STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, August 31, 2014

Falcao aitosa Man City kumfuata Ronaldo Madrid

https://pbs.twimg.com/profile_images/3079281026/5ddb6ef52b6aa1e61e9196fac65bf9a0.jpeg 
NDOTO za klabu ya Manchester City kumnasa nyota wa Colombia anayeichezea Monaco, Ramadel Falcao zinaendelea kuyeyuka baada ya kuwepo taarifa mshambuliaji huyo anajiandaa kutua Real Madrid.
Mshambuliaji huyo ameeleza nia yake ya kutataka kutua Madrid kuungana na akina Ronaldo na James Rodriguez
Falcao aliweka taarifa yake kwamba ndoto yake ya kwenda Madrid itakamilika.
Alieleza hilo kupitia mtandao wa jamii wa Instagram. Lakini baada ya muda mchache akaitoa post hiyo.
Hali ambayo imeonyesha uhamisho wake unaendelea kushughulikiwa.
Man City ilikuwa inapambana kumpata Falcao ambaye anaendelea kuichezea AS Monaco ya Ufaransa.
Mchezaji huyo jana alikuwa jukwaani wakati 'chama' lake kiliambulia sare ya 1-1 dhidi ya Lille katika Ligue1.

Ronaldo amtabiria makubwa Di Maria

http://www2.pictures.zimbio.com/gi/Cristiano+Ronaldo+Angel+Di+Maria+Real+Madrid+OQaX2hmg7S7l.jpgMSHAMBULIAJI nyota wa klabu ya Real Madrid, Cristiano Ronaldo, amemtabiria mafanikio mchezaji mwenzake wa zamani Angel Di Maria katika klabu yake mpya ya Manchester United. 
Nyota huyo wa kimataifa wa Argentina jana alianza makeke yake akiwa na kikosi chake kipya ambacho hata hivyo kilishindwa kufurukuta ugenini baada ya kulazimishwa suluhu na timu iliyopanda daraja Burnley.
Usajili wa nyota huyo umevunja rekodi nchini Uingereza na ilikuja baada ya kushindwa kupata nafasi katika kikosi cha Carlo Ancelotti huku akipewa jezi namba saba ambayo imewahi kutimiwa na Ronaldo wakati akiwa United. 
Ronaldo ambaye alicheza misimu sita na United, anaamini kuwa uhamisho huo ndio Di Maria aliokuwa akihitaji na ana uhakika nyota huyo anaweza kuisaidia timu hiyo kubadili mwelekeo baada ya kuanza vibaya msimu mpya wa Ligi Kuu. 
Akihojiwa Ronaldo ambaye jana ametunukiwa tuzo ya mchezaji bora wa mwaka barani Ulaya katika sherehe zilizofanyika jijini Monaco, amesema Di Maria kwenda United ni jambo ambalo litamsaidia kwani anaamini amekwenda katika moja ya klabu bora duniani hivyo anamtakia mafanikio akiwa huko. 
Ronaldo aliendelea kudai kuwa amezungumza naye na kumwambia kuwa jezi namba aliyopewa ina majukumu makubwa lakini anadhani ataitendea haki jezi hiyo kwani ni mchezaji mahiri.

HUYU NDIYE MSHINDI WA TMT 2014


MSHIRIKI kutoka Mtwara, Mwanaafa Mwinzago ameibuka kidedea katika Shindano la Tanzania Movie Talents (TMT) lililofanyika usiku wa kuamkia leo kwenye Ukumbi wa Mlimani City, jijini Dar es Salaam.
Katika shindano hilo ambalo washiriki 10 walikuwa wakizitolea macho Shilingi milioni 50, Mwanaafa aliweza kuzoa kura nyingi zaidi na hivyo kujiwekea kibindoni mamilioni hayo na kuwatimulia vumbi washiriki wengine.
Awali kabla ya kutangazwa mshindi, Mwenyekiti wa Kampuni ya Proin Promotions, Johnson Lukaza alitoa ahadi kwamba kampuni hiyo itajitolea kumsomesha mtoto Mwanaafa ili aweze kufanikiwa kufikia malengo yake.
Mwanaafa ndiye mshiriki mdogo kuliko wote katika shindano hilo lililoandaliwa na Proin Promotions ambapo miongoni mwa majaji watatu, wawili walikuwa waigizaji maarufu nchini, Single Mtambalike ‘Ritchie Rich’ na Yvonne Cherie ‘Monalisa’. Jaji Mkuu alikuwa Roy Sarungi.
Mara baada ya kutangazwa mshindi, Mwanaafa aliangua kilio cha furaha kuonesha kutoamini kwamba amefanikiwa kunyakua mamilioni hayo huku akihaha huku na kule kumtafuta mama yake jukwaani.
Hata baada ya kuitwa na kukabidhiwa hundi ya Shilingi milioni 50 na Mwenyekiti wa Proin Promotions, Mwanaafa aliendelea kububujikwa machozi ya furaha kuonesha kabisa kutoamini kinachotokea usiku huo.

