STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, January 11, 2015

Sevilla yazidi kuchanja mbuga La Liga

http://videosdelbetis.com/wp-content/themes/Video/thumb.php?src=http://videosdelbetis.com/wp-content/uploads/2013/11/sfc.jpg&w=630&zc=1&q=80&bid=1TIMU ya Sevilla ikiwa uwanja wa ugenini ilipata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Almeria na kujiweka katika nafasi nzuri katika mbio zao kwenye Ligi Kuu ya Hispania, La Liga.
Sevilla ilijikuta ikisubiri hadi kwenye kipindi cha pili kuweza kupata mabao yake hayo ambayo yalifungwa na Iborra katika dakika ya 58 kabla ya Coke kuongeza jingine dakika tano baadaye na kuifanya timu hiyo kufikisha pointi 36 na kushika nafasi ya nne.
Mashabiki wa soka wanatarajia kupata burudani baadaye wakati Barcelona itakayokuwa nyumbani itaikaribisha mabingwa watetezi wa ligi hiyo, Atletico Madrid zinazofukuzana nyuma ya vinara Real Madrid ambayo jana ilizinduka katika ligi hiyo klwa kushinda mabao 3-0 dhidi ya Espanyol.

Mgambo JKT yaitoa nishai Ruvu Shooting Mkwakwani


http://tplboard.co.tz/assets/uploads/files/273f8-63.jpg
Mgambo JKT waliopata ushindi dhidi ya Ruvu Shooting
TIMU ya Mgambo JKT imeitoa nishai Ruvu Shooting katika mfululizo wa Ligi Kuu Tanzania Bara mchezo pekee uliochezwa  leo kwenye uwanja wa Mkwakwani Tanga baada ya kuicharaza bao 1-0.
Ruvu Shooting inayonolewa na kocha Mkenya, Tom Oloba ilishindwa kuhimili vishindo vya maafande wenzao licha ya tambo zilizokuwa zikitolewa na uongozi wa klabu hiyo chini ya Msemaji wao, Masau Bwire.
Bao hilo la wenyeji liliwekwa kimiani na Full Maganga katika dakika ya 44, likiwa ni bao la kwanza kwa mchezaji huyo ambaye amekuwa na kismati cha kuzitungua Simba na Yanga.
Kwa ushindi huo Mgambo imefikisha pointi 12 na kuchupa kutoka nafasi ya 12 hadi nafasi ya nane wakiing'oa Ruvu Shooting ambayo imesaliwa na 11.
Msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara baada ya mchezo wa leo:
                                 P   W    D    L    F    A   GD   Pts
01. Mtibwa Sugar       08  04  04  00  11  04  07   16
02. JKT Ruvu             10  05  01  04  10  09   01  16
03. Yanga                  08  04  02  02  11  07   04  14
04.  Azam                  08  04  02  02  10  06   04  14
05.  Kagera Sugar      09  03  05  01  07  04   03  14
06.  Polisi Moro          10  03  05  02  09  08   01  14
07. Coastal Union      09  03  03   03  09  08   01  12
08.  Mgambo JKT      09  04  00  05   05    09  -4  12
09. Ruvu Shooting    10  03  02   05   05   08  -3  11
10. Stand Utd           10  02  05   03   07   12  -5  11
11. Ndanda Fc          10  03  01   06  10    14  -4  10
12. Simba                08  01  06   01   07   07  00  09
13. Mbeya City         08   02  02   04  03   06  -3   08
14. Prisons               09  01  04   04  06   08  -2   07

Wafungaji Bora:
5-
Didier Kavumbagu(Azam)
4-
Rama Salim (Coastal), Danny Mrwanda, Simon Msuva (Yanga) Ame Ally (Mtibwa), Samuel Kamuntu (JKT Ruvu)

3- Ally Shomari, Emmanuel Okwi (Simba), Rashid Mandawa (Kagera Sugar), Jacob Massawe (Ndanda)
2- Shaaban Kisiga, (Simba), Nassor Kapama (Ndanda) Salum Kanoni (Kagera), Aggrey Morris (Azam),  Najim Magulu, Jabir Aziz (JKT Ruvu), Amissi Tambwe, Jerry Tegete (Yanga), Ibrahim Kihaka (Prisons), Mussa Mgosi (Mtibwa), Heri Mohammed, Mussa Said (Stand Utd), Ally Nassor (Mgambo),  Malimi Busungu (Mgambo), Nicolaus Kabipe (Polisi)
1- Joseph Owino (Simba), Coutinho, Kelvin Yondan, Haruna Niyonzima, Jaja (Yanga), Deo Julius, Steven Mazanda (Mbeya City), Bakari, Imani Mapunda, Said Bahanuzi (Polisi-Moro), Kipre Tchetche,  Aggrey Morris, SHomar Kapombe, John Bocco  (Azam), Ernest Joseph, Paul Ngalema,  (Ndanda), Jacob Mwaitalako,  Laurian Mpalile, Amir Omary, Hamis Mahingo (Prisons), Lutimba Yayo, Kennedy Masumbuko, Joseph Mahundi, Hussein Sued,Itubu Intembe (Coastal), Ramadhani Pella, Full Maganga (Mgambo), Said Mkopi, Vincent Barnabas (Mtibwa), Amos Mgina, Najim Magulu, (JKT Ruvu), Salum Kamana, Shaaban Kondo (Stand Utd), Paul Ngwai, Atupele Green(Kagera Sugar), Juma Nade, Abdulrahman Mussa, Thomas Mathayo , Hamis Kasanga ,Zubeiry Dabi (Ruvu Shooting)

Inter Milan yatamba nyumbani,

Nemanja Vidic
Vita ya Inter Milan dhidi ya Genoa leo
KLABU ya Inter Milan imefanikiwa kuifumia Genoa kwa kuicharaza mabapo 3-1 katika mechi kali ya Ligi Kuu ya Italia, Serie A, wakati AS Roma na mahasimu wao Lazio wametoshana nguvu ya maba0 2-2.
Inter ikiwa nyumbani ilipata ushindi huo kupitia mabao ya Palacio katika dakika ya 12, Mauro Icardi dakika ya 39 na Nimanja Vidic dakika mbili kabla ya mechi kumalizika, huku bao la wageni lilifungwa na Izzo dakika ya 85.
Katrika mechi nyingine za ligi hiyo,
Atlanta ikiwa nyumbani imelazimishwa sare ya 1-1 na Chievo Verona, Cagliari ikainyoa Cesena mabao 2-1 na Fiorentina ikipata ushindi mtamu nyumbani dhidi ya Palermo baada ya kuinyoa mabao 4-3.
Nayo Hellas Verona ikiitafuna Parma waliowafuata kwao kwa mabao 3-1 na Mahasimu wa jiji la Roma, AS Roma na Lazio zilishindwa kutambiana kwa kutoka sare ya 2-2 na Sampdoria iliilaza Empoli kwa bao 1-0 baadaye Napoli watakuwa wenyeji wa vinara Juventus.

