STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, March 8, 2014

Arsenal yatinga Semi Fainali ya FA, yaifumua Everton 4-1

Arteta kifungwa mkwaju wake wa penati

Arsenal v Everton
Lukaku akishangilia bao lake ambalo halikuisaidia Everton kwa Arsenal leo
Giroud scores
Mtokea benchi Oliver Giroud akiwatoka washindi na kufunga moja ya mabao yake mawili leo

KIUNGO Mesut Ozil amefunga bao boa na kusaidia jingine lililtumbulizwa kimiani na Oliver Giroud wakati Arsenal ikiifumua Everton kwa mabao 4-1 na kutinga hatua ya Nusu Fainali ya Kombe la FA kwa mara ya kwanza tangu mwaka 2009.
Ozil ambaye amekuwa na wakati mgumu kwa mashabiki wa Arsenal tangu alipokosa mechi ya Arsenal dhidi ya Liverpool walipofungwa mabao 5-1 na kuja kukosa penati kwenye Ligi ya mabingwa Ulaya dhidi ya Bayern, alionyeha kiwango cha juu katika mchezo huo uliochezwa uwanja wa Emirates.
Kiungo huyo wa Ujerumani alifunga bao la kuongoza dakika ya 7 kwa pasi ya Santi Cazorla kabla ya Romelu Lukaku kuisawazishia Everton bao dakika ya 32 na kufanya timu hizo ziende mapumziko zikiwa sare ya 1-1.
Kipindi cha pili kilianza kwa Arsenal kujiongezea bao la pili kwa amkwaju wa penati  dakika ya 68 iliyofungwa na Mikel Arteta kabla ya mtokea benchi Giroud kufunga mengine mawili dakika za saba za mwisho za mchezo huo.
Mchezaji huyo alifunga bao lake la kwanza na la tatu katika mchezo huo dakika ya 83 akimalizia kazi ya Bacary Sagna na dakika mbili baadaye kuongeza jingine baada ya kazi nzuri ya Ozil na kuiofanya Arsenal kuibuka kidedea kwa maba0 4-1 na kutina Nusu Fainali ya michuano ya Kombe hilo.

Michezo mingine ya Robo Fainali ya michuano hiyo itachezwa kesho kwa mechi itakayozikutanisha Sheffield United dhidi ya Charlton Athletic mechi itakayochezwa mapema kabla ya Hull City kuvaana na Sunderland na Manchester City usiku kuvaana na Wigan Athletic.

Manchester Utd yaifumua West Brom 3-0

http://news.bbcimg.co.uk/media/images/73455000/jpg/_73455370_73455369.jpg
Wayne Rooney akifunga bao la pili la Manchester Utd leo
Man Utd defender Phil Jones heads his side into the lead at West Brom
Jones akifunga bao la kwanza la Mashetani Wekundu kwa kichwa

MASHETANI wekundu wakiwa ugenini muda mfupi uliopita imepata ushindi mnono wa mabao 3-0 dhidi ya West Bromwich kiatika mechi ya Ligi Kuu ya England na kuifanya timu hiyo kuiengua Everton kwenye nafasi ya sita ikiifupumua Tottenham Hotspur inayoshuka dimbani baadaye dhidi ya Chelsea.
Mabao ya Phil Jones la dakika ya 34 kwa pasi ya Robin van Persie  lililidu kipindi cha kwanza na mengine ya kipindi cha pili kupitia wa Wayne Rooney dakika ya 65 na Danny Welbeck  kwa pasi ya Rooney dakika ya 82 ilitosha kuifanya Manchester United kuibuka na ushindi wa mabao 3-0 na kufikisha pointi 48 sawa na Everton, lakini wakitangulia mbele kwa uwiano wa mabo ya kufunga na kufungwa.
Ushindi huo wa ugenini umekuwa afueni kwa kocha David Moyes kuelekea kwenye mbio za kupata nafasi ya ushiriki wa Ligi ya Mabingwa Ulaya mwakani baada ya mbio za ubingwa kuwa mbali kwao kwa sasa na kuelekea kutemeshwa taji lake.

Tambwe, Mgosi walimwa faini, kisa...!

Tambwe wa Simba
Mgosi
STRIKA nyota wa Simba, Amissi Tambwe amepigwa faini ya Sh 500,000 kwa kuonyesha ishara ya matusi wakati akishangilia bao lake.

Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), limesema Tambwe alionyesha alama ya matusi kutumia kidole chake wakati anashangilia.

Tambwe alifanya hivyo baada ya kuifungia Simba bao wakati ilipoivaa Mbeya City mjini Mbeya.

Mechi hiyo ilimalizika kwa sare ya bao 1-1, Tambwe raia wa Burundi akiwa ni shujaa wa Simba.

Hadi sasa Mrundi huyo ana mabao 17 akiwa kileleni kwa upachikaji mabao.

Naye, mshambuliaji wa Mtibwa Sugar, Musa Mgosi amepigwa faini ya sh. 500,000 kwa kosa la kupiga uwanjani kwenye mechi dhidi ya Ashanti United ambapo vilevile atakosa mechi tatu za ligi. Coastal Union imepigwa faini ya sh. 500,000 kwa washabiki wake kumrushia chupa za maji kipa wa Mbeya City.