Spurs, Liverpool ni vita tupu, Arsenal kujiuliza ugenini

http://screaming-eagles.com/wordpress/wp-content/uploads/2013/12/Tottenham-vs-Liverpool.jpghttp://337sports.net/wp-content/uploads/2014/08/Leicester-City-vs-Arsenal.jpg
WAKATI jinamizi baya likiendelea kuiandama Machester United baada ya kulazimishwa suluhu na timu iliyopanda daraja Burnley, huku majirani zao Machester City wakibamizwa nyumbani na Stoke City, leo ni zamu za Tottenham Hotspur na Liverpool kuonyeshana kazi katika Ligi Kuu ya England.
Mechi hiyo inayosubiriwa kwa hamu itapigwa kwenye uwanja wa White Hart Lane, London ya Kaskazini Spurs ikitaka kuendeleza maajabu yake ya kupata ushindi mfululizo katika ligi pia wakitaka kurejea kileleni baada ya kuenguliwa na Chelsea iliyoifumua Everton ikiwa uwanja wa ugenini mabao 6-3.
Mbali na mechi hiyo leo pia katika ligi hiyo kutakuwa na mechi nyingine mbili Arsenal ikiwa ugenini itavaana na Leicester City na Aston Villa kuikaribisha Hull City.
Liverpool ambayo ilimnyakua mshambuliaji mpya toka AC MIlan, Mario Balotelli imetamba kuwa itaanza kumtumia mchezaji huyo katika mechi hiyo, ikiamini atashirikiana na wenzake kurejesha heshima baada ya wiki iliyoipita kufumuliwa mabao 3-1 na mabingwa watetezi Manchester City.
Vijana hao wa Branden Rodgers wanahitaji ushindi katika mechi hiyo ya ugenini ili kuwatuliza mashabiki wao ambao wanaamini pengo la Luis Suarez aliyewapa raha msimu uliopita bado halijapata wa kuliziba labda baada ya ujio wa 'mtukutu' Mario Balotelli aliyerejea katika ligi ya England baada ya miezi kadhaa.
Mbali na mashabiki wa kandanda kuwa na hamu ya kutaka kuona Supr Mario atafanya kitu gani leo mbele ya Spurs inayotambia nyota kadhaa akiwamo Emmanuel Adebayor na ambayo haijaruhusu wavu wake kuguswa tangu ligi hiyo ilipoanza Agosti 16.
Katika pambano la Arsenal iliyoanza kwa ushindi kabla ya kuponea chupuchupu kipigo toka kwa Everton wiki ijayo itakuwa na hamu ya ushindi ili kuendeleza furaha yao ya kufuzu hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa msimu wa 17 mfululizo baada ya kuilaza Besiktas ya Uturuki katikati ya wiki.
Baoa la nyota wake mpya kutoka Chile, Alexis Sanchez lilitosha kumtuliza Arsene WEnger ambaye amekuwa akimkingia kifua mashambuliaji huyo baada ya kuanza ligi bila kuonyesha vitu vyake vilivyomfanya Arsenal wamsajili baada ya Kombe la Dunia la nchini Brazili akitokea Barcelona.
Je, ni Spurs itakayoendeleza wimbi la ushindi au LIverpool itakayofufukia mikononi mwa Super Mario au ni Arsenal kupata ushindi ugenini leo? Tusubiri!

INATISHA! VIKONGE 38 WAUWAWA SHINYANGA

Jumla ya vikongwe 38 wameuawa  mkoani Shinyanga katika matukio tofauti, yakiwamo ya kuhusishwa na uchawi na ushirikina na wengine kudaiwa kutowapa urithi watoto wao matokeo yake watoto kuua wazee wao
Akizungumza na waandishi wa habari juzi kamanda wa jeshi la polisi mkoani Shinyanga SACP Justus Kamugisha,alisema vikongwe wamekuwa wakiuawa, bila ya kuwa na hatia kutokana na kuhisiwa kuwa ni wachawi.
Alisema mbali na imani za kishirikina vikongwe wengine wamekuwa wakiuawa kikatili wakidaiwa kung’ang’ania mali na kutowagawia watoto wao hivyo watoto hao kuamua kutekeleza mauaji hayo.
Kamugisha alifafanua katika kipindi cha mwezi Januari hadi Desemba mwaka jana (2013), jumla ya vikongwe 27 wameuawa yaani katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga vijijini vikongwe 11, Kahama 9 na   Kishapu 7.
Aliongeza kuwa katika kipindi cha mwezi Januari hadi Julai mwaka huu (2014),vikongwe 11 wameuawa,ikiwa katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga vijijini vikongwe 6,  Kahama 4, Kishapu mmoja.
“Jumla kuu ya vikongwe waliouawa katika kipindi cha mwaka jana hadi Julai  mwaka huu wa 2014,ni 38”,alisema kamanda Kamugisha
Kufuatia mauaji hayo kamanda Kamugisha aliwataka wakazi wa mkoa wa Shinyanga kuacha kuendekeza imani za kishirikina,ambazo zimekuwa zikichangia kwa kiasi kikubwa mauaji hayo ya vikongwe, huku akiwataka vijana kushighulisha ili kujipatia kipato na kuacha dhana tegemezi ya mirathi.
Kamugisha alisema katika msimu wa mwaka huu wa mwaka 2014/2015, atahakikisha anakomesha uhalifu mkoani Shinyanga, pamoja na kutokomeza mauaji hayo ya vikongwe na watu wenye ulemavu wa ngozi (albino). 
Aidha aliwataka wananchi likiwamo na jeshi la jadi sungu sungu kushirikiana kwa pamoja na  kuhakikisha, wanawakamata wahalifu, ili kuwafikisha katika vyombo vya dola, na kuchukuliwa hatua kali za kisheria ili liwefundisho kwa watu wengine.
Aliongeza kuwa hivi sasa anatarajia kusambaza polisi kata, kwa kila kata kwani baadhi ya kata hazina polisi hao, hali ambayo itasaidia kushirikiana kwa ukaribu na wananchi katika kuhakikisha anawatia nguvuni waharifu.

Simba yairarua KMKM x5 Zenji

Tambwe akishangilia moja ya mabao yake na Ramadhani Singano 'Messi'
KLABU ya soka ya Simba imeirarua bila huruma mabingwa wa Zanzibar, KMKM kwa kuicharaza mabao 5-0 katika mchezo wa kirafiki kujiandaa na Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara iliyochezwa usiku wa kuamkia leo visiwani humo.
Pambano hilo lililochezwa kwenye uwanja wa Amaan,  ilishuhudia vijana wa kocha Ally Bushiri ‘Bush’ ambayo katikati ya wiki walichezea kichapo cha mabao 2-0 toka kwa Yanga ikienda mapumziko ikiwa tayari imeshashindiliwa mabao 4-0.
Simba ilipata mabao yake kupitia kwa  Amisi Tambwe aliyefuinga mawili,, Amri Kiemba, Shaaban Kisiga ‘Marlone’ na Elias Maguli.
Kiemba alianza kuifungia Simba bao dakika ya tatu ya mchezo baada ya kumalizia pasi murua ya Pierre Kwizera kabla ya Tambwe kufunga la pili dakika ya 14 na kuongeza jingine dakika  23 kabla ya Kisiga kufunga la nne dakika ya 37 na katika kipindi cha pili Maguli kuhitimisha karamu hiyo ya magoli.

