STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, February 25, 2014

Ajali tena! Watu watano wafa Kilimanjaro, wanne taaban


PIcha hii haihusiki na habari hii, ila ni kati ya ajali ambazo zimekuwa zikichukua roiho za watanzania wenzetu kila uchao
AJALI za barabarani zimeendelea kuteketeza roho za watanzania baada ya watu watano kufariki katika ajali iliyohusisha magari mawili katika eneo la Boma Ng'ombe wilayani Hai mkoani Kilimanjaro.
Kwa mujibu wa taarifa zilizothibitishwa na jeshi la Polisi mkoani Kilimanjaro, watu hao walifariki jana jioni katika njia ya mzunguko ya uwanja wa ndege wa kimataifa ya KIA ikihusisha magari mawili yaliyogongana ubavuni ambapo watu wengine wanne walijeruhiwa.
Inadaiwa mwendo kasi ya magari hayo ndiyo yaliyosababisha vifo vya watu hao watano wakiwamo wanaume watatu na wanawake wawili ambao miili yao iliharibika.
Abiria wanne walionusurika kufa wapo katika hali mbaya na wamelazwa katika hospitali ya mkoa ya Maweni kwa ajili ya matibabu.

Man Utd kuvuna nini Ugiriki katika UEFA Champion League?!


ATHENS, Ugiriki
KIVUMBI cha Ligi ya Mabingwa Ulaya (UEFA Champion League) kinatarajiwa kuendelea tena leo na kesho kwa mechi nne za kumalizia mkondo wa kwanza wa hatua ya 16 Bora kuwania kucheza Robo Fainali ya michuano hiyo.
Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya England, Manchester United ambayo imefufuka kwenye ligi ya nyumbani leo itakuwa ugenini nchini Ugiriki kuvaana na Olympiakos Piraeus wiuki moja baada ya timu za Manchester City na Arsenal kupoteza mechi zao za nyumbani dhidi ya Barcelona na Bayern Munich.
Mechi nyingine ya leo itazikutanisha timu za Zenit St Petersburg dhidi ya wana fainali wa mwaka jana,  Dortmund ya Ujerumani.
Katika mechi ya Manchester United dhidi ya Olympiakos Piraeus, wagiriki hao hawajawahi kufanya vyema mbele ya Mashetani Wekundu, japo wenyewe wamenukuliwa wakiapa kwamba piga ua leo ni lazima waigaragaze vijana wa David Moyes.
Mashetani Wekundu waliopata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Crysral Palace kwenye mechi yao ya ligi mwishoni mwa wiki, itahitaji kufanya vyema leo ugenini ili kufufua matumaini ya timu za England kuvuka katika hatua hiyo.
Hata hivyo itakuwa na kazi ngumu kuhakikisha wanaifunga  vinara hao wa Ligi Kuu ya Ugiriki ambao wamefika hatua hiyo ya mtoano kwa mara ya kwanza ndani ya kipindi cha miaka minne.
Wagiriki hao wataweka historia kama wataifunga United baada ya kupoteza mara nne katika michuano ya hivi karibuni ilipokutana nayo.
Hata hivyo, kwa sasa Olympiakos Piraeus ipo katika kiwango kizuri baada ya kucheza mechi 26 za ligi bila kupoteza huku ikiongoza kileleni mwa Ligi Kuu ya Ugiriki maarufu kama Super League.
Wakati United Jumamosi ikishinda 2-0 dhidi ya Crystal Palace, Olympiakos iliichapa OFI Crete mabao 4-0 huku Mserbia Marko Scepovic aliyesajiliwa hivi karibuni akifunga mara tatu ‘hat-trick’ yake ya kwanza katika maisha yake kisoka.
"Ningependa kuona hali kama hii, na hamu ya wachezaji wangu dhidi ya United kama walivyoonyesha dhidi ya OFI," kocha Michel alisema wakati timu yake ikipata ushindi wa 24 katika mechi 26 za ligi ilizocheza.
"Kila mechi tunakabiliana nayo kwa umakini sana na tunaamini tutapata matokeo mazuri sana Jumanne (leo)," alisema mshambuliaji huyo wa zamani na wa Real Madrid na Hispania ambaye kwa sasa ana miaka 50.
"Tumegeuza ukurasa mpya na akili zetu sasa tunazielekeza katika Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya United, ninaweza kuona hamu ndani ya macho na katika sura ya wachezaji wangu; wako tayari kwa hilo," aliahidi katika ukurasa wake wa Facebook juzi.
Michel atawakosa baadhi ya wachezaji wake wakongwe baada ya mshambuliaji wa zamani wa Argentina Javier Saviola kuwa majeruhi wa mguu. Kukosekana kwa Saviola inamaana Mnigeria Michael Olaitan mwenye miaka 21 kwa sasa, ambaye amefunga mabao nane katika mechi 15 alizocheza, atapata nafasi ya kuanza sambamba na kiungo mshambuliaji wa Argentina Alejandro Dominguez atakayecheza nyuma yake.
United imesafiri kwenga Ugiriki hiyo ikiwa nafasi pekee kwao msimu huu ya kutwaa kombe lakini hata hivyo matarajio hayo ni madogo sana kwa ubora wao kwa sasa.
Katika mechi hiyo, United itakuwa ikimtegemea zaidi Wayne Rooney (pichani) aliyepewa mkataba mnono wa paundi 300,000 kwa wiki huku akifunga bao safi mwishoni mwa wiki.
Pia, kocha David Moyes atakuwa na uwanja mpana zaidi wa kumjumuisha Marouane Fellaini katika kikosi chake cha kwanza baada ya kuwa majeruhi kwa muda mrefu.
Juu ya pambano la Zenit dhidi ya Dotmund, mashabiki wa timu ya Ujerumani watapewa ofa ya chai na vitafunwa kwa Zenit St Petersburg leo, lakini ukarimu huo hautakuwapo dimbani kwani miamba hiyo ya Urusi imepania kufika robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa mara ya kwanza.
Kocha wa Zenit, Luciano Spalletti anafurahia kiwango cha timu yake kwa sasa; "Tumecheza Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa muda mrefu sasa, na tumepigana vema msimu huu. Tumekuwa na wachezaji wengi bora jambo linalomaanisha tunaweza kucheza kwa kiwango hiki."
Aliongeza: "Tulitoka sare nyumbani na Porto tulipopaswa kushinda, na ilikuwa hali kama hiyo dhidi ya Austria Vienna, tulipocheza tukiwa 10 uwanjani zaidi ya sasa moja.
"Tulipaswa kunyakua pointi nyingi zaidi, lakini kwa ujumla tunaweza kuwa na furaha kwa kiwango chetu."
Dortmund ilisonga mbele baada ya kuwa kinara wa kundi lao lilokuwa likizijumuisha Napoli, Arsenal na Olympique Marseille kwa kufikisha pointi 12 sawa na vijana wa Arsene Wenger na wa Rafa Benitez lakini wastani mzuri wa mabao ya kufunga na kufungwa ndiyo yaliyoibeba miamba hiyo ya Ujerumani ambayo msimu huu haitisha kwenye ligi ya nyumbani.
Baada ya kutwaa ubingwa wa Bundesliga 2011 na 2012 na kumaliza ya pili msimu uliopita, imekuwa ikipanda na kushuka msimu huu na kwa sasa inashika nafasi ya tatu.
Jumamosi ilipata kipigo kikubwa zaidi ugenini msimu huu baada ya kuchapwa 3-0 na Hamburg SV lakini kocha Juergen Klopp anaamini watafanya vizuri leo.
"Tumewahi kufanya vizuri katika Ligi ya Mabingwa Ulaya baada ya kufanya vibaya kwenye ligi ya nyumbani," alisema.
"Ni mashindano tofauti kabisa," aliongeza kiungo Nuri Sahin. "Tutajiandaa vema huko St Petersburg na tunahitaji kupata matokeo mazuri na kurudi nayo Dortmund."

