STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, August 19, 2016

Mtamkoma! Kessy ruksa kukipiga Jangwani msimu huu

Kessy akiwajibika kwenye mechi ya Ngao ya jamii dhidi ya Azam
Na Rahma Kimwaga
YANGA inayojiandaa kupaa kwenda zao DR Congo huenda ikawa inatabasamu kwa furaha baada ya beki waliyekuwa wakimpigania kutoka Simba, Hassan Kessy kupewa uhalali wa kuanza kuitumikia timu hiyo katika Ligi Kuu Bara msimu huu.
Kessy aliyekuwa akiwekewa zengwe na Simba, licha ya ukweli ilishamaliza naye mkataba na ilionyesha wazi kutomhitaji baada ya kumfungia mechi tano za mwishoni mwa msimu uliopita kwa kitendo cha kunmchezea rafu Edward 'Rddo' Christopher aliyekuwa akiichezea Toto Africans aliyesajiliwa Kagera Sugar kwa sasa.
Kamati ya Sheria na Haki za Wachezaji ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF)  lilipitisha jina la Kessy kuichezea Yanga sambamba na usajili wa klabu nyingine kwa msimu wa 2016-2017.
Kamati hiyo imepitisha jina la Hassan Ramadhani ‘Kesi’ kuitumikia Yanga kuanzia msimu huu 2016/17 baada ya kuona kuwa hana tatizo katika usajili badala yake madai ambayo pande husika zinaweza kudaiana wakati mchezaji anaendeleza kipaji chake.
Kamati hiyo chini ya Mwenyekiti wake, Richard Sinamtwa imepitia usajili wa timu zote na kujiridhisha kwamba suala la mchezaji Hassan Kessy limeegemea kwenye madai na si usajili ambako Simba ndiye mdai kwa kumtuhumu mchezaji huyo kuwa alianza kuitumikia Young Africans kabla ya kumaliza mkataba wake Simba SC. Mkataba wake ulifika mwisho, Juni 15, 2016.
Kama ni madai Simba inaweza kuendelea kumdai Kessy au Young Africans wakati mchezaji huyo anatumika uwanjani kwa mwajiri mpya. TFF inafuatilia na kuangalia haki ya Simba namna ya kupata haki yake baada ya kuwasilisha madai kuhusu kuvunja mkataba na mwajiri wake wa zamani.
Kanuni hazimzuii mchezaji kuendelea kucheza kwa hoja ya madai badala yake suala hilo linaweza kumalizwa wakati mashindano yanaendelea. Kamati inaendelea kupitia malalamiko na pingamizi za wachezaji wengine na inatarajiwa kutoa taarifa rasmi kuhusu wachezaji wote wakati wowote kuanzia sasa.
Katika hatua nyingine Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limezionya timu shiriki za ligi hiyo kutochezesha wachezaji wa kigeni kama hawana vibali vya kuishi, kufanya kazi na leseni inayomruhusu kucheza ligi husika kwa mujibu wa sheria za nchi na kanuni za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.
Vibali vya kuishi na kufanya kazi vinatolewa na Idara ya Uhamiaji Tanzania (Uhamiaji) wakati leseni ya kucheza inatolewa na TFF.
Vilevile TFF imeziagiza klabu kulipia ada za ushiriki kwa kila timu; leseni za wachezaji, ada za wachezaji na ada za mikataba.
Mchezaji hatapewa leseni ya kucheza kama uongozi wa timu hautakamilisha taratibu za malipo.
TFF pia imezikumbusha timu zinazoshiriki Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kwamba hazitapewa leseni ya mchezaji yeyote ambaye timu haikuleta mkataba wakati wa maombi ya usajili, hii ni kwa mujibu wa kanuni ya 68 vipengele vya 1, 2, 3 na 8 ya Ligi Kuu ya Tanzania toleo la 2016/2017.
Kila timu inatakiwa kuleta nakala tatu za mkataba wa mchezaji, ili kamati ya katiba, sheria na hadhi za wachezaji iweze kupitia na TFF iweze kuidhinisha mikataba hiyo. Baada ya hapo timu na mchezaji, watakuja kuchukulia mikataba hiyo hapa TFF. Ni matarajio yetu kuwa kila klabu itatimiza wajibu wake ili kuondoa migogoro kati ya timu na mchezaji na mchezaji na timu. Tunategemea kupata ushirikiano.

KUMEKUCHA VODACOM PREMIER LEAGUE 2016-2017

Mabingwa watetezi Yanga
Simba
Azam
NA RAHIM JUNIOR
MSIMU mpya wa Ligi Kuu Tanzania Bara maarufu kama Vodacom Premier League, VPL unatarajiwa kuanza rasmi kesho Jumamosi kwa michezo mitano, huku mtetezi Yanga ikila shushu hadi Agosti 31 kwa vile ina majukumu ya kimataifa.
Yanga inatarajiwa kuondoka siku ya Jumapili kwenda Lubumbashi nchini DR Congo kumaliza mchezo wake wa kukamilisha ratiba ya michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya wenyeji TP Mazembe itakayochezwa Jumanne ijayo.
Kwa mujibu wa ratiba ya VPL, kesho kuitakuwa na michezo itakayohusisha Simba ambayo itaialika Ndanda ya Mtwara kwenye Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam, huku Azam itakuwa mwenyeji wa African Lyon Uwanja wa Azam Complex, Chamazi.
Mjini SHinyanga kwenye Uwanja wa Karambage, Stand United itakwaruzana na Mbao FC ya Mwanza inayoshiriki ligi hiyo kwa mara ya kwanza, wakati Mtibwa Sugar itaikaribisha Ruvu Shooting ya Pwani kwenye Uwanja wa Manungu, Turiani mjini Morogoro.
Mechi nyingine itazihusisha Maafande wa Prisons ya Mbeya itakayosafiri hadi mjini Songea, Mkoa wa Ruvuama kuvaana na wenyeji wao Majimaji kenye Uwanja wa Majimaji.
Ligi hiyo itaendelea Jumapili kwa mchezo mmoja tu,  Kagera Sugar itaialika Mbeya City kwenye Uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga kabla ya Jumatano
Toto Africans haijavaana na Mwadui kwenye uwanja wa CCM Kirumba. Mechi hizo zimehamishiwa hapo kwa vile Uwanja wa Kaitaba, Bukoba bado haujakamilika kukaratabiwa na ule wa CCM Kirumba kuwa na kazi nyingine likiangushwa Tamasha la Fiesta 2016.
Ligi hiyo inaanza huku karibu timu zote zimefanya usajili wa maana na baahi kubadilisha benchi la ufundi la timu zao.
Klabu nne pekee ndizo ambazo zinashiriki ligi hiyo zikiwa na makocha wao wa msimu uliopita na zilizosalia zimebadilisha kwa kuwaleta wapya ama kubadilishana na wapinzani wao kama ilivyo kwa Mtibwa Sugar na Kagera Sugar.
Kocha Mecky Maxime aliyekuwa Mtibwa ametua Kagera Sugar na nafasi yake kuchukuliwa na Salum Mayanga aliyekuwa akiinoa Prisons Mbeya.
Makocha wengine wapya katika ligi hiyo ni Zeben Hernandez kutoka Hispania anayeinoa Azam, Joseph Omog wa Simba, Rogasian Kaijage wa Toto Africans na Etienne Ndeyirageji wa Mbao FC anayetokea Burundi.
JKT Ruvu iliyosukwa upya pia ina kocha mpya Hamis Malale 'Hamsini' aliyekuwa Ndanda wakati Ndanda sasa inanolewa na Joseph Lazaro aliyekuwa Mgambo JKT iliyoshuka daraja, huku Ruvu Shooting ikiwa na kocha mpya Seleman Mtingwe.
Africna Lyon naye inashiriki ligi hiyo baada ya kurejea kutoka Ligi Daraja la Kwanza ikiwa na kocha wa zamani wa Simba, Dragan Popadic akisaidiwa na Ramadhani Aluko, huku Majimaji Songea ikiwa chini ya Kocha Juma Mhina.
Mbali na makocha msimu huu utashuhudia vikosi vinavyoundwa na wachezaji wapya waliosajili kwenye timu hizo shiriki gumzo likiwa ni usajili wa straika kutoka Burundi, Laudit Mavugo na wakali wengine ndani ya kikosi hicho akiwamo, Shiza Kichuya, Federick Blagnon, Method Mwanjali na Mussa Ndusha.
Je, unadhani ni timu ipi itaanza msimu na mguu mzuri? Tusubiri baada ya dakika 90 za mipambano hiyo na ile ya kesho.


