STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, December 19, 2014

Mesul Ozil akaribia kurudi Arsenal

http://www.brandish.tv/wp-content/uploads/2014/10/36204.jpgKIUNGO nyota wa klabu ya Arsenal, Mesut Ozil amebainisha kuwa anakaribia kurejea kutoka katika majeruhi yaliyokuwa yakimsumbua na kusisitiza ataweza kubadilisha mwelekeo wa timu hiyo.
Nyota huyo wa kimataifa wa Ujerumani amecheza mechi tisa pekee msimu huu, baada ya kupata majeraha ya goti mwezi Oktoba mwaka huu.
Arsenal imekuwa ikiyumba toka kuumia kwa nyota huyo wa zamani wa Real Madrid ambapo kwasasa wanashika nafasi ya sita katika msimamo wa Ligi Kuu.
Ozil aliuambia mtandao wa klabu hiyo anafanya bidii kila siku ili aweze kuwa fiti na hadhani kama itakuwa ni kipindi kirefu sana kabla ya hajarejea tena uwanjani.
Ozil aliendelea kudai kuwa ana matumaini ya kurejea mazoezini tena haraka iwezekanavyo ili aweze kuisaidia timu yake.
Arsenal ina kibarua kizito Jumapili hii pale watakaposafiri kuifuata Liverpool katika Uwanja wa Anfield na ushindi katika mchezo huo utakuwa muhimu ili kuwaweka katika nafasi nzuri ya kukaa katika nafasi nne za juu katika msimamo wa ligi

Manchester City kuikamata Chelsea kesho?

http://news.bbcimg.co.uk/media/images/64785000/jpg/_64785248_goal-getty.jpgMABINGWA watetezi wa Ligi Kuu ya England, Manchester City ambayo imerudi katika kasi itakuwa na nafasi ya kutoa presha kubwa katika mbio za ligi hiyo dhidi ya vinara Chelsea kwa mara ya kwanza msimu huu endapo kesho watashinda dhidi ya Crystal Palace.
Wakati Chelsea haitacheza dhidi ya Stoke City hadi Jumatatu, ushindi wa City kwenye Uwanja wa Etihad dhidi ya Palace ambayo imeshindwa kuibuka na ushindi kwenye mechi nne za Ligi Kuu, itakifanya kikosi hicho cha Manuel Pellegrini kufikisha pointi 39 ambazo ni sawa na za vijana wa Jose Mourinho.
Msimu huu vinara Chelsea wamewahi kuongoza kwa pointi nane zaidi, lakini City imeshinda mechi tano za mwisho za Ligi Kuu, wakati Frank Lampard alifunga na kuiwezesha timu hiyo ya Pellegrini kuibuka na ushindi wa 1-0 dhidi ya timu inayoburuza mkia ya Leicester City mwishoni mwa wiki iliyopita hivyo kuikaribia kwa pointi.
Hata hivyo, City itashuka uwanjani bila kumenyana na timu hiyo inayoshika nafasi ya 16 katika ligi, bila mshambuliaji wao Sergio Aguero, Stevan Jovetic na Edin Dzeko, wakati pia nahodha na beki wa kati Vincent Kompany naye akikumbwa na majeraha kwenye mechi dhidi ya Leicester.
Lakini licha ya lundo hilo la majeraha katika safu ya ushambuliaji, Pellegrini anaamini kikosi chake kitapata wachezaji sahihi wakuwasaidia kuibuka na ushindi dhidi ya Palace.
"Wiki hii tutafanya kazi na wachezaji ambao wataweza kucheza nafasi hiyo," Pellegrini aliwaambia wanahabari. "Kwa kipindi hiki tunajaribu kuwaweka fiti wachezaji wote kwa sababu hatuna mshambuliaji.
"David Silva, Samir Nasri na wengine waliobaki pia wanafunga hivyo lazima tuone katika wiki njia gani iliyo sahihi kucheza kwa siku zijazo hadi washambuliaji wetu watakapokuwa fiti."

Angel di Maria amfunika Lionel Messi kwao Argentina

http://media.themalaysianinsider.com/assets/uploads/articles/lionel-messi-reuters-062214.jpg.JPGKIUNGO wa Manchester United, Angel Di Maria amewapiku Lionel Messi na Sergio Aguero na kushinda tuzo ya mchezaji bora wa mwaka wa Argentina anayecheza soka nje ya nchi.
Di Maria (26), alikuwa miongoni mwa kikosi cha Argentina kilichofurukuata na kufika fainali ya Kombe la Dunia nchini Brazil, wakati pia alikuwa silaha muhimu kwa klabu yake ya zamani ya Real Madrid wakati ikiutwaa ubingwa wa Ulaya kwa mara ya 10 (La Decima) msimu uliopita.
Mchezaji huyo wa Kimataifa wa 'The Albiceleste', ambaye pia ametwaa Kombe la Mfalme (Copa del Rey) na UEFA Super Cup akiwa na Madrid 2014, amekuwa mchezaji ghali zaidi katika historia ya usajili Uingereza  baada ya Agosti kuijunga na United kwa paundi milioni 59.7.
Di Maria amefunga mabao matatu kwenye mechi 11 tangu ajiunge na Mashetani Wekundu (Red Devils) hao, ingawa ametupwa nje mechi tatu kutoka na kuwa majeruhi.
Hiii ni mara ya kwanza kwa Messi kushindwa kutwaa tuzo hiyo ya 'Olimpia de Plata' tangu 2006, licha ya mchezaji huyo wa Barcelona kufunga mabao 56 kwa klabu na nchi yake mwaka huu na kutwaa tuzo ya Mpira wa Dhahabu kwa nchi yake kutokana na kuwa mchezaji bora wa michuano ya Kombe la Dunia.
Aguero pia amefurahia kuvutia mwaka huu baada ya kuisaidia Manchester City kutwaa ubingwa wa England msimu uliopita wakati pia kwa sasa akiongoza kwa ufungaji akiwa na mabao 14 msimu huu.
Kadhalika, Lucas Pratto wa Velez Sarsfield ameshinda tuzo ya mchezaji bora wa ndani wa Argentina.