Arsenal yaitoa nishai Stoke City Sanchez azidi kung'ara

The Arsenal players join star man Sanchez in celebration of his second goal of the afternoon
Wachezaji wa Arsenal wakipongezana
Arsenal defender Koscielny (6) heads the north London club into an early lead at the Emirates after just six minutes
Laurent Koscielny akifunga bao la kwanza la Arsenal kwa kichwa
MABAO mawili kutoka kwa Alexis Sanchez na jingine la beki Laurent Koscielny yameiwezesha Arsenal kupata ushindi mujarabu nyumbani dhidi ya 'wagumu' Stoke City katika mfululizo wa mechi za Ligi Kuu ya England.
Ushindi  huo umekuja wakati Arsenal ikitoka kupokea kipigo cha mabao 2-0 toka kwa Southampton, ambapo kiungo Mesut Ozil, alirejea uwanjani katika pambano hilo la Emirates baada ya kuwa nje miezi mitatu.
Wenyeji walianza kuandika bao dakika ya 6 kupitia Koscielny kabla ya Sanchez kuongeza la pili dakika ya 33 na kuja kuongeza jingine dakika nne tangu kuanza kwa kipindi cha pili.
Katika pambano hilo Arsenal ilijikuta ikimpoteza beki wake Mathieu Debuchy aliyeumia bega mapema na nafasi yake kuchukuliwa na Bellerin dakika chache baada ya Koscielny kufunga bao la kuongoza kwa kichwa akimaliza krosi ya Sanchez ambaye kwa mabao mawili ya leo amefikisha mabao 12 katika ligi hiyo anayoicheza kwa msimu wa kwanza.

Kwa ushindi hio Arsenal imefikisha pointi 36 na kulingana na Southampton na kukamata nafasi ya tano wakati wapinzani wao wamesaliwa na pointi26 na kusalia kwenye nafasi ya 11.
Muda mchache ujao Manchester United watakuwa uwanja wa Old Trafford kupepetana na Southampton katika mechi nyingine ya ligi hiyo ambayo baadhi ya nyota wa Man Utd waliokuwa nje kwa majeraha watarejea dimbani.
Wachezaji hao ni Daley Blind na Angel di Maria  ambao wapo kwenye kikosi cha kwanza cha kocha Louis Van Gaal.


Saturday, January 10, 2015

Ozil arejea Arsenal, Rojo, Blind waipa furaha Man Utd

Kipa Valdes akiwa na wachezaji wenzake wapya wa Manchester United

Daley Blind akifanya mazoezi hapa akiwa na Dogo Andreas Pereira
Rojo naye alipasha na wenzake
WAKATI Manchester United wakichelekea kurejea tena dimbani kwa nyota wake Marcos Rojo na Daley Blind, Kiungo Mesut Ozil wa Arsenal naye amepona na huenda akarejea uwanjani kesho wakati Arsenal inakipiga dhidi ya Stoke City.
Mashetani Wekundu wanatarajiwa kuwa nyumbani kuwavaa Southampton baada ya kupata sare mbili mfululizo ugenini katika Ligi Kuu ya England, lakini ikiwa na furaha kurejea kwa nyota hao sambamba na kumnasa kipa wa zamani wa Barcelona, Victor Valdes waliyemsainisha.
Kama ilivyo kwa Manchester, Arsenal wenyewe wanafurahi baada ya Ozil kurejea Ligi Kuu England baada ya kukaa nje miezi mitatu kutokana na maumivu ya goti.
Kocha Arsene Wenger amesema Ozil amekuwa akifanya mazoezi na wenzake na sasa yuko fiti, hata hivyo inaonekana ataanzia benchi.
Mjerumani huyo aliyejiunga na Arsenal akitokea Madrid aliumia katika mechi dhidi ya Chelsea, Oktoba mwaka jana.
Ozil ndiye mchezaji ghali zaidi Arsenal iliyompata kwa kitita cha pauni milioni 42.5.

Real Madrid yazinduka yaipiga Espanol 3-0

Gareth Bale
Bale akishangilia bao lake wakati Real ikiiadhibu Espanyol
Real Madrid v Espanyol
Nacho akishangilia bao lake
LICHA ya kucheza pungufu timu ya Real Madrid imepata ushindi wa mabao 3-0 nyumbani katika  Ligi Kuu ya Hispania dhidi ya Espanyol na kuzidi kujichimbia kileleni mwa msimamo wa ligi hiyo.
Fabio Coentrao alilimwa kadi nyekundu kaytika dakika ya 53, lakini mabao ya James Rodriguez katika dakika ya 12 , Gareth Bale dakika ya 28 na  lile na Nacho la dakika ya 70 yalitosha kuwapa ushindi muhimu Real Madrid iliyoshuhudia nahodha wake, Cristiano Ronaldo akitoka uwanjani bila kufunga bao ikiwa ni mara ya kwanza baada ya muda mrefu msimu huu.
Kwa ushindi hio Madrid wamefikisha pointi 42 na kuiacha Barcelona ikiwa nafasi ya pili na pointi 38 sawa na ilizonazo nazo Atletico Madrid ambazo zinatarajiwa kushuka dimbani kesho.
Katika mechi nyingine ya ligi hiyo iliyochezwa leo, Malaga ikiwa nyumbani ililazimishwa sare ya 1-1 na  Villarreal na hivi sasa Celta Viro ipo dimbani kuumana na Valencia nyumbani kwao na tayari wamekubali bao 1-0.