Ratiba ilivyo:
Kesho Jumamosi
Simba            v Ndanda
Stand Utd       v Mbao
Mtibwa Sugar v Ruvu Shooting
Azam             v African Lyon
Majimaji         v Prisons

Jumapili

Kagera Sugar v Mbeya City

Jumatano

Toto African    v Mwadui
 


Friday, June 24, 2016

Klopp amfungia kazi Sadio Mane, ataka kumng'oa Southampton

https://www.thesun.co.uk/wp-content/uploads/2016/04/2626524.main_image.jpg
Sadio Mane aliyeingia rada za Liverpool
VIJOGOO vya Anfield, Klabu ya Liverpool imeingia mawindoni  kumwinda straika wa Southampton, Sadio Mane katika uhamisho wa kitita cha Pauni Milioni 30.
Mkufunzi wa klabu hiyo, Jurgen Klopp anamtaka nyota huyo wa Senegal mwenye  miaka 24 ili kuimarisha safu ya ushambuliajina amepanga kuufanya uhamisho wake kuwa wa kihistoria katika klabu hiyo.
Liverpool na Southampton zitaendelea kufanya mazungumzo kuhusu mpango huo, huku kitita hicho cha uhamisho huo kikiwa kuwa ni suala muhimu zaidi.
Southampton inadaiwa kutaka Pauni Milioni 40 kwa Mane aliyefunga mabao 11 katika mechi 37 alizocheza msimu uliopita wa EPL.
Kitita hicho ni zaidi ya Pauni Milioni 10 ya kile kinachopendekezwa kutolewa na Liverpool, jambo ambalo limefanya mazungumzo kurefushwa zaidi ili kupata muafaka kabla ya njyota huyo kuachiwa atue Anfield.
Southampton ipo mbioni pia kumsaka mrithi wa Ronald Koeman aliyejiunga na klabu ya Everton hatua ambayo huenda ikachelewesha mpango huo.
Klopp alipendezwa na Mane ambaye alihusishwa sana na uhamisho wa Old Trafford wakati wa Louis Van Gaal wakati alipofunga mara mbili baada ya Southampton kutoka nyuma 2-0 na kuiadhibu Liverpool 3-2.

Southampton yampotezea Pellegrini, njia nyeupe kwa Puel

https://www.thesun.co.uk/wp-content/uploads/2016/06/nintchdbpict000233254556.jpg?w=688
Manuel Pellegrini
http://i.eurosport.com/2016/02/06/1790003-37797351-2560-1440.jpg?w=1050
Claude Puel
http://e0.365dm.com/16/06/768x432/victor-wanyama-spurs_3489343.jpg?20160623221243
Victor Wanyama aliyetua Spurs
IKIWA imeshampoteza kiungo mkabaji wake, Mkenya Victor Wanyama, klabu ya Southampton imedaiwa kuachana na mpango kumnyakua kocha wa zamani wa Manchester City, Manuel Pellegrini.
Klabu hiyo ilidaiwa ilikuwa mbioni kumpa ajira Kocha Pellegrini mwenye miaka 62 ili kuziba nafasi ya Ronald Koeman aliyetimkia Everton, hata hivyo mpango huo umefutwa na sasa inaelezwa njia nyeupe kwa Mfaransa, Claude Puel wa klabu ya Nice.
Imeelezwa Southampton imeachana na Pellegrini na kumgeukia Puel anayeinoa Nice kutokana na kubaini katika mazungumzo yao Kocha huyo kutoka Chile hawezi kuendana na falsafa ya klabu hiyo katika suala zima la maendeleo ya soka la vijana.
Mashabiki wa klabu hiyo wamekuwa na shauku kubwa ya kumuona bosi huyo wa zamani wa Real Madrid na Villareal, aliyetwaa taji la Ligi Kuu ya England miaka miwili iliyopita akitua klabu kwao ili kuchukua nafasi ya Kocha Ronald Koeman aliyewakacha na kuhamia Everton mapema mwezi huu kwa ajili ya msimu ujao.
Southampton inahaha kusaka kocha wakati kiungo wake Mkenya Victor Wanyama akiwa ametimka zake Tottenham Hotspur aliposaini mkataba wa miaka mitano kwa ajili ya msimu ujao na kumpa nyota huyo fursa ya kukipiga Ligi ya Mabingwa Ulaya
.

Mchezaji alimwa kadi nyekundu kwa kupupua uwanjani

http://cdn.adelove.com/wp-content/uploads/2016/06/Adam-Lindin-Ljungkvist.jpg
PERSHAGEN, Sweden
SIKIA hii. Inawezekana haijawahi kutokea kokote, ila mwamuzi mmoja wa soka nchini Sweden amemlima kadi mbili za njano kisha kumtoa kwa nyekundu, beki wa  Pershagen SK, Adam Lindin Ljung-kvist kwa kosa la kupupua (kujamb**) uwanjani.
Beki huyo wa timu hiyo ya ligi ya daraja la chini alikumbwa nakisanga hicho katika mechi dhidi ya
Järna SK na alipokuwa katika harakati za kushangaa kuhusiana na hatua ya refa huyo, alipigwa kadi nyekundu na kuondolewa uwanjani.
Mwamuzi huyo alitaja kitendo cha Adam cha kutoa ushuzi kama tabia isiyo njema kwa mchezaji.
Lakini kulingana na Adam, alidhani alikuwa akifanya hivyo kimaumbile tu na wala hakuwa na nia ya kumchafulia refa hewa.
Taarifa hiyo imeibua malumbano makubwa kote duniani katika mtandao wa kijamii, huku wengine wakisema kuwa hiyo ni mara ya kwanza kwa mchezaji soka kupigwa kadi nyekundu kwa sababu ya kuchafua hewa.

