STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, June 10, 2016

HIVI NDIVYO UEFA EURO CUP 2016 ITAKAVYOPIGWA UFARANSA

https://s3.eu-central-1.amazonaws.com/panadeuro/assets/fb_image-25449d6e90be250b3d2921a7e0e0ac87.png
UNAWEZA kujua kuwa leo Ijumaa usiku ndio vumbi la fainali za Kombe la Mataifa ya Ulaya 'UEFA Euro 2016 litaanza kutimka nchini Ufaransa, lakini huenda hujui makundi na wala rariba nzima ya michuano hiyo ilivyo.
MICHARAZO MITUPU inakuletea kwa ufupi makundi ya michuano hiyo ya Ulaya ambayo ni ya pili kwa ukubwa baada ya Fainali za Kombe la Dunia, ratiba na jinsi siku 30 zitakazotumika kwa timu 24 kuonyeshana kazi hadi mchezo wa fainali wa
kupatikana kwa bingwa wa mwaka huu mnamo Julai 10, ebu chungulia;


MAKUNDI YALIVYO:
KUNDI AUfaransa
Uswisi
Romania
Albania   

KUNDI B

England   
Urusi
Slovakia
Wales   

KUNDI C

Ujerumani
Poland
Ukraine
Ireland ya Kaskazini

KUNDI D

Hispania
Croatia   
Jamhuri ya Czech
Uturuki

KUNDI E

Ubelgiji
Italia
Sweden   
Jamhuri ya Ireland   


KUNDI F

Ureno
Austria   
Hungary   
Iceland   


RATIBA ILIVYO
KUNDI A
Juni 10, 2016
Ufaransa v Romania- St-Denis

Juni 11, 2016

Albania v Uswisi- Lens

Juni 15, 2016

Romania v Uswisi- Paris
Ufaransa v Albania- Marseille

Juni 19, 2016

Romania v Albania-  Lyon
Uswisi v Ufaransa- Lille

KUNDI B
Juni 11, 2016

Wales v Slovakia- Bordeaux
England v Urusi- Marseille

Juni 15, 2916

Urusi v Slovakia- Lille
England v Wales- Lens

Juni 20, 2016

Urusi v Wales- Toulouse
Slovakia v England- St-Etienne

Kundi C
Juni 12, 2016

Poland v Ireland ya Kaskazini- Nice
Ujerumani v  Ukraine- Lille

Juni 16, 2016

Ukraine vIreland ya Kaskazini- Lyon
Ujerumani v Poland - St-Denis

Juni 21, 2016

Ukraine v Poland- Marseille
Ireland ya Kaskazini v Ujerumani- Paris

Kundi D
Juni 12, 2016

Uturuki v Croatia- Paris

Juni 13, 2016

Hispania v Jamhuri ya Czech- Toulouse

Juni 17, 2016

Jamhuri ya Czech v Croatia-  St-Etienne
Hispania  v Uturuki- Nice

Juni 21, 2016

Jamhuri ya Czech v Uturuki- Lens
Croatia v Hispania- Bordeaux

Kundi E
Juni 13, 2016

Jamhuri ya Ireland v Sweden- St-Denis
Ubelgiji v Italia- Lyon

Juni 17, 2016

Italia v Sweden- Toulouse
Ubelgiji v Jamhuri ya Ireland- Bordeaux

Juni 22, 2016Italia v Jamhuri ya Ireland- Lille
Sweden v Ubelgiji- Nice

Kundi F
Juni 14, 2016Austria v Hungary- Bordeaux
Ureno  v Iceland- St-Etienne

Juni 18, 2016Iceland v Hungary- Marseille
Ureno v Austria- Paris

Juni 22, 2016Iceland v Austria- St-Denis
Hungary v Ureno- Lyon

Mtoano 16 BoraJuni 25, 2016:Mechi 1: Mshindi wa Pili Kundi A v Mshindi wa Pili Kundi C- St-Etienne
Mechi 2: Mshindi Kundi D vMshindi wa Tatu B/E/F- Lens
Mechi 3: Mshindi Kundi B v Mshindi wa Tatu A/C/D- Paris

Juni 26, 2016:
Mechi 4: Mshindi Kundi F v Mshindi wa Pili Kundi E- Toulouse
Mechi 5: Mshindi Kundi C v Mshindi wa Tatu A/B/F - Lille

 

Juni 27, 2016:Mechi 6: Mshindi Kundi E v Mshindi wa Pili Kundi D- St-Denis
Mechi 7: Mshindi Kundi A v Mshindi wa Tatu C/D/E- Lyon
Mechi 8: Mshindi wa Pili Kundi B v Mshindi wa Pili Kundi F- Nice


Robo Fainali:Juni 30, 2016
RF1-Mshindi Mechi 1 v Mshindi Mechi 2- Marseille
 

Julai 01, 2016
RF2-Mshindi Mechi 3 v Mshindi Mechi 4-  Lille

Julai 2, 2016
RF3-Mshindi Mechi 5 v Mshindi Mechi 4- Bordeaux
Julai 3, 2016
RF4-Mshindi Mechi 7 v Mshindi Mechi 8- St-Denis
Nusu Fainali:

Julai 6, 2016
NF1-Mshindi QF1 v Mshindi QF2- Lyon
Julai 7, 2016
NF2-Mshindi QF3 v Mshindi QF4- Marseille
Fainali:
Julai 10, 2016
Mshindi NF1 v Mshindi NF2- St-Denis