IDFA yaitakia kila la heri Yanga kesho Misri

Yanga yenye kibarua kizito kesho mjini Alexandria
UONGOZI wa Chama cha Sokla Wilaya ya Ilala (IDFA) umeitakia kila la heri na kuwaomba watanzania kuiombea dua njema wawakilishi pekee wa michuano ya kimataifa, Yanga katika mchezo wao wa kesho dhidi ya Al Ahly ya Misri.
Yanga wataumana na wenyeji wao katika mchezo wa marudiano wa Ligi ya Mabingwa Afrika ambayo Al Ahly ndiyo watetezi wake, ili kuamua hatma ya  kuvuka hatua ya 32 Bora kutinga 16 Bora ya michuano hiyo mikubwa barani Afrika kwa ngazi ya klabu, mechi ikichezwa mji wa Alexandria badala ya Cairo.
Kwa kutambua Yanga ina kibarua kizito mbele ya Ahly hiyo kesho, uongozi wa IDFA ambao ni walezi wa klabu za Ilala ikiwamo Simba na Yanga, wamewaomba watanzania kuiombea dua njema timu hiyo na wao wenyewe (IDFA)  wakisema wanaitakia kila la heri kuweza kuwang'oa Wamisri.
Katibu Mkuu wa chama hicho, Daud Kanuti aliiambia MICHARAZO kuwa, IDFA ipo katika maombi kuiombea Yanga ifanye vyema na kuendelea kupeperusha bendera ya taifa na kuwaomba wadau wengine wa soka bila kujali itikadi zao kuwaombea dua njema wawakilishi hao wavuke hatua hiyo.
Kanuti alisema kufanya vyema kwa Yanga katika mechi hiyo na michuano hiyo ya Mabingwa, ni sifa kwa Tanzania na kuongeza, anaamini wachezaji wa Yanga wakicheza 'jihad' na tahadhari kubwa dhidi ya wapinzani wao wanaweza kurejea kilichofanywa na Simba.
Kanuti alisema anaamini wachezaji  wameandaliwa kisaikolojia ili kuhimili vitimbi wanavyoweza kukutana navyo Misri kama ilivyo kawaida ya mechi za timu za kiarabu wanapokuwa uwanja wa nyumbani.
"IDFA tunaitakia kila la heri na kuiombea dua njema ili ifanye vyema kwenye mechi yake ya Jumapili, chama tumefurahishwa na ilichokifanya katika mchezo wa kwanza na tunaamini watarejea tena ugenini," alisema.
"Wana nafasi ya kurejea ilichofanywa na watani zao walipoing'oa Zamalek katika ardhi yao mwaka 2003, ila ni muhimu wachezaji wakaandaliwa kupambana na kuweka akili zao katika pambano hilo ili kuivusha Yanga katika hatua hiyo," aliongeza Kanuni.
Kanuti alisema IDFA inatambua mchezo huo wa kesho utakuwa mgumu kwa vile Al Ahly itakuwa nyumbani na rekodi zinaonyesha timu za kiarabu huwa wagumu kufungwa kwao, lakini Yanga ikipambana itawaondosha watetezi hao kama ilivyofanya Simba kwa Zamalek mwaka 2003.
Katika mwaka huo Simba ilishinda nyumbani bao 1-0 dhidi ya Zamalek pia ya Misri waliokuwa watetezi wa Ligi ya Mabingwa mwaka huo kisha kwenda kukubali kipigo kama hicho ugenini mjini Cairo na kupigiana penati na Simba kuibuka kidedea kuingia hatua ya makundi.
Iwapo Yanga itafanikiwa kuing'oa Ahly huenda ikakutana kwenye raundi inayofuata kati ya timu ya Berekum Chelsea ya Ghana au Ahly Benghazi ya Libya ambazo zilitoka sare ya 1-1 katika mechi yao ya awali na zinatarajiwa kurudiana leo.

Ushirikina waiponza Simba, TFF yakunjua kucha

Kikosi cha Simba na kocha wao, Logarusic (kulia waliosimama)
BODI ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) imeipiga faini ya jumla ya sh. milioni moja klabu ya Simba kutokana na makosa mbalimbali ikiwemo vitendo vinavyoashiria ushirikina uwanjani.

Simba ilifanya vitendo hivyo katika mechi yake dhidi ya Mbeya City ambapo imepigwa faini ya sh. 500,000. Pia imepigwa faini nyingine ya sh. 500,000 kwa makocha wake Loga, Selemani Matola na Idd Pazi kuingia uwanjani na kumzonga mwamuzi kwenye mechi hiyo.

Mbeya City imepigwa faini ya sh. 300,000 kwa washabiki wake kuingia uwanjani kwenye mechi dhidi ya Kagera Sugar iliyochezwa mjini Bukoba. Klabu za Yanga na Coastal Union zimepigwa faini ya sh. 500,000 kila moja kwa washabiki wao kurusha chupa za maji uwanjani wakati timu hizo zilipopambana jijini Tanga.

Kiungo wa Mtibwa Sugar, Shabani Nditi amepigwa faini ya sh. 500,000 kwa kumpiga mchezaji wa Simba, wakati Salvatory Ntebe pia wa Mtibwa Sugar amepigwa faini ya sh. 500,000 kwa kumtukana refa kwenye mechi dhidi ya Mbeya City.

Nayo JKT Ruvu imepigwa faini ya sh. 300,000 kwa kuchelewa kufika uwanjani kwenye mechi dhidi ya Simba iliyochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Vilevile wamiliki wa Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga wameandikiwa barua ya kufanya marekebisho ya vyumba vya wachezaji, kwa vile havina hewa ya kutosha.

Kwa upande wa Ligi Daraja la Kwanza (FDL) klabu zilizopigwa faini kutokana na makosa mbalimbali ni Friends Rangers (sh. 200,000), Lipuli (sh. 200,000), Majimaji (sh. 400,000), Polisi Morogoro (sh. 400,000) na Transit Camp (sh. 200,000).

Kocha Msaidizi wa Polisi Morogoro, John Tamba atapelekwa kwenye Kamati ya Maadili kutokana na vitendo visivyo vya kimaadili katika mechi dhidi ya Burkina Faso.

Kiongozi wa Lipuli, Hamis Kiemba na wachezaji Boniface Sawaka, George Enock na Green Paul watapelekwa katika Kamati ya Nidhamu kutokana na utovu wa nidhamu waliofanya kwenye mechi dhidi ya Kimondo.

Naye mchezaji Sangalau Nyamoka wa JKT Kanembwa aliyelalamikiwa uhalali wake na Polisi Tabora suala lake linapelekwa Kamati ya Nidhamu.

Huyu ndiye kocha mpya wa Taifa Stars


Na Mahmoud Zubeiry, Dar es Salaam
KOCHA mpya wa timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars ni Martinus Ignatius ‘Mart’ Nooij ambaye anatarajiwa kutambulishwa rasmi Machi 24 mwaka huu na Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Jamal Emil Malinzi.
Tangu TFF kusema inatafuta kocha mpya atakayerithi mikoba ya Mdenmark, Kim Poulsen, BIN ZUBEIRY imekuwa ikifuatilia kwa undani mwalimu mpya wa Stars atakuwa nani na sasa inaibuka na jibu ni Mart Nooij.
Tayari Nooij ambaye kwa sasa ni kocha wa St George ya Ethiopia amekwishasaini Mkataba wa miaka miwili na TFF na atakuja nchini mwishoni mwa mwezi huu.
Atatutoa?; Kocha mpya wa Taifa Stars Mart Nooij anatarajiwa kutua nchini mwishoni mwa mwezi huu