Yanga yakwama kotekote dhidi ya Tp Mazembe


Kikosi cha Yanga

Mashabiki wa Yanga
WAMEKWAMA kotekote. Klabu ya Yanga ilipanga mechi yao dhidi ya TP Mazembe ichezwe usiku wa Jumatano, Shirikisho la Soka Afrika (CAF) likaigomea. Haikuchoka ikatafuta mbinu nyingine na kuzuia kigoma cha Wakongo kinachoshangilia bila kuchoka wakiungane na watani zao, Simba kwenye Uwanja wa Taifa kwa kutaka kuhodhi majukwaa yote, nalo likagonga mwamba mbele ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) iliyowagomea leo Ijumaa.
TFF kupitia Afisa Habari wake, Alfred Lucas imesema Yanga hairuhusiwi kuyakalia majukwaa yote kama walivyoomba na wakidhubutu wataipata freshi, kwani Kamati ya Mashindano imegomea mchongo wao huo.
Akizungumza leo, Lucas alisema mpango huo wa Yanga hakubaliki na kwamba watatumia jukwaa lao na mengine watatumia wapinzani na watu wengine watakaofika uwanjani Jumanne ijayo, siku itakayopigwa mechi hiyo.
Mechi hiyo itapigwa Saa 10 jioni ya Juni 28 na sio Saa 1:30 usiku wa Jumatano kama walivyoomba awali Yanga kwa sababu wamechelewa kuwasilisja ombi hilo ofisi za CAF ambazo zimewajibu kuwa ratiba itakuwa ile ile ya awali ya Juni 28.
Yanga inahitaji ushindi kwenye mchezo huo wa pili kwao na wa kwanza nyumbani katika Kundi A ya michuano ya Kombe la Shirikisho baada ya kulala ugenini 1-0 dhidi ya MO Bejaia ya Algeria.
Mazembe wanatarajia kutua nchini Jumapili wakipishana saa chache tu na Yanga ambao kwa sasa wapo kambini Antalya wakijifua kujiandaa na mchezo huo.
Baada ya mechi hiyo Yanga inayonolewa na Kocha Hans Pluijm itawasubiri Waghana wa Medeama kwa mchezo wao mwingine katikati ya Julai kabla ya kuifuata kwao Ghana, ambapo ni lazima ishinde mechi hizo tatu kufufua tumaini ya kutinga nusu fainali ili waogelee mihela ya CAF kupitia michuano hiyo ya pili kwa ukubwa Afrika kwa ngazi za klabu baada ya Ligi ya Mabingwa Afrika.


Msimamo wa Kundi A:

Mazembe  1 1 0 0 3 1 3
Bejaia       1 1 0 0 1 0 3
Yanga       1 0 0 1 0 1 0
Medeama  1 0 0 1 1 3 0 

Mbeya City yaibomoa Prisons, yamnyakua mfungaji wao mkali

IMG_20160623_220042
Mkopi akisaini mkataba wa kuichezea Mbeya City
MSHAMBULIAJI nyota wa kikosi cha Prisons-Mbeya, Mohammed Mkopi ameikacha timu hiyo na kutua Mbeya City FC.
Mkopi aliyesaidia na Jeremiah Juma kuibeba Prisons katika Ligi Kuu Bara msimu uliopita wakifunga jumla ya mabao 21 amesaini kandarasi ya mwaka mmoja.
Mara baada ya kusaini kandarasi hiyo, Mkopi, aliyewahi kucheza pia timu ya Mtibwa Sugar alisema  kuwa anamshukuru Mungu kwa kufanikiwa kujiunga na City timu ambayo alikuwa na ndoto za kuichezea  hata kabla ya kusajiliwa na Prison msimu uliopita.
“Kabla sijasajiliwa na Prisons ndoto yangu ilikuwa ni kucheza kwenye timu hii, nashukuru Mungu baada ya msimu mmoja hili limefanikiwa, nitakuwa hapa msimu ujao, lengo langu ni kufanya kazi kwa nguvu  ili niendelee kuwa sehemu ya kikosi hiki kwa muda mrefu zaidi” alisema aliyefunga mabao matano msimu uliopita.

Hivi hili ni soka kweli au vita?

Magoli yaliyowavuruga Waarabu wa ES Setif na kulianzisha

CAF yaing'oa ES Setif kwa vurugu Ligi ya Mabingwa Afrika

http://www.aps.dz/en/media/k2/items/cache/4e4b1fc9eeea638a4484d9ff6d1e996c_XL.jpg
Entente Sportivo Setif iliyong'oka Afrika kwa vurugu
Hali ilivyokuwa katika mechi hiyo kwa vurugu za mashabiki wa ES Setif
SHIRIKISHO la Soka Afrika (CAF) limeiondoa klabu ya ES Setif ya Algreia kutokana na vurugu za mashabiki wao wakati wa pambano lao dhidi ya Mamelodi Sundowns, ambapo matokeo yake yamefutwa kwa sasa.
Katika mchezo huo uliopigwa wiki iliyopita mjini Setif, Algeria, Mamelodi iliitambia wenyeji kwa mabao 2-0 na kuibua hasira kwa mashabiki wa klabu hiyo ya Algeria kwa kulianzia mbungi wakirusha mawe, chupa na kufyatua fataki kasi cha kuhatarisha usalama na kufanya mwamuzi kulisimamisha pambano kabla ya muda.
Baada ya Kamati ya Utendaji ya CAF inayohusika na mashindano ngazi ya klabu kukutana na kupitia ripoti ya mchezo huo imeridhika na kuamua kuiondoa Setif kwa kukutwa na hatia ya kushindwa kuthibiti mashabiki wake.
Kwa maana hiyo matokeo ya mchezo huo yamefutwa na Mamelodi pamoja na timu za Enyima ya Nigeria na Zamalek ya Misri wamebakishwa kwenye kundi hilo la B, ambalo kwa sasa litakuwa likiongozwa na Zamalek waliifunga Enyimba ugenini kwa bao 1-0.
Kwa muda mrefu klabu kutoka Afrika Kaskazini kupitia mashabiki wake wamekuwa wepesi wa kufanya vurugu na kuvuruga mechi zinazochezwa viwanja vyao vya nyumbani na hata ugenini kwa kurusha fataki na vikokoro vingine hasa zikifungwa.

