riffat Khamis                           (Ndanda)
    Victor Hangaya                         (Prisons)
    Mbaraka Yusuf                 (Kagera Sugar)
    Rafael Daud                        (Mbeya City)
    Venance Joseph                 (African Lyon)
4-Peter Mapunda                         (Majimaji)
    Kelvin Sabato                   (Stand United) 
    Laudit Mavugo                           (Simba)
    Marcel Boniventure                 (Majimaji)
    Boniface Maganga                       (Mbao)
    Deus Kaseke                              (Yanga)
    Shaaban Kisiga              (Ruvu Shooting)
    Mohammed Ibrahim 'MO'            (Simba)   
    Tito Okello                          (Mbeya City)
3- Hood Mayanja                   (African Lyon)
    Ibrahim Ajib                              (Simba)
    Abdalla Mfuko                         (Mwadui)
    Subianka Lambert                    (Prisons)
    Ditram Nchimbi                  (Mbeya City)
    Wazir Junior                      (Toto African)
    Issa Kanduru                 (Ruvu Shooting)
    Ally Nassor 'Ufudu'          (Kagera Sugar)
    Kelvin Friday                   (Mtibwa Sugar)
    Mfanyeje                                (Majimaji)
    Francisco Zukumbawira                (Azam)
    Shaaban Idd                               (Azam)
    Jamal Mnyate                             (Simba)
    Jamal Soud                       (Toto Africans)
2- Adam Kingwande              (Stand United)
    Samuel Kamuntu                    (JKT Ruvu)
    Vincent Philipo                             (Mbao)
    Mcha Khamis                               (Azam)
    Danny Mrwanda                (Kagera Sugar)
    Pastory Athanas                 (Stand United)
    Paul Nonga                                (Mwadui)
    Adeyum Saleh                    (Stand United)
    Jacob Massawe                   (Stand United)
    Fully Maganga                  (Ruvu Shooting)        
    Themi Felix                       (Kagera Sugar)
    Mudathir Yahya                             (Azam)
    Atupele Green                         (JKT Ruvu)
    Jerry Tegete                              (Mwadui)
    Jamal  Mwambeleko                      (Mbao)
    Vincent Barnabas              (Mtibwa Sugar)
    Adam Salamba                  (Stand United)
    Jaffar Salum                     (Mtibwa Sugar)

Diamond akikinukisha Gabon, Vita ya Afcon 2017 imeiva

Zimbabwe
Guinea Bissau

Senegal

Watetezi Ivory Coast
Taji linalowaniwa
Ghana
Uganda

LIBREVILLE, GABON
KUMEKUCHA. Kesho Jumamosi pazia la michuano ya Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (Afcon 2017), kusaka bingwa wa bara la Afrikalitafunguliwa.
Wenyeji wa michuano hiyo Gabon, itakata utepe kwa kuvaana na Guinea Bissau kabla kabla ya wababe Cameroon kukwaruzana na Burkina Faso katika pambano jingine tamu linalosubiriwa kwa hapo kwenye ufunguzi wa michauno hiyo.
Tanzania ambayo ina miaka karibu 37 inajifariji kwa kuwakilishwa na mwimbaji wa muziki wa kizazi kipya, Naseeb Abdul 'Diamond Platinumz' atakayepamba sherehe za ufunguzi sambamba na wakali wa Nigeria akiwamo Mr Flavor.
Tanzania ilishiriki mara ya kwanza na mwisho mwaka 1980 ilipofanyikia Nigeria, lakini pamoja na kukosekana kwao bado mashabiki wa soka watazitumia runinga zao kufuatilia michuano hiyo itakayofikia tamati Februari 5 wakati Bingwa atakapofahamika.
MICHARAZO MITUPU inakuletea orodha ya vikosi vitakavyochuana kwenye michuano hiyo pamoja na ratiba nzima ya Afcon 2017.

ALGERIA
Makipa: Malik Asselah (JS Kabylie), Rais M’Bolhi (Antalyaspor/TUR), Chemseddine Rahmani (Mouloudia Bejaia)
Mabeki: Mohamed Benyahia, Mohamed Meftah (both USM Alger), Hichem Belkaroui (Esperance/TUN), Mokhtar Belkhiter (Club Africain/TUN), Ramy Bensebaini (Rennes/FRA), Liassine Cadamuro (Servette/SUI), Faouzi Ghoulam (Napoli/ITA), Aissa Mandi (Real Betis/ESP), Djamel Mesbah (Crotone/ITA)
Viungo: Mehdi Abeid (Dijon/FRA), Nabil Bentaleb (Schalke/GER), Yacine Brahimi (Porto/POR), Rachid Ghezzal (Lyon/FRA), Adlene Guedioura (Watford/ENG), Riyad Mahrez (Leicester City/ENG), Saphir Taider (Bologna/ITA)
Mastraika: Baghdad Bounedjah (Al Sadd/QAT), Sofiane Hanni (Anderlecht/BEL), Islam Slimani (Leicester/ENG), El Arabi Hillel Soudani (Dinamo Zagreb/CRO)
Kocha: George Leekens (Ubelgiji)

BURKINA FASO
Makipa: Herve Koffi (ASEC/CIV), Moussa Germain Sanou (Beauvais/FRA), Aboubacar Sawadogo (Kadiogo)
Mabeki: Yacouba Coulibaly (Bobo), Issoufou Dayo (Berkane/MAR), Bakary Kone (Malaga/ESP), Souleymane Kouanda (ASEC/CIV), Patrick Malo (Smouha/EGY), Issouf Paro (Santos/RSA), Steeve Yago (Toulouse/FRA)
Viungo: Prejuce Nacoulma, Alain Traore (both Kayserispor/TUR),Cyrille Bayala (Sheriff Tiraspol/MDA), Adama Guira (Lens/FRA), Charles Kabore (Krasnodar/RUS, capt), Bakary Sare (Moreirense/POR), Blati Toure (Omonia Nicosia/CYP), Abdoul Razack Traore (Karabuspor/TUR), Bertrand Traore (Ajax Amsterdam/NED), Jonathan Zongo (Almeria/ESP)
Mastraika: Aristide Bance (ASEC/CIV), Banou Diawara (Smouha/EGY), Jonathan Pitroipa (Al Nasr/UAE)
Kocha: Paulo Duarte (Ureno)

CAMEROON
Makipa: Jules Goda (Ajaccio/FRA), Georges Mbokwe (Coton Sport), Fabrice Ondoa (Sevilla/ESP)
Mabeki: Fai Collins (Standard Liege/BEL), Mohamed Djeitei (Nastic Tarragone/ESP), Ernest Mabouka (Zilina/SVK), Michael Ngadeu Ngadjui (Slavia Prague/CZE), Jonathan Ngwem (Progresso Sambizanga/ANG), Nicolas Nkoulou (Lyon/FRA), Ambroise Oyongo (Impact Montreal/CAN), Adolphe Teikeu (Sochaux/FRA)
Viungo: Franck Boya (Apejes Academy), Arnaud Djoum (Hearts/SCO), Georges Mandjeck (Metz/FRA), Edgar Salli (Saint-Gallen/SUI), Sebastien Siani (Ostend/BEL)
Mastraika: Vincent Aboubakar (Besiktas/TUR), Christian Bassogog (Aalborg/DEN), Benjamin Moukandjo (Lorient/FRA), Clinton Njie (Marseille/FRA), Robert Ndip Tambe (Spartak Trnava/SVK), Karl Toko-Ekambi (Angers/FRA), Jacques Zoua (Kaiserslautern/GER)
Kocha: Hugo Broos (Ubelgiji)
 