Tiko Hassan: Kimwana anayetaka mabadiliko, nidhamu Bongo Movie

Msanii Tiko Hassan katika pozi
"NAAMINI kama wasanii wa kike watajitambua na kutulia kwa kuepuka skendo na mambo ya upuuzi ni rahisi kwao kupata tenda zinazoweza kuwaingizia pato la ziada nje ya fani zao kama ilivyo kwa wanamichezo au wasanii wa kimataifa wanaotamba kwa utajiri duniani."
Ndivyo anavyosema Tiko Hassan 'Tiko' mmoja wa waigizaji nyota wa filamu nchini, akizungumzia namna anavyokerwa na baadhi ya wasanii wenzake wa kike wanavyojisahau na kujikita kwenye mambo ya ovyo kiasi cha kuchafua sifa ya sanaa na kuwafanya wasanii wote kuonekana wa ovyo.
"Kwa kweli hili jambo linakera kwa sababu jamii inatutazama kama watu tusiojiheshimu na hata wakati mwingine tunakosa nafasi ya kutumika kama mabalozi wa kutangaza bidhaa na huduma za taasisi kwa sababu ya mambo tunayofanya, imefika wakati wasanii tukabadilika," anasema.
Tiko anasema ingawa kila mtu ana uhuru wa kufanya atakalo, bado wasanii wanapaswa kuwa mstari wa kwanza kulinda maadili na nidhamu ya sanaa kwa sababu inawasaidia kuwaingizia kipato hata kama siyo cha kuridhisha, lakini bado ni ajira inayopaswa kuheshimiwa.
Mwanadada huyo aliyeanza kujihusisha na sanaa tangu akiwa Shule ya Msingi Mbagala Kizuiani kisha Al Haramain, anasema kuna haja vyombo vinavyosimamia sanaa kuwa wakali dhidi ya watu wachache wanaotaka kuwaharibia kazi.
Shabiki huyo wa Yanga, anasema anaamini vyombo kama Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA), Shirikisho la Filamu Tanzania (TAFF) na hata Bongo Movie Unity wakiwa wakali wanaweza kufanya 'wavamizi' katika fani ya uigizaji kujiondoa wenyewe na kwenda kufanya upuuzi huo kwingine.

NANDIPHA
Tiko anayependa kula ugali kwa dagaa na bamia na wakati mwingine wali kwa kuku au kisamvu na maharage na kunywa juisi anasema licha ya kipaji cha kuzaliwa cha sanaa, lakini alijikuta akivutiwa na uigizaji kutokana na uigizaji wa Lesego Motsepe 'Nandipha' wa Isidingo the Need.
"Huyu dada ambaye kwa sasa ni marehemu alinifanya nami kuota kuja kuwa muigizaji kwa sababu nilikuwa navutiwa naye kupitia igizo lao la refu linaloendelea mpaka leo kwenye runinga la 'Isidingo the Need'," anasema.
Anasema baada ya kuonyesha makeke katika sanaa shuleni katikati ya miaka ya 2000 alijitosa jumla kwenye sanaa hiyo kupitia kundi la Shirikisho Msanii Afrika.
"Nakumbuka mwaka 2006 ndipo nilijitosa jumla kupitia Shirikisho Msanii Afrika na igizo langu la kwanza lilikuwa 'Chozi' kabla ya kufuatiwa na 'Darubini' kisha nikahamia kwenye filamu," anasema.
Anasema kazi ya kwanza kuicheza ilikuwa 'The Living Ghost' kisha kufuatiwa na utitiri wa filamu kama 'The Devil's Soul', 'Limbwata', 'Check in the Bible', 'My Son' , 'Melvin', Foolish Age na nyingine.
Mwanadada huyo anayefurahia sanaa kumbadilisha maisha yake kutoka kuwategemea wazazi mpaka kujitegemea mwenyewe na akiendesha biashara inayomuingizia pato la ziada anasema kati ya kazi zote alizocheza, filamu ya 'Limbwata' kwake ndiyo bomba  kwake.
"Limbwata, ndiyo filamu ambayo naamini nimeitendea haki, japo kazi nyingine ikiwamo  ya Melvin pia zinanisisimua," anasema.
Tiko anayeota kuja kuwa msanii wa kimataifa pamoja na kumiliki kampuni yake, mbali na uigizaji pia ni muimbaji na mjasiriamali akijihusisha na biashara ya urembo na nguo za wanawake.
Tiko Hassan
FURAHA
Tiko Hassan aliyezaliwa miaka kadhaa iliyopita jijini Dar es Salaam, anasema hakuna tukio la furaha kwake kama siku alipojifungua mwanae kipenzi aitwaye Aisha mwenye miaka nane, ambaye anadai ni kama rafiki na mfariji wake.
"Kwa kweli hili ndilo tukio la furaha kwangu. Aisha amenifanya nijisikie mwenye furaha na kwenye matukio ya huzuni hakuna linaloniliza kama nilipompoteza baba yangu mwaka 2005," anasema.
Msanii huyo aliyesomea kozi ya Uongozi ya Utalii katika Chuo cha African Tourism College, anasema kwa wasanii wa Bongo anamzimia na kumkubali sana Ahmed Salim maarufu kama 'Gabo' akidai akipewa sapoti kubwa anaweza kuwa 'nembo' ya Tanzania kwani ana kipaji na anajua kuigiza.
"Aah! Gabo hana mpinzani kwa sasa Tanzania, licha ya kuibuka siku za karibuni, lakini akiwezeshwa zaidi anaweza kuitoa kimasomaso Tanzania kwa kipaji alichoinacho na umahiri wake katika kuigiza," anasema Tiko ambaye hajaolewa ila ana mchumba anayetarajia kufunga naye ndoa.
Kuhusu sanaa ya Tanzania, Tiko anasema bado inahitaji mabadilkio makubwa, hasa wasanii wakongwe kujitolea kuwasaidia chipukizi badala ya kuwabania kwa kuamini watafunikwa.
"Pia ni lazima wasanii tupendane na kushirikiana bila kubaguana kwa nia ya kuendeleza mbele sanaa yetu na hasa katika kukabiliana na unyonyaji tunaofanyiwa," anasema.
Tiko anayependa kutumia muda wake wa mapumziko kuangalia movie, kuogelea, kulala na kupika anasema kama siyo sanaa huenda angekuwa 'Mama Ntilie' kwa sababu ya kupenda shughuli za jikoni na hasa kupikapika.
"Wallah, kama siyo kipaji cha sanaa naamini ningekuja kufanya kazi ya Mama Ntilie napenda sana kazi ya kupika," anasema.
Tiko anasema ukiondoa Mungu aliyemjalia kipaji na afya na kila kitu kinachomfanya amshukuru kila saa, pia anawashukuru mno wazazi wake, mchumba wake, wasanii wenzake, ndugu na jamaa wote waliomsaidia kwa namna moja au nyingine kumfikisha hapo alipo.
"Kwa kweli mbali na Mungu ninayemshukuru kila dakika kwani bila ya yeye nisingekuwa Tiko Hassan, pia nawashukuru mno wazazi wangu, mchumba wangu, marafiki na wote wanaoniunga mkono katika shughuli zangu ninazofanya kuanzia za sanaa na zile za ujasiriamali," anasema.

