STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, December 9, 2014

Msafara wa viongozi CHADEMA watekwa nyara

http://www.gumzolajiji.com/wp-content/uploads/2014/09/SAM_7117.jpg
Mwenyekiti wa Chadema wilaya ya Kahama, Juma Protas
MSAFARA wa viongozi na wanachama wa chama Demokrasia na Maendeleo Chadema wa Kanda ya ziwa Magharibi wametekwa na watu wanaodhaniwa kuwa ni majambazi wakati wakitoka kwenye mkutano wa uzinduzi wa kampeni za serikali za Mitaa kata ya Bulyanhulu wilayani Kahama mkoani Shinyanga.

Akizungumza na waandishi wa habari,  Mwenyekiti wa Chadema wilaya ya Kahama, Juma Protas alisema tukio hilo lilitokea  juzi katikati ya Kijiji cha  Kalagwe kata ya Ntobo na Kijiji cha Nyambula  Kata ya Ngongwa majira ya Saa 3:30 Usiku wakati wakitoka kwenye Kampeni  Kijiji cha Kakola.
Akizungumzia tukio hilo Protas alisema walipofika eneo la Daraja walikuta magari matatu  yamesimama pembeni ambayo ni Basi la Jordan ambalo lilikuwa linatoka mkoani Geita kuelekea Kahama,Roli aina ya Fuso na Gari ndogo inayomilikiwa na Kampuni ya TBL kupitia bia ya Balimi ambayo nayo yalikuwa yametekwa.
Alisema wakati wanajaribu kuyapita magari hayo ghafla waliona Mawe na Miti ambayo ilikuwa imetandazwa barabarani  na ndipo majambazi hao waliamuru Msafara huo ambao ulikuwa na magari mawili wenye watu 10 wasimame na watoe simu na fedha walizokuwa nazo.
“Tulisikia sauti  wakisema zimeni  taa za gari na muziki na hatuwezi kuwadhuru nyinyi Makamanda ila tunataka fedha na simu, na tupo kazini mnatakiwa kuwalaumu viongozi waliokula Pesa za Escrow  bila hiyo tusingefanya haya mnayoyaona”alifafanua Protas.
Aliwataja waliokuwemo kwenye msafara huo kuwa ni mratibu wa Kanda ya ziwa mashariki Renatus  Mzemo, Mwenyekiti wa Kamati ya Rasilimali Kanda ya ziwa Magharibi, Emmanuel Mbise na Mwenyekiti wa Kamati ya Uenezi wa chama hicho Kanda hiyo Juma Protas ambaye ndiye Mwenyeki wa Chadema.
Viongozi hao  wa Chadema walikuwa wamepanda gari aina ya Toyota  Prado yenye no. T 707  BBP ambayo hata hivyo ilivunjwa baadhi ya vioo.
“Tuliibiwa fedha  tathimini zaidi ya shilingi laki tisa pamoja na simu 11 ambazo hazikufahamika mara moja thamani yake na gari yetu moja ambayo ni ya mdau alyejitolea kutusaidia ilivunjwa vioo na ile ya M4C yenyewe walisema hawawezi kuivunja maana ni wananchi walichanga kuinunua”,aliongeza Protas
“Kulikuwa na magari mengi tuliyoyakuta yametekwa na abiria walinyang’anywa simu na fedha zao, pia kulikuwa na Mwalimu mmoja wa Shule ya Msingi Lunguya ambaye alitekwa akiwa na pikipiki na wakamfunga  Kwenye mti pamoja na ddugu yake  na baada ya kuchukua fedha walitoweka kusikujulikana”,AliongozeaMwenyekiti huyo.
Hata hivyo Jeshi la Polisi wilayani Kahama lilifika eneo hilo   baada ya kupewa taarifa na abiria waliokuwa kwenye basi ambalo lilitekwa  na kukuta majambazi hayo yakiwa yametokomea kusikojulikana  na kutoa msaada wa kiusalama kwa magari  yote na abiria waliotekwa.
MALUNDE

Simba yamalizana na beki wa Gor Mahia

OWINO (KUSHOTO) AKIWA KAZINI NA GOR MAHIA.
KLABU ya Simba imemalizana na beki David Owino wa Gor Mahia.
Uongozi wa Simba kupitia kamati yake ya usajili, imefanya mazungumzo na beki huyo na kumalizana naye, kilichobaki ni suala la kuanguka saini tu.
Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili, Zacharia Hans Poppe amesema wanachosubiri ni kumuona na kumalizana naye katika usajili.
"Kweli mazungumzo yamekwenda vizuri na Gor Mahia pia wamekubali, suala ni kukutana naye na kujua nini cha kufanya," alisema Hans Poppe.

SALEHJEMBE

Platini asema ni muda muafaka Blatter kuondoka FIFA

http://i.telegraph.co.uk/multimedia/archive/02785/PlatBlat_2785870b.jpg
Mzee muda wa kuondoka FIFA, umewadia au we unaonaje? Platini (kushoto) akiteta jambo la Sepp Blatter wa FIFA
RAIS wa Shirikisho la Soka la Ulaya, UEFA, Michel Platini amekataa kumuunga mkono Sepp Blatter au mpinzani wake Jerome Champagne katika uchaguzi wa Shirikisho la Soka Duniani,FIFA utakaofanyika mwakani.
Platini amedai kuwa anatumaini ataibuka mgombea mwingine wa tatu katika kinyang’anyiro hicho, ambaye huenda akamuunga mkono. 
Akihojiwa na rekodi moja nchini Ufaransa, Platini amesema anadhani muda umefika kwa Blatter ambaye anagombea kwa kipindi cha tano toka ateuliwe kwa mara ya kwanza mwaka 1998, kuondoka. 
Platini amesema alimuunga mkono Blatter mwaka 1998 kwa sababu alifikiri ni mtu sahihi kwa muda ule lakini baada ya vipindi vitano alivyoongoza anadhani ni muda muafaka wa kuleta mtu mwingine katika nafasi hiyo. 
Rais huyo wa UEFA aliendelea kudai kuwa taswira ya FIFA hivi sasa imeharibika vibaya kutokana na kshafa mbalimbali ndio maana anaona itakuwa vizuri kwa Blatter kuondoka lakini hadhani kama yeye mwenyewe anahitaji kuondoka. 
Akiulizwa nani atamuunga mkono katika uchaguzi huo, Platini amesema hana chaguo kwa wagombea wote wawili waliochaguliwa na akitegemea kujitokeza kwa mgombea mwingine katia uchaguzi huo.