Ulikuwa mchakato makini, uliohusisha wataalamu na washauri wa kimataifa juu ya masuala ya ufundi ya soka ambao umefanikisha kupatikana mwalimu huyo wa Kiholanzi aliyezaliwa Julai 3, mwaka 1954 mjini Beverwijk, Uholanzi.
Nooij amewahi kuwa mwalimu maalum katika programu za maendeleo ya soka katika Chama cha Soka Uholanzi (DFA) na pia amewahi kufundisha timu ya EVC 1913 ya Marekani na baadaye Kazakhstan.
Alikuwa kocha wa timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 20 ya Burkina Faso katika Fainali za Kombe la Dunia mwaka 2003 na mwaka 2004 alikuwa kocha wa muda wa klabu ya FC Volendam ya Uholanzi.
Mwaka 2007 aliteuliwa kuwa kocha wa Msumbiji na akaiwezesha kufuzu kwenye Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika mwaka 2010, hiyo ikiwa ni mara ya kwanza Mambas wanashiriki AFCON baada ya msoto wa miaka 12.
Hata hivyo, katika fainali hizo, Msumbiji ilishika mkia katika kundi lake baada ya kuambulia sare moja na kufungwa mechi mbili. Baada ya kukosa tiketi ya  AFCON 2012, Nooij akajiuzulu Septemba mwaka 2011 na nafasi yake kuchukuliwa na Mjerumani, Gert Engels.
Aprili 19 mwaka 2012, aliajiriwa na klabu ya Santos ya Afrika Kusini, ambako hata hivyo alifukuzwa Desemba 18, mwaka 2012 na kunyakuliwa na St George ya Ethiopia anakoendelea na kazi hadi sasa.
Baada ya kusaini Mkataba wa miaka miwili na TFF kuja kuifundisha Stars, Nooij anasubiri barua maalum ya kuruhusiwa kuondoka baada ya kukamilisha taratibu za kuvunja Mkataba uliokuwa unaelekea ukingoni na klabu hiyo ya Addis Ababa.
Yanga SC pia inafundishwa na kocha Mholanzi, Hans van der Pluijm.
Chanzo: Bin Zubeiry

Friday, March 7, 2014

Jack Wilshere awatuliza mashabiki wa Arsenal

JACK Wilshere amewapoza mashabiki wake baada ya vipimo kwenye mguu wake kuonyesha kwamba hana tatizo kufuatia mechi ya kirafiki ya England waliyoshinda 1-0 dhidi ya Denmark juzi.
Kiungo huyo wa Arsenal, aliachwa amelala chini kwenye uwanja wa Wembley kufuatia kuchezewa vibaya na Daniel Agger tukio lililolazimisgha mchezo kusimama wakati akihitaji matibabu.
Wilshere aliendelea kucheza baadaye kabla ya kutoka na nafasi yake kuchukuliwa na Adam Lallana muda mfupi kabla ya dakika ya 60. Kiungo huyo (22) haraka aliwapoza mashabiki wake waliohofu kwamba huenda ameumizwa vibaya kufuatia kuvaana na beki huyo wa Liverpool.
"Niko poa," alisisitiza kwa Sky Sports. "Panauma kidogo lakini ni mchubuko tu. Nimefanyiwa vipimo na tayari imeonyesha ni mchubuko tu hivyo itakuwa poa."

Dihile: Bado niponipo sana langoni

Dihile (chini)
KIPA mkongwe na nyota wa zamani wa Taifa Stars, Shaaban Dihile anayeidakia JKT Ruvu ameweka bayana kwamba hana mpango wa kustaafu soka kwa sasa kama alivyotangaza nahodha wake, Husseni Bunu waliojiunga wote katika timu hiyo mwaka 2005.
Akizungumza na MICHARAZO, Dihile alisema bado yupo sana dimbani katika kuendelea kucheza soka akiamini uwezo na umri unamruhusu kufanya hivyo kwa muda mrefu.
Dihile, alisema kwa nafasi ya kipa kadiri umri unavyosonga mbele ndivyo uimara wa makipa unavyoimarika na kwamba hadhani kama atatundika 'glovu' zake mapema katika misimu ya karibuni.
"Sijafikiria kustaafu kwa sasa, bado najiona nina uwezo na umri wa kuendelea kucheza kwa muda mrefu, japo kustaafu kunategemea mambo mengi ukiacha suala la umri," alisema.
Alisema kupata majeraha makubwa ni sababu inayowaondoa wachezaji uwanjani na kwa bahati nzuri yeye hajawahi kupatwa na kitu hicho hivyo haoni sababu ya kutundika glovu zake kwa sasa, labda kama ataamua mwenyewe kwa masuala mengine ikiwamo kutaka kuzisimamia miradi yake ya biashara anayoiendesha kwa sasa.
"Ya Mungu mengi, naweza kufanya maamuzi hayo labda kutaka kusimamia biashara zangu, lakini kwa sasa zinaendelea vyema ndiyo maana sina mpango wa kustaafu kwani najiona bado sana kisoka," alisema Dihile aliyewahi kuichezea Pan Africans ya jijini Dar.
Nahodha wa JKT Ruvu, Hussein Bunu alinukuliwa na MICHARAZO katika mahojiano yake maalumu wiki iliyopita akidai huu ni msimu wake wa mwisho kucheza kwa vile atatundika 'daluga' zake na kujikita kwenye ukocha aliouanza kwa sasa.

Thursday, March 6, 2014

Ajali nyingine basi la AM Coach lagongana na lori Tabora


Ajali mbaya ya basi la kampuni ya AM Coach lenya namba T 763 AYN imetokea leo asubuhi mkoani Tabora baada ya basi hilo kugongana na lori mali ya kampuni ya soda ya Coca Cola lenye namba za usajili T 256 BPP

Kwa mujibu wa taarifa kutoka Tabora ajali hiyo ilitokana lori hilo kutaka kulipita basi bila kuwa makini na kisha kwa ufinyu wa barabara hiyo ndipo ikatokea 'mzinga' huo.
Mmoja wa abiria aliyenusurika alinukuliwa akisema kuwa;

"Dereva wa lori kajaribu kutukwepa lakini ufinyu wa barabara, mbele kuna lori scania linakuja,kwa hiyo akajikuta kagonga kushoto kwake na kulia kwake ila lori la kushoto kwetu halikusimama

Dereva wetu akashindwa kurudi upande wa kushoto kwa sababu kulikuwa na lori ambalo alikuwa anataka kulipita, basi letu lilikuwa 'linaovertake'(linataka kupita), basi nia AM Coach na lori ni la Coca Cola"

Bado haijafahamika madhara makubwa ya ajali hiyo ila taarifa zinafuatiliwa.
Ajali hiyo imekuja siku chache baada ya watu saba kupoteza maisha yao katika ajali mbaya iliyotokea eneo la Chalinze mkoani Pwani ikihusisha magari mawili ikiwamo Coaster iliyokuwa imebeba abiria.
EDDY

Neymar ampagawisha 'dogo' Sauzi

Katika hali ambayo haikutarajiwa na wengi, mtoto mdogo anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka mitano jana usiku alivamia ndani ya uwanja wakati Brazil ilipokuwa ikimenyana na Afrika Kusini na kwenda moja kwa moja kwa mshambuliaji Neymar wa Brazil. 
Katika kuonyesha furaha ya kufuatwa na mchezaji huyo, Neymar aliamua kumkumbatia na kisha wachezaji wote wa Brazil waliamua kumbeba juu. Katika mechi hiyo, Brazil iliinyuka Afrika Kusini mabao 5-0, huku Neymar akifunga mabao matatu (hat trick).