Falcao anogewa OT, awang'ang'ania Mashetani Wekundu

http://static.guim.co.uk/sys-images/Football/Pix/pictures/2014/10/5/1412513205570/Radamel-Falcao-celebrates-012.jpg
Falcao akishangalia moja ya mabao yake
MSHAMBULIAJI nyota wa Colombia anayeichezea Manchester United kwa mkopo, Radamel Falcao amesisitiza kwamba anataka kubaki Manchester United lakini anafahamu kwamba anapaswa kukomaa ili apate nafasi zaidi ya kucheza katika kikosi cha Louis van Gaal.
Dili la kulipa euro milioni 56 kwa Monaco ili kubadili uhamisho wake wa mkopo uwe wa kudumu tayari umeafikiwa, ingawa Man U wanalo chaguo la kusubiri hadi mwisho wa msimu kuona kama wanaridhishwa na uzima na kiwango cha strika huyo kabla ya kukamilisha uhamisho.
Falcao amecheza mechi nane tu za Ligi kuu ya England msimu huu kutokana na maumivu ya 'kiazi' cha mguu na mshambuliaji huyo amesema hatma yake bado haijaamuliwa.
"Kwa upande wangu, ndiyo, nataka kubaki, lakini lazima nichanganue hali iliyopo," alisema Falcao.
"Nitaona kama nitachezeshwa zaidi na kuona maamuzi yatakayochukuliwa na bodi. Lakini kwa upande wangu, nataka kubaki.
"Naona kwamba timu tayari inanihitaji. Kila ninapopata fursa ya kuingia uwanjani najaribu kufanya kilichobora kwa ajili ya kocha na kuisaidia timu.
"Kila mcheza soka anataka kuchezeshwa, hakuna anayekuwa na furaha asipocheza, anapokaa benchini, lakini kila ninapopewa fursa, iwe kwa dakika tano, 10, 20 au 90, najituma niwezavyo."

Makubwa yaibuka kifo cha Ebosse, yadaiwa alipigwa

http://i.ytimg.com/vi/nRgfnT26dgY/hqdefault.jpg
Ebosse siku alipokuwa akiipigiania roho yake

http://news.bbcimg.co.uk/media/images/79828000/jpg/_79828541_ebosse.jpg
Ebosse enzi za uhai wake akiwajibika uwanjani

IMEFAHAMIKA kuwa nyota wa kimataifa wa Cameroon, Albert Ebosse aliyefariki uwanjani wakati wa mechi ya Ligi Kuu ya Algeria kuwa alipigwa na siyo kama alishambuliwa na kitu chenye nchi kali dimbani.
Vipimo vipya vya uchunguzi vimedai kuwa mchezaji huyo aliyekuwa akiichezea JS Kabylie alifariki kwa kupigwa na sio kupigwa na kitu chenye ncha kali kama ilivyodaiwa hapo awali. 
Mshambuliaji huyo aliyekuwa na umri wa miaka 24 alifariki dunia Agosti mwaka huu baada ya timu yake kufungwa katika mchezo wa soka. 
Matokeo ya uchunguzi uliofanywa na mamlaka za Algeria ulibaini kuwa mchezaji huy alifariki dunia kwa kupigwa na kitu chenye ncha kali kichwani. 
Lakini vipimo vipya vilivyofanyika kwa ombi la wanafamilia vimedai kuwa kifo cha Ebosse kimetokana na kushambuliwa kwa kupigwa ikihisiwa kuwa katika chumba cha kubadilishia nguo. 
Ripoti hiyo ya Andre Moune inadai kuwa Ebosse alijeruhiwa maeneo kadhaa katika mwili wake huku kukiwa na dalili za kupambana wakati akishambuliwa. Familia ya mchezaji huyo imesema itafikisha ushahidi huo mpya kwa Shirikisho la Soka la Cameroon sambamba na Shirikisho la Soka la Afrika kwa ajili ya hatua zaidi.

Thursday, December 18, 2014

Chelsea wapewa Liverpool Kombe la Ligi, Spur v Sheffield Utd


http://i2.mirror.co.uk/incoming/article4591109.ece/alternates/s615/Liverpool-v-Chelsea.jpg
Kivumbi kitakuwa kwao Januari 20/27
http://www.capitalonecup.co.uk/cms_images/trophypitchside800x600304-589134_478x359.jpg
DROO ya Nusu Fainali ya michuano ya Kombe la Ligi maarufu kama Capital One, imetoka ikionyesha kuwa Chelsea watakutana uso kwa uso na Liverpoo ambayo usiku wa jana ilipata ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya timu ya AFC Bournemouth.
Vijogoo vya London ya Kaskazini, Tottenham Hotspur walioifumua Newcastle United kwa mabao 4-0 yenyewe imepangwa kumenyana na Sheffiled United katika hatua hiyo ya nusu fainali.
Chelsea walioilaza Derby Count mabao 3-1 wataanzia ugenini kwenye uwanja wa Anfield na kama mambo yataenda kwa sare watarudi nyumbani kuivutia pumzi wapinzani wake.
Kwa upande wa Spurs wenyew wataanza nyumbani kabla ya kumalizia ugenini na mechi za mkondo wa kwanza zitachezwa Januari 20, 2015 na zile za marudiano kujua timu mbili zitakazocheza fainali.

Polisi yazuia mazishi ya Aisha Madinda, kisa....!