Friday, August 29, 2014

Samuel Eto'oo afunguka 'Sina bifu na Mourinho'

MSHAMBULIAJI mpya wa Evetrion, Samuel Eto'o ametupilia mbali madai kuwa ana bifu na Jose Mourinho wakati timu yake ikijiandaa kuivaa Chelsea katika mechi ya Ligi Kuu tya England kesho Jumamosi.
Eto’o, Mchezaji wa Kimataifa wa Cameroon, na Meneja wa Chelsea Jose Mourinho walikuwa pamoja huko Inter Milan na kutwaa UEFA CHAMPIONS LIGI pamoja na akaja England Mwaka mmoja uliopita kuungana na Mourinho huko Chelsea.
Lakini uhusiano wa Eto’o na Mourinho ulipata msukosuko pale Mreno huyo aliponaswa kwenye Kamera bila kujijua akidhihaki Umri wa Eto’o na kudai ni Mzee kupita Miaka inayodaiwa anayo.
Mara baada ya tukio hilo Eto’o, mwenye Miaka 33, alifunga Bao akiichezea Chelsea na kwenda kushangilia mithili ya Mzee akishika Kibendera cha Kona kama Mkongojo huku akijishika Kiuno ili kumdhihaki Mourinho.
Akiongea na Wanahabari mara tu baada ya kutambulishwa kama Mchezaji mpya, Eto’o alipuuza madai hayo ya kuwa na bifu na Mourinho na badala yake kusema anamshukuru Mourinho kwa kumleta Ligi Kuu England.

Nae Meneja wa Everton Roberto Martinez amedokeza kuwa huenda Mkongwe huyo wa Cameroon akaivaa Chelsea Jumamosi wakati watakapopambana Goodison Park katika Mechi ya Ligi Kuu England.

Mashali kumvaa Mkenya Novemba 4

 Bondia Thomas Mashali katikati akisaini mkataba wa kucheza na Henry Wandera kutoka Kenya Novemba 4 katika ukumbi wa New Madiba 'Korini' uliopo Tandale Dar es salaam. Wanaoshudia kushoto ni Rais wa Oganaizesheni ya Ngumi za kulipwa nchini TPBO, Yassini Abdallah 'Ustaadh' na promota wa mpambano huo Khamis Ally.
 Rais wa TPBO Yassin Abdallah akirekebisha mkataba wa bondia Thomas Mashali katikati atakayepambana na mkenya Henry Wandera Novemba 4 katika ukumbi wa New Madiba 'Korini' uliopo Tandale Dar es salaam kulia ni  promota wa mpambano huo Khamis Ally 
Bondia Thomas Mashali katikati akiwe Dole Gumba katika mkataba wa kucheza na Henry Wandera kutoka Kenya Novemba 4.
****
BONDIA Thomas Mashali 'Simba Asiyefugika' anatarajia kupanda tena ulingoni Novemba 4 kumvaa Mkenya Henry Wandera katika pambano litakalofanyika katika ukumbi wa New Madiba zamani Korini.
Mashali anapigana akiwa na historia ya kupoteza mpambano wake wa mwisho zaidi ya bondia Mada Maugo ambapo walicheza katika uwanja wa taifa na kupoteza kwa pointi mpambano huo.
Akizungumzia mpambano huo Mashali amesema hatokubali kupoteza tena mchezo huo ukizingatia anachezea nyumbani mahali alipozaliwa na ndipo alipoanzia ngumi maeneo ya Tandale.
"Sintokubali niaibike mbele ya ndugu zangu hivyo nawaambia wapenzi waje kwa wingi kuangalia Mashali anavyofanya kazi yake ya mchezo wa masumbwi.
Naye promota wa mpambano huo Khamis Ally amewahakikishia kuwa sehemu ya kuegeshea magari ni kubwa na ulinzi ni wa kutosha kifupi katika ulinzi tumejipanga vizuri pia siku hiyo kutakuwa na mapambano mengine mazuri ya utangulizi ambapo mabondia wengi wamejitokeza kucheza siku hiyo.
Siku hiyo pia kutakuwa na uuzwaji wa DVD ambazo zinatoa mwanga kwa mchezaji kujua mchezo na kufahamu zaidi mbinu mpya zitumiwazo na mataifa mbali mbali Duniani.
Wakiwemo mabondia bingwa wa dunia kama Manny Pacquaio, Floyd Maywether, Amir Khan, Muhammed Ali, Mike 'Iron' Tyson na wengine wengi wanaotamba na waliotamba katika mchezo huo wa masumbwi Duniani.
Kocha wa Kimataifa wa mchezo wa ngumi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' ametoa wito kwa makampuni mbalimbali kujitokeza kutoa sapoti ya mchezo wa masumbwi kwani ndio mchezo pekee unaoweza kututoa kimasomaso watanzania tukafurahi.

Kikwazo cha Tanzania kuandaa AFCON 2017 HIKI HAPA!

http://bigeye.ug/wp-content/uploads/2014/08/afcon-trophy.pngSHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limeliandikia Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) kutaka kipengele cha kutaka kwanza nchi iandae Fainali za Afrika kwa Vijana ndiyo iwe na sifa ya kuandaa Fainali za Afrika (AFCON) kiondolewe.
TFF ilishapeleka barua CAF kutaka kipengele hicho kiondolewe, na kutaka kijadiliwe katika Congress (Mkutano Mkuu) ijayo ya CAF.
Tanzania imeshaiandikia CAF barua kuomba uenyeji wa Fainali za AFCON za 2017 baada ya Libya iliyokuwa imepewe uenyeji huo kujitoa. Uamuzi wa Tanzania kuomba kuandaa fainali hizo ulifanywa na Kamati ya Utendaji ya TFF iliyokutana Agosti 24 mwaka huu.