Party maalum Siku ya Wanawake kufanyika Mango Garden




KATIKA kusherehekea siku ya Wanawake Jumamosi hii tarehe 08-03-2014 Bendi yako PENDWA ya Twanga Pepeta ikishirikiana na Mdau wake mkubwa Christer Bella Mwingira na Rukia Saloon, kwa pamoja wameandaa bonge la Pati kwa ajili ya kusherehekea sikukuu hii.
Pati linataraji kufanyika ndani ya Twanga City Mango Garden ambapo muonekano wake utakuwa tofauti na siku za kawaida kwa kuwa ukumbi utapambwa vilivyo.
Mavazi rasmi yatakuwa ni ya ya rangi NYEKUNDU, NYEUPE na NYEUSI.
Zawadi kedekede zitatolewa na Rukia Saloon na Christer Bella Mwingira kama vitenge na Khanga ambayo ni mavazi rasmi ya mwanamke.
Kutakuwa na ofa maalum kwa ajili ya akina mama toka kwa Mkurugenzi wetu Asha Baraka kwa kila atakayefika katika onyesho atalipia Tshs 5,000. kuanzia saa mbili mpaka saa nne usiku.
Kiingilio kitakuwa ni Tshs 10,000. kwa VIP pamoja na kinywaji na kawaida ni Tshs 7,000/=

Shigongo afafanua madhara ya Ugonjwa wa Ini


Shigongo akizungumza kwa masikitiko jinsi watu wengi walivyo kwenye hatari ya kufa kwa ugonjwa wa ini.

…Akiwa na jopo la madaktari. Kushoto ni Dk. Mtebe Majigo, Mganga Mkuu wa Amana, Meshack Shing'wela (wa pili kulia) na Daktari Kiongozi Andrew Method.

Ndeonasio Towo kutoka Damu Salama akielezea umuhimu wa wananchi kupima damu kubaini maradhi mbalimbali bila kusahau virusi vya homa ya ini.
Mwakilishi kutoka SD Tanzania ambao ni wadau wa ugonjwa huo, Phillip Sawe, akielezea umuhimu wa kupima mapema ugonjwa huo kabla mwili haujashambuliwa.
Daktari Kiongozi wa Hospitali ya Amana, Andrew Method (kulia) akisistiza jambo.
Mapaparazi kazini.
Shigongo akimueleza jambo, Mganga Mkuu wa Hospitali ya Amana.
Meneja Mkuu wa Global Publishers, Abdalah Mrisho (kushoto) na Mwakilishi kutoka Sanofa, Edwin Kisimbo, wakifuatilia kwa makini kilichokuwa kikiendelea.
Dk. Majigo (wa pili kulia) akielezea ugonjwa huo unavyoambukiza kwa njia ambazo huambukiza Ukimwi.
Meshack Shing'wela akifafanua jambo.
…Akimshukuru Shigongo kwa kuanzisha kampeni za kutokomeza ugonjwa huo.
MKURUGENZI wa Kampuni ya Global Publishers Ltd, Eric Shigongo, na wadau mbalimbali wa afya leo walizungumzia madhara ya ugonjwa hatari wa homa ya ini kwenye mkutano na wanahabari uliofanyika Hospitali ya Mkoa wa Ilala, Amana Jijini Dar.
Miongoni mwa wadau waliokuwa kwenye mkutano huyo ni madaktari mbalimbali, Sanofa ambao huhusika na vipimo vya ugonjwa huo, Damu Salama ambao huhusika na upimaji wa damu na SD Tanzania.
(PICHA : RICHARD BUKOS / GPL)

Ujerumani, England, Ureno zaua kirafiki Ulaya


article-2574068-1C10556200000578-473_634x396
Ujerumani wakishangilia goli lao dhidi ya Chile
Ronaldo akipambana na kuweka rekodi ya mabao dhidi ya Cameroon walioizabua 5-1

Messi alishindwa kuibeba Argentina dhidi ya Romania
Italia walitepeta kwa Hispania 1-0, Diego Costa akiichezea timu yake hiyo kwa mara ya kwanza

Sturridge akishangilia bao liliuloibeba England jana
UJERUMANI usiku wa jana imefanikiwa kuizabua Chile kwa kuwalaza bao 1-0, huku England nayo ikipata ushindi kama huo kwa Denmark, na Brazili ikiifanyizia Afrika Kusini kwa kuifunga kwao mabao 5-0.
Bao la Ujerumani katika mechi yake na Chile lilifungwa na Mario Gotze aliyeshirikiana vyema na Mesut Ozil.
Matokeo mengine ya michezo ya kirafiki ya kimataifa inayotambuliwa na FIFA iliyochezwa jana na alfajiri ya leo Hispania iliilaza Italia baop 1-0 na kudhihirisha haikuiotea kwenye Fainali za Ulaya walipoisasambua mabao 4-0 mpaka kumfanya Mario Balotelli kumwaga chozi.
Mexixo na Nigeria zenyewe zilishindwa kufungana, Ivory Coast ikitoka sare ya mabao 2-2  na Belgiaum, huku Ureno ikiifumua Cameroon kwa mabao 5-1 Cristiano Ronaldo akifunga mawili na kuweka rekodi ya kuwa mfungaji wenye mabao mengi kwa timu ya taifa lake akimzidi Pauleta.
amabaoUshirikiano wa kiungo wa Bayern Munich Mario Gotze na kiungo wa Arsenal Mesut Ozil ulizaa matunda jana usiku katika mchezo wa kirafiki baina ya Ujerumani dhidi ya Chile.
Wachezaji wawili walishirikiana vizuri katika goli la ushindi lilofungwa na Gotze kutoka na pasi nzuri ya mwisho ya Ozil. Mchezo ulimalizika kwa matokeo ya 1-0.

Matokeo Mengine ni kama ifuatavyo
Japan     4 - 2     New Zealand    
Iran     1 - 2     Guinea    
Russia     2 - 0     Armenia    
Bulgaria     2 - 1     Belarus    
South Africa     0 - 5     Brazil    
Algeria     2 - 0     Slovenia    
Namibia 1-1 Tanzania
Greece     0 - 2     Korea Republic    
Hungary     1 - 2     Finland    
Montenegro     1 - 0     Ghana    
Czech Republic     2 - 2     Norway    
Israel     1 - 3     Slovakia    
Bosnia-Herzegovina     0 - 2     Egypt    
Cyprus     0 - 0     Northern Ireland    
Colombia     1 - 1     Tunisia    
Turkey     2 - 1     Sweden    
Romania     0 - 0     Argentina        
Ukraine     2 - 0     United States    
Austria     1 - 1     Uruguay    
Switzerland     2 - 2     Croatia    
Germany     1 - 0     Chile    
Republic of Ireland   1 - 2     Serbia    
Belgium     2 - 2     Côte d'Ivoire    
Poland     0 - 1     Scotland    
Wales     3 - 1     Iceland    
France     2 - 0     Netherlands    
England     1 - 0     Denmark    
Australia     3 - 4     Ecuador    
Portugal     5 - 1     Cameroon    
Spain     1 - 0     Italy    
Honduras     2 - 1     Venezuela    
Mexico     0 - 0     Nigeria        
Costa Rica     2 - 1     Paraguay

Yanga wapaa kuifuata Al Ahly ikijiamini

KIKOSI cha wachezaji 18 na viongozi wa klabu ya Yanga wameodnoka nchini usiku wa kuamkia leo kuelekea Misri kwa ajili ya pambano lao la marudiano dhidi ya Al Ahly wakijiamini wanaenda kumaliza kazi.