HABARI zilizopatikana hivi punde zinasema kuwa Jeshi la Polisi limesitisha kufanyika kwa mazishi ya aliyekuwa Mnenguaji wa bendi za African Stars 'Twanga Pepeta' Aisha Madinda,ili kufanya uchunguzi wa kina juu ya kifo chake.
Akihojiwa katika kipindi cha XXL, mtoto mkubwa wa marehemu alisema wamekubaliana na serikali wafanye uchunguzi wa kinaili hata kama akizikwa basi azikwe ikifahamika kipi kilichomuua, kwa sababu mama yake hakuwa mgonjwa kabla ya kukumbwa na mauti.
Tangu jana baada ya kusambaa kwa kifo cha mnenguaji huyo aliyepitia makundi mbalimbali kabla ya kutua katika shoo za bendi, kulikuwa na maelezo ya kutatanisha juu ya kifo chake na mtoto huyo wa marehemu, aitwaye Feisal Mbegu alinukuliwa kuwa mama yake hakuwa mgonjwa na aliwasiliana naye jana yake akiwa buheri wa afya.
Inaelezwa kuwa mwili wa Aisha Madinda ulipelekwa hospitali ya Mwananyamala akiwa keshafariki na mwanamke mmoja anayetajwa kuwa rafikie aitwaye, Samira, huku ikielezwa kuwa aliondoka kwao KIgamboni ili kwenda kwenye mazoezi ya bendi ya Twanga Pepeta ambapo hata hivyo uongozi wa bendi hiyo umekana msanii wao huyo wa zamani kuwahi kwenda kufanya mazoezi kwao.
Awali mazishi hayo yalipangwa kufanyika leo nyumbani kwa wazazi ao, Kigaamboni.

Prof Tibaijuka agomaa kujiuzulu, adai hata JK atamshangaa akifanya hivyo

http://www.fullshangweblog.com/wp-content/uploads/2014/06/DSC_0019.jpg
Prof Tibaijuka
TOFAUTI na matarajio ya wengi kwamba huenda angefuata nyayo za Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Fredrick Werema aliyetangaza kubwaga manyanga kwa hiari yake, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Prof. Anna Tibaijuka amegoma kujiuzulu kwa kudai haoni sababu ya kufanya hivyo
Akziungumza mapema leo jijini Dar es Salaam, Waziri huyo alisema watu wanaona kujiuzulu ni 'fasheni' ila kwake hayupo kwenye mkumbo huo na wala hana mpango huo kabisa.
"Nikijiuzulu hata Rais atanishangaa maana katika yale mapendekezo ya Bunge hakuna sehemu iliyonitaka kujiuzulu" alisema Prof Tibaigana.
Prof Tibaijuka, alisema kilichomfanya akutane na waandishi wa habari ni kuzungumzia yale aliyokosa nafasi ya kutolea ufafanuzi juu ya tuhuma zinazomkabili katika sakata la uchotwaji wa fedha za Akaunti ya Tegeta Escrow.

Wednesday, December 17, 2014

Ander Herrera akanusha kupanga matokeo

http://www4.pictures.zimbio.com/gi/Manchester+United+v+Valencia+ODBuEmnisftx.jpg
KIUNGO wa klabu ya Manchester United, Ander Herrera amesisitiza kuwa hajawahi kushiriki zoezi lolote la upangaji matokeo wakati akiitumikia timu ya Real Zaragoza.
Nyota huyo wa kimataifa wa Hispania ametajwa katika kundi la watu 41 wakiwamo  wachezaji, makocha na wakurugenzi katika uchunguzi wa kashfa ya upangaji matokeo katika Ligi Kuu nchini Hispania maarufu kama La Liga.
Herrera aliandika katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa facebook kuwa hajawahi na kamwe hatathubutu kujihusisha na suala la upangaji matokeo kwani anaupenda mchezo wa soka na anaamini katika mchezo wa haki ndani na nje ya uwanja.
Waendesha mashitaka katika kashfa hiyo wanadai kuwa fedha taslimu euro 965,000 zililipwa kwa kocha Javier Aguirre na wachezaji tisa wa Zaragoza, ikiwa ni pamoja na Herrera, kabla ya mchezo wa La Liga mwishoni mwa msimu wa 2010-2011.
Herrera aliondoka Zaragoza na kujiunga na timu ya nyumbani kwao ya Athletic Bilbao mwezi Agosti 2011, kabla ya kujiunga na United mwezi Juni 2014.
Wengine waliohuzsishwa na kadhia hiyo ni nahodha wa Atletico Madrid, Gabi na beki Montero na kocha wa zamani wa Zaragoza aliyepo Japan kwa sasa.

Waziri Ghasia akomaa, awafuta kazi wa chini yake

WAZIRI  wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Hawa Ghasia ametangaza kuwafuta kazi Wakurugenzi wa sita na wengine watano kuwasimamisha kutokana na matukio ya kuvurugwa kwa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Vijiji na Vitongoji uliofanyikja Jumapili.
Pia Waziri Ghasia alisisitiza kuwa hawezi kujiuzulu kwa uzembe huo uliotia doa uchaguzi huo na badala yake amewaadhibu wa chini yake na jukumu la kujiuzulu analiacha kwa mamlaka iliytomteua licha ya kukiri uzedmbe uliofanywa na wasaidizi wake umelitia hasara taifa..
Akizungumza leo jijini Dar, Waziri Ghasia aliwataja wakurugenzi waliofutwa kazi ni Benjamin A Majoya aliyekuwa Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Mkuranga, Mkurugenzi Mtendaji wa Kaliua, Abdallah Ngodi, Masalu Mayaya wa Kasulu, Goody Pamba wa Serengeti, Julisu Madiga wa Sengerema na Simon Mayeye wa Bunda.
Wakurugenzi waliosimamishwa kazi ni Felix Mabuiga wa Hanang', Fortrunatus Fwema wa Mbulu, Isabela Chilumba wa Ulanga, Pendo Malabeja wa Kwimba na William Shimwela wa Sumbawanga Manispaa.
Waziri Ghasia alisema waliosimamishwa ni sababu ya kupisha uchunguzi na waliofutwa watapangiwa kazi nyingine za taaluma zao na kuongeza wakurugenzi wengine watatu wamepewa onyo kali.
Walioonywa niu Mohammed Maje wa Rombo, Hamis Yuna wa Busega na Ilala, Mvomero na Hai.
Uchaguzi huo uliofanyika Jumapili ulikumbwa na dosari mbalimbali zikiwamo kucheleweshwa kwa vifaa vya kupigia kura, karatasi kuwa na kasoro mbalimbali na kukwamisha kufganyika kwa uchaguzi kwa baadhji ya maeneo na kwingine kurudiwa.