Malinzi kuzuru Kanda ya Kaskazini, mechi za Electronic kupigwa TA, BK

http://in2eastafrica.net/wp-content/uploads/2013/10/Jamal-Malinzi.jpgTIMU za Mgambo Shooting na African Sports za Tanga zitapambana Jumapili (Agosti 31 mwaka huu) katika mechi ya majaribio ya matumizi ya tiketi za elektroniki itakayochezwa kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga kwa kiingilio cha sh. 1,000 tu.
Mechi nyingine ya tiketi za elektroniki siku hiyo itachezwa Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba kwa kuzikutanisha timu za Kagera Sugar na Geita Gold SC ya mkoani Geita. Geita Gold iko Daraja la Kwanza.
Kabla ya mechi hizo, Ijumaa (Agosti 29 mwaka huu) saa 3 asubuhi kwenye viwanja hivyo kutakuwa na mafunzo ya matumizi ya tiketi za elektroniki pamoja na jinsi mfumo huo unavyofanya kazi.
Washiriki wa mafunzo hayo ni wasimamizi wa vituo vya Tanga na Bukoba, viongozi wa vyama vya mpira wa miguu vya mikoa ya Kagera (KRFA) na Tanga (TRFA), makatibu na maofisa habari wa klabu za Kagera Sugar, Mgambo Shooting, African Sports na Geita Gold, mameneja wa viwanja vya Kaitaba na Mkwakwani na wasaidizi wao, maofisa usalama wa TRFA na KRFA, wachanaji tiketi, wasimamizi wa milangoni, wasaidizi (stewards) na waandishi wa habari.
Wakati huo huo Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi atatembelea mikoa ya Arusha, Kilimanjaro na Manyara.
Katika ziara hiyo atakutana na viongozi na kuangalia hali hali ya mpira wa miguu katika mikoa hiyo na mahitaji yake. Pia atazungumzia maono (vision) ya TFF katika mpira wa miguu.
Rais Malinzi atawasili mkoani Manyara, Agosti 29 mwaka huu, na ataanza ziara rasmi katika mkoa huo Agosti 30 mwaka huu. Agosti 31 mwaka huu atakuwa Arusha, na kumalizia Septemba 1 mkoani Kilimanjaro.
Katika ziara hiyo, Rais Malinzi atafuatana na Mkurugenzi Msaidizi (Wanachama) wa TFF, Eliud Mvella. Pia Septemba 8 mwaka huu, Rais Malinzi ataanza ziara ya mikoa ya Iringa, Mbeya na Njombe.

Kenya, Rwanda, Uganda kuandaa pamoja Afcon 2017?

http://www.thepeople.co.ke/wp-content/uploads/2014/04/Screen-Shot-2014-04-12-at-8.13.22-AM.png
Sam Nyamweya
NAIROBI, Kenya
KENYA, Rwanda na Uganda zinajadili uwezekano kupeleka maombi Shirikisho la Soka barani Afrika (CAF) kuandaa kwa pamoja fainali za Mataifa ya Afrika (Afcon) 2017.
Mwenyekiti wa Shirikisho la Soka nchini Kenya (FKF), Sam Nyamweya Jumatano alithibitisha kuwa mipango iliyopo ni kwa nchi tatu kuungana kuomba kuwa mwenyeji wa michuano hiyo ya Afrika ili kupunguza gharama.
 "Ni mwenye furaha kwamba Uganda na Rwanda wamepokea kwa mikono miwili wazo la FKF la kuungana kuomba uenyeji wa Mataifa ya Afrika 2017 ambayo ipo wazi kutokana na Libya kujitoa kuwa mwenyeji," alisema Nyamweya.
Libya haitakuwa mwenyeji wa Afcon 2017 kutokana na mapigano ya kisiasa nchini humo ambayo yamesababisha kuchelewa kwa mipango ya ujenzi wa viwanja vitakavyotosha timu 16 zinazoshiriki michuano hiyo.
Nchi hiyo ya Kaskazini mwa Afrika ilipanga kujenga viwanja 11 kwa gharama ya Dola za Kimarekani 314 ikiwa ni pamoja na unaochukua watazamaji 60,000 eneo la kambi ya jeshi jijini Tripoli.
CAF imekaribisha maombi kwa nchi zinazohitaji kuandaa michuano hiyo, na milango ipo wazi hadi Septemba 30. Uamuzi wa nchi itakayopewa nafasi hiyo ya Libya utatolewa mwakani.

Waamuzi, makamisaa kutahiniwa Sept 5

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgGe9znsbu8-SC-K7pcwh_X4R1keXlQEZ6eKkKsYFEcEiMd59lZ-pvZBtMypkT-3vsbM6KKk8-HTX-AtQvj4Qa97tZCeIIr-3noVEg8sxx5YnUqt3q9IZm6Ar3VB-IJWfyVSQQ5vhOcAT9D/s1600/DSC_8192.JPG
Waamuzi wanatakiwa kuwa fiti kama hivi wawapo uwanjani
MTIHANI wa utimamu wa mwili (physical fitness test) kwa waamuzi wanaotaka kuchezesha mechi za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) na Ligi Daraja la Kwanza (FDL) msimu huu utafanyika katika vituo viwili kuanzia Septemba 5-6 mwaka huu.
Waamuzi watakaoshiriki mtihani huo ni wenye beji za Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) na wale wa class one. Pia kutakuwa na semina wa makamishna wanaotaka kusimamia mechi za VPL na FDL ambayo itafanyika Septemba 7 mwaka huu.
Vituo vya mtihani huo ni Dar es Salaam na Shinyanga. Kituo cha Dar es Salaam ni kwa waamuzi na makamishna kutoka mikoa ya Dar es Salaam, Dodoma, Iringa, Kilimanjaro, Lindi, Mbeya, Morogoro, Mtwara, Njombe, Pwani, Ruvuma na Tanga.
Kituo cha Shinyanga ni kwa waamuzi na makamishna kutoka mikoa ya Arusha, Geita, Kagera, Katavi, Kigoma, Manyara, Mara, Mwanza, Rukwa, Shinyanga, Simiyu, Singida na Tabora.
Waamuzi wote ambao wamechezesha VPL na FDL msimu wa 2013/2014 na kupata matatizo au kuondolewa kwenye ligi hawahusiki na mtihani huo.
Washiriki wanatakiwa kufika kituoni siku moja kabla.Wasimamizi ni Charles Ndagala, Israel Mujuni, Issarow Chacha, Joan Minja, Pascal Chiganga, Riziki Majala, Said Nassoro, Salum Chama, Soud Abdi, Victor Mwandike na Zahara Mohamed.