Hizi ndizo rekodi za Mbeya City msimu wa 2015-2016

IMG_7987
Kikosi cha Mbeya City cha msimu uliopita
NA DISMAS TENI, MBEYA CITY
BAADA ya kumalizika kwa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara  2015/16  na Mbeya City fc kumaliza ikiwa kwenye nafasi ya 8 baada ya kuweka kibindoni jumla ya Pointi 35,  kufuatia  mabao  32  ya kufunga na kufungwa 34 kwenye michezo 30 ya msimu mzima.
Hapa chini ni rekodi kadhaa kutoka benchi la ufundi zimetoka  na kati ya hizo baadhi  zinaonyesha kuwa, magolikipa watatu wa kikosi cha kwanza, Juma Kaseja, Haningtony Kalyesubula na Geoffrey Mwalyego  waliokuwa wakisimama langoni  kwa kupishana kwenye michezo tofauti wamewajibika kwa asilimia 33.33 katika ushindi, sare na hata kupoteza mchezo katika mechi zote 30 za msimu.
Katika rekodi hizo zinaonyesha,  Juma  Kaseja  alicheza michezo 17 na kuruhusu kufungwa mabao 20, Haningtony Kalyesubula alicheza michezo 13 na kufungwa mabao 14 wakati Geoffrey Mwalyego yeye hakupata nafasi ya kucheza mchezo hata mmoja.
Wakati Mlinzi Hassan Mwasapili akiweka rekodi ya kucheza mechi nyingi zaidi kikosini kuliko mchezaji yoyote kwa kucheza mechi 28 na kukosa 2  pia kufunga mabao 2  katika mechi zote 30, Mlinzi wa kati Haruna Shamte amemaliza akiwa na rekodi ya kupata kadi nyingi zaidi kuliko mchezaji yoyote akiwa na  jumla ya kadi 8, kati ya hizo 6 zikiwa za njano na 2 nyekundu.
Kiungo Rafael Daud ndiye kinara wa mabao kikosini akimaliza msimu kwa kufunga mabao 6,na kuifikia rekodi ya Mwegane Yeya aliyoiweka 2013/14,  ingawa  pia  ukurasa wake ukionyesha kuwa alipata kadi 2 za njano.
Mlinzi na kiungo Aboubakary Shaaban akiweka rekodi ya kucheza ligi kuu akiwa na umri mdogo zaidi kuliko wachezaji wote wa City, akicheza mechi yake ya kwanza dhidi ya Coastal Union jijini Tanga akiwa na umri wa miaka 17 na siku 129.
David Kabole alicheza mechi 1 na kufunga bao 1 hii ilikuwa kwenye mchezo dhidi ya JKT Ruvu ambao City ilipata ushindi wa 3-0 lakini baada ya hapo hakuonekana tena dimbani  hii ni baada ya kiwango chake kuporomoka kwa kasi na kujikuta akitolewa kwa mkopo kwenda Fc Kimondo na kumpisha Salvatory Nkulula  aliyeingia kikosini na kufanikiwa kucheza  mechi 6 akifunga mabao 4.
Rekodi pia  zinaonyesha 2015/16 ndiyo msimu  pekee ambao City imekuwa chini ya makocha watatu, ikianza na Juma Mwambusi  aliyeondoka  baadae, na nafasi yake kushikwa na Abdul Mingange  ambaye  alidumu kikosini kwa miezi 3, kufuatia matatizo ya kifamilia Mingane  aliachia nafasi hiyo na kumpisha kocha wa sasa Kinnah Phiri.
Licha ya kushinda 4-0 dhidi ya Coastal Union kwenye mchezo wa duru ya pili April 4 kwenye uwanja wa Sokoine jijini hapa, ushindi mkubwa wa City msimu huu ulikuwa ni ule wa bao 5-1 dhidi ya Toto Africans katika mechi ya kukata nashoka iliyopigwa jijini Mbeya, huku kipiko kikali kikiwa ni kile cha mabao 4-1 ilichokipa kutoka kwa Ndanda Fc huko Nangwanda Sijaona.
Katika nyota walisajiliwa wakati wa dirisha dogo Haruna Moshi  ameonekan kung’ara zaidi akifanikiwa kumaliza msimu akiwa amefunga mabao 3, sambamba na Ramadhani Chombo,Abdalah Juma na Ditram Nchimbi  waliofunga 2 kila mmoja ingawa Abdalah Juma hakumudu kuitumikia timu kwa kiwango kutokana na majereha ya mara kwa mara.
2015/16 ndiyo msimu pekee ambao City imeshinda mechi mbili pekee ugenini, 2-1 dhidi ya JKT Ruvu, Karume Dar na 1-0 dhidi ya Mgambo JKT, Mkwakwani, Tanga,  huku pia ikivuna pointi 3 za sare ugenini  dhidi ya Toto Africans, Coastal Union na Mwadui Fc.

Kumekucha UEFA Euro Cup 2016! Nani kucheka?

https://i.ytimg.com/vi/cpdvLwDjjms/maxresdefault.jpg
PAZIA la michuano ya Fainali za Kombe la Ulaya 'UEFA Euro 2016' linafunguliwa rasmi leo kwa pambano moja tu la wenyeji Ufaransa dhidi ya Romania.
Pambano hilo linaashiria kuanza kwa vita ya kuwania taji la michuano hiyo ambalo kwa misimu miwili mfululizo limekuwa likishikiliwa na Hispania waliotwaa katika fainali za mwaka 2008 na 2012.
Ufaransa waliowahi kunyakua mara mbili taji hilo mwaka 1984 wakiwa wenyeji na 2000 nchini Ubelgiji/ Uholanzi ikiwa imetoka kutwaa Kombe la Dunia mwaka 1998 wakiwa pia wenyeji, inapewa nafasi kubwa ya kufanya kweli safari hii wakiwa kama wenyeji, lakini ni kutokana na kuwa na kikosi kinachoundwa na wachezaji mahiri na wajanja wa soka.
Hii ni mara ya tatu kwa nchi hiyo kuandaa fainali hizo baada ya ile ya kwanza mwaka 1960 na 1984, ambako kucheza kwenye viwanja vyake vya nyumbani na mashabiki watakaowatia nguvu na uimara wa kikosi chake ni dhahiri wakilikosa taji Ufaransa itabidi wajutue kwelikweli.
Pambano hili litakalopigwa majira ya saa 4;00 usiku kwa saa za Afrika Mashariki, litatanguliwa na mashamsham ya uzinduzi kabla ya wanaume 22 kuonyeshana kazi kwenye dimba la Stade de France, Saint-Denis likihukumiwa na Mwamuzi Viktor Kassai kutoka Hungary.
pambano hilo la Kundi A linatarajiwa kuwa kivutio kikubwa kutokana na mafanikio makubwa ya vijana wa Ufaransa katika klabu zao kwenye Ligi Kuu tofauti za Ulaya akiwamo Paul Pogba ambaye kwa sasa amekuwa gumzo kutokana na kuwindwa na klabu kubwa duniani baada ya kutwaa mataji manne mfululizo ya Ligi ya Ufaransa.
Hata hivyo kama wenyeji wanapaswa kuwa makini dhidi ya Romania wanaoumana nao leo na hata washiriki wengine wa kundi hilo zikiwamo Uswisi na Albania.
Kipute cha michuano hiyo kitaendelea kesho Jumamosi kwa mechi tatu, moja ikiwa ya kundi A kati ya Uswisi na Albania itakayopigwa mapema saa 10 jioni na mbili za Kundi B.
Mechi hizo zitazikitanisha Wales dhidi ya Slovakia majira ya saa 1 jioni kabla ya England kuvaana na Russia saa 4 usiku, mechi zinazosubiriwa kwa hamu kubwa na mashabiki wa soka duniani wakiwamo wa Tanzania.