Msafara huo umeondoka bila nyota wake kutoka Uganda,Hamis Kiiza na Emmanuel Okwi waliokuwa nchini Zambia kuichezea timu yao ya taifa Uganda The Cranes ambao walilala 2-1 kwa wenyeji wao Chipolopolo.
Hata hivyo wachezaji hao wanatarajiwa kuungana nao wenzao nchini Misri baadaye leo mchana wakitokea Zambia tayari kuivusha Yanga kwenye hatua ya 32 na kuipeleka katika 16 Bora mbele ya mabingwa wateteziu hao wa Ligi ya Mabingwa Afrika na mabingwa wa kihistoria wa michuano hiyo.
Wachezaji waliondoka kwenda kuiua Al Ahly ni  Ally Mustapha ‘Barthez’, Juma Kaseja, Deogratius Munishi ‘Dida’, Nadir Haroub ‘Cannavaro, Juma Abdul, Kelvin Yondani, Mbuyu Twite, Oscar Jushua, Nizar Alfan, Franck Domayo, Athumani Iddi ‘Chuji’, Simon Msuva, Mrisho Ngasa, Said Bahanuzi, Haruna Niyonzima, Didier Kavumbagu, David Luhende na Jerry Tegete.
Kwa mujibu wa uongozi wa Yanga mpaka sasa hawajajua mechi yao itakayochezwa Jumapili usiku itafanyika kwenye uwanja gani baada ya uongozi wa Al Ahly kuficha taarifa hizo mpaka jana mchana.
Hata hivyo, Afisa Habari wa Yanga, Baraka Kizuguto aliyetangulia Cairo alsema huenda  mchezo huo ukachezwa kwenye Uwanja wa Arab Contractors uliopo jijini Cairo. na kwamba maandalizi ya kuipokea timu yao inaendelea vyema kujipanga kuivaa wenyeji wao ambao hawaamini mpaka sasa kama walefungwa na timu ya Afrika Mashariki .

Cannavaro atamba Yanga itafanya maajabu Cairo

 
NAHODHA wa klabu ya Yanga, Nadir Haroub 'Cannavaro' amesema kwamba kikosi chao kitafanya maajabu kwenye mechi yao ya marudiano dhidi ya mabingwa watetezi wa Ligi ya Klabu Bingwa Afrika, Al Ahly ya Misri siku ya Jumapili.
Yanga itaumana na Al Ahly katika mechi yao ya marudiano ya hatua ya kwanza itakayochezwa usiku wakiwa na ushindi wa 1-0 waliopata katika pambano lao la awali jijini Dar es Salaam kupitia goli lililofungwa kwa kichwa katika dakika ya 82 na nahodha huyo.
Akizungumza na MICHARAZO, Cannavaro alisema wanajua wa mchezo huo utakuwa ni mgumu, lakini wanaenda Cairo kuhakikisha wanatimiza ndoto zao za kuivusha Yanga kwenye 16 Bora.
"Tutaenda kupambana japo tunatarajia ushindani mkubwa baada ya kuwafunga hapa nyumbani," alisema beki huyo wa kati.
Cannavaro alisema wachezaji karibu wote watakaokuwa kwenye msafara wao uliotarajiwa kuondoka usiku wa jana, wamepania kuhakikisha Yanga inaing'oa Al Ahly na kurejea kilichowahi kufanywa na watani zao Simba mwaka 2003.
Katika mwaka huo Simba iliwafunga waliokuwa watetezi wa Ligi ya Mabingwa, Zamalek pia ya Misri kisha kwenda kukubali kipigo cha 1-0 ugenini na kufanya timu hizo zikipigiane penalti na Simba kushinda kwa mikwaju 3-2.
"Tupo tayari kwa vita na Inshallah tutapambana mpaka kieleweke mjini Cairo kwa sababu tumepania kuifikisha mbali timu yetu, " alisema Cannavaro.
Bao la Cannavaro alililofungwa kwa kichwa cha kuchupia liliiwezesha Yanga kuvunja uteja kwa timu za Afrika Kaskazini zikiwamo kutoka Misri uliodumu kwa miaka zaidi ya 30 na watalazimika kupata japo sare ugenini ili kusonga mbele.

'Simba hatuhusiki uvunjwaji wa viti Taifa'

UONGOZI wa Klabu ya Soka ya Simba umesema kuwa hauhusiki na vurugu za kuvunja viti zilizotokea kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam wakati Yanga inacheza mechi yake ya mabingwa wa Ligi ya Klabu Bingwa Afrika, Al Ahly ya Misri.
Simba ilisema jana kuwa imeamua kutoa taarifa hiyo kutokana na kuwapo kwa 'uvumi' kwamba klabu hiyo huenda ikapigwa faini kufuatia baadhi ya mashabiki wake kudaiwa kuvunja viti siku ya mchezo huo.
Baadhi ya picha zilizoonekana kwenye vyombo vya habari zilionyesha mashabiki waliovaa jezi nyekundu na wengine njano wakirushiana viti na kuacha kushangilia.
Afisa Habari wa klabu hiyo, Asha Muhaji, alisema kuwa mashabiki wa Simba hawawezi kuvunja viti kwa sababu mechi hiyo ilikuwa inawahusu wapinzani wao, Yanga na Al Ahly.
Muhaji alisema kuwa si kila shabiki aliyevaa jezi nyekundu ni wa Simba kwa sababu rangi hiyo inavaliwa na klabu mbalimbali za hapa nchini kama Coastal Union, Small Simba na Al Ahly iliyokuwa inashiriki mchezo huo.
"Sisi tunaamini waliofanya vurugu ni mashabiki wa Al Ahly ambao ndio walikuwa na wapinzani wa Yanga, inashangaza Simba tunatajwa kuhusika na vurugu hizo katika mechi tusiyokuwa na maslahi nayo," alisema Muhaji.
Aliongeza kwamba Simba inataka kuweka wazi kuwa vurugu zilizofanyika katika mchezo huo haziwezi kuhusishwa na klabu yao kwa namna yoyote.
Mara kadhaa mwenyekiti wa Simba, Ismail Aden Rage, amekuwa akisisitiza mashabiki wa soka kuwa wazalendo pale timu mojawapo inapokuwa inapeperusha bendera ya nchi kushangilia na kuacha mazoea ya kuzomea.
Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limesema linaendelea kufanya uchunguiz juu ya tukio hilo kabla ya kutoa tamko, japo imelaani vurugu hizo na kuwaonya mashabiki kuwa wastaarabu kwa kuwa uwanja wa Taifa siyo wa klabu chache bali ni wa Watanzania wote.