Vurugu hizi ndizo zilizoing'oa ES Setif Ligi ya Mabingwa Afrika

Thursday, June 23, 2016

RB Battery yanogewa Mbeya City, yaongeza mkataba mpya

KAMPUNI ya BinSlum Tyre ya jijini Dar es Salaam, leo Alhamisi imesaini mkataba mpya wa miaka miwili wenye thamani ya Sh. 360 Milioni kuendelea kuidhamini klabu ya Mbeya City FC.
777
Mara baada ya kusaini mkataba huo, Kaimu Mkurugenzi wa kampuni hiyo, Mohammed BinSlum alisema, licha ya City kuwa na matokeo yasiyoridhishwa kwa msimu uliopita, lakini wameridhishwa kwa kiasi kikubwa namna ambavyo timu hii ilishiriki katika kuitangaza bidhaa yao  na kuifikisha sehemu ilipostahili kufika.
“City haikuwa na matokeo mazuri msimu ulipopita, lakini hatuna shaka na namna walivyoitangaza bidhaa yetu, imani yetu kubwa ni kuwa  mkataba huu mpya itakuwa chachu kwao ya kufanya vizuri zaidi msimu ujao,”  alisema BinSlum.
Naye Meya wa Jiji la Mbeya, David Mwasilindi, aliishukuru kampuni ya BinSlum kwa kuthamini mchango wa City licha ya matokeo mabaya  msimu uliopita ambapo timu hiyo ilimaliza katika nafasi ya nane.
“Hatukuwa sawa msimu uliopita, matokeo tuliyoyapata si yale ambayo tumekuwa tukiyapata misimu miwili iliyopita, imani yangu kubwa tutafanya vizuri msimu ujao, nawashukuru BinSlum kwa kutambua mchango wetu kwao, hii ni chachu kwetu kuelekea mafanikio ya msimu ujao” alisema.
ccc

Chelsea yammezea mate Koulibaly wa Napoli,

http://img.20mn.fr/txPrUEwrTRCJig7saa8abQ/2048x1536-fit_kalidou-koulibaly-lors-lazio-naples-18-janvier-2015.jpg
Kalidou Koulibaly
IKIJIANDAA kumpokea Kocha wake mpya, Antonio Conte, klabu ya Chelsea imedaiwa ipo kwenye mawindo dhidi ya beki wa Napoli, Kalidou Koulibaly ikitoa  ofa ya Pauni Milioni 19.2.
Chelsea imekuwa ikimzimia kupita kiasi beki huyo wa kimataifa wa Senegal, ambaye ameingia katika mzozo na klabu yake kuhusiana na uhamisho wake.
Licha ya mzozo huo, tayari kuna taarifa kwamba ofa hiyo ya Chelsea imeshakataliwa na Napoli ikidaiwa inataka kitita cha Pauni Milioni 30, ili imuachie nyota huyo mwenye umri wa miaka 24.
Klabu ya Napoli ilichukizwa na Koulibaly kufuatia madai aliyotoa kuwa yuko tayari kuzungumza na Chelsea.
Beki huyo alisema hajazungumza na Kocha Antonio Conte, lakini anadhani hilo litafanyika hivi karibuni, baada ya kumaliza majukumu yake ya Euro akiiongoza timu ya taifa ya Italia iliyotinga hatua ya 16 Bora kwa sasa nchini Ufaransa

Copa America 2016 ni Chile na Argentina tena

Fun and games in Chicago. 
https://heavyeditorial.files.wordpress.com/2016/06/gettyimages-542227446.jpg?quality=65&strip=all&strip=allCHILE imetinga fainali za Copa America kwa mara ya pili mfululizo na watavaana na Argentina katiak mechi inayorejea fainali za mwaka jana ambapo ilibeba taji kwa ushindi wa bao 1-0.
Watetezi hao walipata ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Colombia katika mechi ya Nusu Fainali iliyosimama kwa muda wa saa mbili kutokana na hali mbaya ya hewa ya jiji la Chicago lililotumiwa kwa mchezo huo mkali.
Mabao ya mapema ya kipindi cha kwanza kupitia kwa Charles Aranguiz aliyefunga dakika ya 7 na jingine la Jose Fuenzalida aliyetumbukiza kimiani dakika 11 yalitosha kwa Chile kutinga fainali na sasa itavaana na Argentina iliyotangulia mapema jana.
Argentina iliisasambua wenyeji Marekani kwa kuicapa mabao 4-0, huku nahodha Lionel Messi akifunga bao la tatu lililomfanya aweke rekodi ya kuwa Mfungaji Bora wa muda wote wa taifa hilo akifikisha bao la 55 na kuipiku rekodi ya Gabriel Batistuta aliye na mabao 54.
Katika fainali zilizopita Argentina ilikubali kipigo cha mkwaju ya penalti 4-1 na kuwapa wenyeji Chile taji lao la kwanza katika historia ya michuano hiyo iliyoasisiwa miaka 100 iliyopita (1916).
Pambano hilo la fainali za mwaka huu zitachezwa Jumapili kwenye Uwanja wa
MetLife, East Rutherford ambapo pia mbali na mataifa hayo kusaka ubingwa pia zitakuwa katika vita ya nyota wao, Eduardo Vargas wa Chile mwenye mabao 6 na Messi mwenye mabao matano watakaokuwa wakiwania Kiatu cha Dhahabu
.

Chile ilivyoifuata Argentina fainali za Copa America 2016

Ronaldo azinduka, Ureno yapenya 16 Bora, Ufaransa, Ireland kimbembe

ronaldo.jpg
Ronaldom akishangilia moja ya mabao yake ya usiku wa kuamkia leo yaliyoibeba Ureno kuambulia sare na kutinga 16 Bora
CRISTIANO Ronaldo ameondoa gundu kwa kuifungia timu yake mabao mawili wakati Ureno ikisaka sare ya tatu mfululizo katika mechi zake za Kundi F za michuano ya Kombe la Mataifa ya Ulaya (Euro 2016) dhidi ya Hungary.
Timu hizo zilitoshana nguvu kwa kufungana mabao 3-3, huku Ureno kupitia Ronaldo wakilazimika kusawazisha mara zote kuambulia pointi iliyowabeba kama mshindwa bora.
Sare hiyo imeisaidia Ureno kuingia hatua ya mtoano ya 16 Bora kama mshindi wa tatu na sasa itakutana na Croatia katika mechi itakayopigwa Jumamosi hii.
Iceland inayoshiriki kwa mara ya kwanza imendelea kufanya maajabu kwa kupata ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Austria na kusonga mbele kama mshindi wa pili wa kundi hilo wakilingana pointi na vinara Hungary.
Italia nayo ilipoteza mechi yake ya mwisho dhidi ya Ireland nma Belgium ikaizabua Sweden bao 1-0 na kumtia aibu Zlatan Ibrahimovic ambaye amestaafu timu hiyo akishindwa kuifungia timu yake bao lolote katika fainali hizo za Euro 2016. Sweden imeaga michuano hiyo ikiwa ina pointi moja na bao moja la kufunga.
Kwa mujibu wa ratiba ya hatua hiyo ya 16 Bora, wenyeji Ufaransa watavaana na Ireland na kukumbushia tukio la mwaka 2010 wakati Thierry Henry alipoivusha timu yake kwa bao la mkono dhidi na wapinzani wao hao.
Ratiba kamili ya 16 Bora ipo hivi:
Juni 25, 2016
Uswisi  v    Poland       
Wales    v   Ireland ya Kaskazini
Croatia v    Ureno