Haya ndiyo matokeo ya EPL kwa leo

Balotelli akichuana na mchezaji wa Sunderland
City ilipong'ang'aniwa na Everton ugenini leo
Chelsea wakipongezana baada ya kupata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Newcastle Utd
Sunderland     0 - 1     Liverpool
Burnley     2 - 1     Queens Park Rangers
Chelsea     2 - 0     Newcastle United
Everton     1 - 1     Manchester City
Leicester City     1 - 0     Aston Villa
Swansea City     1 - 1     West Ham United
West Bromwich …     1 - 0     Hull City    
Crystal Palace     2 - 1     Tottenham Hotspur

Fainali Mapinduzi ni Simba na Mtibwa

http://taarifa.co.tz/wp-content/uploads/2015/01/simba1.jpg
Simba waliowafuata Mtibwa Fainali za Kombe la Mapinduzi
Mtibwa Sugar (jezi za kijani) watakaoumana na Simba siku ya Jumanne
KLABU ya Simba imefanikiwa kutinga Fainali za michuano ya Kombe la Mapinduzi 2015 baada ya kuing'oa Polisi ya Zanzibar na sasa wanatarajiwa kukutana na Mtibwa Sugar siku ya Jumanne.
Mtibwa ilifanikiwa kufuzu hatua hiyo mapema leo jioni baada ya kuiondosha kwa mikwaju ya penati 4-3 'wababe' wa Yanga, JKU baada ya kumaliza dakika 90 wakiwa sare ya 0-0.
Simba iliyoonyesha mabadiliko makubwa tangu ianze kunolewa na kocha Goran Kopunovic, walipata nafasi hiyo muda mchache uliopita baada ya kupata ushindi wa bao 1-0 katika Nusu Fainali ya pili iliyochezwa uwanja wa Amaan. Zanzibar.
Bao lililoipelekea Simba kwenye hatua hiyo na kurejesha kumbukumbu ya nusu fainali ya mwaka 2010 ambapo timu hizo zilikutana na Mtibwa kuibuka wababe kabla ya kwenda kutwaa taji kwa kuilaza Ocean View bao 1-0.
Pia fainali hizo zinarejesha pia fainali ya ABC Top 8 iliyocvhezwa mwaka juzi na Simba kuilaza Mtibwa kwa mabao 4-3.
Mechi hiyo ya faionali itachezwa usiku wa Jumanne kwenye uwanja wa Amaan huku kila timu ikiwa na matumaini makubwa ya kutwaa taji hilo lililokosa mwenyewe baada ya KCCA ya Uganda kutemeshwa hatua ya Robo Fainali baada ya kufungwa kwa penati na Polisi.

JKT Ruvu waikamata Mtibwa Sugar,, yailaza Stand Utd Ndanda

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjjrGUIMxPw7cdxPgyXtAxRJHOSLFdOsz_Yetg7EBn6y-K7pPB3ToQogwImAjfSZceVrbx9aUL72b0URIua7OK30a6XbaCvr5aiWZXfZNKy95h3Kn2aQ1qmkPYpYSe6mpm7NGtNDBnXSwLZ/s640/DSC_0805.JPG
KIkosi cha JKT Ruvu kilichochupa hadi naasi ya pili ikiziengua Yanga na Azam
MAAFANDE wa JKT Ruvu jioni ya leo wamepata ushindi muhimu wa mabao 2-1 dhidi ya Stand United ya Shinyanga na kuikamata Mtibwa Sugar ambao wapo kwenye michuano ya Kombe la Mapinduzi 2015.
Samuel Kamuntu na Amos Mgina waliifungia mafaande hao mabao hayo na kuifanya timu hiyo inayonolewa na kocha Fred Felix Minziro katika mchezo uliochezwa uwanja wa Chamazi na kuifanya ifikishe pointi 16 sawa na Mtibwa waliosalia kileleni. Bao la wageni Stand lilifungwa na Mussa Said.
JKT waliotangulia michezo miwili mbele dhidi ya Mtibwa inatoautiana na vinara hao mabao ya kufunga na kufungwa, Mtibwa ikiwa na 11 na kuungwa manne ilihali JKT ikiwa na mabao 10 na kufungwa 9.
Katika mechi nyingine iliyochezwa mjini Mtwara, wenyeji Ndanda Fc ililazimishwa sare ya bao 1-1 dhidi ya Polisi Morogoro.
Wageni walitangulia kupata bao kupitia Said Bahanuzi kabla ya wenyeji kuchomoa kupitia Jacob Massawe na kumanya mshambuliaji huyo wa zamani wa Toto African na African Lyon kuikisha bao la tatu msimu huu.
Ligi hiyo itaendelea kesho kwa mechi moja tu itakayowakutanishja wenyeji Mgambo JKT itakayoikaribisha Ruvu Shooting kwenye uwanja wa Mkwakwani Tanga.

Friday, January 9, 2015

KICHOMI NI JASHO NA DAMU-BETHA SHAIBU

MSANII na mtayarishaji chipukizi wa filamu nchini, Betha Shaibu amesema 'limemtoka' jasho na damu katika kufanikisha kuitengeneza filamu yake ya kwanza iitwayo 'Kichomi' ambayo inatarajiwa kuachiwa mwezi huu.
Akizungumza na MICHARAZO, Betha alisema filamu hiyo iliyoshirikisha mastaa kadhaa nchini ni moja ya filamu ya kimapenzi yenye mafunzo makubwa kwa jamii na hasa watumiaji wa mitandao ya kijamii.
Betha alisema anaomba Mungu filamu hiyo iingie sokoni ili mashabiki waone tofauti iliyopo kati ya kazi hiyo na nyingine kwa namna msuko wa filamu hiyo ulivyo.
"Kwa kweli sijapumua mpaka kazi iingie sokoni, najua mwanzo ni mgumu lakini nimekubali kupambana ili kusimama kwa kutambua nina kipaji kikubwa cha utunzi na uigizaji," alisema Betha.
Ndani ya filamu hiyo ya 'Kichomi', Betha ameshirikiana na wakali kama Hemed Suleiman, Sabrina Omari, Mzee wa Majanga na wengine na imetengenezwa kupitia kampuni ya Red Leaf Entertainment.

