STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, March 29, 2014

Hivi ndivyo Shule ya Joyland ilivyowapa faraja yatima wa Chamazi

Wanafunzi wa Joyland Pre& Primary wakiwa wamejichangana na yatima wa kituo cha Yatima Trust Fund huku walimu wao wakiwa wamesimama

Walimu wa Shule ya Joyland wakijitambulisha mbele ya hadhara mchana wa leo kabla ya kukabidhi msaada wao kwa yatima
Mkurugenzi wa Shule ya Joyland, Fred Otieno akizungumza kabla ya kukabidhi msaada kwa yatima wa kituo cha Yatima Trust Funds
Wanafunzi wa Joyland wakiwa wamekaa kando ya yatima wa kituo cha Yatima Trust Fund
Baadhi ya yatima wanaolelewa na kituo cha Yatima Trust Funds wakiwa makmini kufuatilia matukio yaliyokuwa wakiendelea kwenye hafla ya kukabidhiwa misaada na Shule ya Joyland
Watoto wakiwa bize kufuatilia matukio kwenye hafla iliyofanyika leo Chamazi
Yatima wanaolelewa kituo cha Yatima Trust wakionyesha ujuzi wao wa kunengua
Wnachuana kucheza muziki uliokuwa unaporomoshwa
Kama Super Nyamwela! Dogo ana kipaji cha kucheza muziki nouma!
Bendi ya Shule ya Joyland ilikuwapo kuwatumbuiza yatima siku ya leo yaani ilikuwa faraja kubwa kwa watoto hao
Mkurugenzi wa Joyland Pre& Primary, Fred Otieno akiomba kabla ya shughuli kuanza...yaani kama Pastor
Ameen! Walimu na watoto wakitikia sala ya mambi kabla ya shughuli kuanza leo Chamazi.
Ameeen! Watoto wakiitikia dua
Baadhi ya yatima wakiwa wamewabeba wanafunzi wa Joyland waliowatembelea kituoni kwao leo na kukabidhiwa msaada ya vitru mbalimbali vyenye thamani ya Sh. Mil. 5
Utoto bana! wenzake wanaangalia mbele yeye anaangalia nyuma, lakini ni raha tupu!
Baadhi ya walimu wa Joyland wakiwa katika pozi kuangalia usalama wa watoto wao na yatima waliowatembelea
Yaani hawa madogo walifanya hata wenzao wasahau kucheza muziki kuwashuhudia vizuri wanavyochuana kunengua kwa raha zao
We angalia mpambano ulivyokuwa halafu toa maoni yako unadhani nani aliibuka mkali wa kudansi
Mkaanga Chips huyu balaa kama Titina Alcapone au Komba Belou Mafwala

Sehemu ya msaada uliotolewa na Shule ya Joyland kwa Yatima Trust Funds
Madam Anna alikuwa bize na mtoto aliyempakata...uchungu wa mwana jamani!
baadhi ya walimu wa Joyland waliowatembelea yatima wa Chamazi
Walimu wa Joyland wakiwa katika pozi

Messi airejesha Barcelona kileleni Hispania

http://img.bleacherreport.net/img/images/photos/002/327/252/hi-res-159041765_crop_north.jpg?w=630&h=420&q=75BAO pekee la mkwaju wa penati lililofungwa na Lionel Messi katika dakika ya 77 limeisaidia Barcelona kupata ushindi wa ugenini dhidi ya Espanyol na kurejea kileleni mwa msimamo wa Ligu Kuu ya Hispania ikiishusha Atletico Madrid.
Barcelona ambayo ilibanwa na wenyeji wao kabla ya kuja kuwazidi wapinzani wao waliompoteza kipa wao Casilla Cortés aliyelimwa kadi nyekundu.
Ushindi huo umeifanya Barcelona kufika jumla ya pointi 75, mbili zaidi ya Atletico Madrid ambayo ina 73 na inatarajiwa kushuka dimbani baadaye na iwapo itashinda inaweza kurejea kwenye kiti chake cha uongozi.
Vijana hao wa Diego Simeone itakuwa ugenini kupepetana na Athletic Club, moja ya mapambano matatu ya ligi hiyo kwa leo, jingine litazikutanisha timu za Celta Vigo dhidi ya Sevilla.
Ligi hiyo itaendelea kesho kwa michezo mingine kadhaa ukiwamo wa Real Madrid watakaokuwa nyumbani kwao Santiago Bernabeu kuikaribishaRayo Vallecano huku wakiuguza vipigi viwili mfululizo toka kwa Barcelona na Sevilla.