Ratiba ilivyo kwa leo na kesho ikiwamo ile ya Kombe la Copa America ni hivi;
Leo Ijumaa
8:30 Usiku– Uruguay v Venezuela -Copa
11:00 Alfajiri– Mexico v Jamaica- Copa
4:00 Usiku– France vs. Romania-Uero

Kesho Jumamosi
8:00 Usiku– Chile v Bolivia-Copa
10:30 Alfajiri– Argentina v Panama-Copa
10:00 Jioni– Albania v Switzerland-Euro
1:00 Usiku– Wales    v. Slovakia-Euro
4:00 Usiku– England v Russia-Euro

Thursday, June 9, 2016

Liverpool yaingia vitani kumwania Jamie Vardy

https://metrouk2.files.wordpress.com/2015/04/football-leicester-citys-jamie-vardy-celebrates-after-scoring-their-first-goal.jpg
Jamie Vardy
LIVERPOOL ipo tayari kuingia kwenye vita ya kumwania straika wa Mabingwa wa England, Jamie Vardy.
Kwa mujibu wa Daily Star, The Kop imekuwa ikimwania mkali huyo wa mabao mwenye umri wa miaka 29 kwa misimu miwili sasa.
Kocha wa Liverpool, Jurgen Klopp, tayari ndani ya kikosi chake kina wanaume wa shoka katika safu yake ya ushambuliaji ikiongozwa na Daniel Sturridge, Divock Origi, Christian Benteke na Danny Ings.
Hata hivyo inaelezwa kuwa Vijogoo hao wa Anfield wapo tayari kumuuza mmoja wa mastraika hao, huku Benteke akihusishwa zaidi ili kumpisha Vardy, kwa vile ni kama hayupo kwenye mipango ya Kocha Klopp.
Klabu ya Arsenal imekuwa nayo ikimsaka straika huyo, ila mwenyewe amedaiwa hajaamua lolote kwa sasa mpaka baada ya michuano ya fainali za Euro 2016 inayoanza kesho Ijumaa huko Ufaransa akiiwakilisha nchi yake ya England.

Luke Shaw amtumia ujumbe Mourinho tayari kwa kazi OT

http://static.independent.co.uk/s3fs-public/thumbnails/image/2014/10/28/08/Luke-Shaw-2.jpgYUPO tayari kwa kazi, asikuambie mtu. Beki mahiri  wa pembeni wa Manchester United, Luke Shaw amemtumia ujumbe Kocha wake mpya, Jose Mourinho akisema kwamba yupo fiti kwa ajili ya maandalizi ya msimu mpya.
Nyota huyo aliyeshindwa kuitumia Mashetani Wekundu kwa msimu mzima kutokana na kuvunjia mguu mara mbili wakati akiipigania klabu yake katika Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya PSV Eindhoven, alitumia akaunti yake ya instagram kumfikishia ujumbe kocha wake.
"Nipo tayari" alisema Shaw.
Siku baada ya siku naendelea vema na nazidi kuimarika," aliongeza beki huyo wa zamani wa klabu ya Southampton.

Maskini Agger! Aamua kutundika daluga bila kupenda

http://i1.manchestereveningnews.co.uk/incoming/article660491.ece/ALTERNATES/s615/C_71_article_1584808_image_list_image_list_item_0_image.jpgHANA namna. Maumivu ambayo yamekuwa yakimuandama mara kwa mara nyota wa zamani wa Liverpool, Daniel Agger yamemfanya atundike daluga. Agger ametangaza kustaafu soka akiwa  ndio kwanza ana umri wa miaka 31 tu. Beki huyo amekuwa akisumbuliwa kwa kipindi kirefu cha soka lake la majeruhi aliandika katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa twitter kuelezea uamuzi wake huo. Agger aliandika katika twitter akiwashukuru wale wote waliomuunga mkono katika kipindi chote na kuongeza japo ni uamuzi mgumu, lakini anadhani ni sahihi kwa afya yake.
Beki huyo wa kimataifa wa Denmark aliyeondoka Liverpool mwaka 2014 baada ya kuitumikia kwa miaka nane na kurejea katika klabu yake ya utotoni ya Brondby, amewahi kuichezea nchi hiyo mechi 75. Mkali huyo ameingia katika orodha ya nyota waliowahi kustaafu soka mapema kabla ya wakati wao kwa sababu mbalimbali ikiwamo majeruhi yasiyoisha.

Ronaldo, Messi hawashikiki kwa mkwanja mnene duniani

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgY8PvBrWzFoQIsf0lo44zBa1a5LOgQGVqaoJ90UrwDJJgXi6t_8HUQACiYEVoOsmc7yvAiWq9bU1MxejhpuojP57RhYySRr985IDkhFY-SDoKpnHzRkpsJcPrNdqi1JLmYe4aRX5wQzxo/s1600/lionel_messi_vs_cristiano_ronaldo.jpgWANANUKA pesa. Labda ubishe tu, lakini imefichuliwa kuwa nyota wanaochuana kwa sasa duniani, Lionel Messi na Cristiano Ronaldo ndio wanamichezo wanaolipwa zaidi duniani.
Kwa mujibu wa Jarida maarufu la Forbes la Marekani limewataja nyota hao kuwa vinara duniani kwa kuvuta mkwanja wa maana wakiwazidi wanamichezo wengine.
Nyota wa Real Madrid, Ronaldo ndiye anayeongoza orodha hiyo kwa kukunja kitita cha Pauni Milioni 60.9 katika kipindi cha miezi 12 iliyopita, huku nyota wa Barcelona Messi akijikusanyia kiasi cha Pauni Milioni 56.3.
Mkali wa mchezo wa Gofu, Tiger Woods na bondia Floyd Mayweather ndio waliokuwa wakitawala orodha hizo kwa muongo mmoja uliopita, lakini Woods akiandamwa na majeruhi na kushuka kiwango na Mayweather akiwa amestaafu Ronaldo na Messi wamepanda na kuongoza orodha hiyo kilaini.
Ronaldo anakuwa mwanamichezo wa pili kutoka katika timu baada ya nguli wa mpira wa kikapu Michael Jordan kuongoza orodha hizo toka jarida hilo lilipoanza kukokotoa vipato vya nyota vya wanamichezo mbalimbali mwaka 1990.
Nyota wengine waliopo katika orodha hiyo ni nyota wa mpira wa kikapu Lebron James anayeshika nafasi ya tatu kwa kuingiza Pauni Milioni 53.4, nyota wa tenisi Roger Federer anashika nafasi ya nne akiingiza Pauni Milioni 46.9 na mkali mwingine wa Kikapu, Kevin Durant anakamilisha Tano Bora kwa kuingiza Pauni Milioni 38.6.
Mastraika matata kwa kufumania nyavu Neymar, Zlatan Ibrahimovic na Gareth Bale ndio wachezaji soka wengine pekee waliopo katika orodha hiyo wakiwa katika nafasi ya 21, 22 na 25 kwa kuingiza kiasi cha Pauni Milioni 25.8, 25.7 na 24.7.