Sikinde yapangua safu ya uongozi, Hemba 'aula'

BENDI kongwe ya muziki wa dansi nchini, Mlimani Park 'Sikinde' imepangua safu yake ya uongozi kwa kuunda Kamati Maalum inayoongozwa na wanamuziki watatu wa bendi hiyo.
Akizungumza na MICHARAZO, Katibu wa Kamati hiyo ya bendi, Abdallah Hemba alisema kuwa karibu mwezi mzima sasa bendi yao imepangua safu ya uongozi na kuunda kamati ambayo anaiongoza yeye na wenzake wawili.
Hemba alisema viongozi wenzake wanaoiongoza Sikinde ni mcharaza gitaa mahiri, Mjusi Shemboza na Ally Jamwaka.
"Kwa sasa Sikinde inaongozwa na Kamati maalum ambayo naiongoza mimi na akina Mjusi Shemboza na Ally Jamwaka," alisema Hemba ambaye ni muimbaji mahiri wa bendi hiyo.
Katika hatua nyingine, Hemba alisema kwa sasa bendi yao inasikiliza ofa toka kwa waratibu wa muziki kwa ajili ya shoo na mahasimu wao Msondo Ngoma.
"Bado hakuna hakika kama tutafanya shoo na Msondo ili tunasikiliza ofa, sisi tupo tayari wakati wowote kupambana na wapinzani wetu," alisema Hemba mmoja ya wanamuziki  waandamizi wa bendi hiyo iliyoanzishwa rasmi mwaka 1978.

Shamsa: Sikuwa naigiza, kipigo cha Simba kiliniliza Taifa

Shamsa Ford katika pozi
Shamsa akiangua kilio jukwaani wakati Yanga wakitungulia 2-0 na Simba
MUIGIZAJI nyota wa filamu nchini, Shamsa Ford ambaye alimwaga chozi wakati Yanga ikikandikwa mabao 2-0 na Simba, amesema hakuwa anaigiza 'kilio' isipokuwa uchungu wa kipigo ndiyo uliomfanya amwage machozi hadharani.
Shamsa, amesema yeye ni shabiki na mpenzi mkubwa wa Yanga kiasi kwamba amekuwa hakosekani kwenye mechi zao na kipigo hicho toka kwa Simba kilimuuma na kinaendelea kumuuma isivyo kawaida.
"Mungu wangu, kuna watu wamenipiga picha! Jamani...Ni kweli kipigo kiliniliza na kinaendelea kuniuma mpaka sasa...kwa nini iwe kwa Yanga tu kila mara," alihoji Shamsa.
Muigizaji huyo ambaye anatamba kwa sasa na filamu ya 'Chausiku' alisema mpaka sasa hajui kitu gani kilichoikuta Yanga kwenye uwanja wa Taifa katika pambano la Nani Mtani Jembe la kucharazwa mabao 2-0 ikiwa ni mara ya pili baada ya mwaka jana kunyukwa mabao 3-1.
Shamsa ni miongoni mwa waigizaji walio mashabiki wa Yanga, wengine ni Vincent Kigosi 'Ray' ambaye alikuwa na wakati mgumu juu ya matokeo hayo baada ya 'kupinga' na jacob Stephen Jacob 'JB' ambayer ni mnazi wa kutupwa wa Simba.

TANZIA! Mnenguaji Aisha Madinda afariki Dar

image
Aisha Madinda enzi za uhai wake
TASNIA ya sanaa imezidi kupata majozi baada ya aliyekuwa mnenguaji wa bendi za African Stars 'Twanga Pepeta' na Extra Bongo, Aisha Mohammed Mbegu 'Aisha Madinda' amefariki dunia mchana huu akiwa ndani ya Bajaj wakati akiwahi hospitali ya Mwananyamala.
Taarifa ambazo MICHARAZO imezipata zinasema kuwa Aisha Madinda alikodisha Bajaj na wakiwa kwenye foleni alikumbwa na mauti na mwili wake kwa sasa upo hospitali ya Mwananyamala ukiwa umehifadhiwa.
Akiongea na EATV Mkurugenzi wa bendi ya Twanga Pepeta amesema kuwa alipewa taarifa na daktari mmoja kuwa wameona kama mwili wa Aisha Madinda hospitalini hapo, ndipo akatuma watu kwenda kuangalia akiwemo Luiza Mbutu ili kuhakikisha kama kweli ni yeye ndipo walipogundua ni yeye.
“Mimi nipo njiani natoka Kigoma kuja Dar es Salaam, ni habari ya kusikitisha sana maana Aisha amefariki katika mazingira ya kutatanisha sana, jana alikuwa mzima na anachati na watu kwenye simu leo napigiwa simu mwili wake umekutwa umehifadhiwa kwenye hospitali ya Mwananyamala, hata sielewi nini kimetokea,” amesema Asha Baraka.
Hata hivyo taarifa ambazo hazijathibitishwa zinadai kuwa Madinda aliita dereva wa bajaj nma kuomba apelekwe Mwananyamala Hospitali na kukumbwa na mauti njiani bila dereva kujua mpaka akiwa hospitalini hapo.
Inaelezwa kuwa msiba wa marehemu Aisha uko Kigamboni na huenda akazikwa kesho huko huko.
MICHARAZO inaendelea kufuatilia na kitakachopatikana tutawafahamisha zaidi juu ya msiba huu ambao umekuja siku mooja tu baada ya Mkongwe Shem Ibrahim Karenga kufariki na kuzikwa jana jijini Dar.