Hatimaye Pele atoka Hospitalini

http://www.bnci.com.br/blog/images/2014/03/pele-esteira-4.jpg
Pele
GWIJI wa zamani wa soka duniani, Mbrazil Pele ameruhusiwa kutoka hospitali leo baada ya kupona maambukizi ya mkojo aliyopata kutokana na kufanyiwa upasuaji wa kuondoa mawe katika figo wiki tatu zilizopita. 
Katika taarifa yao madaktari wa hospitali ya Albert Einstein iliyopo jijini Sao Paulo wamedai kuwa nguli huyo kwasasa yuko hali njema hivyo hakuna umuhimu wa kuendelea kumuweka hapo. 
Pele alifanyiwa upasuaji wa kuondoa mawe katika figo yake Novemba 13 mwaka huu lakini alilazwa tena hospitalini hapo siku 10 baadae baada ya kupata maambukizi katika njia ya mkojo. 
Nguli huyo mwenye umri wa miaka 74 aliwahakikishia mashabiki wake kwamba bado yuko fiti katika picha ya video iliyotolewa Ijumaa iliyopita ikimuonyesha kitabasamu huku akipiga gitaa akiwa amezungukwa na familia yake.

Breaking News! Vurugu kubwa Dumila, kadhaa wajeruhiwa


Na Dunstan Shekidele, MOROGORO
WATU kadhaa wamejeruhiwa katika vurugu zilizotokea jioni hii huko Dumila mkoani Morogoro kati ya wakulima na wafugaji ambapo polisi wameingilia kati na kutumia mabomu ya machozi kutuliza ghasia hizo.
Chanzo cha vurugu hizo kinadaiwa kuwa ni kukatwa mkono kwa mkulima mmoja aishiye Kijiji cha Mketeni wilayani Kiloasa wakati akibishana na mfugaji ambaye ni kabila la Kimasai kuhusu eneo la kulishia mifugo.
Kufuatia kitendo hicho cha kukatwa mkono, mkulima huyo aliwafuata wenzake na kuwapa taarifa ambapo walikusanyika na kuanzisha vurugu dhidi ya wafugaji wa eneo hilo.
Baada ya kuona kuwa bado haitoshi na baadhi ya wafugaji kukimbia, wakulima walimalizia hasira zao katika Barabara ya Morogoro - Dodoma ambapo waliamua kuifunga kwa takribani masaa mawili huku wakichoma matairi.
Polisi wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) waliingilia kati na kutumia mabomu ya machozi kuwatawanya wakulima ambao pia walikuwa tayari wamevamia baadhi ya nyumba za kulala wageni zinazomilikiwa na wafugaji eneo hilo na kufanya uharibifu.
Majeruhi katika vurugu hizo wamepelekwa hospitali kwa huduma ya kwanza.
GPL

Stars Maboresho yanyolewa 2-1 Taifa


Furaha ya kupata bao la kuongoza
hekaheka katika lango la Burundi
Kosakosa langoni mwa vijana wa Intamba Murugamba
Burundi wakiwakimbiza Stars Maboresho
Stars wakiokoa hatari langoni mwao
KIKOSI cha timu ya Taifa Stars Maboresho kimeendeleza unyonge wa Tanzania mbele ya Burundi baada ya kukubali kipigo cha mabao 2-1 katika pambano la kirafiki na kimataifa lililochezwa kwenye uwanja wa Taifa kama sehemu ya kusherehekea siku ya Uhuru wa Tanganyika.Stars Maboresho walianza kuandika bao dakika ya 11 kupitia Yusuf Rashid kabla ya Burundi kucharuka na kurejesha bao hilo dakika ya 25 kupitia Fabrice Mimimahanzwe na kwenda mapumziko wakiwa 1-1 na kipindi cha pili kuruhusu wageni kupata bao la ushindi lililovuruga 'pilau' la Uhuru.
Bao hilo liliwekwa kimiani na Nassor Niyonkulu aliyemalizia krosi pasi ya kutoka kushoto mwa uwanja na kupiga mpira uliosindikizwa wavuni na kipa Aishi Manula.

Arsenal v Hull City, City wapewa kibonde FA Cup

The FA Cup third-round draw was made on Monday evening and produced some brilliant tiesRATIBA ya Rasundi ya Tatu ya michuano ya Kombe la FA nchini Uingereza imetoka kwa Arsenal kupangiwa Hully City wakati Manchester City wakipewa kibonde Sheffield Wednesday.
Mechi ra raundi zitaanza kuchezwa kati ya Januari 3 na 5 mwakani na ratiba kamili ni kama ifuatavyo;