Real Madrid yawinda rekodi mpya kwa Pogba

http://static.independent.co.uk/s3fs-public/thumbnails/image/2015/08/25/20/pg-64-pogba-1-getty.jpg
Paul Pogba anayeingia rada za Real Madrid
MWENDO wa noti tu. Klabu ya Real Madrid ipo tayari kumwaga mkwanja wa nguvu ili kuipiku Manchester United inayotaka kumrejesha kikosini, Paul Pogba anayekipiga Juventus.
Klabu hiyo imedaiwa ipo tayari kutoa Pauni Milioni 94 ili kunasa saini ya Pobga anayewindwa na klabu yake ya zamani Man United walio tayari kuvunja benki na kumwaga Pauni Milioni 78.
Kwa mujibu wa gazeti maarufu la michezo la Gazzetta dello Sport la Italia limesema kuwa, Real Madrid imepania kumnasa kiungo huyo fundi kutoka Ufaransa, licha ya kwamba katika mbio hizo pia Matajiri wa Manchester City wapinzani wakuu wa Man United nao wanammendea kimyakimya.
Iwapo Rela itafanikiwa kumnasa Pogba kwa kiwango hicho cha fedha itakuwa imevunja rekodi inayoshikilia kwa sasa ya kumnasa Gareth Bale misimu mizili iliyopita ilipomwaga kiasi cha Pauni Milioni 80.
Gazeti hilo limefichua kuwa, Mkurugenzi wa Juventus Giuseppe 'Beppe' Marotta wiki ijayo anatarajiwa kutua Hisapnia kwa ajili ya mazungumzo ya uhamisho wa Alvaro Morata, lakini pia suala la Pobga litagusiwa.
Mashetani Wekundu pia walikuwa wakimnyatia Moratta, lakini inaonekana wazi Jose Mourinho atachemsha mbele ya mabosi wake wa zamani Real Madrid.

http://img.kiosko.net/2016/06/09/it/gazzetta_sport.750.jpg
gazeti lililodokeza mipango ya Real kutaka kuvunja rekodi ya kumnyakua Pogba

Rodriguez azigonganisha Manchester City, United

https://metrouk2.files.wordpress.com/2014/06/875x10001.jpg
James Rodriguez

KLABU ya Manchester City imeingia kwenye vita dhidi ya mahasimu wake, Manchester United katika mbio za kumwania nyota wa Real Madrid, James Rodriguez.
Nyota huyo wa kimataifa wa Colombia amekuwa akiwindwa pia na mabingwa wa Ufaransa, PSG, lakini duru la kispoti zinadokeza kuwa, Rodriguez ambaye kusalia kwake Santiago Bernabeu ni majaliwa anawindwa na mabingwa hao wa zamani wa England.

City chini ya kocha mpya, Pep Guardiola imevutiwa na Mfungaji Bora huyo wa Kombe la Dunia 2014 na kwamba wapo tayari kumwaga kitita ili kumnyakua.
Klabu za PSG na Bayern Munich iliyo chini ya Kocha mpya, Carlo Ancelotti aliyewahi kumnoa Rodriguez wakati akikinoa kikosi cha Blancos, nao wanatajwa kumnyemelea mkali huyo ambaye amekuwa hana raha Real Madrid kutokana na kuishia benchini.
Rodriguez ambaye ni nahodha wa Colombia kwa sasa yupo kwenye vita ya kuisaidia timu yake kufanya vema katika michuano ya Copa America 2016 inayochezwa Marekani.

Paul Pogba awaota kina Pele, Diego Euro 2016 watamkoma!

http://bolavip.cdnfsn.com/img/rankings/x/n1406834042.jpg
Paul Pogba
MBONA mtamkoma. Kiungo nyota wa Juventus aliyewahi kukipiga kwa Mashetani Wekundu, Manchester United, Paul Pogba amefunguka kwa kudai kuwa anataka akumbukwe kwa soka lake kama ilivyokuwa kwa kina Diego Maradona wa Argentina na Pele wa Brazil.
Pogba ambaye atakuwa na jukumu la kuisaidia nchi yake kwenye fainali za Kombe la Mataifa ya Ulaya (Uefa Euro 2016) inayofanyika kwao Ufaransa, alisema kuwa,  amepania kufikia malengo yake hayo kwa kujituma na kuhakikisha kila siku anaimarika.
Kiungo huyo aliyeiwezesha Juventus kunyakua mataji manne ya Ligi Kuu ya Serie A na kucheza fainali za Ligi ya Mabingwa Ulaya mwaka jana, amekuwa akizidi kuimarika na kuwa mmoja ya nyota wanaomezewa mate kwa ubora wake wa soka.
Pogba aliondoka United kuelekea kwa Kibibi Kizee cha Turin mwaka 2012 na akihojiwa na runinga ya ESPN, Pogba alisema  kwasasa hadhani kama ameshafanya lolote la maana katika soka kwa vile bado kuna mataji mengi hajawahi kushinda ikiwamo Ligi ya Mabingwa Ulaya, Kombe la Dunia na hata Euro.
Hivyo amesema kuwa atapambana kiume katika ushiriki wake wa soka ili kuona anafika kule ambako kina Diego na Pele walifikia kiasi cha kubaki kuwa gumzo licha ya kustaafu kitambo na kuibuka kwa nyota mbalimbali duniani kwa sasa.

Adidas yaiomba radhi Colombia kwa kuchapia tangazo

Tangazo lililozua gumzo kwenye mitandao ya kijamii hasa twitter ambapo Adidas ilishambuliwa kabla ya kuliondoa na kuomba radhi
WAUNGWANA. Kampuni ya vifaa vya michezo ya Adidas imeonyesha uungwana kwa kuomba radhi kwa kosa la kuliandika vibaya jina la Colombia katika matangazo yake yanayohusu jezi mpya wanazotumia timu ya taifa ya nchi hiyo katika michuano ya Copa America 2016.
Tangazo hilo ambalo linawaonyesha wachezaji wa Colombia wakiwa katika jezi nyeupe liliondolewa baada ya mitandao ya kijamii kushambulia kwa kwa kuliandika vibaya jina la nchi hiyo ambapo badala ya kuandika Colombia waliandika Columbia.
Katika taarifa yake kampuni hiyo yenye makao yake makuu huko Portland, Oregon imedai kuwa wanathamini ushirikiano wao na Shirikisho la Soka la Colombia na kuwaomba radhi kwa makosa hay
o yaliyofanyika. Kampuni hiyo imekuwa ikitengeneza sare za Colombia tangu mwaka 2011.