KOZI YA UKUFUNZI WA UTAWALA YA FIFA KUFANYIKA DESEMBA

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg-2-gEQjN-kUTDr5XYxr2xEbeHBZeqpiBVaxDBdXtEHTCTfXJMtFnrt4_lV5Gtu_cfAfZtDPsXoHZdVtbLhyphenhyphenBQsa9f8OgTtpmurttsK_XY2cD3KZVsKqVdjpzI97j-jLPVmU6Qy3ft4BE/s1600/mwesigwa.JPG
Katibu Mkuu wa TFF, Celestine Mwesigwa aliyesimama
SHIRIKISHO la Soka Tanzania,TFF kwa kushirikiana na Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) wameandaa kozi ya ukufunzi wa utawala itakayofanyika Desemba mwaka huu.
Kozi hiyo itakayoendeshwa na wakufunzi kutoka FIFA itafanyika jijini Dar es Salaam kuanzia Desemba 1 hadi 5 mwaka huu, ambapo sifa ya chini ya elimu kwa wanaotaka kushiriki ni kidato cha nne.
Kwa wanaotaka kushiriki kozi hiyo wanatakiwa kutuma maombi yao kwa Katibu Mkuu wa TFF. 
Mwisho wa kupokea maombi hayo ni Septemba 5 mwaka huu ambapo wanatakiwa pia kuwasilisha nakala za vyeti vyao vya kitaaluma.

Wenger akiri Giroud kuwa nje, akiwakana Falcao, Song Emirates

http://static.goal.com/310700/310713_heroa.jpg
Arsene Wenger
http://www.footmercato.net/images/a/falcao-cible-potentielle-des-gunners_101362.jpg
Falcao
http://www.standard.co.uk/incoming/article8026635.ece/alternates/w620/alex-song.jpg
Alex Song
MENEJA wa Arsenal , Arsene Wenger amethibitisha kuwa Olivier Giroud anatarajiwa kuwa nje ya uwanja hadi angalau Desemba kutokana na majeraha ya kifundo cha mguu lakini akasisitiza kuwa hana mpango wa kusaka mshambuliaji mwingine yeyeote akiwakana Radamel Falcao, Alex Song na Danny Welbeck.
Giroud (27), ambaye alikuwa mfungaji bora wa Arsenal msimu uliopita akitupia mabao 22 katika michuano yote, anatarajiwa kuwa nje ya uwanja kwa muda wa kufikia miezi minne kufuatia kufanyiwa upasuaji wa 'enka' aliyoumia katika mechi ya Jumamosi iliyomalizika kwa sare ya 2-2 ugenini dhidi ya Everton katika Ligi Kuu ya England.
Alipoulizwa kuhusu Falcao, Wenger alisema nyota huyo wa Napoli hayumo katika mipaka ya bei anayoweza kutoa na akabainisha kwamba pia hamhitaji Welbeck. Kuhusu uwezekano wa kumsajili Song, Mfaransa huyo alisema: "Alex Song hatarejea hapa."
Kocha huyo akasema kuhusu nyota wa Chile, aliyefunga goli la ushindi katika mechi ya "kapu" ya Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya dhidi ya Besiktas: "(Alexis anaweza kucheza kama mshambuliaji wa kati) kwa miezi mitatu ama minne? Anaweza kucheza pale maisha yake yote.
"Nilimnunua acheze kama mshambuliaji wa kati, siyo kwenye wingi. Naamini huwezi kununua kila pale mchezaji anapoumia. Kama umepata majeruhi Septemba mosi bado utatakiwa kuishi nalo.
"Nilimnunua Sanchez awe mshambuliaji, Walcott anaweza kuwa mshambuliaji mzuri, (Lukas) Podolski anaweza kucheza pale, (Yaya) Sanogo ni mshambuliaji mzuri sana, (Joel) Campbell ukimuuliza yeye ni nani, atasema ni mshambuliaji. Wote ni wachezaji wa ubora wa juu.
"Kupata wachezaji bora zaidi ya tulionao itakuwa ngumu sana."

BRAD PITT NA ANGELINA JOLIE WAOANA!


Jolie na Pit walichumbiana mwaka 2012
NYOTA wa filamu duniani, Brad Pitt na Angelina Jolie ambao wameishi kwa muda mrefu kama mke na mume, wamefunga ndoa rasmi.
Pitt, mwenye umri wa miaka 50 na Jolie mwenye umri wa miaka 39, walifunga pingu za maisha nchini Ufaransa Jumamosi na kumaliza miaka mingi ya sintofahamu ikiwa watawahi kuoana.
Waigizaji hao inaarifiwa walioana katika sherehe iliyofanywa kimya kimya katika kanisa ndogo eneo la Chateau Miraval Ufaransa.
Sherehe hio ilifanyika kwa faragha na kuhudhuriwa tu na familia za wawili hao pamoja na marafiki zao.
Watoto wao pia walihusishwa katika sherehe hiyo.
Jolie aliambatana na wanawe wakubwa wa kiume, Maddox na Pax, wenye umri wa miaka 13 na 10 mtawalia.
Watoto wao wa kike Zahara na Vivienne, wote waliwarushia mauwa wazazi wao walipokuwa wanatembea kuelekea kanisani. Inaarifiwa sherehe hiyo haikufuata dini yoyote.
Wacheza filamu hao walianza uhusiano wao wa kimapenzi mwaka 2005 walipoigiza katika filamu ya 'Mr and Mrs Smith'. Walichumbiana Aprili mwaka 2012.
Kabla ya ndoa yake kwa Jolie, Pit alikuwa amemuoa muigizaji, Jennifer Aniston, wakati Jolie alikuwa ameolewa na Jonny Lee Miller na Billy Bob Thornton. Ndoa yake kwa wawili hao ilivunjika
BIG