Maromboso atoa kilio chake kwa serikali



Maromboso katika pozi tofauti
MUIMBAJI anayekuja juu nchini anayefanya kazi katika kundi la Yamoto Band, Mbwana Yusuf Kilangi 'Maromboso', ameiomba serikali na mamlaka nyingine zinazosimamia fani ya sanaa kuwashughulikia wezi wa kazi zao.
Maromboso alisema miongoni mwa wezi wanaopaswa kushughulikiwa ni wale wanaoedesha shughuli za kuchoma (burn) CD na kuingiza nyimbo za wasanii kwenye simu na vifaa vingine kwani wanawakosesha wasanii mapato.
"Tunaibiwa na wezi wamekuwa wakiachwa mitaani wakifanya shughuli hizo bila vyombo husika kuwachukulia hatua, hawa ni wezi na wanapaswa kushughulikiwa wanatunyima mapato," alisema.
Alisema wakati msanii au kundi likitumia gharama kubwa kurekodi kazi zao, wanaochoma CD na kuingiza nyimbo katika simu mitaani wanaifanya bila kulipa kodi wala gharama nyingine na kudai hiyo siyo haki.
"Watu hawa ndiyo wanaowafanya mashabiki wasisumbuke kwa sasa kununua kazi zetu kwa vile wanajua wataenda kutumia fedha kidogo tu kupoata kazi nyingi kwa mkupuo, Inauma sana," alisema.
Maromboso ni mmoja wa waimbaji wanne wanaounda kundi la Yamoto Band linalotamba na nyiumbo kama Yamoto, Nitajuta, Niseme, Inno na nyingine zinazotamba nchini wakiwa chini ya Mkubwa na Wanae.

Shamsa Ford: 2014 ulikuwa mwaka wangu


WAKATI akitarajiwa kuuza sura kwenye filamu nyingine mpya iitwayo 'Chale Mvuvi', muigizaji Shamsa Ford amefichua kuwa alikuwa na mwaka mzuri wa 2014 kiasi cha kumshukuru Mungu.
Akizungumza na MICHARAZO, Shamsa alisema hakuna mwaka aliofurahia fani yake ya uigizaji kama mwaka huu wa 2014 kutokana na kupata mafanikio makubwa kiasi cha kujivunia.
"Siyo Siri namshukuru Mungu kwa kunisaidia kuwa na mwaka mzuri na tarajio langu ataniwezesha mwaka ujao uwe kama huu," alisema.
Shamsa alidokeza kuwa anatarajiwa kuonekana kwenye filamu mpya iitwayo 'Chale Mvuvi' aliyoigiza na wasanii kadhaa wa Tanzania Bara na Zanzibar.
Alisema mbali na yeye na Baba Haji, filamu hiyo imewashirikisha pia, Haji Kanuti na Mzee Kombora na ni filamu ya kijamii yenye mafunzo makubwa na ambayo imewaunganisha wasanii wa pande mbili za Muungano.
"Hii siyo filamu yangu, lakini nimeishiriki na Baba Haji na tumeigizia visiwani Zanzibar, siyo ya kuikosa kwani ina mafunzo makubwa kwa jamii," alisema Shamsa.

Rais Jamali Malinzi kushuhudia Fainali za Kawambwa Cup 2014

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEht2Pd9_UarV_MSC5Gq5pjX7o1qlmlEOi3kk_x1n9azU99f4kHAWUOBZzuXTP7rgj_QQ4Vd-Wff4lelvZYDurV9EIZrCnOh5FR0rd_32RnW9munYjmjjNskCuCp26Ndc_6Zuod7ksUjaHrL/s1600/016.JPGRAIS wa Shirikisho la Soka la Tanzania (TFF), Jamal Malinzi anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika mchezo wa Fainali za Mashindano ya Kombe la Kawambwa 2014 itakayochezwa Desemba 20 mjini Bagamoyo.
Kwa mujibu wa Msemaji wa michuano hiyo, Masau Bwire michezo ya nusu fainali za michuano hiyo inatarajiwa kuchezwa kuanzia Ijumaa kwa kuzikutanisha timu za Zing Zong na Mwambao.
Pambano la pili la nusu fainali za michuano hiyo itazikutanisha timu za Mapinga heroes dhidi ya New Stars na mechi zote zitakchezwa kwenye uwanja wa Mwanakalenge mjini Bagamoyo.
Bwire alisema washindi wa mechi hizo za nusua fainali watakutana kwenye fainali itakayochezwa Desemba 20 na mgeni rasmi atakuwa Rais wa TFF, Jamal Malinzi.
Alisema kuwa mbali na Malinzi pia fainali hizo zinatarajiwa kuhudhuria na viongozi wengine mbalimbali walioalikwa  na kutakuwa na michezo mimngine ya kusisimua katika kupamba fainali hizo.
Miongoni mwa michezo itakayochezwa siku hiyo ni pamoja na ile ya kuvuta kamba kwa wazee, kukimbiza kuku na kina mama kukimbia kwenye magunia mbali na burudani ya ngoma na Bongofleva.
Mshindi wa michuano hiyo inayodhaminiwa na Mbunge wa Bagamoyo, Dk Shukuru Kawambwa atanyakua Kombe kubwa na zawadi wa Pikipiki huku timu nyingine zikipata vikombe na zawadi nyingine ambazo zimeandaliwa kwa ajili ya michuano hiyo.

Taifa Stars, Intamba Murugamba leo Taifa

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhifuz9t7Y3fbFlEsJWzFqquZ1aaF6_DUgm80KzOToI2ybRZAe6rXvGp40l3lPx2b6wFjAX8t80WU09bbJP6u_98sEzq8jTp0ELUwy7n6DJO5jf-PqyqOqBZcfDI5qQsfTv9QtOYBznCZc/s1600/Staz.jpg
Kikosi hiki cha Taifa Stars Maboresho kilinyukwa mabao 3-0 na Burundi katika sherehe kama hizi za Uhuru mwaka jana
KIKOSI  cha Taifa Stars Maboresho kimerejea Dar es Salaam kutoka Bulyanhulu mkoani Shinyanga ambapo kiliweka kambi kwa ajili ya mechi ya kimataifa dhidi ya Burundi itakayochezwa leo. Timu hiyo ambayo jana asubuhi ilifanya mazoezi kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, ilitua Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) juzi kwa ndege ya Fastjet saa 12.30 jioni na kwenda moja kwa moja kambini hoteli ya Tansoma. Nayo timu ya Taifa ya Burundi ilitua nchini jana saa 10 jioni kwa ndege ya RwandAir. Kikosi hicho kitafikia hoteli ya Tiffany Diamond kitakwenda moja kwa moja Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ambapo kitafanya mazoezi kuanzia saa 11 jioni. Kiingilio cha mechi kati ya Tanzania na Burundi itakayochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 10 jioni kitakuwa sh. 3,000 kwa viti vya raungi ya chungwa, bluu na kijani wakati VIP B na C ni sh. 5,000 tu.
Katika mechi mbili zilizopita baina ya timu hiyo kwenye michezo ya kirafiki ya kimataifa Stars imeshindwa kufurukuta baada ya awali kupigwa 3-0 uwanja wa Taifa kwenye sherehe kama hizi za Uhuru kupitia Maboresho na kisha 2-0 Stars yenyewe mjini BUnjumbura, Burundi.
Je, Stars Maboresho imeimarika kuweza kulipa kisasi kwa Intamba Murugamba? Tusubiri!