Neymar Jr matatani kwa udanganyifu, kuburuzwa kortini


MSAMBWENI. Straika nyota wa Brazili anayeichezea klabu ya Barcelona, Neymar Jr, ameingia matatani baada ya Waendesha Mashitaka nchini Hispania kutaka ashitakiwe kwa kosa la udanganyifu.
Waendesha Mashitaka hao kutoka Mahakama ya Juu ya Makosa ya Jinai Hispania, wanamtuhumu Neymar na baba yake kuficha ukweli wa thamani halisi ya uhamisho wake kutoka Santos kwenda Barcelona.
Barcelona ilitangaza kumnunua Neymar kwa kitita cha Euro Milioni 57 mwaka 2013, huku wazazi wake, Neymar da Silva Santos na Nadine Goncalves sa Silva Santos wakivuta mkwanja wa haja wa Euro Milioni 40 na klabu yake ya zamani Santos wakipata Euro Milioni 17.
Lakini waendesha mashtaka hao wamesema ada ya uhamisho ya nyota huyo ilifikia kitita cha Euro Milioni 83, ingawa pande zote mbili zimekanusha kufanya jambo lolote baya kwenye uhamisho huo.

Tattoo zamponza msela, apasuliwa mara 25 kuzifuta usoni

Akianza matibabu
zilipokuwa zikiondolewa kwa operesheni maalum
Picha tofauti kuelekea kuziondoa tattoo zake usoni
http://www.smh.com.au/content/dam/images/1/m/u/g/a/image.related.articleLeadwide.620x349.1mug6.png/1320183665650.jpg
Alivyo sasa bila Tattoo
AMA kweli ujanja mwingi mbele kiza. Hebu soma kisanga kilichompata huyu jamaa ambaye alikuwa kinara wa kundi moja la wakora nchini Ujerumani.
Msela huyo kwa kutaka kujifanya anaenda na wakati alijichora tattoo kadhaa mwilini mwake, lakini mwishoni wa yote amejikuta akipata maumivu na kutoboka kiasi kikubwa cha fedha baada ya kufanyiwa upasuaji mara 25 ili kuzifuta tattoo hizo za usoni.
Inaelezwa jamaa huyo, Bryon Widner alitumia kiasi cha Pauni 20, 233 ambazo ni kama Shs. 63.9 Milioni, huku akisimulia namna alivyopata maumivu makali kwa ajili ya kusafisha uso wake kuondoa tattoo hizo.
Widner alisema kuwa, alipitia maumivu makali sana ili kusafisha sura yake na kuzitoa tattoo hizo na alitumia muda wa miezi 16 katika operesheni hizo 25 ili kuweka sawa sura yake.
Upasuaji huo wa kuondoa tattoo hizo za usoni kati ya tattoo kibao alizojichora mkora huyo ulifanywa na Dk Bruce Shack wa Vanderbilt University Medical Center kilichopo mjini Nashville.
Kitu cha kufutia ni kwamba licha ya kadhia zote hizo, kwa sasa Widner amesafishika sura yake akiwa hana kovu lolote usoni, jambo linalompa faraja.

Wednesday, June 8, 2016

Man City kumekucha! Yaingia vita ya kumwania Aubameyang

https://i.guim.co.uk/img/media/aa83556e4ff4a53c273d8fc73c14e1e6bd7105d7/0_80_3000_1800/master/3000.jpg?w=620&q=85&auto=format&sharp=10&s=53bd60055f2d7d1fab6d5d30c9526dd8KLABU ya Manchester City inadaiwa ipo mbioni kuingia kwenye orodha ya timu zinazomwania straika wa Borussia Dortmund ma Mchezaji Bora wa Afrika 2015, Pierre-Emerick Aubameyang.
City wana matumaini ya kumsana nyota huyo wa kimataifa wa Gabon mwenye umri wa miaka 26 katika kipindi hiki cha kiangazi. Aubameyang anatajwa kuwa mmoja kati ya washambuliaji bora Ulaya baada ya kuonyesha kiwango kikubwa Dortmund akifunga mabao 39 katika mashindano yote msimu uliopita.
Meneja mpya wa klabu hiyo, Pep Guardiola anafahamu vyema kipaji cha Aubameyang na ameona kuwa anaweza kumfaa katika mipango yake ya baadae. City wanadaiwa kuwa tayari kumsaidia Guardiola katika usajili kwa kujiandaa kuvunja rekodi ya usajili kwa kumleta nyota huyo Etihad.

Leseni za klabu zimeanza kutolewa na TFF, mshindwe ninyi

http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2016/04/Rais-wa-Shirikisho-la-Mpira-wa-Miguu-Jamal-Malinzi-akioneshwa-kukerwa-na-waamuzi-kuuza-mechi.jpg
Rais wa TFF, Malinzi
NA ALFRED LUCAS
SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) limeanza kutoa fomu za Leseni za Klabu (Club Licensing) za Ligi ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) na zile za Ligi Daraja la Kwanza ya StarTimes.
Klabu hizo zitatumiwa fomu hizo na kutakiwa kuzijaza na kuzirejesha kabla ya Juni 19, mwaka huu ikiwa ni siku 10 mara baada ya Bodi ya Ligi ya TFF (TPLB) kuwatuamia fomu hizo. Klabu itakayojaza fomu hizo kwa wakati ndiyo ambayo maombi yake ya leseni yatashughulikiwa mapema.
Tayari TFF imeteua Kamati ya Leseni ya Klabu (Club Licensing Committee) ambayo ndiyo yenye jukumu la kupitia maombi ya leseni kwa klabu za Ligi Kuu na Ligi Daraja la Kwanza na kutoa uamuzi wa kuzikubali au kuzikataa kwa kuzingatia Kanuni ya Leseni ya Klabu.
Wajumbe walioteuliwa kwenye Kamati hiyo inayoundwa kwa mara ya kwanza ni Wakili Lloyd Nchunga (Mwenyekiti), Wakili Emmanuel Matondo (Makamu Mwenyekiti), David Kivembele, Hamisi Kissiwa na Prof. Mshindo Msolla.
Klabu zinatakiwa kuchukua fomu za maombi TFF ambapo baada ya kuzirejesha zitafanyiwa kazi ambapo zile zitakazokuwa zimekidhi matakwa ya Kanuni husika zitapatiwa leseni husika ili zishiriki michuano ya Ligi Kuu ya Vodacom na Ligi Daraja la Kwanza ya StarTimes kwa msimu wa 2016/2017.
Kwa klabu ambazo zitashindwa kukidhi matakwa ya leseni yanayolenga kuhakikisha mpira wa miguu unaendeshwa kwa weledi na kupiga vita upangaji matokeo katika maeneo matano ya wachezaji (sporting), viwanja (infrastructure), utawala (administrative and personnel), umiliki wa klabu (ownership) na fedha (financial), hazitapa leseni hivyo kutokuwa na sifa ya kushiriki ligi.Klabu ambazo zitanyimwa leseni na kutoridhika na uamuzi huo, zitakuwa na fursa ya kukata rufani kwenye Kamati ya Rufani ya Nidhamu ya TFF. Kwa mujibu wa Ibara ya 5(3) ya Kanuni ya Leseni ya Klabu ya TFF, Kamati hiyo ndiyo itakayosikiliza rufani zinazopinga uamuzi wa Kamati ya Leseni ya TFF.