Monday, February 24, 2014

Hussein Bunu achekelea 'kuitungua' Simba Taifa


MSHAMBULIAJI wa JKT Ruvu, Hussein Bunu amesema amejisikia fahari mno kufanikiwa kuwatungua Simba na kupelekea kuipa kipigo timu hiyo kongwe akidai kuwa JKT walikuwa bora kuliko wapinzani wao.
JKT Ruvu iliizamisha Simba kwa mabao 3-2 katika mechi iliyochezwa kwenye uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam na Bunu alifunga bao la kuongoza dakika ya 13 tu ya mchezo kabla ya Emmanuel Switta kufunga mengine.
Akizungumza na MICHARAZO leo, Bunu alisema ingawa amekuwa akifunga mabao, katika mechi mbalimbali tangu aanze kucheza soka, lakini goli la juzi dhidi ya Simba limempata furaha kubwa kwa sababu limeibeba timu yao kuzoa pointi 3.
"Kwa kweli nimejisikia furaha sana kuwatungua Simba, bao langu nalitoa kwa familia yangu na hasa wanangu, naamini tulistahili ushindi kwani tulikuwa bora kuliko wapinzani wetu," alisema Bunu.
Bunu anayecheza pamoja na nduguye Abdallah Bunu katika timu hiyo alisema wachezaji wote wa JKT Ruvu walikuwa na lazima ya kushinda mechi hiyo baada ya kufanya vibaya mechi zao tatu zilizopita wakifungwa jumla ya mabao nane.
Walianza kwa kufungwa mabao 2-0 na Ruvu Shooting kisha kutoka suluhu na Oljoro kabla ya kuangamizwa 6-0 na Prisons.
Katika mechi hiyo ya jana mbali na Bunu mabao mengine yalioisaidia timu hiyo inayonolewa na kocha Fred Minziro yalifungwa na Emmanuel Switta aliyefunga mawili kabla ya Amissi Tambwe kuiopatia Simba mabao ya kufutia machozi.

HAYA NI MAMBO 9 USIYOYAJUA YA RAIS ROBERT MUGABE



RAIS wa Zimbabwe, Robert Mugabe amefikisha miaka 90 na wikendi hii alikuwa na bonge la sherehe siyo mchezo nchini humo katika kusherehekea maisha marefu ya kiongozi huyo.
Mugabe, alizaliwa katika kijiji cha Kutama, kusini-magharibi mwa jiji kuu Harare, alisomeshwa na wayesuti, na baadaye akawa mwalimu kabla kujiingiza katika harakati za kupigania uhuru wa Zimbabwe.
Uwanaharakati wake ulimfanya afungwe gerezani kwa miaka 11, na baadaye mwaka 1980 akawa rais wa kwanza wa Zimbabwe. Yafuatayo ni mambo tisa ambayo huenda huyajui kumhusu kiongozi huyu na ambaye yamemwezesha kuwa rais kwa muda mrefu mno.

1) Zoezi na vyakula vya kienyeji

Mugabe akionekana kuwa na furaha mno
Mugabe anapenda kufanya mazoezi. “Mimi hujihisi mgonjwa wakati sijafanya mazoezi ya viuongo vya mwili,” Bw. Mugabe alisema miaka mitatu iliyopita. Huwa anaamuka kati ya saa kumi na kumi na moja alfajiri, na kutokana na jamaa zake wa karibu, husikiliza BBC idhaa ya dunia.
Siri nyingine ya kuishi kwake kwa muda mrefu ni kuwa ywapenda sana-chakula cha kienyeji kinacholiwa sana Zimbabwe. Kisha pia, havuti sigara, ila hunywa pombe kidogo anapokula.

2) 'Kufufuka'

Ingawa kumekuwa na uvumi mara nyingi kuwa Mugabe hana afya nzuri, afya yake na kazi yake ya kisiasa yaendelea vyema kabisa. Kuhusu afya yake Mugabe alipohojiwa wakati mmoja alisema,“ Nimekufa mara nyingi-hapo ndipo humwelekea Yesu Kristo. Yesu alikufa mara moja, na akafufuka mara moja,” alisema alipotimia miaka 88.
Ingawa alilelewa katika familia ya kikatoliki-mamake alikuwa mcha Mungu-alisema alipohojiwa na kituo cha habari cha Afrika Kusini, SABC, miaka michache iliyopita, kuwa yeye si Mkristo anayetumikia dini kwa sana.

3) Shabiki mkubwa sana wa kriketi

Kwa muda mrefu amedhihirisha hadharani mapenzi ya mchezo wa kriketi. Ni patroni wa jumuiya ya mchezo wa kriketi wa Zimbabwe, ambapo nyumba yake ipo karibu na uga wa michezo wa Harare, ambapo anaweza kutazama kwa makini wakati wa michezo wa kitaifa.
“Kriketi yafanya watu wawe wangwana, na pia inawafanya watu kuwa wema,” Bw. Mugabe alisema miaka kadhaa baada ya Zimbabwe kujinyakulia uhuru. “Nataka kila mtu acheze kriketi Zimbabwe; nataka nchi ya Zimbabwe iwe nchi ya wangwana.”

4) Hapendi kushindwa

Alipokuwa kijana, Mugabe alikuwa mmakinifu na mzuri kabisa katika mchezo wa tennis,” alisema aliyekuwa mwalimu katika shule ya Wakatoliki alikosomea Mugabe. Ila, aliposhindwa katika mchezo huo, aliitupa raketi yake chini kwa hasira.
Mugabe amekiri kuwa hakuwa mzuri katika mchezo wa kandanda alipokuwa mdogo, ila kwa sasa, anapenda kuutazama mchezo huo.
Yeye ni shabiki wa vilabu vya Chelsea na Barcelona vilivyoko Uingereza na Uhispania mtawalia. “ Ninapotazama kandanda, sitaki usumbufu kutoka kwa mtu yeyote,” alisema mwaka wa 2012. “Hata mke wangu anajua mahala pa kukaa wakati wanapofunga bao uwanjani, hata mimi pia hufunga bao kwangu kwa kupiga mateke vitu vyovyote vilivyoko mbele yangu.”

5) Alipata mtoto akiwa miaka 73

Familia ya Mugabe
Ana watoto watau na mke wake wa pili, Grace Marufu, aliyekuwa karani wake. Mtoto wao wa tatu alizaliwa 1997, mwaka mmoja baada ya wao kufunga ndoa.
Mwanawe wa kwanza, Nhamodzenyika, alikufa kutokana na Malaria akiwa miaka mitatu bado wakiwa Ghana. Bw. Mugabe alinyimwa ruhusa ya kuenda Accra kuungana na mkewe kwa mazishi ya mwanawe, kwani alikuwa mfungwa wa kisiasa wa serikali ya enzi hiyo ya Rhodesia.

6) Anampenda Cliff Richard kumliko Bob Marley

Mwanasiasa wa Zimbabwe ambaye kwa sasa ni hayati, Edgar Tekere, alimwambia mwandishi wa BBC, Brian Hungwe, kuwa alipokuwa akitayarisha kadhia ya kusherehekea uhuru wa Zimbabwe 1980, Bw. Mugabe hakumtaka muimbaji Bob Marley aalikwe kutumbuiza watu, ila alimtaka muimbaji maarufu wa Uingereza, Cliff Richard. Pia anampenda Muimbaji, Jim Reeves.
Mugabe anawachukia sana wanamitindo wa rasta, na waimbaji wa mitindo ya reggae. Aliwaonya vijana wa Zimbabwe: “ Nchini Jamaica, wana uhuru wa kutumia bhangi, na wanaume huwa wakati wote wamelewa. Hawataki kuenda shule; wanataka tu kuimba, na kufuga rasta. Kama Zimbabwe, tusielekee hapo.”

7) Mvaaji wa nguo maridadi

Anapenda sana suti zinazoutosha mwili wake visawasawa na tai zinazofanana na kitambaa. Hwavutia sana wanamitindo nchini Zimbabwe kwa mavazi yake. Ila, mwanamitindo ambaye humshonea nguo zake ,Khalil Parbhoo anasema: “Bado huavlia kama mabwana wa Uingereza –hivyo ndivyo anavyopenda."