Arsene Wenger apata mtetezi Arsenal

http://i3.mirror.co.uk/incoming/article4568785.ece/alternates/s615/Arsenal-v-Anderlecht.jpg
NYOTA wa zamani wa Uingereza, Gary Lineker amewaponda mashabiki wa Arsenal ambao wanamzomea meneja wa timu hiyo Arsene Wenger.
Kuna picha za video zilizotoka zikionyesha Wenger mwenye umri wa miaka 65 akizomewa na mashabiki wakati akipanga treni kufuatia Arsenal kuchapwa mabao 3-2 na Stoke City Jumamosi iliyopita.
Mshambuliaji huyo aliyewahi kuwa Mfrungaji Bora wa Kombe la Dunia, ambaye kwasasa ni mtangazaji wa michezo wa BBC aliandika katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii akiwaponda mashabiki hao kwa kukosa heshima pamoja na matokeo hayo baada ya kuona picha hizo za video.
Katika mchezo huo uliofanyika katika Uwanja wa Britania Arsenal walikuta wakiwa nyuma kwa mabao 3-0 mpaka kufikia muda wa mapumziko.
Kocha huyo pia alijikuta katika wakati mgumu mbele ya mashabiki wa Arsenal kufuatia ushindi wa bao 1-0 dhidi ya West Bromwich Albion.

Robin van Persie aipeleka Man Utd katika 3 Bora

Kitu! Van Persie akifunga bao la pili kwa kichwa akiunganisha mpira wa adhabu ndogo
Vijana wa Van Gaal wakishangilia bao lao
Kuna maswali tena jamaniiiii!
Van Persie akifunga bao la kwanza
MSHAMBULIAJI wa Kiholanzi, Robin van Persie usiku wa jana aliiwezesha klabu yake ya Manchester United kukwea hadi nafasi ya tatu baada ya kuisambatarisha Southampton nyumbani kwao kwa kuwafunga mabao 2-1 katika Ligi Kuu ya England.
Van Persie aliandika mabao hayo katika dakika ya 12 na 71 na kuifanya Mashetani Wekundu hao kufikisha pointi 28 na kuziengua timu za Southampton na West Ham United na kuzipa presha Manchester City na Chelsea waliopo kileleni kwa sasa.
Bao la wenyeji liliwekwa kimiani na Pelle dakika ya 31 ambalo lilikuwa la kusawazisha kabla ya 'Vijana Watakatifu' kutepeta kipindi cha pili kwa bao la pili la van Persie.


Ruvu Shooting yanyakua kifaa cha zamani cha Yanga

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjTlRl4RGaDMzreVo6i9A2CHl46GExRf6WDar2iMDwxH4ch6sxGbqGn7eGHfRDcHLwbMohboNtiKmVO1OjO8LStYLQ271hgDqpYI54PYsS5nWzeoYoVQVdM-65jf7wfY5wZv7e0l7UMoz0o/s1600/DSC_8206.JPG
Yahya Tumbo (kushoto) akichuana na beki wa Bnadari katika Ligi Kuu ya Zanzibar hivi karibuni. Mchezaji huyo ametua Ruvu Shooting akitokea Mtende Rangers
KLABU ya Ruvu Shooting  imefanikiwa kumsainisha mkataba wa miezi 18, Kiungo Mshambuliaji wa zamani wa Yanga na Azam, Yahya Tumbo aliyekuwa akiichezea Mtende Rangers inayoshiriki Ligi Kuu Zanzibar.
Tumbo, anayeongoza orodha ya wafungaji bora katika ligi ya visiwa hivyo maarufu kama Grand Malta akiwa na mabao 7 alisaini mkataba huo na Ruvu Shooting jana Jumatatu ili kuitumikia katika Ligi Kuu Bara.
Ruvu imemsajili mchezaji huyo aliyekuwa na mkataba na klabu yake inayoongoza msimamo wa ligi ya visiwani baada ya kumalizana na klabu yake pamoja na Chama cha Soka za Zanzibar, ZFA.
Msemaji wa Ruvu, Masau Bwire alisema kuwa, wamemnyakua mchezaji huyo ili kuimarisha kikosi chake baada ya awali kumdaka Betram Mombeki aliyewahi kuichezea Simba.
'Usajili wa Tumbo, mchezaji hatari katika kufumania nyavu ni ishara kwamba timu yetu imedhamiria kufanya vizuri ligi itakapoendelea katika msimu huu," alisema Bwire.
Bwire alisema anaimani na washambuliaji hao kuwa wataibeba Ruvu katika ligi hiyo iliyosimama tangu Novemba 9 na itakayoendelea tena Desemba 26.
Tumbo ametua Ruvu akitokea Mtende Rangers iliyopo kileleni kwa sasa wakati ligi ikiwa imesimama visiwani humo  ikiwa na pointi 19 ikifuatiwa na Zimamoto yenye pointi 18, huku mshambuliaji huyo akiwa kinara wa mabao 7 akifuariwa na Amour Janja wa JKU mwenye mabao matano.
Bwire aliongeza kuwa mbali na kuwasajili wachezaji wawili, yaani Mombeki na Tumbo, pia kuna wachezaji wanne wanaoendelea kufanyiwa majaribio katika timu yao na endapo viwango vyao vitamridhisha kocha Tom Oloba watasajili kuingozea nguvu Ruvu.
Ruvu Shooting imeenda mapumziko ikiwa katika nafasi ya 11 baada ya kukusanya jumla ya pointi saba baada ya kucheza mechi saba.