Serengeti Boys kambini kuisubiri Shelisheli

http://www.eatv.tv/sites/default/files/styles/detailpageimg/public/2016/03/21/serengeti%20boys.jpg?itok=F-SUOdMWNA ALFRED LUCAS
TIMU ya soka ya taifa ya vijana U17 'Serengeti Boys' inataingia kambini Juni 13, 2016 kujiandaa na mchezo wa kufuzu fainali za kuwania Kombe la Mataifa ya Afrika dhidi ya vijana wenzao wa Shelisheli utakaofanyika Juni 25, mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam.
Mchezo wa marudiano kati ya Serengeti Boys na Shelisheli utachezwa Julai 2, 2016 huko Shelisheli.
Katika kuajindaa na mchezo huo, Serengeti Boys ilifanya ziara India ambako walishiriki mashindano ya vijana ya Kimataifa yanayotambuliwa na FIFA (AIFF International Youth Tournament 2016) kabla ya kurudi na rekodi ya kupigiwa mfano si tu katika Tanzania na kwa nchi za Afrika Mashariki.
Kadhalika Serengeti Boys ilicheza mfululizo michezo saba  ya kimataifa bila kufungwa dhidi ya Misri (2), India, Korea Kusini, Malaysia na Marekani (USA). Kabla ya hapo timu hiyo ilicheza michezo kadhaa ya ndani na timu za chini ya umri wa miaka 20 bila kupoteza hata mchezo mmoja.
Katika mashindano ya AIFF, timu hiyo pekee kutoka Afrika na ambayo ilikua kipenzi cha mashabiki katika jiji la Goha ilicheza na timu ambazo ziko juu katika hatua za juu katika mtoano wa kuwania kushiriki Kombe la Dunia kupitia mabara yao yaani CONCACAF (USA) na AFC (India, Korea na Malaysia).
Haishangazi nchi nyingi za Ulaya, Asia na Marekani zimeulizia uwezekano wa timu hii kutembelea nchi zao kwa michezo ya kirafiki.
Awali timu ya Serengeti Boys ilipewa nafasi ndogo ya kufanya vizuri kwa sababu ya rekodi zilizokuwa zinaiweka Tanzania katika viwango vya chini katika umri huo kwa nchi za Afrika Magharibi na Kaskazini zilikuwa juu zaidi na vilevile ukweli wa kwamba timu kama USA, Korea, Malasyia na India zilikuwa na bajeti kubwa iliyogharamiwa na Serikali zao na walikuwa na vifaa vya kila namna kiasi cha kuomba magari kwa ajili ya vifaa vya mazoezi na mechi.
Serengeti Boys ilimaliza Mashindano ya AIFF katika nafasi ya tatu kwa kuifunga Malaysia mabao 3-0. Serengeti Boys na Bingwa Korea hawakupoteza mchezo hata mmoja na awali walipokutana walitoka sare ya 2-2.

Rais Obama ayakosa mazishi ya Muhammad Ali

http://cdn-mf1.heartyhosting.com/sites/mensfitness.com/files/styles/photo_gallery_full/public/ali_rotator.jpg?itok=CnLNStFo
Muhammad Ali enzi za uhai wake
http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2016/06/382dab0f0ef23504d829de029e0e543f-702x336.jpgMWILI wa bingwa mara wa tatu wa Dunia kwa uzito wa juu, Muhammad Ali unatarajiwa kuzikwa keshokutwa Ijumaa, lakini cha kusikitisha ni kwamba hatazikwa na Rais wa Marekani, Barack Obama.
Muingiliano wa mazishi hao wa shujaa huyo na mwanaharakati wa kuwatetea watu weusi kupitia ngumi, kiasi kwamba leo Marekani inaongozwa na Rais mwenye asili ya Afrika na yale ya mahafali za binti wa Obama ndio sababu ya Obama kukosa mazishi hao.
Viongozi kadhaa kutoka sehemu mbalimbali duniani watakuwa miongoni mwa maelfu ya waombolezaji watakaohudhuria mazishi hayo huko Louisville, Kentucky ambako Ali alizaliwa mwaka 1942.
Ikulu ya Marekani imesema kuwa Obama na mkewe Michelle wanatarajiwa kuwa katika mahafali ya binti yao Malia huko Washington, DC.
Ali alifariki dunia wiki iliyopita hospitalini huko Phoenix, Arizona akiwa na umri wa miaka 74.
Hata hivyo familia ya Obama inatarajia kutuma barua kwa familia ya Ali ambayo itawasilishwa na mshauri mwandamizi wa Ikulu Valerie Jarrett ambaye anamfahamu Ali.
Msemaji wa familia ya Ali, Bob Gunnell amesema Obama alizungumza na mjane wa Ali, Lonnie katika simu kumpa pole kwa kifo hicho cha mumewe. Miongoni mwa viongozi watakaohudhuria mazishi hayo ni pamoja na Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan na Mfalme Abdullah wa Jordan.