8) Anamtazama Kwame Nkrumah kama kielelezo kwake

Taarifa kuhusu hali ya kiafya ya Mugabe zimekuwa zikigonga vichwa vya habari karibuni
Bw. Mugabe alipata azma ya siasa akiwa Ghana alipokuwa mwalimu; mahali alipokutana na mke wake wa kwanza, Sally Hayfron.
Aliporudi Zimbabwe, aliwaambia wananchi jinsi Ghana ilivyojinyakulia uhuru na jinsi uhuru ni kitu kizuri. Katika mahojiano mwaka 2003, Mugabe alisema: “Niliwaambia pia kuhusu Kwame Nkrumah jinsi alivyojitolea na kuiongoza Ghana kupata uhuru;Kwame aliwaambia wananchi wa Ghana kuwa Ghana haingekuwa nchi huru bila ya jitihada na kujitolea kwa kila mtu.”

9) Ni mtu mwenye shahada nyingi

Kwa jumla, Mugabe ana shahada saba. Digrii yake ya kwanza ni kutoka katika chuo kikuu cha Fort Hare kilichoko Afrika Kusini. Alisomea digrii zake zingine kwa njia Internet-mbili akiwa gerezani-shahada hizo ni za: elimu, sayansi, sheria na usimamizi.
Amejitapa kuwa na “shahada katika ujuhula” alipokuwa akivionya vyama vya kutetea haki za wafanyakazi nchini Zimbabwe 1998 kila vilipotishia kugoma.
BBC

'Yanga funga hao Al Ahly tupumue mitaani'

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg5CJRmmKDd8vhGknUDtDYVcnpl62wp2oTcEDG45sOMtbAfwDSAFka0I8QuomB9LMv_G83RgVXn8GQnatgjvKr8TudkUaQ_Q9YlB_EOWl_vKXhWb-PaJ5EAPDba42ySX55wVr6_ZlFFH04/s1600/mko+2.jpg
Mkono wa Mkonole
MCHEKESHAJI Fadhil Omar 'Mkono wa Mkonole' ameiangukia timu anayoishabiki ya Yanga, kuhakikisha inafanya kweli mbele ya Waarabu ili kuweza kuzima kebehi wanazopewa na watani zao mitaani.
Mkono aliyepo mjini Morogoro kwa sasa akirekodi filamu mpya alisema yeye ni mnazi mkubwa wa Yanga na amekuwa akiifuatilia katika mechi zake za ndani na za kimataifa, lakini hana furaha kwa kebehi toka kwa watu wa Simba.
"Watani wetu wanatucheka eti, sisi kwa Waarabu ni kama 'Mbwa kwa Chatu', nilikuwa nawaomba wachezaji wa Yanga wasituangushe mbele ya Al Ahly, waifunge kukata mzizi wa fitina na kuwaziba midomo watani wetu," alisema.
Mkono alisema anaamini Yanga wakijipanga vyema kwa mechi ya awali ya ugenini kabla ya kuja kumalizana nao jijini Dar es Salaam wanaweza kurejea rekodi ya Simba ya mwaka 2003 waliivua ubingwa Zamalek.
"Yanga ikikaza msuli na kujipanga vyema wanaweza kurejea yaliyofanywa na Simba mwaka 2003, tunajisikia wanyonge kwa kejeli za watu wa Simba wakidai eti safari yetu kimataifa imefikia tamati kwa Al Ahly," alisema.
Yanga iliyokuwa Comoro inatarajiwa kuvaana na Al Ahly mwishoni mwa wiki hii baada ya kutinga raundi ya pili ya Ligi ya Mabingwa Afrika kwa kuing'oa Komorozine kwa jumla ya mabao 12-2.
Msanii huyo alisema haoni sababu ya Yanga kushindwa kuifanyizia Al Ahly ambao pia ndiyo mabingwa watetezi wa michuano hiyo kwa madai Jangwani wana kikosi imara na kocha mzoefu, Johannes van Der Pluijm.
Pambano hilo linatarajiwa kuchezwa siku ya Jumamosi kwenye uwanja wa Taifa, na Yanga inahitajika kushinda idadi kubwa ya mabao ili kurahisisha pambano lao la marudiano wiki ijayo mjini Cairo.
Al Ahly ndiyo mabingwa watetezi na pia wanashikilia taji la Super Cup iliyotwaa Alhamis iliyopita baada ya kuilaza CS Sfaxien ya Tunisia kwa mabao 3-2 huku wakishuhudiwa na kocha msaidizi wa Yanga, Charles Boniface Mkwasa 'Master' aliyetumwa kwenda kufanya ushushushu.

Beki Atletico Madrid presha tupu dhidi ya Real Madrid jumapili

https://pbs.twimg.com/profile_images/378800000708295411/f912c666061f41dffd5b2d51ee982b30.jpeg
Filipe Luis wa Atletico Madrid
BEKI wa Atletico Madrid, Filipe Luis amesema akili zao kwa sasa zipo kwenye mechi yao ijayo dhidi ya mahasimu wao wa jiji la Madrid, Real Madrid.
Timu hizo zinatarajiwa kuvaana Jumapili kwenye mechi ya Ligi Kuu ya Hispania huku zikiwa kwenye mbio za kuwania ubingwa unaoshikiliwa na Barcelona.
Vijana wa kocha Diego Simeone wataivaa Real wakiwa wanauguza kipigo cha mabao 3-0 walichopewa jana ugenini na Osasuna, ambapo Filipe alisema wasingependa kurudia makosa katika mechi hiyo ya mahasimu wao.
Makosa yaliyofanywa na safu yake ya Atletico yaliifanya wenyeji kupata mabao hayo matatu yaliyoibakisha timu hiyo kwenye nafasi ya tatu nyuma ya Barcelona wakiachwa pointi tatu nyuma na Real Madrid wanaoongoza msimamo wa ligi.
Beki huyo wa Kibrazil, anafahamu ugumu unaowakabili dhidi ya timu hiyo kwenye kiwango bora kwa sasa Real Madrid.
Hata hivyo alinukuliwa akisema kuwa watahakikisha wanafanya kila njia kuhakikisha wanapata ushindi ili kuendeleza mbio zao za kuwania ubingwa.
"Tuna muda mrefu wa wiki nzima ya kufanya mazoezi na kujiandaa vyema kabla ya kuvaana na wapinzani wetu," Filipe alinukuliwa na tovuti ya klabu hiyo ya Atletico Madrid.
Beki huyo alisema kukabiliana na Real ni nafasi nzuri kwao ya kuthibitisha kuwa ni timu kubwa na matoeko ya jana hayawezi kuwavunja nguvu kwa sababu yanapaswa kusahauliwa na kuangali yaliyopo mbele yao.

Tomas Rosicky haondoki Arsenal-Wenger

http://img.thesun.co.uk/aidemitlum/archive/00861/Tomas_Rosicky_861146a.jpg
Tomas Rosicky
MENEJA wa Arsene Wenger, amethibitisha kuwa, Kiungo kutoka Czech Tomas Rosicky atasalia katika kikosi hicho hata baada ya msimu huu.
Rosicky aliyejiunga na Arsenal mwaka 2008 akitokea Borussia Dotmund ya Ujerumani na ameichezea klabu hiyo jumla ya mechi 208 mpaka sasa.
Kiungo huyo mwenye umri wa miaka 33 amekuwa hapati nafasi katika kikosi cha kwanza kwa siku za karibuni, jambo lililozua maneno kwamba huenda angeondoka mapema klabu hapo.
Lakini kocha Wenger alinukuliwa jaa akisisitiza kuwa mchezaji huyo ataendelea kusalia klabu kwao kwa msimu mwingine ujao.