DR CONGO
Makipa: Joel Kiassumbua (Wohlen/SUI), Nicaise Kudimbana (Antwerp/BEL), Ley Matampi (TP Mazembe)
Mabeki: Jordan Ikoko (Guingamp/FRA), Joyce Lomalisa (V Club), Chancel Mbemba (Newcastle/ENG), Issama Mpeko (Mazembe), Fabrice N'Sakala (Alanyaspor/TUR), Marcel Tisserand (Ingolstadt/GER), Gabriel Zakuani (Northampton/ENG, capt)
Viungo: Merveille Bope (Mazembe), Herve Kage (Kortrijk/BEL), Neeskens Kebano (Fulham/ENG), Jacques Maghoma(Birmingham/ENG), Paul-Jose M'Poku (Panathinaikos/GRE), Remy Mulumba (Ajaccio/FRA), Youssouf Mulumbu (Norwich/ENG)
Mastraika: Cedric Bakambu (Villarreal/ESP), Jeremy Bokila (Al Kharitiyat/QAT), Jonathan Bolingi (Mazembe), Jordan Botaka (Charlton/ENG), Dieumerci Mbokani (Hull City/ENG), Firmin Ndombe Mubele (Al Ahly/QAT)
Kocha: Florent Ibenge
EGYPT
Makipa: Sherif Ekramy (Al Ahly), Essam El Hadary (Wadi Degla, capt), Ahmed El Shennawy (Zamalek)
Mabeki: Ahmed Fathy, Ahmed Hegazy, Saad Samir (all Ahly), Ahmed Dwidar, Ali Gabr (both Zamalek), Ahmed Elmohamady (Hull City/ENG), Omar Gaber (Basel/SUI), Karim Hafez (Lens/FRA), Mohamed Abdel-Shafi (Ahly Jeddah/KSA)
Viungo: Tarek Hamed, Ibrahim Salah (both Zamalek), Abdallah El Said (Ahly), Mahmoud Hassan (Mouscron/BEL), Mohamed Elneny (Arsenal/ENG), Amr Warda (Panetolikos/GRE)
Mastraika: Ahmed Hassan (Braga/POR), Marwan Mohsen (Ahly), Mahmoud Abdel-Moneim (Ahly Jeddah/KSA), Mohamed Salah (Roma/ITA), Ramadan Sobhy (Stoke City/ENG)
Kocha: Hector Cuper (Argentina)

GABON
Makipa: Anthony Mfa Mezui (clubless), Yves Stephane Bitseki Moto (Mounana), Didier Ovono (Ostend/BEL)
Mabeki: Aaron Appindangoye (Laval/FRA), Bruno Ecuele Manga (Cardiff City/WAL), Franck Perrin Obambou (Stade Mandji), Johann Serge Obiang (Troyes/FRA), Benjamin Ze Ondo (Mosta/MAL), Lloyd Palun (Red Star/FRA), Andre Biyogho Poko (Karabukspor/TUR), Yoann Wachter (Sedan/FRA)
Viungo: Guelor Kanga Kaku (Red Star/SRB), Mario Lemina (Juventus/ITA), Levy Clement Madinda (Nastic Tarragona/ESP), Didier Ndong (Sunderland/ENG), Junior Serge Martinsson Ngouali (Brommapojkarna/SWE), Merlin Tandjigora (Meixian Hakka/CHN), Samson Mbingui (Raja Casablanca/MAR)
Mastraika: Serge Kevyn Aboue Angoue (Uniao Leiria/POR), Pierre-Emerick Aubameyang (Borussia Dortmund/GER, capt), Cedric Ondo Biyoghe (Mounana), Denis Athanase Bouanga (Tours/FRA), Malick Evouna (Tianjin Teda/CHN)
Kocha: Jose Antonio Camacho (Hispania)

GHANA
Makipa: Razak Braimah (Cordoba/ESP), Adam Kwarasey (Rosenborg/NOR), Richard Ofori (Wa All Stars)
Mabeki: Harrison Afful, Jonathan Mensah (both Columbus Crew/USA), Frank Acheampong (Anderlecht/BEL), Daniel Amartey Leicester City/ENG), John Boye (Sivasspor/TUR), Edwin Gyimah Orlando Pirates/RSA), Baba Rahman (Schalke/GER), Andy Yiadom Barnsley/ENG)
Viungo: Afriyie Acquah (Torino/ITA), Emmanuel Agyemang-Badu (Udinese/ITA), Christian Atsu (Newcastle/ENG), Ebenezer Ofori (AIK Stockholm/SWE), Thomas Partey (Atletico Madrid/ESP), Samuel Tetteh (Leifering/AUT), Mubarak Wakaso (Panathinaikos/GRE)
Mastraika: Ebenezer Assifuah (Sion/SUI), Andre Ayew (West Ham/ENG), Jordan Ayew (Aston Villa/ENG), Asamoah Gyan (Al Ahly/UAE, capt), Bernard Tekpetey (Schalke/GER)
Kocha: Avram Grant (Israeli)

GUINEA-BISSAU
Makipa: Rui Dabo (Cova Piedade/POR), Papa Mbaye (Aguadulce/ESP), Jonas Mendes (Salgueiros/POR)
Mabeki: Mamadu Cande (Tondela/POR), Eridson (Freamunde/POR), Emmanuel Mendy (Ceahlaul Piatra Neamt/ROU), Rudinilson Silva (Lechia Gdansk/POL), Agostinho Soares (Sporting Covilha/POR), Juary Soares (Mafra/POR)
Viungo: Tony Silva Brito, Toni Silva, Zezinho (all Levadiakos/GRE), Bocundji Ca (Paris FC/FRA, capt), Idrissa Camara (Avellino/ITA), Francisco Junior (Stromsgodset/NOR), Jean-Paul Mendy (Quevilly-Rouen/FRA), Piqueti (Sporting Braga/POR), Sana (Academico Viseu/POR), Naní Soares (Falgueiros/POR)
Mastraika: Amido Balde (Maritimo/POR), Abel Camara(Belenenses/POR), Joao Mario (Chaves/POR), Frederic Mendy (Ulsan Hyundai/KOR)
Kocha: Baciro Cande

IVORY COAST
Makipa: Sylvain Gbohouo (TP Mazembe/COD), Ali Badra Sangare (Tanda), Mande Sayouba (Stabaek/NOR)
Mabeki: Serge Aurier (PSG/FRA), Mamadou Bagayoko (Saint-Trond/BEL), Eric Bailly (Manchester Utd/ENG), Simon Deli (Slavia Prague/CZE), Wilfried Kanon (ADO Hague/NED), Lamine Kone (Sunderland/ENG), Adama Traore (Basel/SUI)
Viungo: Victorien Angban (Granada/ESP), Geoffrey Serey Die (Basel/SUI, capt), Cheick Doukoure (Metz/FRA), Franck Kessie (Atalanta Bergamo/ITA), Yao Serge N'Guessan (Nancy/FRA), Jean-Michaël Seri (Nice/FRA)
Mastraika: Wilfried Bony (Stoke City/ENG), Max-Alain Gradel (Bournemouth/ENG), Salomon Kalou (Hertha Berlin/GER), Jonathan Kodjia (Aston Villa/ENG), Nicolas Pepe (Angers/FRA), Giovanni Sio (Rennes/FRA), Wilfried Zaha (Crystal Palace/ENG)
Kocha: Michel Dussuyer (Ufaransa)