Thursday, August 28, 2014

Ronaldo ndiye Mchezaji Bora Barani Ulaya

http://www.free-top10.com/Data/Sites/1/Free/Free%20Video/Free-Video-Ronaldo-European-Football-Player-Of-The-Year.jpg 
http://www.sokkaa.com/wp-content/uploads/Neuer-Christiano-and-Robben.jpg
Waliokuwa kwenye Tatu Bora Ulaya
MSHAMBULIAJI nyota wa Ureno anayeichezea klabu ya Real Madrid, Cristiano Ronaldo ametangazwa kuwa Mchezaji Bora wa Ulaya.
Mkali huyo alipata tuzo hiyo baada ya kuwaangusha wachezaji wenzake wawili wanaoichezea Bayern Munich ya Ujerumani.
Ronaldo alitangazwa jioni hii kushinda tuzo hiyo mbele ya Arjen Robben na kipa Manuel Neuer wa Bayern Munich.

Haya ndiyo makundi ya Ligi ya Mabingwa Ulaya 2014

MAKUNDI ya Ligi ya Mabingwa Ulaya yametangazwa jioni hii ambapo Mabingwa wa Engand, Manchester City wamejikuta wakiangukia kundi moja na Bayern Munich huku Liverpool ikiangukia kundi B lenye vigogo Real Madrid.
Kwa mara nyingine Arsenal wameangukia kundi gumu, safari hii wakiwa D lenye timu za Arsenal, 
Borussia Dortmund, 
Galatasaray na Anderlecht.
Chelsea wao wako kundi G lenye timu za 
Schalke, 
Sporting
 na Maribor.
Yacheki makundi yote hapo chini:
Kundi A


Atletico Madrid, Juventus,
 Olympiacos na 
Malmo
Kundi B
Real Madrid, 
Basle, 
Liverpool,
 Ludogorets
Kundi C
Benfica, 
Zenit St. Petersburg,
 Bayer Leverkusen na Monaco
Kundi D
Arsenal, 
Borussia Dortmund,
 Galatasaray na Anderlecht
Kundi E
Bayern Munich,
 Man City, 
CSKA Moscow na 
Roma
Kundi F
Barcelona, 
PSG, 
Ajax, 
Apoel Nicosia
Kundi G
Chelsea,
Schalke, 
Sporting
 na Maribor
Kundi H
FC Porto,
 Shakhtar Donetsk,
 Athletic Bilbao 
na BATE

Michel Platin achomoa kuwania Urais FIFA

KATIKA kinachoonekana kama kumgwaya Rais wa Shirikisho la Soka Duniani, FIFA, Sepp Blatter, Rais wa Shirikisho la Soka barani Ulaya,UEFA, Michel Platini amesema hatagomea nafasi hiyo ya dunia kama ilivyokuwa ikivumishwa.
Platin amesea ni vyema kutilia mkazo kibarua chake cha sasa kuliko UEFA badala ya kushiriki uchaguzi huo wa FIFA.
http://static.guim.co.uk/sys-images/Football/Pix/pictures/2011/5/31/1306848649705/Michel-Platini-and-Sepp-B-007.jpg
Platin (kushoto) na Blatter
Nyota huyo wa zamani wa kimataifa wa Ufaransa alikuwa akiaminika kuwa anafikiria kugombea nafasi nhiyo lakini alifafanua katika mkutano wa vyama 54 vya soka barani Ulaya uliofanyika huko Monte Carlo kuwa atabakia katika nafasi yake hiyo.
Mjumbe wa kamati ya utendaji ya FIFA, Michel D’Hooge alikaririwa akidai kuwa ni ujumbe chanya uliotolewa na Platini na amefurahi kwani inamaanisha kuwa safari hii hakutakuwa na ushindani kati FIFA na UEFA. 
Platini amekuwa akimkosoa vikali Blatter kwa zaidi ya mara moja na mapema mwaka huu alieleza kuwa kiongozi huyo mwenye umri wa miaka 78 amekwisha kama mtu sahihi wa kuiongoza FIFA. 
Blatter aliwahi kudai kuwa ataachia ngazi mwishoni mwa muhula wake huu wa nne lakini alibadili mawazo na uamuzi wake baadae na kuweka wazi kuwa atatetea tena kiti chake katika uchaguzi ujao. 
Blatter amekuwa akifanya kazi FIFA toka mwaka 1975 na alichaguliwa kwa mara ya kwanza kushika nafasi ya urais mwaka 1998.

Alexis Sanchez amkuna Wenger Arsenal

http://pbs.twimg.com/media/BuDK8W3IIAAy0Qv.jpgKIWANGO alichokionyesha mshambuliaji Alexis Sanchez kimemkuna Kocha wa timu ya Arsenal, Arsene Wenger.
Meneja huyo wa Ze Gunners amesema kiwango cha Alexis Sanchez alichoonyesha katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Besiktas imeinyesha kuwa ana ubora wa kumfanya afanikiwe katika Ligi Kuu nchini Uingereza.
Nyota huo aliyesajiliwa kwa paundi milioni 35 akitokea Barcelona alifunga bao pekee katika mchezo huo na kuipa Arsenal ushindi mwembamba wa 1-0 katika Uwanja wa Emirates na kuwafanya kufuzu hatua ya makundi ya michuano hiyo.
Akihojiwa Wenger amesema Sanchez alionyesha mchezo mzuri kwani alikuwa akielewana vyema na wenzake na alikuwa akionyesha ari ya kupambana huku akiwa hatari anapokuwa katika lango la adui. Kocha huyo aliendelea kudai kuwa ubora huo ndio unaotakiwa katika ligi. Bao hilo la kwanza kwa mchezaji huyo toka ajiunge na timu hiyo alilifunga muda mchache kabla ya mapumziko na kuingiza Arsenal katika ratiba ya makundi yaliyopangwa leo.
Hata hivyo Wenger amekiri kuwa aliingiwa na woga kidogo wakati beki wake Mathieu Debuchy alipotolewa nje kwa baada ya kupewa kadi ya pili ya njano zikiwa zimebaki dakika 14 mpira kumalizika.