Taifa Stars angalau, yatoka sare ya 1-1 ugenini Namibia

Na Prince Akbar, Windhoek, Namibia
TIMU ya soka ya taifa ya Tanzania Taifa Stars imetoka sare ya kufungana bao 1-1 na Namibia katika mchezo wa kimataifa wa kirafiki unaotambuliwa na Fifa uliochezwa Jumatano usiku kwenye uwanja wa Sam Nujoma nchini Namibia.
Hadi dakika 45 za kipindi cha kwanza zinamalizika,timu hizo zilikuwa bado hazijafungana na kocha Salum Madadi akafanya mabadiliko katika kipindi cha pili kwa kuwatoa Erasto Nyoni, Ramadhani Singano ‘Messi’ na juma Luizio na nafasi zao kuchukuliwa na Michael Aidan, Athanas Mdam na khamisi Mcha ‘Vialli’.
Kikosi cha kwanza cha Timu ya Taifa, Taifa Stars kikiwa katika picha ya pamoja kabla ya mchezo dhidi ya Timu ya Taifa ya Namibia, Brave Warriors na kutoka sare ya bao 1-1. Taifa Stars inadhaminiwa na Bia ya Kilimanjaro Premium Lager.
Mchezaji wa Taifa Stars, Jonas Mkude  (katikati) akijaribu kupiga mpira katikati ya wachezaji wa timu ya taifa ya Namibia ‘Brave Warriors’ wakati wa mchezo wa kimataifa wa kirafiki baina ya timu hizo mbili katika uwanja wa Sam Nujoma  jana usiku. Tumu hizo zilitoka sare ya bao 1-1. Taifa Stars inadhaminiwa na Bia ya Kilimanjaro Premium Lager.
Mlinzi wa Taifa Stars, Saidi Morad  (kulia) akiwania mpira na mchezaji wa timu ya taifa ya Namibia ‘Brave Warriors’ Lous Jereme  wakati wa mchezo wa kimataifa wa kirafiki baina ya timu hizo mbili katika uwanja wa Sam Nujoma jana usiku. Tumu hizo zilitoka sare ya bao 1-1. Taifa Stars inadhaminiwa na Bia ya Kilimanjaro Premium Lager.
Mlinzi wa Taifa Stars, Erasto Nyoni (kulia) akijaribu kuudhibiti mpira mbele ya mchezaji wa timu ya taifa ya Namibia ‘Brave Warriors’ Puriza Hosea wakati wa mchezo wa kimataifa wa kirafiki baina ya timu hizo mbili katika uwanja wa Sam Nujoma  jana usiku. Tumu hizo zilitoka sare ya bao 1-1. Taifa Stars inadhaminiwa na Bia ya Kilimanjaro Premium Lager.
Stars, inayodhaminiwa na Bia ya Kilimanjaro Premium Lager ndio walikuwa wa kwanza kupata bao katika dakika ya 86 baada ya kona  iliyopigwa na Khamisi Mcha ‘Vialli’ aliyetokea benchi na kuingia moja kwa moja nyavuni bila kuguswa.
Namibia walisawazisha bao hilo katika dakika ya tano ya muda wa nyongeza baada ya kutimu dakika 90 za kawaida, lililofungwa na Nekundi Haleluya Panduleni kwa adhabu.
Refa wa mechi hiyo aliingia lawamani kwa kuzidisha muda kupita kiasi, kwani mwamuzi wa mezani alionyesha dakika tano za nyongeza lakini muamuzi alichezesha dakika tano nyingine hivi kuwawezesha Namibia kupata bao.
Lakini katika hali ya kushangaza waamuzi toka nchini Zambia na msimamizi wa mechi toka nchini Afrika Kusini waliopangiwa kuchezesha mchezo huo hawakutokea, na badala yake shirikisho la soka Namibia NFA, wakaamuru mchezo huo uchezeshwe na waamuzi wa Namibia kwa makubaliano ya pande zote mbili.
Mwalimu Salum Madadi alisema licha ya kuwakosa wachezaji wengi nyota, kikosi hiki kilipigana hadi dakika ya mwisho na ameridhishwa na matokeo yaliyopatikana.
Wachezaji walioshindwa kujiunga na kikosi cha Stars ni Mbwana Samatta, Thomas Ulimwengu na Mwinyi Kazimoto ambao hawakuruhusiwa na vilabu vyao kutokana na kukosekana na usafiri wa kuwarudisha vilabuni kwa muda unaotakiwa.
Wengine walioshindwa kufika ni Edward Charles na Hassan Masapili ambao hati zao za kusafiri hazikuwa zimekamilika. Viwango
Matokeo haya huenda yakaiweka Stars kwenye nafasi nzuri ya viwango vya Fifa kwa kupata sare ugenini.
BIN ZUBEIRY