MALI
Makipa: Soumaila Diakite, Djigui Diarra (both Stade Malien), Oumar Sissoko (Orleans/FRA)
Mabeki: Mahamadou N'Diaye, Charles Traore (both Troyes/FRA), Ousmane Coulibaly (Panathinaikos/GRE), Salif Coulibaly (TP Mazembe/COD), Mohamed Konate (Berkane/MAR), Youssouf Kone Lille/FRA), Hamari Traore (Reims/FRA), Molla Wague Udinese/ITA)
Viungo: Yves Bissouma (Lille/FRA), Lassana Coulibaly (Bastia/FRA), Moussa Doumbia (Rostov/RUS), Mamoutou N'Diaye (Royal Antwerp/BEL), Samba Sow (Kayserispor/TUR), Yacouba Sylla (Montpellier/FRA, capt), Adama Traore (Monaco/FRA), Sambou Yatabare (Werder Bremen/GER)
Mastraika: Kalifa Coulibaly (Gent/BEL), Moussa Marega (Guimaraes/POR), Bakary Sako (Crystal Palace/ENG), Moustapha Yatabare (Karabukspor/TUR)
Kocha: Alain Giresse (Ufaransa)

MOROCCO
Makipa: Yassine Bounou (Girona/ESP), Yassine El Kharroubi (Lokomotiv Plovdiv/BUL), Munir Mohamedi (Numancia/ESP)
Mabeki: Amine Attouchi (Wydad Casablanca), Mehdi Benatia (Juventus/ITA, capt), Fouad Chafik (Dijon/FRA), Manuel Da Costa (Olympiacos/GRE), Nabil Dirar (Monaco/FRA), Hamza Mendyl (Lille/FRA)
Viungo: Karim El Ahmadi (Feyenoord/NED), Youssef Ait Bennasser (Nancy/FRA), Aziz Bouhaddouz (Saint-Pauli/GER), M’bark Boussoufa (Al Jazira/UAE), Mehdi Carcela (Granada/ESP), Fayçal Fajr (Deportivo Coruna/ESP), Omar El Kaddouri (Napoli/ITA), Mounir Obbadi (Lille/FRA), Romain Saiss (Wolves/ENG)
Mastraika: Rachid Alioui (Nimes/FRA), Youssef El Arabi (Lekhwiya/QAT), Khalid Boutaib (Strasbourg/FRA), Youssef Ennesyri (Malaga/ESP)
Kocha: Herve Renard (Ufaransa)

SENEGAL
Makipa: Abdoulaye Diallo (Caykur Rizespor/TUR), Khadim N'Diaye (Horoya/GUI), Pape Seydou N'Diaye (Niarry Tally)
Mabeki: Saliou Ciss (Valenciennes/FRA), Lamine Gassama (Alanyaspor/TUR), Kalidou Koulibaly (Napoli/ITA), Cheikh M'Bengue (Saint-Etienne/FRA), Kara Mbodj (Anderlecht/BEL), Zargo Toure (Lorient/FRA)
Viungo: Mohamed Diame (Newcastle/ENG), Papakouli Diop (Espanyol/ESP), Idrissa Gueye (Everton/ENG), Cheikhou Kouyate (West Ham/ENG, capt), Papa Alioune Ndiaye (Osmanlispor/TUR), Cheikh N'Doye (Angers/FRA), Henri Saivet (Saint-Etienne/FRA)
Mastraika: Keita Balde (Lazio/ITA), Famara Diedhiou (Angers/FRA), Mame Biram Diouf (Stoke/ENG), Moussa Konate (Sion/SUI), Sadio Mane (Liverpool/ENG), Ismaila Sarr (Metz/FRA), Moussa Sow (Fenerbahce/TUR)
Kocha: Aliou Cisse

TOGO
Makipa: Kossi Agassa (clubless), Cedric Mensah (Le Mans/FRA), Baba Tchagouni (Marmande/FRA)
Mabeki: Serge Akakpo (Trabzonspor/TUR), Vincent Bossou (Young Africans/TAN), Djene Dakonam (Saint-Trond/BEL), Maklibe Kouloun (Dyto), Gafar Mamah (Dacia/MDA), Sadate Ouro-Akoriko (Al Khaleej/KSA), Hakim Ouro-Sama (Port)
Viungo: Lalawele Atakora (Helsingborgs/SWE), Franco Atchou (Dyto), Floyd Ayite (Fulham/ENG), Ihlas Bebou (Fortuna Dusseldorf/GER), Matthieu Dossevi (Standard Liege/BEL), Henritse Eninful (Doxa/GER), Serge Gakpe (Genoa/ITA), Alaixys Romao (Olympiacos/GRE), Prince Segbefia (Goztepe/TUR)
Mastraika: Emmanuel Adebayor (clubless, capt), Komlan Agbeniadan (WAFA/GHA), Razak Boukari (Chateauroux/FRA), Kodjo Fo-Doh Laba(Berkane/MAR)
Kocha: Claude le Roy (Ufaransa)

TUNISIA
Makipa: Moez Ben Chrifia (Esperance), Rami Jeridi (Sfaxien), Aymen Mathlouthi (Etoile Sahel, capt)
Mabeki: Zied Boughattas, Hamdi Nagguez (both Etoile Sahel), Aymen Abdennour (Valencia/ESP), Chamseddine Dhaouadi (Esperance), Slimen Kchok (CA Bizertin), Ali Maaloul (Al-Ahly/EGY), Hamza Mathlouthi (Sfaxien), Mohamed Ali Yaakoubi (Caykur Rizespor/TUR), Syam Ben Youssef (Caen/FRA)
Viungo: Mohamed Amine Ben Amor, Hamza Lahmar (both Etoile Sahel), Larry Azouni (Nimes/FRA), Ahmed Khalil (Club Africain), Wahbi Khazri (Sunderland/ENG), Youssef Msakni (Lekhwiya/QAT), Ferjani Sassi (Esperance), Naim Sliti (Lille/FRA)
Mastraika: Ahmed Akaichi (Ittihad Jeddah/KSA), Saber Khalifa (Club Africain), Taha Yassine Khenissi (Esperance)
Kocha: Henryk Kasperczak (Poland)

UGANDA
Makipa: Salim Jamal (Al Merrikh/SUD), Robert Odongkara (Saint George/ETH), Denis Onyango (Mamelodi Sundowns/RSA)
Mabeki: Timothy Awany, Joseph Ochaya (both KCCA), Shafiq Batambuze (Tusker/KEN), Denis Iguma (Al Ahed/LIB), Isaac Isinde (clubless), Murushid Juuko (Simba/TAN), Nicholas Wadada (Vipers)
Viungo: Khalid Aucho (Baroka/RSA), Mike Azira (Colorado Rapids/USA), Geoffrey Kizito (Than Quang Ninh/VIE), William Kizito (Rio Ave/POR), Tony Mawejje (Throttur/ISL), Hassan Wasswa (Nijmeh/LIB),Moses Oloya (Hanoi T and T/VIE), Godfrey Walusimbi (Gor Mahia/KEN)
Mastraika: Geoffrey Massa (Baroka/RSA, capt), Farouk Miya (Standard Liege/BEL), Yunus Sentamu (Ilves/FIN), Geofrey Sserunkuma (KCCA), Muhammad Shaban (Onduparaka)
Kocha: Milutin Sredojevic (Serbia)