Safari ya Inspekta Haroun Japan sasa April

MSANII mkongwe wa muziki wa kizazi kipya nchini, Rashid Kahena 'Inspekta Haroun' a.k.a Babu anatarajiwa kwenda nchini Japan baadaye mwaka huu baada ya awali kushindwa kufanya hivyo mwishoni mwa mwaka jana.
Inspekta Haroun aliliambia gazeti hili kuwa, ziara yake kwenda kutengeneza kazi mpya chini ya kampuni ya Hyper Production chini ya Deejay Kay Dee Beatz ilipangwa kufanyika Desemba mwaka jana, lakini ilishindikana baada ya kukosa visa.
Alisema hivyo wamekubaliana na 'mabosi' wake safari hiyo sasa iwe mwezi April akimini kuwa kila kitu kitaenda sawa kwa ajili ya kwenda kufanya kazi chini ya lebo hiyo.
"Safari yangu ya kwenda Japan kuingia mkataba wa kufanya kazi chini ya lebo ya Hyper Production imekwama kwa kukosa visa na sasa itafanyika Aprili kwa kuamini kila kitu kitakuwa kimekamilika, ingawa tayari kampuni hiyo imetengeneza video za nyimbo zangu mbili ambazo nitaziachia hivi karibuni mashabiki wapate burudani," alisema.
Babu alisema video hizo ni za nyimbo za 'Mungu Ndiye Anayepanga alioimba na Sir Juma Nature na ule wa 'Bado Hujachelewa' alioimba pekee yake ambapo kampuni hiyo ilifanya kazi ya kuzichanganya picha na kuongeza vionjo baada ya kuvutiwa na nyimbo hizo.

K-One Suma Lee wana ngoma mpya kwa Baucha

BAADA ya kutamba na nyimbo za 'Yule' aliyoimba na Maunda Zorro na 'Jimama Zamiela', msanii K-One anajiandaa kufyatua 'ngoma' mpya aliyomshirikisha mkali wa zamani wa Parklane, Suma Lee.
Akizungumza na MICHARAZO, Mkurugenzi wa Baucha Records inayommilikia msanii K-One, Ali Baucha alisema wimbo huo upo hatua ya mwisho kabla ya kuachia rasmi mwezi ujao ukiwa umetengenezwa katika studio zake.
Baucha alisema wimbo huo ambao bado haujapewa jina ni kati ya kazi tatu mpya za studio hizo zinazotarajiwa kuachiwa karibuni, wimbo mwingine ukiwa ni wa Fizzo aliyemshirikisha Mshindi wa BSS 2013, Walter Chilambo.
"Baucha Records kwa sasa tupo katika maandalizi ya kutoa kazi mpya baada ya kuhamisha studio mahali tulipokuwapo awali pale Magomeni Mapipa, na kati ya kazi hizo moja ni wa K-One akiimba na Suma Lee na mdogo wangu anayeishi Ujerumani pamoja na ule wa Fizzo anaoimba na Walter Chilambo," alisema Baucha mmoja wa watayarishaji mahiri wa muziki wakongwe nchini.

Michuano ya Taifa ya Soka kwa wanawake kuanza kesho

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhcLvLEgI1HLK7c-HmKa5lTL3-7Sz3hW-nNnR1ogOhAVkhVKc6ERg0HahgcfqOkBf4_82s6MMwonfDQO7d_g2raIBEMLzyQP0shox0pazxJwKSHQDgzmt-H2s4PIlBvwSC8RTQiBheP3ss/s1600/IMG_8106.JPGMICHUANO ya soka ya Kombe la taifa kwa timu za Wanawake inatarajiwa kuanza kesho Jumamosi ambapo mechi ya kwanza za raundi ya kwanza zitachezwa kesho kwenye miji 11 tofauti nchini.
Katika mashindano hayo yanayodhaminiwa na kampuni ya Proin, Geita itakuwa mwenyeji wa Kagera (Uwanja wa Geita), Tabora itacheza na Kigoma kwenye Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mjini Tabora, Simiyu na Shinyanga (Uwanja wa Simiyu), Arusha na Manyara (Sheikh Kaluta Amri Abeid), na Kilimanjaro na Tanga (Uwanja wa Ushirika).
Mechi nyingine ni Lindi itaikaribisha Mtwara kwenye Uwanja wa Ilulu, Ruvuma na Njombe (Uwanja wa Majimaji), Mbeya na Iringa (Uwanja wa Sokoine), Katavi na Rukwa (Uwanja wa Katavi), Dodoma na Singida (Uwanja wa Jamhuri) na Pwani itakuwa mwenyeji wa Morogoro katika Uwanja wa Mabatini.
Timu hizo zitarudiana Januari 13 mwaka huu, ambapo baada ya matokeo ya nyumbani na ugenini timu iliyoshinda ndiyo itakayoingia hatua inayofuata ambayo pia itashirikisha mikoa ya kisoka ya Ilala, Kinondoni na Temeke.
Hatua hiyo, mechi zake za kwanza zitachezwa Januari 17 mwaka huu wakati zile za marudiano zitafanyika Januari 21 mwaka huu.
Baada ya hapo, hatua itakayofuata ni robo fainali, nusu fainali na fainali ambayo ndiyo itakayotoa bingwa wa michuano hiyo inayofanyika kwa mara ya kwanza nchini.

Wazee wa 4 waaga Mapinduzi Cup, wapigwa kidude na JKU

* Nusu fainali ni Simba v POlisi, Mtibwa v JKU

BAADA ya kutamba kwa kugawa 'dozi' nono ya mabao manne manne kwa wapinzani wao katika mechi ya makundi kabla ya kupunguzwa na Shaba kwa kuishinda bao 1-0, Yanga imeaga michuano ya Kombe la Mapinduzi kwa kufungwa bao 1-0 na JKU.
Yanga waliosheheni wachezaji 'ghali' na mastaa wanaotamba Afrika Mashariki walishindwa kufurukuta kwa maafande hao wa Jeshi la Kujenga Uchumi visiwani Zanzibar kunakofanyikia michuano hiyo itakayofikia tamati Jumanne.
Bao lililowazima Yanga na kuhitimisha tambo zake liliwekwa kimiani na Amour Omary 'Janja' aliyemfikia Andrey Coutinho aliye na mabao matatu katika orodha ya wafungaji.
Janja alifunga bao hilo lililokuwa la tatu kwake katika dakika ya 72 na kuwaacha vijana wa Hans van der Pluijm wakijilaumu kutokana na kukosa mabao mengi ya wazi katika muda wote wa pambano hilo lililochezwa uwanja wa Amaan.
Ushindi huo kwa JKU imeifanya timu hiyo kutinga Nusu Fainali na kupata nafasi ya kuvaana na Mtibwa Sugar waliowang'oa Azam kwa mikwaju ya penati baada ya kumaliza pambano lao kwa kufungana bao 1-1, Azam wakilazimika kusawazisha dakika za jioni kupitia Kipre Tchetche baada ya Shomar Ally kutangulia kufunga.
JKU imekuwa timu ya tatu kutoka kundi C ambazo zote zimepenya robo fainali na kutinga pia Nusu Fainali.
Nyingine ni Simba ambayo itaumana kesho na Polisi Zanzibar waliowavua taji la michuano hiyo KCCA ya Uganda kwa mikwaju ya penati baada ya kutoka suluhu ndani ya muda wa kawaida na Mtibwa Sugar ambao ni Vinara wa Ligi Kuu Tanzania Bara.