Kocha Mexime awakuna wachezaji Mtibwa Sugar

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjVzufGN29F3EQO9M7DaKGF8TdIspdiztoQgVTGD8zWO2W1YB8ab9wJMCTc5-pqvYnHKlB2JLmq-wB7XAxld2-4Kh7Xb9sz0CVRFZKAKfjnWABu_wB-VYdQ1hq18g8-TqWULxVQIjQbjic/s1600/IMG_0621.JPG
Benchi la ufundi la Mtibwa Sugar
MSHAMBULIAJI nyota wa Mtibwa Sugar, Abdallah Juma amemwagia sifa kocha wake, Mecky Mexime huku akiitabiria Mtibwa kufanya vema kwenye msimu wa Ligi Kuu Tanzania Bara.
Abdallah maarufu kama 'AJ' aliyeifungia Mtibwa mabao manne msimu uliopita ikiwamo hat trick wakati wakiizamisha JKT Oljoro, alisema tangu kocha wao amerejee toka masomoni amekuwa akiwapa mbinu ambazo zinawafanya kuzidi kuwa wakali na kufufua ari zao.
Nyota huyo wa zamani wa AFC Arusha, Kagera Sugar na Simba, alisema kwa namna kocha wao anavyowapa mbinu za kinazohusu mikasa aliyokutana nayo katika maisha yake.
"Kocha wetu ni kama 'amezaliwa' upya, yupo tofauti na msimu uliopita kwa jinsi anavyotupa mbinu mpya ambazo tunaamini zitaifanya Mtibwa Sugar itishe kwenye ligi ya msimu huu," alisema.
Abdallah alisema mpaka Septemba 20 ligi itakapoanza kwa wao kuwakaribisha Yanga kwenye uwanja wa Jamhuri watakuwa wameiva na kuanza mbio zao za kurejesha heshima yao baada ya kushindwa kufanya vema ligi iliyopita.
Mshambuliaji huyo alisema anaamini msimu wa 2014-2015 utakuwa wa Mtibwa Sugar licha ya kwamba wadau wa soka wanaziangalia Simba, Yanga, Azam na pengine Mbeya City baada ya msimu uliopita kupanda Ligi Kuu na kuonyesha kiwango cha hali ya juu.

Misri yaongeza idadi inayowania AFCON 2017

CHAMA cha Soka nchini Misri kiomeongeza idadi ya nchi zinazowania uaandaaji wa Fainali za Afrika 2017 baada ya kujitosa kwenye kinyang'anyiro hicho ambacho Tanzania nacho imeingia tangu juzi.
Misiri ilianda mara ya mwisho fainali hizo mwaka 2006 na inawania nafasi hiyo na nchi nyingine baada ya waliokuwa wawe wenyeji, Libya kutangaza kujitoa.
Vita vya wenyewe kwa wenyewe vinavyoendelea nchini Libya viwalazimisha kujitoa kwa mara ya pili baada ya mwaka jana kushindwa na kuiachia Afrika Kusini kuandaa.
Kutokana na hali hiyo ambayo imeikwaza nchi hiyo kutekeleza mikakati ya ujenzi wa viwanja na kuifanya Shirikisho la Soka Barani Afrika-CAF kutafuta mwenyeji mwingine wa michuano hiyo. 
Chanzo kimoja cha habari kutoka ndani ya EFA kimebainisha nia ya kutaka kuwa mwenyeji wa michuano hiyo lakini bado hawajafanya uamuzi wa mwisho kuhusiana na suala hilo. 
Makamu wa rais wa EFA Hassan Farid naye alithibitisha nia yao hiyo lakini amesema bado wanataka kuzungumza na baadhi ya wizara serikalini ili kupata ushirikiano wao. 
Misri ni mojawpao ya nchi chake barani Afrika zenye miundo mbinu mizuri ya kuandaa michuano mikubwa kama Afcon.

Rooney nahodha mpya England Hodgson atangaza kikosi

http://static.guim.co.uk/sys-images/SPORT/Pix/pictures/2012/6/27/1340795627494/Roy-Hodgson-008.jpg
Sasa wewe ni nahodha wa kikosi usiniangushe, Kocha Hodgson akifurahia jambo na Rooney
NYOTA wa klabu ya Manchester United, Wayne Rooney ametajwa kuwa nahodha mpya wa timu ya taifa ya Uingereza Three Stars na kocha Roy Hodgson. 
Nyota huyo mwenye umri wa miaka 28 amechukua kitambaa hicho akimrithi kiungo wa Liverpool Steven Gerrard aliyestaafu rasmi soka la kimataifa baada ya nchi hiyo kutolewa katika michuano ya Kombe la Dunia. 
Mshambuliaji huyo nyota amefunga mabao 40 katika mechi 95 za kimataifa na alitajwa kuwa nahodha wa United na kocha Louis van Gaal mapema mwezi huu. 
Rooney alithibitisha uteuzi huo katika mtandao wake na kudai kuwa ataitumikia nafasi hiyo kwa bidii na kujivunia huku akidai kuwa zilikuwa ndoto zake za muda mrefu. 
Rooney ataanza kuvaa beji rasmi akiwa na timu ya taifa Septemba 3 mwaka huu wakati Uingereza watakapoikaribisha Norway katika Uwanja wa Wembley kwa ajili ya mchezao wa kirafiki wa kimataifa.
Kocha huyo amekitangaza kikosi cha wachezaji wake watakaocheza mechi hiyo na ile ya kuwania kufuzu EURO 2016 dhidi ya Uswisi akiwajumuisha wachezaji wanne ambao hawajawahi kabisa kuichezea timu hiyo.
Makinda hao waliotwa katika timu hiyo ni Jack Colback, Calum Chambers, Danny Rose na Fabian Delph, huku Andros Townsend akirejeshwa kikosini tena.
 