ZIMBABWE
Makipa: Donovan Bernard (How Mine), Takabva Mawaya (ZPC Kariba), Tatenda Mkuruva (Dynamos)
Mabeki: Teenage Hadebe, Lawrence Mhlanga (both Chicken Inn), Onismor Bhasera (SuperSport Utd/RSA), Bruce Kangwa (Azam/TAN), Oscar Machapa (V Club/COD), Elisha Muroiwa (Dynamos), Costa Nhamoinesu (Sparta Prague/CZE), Hardlife Zvirekwi (CAPS Utd)
Viungo: Kudakwashe Mahachi, Danny Phiri (both Golden Arrows/RSA), Khama Billiat (Mamelodi Sundowns/RSA), Willard Katsande (Kaizer Chiefs/RSA, capt), Marvelous Nakamba (Vitesse Arnhem/NED)
Mastraika: Tinotenda Kadewere (Djurgardens/SWE), Cuthbert Malajila (Wits/RSA), Nyasha Mushekwi (Dalian Yifang/CHN), Knowledge Musona (Ostend/BEL), Tendai Ndoro (Orlando Pirates/RSA), Evans Rusike (Maritzburg/RSA), Mathew Rusike (CS Sfaxien/TUN)
Kocha: Kallisto Pasuwa

Makundi yapo hivi:



Ratiba ipo hivi:
Jumamosi 14 Januari 2017


   
Gabon v Guinea-Bissau Stade d'Angondje 18:00
Burkina Faso v Cameroon Stade d'Angondje 21:00
Jumapili 15 Januari 2017
       
Algeria v Zimbabwe Stade de Franceville 18:00
Tunisia v Senegal Stade de Franceville 21:00
Jumatatu  16 Januari 2017
       
Cote d'Ivoire v Togo Stade d'Oyem 18:00
DR Congo v Morocco Stade de Franceville 21:00
Jumanne  17 Januari 2017
       
Ghana v Uganda Stade de Port Gentil 18:00
Mali v Egypt Stade de Port Gentil 21:00
Jumatano 18 Januari 2017
       
Gabon v Burkina Faso Stade d'Angondje 18:00
Cameroon v Guinea-Bissau Stade d'Angondje 21:00
Alhamis  19 Januari 2017
       
Algeria v Tunisia Stade de Franceville 18:00
Senegal v Zimbabwe Stade de Franceville 21:00
Ijumaa  20 Januari 2017
       
Cote d'Ivoire v DR Congo Stade d'Oyem 18:00
Morocco v Togo Stade d'Oyem 21:00
Jumamosi 21 Januari 2017
       
Ghana v Mali Stade de Port Gentil 18:00
Egypt v Uganda Stade de Port Gentil 21:00
Jumapili 22 Januari 2017
       
Guinea-Bissau v Burkina Faso Stade de Franceville 21:00
Cameroon v Gabon Stade d'Angondje 21:00
Jumatatu  23 Januari 2017
       
Senegal v Algeria Stade de Franceville 21:00
Zimbabwe v Tunisia Stade d'Angondje 21:00
Jumanne  24 Januari 2017
       
Togo v DR Congo Stade de Port Gentil 21:00
Morocco v Cote d'Ivoire Stade d'Oyem 21:00
Jumatano 25 Januari 2017
       
Egypt v Ghana Stade de Port Gentil 21:00
Uganda v Mali Stade d'Oyem 21:00





































































Barcelona, Real Madrid zatenganishwa

BAADA ya mechi za marudiano ya Kombe la Mfalme (Copa del Rey), droo ya Nane Bora ya michuano hiyo ya nchini Hispania imetoka, huku vigogo Barcelona na Real Madrid zikitenganishwa kwenye hatua hiyo.
Katika droo hiyo Real Sociedad itavaana na Barcelona, wakati Real Madrid wakipewa Celta Vigo wakianzia nyumbani, huku Alcorcon itamalizna na Alaves na Atletico Madrid itakwaruzana na Eibar.
Mechi hizo kwa mujibu wa ratiba zitaanza kuchezwa Januari 18-19 na marudiani zitachezwa kati ya Januari 25/26 kwa ajili ya kupata timu za kutinga nusu fainali.
Katika hatua hiyo ya Nane Bora ni klabu moja tu ya Ligi Daraja la Pili ya Alcorcon iliyopenya na zilizosalia zipo La Liga.

Ratiba kamili ipo hivi:

Real Sociedad   v Barcelona
Alcorcon           v Alaves
Atletico Madrid  v Eibar
Real Madrid      v Celta Vigo

Taifa Stars, Uganda The Cranes hapatoshi Afcon 2019

Kikosi chja Tanzania
Droo ya kuwania fainali za Afcon 2019
DROO ya kuwania fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika kwa mwaka 2019 zitakazofanyika nchini Cameroon imefanyika jana usiku na Tanzania kuwekwa kundi moja pamoja na Uganda, Cape Verde na Lesotho.
Tanzania ambayo haijashiriki fainali hizo tangu mwaka 1980 kama itakomaa katika maandalizi mazuri inaweza kusonga mbele kwani safari hii kundi lao sio tishio kama ilivyokuwa katika mbio za  kwenda Afcon 2017.
Katika mbio Tanzania ilipangwa na vigogo Misri, Nigeria na Chad kabla nchi hii haijajitoa kundini.
Katika droo hiyo Kenya pia itaanzia hatua ya makundi, ikiwa imepangwa Kundi F pamoja na Ghana, Ethiopia na Sierra Leone, wakati Rwanda ipo Kundi H pamoja na Ivory Coast, Guinea na Afrika ya Kati (CAR).
Mshindi wa kila kundi atafuzu moja kwa moja AFCON ya 2019, wakati timu nyingine tatu zitakazomaliza nafasi ya pili na wastani mzuri zaidi ya nyingine zitafuzu kama washindi wa pili bora.
Michuano hiyo itaanzia kwa hatua ya mchujo, Raundi ya Awali itakayohusisha timu za Comoro, Djibout, Madagascar, Mauritius, Sao Tome E Principe na Sudan Kusini.
Timu zitakazofuzu hapo zitaingia moja kwa moja kwenye makundi A, B na C kukamilisha idadi ya timu nne nne. Kundi Ab lina timu za Senegal, Equatorial Guinea na Sudan, B kuna wenyeji Cameroon, Morocco na Malawi na C kuna Mali, Gabon n Burundi.
Cameroon ikiongoza Kundi, mshindi wa pili atafuzu moja kwa moja na kama itashika nafasi ya tatu au ya nne, mshindi wa kwanza atafuzu moja kwa moja na mshindi wa pili atawania nafasi tatu za ziada za kufuzu kama mmoja wa washindi wa pili bora.
Hatua ya mchujo itachezwa kati ya Machi 20 na 28 wakati mechi za kwanza za makundi zitaanza Juni 5 na 13, za pili Machi 19 na 27 2018, za tatu Septemba 3 na 11, 2018 za nne Oktoba 8 na 16, 2018 na za tano Novemba 5 na 13, 2018.
Mbali za Afcon 2019 Tanzania pia itakuwa na kibarua cha kuwania fainali za Chan 2018 zitakazofanyika nchi ya Kenya.