Jose Mourinho aanza mambo Man United

http://static.independent.co.uk/s3fs-public/styles/article_large/public/thumbnails/image/2016/06/08/13/eric-bailly-2.jpg
Eric Bailly
MBONA mtamkoma. Kocha Mkuu wa Manchester United, Jose Mourinho ameanza makeke yake baada ya klabu yake kumnasa beki wa Villarreal, Eric Bailly.
Nyota huyo wa kimataifa wa Ivory Coast mwenye umri wa miaka 22 amejiunga na United kwa ada ya Pauni Milioni 30 na kupewa mkataba wa miaka minne.
Akihojiwa Bailly amesema ndoto zake zimetimia za kujiunga na United na kucheza soka katika kiwango cha juu kama siku zote alivyotaka iwe.
Kocha Mourinho amesema Bailly ana nafasi kubwa ya kuja kuwa mmoja wa wachezaji bora duniani.
Bailly alijiunga na Villarreal kwa kitita cha Pauni Milioni 4.4 Januari mwaka 2015 na kucheza katika kila mechi wakati Ivory Coast ikishinda taji la Mataifa ya Afrika wiki chache baadae.
Huo unakuwa usajili wa kwanza wa Mourinho toka atue Old Trafford huku pia wakitajwa kumwania pia mshambuliaji wa Paris Saint-Germain, Zlatan Ibrahimovic.

Malinzi amlilia Stephen Keshi aliyefariki leo

http://stargist.com/wp-content/uploads/2014/05/Stephen-Keshi-Stargist.jpg
Keshi enzi za uhai wake
NAHODHA na Kocha wa zamani wa Nigeria, Stephen Keshi amefariki dunia ghafla leo Jumatano na kuleta mshtuko mkubwa kwa mashabiki wa soka nchini humo na kwingineko Afrika.
Nchini Tanzania  Rais wa Shirikisho la Soka(TFF), Jamal Malinzi naye ni miongoni mwa walioshtushwa na kifo hicho na kuweka bayana alivyopokea kwa masikitiko makubwa taarifa za msiba huo0 wa Keshi (54) na kutuma salamu zake za pole. Rais Malinzi ametuma salamu za rambirambi kwa Rais wa Shirikisho la Soka Nigeria (NFF), Amaju Pinnick, familia ya marehemu Keshi pamoja na ndugu, jamaa, marafiki walioguswa na msiba huo wa gwiji huyo aliyepata kuwa nahodha wa kikosi cha Taifa Nigeria ‘Super Eagles’.
Katika rambirambi ambazo zimefika pia katika Ofisi za Shirikisho la Soka Afrika (CAF) na Shirikisho la Soka Duniani (FIFA), Rais Malinzi amesema kuwa japo Keshi ametangulia mbele za haki, mchango wake kwenye soka hautasahaulika kwani atabaki kuwa alama ya maendeleo ya mchezo wa soka.

Benteke ambeep Klopp, atasepa kama atamzingua

http://i3.mirror.co.uk/incoming/article6908832.ece/ALTERNATES/s615b/Liverpool-vs-Bordeaux-Europa-League-Group-Stage.jpg
Benteke
ANAONDOKA. Mshambuliaji nyota wa kimataifa wa Ubelgiji, Christian Benteke amesema anataka kubakia Liverpool, lakini amekiri anaweza kuangalia mahali pengine kama hatakuwepo katika mipango ijayo ya Kocha Jurgen Klopp.
Strika huyo aliyepo na kikosi chao kwenye fainali za Kombe la Ulaya Euro 2016, alijiunga na Liverpool akitokea Aston Villa kwa kitita cha Pauni Milioni 32.5 kiangazi mwaka jana.
Mkataba wake ulikuwa wa miaka mitano lakini amekuwa akishindwa kuonyesha cheche zake Anfield tangu Kocha Klopp alipomrithi Branden Rodgers.
Nyota huyo bado anapenda kuendelea kubakia hapo, lakini kama atakuwa nje ya mipango ya Klopp anaweza kuangalia mahali pengine atakapoweza kupata nafasi ya kucheza.
Akihojiwa Benteke amesema akiwa na umri wa miaka 25 sasa sio kwamba ni mkubwa sana au mdogo lakini muhimu ni kupata muda mwingi wa kucheza.

Didier Kavumbagu anukia Mbeya City

Didier Kavumbagu (kulia) akiwa na nyota wenzake wa Azam FC
NYOTA wa timu ya Taifa ya Burundi ‘Intamba Mu rugamba’ Didier Kavumbagu anaweza kuwa mchezaji wa kwanza kutangazwa kujiunga na kikosi cha Mbeya City Fc ya jijini Mbeya kinachoshiriki ligi kuu ya soka Tanzania bara muda wowote kuanzia sasa.
Katibu Mkuu wa City, Emmanuel Kimbe, mchana huu ameidokeza mtandao wa mbeyacityfc.com kuwa mazungumzo ya kumnasa nyota huyo wa timu ya taifa ya Burundi aliyekuwa akicheza kwenye kikosi cha Azam Fc ya jijini Dar es Salaam msimu uliomalizika yako kwenye hatua nzuri na tayari wakala wa mchezaji huyo amekwishaainisha yale yote muhimu yanayohitaji kwa ajili ya kuipata huduma yake likiwemo suala la kipengele cha kumruhusu kwenda kufanya majaribio nje ya nchi endapo yatapatikana.
“Tulianza mchakato wa kumpata Kavumbagu mapema kabisa, baada ya kukwama kwenye dirisha dogo Januari mwaka huu, tulikubaliana kuwa hitimisho litakuwa kwenye majira haya ya kiangazi, tayari nimezungumza na wakala wake, tuko kwenye hatua za mwisho kwa sababu ameshaanishia yale yote yanayohitajika, kwa maana hiyo basi, endepo tutamalizia vizuri hatua iliyobaki, muda wowote kuanzia sasa tunaweza kumtangaza kama mchezaji wetu," alisema Kimbe.
Akiendelea zaidi Kimbe alisema kuwa, Kavumbagu ni moja ya nyota walio kwenye orodha ya kocha Kinnah Phiri aliyoomba wasajiliwe ili kuiimarisha timu kwenye eneo la ushambuliaji akilenga kuwa wachezaji wenye uwezo wa kufunga kufuatia tatizo la umaliziaji lililoikuba City  kwenye michezo kadhaa ya mzunguko wa pili wa ligi  licha ya kucheza vizuri kwenye maeneo mengine.
“Tunayo majina  kadhaa ambayo kocha wetu ameomba wasajiliwe kulingana na mahitaji aliyonayo, Kavumbagu anaweza kuwa  wa kwanza kati yao,wengine watafuata kwa mujibu wa taratibu zetu, tunataka kufanya usajili makini ili kuimarisha timu na hatimaye tuwe na kikosi kitakachotupatia matokeo mazuri msimu ujao  hii ni baada ya mapito msimu uliopita”.
Kavumbagu  alianza kuichezea timu ya taifa ya Burundi mwaka 2009 na alikuwa mmoja wa nyota waliokiwakilisha kikosi hicho  kwenye michezo ya kutafuta kufuzu Kombe la Mataifa Afrika 2012 na kufunga mabao 2.
Kwa upande  mwingine   Kimbe  amedokeza kuhusu nyota ambao hawatakuwa sehemu ya kikosi cha City msimu ujao, na kusema kuwa  ni vizuri kuendelea kusubiri  kwa sababu muda si mrefu  taarifa  juu ya hilo itatolewa.