Kikosi kamili ni kama ifuatavyo; MAKIPA: Fraser Forster (Southampton), Ben Foster (West Bromwich Albion), Joe Hart (Manchester City)
MABEKI: Leighton Baines (Everton), Gary Cahill (Chelsea), Calum Chambers (Arsenal), Phil Jagielka (Everton), Phil Jones (Manchester United), Danny Rose (Tottenham Hotspur), John Stones (Everton)
VIUNGO: Jack Colback (Newcastle United), Fabian Delph (Aston Villa), Jordan Henderson (Liverpool), James Milner (Manchester City), Alex Oxlade-Chamberlain (Arsenal), Raheem Sterling (Liverpool), Andros Townsend (Tottenham Hotspur), Jack Wilshere (Arsenal)
WASHAMBULIAJI: Rickie Lambert (Liverpool), Wayne Rooney (Manchester United), Daniel Sturridge (Liverpool), Danny Welbeck (Manchester United).

Eto'o, Xabi Alonso kama Lampard soka la kimataifa

http://www.tiemporeal.mx/files/image/0/416/5117b02d5f66c.jpg
Samuel Eto'o
frank-lampard-volley
Lampard
http://www1.pictures.zimbio.com/gi/Xabi+Alonso+Portugal+v+Spain+UEFA+EURO+2012+3JngxodQREjl.jpg
Xabi Alonso

SIKU chache baada ya Frank Lampard kutangaza kustaafu soka la kimataifa – jana ilikuwa siku nyingine kwa wanasoka wawili wa kimataifa barani nao walitangaza uamuzi wa kuachana na soka la kimataifa.

Samuel Eto’o na Xabi Alonso kwa wakati tofauti jana walitumia mitandao ya kijamii kutangaza uamuzi wao wa kuachana na soka la kimataifa.
Alianza Xabi Alonso kupitia mtandao wa Twitter kutangaza kustaafu kuichezea timu ya taifa ya Spain.
Kiungo huyo wa Real Madrid ameshaitumikia Spain kwa muda wa miaka 11 na ameifungia nchi hiyo magoli 16 katika mechi 114.
Wakati huo huo mfungaji mabao mengi zaidi wa timu ya taifa ya Cameroon Samuel Eto’o ametangaza kustaafu soka la kimataifa.
Mshambuliaji huyo ambaye ameifungia Cameroon mabao 56 amejiunga na Everton ya Uingereza juzi .
Kufuatia kauli hiyo mshambuliaji huyo sasa hatakuwepo katika kipindi chote cha cha kombe la mataifa bingwa barani Afrika mwezi Januari mwakani.
“Nataka kuwajuza kuwa nimestaafu mashindano yote ya kimataifa ”aliandika Etoo katika mtandao wake wa kijamii wa Instagram .

Bosi wa zamani wa TBS atupwa jela miaka mitatu

Charles Ekelege akiwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam leo ambapo alihukumiwa kutumikia kifungo cha mwaka mmoja baada ya kupatikana na hatia ya matumizi mabaya ya madaraka na kulipa faini ya sh.milioni 68.
Ekelege akiteta jambo na kijana aliyedaiwa kuwa ni mtoto wake.


 Ekelege akiteta jambo na familia yake akiwa Mahakamani hapo.

Hapa Ekelege akiwa amekaa nje ya Mahakama hiyo na familia yake  kabla ya kuhukumiwa.

 Askari polisi akiwa na familia ya Ekelege (wa pili kulia), wakati akitoka kwenye mahakama hiyo ----
Aaliye kuwa Mkurugenzi wa Shirika la viwango Tanzania TBS Bw Charles Hekelege, ametiwa hatiani na kufungwa miaka mitatu jela baada ya kukutwa na kosa la kuhujumu uchumi. Hekelege amefungwa jumla ya miaka mitatu jela kwa makosa matatu kila kosa moja mwaka mmoja kwa maana hiyo atatumikia mwaka moja gerezani.
www.habariza jamii.com

Afande Bright aachia mpya za Injili

Kava la albamu ya Afande Bright linavyoonekana kwa wanayoitaka wanaweza kuwasiliana kwa namba zinazoonekana chini kushoto kwenye kava hilo
Afande Bright katika pozi
MSANII aliyekuwa anakuja juu kwenye muziki wa kizazi kipya aliyejitosa kwenye muziki wa Injili baada ya kuponea chupuchupu kufa ajalini, Bright Mbwilo 'Afande Bright' ameachia albamu yake ya kwanza ya miondoko hiyo mipya iitwayo 'Ahsante Bwana'.
Akizungumza na MICHARAZO, Bright alisema albamu hiyo ambayo kwa sasa ipo sokoni wakati akijipanga kuitengenezea video yake, ina nyimbo nane.
Bright alizitaja nyimbo hizo ni 'Ahsante Bwana', 'Upendo', 'Vita', 'Hamjui', 'Itakuwaje', 'Twakuheshimu', 'Jinsi Gani' na 'Vita Remix', huku akisema karibu nyimbo zote ni simulizi la kweli zilizowahi kumpata au kuwapata watu wake wa karibu.
"Baada ya kunusurika katika ajali mjini Morogoro, nimeamua kumgeukia Mungu na sasa naimba muziki wa Injili nikiwa nimeachia albamu inayofanya vyema sokoni na kwenye vituo vya redio iitwayo 'Ahsante Bwana' yenye nyimbo nane," alisem Bright.
Aliongeza kabla ya kutumbukia kwenye muziki huo wa kumtukuza MUNGU alikuwa kiimba muziki wa kizazi kipya na aliwahi kutoa albamu moja iliyofanya vyema sokoni iitwayo 'Tanzania' iliyokuwa na nyimbo nane.
Baadhi ya nyimbo hizo ni 'Tanzania', 'Ndani ya Dancehall', 'Zako Style', 'Kiza Kinene', 'Jakaya', 'Nimedata', 'Hawapendi', 'Watanzania', 'Nikiachwa leo' na 'Leave Me Alone'.