Wednesday, March 5, 2014

Yanga kuivaa Alh Ahly J'2 usiku, kikosi kuondoka leo usiku

Kikosi cha Yanga kilichoibana Al Ahly kwa kuilaza 1-0 jijini Dar jumamosi iliyiopita
IMETHIBITIKA kuwa, wawakilishi pekee wa Tanzania kwenye mashindano ya Klabu Bingwa Barani Afrika timu ya Young Africans itacheza mchezo wa marudiano siku ya jumapili jijini Cairo dhidi ya timu ya Al Ahly ukiwa ni mchezo utakaotoa picha halisi ni timu gani itasonga mbele katika hatua ya 16 bora.
Ikiwa ni takribani siku tano kabla ya kufanyika mchezo wenyewe wenyeji Al Ahly wameshindwa kuweka wazi ni uwanja gani utakaotumika kwa ajili ya mchezo huo huku Meneja wa klabu hiyo Abdoulazi akisema huenda mchezo ukachezwa jijini Cairo au Alexandria na kusema majibu kabili yatapatikana siku ya jumatano mchana.
Wenyeji wameiandalia timu ya Young Africans kufikia katika Hoteli ya Baron iliyopo maneneo ya Uwanja wa michezo wa kimataifa Cairo huku pia wakiipangia timu kufanya mazoezi katika uwanja wao uliopo eneno la Nasri City.
Katika mchezo wa awali uliofanyika mwishoni mwa wiki kwenye dimba la Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam Young Africans ilifanikiwa kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Al Ahly ambao ni mabingwa watetezi wa kombe hilo shukrani kwa bao la Nahodha wa timu Nadir Haroub "Cannavaro" aliyetikisha nyavu dakika ya 82 ya mchezo.
Mara baada ya mchezo huo kikosi cha mholanzi Hans Van der Pluijm kiliingia kambini jana jioni katika hotel ya Ledger Bahari Beach tayari kwa maandalizi ya mchezo marudiano ambapo timu imeendelea kufanya mazoezi katika uwanja wa Boko Beach Veterani.
Kuelekea mchezo huo wa jumamosi tayari uongozi wa Young Africans ulishaanza kufanya maandalizi ya safari ambayo inatarajiwa kuwepo kabla ya mwisho mwa wiki hii huku msafara ukitarajiwa na kuwa idadi ya watu 35, wakimwemo viongozi, benchi la ufundi pamoja na wachezaji 19.
Hali ya wachezaji ni nzuri, kiafya, fikra na morali ya kuelekea mchezo wenyewe bado ni kubwa kwani bench la ufundi na wachezaji wanaamini maandalizi wanayoyafanya yatasaidia kupelekea kupata ushindi katika mchezo huo na kuweza kusonga mbele katika hatua ya 16 bora.
Baadhi ya wachezaji wanaotarajiwa kuondoka usiku wa leo kuifuata Al Ahly ni makipa Deogratius Munishi 'Dida' na Juma Kaseja, Nadir Haroub 'Cannavaro, David Luhende, Oscar Joshua, Kelvin Yondani, Simon Msuva, Mrisho Ngasa, Haruna Niyonzima, Didier Kavumbagu, Juma Abdul, Frank Domayo, Mbuyu Twite, Rajab Zahir na Said Bahanuzi.
Okwi na Kiiza, wataungana na kikosi hicho Alhamisi wakitokea Lusaka, walipo na timu yao ya Taifa ya Uganda ( The Cranes) ambayo jana ilikuwa inacheza na Zambia (Chipolopolo) mechi ya kimataifa ya kirafiki.
Yanga inahitaji ushindi au sare ya aina yoyote ili iweze kusonga mbele kwenye michuano hiyo.
Maandalizi ya sehemu ya kambi ambapo timu itafikia jijini Cairo tayari yanaendelea vizuri kwa kushirikiana na Ubalozi wa Tanzania ambapo kwa upande wa klabu ya Young Africans Afisa Habari Baraka Kizuguto tayari yupo nchini Misri kwa siku ya pili akiendelea kuweka mambo sawa.
Mchezo wa jumapili unatarajiwa kufanyika katika uwanja wa Arab Contractors uliopo jijini Cairo huku mechi hiyo ikichezwa bila ya mashabiki kufuatia Serikali ya Misri kuzuia mashabiki wa soka kutokana na mashabiki hao kufanya vurugu katika mchezo wa Fainal ya Super Cup dhidi ya CS Sfaxien na kupelekea askari kadhaa kujeruhiwa.

Wawili waongeza mkataba Arsenal na kumpa ahueni Wenger

350594_heroaBaada ya kupoteza mechi yake iliyopita ya ligi kuu ya England klabu ya Arsenal leo imewapa habari nzuri mashabiki wake baada ya kutangaza wachezaji wao wawili wameongeza mikataba ya kuendelea kuitumikia klabu hiyo.
Nahodha wa timu hiyo Mjerumani Per Mertesacker na kiungo Thomas Rosicky wote wametangazwa kuongeza mikataba yao.
“Tunayo furaha kutangaza kwamba Mertesacker na Rosicky wameongeza mikataba ya kuendelea kuwepo hapa,”  Arsene Wenger aliuambia mtandao rasmi wa klabu hiyo.
“Ni wachezaji wazuri na wenye uzoefu, na wameshaonyesha kila siku kwamba wanaweza kucheza kwenye level ya juu.’ – alimaliza Wenger.
Klabu hiyo hata hivyo haijatoa namba ya miaka kamili ya muda wa mikataba mipya.

Mourinho 'aizuga' Mancehster City mbio za ubingwa England

Jose Mourhino (kulia) na kocha wa Manchester City Manuel Pellegrini  wakisalimiana enzi wakiwa Hispania
LONDON, England
KOCHA wa Chelsea, Jose Mourinho amesema watakuwa wanabadilisha nafasi za mbio za ubingwa wa Ligi Kuu England na Manchester City kutokana na kikosi hicho cha Manuel Pellegrini kuwa na mechi mkononi.
Miamba hiyo ya Stamford Bridge inaizidi City kwa pointi sita baada ya mwishoni mwa wiki kuibuka na ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Fulham, lakini mabingwa wa Kombe la Ligi (Capital One Cup) wana mechi mbili mkononi na wastani mzuri wa mabao ya kufunga na kufungwa kuliko Chelsea.
Pellegrini anawinda mafanikio makubwa kwa kutwaa makombe matatu baada ya kuiongoza City kushinda 3-1 dhidi ya Sunderland Jumapili kwenye Uwanja wa Wembley na kutwaa ubingwa wa Capital One Cup, jambo ambalo Mourinho anasisitiza kuwa kocha huyo raia wa Chile yupo katika nafasi nzuri ya mbio za ubingwa.
"Ninapenda kuwa na bahati mkononi, na City tu ndiyo yenye bahati mkononi mwake," Mourinho alisema. "Kama nitashinda kila mchezo hadi mwishoni mwa msimu, zote 10 – kama hatutaweza labda hatutakuwa mabingwa.
"Kama [City] itashinda mechi zote 12 ilizo nazo, watakuwa mabingwa. Wana bahati mkononi mwao."

Wavuvi wawili wauwawa kwa risasi wakivua samaki mtoni

Na   Walter Mguluchuma, Katavi
WATU wawili  James  Mauto  21 Mkazi wa Kijiji  cha  Ugala Wilaya ya Mlele   na  January  Marekani  18 Mkazi wa Kijiji  cha Mtapenda  Tarafa ya Nsimbo Wilaya ya Mlele  mkoa  wa Katavi wameuwawa  kwa kupigwa  risasi   na Askari wa Geme Reserve wakati  wakiwa wanavua  samaki  ndani ya   Hifadhi  ya Pori la akiba la Ugala na mwenzao mmoja kujeruhiwa  kwa Risasi sehemu ya mbavu zake
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi wa Mkoa  wa Katavi Dhahiri Kidavashari   tukio hilolilitokea hapo  Februari  28 mwaka huu majira ya saa  tisa Alasiri  ndani ya Hifadhi ya pori  la akiba la Ugala Wilayani Mlele Mkoa wa Katavi 