Thursday, January 12, 2017

SIMBA, AZAM NI ZAIDI YA VITA KOMBE LA MAPINDUZI 2017

Kikosi cha Simba
Wababe wa Chamazi, Azam FC
Na Rahma White
HABARI ndio hiyo. Leo Alhamisi ndio kilele cha sherehe za Mapinduzi, ukiwa ni mwaka wa 53, lakini kazi bwana ipo kesho kwenye Uwanja wa Amaan.
Unajua nini? Wekundu wa Msimbazi, Simba kesho itavaana na Matajiri wa Azam kwenye pambano la fainali za michuano ya Kombe la Mapinduzi 2017.
Sasa kama ulikuwa haujui ni kwamba Simba ndio klabu iliyotwaa Kombe la Mapinduzi mara nyingi, ikifanya hivyo mara tatu tangu lianze kuchezwa kwa mfumo wa sasa. Pia Simba ndio klabu iliyotinga mara nyingi kwenye fainali  ambapo pambano lao la kesho dhidi ya Azam litakuwa ni la sita sita ikiiacha Mtibwa Sugar waliokuwa wakilingana nao ambayo msimu haikualikwa.
Vinara hao wa Ligi Kuu Bara kesho itavaana na Azam klabu inayofuata kwa kulibeba taji hilo mara nyingi nyuma ya Simba, ikilitwaa mara mbili tena ikiwa klabu pekee kuwahi kulitetea ikifanya hivyo mwaka 2012 na 2013.
Simba imefika hatua hiyo ya fainali za mwaka huu kwa kuitambia Yanga kwa mikwaju ya penalti 4-2 baada ya kumaliza dakika 90 la pambano lao bila milango ya timu hiyo kuguswa, huku Azam ikifika hatua hiyo kwa kuing'oa Taifa Jang'ombe kwa bao 1-0.
Azam ndio klabu ambayo mpaka inafika fainali wavu wake haujaguswa ikiweka rekodi, huku Simba ikifuata ikiruhusu bao moja tu.
Kwa mnasaba huo fainali ya kesho itakuwa tamu ile mbaya kwani, licha ya kila timu kusaka heshima ya kulibeba taji hilo, lakini pia zinataka kuonyesha nani mkali zaidi katika suala zima la kulinda lango lao.
Mchezo huo wa kesho una uhondo zaidi kwenye eneo la kiungo ambako klabu zote zinatambia mafundi walionao ambao wamezifanya kuwa kali katika kuzuia na kushambulia.
Makocha wa pande zote wamekuwa wakijinasibu timu zao kuibuka na ushindi, lakini kwa kulinganisha na rekodi zilizopo ni lazima Simba iwe makini mbele ya Azam ambao waliistaajabisha Yanga kwa kuipiga mabao 4-0.
Ingawa mpaka sasa kwenye michuano hiyo ya Mapinduzi, Azam imekuwa wanyonge wa Simba, lakini kwa namna walivyoizima Yanga ni wazi Simba isiende kichwa kichwa Uwanja wa Amaan kama wanataka kurejesha taji lao hilo walilolipoteza mwaka jana na kuliacha likibebwa na URA ya Uganda.
Kocha Msaidizi wa Simba, Jackson Mayanja amekiri pambano litakuwa gumu, lakini kubwa wanachotaka ni kurudi jijini Dar es Salaam na taji hilo, huku Idd Nassor 'Cheche' akiamini hakuna cha kuwazuia kubeba Kombe la mwaka huu.
Vikosi vya timu hizo vinatarajiwa kuwa hivi;
AZAM: Aishi Manula, Shomari Kapombe, Gadiel Michael, Yakub Mohammed, Aggrey Morris, Stephan Kingue, Salum Abubakar, Frank Domayo, John Bocco, Yahya Mohammed na Joseph Mahundi.
SIMBA:
Daniel Agyei, Janvier Bokungu, Mohammed Hussein, Abdi Banda, Method Mwanjali, Jonas Mkude, Shiza Kichuya, Mzamiru Yasin, Juma Liuzio, Mohammed Ibrahim na James Kotei.

Mabingwa wa Mapinduzi

2007-Yanga
2008-Simba
2009-Miembeni
2010-Mtibwa Sugar
2011-Simba
2012-Azam
2013-Azam
2014-KCCA
2015-Simba
2016-URA
2017-  ''

Utamu wa Ligi Kuu Bara umerudi tena

JKT Ruvu
Toto Africans
Ruvu Shooting
Na Rahim, Junior
ACHANA na pambano la kesho la fainali ya michuano ya Kombe la Mapinduzi,
itakayozikutanisha Simba na Azam kwenye Uwanja wa Amaan, Zanzibar, unaambiwa utamu wa Ligi Kuu Bara nao unarudi rasmi wikiendi hii.
Ligi hiyo iliyokuwa mapumziko ya wiki kama mbili hivi, inarudi kwa michezo itakayochezwa mfululizo kuanzia leo mpaka Jumatano.
Wapinzani wa jadi, maafande wa JKT Ruvu na Ruvu Shooting zinatarajiwa kumaliza ubishi katika pambano linalosubiriwa kwa hamu kwenye Uwanja wa Mabatini, ulioko Mlandizi mkoani Pwani.
Pambano hilo la kisasi linafanyika huku kila timu ikiwa katika hali tofauti, JKT Ruvu wakiwa hoi mkiani, huku wapinzani wao angalau wakipumua maeneo ya juu na wanatambia ushindi wa bao 1-0 iliyopata katika mechi yao ya kwanza.
Kwa mujibu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) ligi hiyo itaendelea Jumamosi kwa pambano jingine la 'derby' ya Mkoa wa Shinyanga kati ya Stand United na Mwadui  zitakazovaana kwenye Uwanja wa Kambarage mjini humo, huku kukiwa hakuna mbabe wa mechi ya awali.
Jumamosi pia kutakuwa na mtanange mwingine mkali wa Kagera Sugar itakayokuwa mwenyeji wa Ndanda ya Mtwara kwenye Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba.
Utamu utaendelea tena Jumapili kwa mchezo mmoja tu ambapo Mbao itaialika African Lyon ya Dar kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.
Kivumbi cha ligi hiyo inayoingoa raundi ya nne ya duru la pili, itaendelea tena Jumatatu kwa mchezo mmoja tu kati ya Prisons Mbeya itakayokuwa mgeni wa Toto Africans kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.
Michezo mitatu ambayo ilikuwa haijapangiwa tarehe hapo awali kwa alama ya TBA ikiwa na maana ya kutajwa baadaye (To Be Announced), tayari Bodi ya Ligi, chombo cha TFF, kinachosimamia na kuendesha ligi, imepanga tarehe.
Jumanne ya Januari 17, 2017, Yanga itakuwa ugenini mjini Songea kuvaana na Majimaji kwenye Uwanja wa Majimaji na siku inayofuata yaani Jumatano, Mtibwa Sugar itakayocheza na Simba kwenye Uwanja wa Jamhuri, Morogoro wakati Azam itakuwa mwenyeji wa Mbeya City Uwanja wa Azam Complex.
Mchezo huu wa Azam na Mbeya City umepangwa kuanza saa 1.00 usiku wakati michezo yote tajwa hapo juu itaanza saa 10.00 jioni lengo likiwa ni kutoa nafasi kwa mashabiki kushuhudia mechi nyingi kupitia Kituo cha runinga cha Azam.