Sabrina Omar, PHD 'wauza sura' katika KICHOMI

SALOME
PHD
WAIGIZAJI nyota wa filamu nchini, Sabrina Omar 'Salome' na Hemed Suleiman 'PHD' wanatarajiwa kuonekana kwenye filamu mpya iitwayo 'Kichomi' ambayo imewashirikisha wakali wengine.
Mtayarishaji wa filamu hiyo, Betha Shaibu aliiambia MICHARAZO jana kuwa, filamu hiyo inayotarajiwa kuachiwa sokoni hivi karibuni, ni kazi yake ya kwanza kupitia kampuni ya Red Leaf Entertainment na kuongozwa na Joseph Jembe na Daudi.
Betha alisema filamu hiyo ya kijamii imewashirikisha nyota wakali kadhaa wenye majina nchini akiwamo Salome, Hemed Suleiman 'PHD', Raheem David 'Kibeberu' na Mzee wa Majanga.
"Ni filamu yangu ya kwanza ambayo nimeigiza kwa jina la Jameth nikishirikiana na wakali kama PHD, Sabrina Omar, Kibeberu na Mzee wa Majanga na inatarajiwa kuwa sokoni ndani ya mwezi huu," alisema Betha.
Betha alisema washiriki wa filamu hiyo wameitendea haki na kuwaomba mashabiki wasikose kuiona mara itakatoka hadharani kwani ina mafunzo makubwa kwa jamii mbali na kuburudisha.

Kitabu cha Steven Kanumba kuzinduliwa leo Landmark Hotel

Steven Kanumba enzi za uhai wake
Mwanamuziki Christian Bella na Mama yake Kanumba, Flora Mtogoha wakikinadi kitabu cha maisha ya marehemu Steven Kanumba kitakachozinduliwa leo pale Ubungo
Mtunzi wa kitabu hicho akikitambuliosha kwa wanahabari huku mratibu wa onyesho la uzinduzi, Frank akifuatilia kwa makini
MWANDISHI wa kitabu kinachohusu maisha ya nyota wa zamani wa filamu, Steven Kanumba kinachoitwa 'The Great Fallen Tree', Emmanuel Zirimwabagabo, amesema mauzo ya kitabu hicho  yataingizwa kwenye mradi wa Kanumba Foundation.
Taasisi hiyo ya inahusika na masuala ya kusaidia wajane na yatima ilianzishwa ikiwa ni njia ya kumuenzi marehemu Kanumba aliyefariki takriban miaka mitatu iliyopita.
Akizungumza na wanahabari, mtunzi huyo raia wa Canada mwenye asili ya DR Congo, alisema amefikia hatua hiyo baada ya kuongea na Mama Kanumba kuhusu ndoto za marehemu Kanumba aliyekuwa akipenda kuwasaidia yatima na alipanga kuwa na taasisi ya kusaidia wajane, lakini alifariki kabla ya kukamilisha ndoto zake.
“Mimi nilikuwa mpenzi wa kazi za Steven Kanumba baada ya kufariki niliumia sana, lakini nikafikiria ni jambo gani ambalo naweza kulifanya ili Kanumba aendelee kuishi japo hatupo naye kimwili lakini kiroho tupo naye,” alisema
“Nilifikiria kuandika kitabu kama sehemu ya heshima yangu kwake shujaa huyu kwetu sisi watu tunaopenda kazi zake, kwani Kanumba kanisaidia kujua kuongea Kiswahili kupitia filamu zake, hivyo napenda kuwe na kitu cha kumkumbuka," alisema Zirimwabagabo aliyetoa kitabu hicho kwa lugha mbili, cha Kiswahili na Kiingereza.
Naye Mama Kanumba, alitoa shukrani zake na akisema hakuwahi kufikiria kama mwanaye alikuwa na thamani kubwa kama hiyo hadi watu wa mataifa mengine kuja kuona kama ni mtu ambaye anatakiwa kuwekewa kumbukumbu kwa kuwekewa kitu au taasisi.
Kitabu hicho cha maisha ya kanumba kitazinduliwa kesho kwenye ukumbi wa Landmark Hotel, Ubungo ambako sherehe hizo zitaenda sambamba na uzinduzi wa taasisi hiyo ya Kanumba Foundation chini ya uratibu wa muigizaji Mohammed Mwikongi 'Frank' na burudani itakayosindikiza uzinduzi huo itatolewa na muimbaji Christian Bella.

2014 ni Yaya Toure tena, aweke rekodi akiifikia ile ya Samuel Eto'o

Yaya  Toure aliyenyakua tuzo ya Mwanasoka Bora akiweka rekodi ya aina yake Afrika
Samuel Eto'o aliyekuwa akishikilia rekodi ilivyofikiwa na Toure
KIUNGO wa kimataifa wa Ivory Coast anayeichezea klabu ya Manchester City, Yaya Toure ameibuka tena kuwa Mwanasoka Bora wa Afrika kwa mara ya nne na kufikia rekodi ya Samuel Eto'o wa Cameroon.
Toure alishinda tuzo hiyo ikiwa ni rekodi ya kuwa mwanasoka wa kwanza kutwaa mara nne mfululizo katika hafila iliyofanyika usiku wa kuamkia leo mjini Lagos Nigeria.
Toure, 31, aliibuka kidedea kwa kupata pointi nyingi mbele ya mshambuliaji wa Borussia Dortimund raia wa Gabon, Pierre-Emerick Aubameyang na kipa wa Nigeria Vincent Enyeama.
Mchezaji huyo aliyeipa City taji la Ligi Kuu msimu uliopita na kuipeleka Tembo ya Ivory Coast kwenye Fainali za Afrika zitakazoanza wiki ijayo, alishatwaa tuzo miaka mitatu iliyopita 2011, 2012 na 2013.