Zola D avunja ukimya na I Don't Care



BAADA ya kimya cha muda mrefu, Mwanahip-hop, Zola D anajiandaa kuachia 'audio' na video ya kazi yake mpya iitwayo 'I Don't Care'.
Akizungumza na MICHARAZO hivi punde, Zola D ambaye pia ni Bondia wa ngumi za kulipwa uzito wa Juu, alisema wimbo huo ambao ni wa kigumu asilia, ameimba kwa kushirikiana na Ramso Latino.
Zola D alisema kuwa kazi hiyo ameitengeneza kwa Man DVD na video chini ya kampuni yake ya 'Under Films na itaachiwa muda wowote kuanza sasa.
Ila MICHARAZO inakupa nafasi ya kuusikiliza wimbo huo kwa mara ya kwanza hapo chini;

Zola D ft Latino - I Don Care.mp3

Sunday, December 7, 2014

Messi amjibu Ronaldo, Barca ikiua 5-1 Hispania

Messi akishangilia moja ya mabao yake leo
Suarez na Pique wakishangilia bao la pili la Barcelona
Kabakisha hat trick mbili tu kumkuta Ronaldo
Akipongezwa na Neymar
Bravo Brother!
Utukuzwe uliyenijalia kipaji hiki cha soka
 STRIKA Lionel Messi amejibu hat trick ya Cristiano Ronaldo baada ya kufunga magoli matatu wakati akiisaidia Barcelona wakiiangamiza wapinzani wa Jimbo la Cataluna, Espaniol kwa mabao 5-1 katika mechi ya La Liga usiku huu.
Messi amefunga mabao hayo na kufanya afikishe jumla ya mabao 256 na kuzidi kumuacha mbali Ronaldo aliyefikisha mabao 200 jana usiku.
Wageni Espanol walikuwa wa kwanza kupata bao lililofungwa dakika ya 13 na Sergio García kabla ya Messi kusawazisha kabla ya mapumziko.
Mkali huyo alifunga bao la pili dakika ya 50 akimalizia kazi ya Suarez kabla ya Gerrard Pique kuongeza bao la tatu dakika ya 53 kwa kichwa na Pedro kuongeza la nne dakika ya 77.
Messi alifikisha hat trick ya 21 na hat trick ya tatu katika mechi nne tofauti zilizopita katika dakika ya 81 kwa kazi nzuri ya Pedro na kuifanya Barcelona kufikisha jumla ya pointi 34 na kukwea hadi nafasi ya pili wakiiengua watetezi Atletico Madrid wenye 32.
katika mchezo mwingine mapema, SEvilla ikiwa ugenini ilinyukwa bao 1-0 na Rayo Vallecano.

Rais JK ateua RC mpya, sita awapangua

http://dar24.com/wp-content/uploads/2013/05/rais-jk-kikwete1.jpg
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Mkuu Mpya mmoja wa Mkoa na kuwahamisha vituo vya kazi wengine sita kuanzia jana, Jumamosi, Desemba 6, 2014.
Taarifa iliyotolewa leo, Jumapili, Desemba 7, 2014 na Katibu Mkuu Kiongozi (KMK), Balozi Ombeni Sefue mjini Dar es Salaam inasema kuwa Rais amemteua Mkuu wa Wilaya ya Karatu, Mkoa wa Arusha, Ndugu Daudi Felix Ntibenda  kuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha.
Ndugu Ntibenda ataapishwa kesho, Jumatatu, Desemba 8, 2014, saa nne asubuhi, Ikulu, Dar Es Salaam.
Taarifa hiyo inasema kuwa wakuu waliohamishwa vituo vya kazi ni Mheshimiwa Elaston Mbwilo anayehamishwa kutoka Mkoa wa Manyara kwenda Mkoa wa Simiyu ambako anachukua nafasi ya Mheshimiwa Paschal Mabiti aliyepewa likizo ya ugonjwa, Mheshimiwa Joel Nkanga Bendera aliyehamishwa Mkoa wa Manyara kutoka Mkoa wa Morogoro na Mheshimiwa Dkt. Rajabu M Rutengwe anayehamishwa Mkoa wa Morogoro kutoka Mkoa wa Tanga.
Wengine ni Mheshimiwa Magalula Saidi Magalula anayehamishiwa Mkoa wa Tanga kutoka Mkoa wa Lindi, Mheshimiwa Mwantumu Bakari Mahiza anayehamishiwa Mkoa wa Lindi kutoka Mkoa wa Pwani na Mheshimiwa Mhandisi Evarist B. Ndiliko anayehamishiwa Mkoa wa Pwani kutoka Mkoa wa Arusha.
Wakuu wengine wa mikoa wanaendelea kubakia katika vituo vyao vya sasa vya kazi.

AC Milan yapigwa kidude ugenini

http://a.espncdn.com/combiner/i/?img=/photo/2014/1130/fc_milan_jc_1296x729.jpg&w=738&site=espnfcMABINGWA wa zamani wa Italia na Ulaya, AC Milan jioni ya leo imedonyolewa ugenini bao 1-0 na Genoa katika mfululizo wa Ligi ya Italia Serie A.
Bao pekee lililowazamisha vijana wa Phillip Inzaghi 'Pippo' lilitumbukizwa wavuni katika dakika ya 32 na beki wa Genoa Luca Antonelli.
Kipigo hicho kimeifanya Milan kusalia nafasi ya saba ikiwa na pointi 21 wakati wenyeji wao wakipanda hadi nafasi ya tatu wakiwa na pointi 26.
Katika mechi  nyingine zilizochezwa leo Napoli ikiwa nyumbani iling'ng'aniwa na Empoli na kutoka sare ya mabao 2-2, Atalanta ikaifumua Cesena kwa mabao 3-2  na Parma ikakubali kichapo cha mabao 2-1 toka kwa Lazio.      