Tuesday, December 16, 2014

Dirisha dogo lafungwa, 15 waombewa ITC

http://www.rockersports.co.tz/wp-content/uploads/2014/11/meshak.jpg
Meshack Abel alipokuwa Bandari Fc
http://shaffihdauda.co.tz/wp-content/uploads/2014/11/wawa-2.jpg
Wawa
 
 USAJILI wa dirisha dogo msimu wa 2014/2015 umefungwa rasmi jana (Desemba 15 mwaka huu) huku wachezaji 15 kutoka nje wakiombewa Hati ya Uhamisho wa Kimataifa (ITC) kutoka nchi mbalimbali.
Wachezaji walioombewa ITC kwa timu za Ligi Kuu ni Abdulhalim Humoud kutoka Sofapaka ya Kenya kwenda Coastal Union, Brian Majwega kutoka KCC (Uganda) kwenda Azam na Castory Mumbara kutoka Three Star Club (Nepal) kwenda Polisi Mara.
Wengine ni  Charles Misheto kutoka SP Selbitiz (Ujerumani) kwenda Stand United na Chinedu Michael Nwankwoeze kutoka Nigeria kwenda Stand United.
Pia wamo Dan Serunkuma kutoka Gor Mahia (Kenya) kwenda Simba, Emerson De Oliveira Neves Roque kutoka Emerson De Oliveira Neves Roque kutoka Bonsucesso FC (Brasil) kwenda Yanga, Halidi Suleiman kutoka Flambeau (Burundi) kwenda Stand United na Juuko Murushid kutoka SC Victoria University (Uganda) kwenda Simba.
Wachezaji wengine ni Kpah Sean Sherman kutoka Aries FC (Liberia) kwenda Yanga, Meshack Abel kutoka KCB (Kenya) kwenda Polisi Morogoro na Moussa Omar kutoka Flambeau (Burundi) kwenda Stand United.
Pia wamo Nduwimana Michel kutoka Flambeau (Burundi) kwenda Stand United, Serge Pascal Wawa kutoka El Merreikh (Sudan) kwenda Azam na Simon Serunkuma kutoka Express FC (Uganda) kwenda Simba.
Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya TFF inatarajia kukutana hivi karibuni kwa ajili ya kupitia usajili wa wachezaji wote walioombewa katika dirisha dogo wakiwemo wale wa mkopo.

Breaking News! Jaji Werema aachia ngazi

http://2.bp.blogspot.com/-HfIVzV9HEPE/Uq2Qh28re9I/AAAAAAAALfk/iZ76iAX0yLA/s640/1.png
jaji Werema aliyetangaza kuachia ngazi mwenyewe

HABARI zilizotufikia hivi punde zinasema kuwa aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Fredrick Werema ametangaza kujiuzulu nafasi yake hiyo.
Habari hizo zinasema Jaji Werema mmoja wa vigogo wanaotuhumiwa kuhusika na sakata la uchotwaji wa fedha za Akaunti za Tegeta Escrow zipatazo zaidi ya Sh Mil 300.
Kwa mujibu wa taarifa hizo zinasema kuwa Jaji Werema ameamua kujiuzulu mwenyewe kwa hiari yake na kwamba Rais Jakaya Kikwete ameafikiana na maamuzi hayo na kumshukuru kwa ujtendaji wake na kumtakia kila la heri katika maisha yake mapya.
Hata hivyo taarifa hizo zinasema kuwa, maamuzi hayo yamekuja baada ya shinikizo kubwa ambalo limekuwa likitolewa kila pembe ya nchi kwa Rais JK kuwawajibisha wote waliotajwa kwenye mapendekezo nane ya Bunge la Jamhuri ya Muungano kuhusiana na sakata hilo ambalo limeitia doa Tanzania mbele ya nchi wahisani.
MICHARAZO itazidi kuwaletea habari zaidi.

Gwiji Shem Karenga afariki, kuzikwa leo Kisutu

Shem Ibrahim Karenga enzi za uhai wake.
MWANAMUZIKI mkongwe nchini aliyekuwa amejaliwa kipaji cha kuimba na kucharaza gitaa kiongozi la Solo, Shem Ibrahim Karenga amefariki dunia jana akiwa katika Hospitali ya Amana  jijini Dar es Salaam alipokuwa akitibiwa na anatarajiwa kuzikwa leo.
Marehemu Kalenga anayekumbukwa kupitia tungo zake mbalimbali zilizochangia kumpa umarufu, alizozifyatua akiwa na bendi mbalimbali kama vile ‘Tucheze Segere’, ‘Muna’, ‘Kila jambo’ na ‘Mbelaombe’, alifariki asubuhi ya jana wakati akiendelea kupatiwa matibabu.
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg4wpGMAyOuYjuumKhAvBULpmmVN7j8iYWt3pn5pydekJm6qKAiT67ntH80ZpBjtDt7c9s5ewZsTIyWO4J9KC5B1o4Ysw0YVAM2VwbCPtbXVXaa8jSxvRwJfjtiRK2dkhGi_ETYZuaP9pM/s1600/DSCN9027.JPG
Mzee Shem Karenga akiwa jukwaani enzi za uhai wake
Kwa mujibu wa Kiongozi wa bendi ya African Minofu, Joseph Matei, marehemu aliugua siku chache zilizopita kabla ya kukumbwa na mauti na kwamba anatarajiwa kuzikwa leo kwenye Makaburi ya Kisutu jijini Dar. 
Gwiji hilo Shem Karenga alizaliwa mwaka 1950, Bangwe, Kigoma na kupata elimu ya msingi katika shule ya kimishionari ya Kihezya kuanzia mwaka 1957 hadi mwaka 1964.  
Mwaka 1964 alijiunga na bendi ya Lake Tanganyika Jazz ambayo maskani yake yalikuwa mjini Kigoma. Mwaka 1972, aliitwa kwenye bendi ya Tabora Jazz kama mwanamuziki mwenye kipaji cha utunzi, mwimbaji na mpigaji wa gitaa la Solo. 
Mwaka 1983 alijiengua kutoka Tabora Jazz na kusimama kabisa kujihusisha na muziki, ambako kilichofuatia ilikuwa ni kifo cha bendi hiyo. 
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEivfVcUbJ3EtZF8fu2-MOehiBeFARjSF0W4Bund8Mk9Yk8pE7YiR7QXlX-T5zL8HBGKVAWTiHGmYR_8WHcw-M_xFKwTjYZTAtr96hyO37PwP9VLqzVfNV2QuAe7U-QsKxqGDtsRQHvaCdA/s1600/PICTURE+07.jpg
Shem Karenga akicharaza gitaa na kuimba kiasi cha kumkuna Mayaula Mayoni (kulia)
Mwaka 1990 aliondoka Tabora na kutua jijini Dar es Salaam. Mwaka 1990 alijiunga na MK Beats. 
Mwaka 1995, MK Beats ilisambaratika, ambako mwaka uliofuata, yaani 1996 alianzisha bendi ya Tabora Jazz Star kwa kushirikiana na Ibrahim Didi. Mpaka mauti yanamfika, Shem Karenga Mkurugenzi Msaidizi katika Bendi ya Tabora Jazz Star ambapo Mkurugenzi Mkuu ni Ibrahim Didi. Moja ya vibao vyake viliwahi kunyakuliwa na kurejewa na kundi la Sokousou Stars kuonyesha alivyokuwa mkali.
MICHARAZO inatoa pole kwa ndugu, jamaa na familia ya marehemu pamoja na wanamuziki na wadau wote wa fani ya muziki nchini kwa msiba huo.
MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU Mahali PEMA PEPONI.