Ni Eto'o pekee aliyekuwa na rekodi ya kutwaa tuzo hiyo mara nne baada ya kufanya hivyo mwaka 2003, 2004, 2005 na 2010.
Katika tuzo nyingine Mwanasoka Bora anayecheza barani Afrika imeenda kwa Firmin Mubele Ndombe (DR Congo), huku Mwanasoka Bora wa Kike tuzo akiwa ni Asisat Oshoala wa Nigeria ambaye pia alinyakua tuzo ya Mwanasoka Bora wa Kike anayechipukia.
Mwanasoka Chipukizi kwa wanaume ilienda kwa Yacine Brahimi (Algeria) wakati tuzo ya Kocha Bora ni; Kheireddine Madoui wa ES Setif.
Timu Bora kwa 2014 ni Algeria kwa wanaume na Nigeria kwa wanawake ilihali Klabu Bora ni ES Setif (Algeria) na Kiongozi Bora ni Rais wa TT Mazembe Moise Katumbi Chapwe.
Orodha ya Mwanasoka Bora Afrika tangu 1995:
1995- George Weah (Liberia)
1996- Nwankwo Kanu(Nigeria)
 1997-    Victor Ikpeba (Nigeria)
1998-    Mustapha Hadji (Morocco)
1999-     Nwankwo Kanu (Nigeria)
2000-    Patrick Mboma (Cameroon)
2001-     El Hadji Diouf (Senegal)
2002-     El Hadji Diouf (Senegal)
2003-     Samuel Eto'o (Cameroon)
2004-    Samuel Eto'o (Cameroon)
2005-     Samuel Eto'o (Cameroon)
2006-    Didier Drogba (Ivory Coast)
2007-     Frederic Kanoute (Mali)
2008-    Emmanuel Adebayor (Togo)
2009- Didier Drogba (Ivory Coast)
2010-     Samuel Eto'o (Cameroon)
2011-     Yaya Toure     (Ivory Coast)
2012-     Yaya Toure (Ivory Coast)
2013-     Yaya Toure (Ivory Coast)
2014-     Yaya Toure (Ivory Coast)

Monday, January 5, 2015

Lukas Podolski awashukuru Arsenal akitua San Siro

http://cdn.caughtoffside.com/wp-content/uploads/2014/12/460208232.jpg
Lucas Podolski
MPANGO wa Lukas Podolski kuhamia Inter Milan kwa asilimia kubwa umekamilika kufuatia  mshambuliaji huyo wa Ujerumani kukutana na kocha wa klabu hiyo Roberto Mancini katika uwanja wa mazoezi wa timu hiyo Jumamosi.
Nyota huyo ameshaaga Arsenal tayari kuanza maisha mapya katika Ligi ya Italia maarufu kwa jina la Seria A.
“Mshindi huyu wa kombe la dunia alikuwepo Centro Sportivo Angelo Moratti leo (jana) kwa lengo la kufahamu uwanja wake mpya wa mazoezi na alikutana na kocha wa Nerazzurri ,” taarifa ya Inter Milani kwa vyombo vya habari ilieza.
Mshambuliaji huyo wa Gunners amecheza mechi 13 tu za michuano yote msimu huu, hakuna aliyoanzishwa, lakini bado alitumia muda wake kuwashukuru mashabiki kwa sapoti yao kuelekea kuondoka kwake.
“Siwezi kuelezea kwa maneno shukrani yangu kwa mashabiki wa Arsenal kwa yote waliyoyafanya kwangu katika miaka yangu niliyokuwapo London,” aliandika katika ukurasa wake wa Instagram.
“Tafadhalini mtambue kuwa moyo wangu daima una nafasi yenu. Natumai nimeacha alama yangu klabuni na kwa mashabiki pia. Natumai tutaonana tena! COYG.”
Nyota huyo mwenye umri wa miaka 29 alijiunga na Arsenal akitokea FC Koln 2012 na mkataba wake wa sasa na Gunners unamalizika Juni 2016.

Azam yafufuka Zanzibar yainyoa KMKM

AZAM FC imezidnuka kwenye michuano ya Kombe la Mapinduzi baada ya kupata ushindi mwembamba wa bao 1-0 dhidi ya Mabingwa wa Zanzibar, KMKM katika mechi iliyochezwa usiku wa jana kwenye uwanja wa Amaan, Zanzibar.
Bao pekee la Azam liliwekwa kimiani katika dakika ya 18 kutokana na kujifunga kwa nahodha wa KMKM, Khamis Ali akijaribu kuokoa mpira wa krosi ya Shomari Kapombe.
Ushindi huo umeifanya Azam kufikisha pointi 4 na kulingana na timu ya KCCA waliotoshana nao nguvu katika mechi yao ya kwanza walipofungana mabao 2-2.
Michuano hiyo inatarajiwa kuendelea leo kwa michezo ya Kundi C Mafunzo wakivaana na Mtibwa Sugar majira ya saa 10:00 jioni uwanja wa Amaan kabla ya usiku Simba watashuka dimbani kuchuana na JKU.

Fernando Torres atambulishwa Atletico Madrid baada ya kurejea

2
Torres alipotambulishwa klabu ya Atletico Madrid
3456MSHAMBULIAJI nyota wa zamani wa Liverpool na Chelsea, Fernando Torres amerejea rasmi kwenye klabu yake ya zamani ya Atletico Madrid ya nchini Hispania.
Torres aliondoka miaka saba iliyopita kwa kujiunga na Liverpool ya England kabla ya kuhamia Chelsea na baadauye kutolewa kwa mkopo AC Milan.
”Nimefurahi sana kurejea klabu yenye nafasi kwenye maisha yangu,niliondoka kwenye klabu hii kwenda kukuza kiwango changu,nafurahi kurejea tena Atletico ikiwa sasa inashindana na vilabu vikubwa ulimwenguni,nimerejea kushinda na mataji na klabu hii niipendayo”.
Hayo yalikuwa maneno ya Torres wakati akizungumza na waandishi wa habari wakati wa utambulisho wake uliohudhuliwa na mashabiki zaidi ya 45,000 kwenye dimba la Vicente Calderon jana.