WEMA SEPETU KATIKA TUHUMA NZITO

TUKIO:Wapigwa na kuvuliwa nguo nyumbani kwa Wema
MSANII Mwema Sepetu 'Madame' ametupiwa tuhuma nzima kutokana na tukio lililotokea nyumbani kwake kwa watu wawili wanaodaiwa kuwa mafundi, kupigwa na kudhalilishwa kwa kuachwa uchi wakidaiwa kuhusika na wizi.
Wema akiwa ndani
Kwa mujibu wa Bongo5.com ambao walizungumza jana na jirani wa Wema aliyetambulika kwa jina la Mama Steve, alisema tukio hilo lilitokea Ijumaa majira ya saa 5 asubuhi mpaka saa 9 jioni.
“Waliopigwa na kulazwa chini uchi wa mnyama ni mafundi ambao wanakujaga kila siku kumtengenezea Wema nyumba yake,” amesema mama huyo. “Sasa baada ya kumaliza kazi yao wakaondoka, baada ya kuondoka wakaitwa tena na kuambiwa kuna simu imeibiwa ndani, ndo mtiti ukaanza.”
“Petit akatumwa akachukue mabaunsa 7 na baada ya kufika wakapandisha muziki mpaka mwisho ili sisi tusisikie nini kinaendelea huko ndani. Sasa kuna mtu alikuwa anapita hapa kwenye geti lao akasikia mtu analia sana ikambidi akachungulie ndo akamkuta fundi watu wawili wamelazwa chini uchi wa mnyama wanapigwa na hawana nguvu kabisa! Ndo yule jamaa kwakuwa alikuwa anamjua yule fundi akaita watu wakaanza kugonga geti ili wafungue lakini hawajafungua geti. Tukawa tunasikia sauti ya Wema ikisema ‘jamani waacheni hao mtawaua’ lakini anasema hivyo wakati yeye inaonyesha ndo alikuwa kinara wa matukio hayo. Wema na ana roho ya kikatili sana. Amefanya matukio mengi lakini hivyo hapana! Yaani kama anataka usalama wake anatakiwa ahame vinginevyo vijana watamfanyika tukio la kinyama sana,” ameongeza mama huyo.
“Baada ya watu kuwa wengi sana pale nje ndo geti likafunguliwa watu wakaingia na kuwachukua wale vijana wakiwa hawajitambui na wapo uchi ndo wakapelekwa hospitali. Sasa baada ya kupelekwa hospitali polisi wa kituo cha Mabatini na wao wakagonga geti wakawa hawataki kulifungua polisi wakapindukia na kuingia ndo wakawakamata baadhi ya watu na kuondoka nao. Hilo ndo tukio alilolifanya mwanadada wenu ambaye anadai alikuwa Miss Tanzania,” alisema Mama Steve.
Pia shuhuda mwingine aliyejitambulisha kwa jina la Mama Samira, alisema amesikitishwa na tukio hilo la kinyama. “Hii ni tabia yake, hata wafanyakazi wake wa ndani anao kaa nao saa zingine anawapiga makofi! Kwakuwa ni ndani kwa ndani sisi majirani hatufuatilii, lakini kwa hilo na sauti yake tumeisikia japo watu wake wanadai hakuwepo,” alisema.
Kwamujibu wa Bongo5.com,mjumbe wa nyumba kumi, Mwarami  alithibitisha kutokea kwa tukio hilo huku akidai hataki kuliongelea sana kwakuwa limeshafika katika kituo cha polisi Mabatini.
Mkuu wa kituo cha polisi cha Mabatini hakupatikana ilikuthibitisha na kutujuza kile kinachoendelea katika sakata hili.
Mtu wa karibu wa Wema, Petit Man aliyetajwa kuhusika kwenye tukio hilo, aliiambia Bongo5.com kuwa watu hao walipigwa lakini hawakuvuliwa nguo. “Yeah kuna tukio limetokwa,lakini hakuna mtu aliyevuliwa nguo,” alisema Petit na baada ya hapo alikata simu.

Shamsa Ford kufungua mwaka na 'Mama Muuza'

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgGYUQewjSfxvYImYYUqeqR5s4zKjOWq18PYY-DuBI8lA3RzxLZBec1QNYfhVy9SwJB3SOuIUhel6gJ4SjEetukwoD7JgVTz7sBmnPBDh_u-X_YikEiCnC5es419mTWWc16yuaz4ZFgtrg/s1600/After+Death.JPG
Shamsa Ford katika pozi
 BAADA ya kuteka nyoyo za mashabiki kwa mwaka 2014 kupitia filamu yake mwenyewe iitwayo 'Chausiku', muigizaji nyota wa filamu nchini, Shamsa Ford anatarajiwa kuufungua mwaka mpya na 'Mama Muuza'.
Akizungumza na MICHARAZO, Shamsa alisema kama ilivyokuwa kwa 'Chausiku', filamu ya 'Mama Muuza', pia  ameiandika mwenyewe na kutamba itakuwa kali na 'funika bovu' kuliko kazi hiyo ya awali.
Shamsa alisema ndani ya filamu hiyo ambayo ndiyo itakayomfungulia mwaka 2014 ameigiza na wasanii mbalimbali akiwamo Baba Haji ambaye pia alikuwamo katika 'Chausiku'.
http://www.bongocinema.com/images/casts/Shamsa_Ford_03.jpg
Mkali Shamsa Ford
"Baada ya Chausiku kunifungia mwaka 2014, natarajia kuufungua mwaka mpya wa 2015 na kazi mpya iitwayo 'Mama Muuza' ambayo humo nimefanya makubwa kuliko hata yale ya 'Chausiku'," alisema.
Katika filamu ya 'Chausiku' moja kati ya filamu mbili alizocheza mwaka huu, nyingine ikiwa 'Hukumu ya Ndoa Yangu', Shamsa amecheza kama 'demu mcharuko' na kustaajabisha wengi tofauti na haiba yake ya upole.
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgn06H7No1Bn4gEy1LuuHo_4kxOESMdn7FfRCRjWx2opt1DZbvduTi4LxKvsTLnceNFspO8SeueIjaoTLt3zuAD9FYRCrXAuc5KE1IOV9MvboGAFwEDmrc4t8Nwf6yzs_MUfOlKhzGsb64/s640/1.jpg
Shamsa Ford
Shamsa alidokeza filamu hiyo imesharekodiwa na kukamilika na kwa sasa inawekwa kwenye foleni kwa ajili ya kuingia mtaani mwakani na kuwataka mashabiki wake kusubiri uhondo huo