Ratiba ya VPL imekaa hivi;
 
Jan 13, 2017   
JKT Ruvu v Ruvu Shooting

Jan 14, 2017Stand United v Mwadui
Kagera Sugar v Ndanda

Jan 15, 2017Mbao v African Lyon

Jan 16, 2017
Toto Africans v Prisons

Jan 17, 2017Majimaji v Yanga

Jan 18, 2017Mtibwa Sugar v Simba
Azam v Mbeya City
 

Zaha aanza mambo Ivory Coast ikiilipua Uganda x3

Straika Serge Aurier akishangilia bao la tatu la Tembo ya Afrika dhidi ya Uganda The Cranes
STRAIKA Wilfried Zaha akiichezea Ivory Coast kwa mara ya pili tangu alipoikana England, ameanza kuonyesha cheche zake baada ya kufunga bao lake la kwanza kwa Tembo hao wa Afrika wakiichapa Uganda kwa mabao 3-0.
Pambano hilo lilikuwa la kirafiki la kimataifa kujiandaa na michuano ya Afcon 2017 inayoanza wikiendi hii na lilichezwa nchini Ivory Coast na kushuhudia mpaka mapumziko hakuna timu iliyoona lango la mwenzake.
Zaha anayeichezea Crystal Palace wa England,  alifunga hilo katika dakika ya 58, ikiwa ni la pili kwa timu yake kwani dakika saba nyuma yake Jonathan Kodjia kuifungia Ivory Coast bao la kwanza.
Bao jingine la Serge Aurier katika dakika ya 72 na kuwazamisha wawakilishi wa ukanda wa Cecafa, Uganda ambayo inaends Gabon ikiwa ni mara ya kwanza tangu miaka 38 iliyopita waliposhiriki fainali hizo za Afrika.
Katika mechi nyingine ya kimataifa za kirafiki kwa maandalizi ya Afcon 2017 itakayochezwa Gabon kuanzia wikiendi hii, Senegal iliitambia Congo kwa mabao 2-0.

Liverpool majanga, yapigwa kidude na Southampton

Nathan Redmond akishangilia bao lake alililowatungua Liverpool usiku wa jana kwenyer Uwanja wa St Mary's katika mechi ya nusu fainali ya Kombe la Ligi (EFL)
LIVERPOOL imekwama aisee, baada ya usiku wa kuamkia leo kuchapwa bao 1-0 na Southampton katika mechi ya Nusu Fainali ya kwazna Kombe la Ligi.
Kwa ushindi huo, Southampton imejiweka katika nafasi nzuri ya kusonga mbele kama itafanya kweli kwenye mechi ya marudiano ugenini Januari 25.
Bao lililowazamisha vijana wa Jurgen Klopp liliekwa kimiani na Nathan Redmond katika dakika ya 20 katika mchezo huo mkali uliopigwa kwenye Uwanja wa St. Mary's mjini Southampton.
Kipigo hicho cha Liverpool kimekuja siku chache tangu walipong;anganiwa na timu ya daraja la chini ya Plymouth katika mechi tya raundi ya tatu ya Kombe la FA ambao watarudiana nao Januari 18.
Wikiendi hii Liverpool itakuwa na kibarua kigumu mbele ya Man United ambayo juzi iklipata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Hull City katika mechi ya kwanza ya nusu fainali ya Kombe la Ligi na kujiweka pazuri kutinga fainali.
Vijana wa Klopp watakuwa na wiki ngumu kwa kutakiwa kucheza mfululizo mara baada ya kuumana na Man United Jumapili hii.

Wenger kumbe hata huyu naye ulimkosa?

KOCHA Arsene Wenger amekuwa akihusishwa na kushindwa kunyakua nyota mbalimbali kutokana na kuwa mgumu kutoa fedha zinazohitajiwa na klabu husika. Orodha hiyo kwa sasa imeangukia kwa beki wa AS Roma. Wakala wa beki huyo Kostas Manolas amedai kuwa AS Roma ilikataa kitita cha euro milioni 40 kutoka Arsenal ili kumnasa nyota huyo msimu huu.
Arsenal walikuwa wakihusishwa na usajili wa beki huyo katika kipindi cha usajili wa kiangazi mwaka jana, lakini suala lake halikufanikiwa baada ya kumchukua Shkodran Mustafi kutoka Valencia badala yake. Wakala wa beki huyo amesisitiza kuwa kiasi cha fedha walichokitaka Roma ndio kilikuwa chanzo kikubwa cha kuvurugika kwa dili hilo. Hata hivyo wakala huyo aliendelea kudai kuwa Kostas anaweza kuondoka Juni mwaka huu ingawa ameondoa uwezekano wa kwenda China.

Schneiderlin huyooo Everton, Man United yakubali kumuuza

HAKUNA namna tena. Klabu ya Manchester United imekubali kumuuza kiungo wake Morgan Schneiderlin kwenda Everton kwa kitita cha pauni milioni 22. Nyota huyo wa kimataifa wa Ufaransa mwenye umri wa maiak 27, alisajiliwa United na Louis van Gaal kwa kitita cha pauni milioni 25 akitokea Southampton Julai mwaka 2015. Toka atue United amecheza mechi 47, lakini msimu huu amefanikiwa kucheza mechi nane pekee chini ya Kocha Jose Mourinho zikiwemo mechi tatu za Ligi Kuu.
Kwa upande mwingine Everton imekubali kumpeleka kwa mkopo mshambuliaji Oumar Niasse mwenye umri wa miaka 26 kwenda Hull City. Nyota huyo wa kimataifa wa Senegal alisajiliwa kwa kitita cha pauni milioni 13.5 kutoka Lokomotiv Moscow Februari mwaka jana, lakini hajafanikiwa kung’ara baada ya kucheza mechi saba pekee.

Ronaldo tisha mbaya, ateuliwa tuzo nyingine

Pichja tofauti zikimuonyesha Ronaldo na tuzo zake za hivi karibuni ikiwamo wa Ballon d'Or anayoibusu
WAMBILI kweli havai moja. Straika wa kimataifa wa Ureno na klabu ya Real Madrid, Cristiano Ronaldo ametajwa katika orodha nyingine ya watakaogombea tuzo ya Mwanamichezo Bora wa Mwaka ya Laureus. Nyota huyo amekuwa na miezi 12 yenye mafanikio baada ya kushinda taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya na Euro 2016. Kiwango kikubwa alichoonyesha kimemfanya kutwaa tuzo za Ballon d’Or na tuzo ya mchezaji bora wa mwaka wa FIFA. Tuzo ya Mwanamichezo Bora wa mwaka hupigiwa kura na wanahabari na Ronaldo atakuwa akishindana na nyota wengine wakiwemo nyota wa mpira wa kikapu Marekani Steph Curry na Lebrone. Pia watakuwepo mwanariadha nyota wa mbio fupi wa Jamaica Usain Bolt, mwanaridha nyota wa Uingereza Sir Mo Farah na kinara wa mchezo wa tenisi duniani Sir Andy Murray. Kama akitwaa tuzo hiyo Ronaldo atakuwa mwanasoka wa kwanza kufanya hivyo toka kuanzishwa kwa tuzo hizo mwaka 2000. Mshindi wa tuzo hiyo anatarajiwa kutangazwa Februari 14 mwaka huu jijini Monaco.