Alieleza siku hiyo ya tukio    James Mauti  na  Januari Marekani walikuwa wakivua samaki ndani ya mto Ugala uliko kwenye  Hifadhi  ya pori la akiba la ugala wakiwa na mwenzao mmoja  aitwaye  Seif Juma  40  Mkazi wa kijiji  cha Mtapenda  Tarafa ya Nsimbo Wilaya ya Mlele
Kamanda Kidavashari alisema  wakati wakiwa wanaendelea kuvua samaki ndani ya mto huo  alitokea Askari  wa Geme Reserve  ambae alikuwa amevalia sare   huku akiwa na silaha  bunduki  ambayo haikuweza kufahamika aina yake
Alisema Askari huyo aliwaamuru  wavuvi  hao wajisalimishe kwake  hata hivyo wavuvi  hao waliokuwa wakiendelea na uvuvi  kufutia amri hiyo ya Askari  waliamua kutupa nyavu zao walizokuwa wakivulia samaki  na kukimbia mbio  kila mmoja sehemu yake
Ndipo Askari huyo  alipoanza  kuwarushia  risasi  wavuvi  hao  na kuwauwa  kwa risasi James Mauto   na Januari  Marekani  na kumjeruhi Seif  Juma sehemu za  mgongoni na kwenye mbavu
Majeruhi  ambae ni Seif  Juma  alifanikiwa  kufika katika kijiji  cha Ugala  na  kutoa taarifa kijijini hapo kwa uongozi wa Serikali ya Kijiji juu ya tukio hilo  na aliweza kupatiwa msaada wa kukimbizwa katika Hospitali ya Wilaya ya Mpanda kwa ajiri ya matibabu
Kamanda Kidashari  alieleza  kuwa mvuvi huyo  ambae ni majeruhi  kwa kuhofia kukamatwa na kuhojiwa  na polisi  baada ya kufikishwa  Hospitali alitoroka  na mpaka sasa  haijajulikana mahari alipo na anatibiwa wapi majeraha yake ya risasi
Alisema  kutokana na tukio hilo kuhusishwa  na Askari  wa Geme  Reserve  katika hifadhi  hiyo  jeshi la polisi Mkoa wa Katavi  linawasiliana  na mkuu wa  kikosi cha  wanyama pori  mkoa wa Tabora  ambako ndio  walikuwa wametoka Akari waliohusika na tukio la mauwaji hayo
Alifafanua  kuwa  tayari mkuu wa Kikosi hicho  cha wanyama pori  ametuma kikosi chake kwenye eneo hilo la tukio  ilikubaini  ni Askari  gani waliokuwa kwenye  doria  eneo hilo  ili kuwabaini  na kisha  sheria ichukuwe mkondo wake  kwa askari  aliyehusika au waliohusika  kwa tukio la mauwaji hayo ya kinyama kwa binadamu hao.
Pambana na Climate Change

Petr Cech hakamatiki Tuzo ya Mchezaji Bora Czech

KIPA wa klabu ya Chelsea ya England, Petr Cech hashikiki katika Tuzo yta Mchezaji Bora wa Mwaka wa Jamhuri ya Czech baada ya kutangazwa tena kuwa mshindi wa mwaka 2013 ikiwa ni mara yake ya sita mfululizo kati ya saba aliyonyakua tuzo hiyo.
Cech (31) ameshinda tuzo hiyo kwa mara ya sita baada ya kupigiwa kura nyingi kutoka kwa wachezaji, makocha, viongozi wa shirikisho la soka na waandishi wa habari.
Kiungo wa Arsenal, Tomas Rosicky ameshika nafasi ya pili wakati mchezaji wa Freiburg, Vladimir Darida akishika ya tatu.
Kipa huyo ndiye tegemeo wa Chelsea inayopigana kunyakua ubingwa kwa msimu huu ikiwa chini na kocha aliyewahi kuipa mafanikio huko nyuma, Jose Mourinho.

Taifa Stars dimbani leo Namibia bila Samatta, Ulimwengu

Taifa Stars
Mbwana Samatta (kulia) atakayelikosa pambano la leo nchini Namibia

TIMU ya Taifa (Taifa Stars), itawakosa nyota wake wanaocheza soka nje ya nchi katika mechi ya kirafiki ya Kimataifa dhidi ya Namibia itakayochezwa leo kwenye Uwanja wa Sam Nujoma jijini Windhoek nchini humo.
Hatua hiyo inakuja baada ya Shirikisho la Soka nchini (TFF) kushindwa kupata usafiri wa uhakika wa kuwarejesha ndani saa 24 katika klabu yao, washambuliaji Mbwana Samatta, Thomas Ulimwengu wanaoichezea TP Mazembe ya DR Congo pamoja na Mwinyi Kazimoto anayeichezea Al-Makhiya ya Qatar.
Stars ya TFF (iliyoteuliwa na shirikisho hilo badala ya kocha), iliondoka nchini juzi alfajiri ikiwa chini ya Kaimu Mkurugenzi wa Ufundi wa shirikisho hilo, Salum Madadi, aliyeshika kwa muda nafasi ya aliyekuwa kocha wa timu hiyo, Mdenmark Kim Poulsen, ambaye alitimuliwa wiki iliyopita.
Ofisa Habari wa TFF, Boniface Wambura, aliliambia NIPASHE jijini Dar es Salaam jana kuwa, Stars itashuka dimbani bila ya wachezaji wake wanaosakata kabumbu la kulipwa nje ya nchi, Ulimwengu, Samata  na Kazimoto.
Alisema wachezaji hao wanakosekana baada ya TFF kukosa ndege ya kuwarudisha katika timu zao ndani ya saa 24 baada ya mechi hiyo kumalizika kama Kanuni za Fifa zinavyoelekeza.
"Ndege tulizopata zinapita Nairobi kwenda Lubumbashi Machi 8, wakati Samata na Ulimwengu wana mechi muhimu ya Ligi ya Mabingwa Afrika mwishoni mwa wiki," alisema Wambura.
Aidha, Wambura alisema Stars itawakosa wachezaji Hassan Mwasapili na Edward Charles ambao wamekosa hati za kusafiria (passport).
Kutokana na kukwama kwa nyota hao, Stars sasa imebaki na wachezaji 15 wakiwamo makipa Mwadini Ally (Azam) na Shaban Kado (Coastal) aliyeitwa kuziba nafasi ya Ivo Mapunda (Simba) aliyefiwa na baba yake mzazi wiki iliyopita.
Mabeki ni Erasto Nyoni, Said Moradi na Aggrey Morris (Azam), Abdi Banda (Coastal) na Michael Aidan (Ruvu Shooting), wakati viungo ni Amri Kiemba (Simba), Jonas Mkude (Simba) na Himid Mao kutoka Azam FC.
Washambuliaji ni Athanas Mdamu (Alliance Mwanza), Haruna Chanongo (Simba), Khamis Mcha (Azam), Ramadhan Singano (Simba) na Juma Luizio kutoka Mtibwa Sugar.