Jennifer Mgendi 'aifumua' Shelina

Muimbaji na muigizaji filamu, Jennifer Mgendi
MUIMBAJI nyota wa muziki wa Injili nchini ambaye pia ni mtayarishaji na muigizaji wa filamu, Jennifer Mgendi amesema anaifanyia marekebisho filamu yake mpya ya 'Shelina' kuwa filamu fupi ya mfumo wa wimbo ili kuzidi kuwapa raha mashabiki wake.
Akizungumza na MICHARAZO, Jennifer alisema ameona ni vema kuibadilisha 'Shelina' kuwa katika mfumo mwingine ili kuwapa ladha tofauti mashabiki wake ambao wamemzoea katika kazi nyingine alizowahi kuzitoa nyuma.
Jennifer alisema atautumia wimbo wake uitwao 'Kaa Chonjo'.
"Nimeamua kufanyia marekebisho filamu yangu ya 'Shelina' na sasa naitengeneza kama filamu fupi ya mfumo wa wimbo, nikiutumia wimbo wa 'Kaa Chonjo," alisema Jennifer anayejiandaa kuachia albamu yake ya nane iitwayo 'Wema ni Akiba'.
Filamu hiyo ya 'Shelina' inakuja wakati akitamba na kazi yake iitwayo 'Mama Mkwe' ambayo inaendelea kusumbua sokoni.
Mbali na 'Mama Mkwe', Jennifer pia amewahi kutamba na filamu nyingine kama  'Chai ya Moto', 'Joto la Roho', 'Teke la Mama', na 'Pigo la Faraja'.

Salha wa Hammer avunja ukimya na Kishtobe cha Mtaa

MUIMBAJI nyota wa muziki wa taarab, Salha Abdallah amevunja ukimya baada ya kutoka kwenye likizo ya uzazi kwa kuibuka na wimbo uitwao 'Kishtobe cha Mtaa' uliopo kwenye albamu mpya ya kundi la Five Star Modern.
Akizungumza na MICHARAZO, Salha maarufu kama 'Salha wa Hammer' alisema wimbo huo ni miongoni mwa nyimbo tano zitakazokuwa katika albamu yao itakayozinduliwa Ijumaa wiki hii.
Salha alisema wimbo huo ni wa kwanza kwake tangu alipoenda likizo ya uzazi na kuwataka mashabiki wajitokeze kwa wingi kwenye uzinduzi huo ili kupata uhondo toka kwake na wanamuziki wote wa Five Star.
"Baada ya likizo ya uzazi, hatimaye natarajia kuanza kazi na wimbo wa 'Kishtobe cha Mtaa' ambao nimekiimba mwanzo mwisho nikisaidiana na akina Mwape Kibwana na wengine kitakuwa kwenye albamu itakayozinduliwa Ijumaa," alisema Salha.
Mbali na wimbo huo wa Salha, albamu hiyo ya 'Kichambo Kinakuhusu' ina nyimbo za 'Big Up Dear', 'Ubaya Hauna Soko', 'Sina Gubu Nina Sababu' na 'Kichambo Kinakuhusu' wenyewe.

Everton yaiangamiza QPR, Redknapp maji ya shingo!

QPR striker Bobby Zamora scores against Everton
Bobby Zamora akimtungia Howard
Everton midfielder Ross Barkley
Barkley akifunga bao la kuongoza la Everton kwa shuti kali
KLABU ya Everton usiku wa kuamkia leo wamepata ushindi mwepesi nyumbani baada ya kuifumua QPr mabao 3-1 na kuzidi kukwea katika Ligi Kuu ya England inayozidi kushika kasi.
Ross Barkley alifunga kwa shuti kabla la mita 20 katika dakika ya 33, kabla ya Kevin Mirallas kufungwa kwa mpira wa adhabu ndogo katika dakika ya 43 na mpira wa kichwa wa Steven Naismith kwenye dakika ya 53 yalitosha kuwaangamiza QPR inayonolewa na kocha wa zamani wa Tottenham Hotspur, Harry Redknapp.
QPR ambao kipigo hicho kilikuwa cha nane ugenini katika ligi ya msimu huu, ilipata bao la kufutia machozi katika dakika ya 80 kupitia Bobby Zamora aliyeuwahi mpira uliotemwa na kipa Tim Howard.
Ushindi huo umeifanya Everton kuitambuka wapinzani wao wa jadi Liverpool wsanaolingana nao pointi 21 na kukaa nafasi ya 10 huku Reds wakiporomoka hadi nafasi ya 11. wakati QPR wamesalia katika nafasi ya tatu toka mkiani wakiwa na pointi 14, nne zaidi ya timu inayoshilikia mkia ya Leicester City.