Juni 26, 2016
Ufaransa    v Ireland       
Ujerumani v Slovakia
Hungary    v Belgium       

Juni 27, 2016
Italia      v Hispania
England v Iceland

Wednesday, June 22, 2016

Hapana chezea Isha Mashauzi

Zaidi ya watu 30 wauwawa Libya

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhCVr1da4GQufI6f7fv74iiVc0627Y6UABJL2guBHijQ6toVF7TK8gi380ZbSoUtUUVH7wRW8kPQLhJ84quuCFQ70x6TfQm4AOJ0kHsrTISXMtUavqoZf2nwsmqE0FxYfqDzLHlJRby3gE/s1600/Wapiganaji+wa+NTC+mjini+Sirte.jpg
Picha haihusiani na taarifa hii
SIMANZI. Zaidi ya watu 30 wamepotea maisha katika mapigano baina ya Jeshi la Libya na wapiganaji wa kikundi cha IS.
Inaelezwa mapigano hato yamesananisha vifo hivyo, huku mamia wakiachwa majeruhi, kipindi hiki ambacho waumini wa Kiislam wapo kwenye Mfungo wa Ramadhani.
Kwa mujibu wa BBC Swahili, Msemaji wa hospitali moja alisema kuwa wapiganaji 36 wameuawa huku wengine karibu 140 wakijeruhiwa katika mji wa Sirte ambao ni ngome ya Islamic state.
Wakati huo huo taarifa zinasema kuwa idadi ya watu waliouawa wakati mlipuko ulitokea katika ghala la silaha kwenye mji ulio magharibi wa Garabulli imeongezeka hadi watu 29.
Ghala hilo liliripotiwa kuwa ndani ya kambi inayotumiwa na wapiganaji kwenye mji wa Misrata pwani ya nchi.

TFF mnatania au mnawataka ubaya Wekundu wa Msimbazi?!

http://www.timesfm.co.tz/wp-content/uploads/2016/04/Alfred-Lucas.png
Afisa Habari wa TFF, Alfred Lucas
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEguD-aZGG5X59TJ_U5wBcN4j_dmq1GHSge94N-6O3EvLKtFeSYpVKM2frwbCVbwcv0jznXiFEatblJrg-Z12VhIt6yK2CbIpq0_jojZb5CdYPWrHCiCJMnlQSiO1lCdWepV75H9GbZSbkk/s1600/MMG25686.jpg
Mashabiki wa Al Ahly wakipewa sapoti na mashabiki wa Simba wakati wa mechi baina ya Wamisri hao na Yanga lililochezwa Uwanja wa Taifa hivi karibuni
BILA shaka Simba watakuwa wanacheka huko walipo, baada ya kulisikia Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) likiwaangukia na kuwataka wawe na uzalendo kwa kuishangilia Yanga itakapokuwa ikiumana na TP Mazembe Jumatano ijayo.
Simba na Yanga kwa miaka mingi zimekuwa zikishindwa kupigana tafu kwenye mechi zao za kimataifa, kwa tabia yao ya kushangilia wageni na kufikia hatua ya kuvaa jezi ya timu pinzani inayocheza na mmoja wao, lakini TFF kupitia Afisa Habari wake, Alfred Lucas imewaomba mashabiki kuwa wazalendo kuisapoti Yanga.
Lucas alisema TFF inawaomba mashabiki waje kwa wingi uwanjani kwa ajili ya kushangilia kwani wanaamini mashabiki ni mchezaji wa 12 na uwepo wao utaongeza ari ya ushindi.
"Tunafahamu mchezo wa Yanga utakuwa na changamoto zake kwa vile  wameanza kwa kufungwa na TP Mazembe wanaongoza kundi lakini tunaamini watafanya vizuri kwani inachezwa kwa mtindo wa ligi hivyo mashabiki waje kushangilia timu zetu.", alisema Lucas.
Yanga itacheza na Mazembe Juni 29 kwenye mchezo wa Kundi A ya michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika na kusisitiza kuwa mafanikio ya Yanga ni faida kwa soka la Tanzania na kuomba mashabiki kujitokeza kwa wingi kuiunga mkono kama ambavyo anataka wajitokeze Jumapili kuishangilia Serengeti Boys itakayocheza na  Shelisheli mchezo wa kuwania kufuzu fainali za Vijana U17 Afrika.

Tayari mashabiki wa Simba wameshaanza kununua jezi za Mazembe ili kuwaunga mkono katika mechi hiyo na iwapo watasikia ombi hilo la TFF lazima wataumia mbavu kwa kucheka kwani ni jambo lisilowezekana kwao kama ambavyo kigogo wa klabu hiyo, Zakaria Hanspoppe aliwahi kukaririwa akisema huwa anahisi kichefuchefu akitajiwa jina la Yanga.

Jose Mourinho kumvuta Matic Man United

Matic na Mourinho walipokuwa Chelsea
KOCHA Mpya wa klabu ya Manchester United, Jose Mourinho anatarajiwa kumchukua nyota wake wa zamani aliyemnoa akiwa Chelsea kwa kubadilishana na Mchezaji wake mmoja kwa mujibu wa duru za kispoti za England.
Imeripotiwa kuwa wakati dirisha la usajili likitarajkiwa kufunguliwa Julai Mosi, Kocha Mourinho anatarajiwa kuitumia shauku ya Meneja mpya wa Chelsea kutoka Italy, Antonio Conte ya kumhusudu beki toka Italia, Matteo Darmian kwa kumtoa kama Ofa ya kumchukua kiungo wa Chelsea Nemanja Matic.
Tayari Mourinho ameshaanza kuisuka upya Man United kwa kumnunua beki wa kati kutoka Villareal, Eric Bailly na anatarajiwa kuongeza wapya wengine.
Matic, Mchezaji wa Kimataifa wa Serbia, alikuwa nyota wa kwanza kwa Mourinho kumnunua aliporudi Chelsea kwa mara ya pili kwa kumsaini mwaka 2014 kutoka Benfica na sasa inaelekea Mourinho anataka kuungana tena na Matic.
Chini ya Mourinho, Matic alikuwa na msimu mzuri wa kwanza huko Stamford Bridge na kuweza kutwaa Ubingwa wa England, lakini Msimu uliopita, hasa Mourinho alipotimuliwa Desemba mwaka jana, Matic hakuwa na namba mara kwa mara kikosini.
Haijulikani kama Matic atakuwa vipi chini ya Kocha Conte ambae bado hajatua rasmi huko Chelsea kwani yupo bado yupo na kikosi cha timu ya taifa ya Italia katika fainali za Euro 2016 zinazoendelea Ufaransa.
Magazeti huko England yamedai Darmian yupo kwenye uhusiano mzuri na Conte katika timu ya Italia, kwani panga pangua hakosi namba na hilo limeleta imani kuwa anamtaka wawe wote Chelsea.
Darmian amekuwa na msimu mchanganyiko Man United ambako alitua mwaka jana kutoka Torino ya Italia na hilo, pengine ndio linamfanya Mourinho amtoe kafara ili amnase Matic ambae hucheza kwa kutumia nguvu katikati ili kuimarisha safu yake mpya.