Mugabe asherehekea miaka 90 akipinga ushoga

Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe akisherehekea siku ya kuzaliwa kwake
Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe akisherehekea siku ya kuzaliwa kwake
 
RAIS mzee kuliko wote barani Afrika na aliyedumu madarakani kwa muda mrefu nchini Zimbabwe, Robert Mugabe jan Jumapili alisherehekea miaka 90 ya kuzaliwa kwake mjini Harare. Katika hotuba iliyotolewa kwa zaidi ya saa nzima, Kiongozi  huyu mkongwe kabisa barani Afrika  alisema hataruhusu wapenzi wa jinsia moja nchini Zimbabwe. Alisema  hilo ndilo linalochangia kusambaa kwa virusi vya HIV na Ukimwi. Mugabe alinukuliwa na vyombo vya habari akielezea kuwa; “tumeumbwa kama wanaume na wanawake ili tuweze kuzaa watoto. Na hivyo ndivyo ilivyo.”
 Bw. Mugabe ambaye ametawala Zimbabwe tangu ilipopata uhuru wake mwaka wa 1980, alisema pia kuwa atapambana na ufisadi.
Matamshi yake yalifuatia kukamatwa kwa baadhi ya maafisa wa ngazi ya juu kutoka kwa shirika la ndege la kitaifa kutokana na  tuhuma za ufisadi uliohusisha dola milioni 10. Baada ya hotuba yake bwana Mugabe alikata keki kadhaa, mojawapo ikiwa na uzani wa kilo 90. Kisha wafuasi wake wakaanza kugawa zawadi ikiwemo mifugo 90 huku mfanyabiashara mmoja akimpa dola elfu 20 taslimu.
Sherehe hizo zaaminika kugharimu takriban dola milioni moja.Wanachama wa upinzani hawakuhudhuria sherehe hizo wakisema wanapinga kushindwa kwa bwana Mugabe kuokoa uchumi wa nchi unaozidi kuzorota. 
VOA

Carlos Tevez aibeba Juventus nchini Italia

Juventus striker Carlos Tevez
NYOTA wa zamani wa Manchester United na Manchester City, Carlos Teves ameendelea kuonyesha makali yake nchini Italia baada ya jana usiku kuisaidia timu yake ya Juventus kupata ushindi kiduchu wa bao 1-0 na kuzidi kujiimarisha kileleni mwa msimamo wa Seria A nchini Italia.
Tevez aliifungia Juve bao pekee katika katika pambano lao dhidi ya Torino lililochezwa kwenye uwanja wao wa nyumbani mjini Torino na kuwazima wapinzani wao wa mji huo na kuzoa pointi tatu.
Muargentina huyo alifunga bao hilo lililokuwa la 14 msimu huu katika dakika ya 30 akimalizia kazi ya Kwadwo Asamoah na kuifanya Juve kufikisha jumla ya pointi 66 ikiiwaacha wanaowafukia Roma walioshinda ugenini juzi kwa pointi 9.
Katika mechi nyingine iliyochezwa jana, Lazio ilipata ushindi wa mabao 3-2 nyumbani dhidi ya Sassuolo na leo ligi hiyo itaendelea kwa mechi mbili zitakazowakutanisha OParma dhidi ya Fiorentina na Napoli kuvaana na Genoa.






















Atletico Madrid yafumuliwa ugenini

 Osasuna celebrate
KLABU ya Atletico Madrid usiku wa kuamkia leo imeangukia pua baada ya kupokea kipigo cha mabao 3-0 ugenini dhidi ya Osasuna na kushindwa kuiengua Barcelona ambao walipoteza mechi yao juzi katika Ligi Kuu ya Hispania.
Kipigo cha timu hizo mbili zimeifanya Real Madrid kupumua kileleni, ikiwa na piinti 63, huku Barcelona na Atletico zikisaliwa na pointi zao 60 kila mmoja baada ya kucheza mechi 25 kila mmoja.
Mabao yaliyoinyong'onyesha Atletico ugenini yalifungwa naCejudo katika dakika ya 6 kabla ua Armenteros kufunga la pili dakika ya 21 na kisha Robert Torres kumalizia kazi dakika tatu kabla ya mapumziko.
Katika mechi nyingine, Rayo Vallecano iliifumuliwa nyumbani na Sevilla kwa bao 1-0, Real Betsi kulala pia nyumbani Athletic Club  na Valencia kutakata kwao kwa kuilaza Granada kwa mabao 2-1.

Ngumi zavumuka tena kanisa la Moravian

http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/c/c1/AgnusDeiWindow.jpg
WIKI ya tatu mfululizo vurugu zimeendeleakatika kanisa la Moravian baada ya jana tena kuibuka kitimtim katika kanisa la Mwananyamala Msisiri A Kinondoni Dar Es Salaam. 
Mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo alilidokeza MICHARAZO kuwa chanzo ilikuwa ni Maaskofu kutoka makao makuu ya kikanda ambao walifika na kutaka kuingia ndani ya Kanisa hilo na kuzuiwa na mmoja wa waumini.
Muumini huyo alidai kwamba Maaskofu hao wasiingie kwani mgogoro uliopo ndani ya kanisa hilo kwani utamalizwa na waumini wenyewe na kwamba kuwepo kwao kungechochea vurugu zaidi.
Wakati Maaskofu wakipinga amri hiyo, waumini ambao walikua ndani ikiwa ndio wanaanza ibada ya kwanza walisikia na ndipo wachache wakatoka nje, wengine wakishinikiza Maaskofu hao waingie huku wengine wakitaka waondoke.
Mabishano makali yaliyofuatiwa na ngumi yalizukabaina ya pande hizo mbili hadi maaskari ambao inaonekana walitonywa mapema hivyo kuwa karibu na eneo la tukio walipoingialia kati na kutuliza mtafaruku huo. 
Hata hivyo bado waumini walishinikiza kutoendelea na ibada hadi Maaskofu wa Kikanda waondoke eneo hilo na waumini kuamua kubaki nje badala ya kuendelea na ibada, wengine wakitimka kwa kuhofia vurugu zaidi.
Baadhi ya waumini waliokuwa wakiondoka walissikika wakisema kuwa heri wahamie makanisa mengine kwani hamkani si shwari tena kanisani hapo.
Inasemekana Maaskofu hao wa Kikanda walifika kanisani hapo ili kuamuru Baraza la Kanisa hilo kuvunjwa ili kupisha uchaguzi mwingine wa viongozi baada ya Baraza hilo kutuhumiwa kufuja pesa za kanisa kwa kutowasilisha mahesabu kwa waumini.
Udondozi zaidi umebaini kwamba kanisa hilo limekuwa na vurugu za chini chini ambazo inasemekana zimeanzia makao makuu ya Kanisa hilo, huku ikielezwa kwamba kumeibuka kambi mbili za uhasama, moja ikishinikiza viongozi waliopo sasa waondoke madarakani huku nyengine ikiunga mkono viongozi hao wabaki hadi uchaguzi mkuu utakapofanyika.
Chimbachimba zaidi toka kwa shuhuda huyo zimebaini kwamba tatizo la msingi ni uongozi uliopo madarakani kutowasilisha mahesabu yaliyokaguliwa (Audited Account) ya Kanisa hilo lenye vitega uchumi vingi ikiwemo Chuo Kikuu cha Theophile Kisanji.
Mgogoro ambao ulifikishwa hadi Kituo cha Polisi Oysterbay ambapo viongozi waliamuriwa kufanya mahesabu hayo na leo kuyawasilisha kwa waumini wao jambo ambalo halikufanyika hadi vurugu zilipoibuka tena.

Mabondia waonyeshana kazi Mbagala

BONDIA Mussa Shuza kushoto akioneshana umwamba na Dackson Kawiani wakati wa mpambano wao uliofanyika katika ukumbi wa Amenya Pub mbagala rangi tatu Kawiani alishinda kwa point

Mabondia Ibrahimu Ahmed kushoto na Mohamed Kashinde wakioneshana ubabe wakati wa mpambano wao uliofanyika mbagala Dar es salaam Kashinde alishinda kwa point 

Bondia Hassani Kidebe kushoto akioneshana ufundi wa kutupa makonde na Shabani Mtengela wakati wa mpambano wao Mtengela alishinda kwa point mpambano.

Sunday, February 23, 2014

TFF yaipa shushu Yanga 'kuiua' Al Ahly

MECHI namba 118 ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kati ya Yanga na Tanzania Prisons iliyokuwa ichezwe Februari 26 mwaka huu itapangiwa tarehe nyingine.