Manchester Utd yatabiriwa kutwaa ubingwa wa England

http://i.huffpost.com/gen/1226648/thumbs/o-PHIL-NEVILLE-570.jpg?6
Phil Neville enzi akiichezea Manchester United kabla ya kutimkia Everton
USHINDI wa mara sita mfululizo katika mechi zake za Ligi Kuu ya England iliyopata klabu ya Manchester United kumetajwa ni dalili za kurejea kwenye 'fomu' yake na kutabiriwa kutwaa ubingwa wa msimu huu.
Nyota na kocha msaidizi wa zamani wa klabu hiyo, Phil Neville, amenukuliwa akisema kwamba klabu hiyo ina nafasi kubwa ya kuwa mabingwa wa England baada ya kutulia kutoka kwenye misukosuko ya msimu msimu uliopita.
"Ndiyo wanaweza'' alisema Neville aliyenyakua mataji sita ya Ligi Kuu ya England akiwa kama mchezaji kabla ya kuangukia kuwa miongoni mwa makocha msaidizi chini ya David Moyes aliyetimuliwa.
 "Wachezaji wanaamini wanaweza kutwaa taji na hilo Louis Van Gaal anaweza kulifanya," alisema Neville.
Kauli ya Neville imekuja baada ya Manchester United kupata ushindi wa sita mfululizo kwa kuifumua Liverpool kwa mabao 3-0 katika pambano lililochezwa siku ya Jumapili.
Kabla ya hapo klabu hiyo ilionekana kuyumba kiasi cha mashabiki kuanza kupoteza imani kwa Van Gaal kabla ya kocha huyo kuwatuliza na kuanza kuwapa raha kwa kushinda mfululizo.
Mechi hizo sita za Manchester United iliyoshinda mfululizo ni hizo hapo chini:

8 November:  Crystal Palace 1-0 (nyumbani)
22 November: Arsenal 2-1 (ugenini)
29 November: Hull 3-0 (nyumbani)
2 December: Stoke 2-1 (nyumbani)
8 December: Southampton 2-1 (ugenini)
14 December: Liverpool 3-0 (nyumbani)

Nyota Manchester Utd katika 'kashfa' ya rushwa Hispania

http://www4.pictures.zimbio.com/gi/Manchester+United+v+Valencia+ODBuEmnisftx.jpg
Ander Herrera anayetuhumiwa kwa upangaji matokeo ya mechi ya La Liga 2011
http://www4.pictures.zimbio.com/gi/Jefferson+Montero+Exeter+City+v+Swansea+City+Rttkn623zmEl.jpg
Montero naye yumo katika mkumbo huo
http://static.goal.com/187500/187540_heroa.jpg
Nahodha Gabi,  naye anatuhumiwa
http://static.weltsport.net/picmon/e9/dVK_baa3z_l.jpg
Kocha Aguirre

KIUNGO nyota wa Manchester United, Ander Herrera na nahodha wa Atletico Madrid, Gabi ni miongoni mwa wachezaji wanaochunguzwa kwa kujihusisha na tuhuma za upangaji wa matokeo ya mechi ya kufungia msimu wa 2010-2011 wa Ligi Kuu ya Hispania.
Wengine waliohusishwa na kadhia hiyo ni Kocha wa zamani wa Real Zaragoza anayefundisha timu ya taifa ya Japan Javier Aguirre na mchezaji wa Swansea City, Jefferson Montero.
Kwa mujibu wa BBC, Mwendesha Mashtaka wa Idara ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini Hispania Alejandro Luzon, ameiagiza Mahakama kumchunguza kocha wa zamani wa klabu ya Real Zaragoza na baadhi ya wachezaji kutokana na tuhuma za kudaiwa kuuza mchezo dhidi ya Levante.
Katika pambano hilo la kufungia msimu Zaragoza ilishinda mchezo huo kwa mabao 2-1 na kuepuka kushuka daraja, lakini sasa imebainika kuwa matokeo hayo yalipangwa baada ya kutembezwa mlungula.
Upande wa mashitaka uliowasilisha mashtaka yake katika Mahakama mjini Valencia jana Jumatatu, unadai kuwa watuhumiwa wanahusishwa na rushwa ya dola million mbili. 
Baadhi ya wachezaji wanaotuhumiwa katika kashfa hiyo ni Kiungo wa Manchester United aliyewahi kukipiga Zaragoza wakati wa mchezo huo kabla ya kuhamia Athletico Bilbao, Ander Herrera, anayeichezea Manchester United, nahodha wa Atletico Madrid, Gabi, Montero na Javier Aguirre.
Inadaiwa kuwa wachezaji wa Lavante walishikishwa fedha ili kupoteza pambano hilo na kuinusuru Zaragoza isishuke daraja katika pambano la Mei 21, 2011.
Jumla ya watu 41 wakiwamo wachezaji, makocha na wakurugezi wa timu hizo mbili wamehusishwa katika upangwaji huo wa matokeo ya pambano hilo.