Azam FC yapata mrithi wa Guardiola wao, anatokea Ronania

Na Rahma Junior
KLABU Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, mchana huu imemtangaza, Aristica Cioaba, kuwa Kocha Mkuu wa kikosi hicho.
Cioaba, 45, anakuja Azam FC kurithi mikoba ya Mhispania Zeben Hernandez, aliyesitishiwa mkataba pamoja na benchi lake zima la ufundi.
Kocha huyo atasaidiana na makocha wazawa, Idd Nassor Cheche na Kocha wa Makipa Idd Abubakar, walioiongoza timu hiyo kutinga hatua ya nusu fainali ya michuano ya Kombe la Mapinduzi, ambapo saa 10.15 jioni ya leo itasaka fainali kwa kukipiga na Taifa ya Jang’ombe.
Akizungumza na mtandao rasmi wa klabu www.azamfc.co.tz Ofisa Mtendaji Mkuu wa timu hiyo, Saad Kawemba, tayari wamefanikiwa kumpata kocha huyo na wameingia naye mkataba wa muda wa miezi sita wenye kipengele cha kuongezwa.
Alisema Cioaba ana uzoefu mkubwa wa soka la Afrika na ataiongoza Azam FC kwa kipindi hiki hadi mwishoni mwa mwa msimu, ambapo baada ya kuisha watakaa tena mezani kufanya tathimini ya mafanikio yake na wapi wanaweza kuendelea kutokana na kazi iliyofanyika.
“Bodi ya Wakurugenzi ya Azam FC inapenda wadau wote wa mpira na wapenzi na mashabiki wa Azam kwamba klabu imempata mwalimu, ambaye ndiye ataiongoza klabu kwa kipindi hiki hadi mwishoni mwa msimu.
“Kwa hiyo kwa mashabiki wetu maana yake ni kwamba tukiingia kwenye mechi inayofuata ya ligi, kocha atakuwa ameanza kazi na Cheche (Idd Nassor) atakuwa msaidizi wake na benchi lake zima alilokuwa nalo hivi sasa litaendelea,” alisema.
Kawemba aliongeza kuwa hivi sasa kocha huyo atakuwa na kikosi visiwani Zanzibar kufuatilia mwenendo wa timu ulivyo na ataendelea kutoa ushauri panapohitajika na ataanza rasmi kukaa kwenye benchi mpaka pale vibali vyake vya kufanya kazi nchini vitakapokamilika.
“Taratibu hizo zitakwenda kwa mujibu wa sheria za nchi, ambapo tutaziheshimu na kuona ya kwamba tutazifanya kwa haraka zaidi ili mwalimu aweze kupata kibali cha kufanya kazi hapa nchini, kwa hayo machache tunawaomba mashabiki wetu wawe watulivu wampe sapoti kocha na wadau wote wa mpira waone ya kwamba tumefanya jambo la kheri,” alisema.
Kauli ya kwanza ya Cioaba
Kwa upande wake Cioaba, alisema kuwa anafuraha kubwa leo hii kusaini mkataba wa kuifundisha timu hiyo huku akiahidi kazi nzuri na kuifanya timu hiyo kuwa bora.
“Najua Azam FC hapa Tanzania ni moja ya timu kubwa yenye historia huko nyuma, napenda kuushukuru uongozi kwa kuniamini na kunipa nafasi kuja kufundisha soka kwenye nchi hii, kwa mashabiki napenda kuwaambia kuwa nalijua soka la Afrika, nimewahi kufundisha Ghana na kupata matokeo mazuri.
“Kuhusu wakati ujao, nina furaha sana kuhusu uongozi walipoongea na mimi wakati tunaweka mipango ya timu ya hapo baadaye na hili ni jambo zuri kwa kocha, kitaaluma nawaahidi mashabiki na watu wote wanaoipenda Azam FC, niko hapa kuwapa mambo mazuri katika kazi yangu kwenye klabu,” alisema.
Msimu uliopita, Cioaba aliiongoza Aduana Stars ya Ghana kushika nafasi ya pili kwenye Ligi Kuu ya Ghana, ambapo anafahamiana kwa ukaribu na nyota wawili wa Azam FC, Yakubu Mohammed na Yahaya Mohammed, waliosajiliwa kutoka timu hiyo katika usajili wa dirisha dogo.
Mbali na kufundisha soka nchini Ghana pia amewahi kufanya kazi kwenye miamba ya Morocco, Raja Casablanca, Al Masry ya Misri na katika nchi za Romania, Kuwait, Oman na Jordan.

Sunday, January 8, 2017

SIMBA NA YANGA HAKUNA JINSI TENA

Simba wakishangilia katika mechi zao za hivi karibuni









Picha zikionyesha kabla ya pambanio la Simba na Jang'ombe Boys lililochezwa jioni ya leo kwenye Uwanja wa Amaan.
USIYEMPENDA kaja. Simba imepata ushindi wa mabao 2-0 na kuifuata Yanga kwenye pambano la nusu fainali ya Kombe la Mapinduzi katika mechi itakayopigwa usiku wa Jumanne.
Mabao mawili ya kila kipindi kutoka kwa Laudit Mavugo yametosha kuzikutanisha timu hiyo ambazo zina upinzani wa jadi katika soka la Tanzania.
Mavugo alifunga bao la kuongoza dakika ya 11 kabla ya kuongeza jingine tamu katika kipindi cha pili dakika ya 54 na kuifanya Simba kubaki kileleni mwa msimamo wa Kundi A ikiwa na pointi 10, pointi ambazo haziwezi kufikiwa na klabu yoyote nyingine iliyopo kwenye kundi hilo.
Watetezi URA ya Uganda usiku itavaana na Taifa Jang'ombe ili kuunga na Simba katika nusu fainali ambapo itakayofuzu itavaana na vinara wa Kundi B, Azam iliyoikandika usiku wa jana Yanga kwa mabao 4-0.
Katika pambano hilo lililoisha hivi punde, Simba iliwazidi ujanja wapinzani wao, licha ya Boys kujitutumua kutaka kuizuia Simba isisonge mbele.
Simba na Yanga zinakutana kwenye pambano la Kombe la Mapinduzi kwa mara ya kwanza tangu walipovaana kwenye fainali ya mwaka 2011 ambapo Yanga ilikandamizwa mabao 2-0.

Lakini hilo litakuwa pambano la nne la watani hao wa jadi kukutana visiwani Zanzibar tangu mwaka 1975 walipokutana kwa mara ya kwanza kwenye Kombe la Kagame na Yanga kushinda na kuvaana tena 1992 na Simba kushinda kwa penalti.
Washindi wa mechi za nusu fainali hizo mbili zitakazochezwa Jumanne zitavaana Ijumaa ijayo kwenye pambano la fainali ya michuano hiyo ya 11 tangu mfumo wa sasa uanze kutumika mwaka 2007 na Yanga kuwa bingwa wa awali.
Simba ndio timu iliyotwaa taji la michuano hiyo mara nyingi, ikifanya hivyo mara tatu na kufuatiwa na Azam iliyobeba mara mbili, huku Yanga, Mtibwa Sugar, Miembeni, KCCA na URA zote za Uganda zikitwaa mara moja moja.