Uamuzi wa kuiondoa mechi hiyo iliyokuwa ichezwe Jumatano kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam umefanywa ili kuipa fursa zaidi Yanga kujiandaa kwa mechi yake ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi Al Ahly ya Misri itakayofanyika Jumamosi (Machi 1 mwaka huu).

Al Ahly na Yanga zitarudiana wiki moja baadaye kati ya Machi 7, 8 au 9 mwaka huu jijini Cairo, Misri.

PSG yaifumua Toulouse nyumbani, Ibrahimovic apiga hat-trick

Zlatan Ibrahimovic akishangilia moja ya mabao yake wakati wakiiangamiza Toulouse nyumbani kwao.
MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu ya Ufaransa, PSG imeendelea kuonyesha dhamira yao ya kutetea taji hilo baada ya kupata ushindi wa kishindo ugenini dhidi ya Toulouse walipoilaza mabao 4-2, huku Zlatan Ibrahimovic akifunga hat-trick yake tatu msimu huu katika ligi hiyo.
Ibrahimovic alianza kwa kufungwa kwa mkwaju wa penati katika dakika ya 32 kabla ya Wissam Ben Yedder kusawazisha dakika moja kabla ya mapumziko.
Kipindi cha pili wageni waliingia kivingine kwa kulisakama lango la wenyeji wao na kufanikiwa kupata bao la pili lililofungwa na Ezequeil Lavezzi katika dakika ya 56 kabla ya Ibarhimovic kurejea tena nyavuni kwa kufunga bao la tatu dakika ya 68 akimalizia kazi nzuri ya Yohan Cabaye.
Ben Yedder alifunga bao la pili kwa wenyeji katika dakika ya 72 na dakika moja kabla ya mchezo huo kumalizika nyota wa Sweden, Ibrahimovic alikamilisha hat-trick yake kwa kufunga bao la nne lilil;oifanya PSG kujikita zaidi kileleni ikifikisha pointi 61 baada ya michezo 26.
Katika mechi nyingine Rennes ilipata ushindi mnono wa mabao 3-0 ugenini dhidi ya Nantes kwa mabao ya Ntep, Konradsen na Toivonen.

Spurs yaduwazwa na Norwich City

Joseph Yobo tackles Paulinho during Norwich's Premier League match with Tottenham.
Norwich walipowashikisha adabu Spurs
BAO pekee lililofungwa na Robert Snodgrass katika dakika ya 47 liliiwezesha Norwich City kupata ushindi mwembamba nyumbani dhidi ya Tottenham Hotspur katika mechi ya Ligi Kuu ya England iliyomalizika muda mchache uliopita.
Kipigo hicho ambacho hakikutarajiwa na Spurs kimeifanya timu hiyo iliyotoka kupoteza mechi yake ya Ligi Ndogo ya Ulaya (Europa League), kusaliwa na  pointi 50 na kubali nafasi ya tano nyuma ya Liverpool iliyoshinda mapema leo waliowazidi pointi sita.
Mfungaji wa bao hilo alifunga kwa pasi ya Bradley Johnson na kuwaduwaza vijana wa Tim Sherwoood waliokuwa wakiwafukuza Liverpool katika mbio za kuwepo kwenye Top 4.

Ajali hii imetokea leo na kuua mmoja Moro

 Mlipuko mkubwa wakati matenki ya mafuta yakilipuka
Askari wa kikosi cha zimamoto wakijaribu kuuzima moto huo

Hakuna cha kufanyika kutokana na moto mkubwa na moshi mwingi wakati magari hayo yakiteketea


 Ankle habari. Leo asubuhi eneo la Mikese, Morogoro, tumekutana na na ajali  mbaya sana ya magari mawili, moja la mafuta, kugongana uso kwa uso na kutumbukia mtaroni na yote kushika moto. Inasadikiwa mtu mmoja ambaye ni dereva wa magari hayo kateketea kabisa kwa moto. Picha na Mdau Sixmund KWA HISANI YA MICHUZI BLOG

AC Milan yaifumua Sampdoria kwao 2-0

Adel Taarabt Adel Taarabt of Milan celebrates after scoring the opening goal during the Serie A match between SSC Napoli and AC Milan at Stadio San Paolo on February 8, 2014 in Naples, Italy.
Adel Taarabt
AC Milan imeendelea kujikongoja kwenye Ligi Kuu ya Seria A baada ya jioni hii kupata ushindi wa pili mfululizo kwa kuilaza Sampdoria nyumbani kwao kwa mabao 2-0.
Adel Taarabt alianza kuiandikia Milan bao la kwanza katika dakika ya 12 bao lililodumu hadi wakati wa mapumziko.
Kipindi cha pili vijana wa Clarence Seedorf waliingia kwa kasi na kupata bao la pili lililofungwa na Adil Rami kwenye dakika ya 58, huku Sampdoria ikimpoteza Lopez aliyeonyeshwa kadi ya pili ya njano na kufuatiwa na nyekundu.
Ushindi huo umeifanya Milan kufikisha pointi 35 na kubaki nafasi ya 9 ya msimamo wa ligi hiyo inayoongozwa na Juventus inayotarajia kushuka dimbani muda mchache kuvaana na Torino.
Katika mechi nyingine za ligi hiyo jana ilishuhudiwa Roma ikipata ushindi ugenini dhidi ya Bologna kwa bao 1-0, Livorno ikilala nyumbani kwa mabao 3-2 dhidi ya Hellas Verona, Udinese na Atalanta zikitoshana nguvu kwa kufungana bao 1-1 sare iliyoipata pia Inter Milan dhidi ya Cagliari na Chievo Verona iliisasambua Catania kwa mabao 2-0.








































Liverpool, Newcastle Utd zashinda England

Jordan Henderson
Jordan Henderson akifunga moja ya mabao yake
Newcastle striker Loic Remy shoots past keeper Brad Guzan for his side's winner against Aston Villa
Luic Remy akifunga bao dakika za jioni likiizima Aston Villa
LIVERPOOL imeendelea kujiimarisha kwenye nafasi ya nne baada ya jioni hii kuikwanyua Swansea City kwa mabao 4-3, huku Newcastle United ikipata ushindi nyumbani dhidi ya Aston Villa kwa bao 1-0 katika Ligi Kuu ya England.
Mabao mawili ya Daniel Sturridge na mengine kama hayo ya Jordan Henderson yalitosha kuizima Swansea iliyokuwa ugenini kwa kuisaidia Liverpool kufikisha jumla ya pointi 56 na kuendelea kujikita kwenye nafasi ya nne ya msimamo wa ligi hiyo.
Sturridge aliiandikia bao Liverpool dakika ya tatu tu ya mchezo akimalizia kazi nzuri ya Raheem Sterling, kabla ya Henderson kuongeza la pili dakika ya 20 kwa pasi ya Sturridge kabla ya Jonjo Shelvey dakika tatu baadaye  na wageni kusawazisha bao dakika ya 26 kupitia kwa Winfried Bony na Sturridge kufunga bao la tatu dakika ya 36 kwa pasi ya Luis Suárez.
Kipindi cha pili kilianza kwa Bony kufunga bao la kusawazisha dakika mbili baada ya mapumziko kwa mkwaju wa penati na Henderson alifunga bao la ushindi dakika ya 74.
Katika mechi nyingine, Newcastle United ikiwa nyumbani iliitandika Aston Villa kwa bao 1-0 , goli hil;o likiwekwa kimiani na  Luic Remy dakika za nyongeza kabla ya pambano hilo kumalizika.
Kwa ushindi huo Newcastle United imechupa hadi nafasi ya nane ikifikisha pointi 40 huku Aston Villa ikisaliwa na pointi zake 28 ikishika nafasi ya 13.