Kumekucha Tamasha ya Dar Filamu 2014

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjLcamPrzOPqAwvFp6SOjwlxLD3rvs3Yew-V6frniQ6-Xn8Z3Wpbjq7k_PHVnYJwQyolBsv3T6sba6tDg2ENJ7iYIz0V8IxEpfAA5EZJw6JFDjRzZEiTIyybgcI8EBaqotLS6eYpt-vtNo/s1600/unnamed+(4).jpgTAMASHA la pili la Filamu la Dar es Salaam (Dar Filamu Festival 2014) linaratajiwa kufanyika kati ya Desemba 19-21 jijini Dar es Salaam na washiriki waliokuwa hawajajitokeza kuomba kushiriki wanatakiwa kufanya hivyo kabla ya kesho saa 10 jioni.
Mmoja wa waratibu wa tamasha hilo ambalo ni maaluma kwa kutangaza kazi za wadau mbalimbali wa filamu mbali na semina mbalimbali zinazoendeshwa juu ya namna ya kuzalisha filamu bora, Myovela Mfaiswa aliliambia MICHARAZO kuwa tamasha lao litafanyikaia viwanja vya Chuo cha Posta, KIjitonyama.
Mfaiswa alisema walitoa muda mrefu kwa washiriki kujitokeza kwa ajili ya ushiriki wa tamasha hilo na mwisho ni kesh Desemba 8 kabla ya kupangwa ratiba ya namna tamasha hilo litakavyoendeshwa kwa siku hizo tatu mfululizo.
"Tamasha leo linatarajiwa kufanyika kwa siku tatu kati ya Desemba 19-21 na siku ya Jumatatu (kesho) ndiyo mwisho wa washiriki kujitokeza kama tulivyoanisha njia mbalimbali za kujiandikisha kwa kujaza fomu iliyopo kwenye mtandao wa www.filamucentral.co.tz na kwingineko," alisema Mfaiswa.
Mfaiswa alisema tamasha la mwaka huu pia litakuwa na mabalozi wake kama ilivyokuwa mwaka jana kwa waigizaji nyota, Vincent Kigosi 'Ray' na Elizabeth Michael 'Lulu' waliobeba jukumu hilo.

Man United yamhakikisha LVG fedha za usajili mpya zipo

http://i.telegraph.co.uk/multimedia/archive/02911/Louis_van_Gaal_2911698b.jpgKOCHA wa klabu ya Manchester United, Louis Van Gaal amehakikishiwa kupewa fedha za kufanya usajili kwenye kipindi cha Majira ya Kiangazi ili kuimarisha kikosi chake.
Uongozi wa klabu hiyo wamemueleka LVG kuwa pesa siyo tatizo kama akiamua kuimarisha kikosi chake katika kipindi cha majira ya kiangazi. 
Van Gaal alitumia kitita cha paundi milioni 150 katika majira ya kiangazi, ukiwemo usajili uliovunja rekodi Uingereza wa paundi milioni 59.7 kwa ajili ya Angel Di Maria lakini bado wanaburuzwa na vinara Chelsea kwa tofauti ya alama 11 katika msimamo wa Ligi Kuu. Kiungo wa ulinzi Kevin Strootman na mabeki Mats Hummels na Diego Godin wote wako katika rada za United. 
Hata hivyo, Ofisa Mkuu wa United Ed Woodward tayari ameshweka wazi kuwa hatataka kuchukua mchezaji kwa mkopo katika kipindi cha usajili wa dirisha dogo Januari. 
Woodward alibainisha mwezi uliopita kuwa tayari wana wachezaji waliowalenga kwa ajili ya usajili ujao wa majira ya kiangazi ila yoyote atakayeweza kupatikana Januari watafanya mipango ya kumchukua.