West Bromwich Albion yamkomalia straika wa Napoli

KLABU ya West Brom ipo kwenye mazungumzo ya kutaka kumnyakua straika wa Napoli, Manolo Gabbiadini.
Kwa mujibu wa duru za kimichezo nchini Uingereza zinasema kuwa Albion inazungumza na klabu ya Napioli inayoshiriki Ligi Kuu ya Italia, Serie A ili kumsajili Gabbiadini.
Straika huyo mwenye miaka 25 pia ananyatiwa na klabu za Wolfsburg, Southampton, huku Everton na Stoke City nazi zikitajwa kwenye mbio hizo.
Wolfsburg walikaribia kumnasa Gabbiadini kwa mkono kwa kiasi cha Puni 15 milioni usajili uliopita na Albioni walijaribu kumnasa Agosti mwaka uliopita na sasa inakula sahani moja kumnasa jumla kwenye usajili huu wa Januari.
Gabbiadini aliifungia timu yake bao dhidi ya Sampdoria na kuisaidia kutoka nyuma na kushinda mabao 2-1.

Mavugo atupia jingine kuipeleka Simba nusu fainali

MRUNDI Laudit Mavugo ameendelea kuwafunga mdomo waliokuwa wakimponda baada ya kutupia tena bao la pili dakika ya 54 na kuifanya timu yake ya Simba kuwa mbele kwa mabao 2-0 dhidi ya  Jang'ombe Boys.
Kama matokeo yatabaki kama yalivyo kwa Simba kushinda mchezo huo haitakuwa na kingine ila kuvaana na Yanga walioshika nafasi ya pili katika kundi B la michuano ya Kombe la Mapinduzi 2017.

Kibarua cha Bilic West Ham shakani

KAZI anayo. Kibarua cha Meneja wa West Ham United, Slaven Bilic kipo hatarini, ikielezwa ana mechi mbili tu kabla ya kufutwa kazi.
Kwa mujibu wa The Sun, limefichua kuwa kibarua cha Bilic kipo kwenye hatihati kama atashindwa kufanya vema kwenye mechi zijazo za timu hiyo.
Mechi hizo zinahusisha pambano dhidi ya Crystal Palace na Middlesbrough hii ikiwa ni baada ya kupokea kichapo cha aibu cha mabao 5-0 juzi Ijumaa kutoka kwa Manchester City katika pambano la Kombe la FA.
Ushindi wa mechi tatu katika mwezi uliopita, West Ham ilijikwamua toka janga la kushuka daraja, lakini bado imekuwa na muelekeo mbaya kitu kinachowatisha mabosi wa klabu hiyo.

Simba v Jang'ombe Boys sasa ni mapumziko

PAMBANO la Simba na Jang'ombe Boys kwa sasa ni mapumziko kwenye Uwanja wa Amaan, Zanzibar, huku Wekundu hao wa Msimbazi wakiwa mbele kwa bao 1-0.
Bao lililofungwa na Laudit Mavugo na kuifanya Simba iwe kwenye nafasi kubwa ya kuvaana na Yanga katika mechi ya nusu fainali kama matokeo yatabaki yalivyo, kwani Mnyama atamaliza nafasi ya kwanza na pointi 10.

Mavugo atupia kambani baada ya miezi miwili

SEMENI tena! Ndivyo unavyoweza kusema baada ya straika wa Simba, Laudit Mavugo kufunga bao lake la kwanza tangu alipofanya hivyo mara ya mwisho Oktoba mwaka jana katika mechi ya Ligi Kuu Bara.
Mavugo amefunga bao hilo dakika 11 ya pambano lao la Kundi A ya michuano ya Kombe la Mapinduzi unaoendelea kwenye Uwanja wa Amaan, Zanzibar dhidi ya Jang'ombe Boys kuwania tiketi ya kucheza nusu fainali ya michuano hiyo.
Kwa sasa pambano linakaribia kwenda mapumziko na Simba inaongoza bao 1-0. MICHARAZO itakuwa inakuletea dondoo kadri mechi inavyoendelea visiwani humo.

Obi Mikel kasepa zake Uchina kiroho safi

HABARI ndio hiyo bwana! Nyota wa Chelsea John Obi Mikel ametangaza kupitia posti kwenye mitandao ya Kijamii kuwa anaihama klabu hiyo na kujiunga na klabu ya Ligi Kuu ya China, Tianjin TEDA.
Mnigeria huyo mwenye miaka 29, alijiunga na Chelsea akiwa na kinda la miaka 19 akitokea klabu ya Lyn  ya Norway mwaka 2006 na kucheza Mechi 374.
Katika msimu huu wa Ligi Kuu ya England, chini ya Kocha Antonio Conte, Mikel hajacheza hata mechi moja na inaelezwa hiyo ni sababu ya kuchukua maamuzi ya kwenda China ambayo imekuwa ikimwaga fedha lukuki kwa mastaa ili kushawishi kutua kwenye ligi yao.
Akiwa na Chelsea, Mikel alitwaa mataji 11 yakiwemo mawili ya Ligi Kuu England na moja la L:igi ya Mabingwa Ulaya.
Akiaga, Mikel alitoa shukran kwa Mmiliki wa Chelsea Roman Abramovich pamoja na mashabiki wa Klabu hiyo, huku bilionea huyo akimtakia kila la heri.

Yanga yakumbana na dhahama mbele ya Azam

Sure Boy aliyekuwa mpishi katika maangamizi ya Yanga jana mjini Zanzibar
Na Rahma White, Z'Bar
BADO hawaamini. Yanga na kikosi chake bora. Ikiwa na Kocha Mzambia George Lwandamina usiku wa jana wamepigwa mabao 4-0 na Azam katika mechi ya kufungia dimba ya Kundi B kwenye michuano ya Kombe la Mapinduzi 2017.
Sio makocha tu, bali hata mashabiki wa klabu hiyo mpaka sasa hawaamini kile kilichowakuta kwa sababu waliamini Azam walikuwa wepesi kwao.
Hata hivyo kwa kuwa soka ni mchezo wenye matokeo ya kikatili, Yanga imelala bao 4-0 na kuweka rekodi ya kupokea kipigo kikubwa tangu mwaka 2012 walipotunguliwa na watani zao wa Simba katika mechi ya Ligi Kuu 2011-2012.
Katika pambano hilo Yanga ilikandikwa mabao 5-0, lakini Azam jana usiku ilisamehe moja na kufunga mabao hayo ikiwa ni mengi kuwahi kuifunga timu kongwe nchini Simba na Yanga na kumaliza kama kinara wa kundi lao.
Mabao ya John Bocco 'Adebayor' lililokuwa la 14 kwake kuitungua Yanga, na mengine ya Waghana Yahya Mohammed na Enoch Agyei-Atta na lile la Joseph Mahundi yalityosha kuinyoosha Yanga iliyocheza ovyo eneo lake la ulinzi.
Mabadiliko ya kutolewa kwa Haji Mwinyi na kuingizwa Geofrey Mwashiuya yaliigharimu Yanga ambayo sasa inasubiri kujua itaumana na Simba au klabu gani katika mechi ya nusu fainali Jumanne ijayo.
Simba itakabiliana na Jang'ombe Boys katika mechi ya kukamilisha ratiba, huku URA na Taifa Jang'ombe zikipapetuana kusaka tiketi za kucheza nusu fainali. Mechi hizo zinapigwa Jumapili hii kwenye Uwanja wa Amaan.
Baadhi ya wachezaji wa Yanga wamesema hawajui mpaka sasa kilichoikuta timu yao kwani walijiandaa kuvaana na Azam, ingawa wamekiri kucheza mfululizo bila mapumziko ni tatizo la kupoteza umakini usiku wa jana.