Simba yafa Taifa, Azam yashindwa kurudi kileleni

 * Yabanwa na Prisons wakiruhusu bao jioni
Simba iliyokufa Taifa mbele ya maafande wa JKT Ruvu
Azam iliyoshindwa kurejea kileleni baada ya kulazimishwa sare ya 2-2
JKT walioitafuna Simba uwanja wa Taifa
Prisons walioendeleza maajabu yake katika duru la pili
WAKATI Azam ikishindwa kurejea kileleni baada ya kulazimishwa sare ya 2-2 na Prisons, 'Wekundu wa Msimbazi', Simba wameendelea kugawa pointi baada ya kuangukia pua mbele ya JKT Ruvu kwa kufungwa 3-2.
Simba inayonolewa na kocha Zdrakov Logarusic 'Loga' ilijikuta ikipoteza pointi 10 katika mechi ya nne baada ya maafande wa JKT Ruvu chini ya kocha Fred Felix Minziro kushtukiza kwa kipigo hicho leo jioni.
Mabao ya Husseni Bunu katika dakika ya 13 na Emmanuel Switta dakika ya 44 na 53 yalitosha kuinyong'onyesha Simba iliyokuwa inarejea nyumbani jijini Dar es Salaam baada ya kupata matokeo mabovu ugenini ikiambulia pointi mbili katika mechi zake tatu.
Hata hivyo vijana wa Simba walipambana na wapinzani wao waliokuwa pungufu na kufanikiwa kurejesha mabao mawili yalifungwa kwa mikwaju ya penati na Amissi Tambwe moja likiwa la penati dk 74 na 86.
Kwa kipigo hicho Simba imesalia kwenye nafasi ya nne ya msimamo ikiwa na pointi zake 32, tatu pungufu na Mbeya City ambayo nayo jana ililala mbele ya Coastal Union ya Tanga kwenye mfululizo wa ligi hiyo.
Katika mechi nyingine iliyochezwa uwanja wa Chamazi, Prisons Mbeya imeendelea kujikongoja baada ya kuibana Azam na kulazimisha sare ya mabao 2-2.
Bao la kusawazisha la Prisons lilifungwa zikiwa zimesalia dakika mbili kabla ya mchezo huo kuisha wakati Azam wakiamini wameibuka na ushindi na pengine kurejea kwenye msimamo wa ligi hiyo baada ya jana kushushwa na Yanga iliyoifumua Ruvu Shooting kwa mabao 7-0.
Wageni Prisons ambao wanafikisha mechi ya tano bila kupoteza mchezo wowote ikijikusanyia jumla ya pointi 11 ndiyo waliokuwa wa kwanza kupata bao lililofungwana na Omega Seme kabla ya Aggrey Morris kuisawazisha.
Kipre Tchetche aliiongozea Azam bao la pili ilikiwa bao lake la 10 kabla ya kuja kutolewa kwa kadi nyekundu kutokana na kupewa kadi ya njano ya pili.
Laurian Mpalila aliiokoa Prisons isiadhirike baada ya kufunga bao la pili na la kusawazisha zikiwa zimeshalia dakika  mbili kabla ya kumalizika kwa pambano hilo na kufanya timu hizo zigawane pointi moja moja.

Msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara 2013-2014    
                                  P    W     D    L    F     A   GD  PTS

01.Yanga                   17   11    05   01   41   12   29  38
02.Azam                    17   10    07   00   31   12   19  37
03.Mbeya City           19   09    08   02   24   16   08  35
04.Simba                    19   08    08   03   35   19   16  32
05.Kagera Sugar         19   06    08   05   16  15   01  26
06.Coastal Union        19   05    10    04  14  09   05  25
07.Mtibwa Sugar        19   06    07    06   23  23   00  25
08.Ruvu Shooting        19  06    07   06    20  26  -06  25
09.JKT Ruvu              19   07    01    11   16  29  -13  22
10.Prisons                   18   04    08    05   17  18  -01  20
11.Mgambo                19   05    05    09   12  27  -15  20
12.Oljoro                    20   02    09    09   15  30  -15  15
13.Ashanti                   18   03    05    10   15  30  -15  14
14.Rhino Rangers        19   02    07    10   12  23  -11  13

Wafungaji:
17- Tambwe Amisi (Simba)
10- Kipre Tchetche (Azam)
09- Elias Maguri (Ruvu Shooting) Hamis Kiiza, Didier Kavumbagu (Yanga)
08-Juma Luizio (Mtibwa Sugar), Mrisho Ngassa (Yanga)
07- Peter Michael (Prisons)
06- Themi Felix (Kagera Sugar), Mwegani Yeya (Mbeya City)
05- Tumba Sued (Ashanti Utd), Jerry Santo (Coastal Union)
04- Jerry Tegete (Yanga), Jonas Mkude, Betram Mombeki (Simba), Bakar Kondo, Salum Machaku (JKT Ruvu), Jerome Lambele (Ruvu Shooting), Abdallah Juma (Mtibwa Sugar)
03- Haruna Chanongo, Ramadhani Singano (Simba), Paul Nonga (Mbeya City), Salum Machaku (JKT Ruvu) Humphrey Mieno, Mcha Khamis (Azam), Amir Omary (Oljoro), Jeremia John (Mbeya City), Said Dilunga (Ruvu Shooting), Simon Msuva (Yanga), Emmanuel Switta(JKT Ruvu), Laurian Mpalila (Prisons)

MAUAJI YA KIKATILI DAR USTAADH AMCHINJA MTOTO


* Muuaji naye auawa, kumbe mgonjwa wa akili
* Alijaza damu kwenye ndoo
Add caption

mwili wa maremu mtoto Jamali aliechinjwa na ustadhi mbagala charambe mianzini
mwili wa marehem ustadhi mohamed kurangwa aliemchnja mtotoukishushjwa katika hospitali ya Temeke
baadhi ya wakazi wakichungulia nyumba lililotokea tukio la mauaji ya kikatili