Binti wa miaka 14 akamatwa akitaka kujilipua bomu

Binti Zahrau akihojiwa
BINTI mmoja aliyefahamika kwa jina la Zahrau Babban Gida (14) ameshikiliwa na jeshi la polisi nchini Nigeria baada ya kukamatwa akiwa katika harakati za kulipua bomu kwa kujitoa mhanga. 
Kwa mujibu wa chanzo cha habari hii, Msichana Zahrau amekamatwa wakati alipokuwa amejifunga mabomu mwili mzima tayari kwa kufanya maangamizi na alichokuwa akikisubiri ni kuripuka tu. na kama angefanikiwa basi angeweza kutoa uhai wa watu zaidi ya 1000 kwa dakika moja tu. 
Zuhrau amezungumza na vyombo vya habari akiwa chini ya ulinzi mkali wa jeshi la polisi la nchini humo na kusema kuwa, amejiunga na kundi la Bokoharamu kutokana na msukumo kutoka kwa baba yake mzazi ambaye ndiye aliyemlazimisha kujiunga na kundi hilo. 
Zahrau ameongeza kuwa alipofika huko kwenye kambi ya Bokoharam aliwakuta wasichana wengi ambao wamepewa mafunzo ya kujitoa mhanga. 
Uchunguzi umebainisha kwamba Bokoharam wameamua kutumia watoto wadogo katika kujitoa mhanga kwasababu watu wazima wamekuwa wakishitukiwa kirahisi katika harakati zao. 
Chanzo: Nigernews

Kachumbari kuzikwa kesho Goba, Dar es Salaam

10898226_10152990764907888_9161307175547706048_n
Flowin Kachumbari
MWANAMUZIKI mpiga drum wa miaka mingi ambaye hivi karibuni alikuwa na bendi yake African Chacha Band, Kachumbari aliyefariki jana anatarajiwa kuzikwa kesho Goba, pembezoni mwa jiji la Dar es Salaam.
Frowin ambaye ni mwenyeji wa mikoa ya Kusini alianzisha bendi yake hii akawa akipiga muziki wa mahadhi ya kwao na kuwa na tenda nyingi katika mahoteli mbalimbali. Alikuwa akisumbuliwa na matatizo ya uti wa mgongo yaliyokuwa yakimsababishia maumivu ya miguu.(Picha kwa Hisani ya William Kaijage)

Barcelona yagongwa na Moyes, yashindwa kuing'oa Real Madrid

Real Sociedad's Xabier Prieto (right) attempts to claim the goal after Alba's header on two minutes
Real Sociedad wakishangilia bao la kujifunga la Barcelona
Former Liverpool striker  Suarez (left) competes with Real Sociedad's Alberto de la Bella as Barcelona chase the game
Suarez akichuana na mchezaji wa Real Sociedad
Barcelona enforcer Javier Mascherano (left) holds off Canales of Real Sociedad during the first half
Javier Mascherano akiwania mpira katika pambano ambalo Barcelona ililala bao 1-0
BAO la kujifunga la dakika ya pili lililotumbukizwa wavuni na Jordi Alba kwa kichwa katika harakati za kuokoa mpira zimeikwamisha Barcelona kukwea kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu ya Hispania baada ya kukubali kichapo cha bao 1-0 ugenini dhidi ya Real Sociedad inayonolewa na kocha David Moyes.
Barcelona walikuwa na nafasi ya kuiengua Real Madrid waliofungwa mabao 2-1 ugenini na Valencia, walishtukizwa na kipigo hicho ambacho na hasa baada ya kuwaanzisha benchi nyota wake Lionel Messi, Neymar na wengine kabla ya kuwaingia ili kuibeba biola mafanikio.
Kwa kipigo hicho Barcelona imesaliwa na pointi 38 ikishika nafasi ya pili nyuma ya Real Madrid yenye pointi 39 ikiwa na mchezo mmoja mkononi, huku Atletico Madrid ikiwa na pointi 38 wakishika nafasi ya tatu.
Ligi hiyo ya Hispania itaendelea leo kwa pambano moja litakalowakutanisha timu zaCardoba itakayoikaribisha Granada.