Yanga yaamua kuwachezesha Mazembe usiku

Kikosi cha Yanga

Mashabiki watakaoishangilia timu yao usiku Uwanja wa Taifa
Baadhi ya nyota wa Yanga akiwamo Nahodha Nadir Haroub Cannavaro atakayekuwepo kuivaa Mazembe
IMEFAHAMIKA kuwa, pambano la Yanga dhidi ya TP Mazembe la Kundi A michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika litapigwa usiku wa Jumatano na sio Jumanne kama ilivyotangazwa awali.
Kwa mujibu kutoka kwa Msemaji wa klabu hiyo, Jerry Muro, mechi yao itapigwa majira ya saa 1:30 usiku kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Muro alisema wameamua kulipeleka pambano lao Jumatano usiku ili kutoa fursa ya mashabiki wengi kuhudhuria baada ya kutoka kazini na wakishakula futari ikizingatiwa kwa sasa waumini wa Kiislam wapo kwenye mfungo wa Ramadhani.
Msemaji huyo alisema maandalizi yao kuelekea kwenye mchezo huo yapo shwari na kwamba wana uhakika wa kuwatumia baadhi ya nyota wao wapya ambao wamewasajili hivi karibuni akiwamo Mzambia, Obrey Chirwa, licha ya kwamba kuna nyota wao wengine watawakosa kwa kasi za njano walizopewa Bejaia Algeria.
Yanga ilipoteza mchezo wao wa kwanza wa kundi hilo dhidi ya MO Bejaia kwa kulala bao 1-0, wakati Mazembe watakaotua nchini Jumapili hii wakitokea kwao Lubumbashi waliitambia Medeama ya Ghana kwa mabao 3-1 na kuongoza msimamo.

Real Madrid yathibitisha kumrudisha Morata Santiago Bernabeu

http://i.dailymail.co.uk/i/pix/2015/09/15/21/2C5ADD7700000578-3235796-image-a-30_1442348975933.jpgWAMEPANIA si mchezo. Mabingwa wa soka Ulaya, Real Madrid wamethibitisha kuwa Alvaro Morata atarejea Santiago Bernabeu kipindi hiki cha kiangazi. Taarifa z klabu hiyo zinasema kuwa, hakuna kizuia kwa mkali huyo kurudia nyumbani.
Awali taarifa za mapema kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Juventus Beppe Marotta zilibainisha kuwa Morata anategemewa kurejea Madrid.
Madrid walikuwa na nafasi ya upendeleo ya kumnunua tena Morata mwenye umri wa miaka 23, ikiwa ni sehemu ya mkataba uliopelekea nyota huyo wa kimataifa wa Hispania kujiunga na Juventus miaka miwili iliyopita na sasa wamethibitisha kufanya hivyo.
Katika taarifa yao iliyotumwa katika mtandao, klabu ya Madrid walithibitisha taarifa hiyo na kudai kuwa Morata atajiunga na mazoezi ya maandalizi ya msimu mpya wa La Liga chini ya Kocha Zinedine Zidane.
Hata hivyo, taarifa hizo zinadai kuwa Madrid wanaweza kumuuza Morata kwa klabu nyingine ili wapate faida zaidi.

Shelisheli lazima wapigwe Taifa, kama unabisha subiri J'Pili


Wachezaji wa Serengeti Boys wakijifua mazoezi kujiandaa na mechi yao dhidi ya Shelisheli
LAZIMA wapigwe! Kocha wa timu ya taifa ya Vijana ya Tanzania U17 ‘Serengeti Boys’, Bakari Shime, amejigamba kuondoka na ushindi dhidi ya Shelisheli katika mchezo wao utakaochezwa Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam Jumapili hii.
Akizungumza jijini Dar es Salaam, Kocha Shime alisema timu yake ameiandaa vya kutosha ikiwa imepata mechi kadhaa za kimataifa za kirafiki hali iliyomwezesha kukisuka vema kikosi hicho.
“Naamini kwa maandalizi haya tutasonga mbele kwenye hatua inayofuata na vijana wana ari ya kwenda Madgascar 2017 kwenye fainali za mashindano haya”, alisema Shime.
Mchezo huo wa kuwania nafasi ya kucheza fainali za Kombe la Mataifa kwa Vijana U17 utachezeshwa na waamuzi toka Ethiopia ambao ni Belay Asserese ambaye ni mwamuzi wa kati na wasaidizi wake ni Tigle Belachew na Kinfe Yilma Kinfe huku mwamuzi wa akiba akiwa  ni Lemma Nigussie na Kamishna wa mchezo huo atakuwa ni Bester Kalombo.
Serengeti Boys iliyoingia kambini  Juni 14, 2016 itarudiana na wapinzani wao  Julai 2, 2016, endapo itafuzu hatua hii itakutana na timu ya Vijana ya Afrika Kusini.
Naye nahodha wa timu hiyo, Issa Makamba amesema wapo tayari kupambana na anaamini ushindi ni wao huku akiwataka mashabiki kuja kuwashangilia.

Man City yakaribia kunasa kifaa kingine kipya

http://estaticos.marca.com/imagenes/2015/09/24/en/football/spanish_football/1443048045_extras_noticia_foton_7_0.jpgWANAMCHUKUA. Klabu ya Manchester City, ipo hatua ya mwisho kumnasa straika wa kimataifa wa Hispania, Nolito kutoka Celta Vigo.
Nyota huyo mwenye umri wa miaka 29 amethaminishwa kwa kiasi cha Euro Milioni 18 katika mkataba wake na Rais wa Celta Vigo, Carlos Mourino tayari ameshadokeza anategemea ataondoka dirisha hili la usajili.
Taarifa zilizotolewa na gazeti la Guardian la Uingereza zimedai kuwa, Man City ina uhakika wa kukamilisha dili hilo na kuongeza kuwa Nolito tayari ameshakubali mambo binafsi katika mkataba wa miaka mitatu atakaopewa wenye thamani ya Euro Milioni 4 kila msimu.
Straika huyo wa zamani wa Barcelona, aliyeichezea timu yake ya taifa ya Hispania katika mechi zote tatu za makundi ya michauno ya Euro 201, awali alikuwa akitajwa kuwindwa na timu yake ya zamani ya Barcelona iliyotaka kumrejesha kikosini.
Nyota huyo mwenye bao moja kwenye michuano hiyo ya Euro inayoendelea nchini Ufaransa, aliondoka Nou Camp mwaka 2011 kwenda Ureno kujiunga na Benfica  kabla ya baadaye kutua Celta Vigo.