Beki kisiki Juma Nyosso hatimaye atua Mbeya City

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEje9rYrWVrElb9fsUMQHY2jU9zqBQk65tljQl44m_eUGTeAfxP9jD_OpJdSAKMszLdzy8Cqh3ADGJ5-u4K8712UuuDgrC1xK6r1pypaUOFh-Y07GeO4wrHdT_2kedEjWIClHemMHctwkXkg/s640/NYOSSO.JPG
Juma Nyosso enzi akiichezea Simba
HATIMAYE beki kisiki wa zamani wa Simba na Coastal Union, Juma Said Nyosso amejiunga na kikosi cha Mbeya City ya Mbeya kwa mkataba wa mwaka mmoja.
Akizungumza mara baada ya kuisaini mkataba huo kwenye ofisi za timu zilizopo jengo la Mkapa Hall jijini Mbeya, Nyoso aliyewahi kucheza pia Ashanti United, alisema amekubali kujiunga na City kwa mkataba wa mwaka mmoja kwa imani kuwa utatosha kuushawishi uongozi wa timu kumpa mkataba mrefu zaidi mara baada ya huu wa sasa.
Kariobu nusu msimu beki huyo wa kati alikuwa hana timu yoyote anayoichezea tangu aachwe na Coastal mapema mzimu huu.
“City ni timu nzuri na imekuwa hivyo toka ilipoanzishwa miaka minne iliyopita, matokeo yaliyoo sasa ni sehemu ya soka ambayo timu yoyote inaweza kuyapata, nimekubari kujiunga na timu kwa mkataba wa mwaka mmoja kwa sababu naamini uwezo wangu uwanjani utawashawishi viongozi kunipa mkataba mrefu zaidi pindi huu utakapo malizika na nina amini hili linawezekana kwa sababu nataka kukaa kwenye timu hii mpaka mpira wangu utakapoisha” alisema Nyosso
Akiendelea zaidi beki huyo aliyewahi pia kucheza kwenye kikosi cha timu ya Taifa ‘Taifa Stars’ alisema kuwa mafanikio iliyopata Mbeya City msimu uliopita yamekuwa sababu kubwa ya yeye kukubari kujiunga na City huku akiamini kuwa amekuja kuongeza nguvu kwenye timu bora ili kuhakikisha mafanikio ya msimu uliopita yanafanikiwa tena.
K wa upande wake Katibu Mkuu wa City Emmanuel Kimbe alimshukuru Nyosso kwa kukubari kujiunga na timu hii huku akiamini kuwa uzoefu alionao mchezaji huyo utasaidia kuimarisha safu ya ulinzi kwenye kikosi cha City.
“Tunamshukuru kukubari kujiunga nasi, imani yetu kubwa kwamba uzoefu alionao utasaidia kuimarisha safu yetu ya ulinzi, hasa ukizingatia matokeo tuliyopata katika michezo saba ya mwanzo wa Ligi hii” alisema Kimbe huku kauli yake hiyo ikiungwa mkono na Kocha Mkuu Juma Mwambusi.
Kwa sasa Nyosso tayari yuko na kikosi cha City kilichosafiri kwenda mjini Songea kwa ajiri ya michezo ya kirafiki.

Ronaldo afikisha mabao 200, sasa kinara wa hat trick La Liga

Cristiano Ronaldo celebrates his clinical hat-trick that sent records tumbling during a 3-0 victory at the Bernabeu
Ronaldo alishangilia moja ya mabao yake jana
Cristiano Ronaldo
Akiendelea kufunga
Cristiano Ronaldo
jamaa huyu balaa!
Real Madrid v Celta Vigo
Akishangilia na wenzake ushindi wa nyumbani Santiago Bernabeu
MWANASOKA Bora Duniani, Cristiano Ronaldo usiku wa jana alifikisha bao lake la 200 katika Ligi Kuu ya Hispania, baada ya kupiga 'hat trick' wakati Real Madrid ikiiangamiza 'Celta Vigo kwa mabao 3-0 katika mfululizo wa ligi hiyo.
Hat trick hiyo ni ya 23 kwa Mreno huyo na kumfanya kuwa mchezaji anayeongoza kwa hat trick nyingi katika La Liga kwa sasa, licha ya kukamata nafasi ya 9 ya wachezaji wenye magoli mengi katika ligi hiyo akiwa nyuma ya mabao 53 dhidi ya  'hasimu' wake, Lionel Messi mwenye mabao 253.
Mabao hayo yamemfanya mchezaji huyo kufikisha mabao 200 katika mechi 178 za La Liga kwa misimu wake wa sita nchini humo na pia ni bao la 23 katika mechi 13 za msimu huu, kiasi ambacho ukichukua mabao ya hasimu wake na ya mshambuliaji mwingine nyota wa Barecelona, Neymar hayafikii idadi hiyo ya mabao.

Ronaldo ambaye hakuwepo katika mechi ya Kombe la Mfalme wakati Real Ikishinda mabao 5-0 dhidi ya Cornellà, alianza kuandika bao la kwanza kwa mkwaju wa penati katika dakika ya 36.
Katika kipindi cha pili mkali huyo aliongeza tena mabao mawili katika dakika ya 65 na na 81 alipomaliza kazi nzuri ya Marcelo na kuifanya Real kuzidi kujichimbia kileleni na kuikimbia Atletico.
Ushindi huo umeifanya Real kufikisha pointi 36 wakati wapinzani wao ambao pia ndio mabingwa watetezi wakiwa na 32.
Katika mechi nyingine ya ligi hiyo jana Athletico Bilbao ililala nyumbani kwa bao 1-0 dhidi ya Cordoba na leo kutakuiwa na michezo mingine kadhaa likiwamo pambano la Barcelona dhidi ya wapinzani wao wa Jimbo la Cataluna, Espaniola.
Wakali wa Hat Trick wa Muda wote La Liga Hawa Hapa:
23- CRISTIANO RONALDO 
22- Di Stéfano and Zarra 
20- Messi
19- Mundo 
16- César
13 Lángara

Saturday, December 6, 2014

Man City yaiua Everton 1-0, yazidi kuipumulia Chelsea

Manchester City v Everton
Yaya Toure akitumbukiza penati yake wavuni kuibeba Manchester City dhidi ya Everton
BAO la mkwaju wa penati lililofungwa na Mwanasoka Bora wa Afrika, Yaya Toure yameiwezesha Manchester City kupatya ushindi mwembamba nyumbani dhidi ya Everton na kupunguza pengo la pointi dhidi ya vinara wa Ligi Kuu ya England, Chelsea kufikia pointi tatu tu.
Toure alifunga bao hilo katika dakika ya 24 baada ya Phil Jagielka kumchezea rafu James Milner na yeye kutofanya ajizi kuukwamisha mpira kimiani na kuifanya City ambao ni mabingwa watetezi kufikisha pointi 33 na kung'ang'ania nafasi ya pili nyuma ya Chelsea ambayo mapema leo mchana ilikubali kipigio cha mabao 2-1 toka kwa wenyeji wao Newcastle United na kusitishiwa mfululizo wake wa ushindi katika msimu huu.
Ligi hiyo inatarajiwa kuendelea siku ya Jumatatu kwa pambano moja tu litakaloikutanisha Southmapton dhidi ya Mashetani Wekundu, Manchester United.