Bondia Omar Kimweri kuja kufunza ngumi, Super D achekelea

Na Mwandishi Wetu
NDONDI ni miongoni mwa michezo maarufu mno hapa Tanzania na duniani kwa ujumla.
Wapo wanamichezo waliojipatia heshima kubwa duniani kutokana na kufanikiwa kupitia mchezo wa ndondi.
Miongoni mwa wanamichezo hao ni nguli Mohammed Ali, Mike ‘Iron’ Tyson, Evender Holyfield, Floyd Mayweather, Manny Pacquiao na wengineo wengi.
Kwa hapa nchini, wapo mabondia waliojitengenezea majina wakiwamo Emmanuel Mlundwa, Habibu Kinyogoli 'Masta' Michael Yombayomba, Stanley Mabesi 'Ninja' Rashid Matumla, Ibrahimu Class 'King Class Mawe'  na wengineo wengi.
Lakini ikumbukwe kuwa ndondi ndio mchezo uliotoa mwanamichezo anayelipwa zaidi duniani kwa sasa ambaye si mwingine bali ni Mayweather, akifuatiwa na mwanasoka raia wa Ureno anayekipiga katika klabu ya Real Madrid ya Hispania, Cristiano Ronaldo.
Anayeshika nafasi ya tatu ni mchezaji wa mpira wa kikapu LeBron James, wakati mwanasoka anayechezea Barcelona ya Hispania, Muargentina Lionel Messi akishika nafasi ya nne, huku wa tano akiwa ni mkali wa mpira wa kikapu, Kobe Bryant.
Pamoja na mafanikio hayo katika ndondi, Tanzania imeonekana kuzidi kulala usingizi wa pono katika suala zima la kuvumbua na kuendeleza vipaji vya mchezo huo kama sehemu ya kutatua tatizo sugu la ajira linaloitesa nchi yetu kwa sasa.
Unapopita huko mitaani, unaweza kukutana na vijana wadogo wakiwa wanafanya mazoezi ya ngumi kwa kutumia vifaa visivyo rasmi ambavyo mwisho wa siku, huishia kuwadumaza badala ya kuwajenga kama walivyotarajiwa.
Hali hiyo imetokana na kukosekana kwa vifaa vya kujifunzia mchezo huo, zikiwamo kumbi na hata wataalam wa kuwapa ujuzi wa kuwawezesha kufikia mafanikioi ya akina Mayweather.
Ni kwa kufahamu hilo, wapo wadau wa ndondi ambao wamekuwa wakijitoa kusaidia vipaji vya ndondi hapa nchini, miongoni mwao akiwa ni Kocha wa Kimataifa wa Ndondi nchini, Rajabu Mhamila ‘Super D’.
Bondia huyo wa zamani, ameshawahi kufanya jitihada kadha wa kadha kuendeleza ndondi hapa nchini, ikiwamo kutoa mafunzo kwa vijana chini ya klabu yake ya Ashanti Boxing Club na kupitia DVD zake zenye mapambano makali yaliyowahi kufanyika hapa nchini na duniani kwa ujumla, yakiwahusisha mabondia nyota.
Katika kuonyesha jinsi anavyoguswa na ndondi, Februari mwaka huu Super D atakuwa na ugeni mkubwa wa bondia Mtanzania anayefanya kazi zake nchini Deer Park, Victoria, Australia, Omari Kimweri ambaye anatua nchini kwa ajili ya kutoa mafunzo kwa wanamasumbwi wa Tanzania.
Akizungumza Dar es salaam jana, Super D anasema kuwa ujio wa Kimweri ni fursa nyingine adimu kwa mabondia wa Tanzania katika kuona ni vipi wanaweza kutimiza ndoto zao za kutoka kimaisha kupitia mchezo huo.
Anasema kuwa Kimweri atatua akiwa na vifaa mbalimbali vya masumbwi ambapo pia atatoa mafunzo na mbinu mpya zinazotumiwa na mabondia wa nje kwa mabondia pamoja na kushuhudia mapambano kadhaa yatakayofanyika kwa kipindi atakachokuwapo hapa nchini.
“Kimweri anakuja akiwa na msafara wa watu kadhaa, akiwamo mwanasoka wa kike, Melanie Gines ambaye ni raia wa Hispania. Akiwa hapa nchini, Melanie atapata fursa ya kukutana na wanasoka wa kike wa hapa , kwani amechezea timu nyingi za Ulaya,  Hispania,” anasema Super D.
Anasema kuwa ujio wa Kimweri umewezeshwa kwa kiasi kikubwa na promota wake, Brian Amatruda ambaye ni miongoni mwa mapromota maarufu nchini kwao Australia, akiwa amekubali kutoa baadhi ya vifaa vya kisasa kutoka Hispania na Marekani kwa ajili ya ziara hiyo.
Super D anasema kuwa Kimweri ambaye ni bingwa wa WBO, atatua nchini akiwa na mikanda yake yote aliyowahi kutwaa, ukiwamo wa ubingwa wa Australia, lengo likiwa ni kuwahamasisha vijana wa kitanzania kujikita zaidi katika ndondi.
“Nimezungumza na Kimweri na ameonyesha kuwa na uchungu wa kuwainua mabondia wa hapa nchini ili waweze kutimiza ndoto zao na anafanya hivyo chini ya mradi wake wa ‘Kimweri Project’ na atakuwa hapa nchini kwa wiki moja,” anasema.
Anasema kuwa ujio wa bondia huyo uliochagizwa na Super D Boxing Coach and Promotion, umelenga kuwahamasiaha mabondia kucheza mara kwa mara ili kupandisha viwango vyao kwani hiyo ndio siri ya mafanikio ya wanamasumbwi wengi duniani.
Mbali ya mafunzo kutoka kwa Kimweri, pia katika ziara zake zote sehemu mbalimbali nchini, kutakuwa na uuzwaji wa DVD za Super D zenye lengo la kutoa mafunzo kupitia mapambano ya mabondia maarufu duniani, akiwamo Floyd Mayweather,Manny Paquaio, Mohamerd Alli, na wa hapa nchini kama Mbwana Matumla, Francis
Miyeyusho, Ibrahimu Class' King Class Mawe' ambaye ni bingwa wa WPBF Africa na wengineo.

Sunday, January 4, 2015

MATOKEO YA FA CUP HAYA HAPA

http://cdn1.theweek.co.uk/sites/theweek/files/styles/theweek_article_main_image/public/fa-cup_1.jpg?itok=vGlcL-92
http://i1.mirror.co.uk/incoming/article3558459.ece/alternates/s2197/Hull-v-Arsenal-FA-Cup-Final.jpg
Mabingwa watetezi wa Kombe la FA Arsenal wapon dimbani kwa sasa Emirates

LIGI Kuu ya England wikiendi hii ilikuwa mapumziko na badala yake imeshuhudiwa mechi za raundi ya tatyu ya michuano mikongwe ya Kombe la FA iliyochezwa tangu Ijumaa na itaendelea hadi Jumanne.
Chini ni baadhi ya matokeo ya michuano hiyo wakati Arsenal ikiwa uwanjani nyumbani wakiongoza bao 1-0 dhidi ya wageni wao Hull City.
Ijumaa: 
Cardiff City     3-1   Colchester United    
Jana:
Charlton Athletic     1-2     Blackburn Rovers  
Rochdale     1-0     Nottingham Forest     
West Bromwich Albion 7-0  Gateshead     
Blyth Spartans     2-3     Birmingham City     
Rotherham United     1-5     AFC Bournemouth     
Huddersfield Town     0-1     Reading     
Tranmere Rovers     2-6     Swansea City     
Bolton Wanderers     1-0     Wigan Athletic
Millwall     3-3     Bradford City    
Derby County     1-0     Southport    

Brentford     0-2     Brighton & Hove Albion  
Fulham     0-0     Wolverhampton Wanderers      
Leicester City     1-0     Newcastle United   
Cambridge United     2-1     Luton Town     

Barnsley     0-2     Middlesbrough    
Preston North End     2-0     Norwich City     

Doncaster Rovers     1-1     Bristol City     
Leo:
Dover Athletic     0-4     Crystal Palace    
Sunderland     1-0     Leeds United    
Queens Park Rangers  0-3     Sheffield United   
Southampton     1-1     Ipswich Town    
Stoke City     3-1     Wrexham    
Manchester City     2-1     Sheffield Wednesday

Aston Villa     1 - 0     Blackpool    
Yeovil Town     0 - 2     Manchester United   
Chelsea     3 - 0     Watford