Wednesday, June 15, 2016

HII NDIYO RATIBA YA LIGI KUU ENGLAND 2016-2017

http://media2.intoday.in/indiatoday/images/stories/epllogofb-story_647_020916090038.jpg
Logo Mpya ya EPL
UTAMU unakaribia. Ratiba ya Ligi Kuu ya England kwa msimu mpya wa 2016-2017 imetoka, ambapo Liverpool imepewa mtihani wa kuanza nyumbani kwa Arsenal Agosti 13,, huku Chelsea wakiwa na Kocha Mpya Antonie Conte wataanzia nyumbani dhidi ya West Ham. Man United ikiwa na Jose Mourinho itaanzia ugenini dhidi ya Bournemouth na Man City ya Pep Guardiola itakuwa nyumba katika ufunguzi wa ligi hiyo dhidi ya Sunderland.
Chungulia ratiba nzima ya ligi hiyo yenye umaarufu mkubwa duniani.
http://www.murrayunitedfc.com.au/wp-content/uploads/2015/04/EPL-Banner.jpg

Ufunguzi Ago 13, 2016
Bournemouth v Man United
Arsenal          v Liverpool
Burnley          v Swansea City
Chelsea          v West Ham
Crystal Palace v West Brom
Everton           v Tottenham
Hull City         v Leicester City
Man City         v Sunderland
Middlesbrough    v Stoke City
Southampton     v Watford

Ago 20, 2016Leicester City     v Arsenal
Liverpool         v Burnley
Man United     v Southampton
Stoke City     v Man City
Sunderland     v Middlesbrough
Swansea City     v Hull City
Tottenham     v Crystal Palace
Watford         v Chelsea
West Brom    v Everton
West Ham     v Bournemouth

Ago 27, 2016
Chelsea         v Burnley
Crystal Palace     v Bournemouth
Everton         v Stoke City
Hull City         v Man United
Leicester City     v Swansea City
Man City         v West Ham
Southampton     v Sunderland
Tottenham     v Liverpool
Watford         v Arsenal
West Brom    v Middlesbrough
Sept 10, 2016
Bournemouth     v West Brom
Arsenal         v Southampton
Burnley         v Hull City
Liverpool         v Leicester City
Man United     v Man City
Middlesbrough     v Crystal Palace
Stoke City     v Tottenham
Sunderland     v Everton
Swansea City     v Chelsea
West Ham      v Watford

Sept 17, 2016Chelsea         v Liverpool
Crystal Palace     v Stoke City
Everton         v Middlesbrough
Hull City         v Arsenal
Leicester City     v Burnley
Man City         v Bournemouth
Southampton     v Swansea City
Tottenham     v Sunderland
Watford         v Man United
West Brom     v West Ham

Sept 24, 2016

Bournemouth     v Everton
Arsenal         v Chelsea
Burnley         v Watford
Liverpool         v Hull City
Man United     v Leicester City
Middlesbrough     v Tottenham
Stoke City     v West Brom
Sunderland     v Crystal Palace
Swansea City     v Man City
West Ham     v Southampton

Okt 01, 2016Burnley         v Arsenal
Everton         v Crystal Palace
Hull City         v Chelsea
Leicester City     v Southampton
Man United     v Stoke City
Sunderland     v West Brom
Swansea City     v Liverpool
Tottenham     v Man City
Watford         v Bournemouth
West Ham      v Middlesbrough

Okt 15, 2016

Bournemouth     v Hull City
Arsenal         v Swansea City
Chelsea         v Leicester City
Crystal Palace     v West Ham
Liverpool         v Man United
Man City         v Everton
Middlesbrough     v Watford
Southampton     v Burnley
Stoke City     v Sunderland
West Brom     v Tottenham

Okt 22, 2016Bournemouth     v Tottenham
Arsenal         v Middlesbrough
Burnley         v Everton
Chelsea         v Man United
Hull City         v Stoke City
Leicester City     v Crystal Palace
Liverpool         v West Brom
Man City         v Southampton
Swansea City     v Watford
West Ham     v Sunderland
 
Okt 29, 2016
Crystal Palace     v Liverpool
Everton         v West Ham
Man United     v Burnley
Middlesbrough     v Bournemouth
Southampton     v Chelsea
Stoke City     v Swansea City
Sunderland     v Arsenal
Tottenham     v Leicester City
Watford         v Hull City
West Brom    v Man City

http://e2.365dm.com/16/03/768x432/leicester-behind-scenes_3431711.jpg?20160315160213Nov 05, 2016Bournemouth     v Sunderland
Arsenal         v Tottenham
Burnley         v Crystal Palace
Chelsea         v Everton
Hull City         v Southampton
Leicester City     v West Brom
Liverpool         v Watford
Man City         v Middlesbrough
Swansea City     v Man United
West Ham     v Stoke City

Nov 19, 2016Crystal Palace     v Man City
Everton         v Swansea City
Man United     v Arsenal
Middlesbrough     v Chelsea
Southampton     v Liverpool
Stoke City     v Bournemouth
Sunderland     v Hull City
Tottenham     v West Ham
Watford         v Leicester City
West Brom    v Burnley

Nov 26, 2016Arsenal         v Bournemouth
Burnley         v Man City
Chelsea         v Tottenham
Hull City         v West Brom
Leicester City     v Middlesbrough
Liverpool         v Sunderland
Man United     v West Ham
Southampton     v Everton
Swansea City     v Crystal Palace
Watford         v Stoke City

Des 03, 2016Bournemouth     v Liverpool
Crystal Palace     v Southampton
Everton         v Man United
Man City         v Chelsea
Middlesbrough     v Hull City
Stoke City     v Burnley
Sunderland     v Leicester City
Tottenham     v Swansea City
West Brom    v Watford
West Ham     v Arsenal

Des 10, 2016Arsenal         v Stoke City
Burnley         v Bournemouth
Chelsea         v West Brom
Hull City         v Crystal Palace
Leicester City     v Manchester City
Liverpool         v West Ham
Man United     v Tottenham
Southampton     v Middlesbrough
Swansea City     v Sunderland
Watford         v Everton

Des 13, 2016

Bournemouth     v Leicester City
Crystal Palace     v Man United
Middlesbrough     v Liverpool
Sunderland     v Chelsea
West Brom    v Swansea City
West Ham     v Burnley
 

Des 14, 2016
Everton         v Arsenal
Man City         v Watford
Stoke City     v Southampton
Tottenham    v Hull City
 

Des 17, 2016
Bournemouth     v Southampton
Crystal Palace     v Chelsea
Everton         v Liverpool
Man City         v Arsenal
Middlesbrough     v Swansea City
Stoke City     v Leicester City
Sunderland     v Watford
Tottenham     v Burnley
West Brom    v Manchester United
West Ham     v Hull City