Simba kweli imepania yasajili nyota wapya kimyakimya

Wachezaji wa Simba wakishanglia moja ya mabao yao katika ligi iliyoisha hivi karibuni
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgIabpUQ1LhhV7WT0QDrMFTU3RkBUGjZcb9Vzjfhh_C9h79PB8OF127G0bCOqwCFY_EuUeS78PmeexLHfJ4mkxmuUUdFOynFb0SGf62Nh03pY0fyVpwyoksIU9nPXaSzZzdtkrBZOR1EHE/s1600/_FDA0288.JPG
Rais wa Simba, Evans Aveva na Mwenyekiti wa Usajili wa Simba, Zakari Hanspoppe
KLABU ya Simba wajanja kwelikweli. Baada ya viongozi wa klabu hiyo kubaini kuwa, wanachama wao wana hasira kwa sababu timu yao haijatwaa ubingwa wa Ligi Kuu Bara tangu mwaka 2011-2012, wameamua kufanya yao.
Wakienda na mwendo wa kimya kimya, viongozi hao wamefanya usajili kamambe bila makeke, kitu ambacho wapinzani wao Yanga na Azam ni lazima wakae chonjo kwa ligi ya msimu ujao.
Viongozi wa Simba ambao wanadaiwa wapo mbioni kuleta vifaa vya kimataifa kutoka Zimbabwe na Malawi, wamewanyakua nyota kadhaa wa klabu mbalimbali za Ligi Kuu Bara wakiwamo kutoka Mtibwa Sugar na Mwadui FC.
Wachezaji hao wameshasaini na kupewa mikataba yao, licha ya kwamba zile mbwembwe ambazo zimezoeleka kipindi kama hiki kwa klabu hiyo katika usajili zimewekwa kando ili kuhakikisha wachezaji wanaowataka wanawatia mkononi.
Micharazo inayo majina ya wachezaji wanne wapya waliosainiwa Msimbazi akiwamo kiungo mmoja fundi, ambaye katika ligi iliyomalizika alifanya yake akiifungia mara kadhaa Mtibwa mabao muhimu.

Kazi hiyo inafanywa kwa ushirikiano mkubwa baina ya matajiri wa Simba na Kamati ya usajili ya klabu hiyo inayoongozwa na Mwenyekiti wake, Zakaria Hanspoppe kwa mapendekezo ya kocha Jackson Mayanja na Benchi lake la Ufundi.
Mkali mwingine ni kiberenge kilichowahi kutamba Azam Fc, huku beki aliyekuwa akiwindwa na timu hiyo kutoka Mwadui, Idd Mobby ikielezwa amepotezewa, kwa sababu analetwa fundi mmoja toka Malawi atakayechukua nafasi ya Juuko Murshid.

Friday, June 3, 2016

Kweli imebaki Stori kwa Rich Mavoko (Official Video )

Ngeleja wenzake wapewa kifyagio na Malinzi

http://www.theworldfolio.com/img_db/timthumb.php?src=img_db/old/13226688671.jpg&w=800&z=1
Mhe. Ngeleja
http://www.thecitizen.co.tz/image/view/-/2841132/medRes/1098071/-/un1399/-/Jamal+Malinzi.jpg
Malinzi
MAJUZI Wabunge wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, walichagua uongozi mpya wa timu yao ya Bunge Sports Club na kama zali, Mbunge wa Sengerema, William Ngeleja akaukwaa Uenyekiti kilaini bila kupingwa, jambo hilo limemvutia sana Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania, TFF, Jamal Malinzi.
Rais huyo wa TFF amepongeza uongozi wa timu hiyo uliochaguliwa mjini Dodoma, ambapo Ngeleja alitwaa kiti akimrithi Idd Azan ambaye alishindwa kurudi bungeni katika Uchaguzi Mkuu wa Taifa wa 2015.
Mbali na Ngeleja, wengine waliopewa kifyagio hicho na Malinzi ni Makamu Mwenyekiti, Esther Matiko; Meneja wa Klabu, John Kadutu pamoja Wajumbe Neema Mgaya, Faida Bakari,  Cosato Chumi, Anna Lupembe na Grace Kihwelu.Malinzi amewatakia kila la kheri Bunge Sports Club na kuwaahidi ushirikiano kutoka TFF katika kuendeleza klabu yao na michezo kwa ujumla nchini.

Kwa Buku 5 tu inaiona Stars, VIP nako bwerere Taifa

MSHINDWE wenyewe. Viingilio vya kuliona pambano la kuwania kwenda kwenye fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON 2017) kati ya Taifa Stars ya Tanzania na Mafarao wa Misri zimewekwa hadharani.
Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limetangaza viingilio hivyo, ambapo kile cha bei ya chini kabisa ni buku tano tu. (Sh 5,000) wakati cha juu kikiwa ni Sh. 10,000. Mnataka nini tena?!
TFF ni kama kimesikia kilio cha mashabiki wa soka, kwa kutangaza viingilio hivyo katika mchezo huo wa kesho Jumamosi kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar.
Mwanangu toroka uje kwa sababu tiketi zimeanza kuuzwa mitaa mbalimbali ya jiji hilo.
TFF imesema watakaolipa Buku 5 watakaa mzunguko wa viti vya rangi ya Chungwa, Kijani na Bluu, wakati wanene wanaotaka kukaa kibosibosi yaani VIP B na C wenyewe watatoboka kiduchu kwa Mwekundu mmoja (Sh. 10,000).
Sasa unajua tiketi zenyewe zinapatikana wapi, wala usikonde ukienda Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Ilala jijini Dar es Salaam utapata, pale  Ukumbi wa Burudani Mbagala Dar Live, Vituo cha mafuta cha Oilcom - Ubungo na Buguruni (Buguruni Shell) na Ofisi za Ukumbi wa burudani Bilicanas, nako utapata.
Halafu hata kesho Jumamosi Juni 4, 2016 tiketi zitauzwa kwenye vituo hivyo na vingine vya Mwenge, Mnazi Mmoja, Makumbusho, Chang’ombe na Mgahawa wa Brake Point ulioko mkabala makaburi ya Kinondoni, Dar es Salaam.
Unangoja nini mwanangu, changamka bhana!