USTAADH Mohamed Kurangwa (36), aliyemuua mwanafunzi wa Shule ya Msingi Nzasa Jamal Salum (12)  kisha naye kuuawa, ametajwa kuwa alikuwa ana matatizo ya akili.
Kurangwa alimuua Jamal mwanafunzi wa darasa la tano juzi jioni nyumbani kwake Mbagala Charambe Mianzini,  kwa kumchinja na kuweka kichwa cha marehemu huyu kwenye miguu ya mtoto huyo, kisha kuupeleka mwili wake choo cha nyumba anayoishi, muuaji.
Muuaji huyo alizoa  damu ya Jamal na  kuijaza kwenye ndoo kisha  kuiweka pembeni ya nyumba yake kabla ya kuingia chumbani kwake, kujifungia na kusoma Koran.
Ustaadhi Kurangwa  ambaye  aliuawa na wananchi,  wakati wa uhai wake alikuwa Imam wa msikiti wa Kareem ulioko Charambe.
MATATIZO YA AKILI
Mdogo wa muuaji  Daudi Kurangwa alisema  kati ya mwaka 1996-1997 marehemu kaka yake alishawahi kuugua ugonjwa wa akili na kutibiwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
Alieleza kuwa baada ya kuruhusiwa kutoka hospitali alikuwa akiendelea kutumia dawa kwa kipindi  lakini aliziacha baada ya kuhisi amepona.
“Kati ya Juni na Julai mwaka jana aliugua tena  na kutibiwa katika hospitali ya Temeke,” alisema na kuongeza kuwa hata hivyo juzi Kurangwa hakuwa na dalili zozote za ugonjwa huo kumrudia.
Kaimu Kamanda wa Mkoa wa Polisi Temeke, Jonathan Shana, akizungumzia tatizo la akili ,  alisema polisi inaendelea na uchunguzi na kueleza kuwa kuna taarifa kuwa muuaji kipindi cha nyuma aliwahi kuugua maradhi ya akili na kwamba kwa hivi karibuni alikuwa ni mzima na hajawahi kuonekana kama anaumwa.
Kamanda Shana alisema ukweli wa tukio hilo haujafahamika na kwamba Kanda Maalum ya Dar es Salaam imeunda kikosi kazi cha kuchunguza tukio hilo.
USHUHUDA WA RAFIKI
Akizungumza na NIPASHE Jumapili nyumbani kwa wazazi wa marehemu Jamal, rafiki wa mtoto huyo aliyenusurika kifo,  Ramadhani Hamisi (11) anayesoma darasa la tano katika  Shule ya Msingi Chemchem, alisema kabla ya kuchinjwa Ustaadhi Kurangwa alianza kumchoma visu mfululizo shingoni..
Ramadhani alisema anaishi na mjomba wake katika nyumba ya Ustadh huyo iliyoko Mianzini Njiapanda, sehemu ambapo imamu huyo alimchinja Jamal
“Siku  ya tukio nilimuomba marehemu Jamal, anisindikize kwenda nyumba  kuchukua kalamu, ilikuwa  saa 10:30 baada ya kupata kalamu hiyo ndani ya chumba tunachoishi na mjomba tulifunga mlango na kuanza kuondoka.
“Wakati  nafunga mlango marehemu Jamal alikuwa jirani yangu akiwa ameshika  madaftari na kalamu,” alisema Ramadhani kwa uchungu.
Aliendelea kueleza kuwa mara Ustadh Kurangwa alitokea akiwa na baiskeli, alipowaona aliiweka pembeni na kuja karibu nao akafungua pazia la mlango wa chumba chake, lakini wakati wanataka kuondoka, ghafla alimkamata Jamal na kuanza kumchoma  kisu sehemu mbalimbali shingoni.
"Nilimshuhudia akimchoma kisu  mara nyingi, Jamal alilia  akisema nisamehe Ustadh, nisamehe Ustadh," aliongeza mtoto huyo huku akitokwa na machozi.
Ramadhani alikimbia hadi nyumbani kwa Jamal  na kumueleza mama yake kuhusu tukio hilo na yaliyoendelea nyuma hakuweza kuyashuhudia tena.
JAMAL ACHINJWA
Mjumbe wa nyumba kumi wa Mtaa wa Mianzin,  Ester Msumba, aliyesema alikuwa wa kwanza kushuhudia tukio hilo, alieleza kuwa  alifika eneo la mauaji baada ya kumsikia  mwanamke mmoja akipiga mayowe kuomba msaada baada ya kuona kiwiliwili cha mtoto kimelala na kichwa chake kimewekwa miguuni.
Alisema mwanamke huyo alikwenda kwenye madrasa ya Ali Munawar  kumpeleka mtoto wake kwa ajili ya kumuanzishia masomo ya ziada, kwa vile licha ya kufundisha dini eneo hilo alilokuwa anaishi Kurangwa linatoa mafunzo hayo ya ziada.
"Baada ya kusikia sauti ya yule mama  nilikimbilia eneo la tukio, hapo nilikuta hali ni mbaya kwani niliona  mwili wa mtoto umelazwa chooni na kichwa chake kiliwekwa miguuni kwake," alisema msumba.
Alisema wakati wa mauaji hayo sauti ya mtoto Jamal  haikusikika hivyo ilikuwa vigumu kupata msaada.
Msumba alisema pamoja na mwili huo, alishuhudia ndoo iliyokuwa na damu iliyochanganywa na maji  kitu kilichoashiria muuaji alikinga damu hiyo kuzuia isitapakae na kusambaa chini.
Sakafu ya choo hicho ilikuwa imejaa damu na familia ilizuiliwa kukitumia kwa muda kupisha uchunguzi.
Baada ya kufanya tukio hilo, Ustadh Kurangwa, alikwenda chumbani kwake na kujifungia huku akisoma Kuran.
"Baada ya kumtafuta kwa muda mtu aliyefanya unyama huo, tuligundua   amejifungia ndani tulipomchungulia tulimuona akisoma Kuran huku kanzu yake ikiwa imetapakaa damu," alisema mjumbe huyo.
USTADHI KURANGWA AUAWA
Wananchi walimvamia  chumbani baada ya kubomoa dirisha na  kumshambulia kwa matofali na mawe hadi alipopoteza fahamu na kumvua nguo kisha kumtoa nje na  kumpiga  hadi alipokata roho.
WAZAZI WA JAMAL
Habiba Selemani (27) mama mzazi wa marehemu Jamal akizungumza na gazeti hili alisema anamuachia Mungu  kifo cha mwanawe.
"Namuachia Mungu kwanini  tukio hili afanyiwe Jamal," alisema mama mzazi, hata  hivyo, alikumbukia kuwa  kabla ya kifo chake  alikuwa anacheza na mdogo wake mwenye miezi sita na kumvisha nguo  alipomaliza aliniaga kwamba anakwenda kucheza.
"Aliniambia anakwenda kucheza lakini kwa mshangao alinieleza kuwa anaona nyota nyingi, sikujali nilimuacha aende zake," aliongeza kusema.
Kwa upande wake   Salimu Ally, ambaye ni baba mzazi, alisema amepokea msiba huo  mshituko mkubwa na hakuamini kilichotokea kwani ni  tukio  la kinyama.
Alieleza kuwa juzi  jioni wakati anakaribia  nyumbani aliwaona wanawake  wanaingia kwenye  nyumba hiyo yalikofanyika mauaji ya  mwanae na kushangaa kwani walikuwa  wanatoka na kulia.
Ally alisema hakujua kilichotokea na kwamba mawazo yake yalikuwa kufika nyumbani kwanza.
“Nilipofika nilimkuta mke wangu analia hajitambui ndipo mpangaji mwenzangu aliponieleza kuwa  mwanangu Jamal  kachinjwa niliumia sana , sikuweza kuamini,” alisema kwa huzuni.
Alikanusha kuwa marehemu mtoto wake alikuwa anasoma kwenye chuo cha Ustaadh huyo na pia hawafahamiani  japo Kurangwa  alimwita na kuingia naye ndani kisha kumchinja.
Mwili wake ungezikwa jana saa 10 jioni  baada ya kupatiwa kibali cha polisi kuchukua maiti kutoka hospitali ya Temeke.
Chanzo:NIPASHE JUMAPILI

Nyamwela afyatua mpya na Tundaman


MNENGUAJI kiongozi wa bendi ya Extra Bongo, Mussa Hassan 'Super Nyamwela' amefyatua wimbo mpya uitwao 'Nyengele' akimshirikisha nyota wa muziki wa kizazi kipya nchini, Tundaman ikiwa ni maandalizi yake ya kupakua albamu yake mpya na ya tatu.
Akizungumza na MICHARAZO, Super Nyamwela alisema wimbo huo ambao ni wa nne katika maandalizi ya albamu hiyo baada ya 'Duvele Duvele', na Maneno Maneno ameurekodia katika studio za C9 Records na anatarajia kuachia wiki ijayo.
Nyamwela alisema katika wimbo huo kama ulivyo 'Duvele Duvele' na 'Tumechete'  umepigwa kiasili kwa ajili ya kuleta vionjo tofauti na kutamba kuwa utakuwa funika bovu kwa namna Tundaman alivyompiga tafu.
"Nipo katika maandalizi ya mwisho ya kuachia audio na video ya wimbo wangu mpya uitwao 'Nyengele' ambao nimeuimba na Tundaman ikiwa ni maandalizi kutoa albamu yangu ya tatu baada ya 'Master of the Tample' na 'Afrika Kilomondo', " alisema Nyamwela.
Nyamwela alisema amepanga ndani ya mwaka huu albamu hiyo ya tatu itakuwa imekamilika na pia itafanyiwa uzinduzi , japo hajajua itafanyika mwezi gani na ukumbi gani.
"Nataka nikamilishe nyimbo zote audio na video kabla ya kuizindua rasmi," alisema Nyawela.