Kumekucha! Maximo atupiwa virago kama Brandts, Pluijm arejeshwa

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEirHsHAOLesgeko6449ITJAGxd3GFzvxJ4YBsnuG54Z_IHmqZpPn0Rcn5HtpJ20BHmV_Xmm3ra1JRpa1YBgtVVw-KSoIGH0WZJvcJpteX_m9EYMWT_OK1dT-MVqydunhScqSyS6RsOndkH5/s1600/DSC_0306.JPG
Marcio Maximo na msaidizi wake Leonardo Neiva wakati wakiinoa Yanga

KAMA ilivyokuwa kwa kocha Ernie Brandts aliyetimuliwa baada ya Yanga kufungwa na Simba kwenye mchezo wa 'bonanza' wa Nani Mtani Jembe, hali hiyo imemkuta Marcio Maximo.
Kocha huyo wa zamani wa Taifa Stars kutoka Brazil ametimuliwa Yanga baada ya kipigo cha mabao 2-0 katika pambano la Nani Mtani Jembe-2.
Taarifa ambazo ni za uhakika toka ndani ya Yanga zinasema kuwa, kocha Maximo amepewa mkono wa kwaheri na nafasi yake inarudi kwa aliyekuwa kocgha wa timu hiyo  Hans Van Der Pluijm.
Mmoja wa viongozi wa kamati ya utendaji ya klabu ya Yanga amesema, Maximo ataondoka nchini ndani ya siku tatu baada ya kukubaliana na uongozi.  
"Si kwamba amefukuzwa, lakini ni makubaliano kwamba anaondoka.  
"Ni kweli, lakini msitake kulikuza hili jambo ionekane kama tumemfukuza," aliuliza na alipotakiwa kujua mrithi ni nani, alikataa kusema.  
Hata hivyo ni kwamba Maximo amepewa mkono wa KWAHERI sambamba na kiungo aliyekuja naye toka kwao, Emerson Oliveira ambaye inaelezwa amekosa ITC japo ukweli ni kwamba ameonekana ni bomu.
Yanga ilimfurusha Brandt na wasaidizi wake, Fred Felix Minziro na Razack Ssiwa baada ya timu yao kulala mabao 3-1 na safari hii Maximo anaondoka na wasaidizi wake akiwamo Mbrazil mwenzake Leonardo Neiva ambaye alimleta baada ya kusaini mkataba.

Monday, December 15, 2014

Ratiba ya Ligi ya Mabingwa hii hapa


KLABU ya Manchester City imepangwa kucheza na Barcelona katika hatua ya mtoano ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya katika ratiba iliyopangwa leo jijini Nyon, Ufaransa. 
Timu hizo zilikutana pia katika hatua hiyo msimu uliopita ambapo Barcelona waliibuka na ushindi wa jumla ya mabao 4-1 na kutinga hatua ya robo fainali ya michuano hiyo. 
Timu zingine ambazo zilikutana msimu uliopita katika hatua hiyo ni pamoja na Paris Saint-Germain ambao watakwaana tena na Chelsea msimu huu. 
Wengine ni mabingwa watetezi Real Madrid ambao watakwaana na Schalke wakati mshindi wa pili msimu uliopita Atletico Madrid wao wataivaa Bayer Leverkusen. 
Mabingwa wa Serie A Juventus wao watawakaribisha Borussia Dortmund huku mabingwa wa Ujerumani Bayern Munich wakicheza na Shakhtar Donetski, Arsenal wenyewe watacheza na Monaco na Porto watakwaana na FC Basel. 
Timu ambazo zilimaliza katika nafasi ya pili katika hatua ya makundi zitacheza mechi zao za kwanza nyumbani kati ya Februari 17/18 na 24/25 huku zile za marudiano zikitarajiwa kuchezwa kati ya Machi 10/11 na 17/18.

Liverpool wapewa Waturuki, Ligi Ndogo ya Ulaya

http://www1.pictures.zimbio.com/gi/Andre+Wisdom+BSC+Young+Boys+v+Liverpool+FC+DEcmweK_E8Sl.jpg 
KLABU ya Liverpool ambayo ilichemsha katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya imepewa timu ya  Besiktas ya Uturuki katika hatua ya timu 32 bora ya michuano hiyo kwenye ratiba iliyopangwa leo. 
Timu zingine zilizoondoshwa katika michuano hiyo ni pamoja na Ajax Amsterdam ambao wamepangiwa kucheza na Legia Warsaw, Anderlecht wao wakipangwa na Dinamo Moscow huku Sporting Lisbon wao wakiwa wenyeji wa Wolfsburg. 
Katika mechi zingine zitazikutanisha timu za AS Roma dhidi ya Feyenoord, Inter Milan wao watacheza na Celtic, Tottenham Hotspurs dhidi ya Fiorentina wakati Athletic Bilbao wao watakuwa wenyeji wa Torino. 
Mechi za mkondo wa kwanza za michuano hiyo zinatarajiwa kuchezwa Februari 19 huku zile za marudian zikitarajiw akuchezwa Februari 26.

Breaking News! Amissi Tambwe atua Yanga

tambwe yanga
HABARI zilizotufikia hivi punde zinasema kuwa dakika chache zilizopita ni kwamba klabu ya Yanga imemsajili mshambuliaji wa Simba aliyeachwa Amisi Tambwe .
Yanga imemsajili Tambwe dakika chache zilizopita ambapo anakuja kujaza nafasi iliyoachwa wazi na Emerson Oliveira wa Brazil aliyetemwa kwa kukosa ITC.
Tambwe ametua Yanga ikiwa ni siku chache baada ya Mganda Hamis Kiiza kuachwa na klabu hiyo na kukimbilia URA ya Uganda baada ya Kpeh Seen Sherman wa Liberia kupewa kandarasi ya kuichezea timu hiyo.
Tambwe amesajiliwa na Yanga baada ya kuachwa na Simba.
Tambwe amesajiliwa na Yanga baada ya kuachwa na Simba.
Tambwe alikuwa mfungaji bora wa ligi msimu uliopita ambapo alifunga mabao 19 kwenye ligi lakini alishindwa kuwika msimu huu baada ya kutopewa nafasi ya kutosha chini ya Patrick Phiri.
Simba imemuacha Tambwe baada ya kumsajili Danny Serunkuma toka Gor Mahia ya nchini Kenya .
Yanga imekamilisha usajili huu saa chache kabla ya dirisha dogo la usajili kufungwa leo na TFF.