Des 26, 2016

Arsenal         v West Brom
Burnley         v Middlesbrough
Chelsea         v Bournemouth
Hull City         v Man City
Leicester City     v Everton
Liverpool         v Stoke City
Man United     v Sunderland
Southampton     v Tottenham
Swansea City     v West Ham
Watford         v Crystal Palace

Des 31, 2016

Arsenal         v Crystal Palace
Burnley         v Sunderland
Chelsea         v Stoke City
Hull City         v Everton
Leicester City     v West Ham
Liverpool         v Man City
Man United     v Middlesbrough
Southampton     v West Brom
Swansea City     v Bournemouth
Watford         v Tottenham

Jan 02, 2017

Bournemouth     v Arsenal
Crystal Palace     v Swansea City
Everton         v Southampton
Man City         v Burnley
Middlesbrough     v Leicester City
Stoke City     v Watford
Sunderland     v Liverpool
Tottenham     v Chelsea
West Brom     v Hull City
West Ham     v Man United

Jan 14, 2017

Burnley         v Southampton
Everton         v Man City
Hull City         v Bournemouth
Leicester City     v Chelsea
Man United     v Liverpool
Sunderland     v Stoke City
Swansea City     v Arsenal
Tottenham     v West Brom
Watford         v Middlesbrough
West Ham     v Crystal Palace

Jan 21, 2017Bournemouth     v Watford
Arsenal         v Burnley
Chelsea         v Hull City
Crystal Palace     v Everton
Liverpool         v Swansea City
Man City         v Tottenham
Middlesbrough     v West Ham
Southampton     v Leicester City
Stoke City     v Man United
West Brom     v Sunderland

Jan 31, 2017Bournemouth     v Crystal Palace
Arsenal         v Watford
Burnley         v Leicester City
Man United     v Hull City
Middlesbrough     v West Brom
Sunderland     v Tottenham
Swansea City     v Southampton
West Ham     v Man City

Feb 01, 2017Liverpool         v Chelsea
Stoke City     v Everton

Feb 04, 2017
Chelsea         v Arsenal
Crystal Palace     v Sunderland
Everton         v Bournemouth
Hull City         v Liverpool
Leicester City     v Man United
Man City         v Swansea City
Southampton     v West Ham
Tottenham     v Middlesbrough
Watford         v Burnley
West Brom     v Stoke City

Feb 11, 2017Bournemouth     v Man City
Arsenal         v Hull City
Burnley         v Chelsea
Liverpool         v Tottenham
Man United     v Watford
Middlesbrough     v Everton
Stoke City     v Crystal Palace
Sunderland     v Southampton
Swansea City     v Leicester City
West Ham     v West Brom

Feb 25, 2017

Chelsea         v Swansea City
Crystal Palace     v Middlesbrough
Everton         v Sunderland
Hull City         v Burnley
Leicester City     v Liverpool
Man City         v Man United
Southampton     v Arsenal
Tottenham     v Stoke City
Watford         v West Ham
West Bro         v Bournemouth

Mar 04, 2017Leicester City     v Hull City
Liverpool         v Arsenal
Man United     v Bournemouth
Stoke City     v Middlesbrough
Sunderland     v Man City
Swansea City     v Burnley
Tottenham     v Everton
Watford         v Southampton
West Brom     v Crystal Palace
West Ham     v Chelsea

Mar 11, 2017Bournemouth     v West Ham
Arsenal         v Leicester City
Burnley         v Liverpool
Chelsea         v Watford
Crystal Palace     v Tottenham
Everton         v West Brom
Hull City         v Swansea City
Man City         v Stoke City
Middlesbrough     v Sunderland
Southampton     v Man United

Mar 18, 2017
Bournemouth     v Swansea City
Crystal Palace     v Watford
Everton         v Hull City
Man City         v Liverpool
Middlesbrough     v Man United
Stoke City     v Chelsea
Sunderland     v Burnley
Tottenham     v Southampton
West Brom     v Arsenal
West Ham      v Leicester City

Apr 01, 2017Arsenal         v Man City
Burnley         v Tottenham
Chelsea         v Crystal Palace
Hull City         v West Ham
Leicester City     v Stoke City
Liverpool         v Everton
Man United     v West Brom
Southampton     v Bournemouth
Swansea City     v Middlesbrough
Watford         v Sunderland

Apri 04, 2017

Arsenal         v West Ham
Burnley         v Stoke City
Hull City         v Middlesbrough
Leicester City     v Sunderland
Man United     v Everton
Swansea City     v Tottenham
Watford         v West Brom

Apr 05, 2017
Chelsea         v Man City
Liverpool         v Bournemouth
Southampton     v Crystal Palace

Apr 08, 2017Bournemouth     v Chelsea
Crystal Palace     v Arsenal
Everton         v Leicester City
Man City         v Hull City
Middlesbrough     v Burnley
Stoke City     v Liverpool
Sunderland     v Man United
Tottenham     v Watford
West Brom    v Southampton
West Ham      v Swansea City

Apr 15, 2017Crystal Palace     v Leicester City
Everton         v Burnley
Man United     v Chelsea
Middlesbrough     v Arsenal
Southampton     v Man City
Stoke City     v Hull City
Sunderland     v West Ham
Tottenham     v Bournemouth
Watford         v Swansea City
West Brom    v Liverpool

Apr 22, 2017Bournemouth     v Middlesbrough
Arsenal         v Sunderland
Burnley         v Man United
Chelsea         v Southampton
Hull City         v Watford
Leicester City     v Tottenham
Liverpool         v Crystal Palace
Man City         v West Brom
Swansea City     v Stoke City
West Ham     v Everton

Apr 29, 2017Crystal Palace     v Burnley
Everton        v Chelsea
Man United     v Swansea City
Middlesbrough     v Man City
Southampton     v Hull City
Stoke City     v West Ham
Sunderland     v Bournemouth
Tottenham     v Arsenal
Watford         v Liverpool
West Brom    v Leicester City

Mei 06, 2017Bournemouth     v Stoke City
Arsenal         v Man United
Burnley         v West Brom
Chelsea         v Middlesbrough
Hull City         v Sunderland
Leicester City     v Watford
Liverpool         v Southampton
Man City         v Crystal Palace
Swansea City     v Everton
West Ham     v Tottenham

Mei 13, 2017Bournemouth     v Burnley
Crystal Palace     v Hull City
Everton         v Watford
Man City         v Leicester City
Middlesbrough     v Southampton
Stoke City     v Arsenal
Sunderland     v Swansea City
Tottenham     v Man United
West Brom    v Chelsea
West Ham     v Liverpool

Mei 21, 2017Arsenal         v Everton
Burnley         v West Ham
Chelsea         v Sunderland
Hull City         v Tottenham
Leicester City     v Bournemouth
Liverpool         v Middlesbrough
Man United     v Crystal Palace
Southampton     v Stoke City
Swansea City     v West Brom
Watford         v Man City