Chelsea yapigwa kimoja, Southampton ikiiua Newcastle Utd

John Terry own goal
Kitu! John Terry akijifunga bao langoni mwake wakati akichuana na Joel Ward huku kipa Petr Cech hakiwa hana la kufanya
Rickie Lambert scores
Rickie Lambet (7) akifunga moja ya mabao yake mawili Southampton ilipoinyuka Newcastle United kwa 4-0
VINARA wa Ligi Kuu ya England, Chelsea imeendelea kunyanyaswa na timu ndogo baada ya leo kukubali kipigo cha bao 1-0 ikiwa ugenini dhidi ya Crystal Palace.
Bao la kujifunga la beki na nahodha wake, Jerry Terry katika dakika ya 52, lilitosha kuinyong'onyesha Chelsea inayonolewa na kocha Jose Mourinho ambayo imesaliwa na pointi 69 baada ya kucheza mechi 32.
Pointi hizo zinaweza kufikiwa na Manchester City iwapo itashinda mchezo wake unaoanza hivi punde dhidi ya  Arsenal na kuwaondoa kileleni kwa tofauti ya uwiano wa mabao ya kufunga na kufungwa.
City hata hivyo kama itashinda itaongoza msimamo huo kwa saa chache tu iwapo Liverpool itapata ushindi katika mechi yao ya kesho nyumbani dhidi ya Tottenham.
Liverpool wapo nafasi ya pili wakiwa na pointi 68 na Ciy ni wa watatu wakiwa na pointi zao 66 na michezoi mitatu mkononi kwa sasa.
Katika mechi nyingine zilizomalizika hivi punde katika ligi hiyo Southmpton ikiwa nyumbani iliitafuna Newcastle United kwa mabao 4-0. mabao ya washindi yalifungwa na Jay Rodriguez, Rickie Lambert aliyefunga mawili na Adam Lallana, huku Stoke City ikitambia Hull City kwa bao 1-0 na Swansea City ikitamba nyumbani kwao kwa kuilaza Norwich City kwa mabao 3-0 na West Bromwich ilishindwa kulinda mabao yake na kulazimishwa sare ya 3-3 na wageni wao Cardiff City.

Bayern Munich bado haishikiki Bundesliga

http://thesoccerdesk.com/wp-content/uploads/2013/11/bayern-munich.jpg
MABINGWA wa Ligi Kuu ya Ujerumani, Bayern Munich, imeendelea kulinda rekodi yao ya kutopoteza mchezo wowote katika ligi hiyo baada ya jioni hii kulazimishwa sare ya 3-3 ma Hoffenheim.
Bavarians waliotetea taji hilo mwanzoni mwa wiki hii kwa kuifunga Hertha Berlin mabao 3-1, ilishutuliwa na wageni wao baada ya  Anthony Modeste alipofunga katika dakika yua 23.
Hata hivyo wenyeji walicharuka na kusawazisha bao kupitia kwa Claudio Pizarro katika dakika ya 31 kabla ya Xherdan Shaqiri kuongeza la pili katika dakika ya 34.
Pizarro aliongeza bao jingine dakika ya 40 na dakika moja kabla ya mapumziko Salihovic aliifungia Hoffenheim bao la pili na kufanya timu yao iende mapumziko wakiwa nyuma kwa mabao 3-2.
Kipindi cha pili wageni waliopo nafasi ya katikati waliendelea kuwasumbua wenyeji wao na kufanikiwa kusawazisha bao katika dakika ya 75 kupitia kwa Roberto Firmino.
Katika mechi nyingine za ligi hiyo Borussia Dotmund ikiwa ugenini ilipata ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Stuttgart, Bayer Leverkusern ililazimishwa sare ya 1-1 na Eintracht Braunschweig.
Nayo timu ya Wolfsburg wakiitandika Eintracht Frankfurt 2-1 na Mainz 05 ikapata ushindi mnono nyumbani kwa kuizabua Augsburg kwa mabao 3-0.

Ashanti Utd yawafumua maafande wa Oljoro JKT

Ashanti United ambao wameibuka na ushindi leo dhidi ya Oljoro JKT ya Arusha
 WATOTO wa Jiji, Ashanti United jioni ya leo imezinduka na kufufua matumaini yao ya kubaki katika Ligi kuu Tanzania Bara baada ya kuwacheza kwata maafande wa Oljoro JKT ya Arusha kwa kuwalaza mabao 2-1 katika pambano pekee la ligi hiyo lililochezwa leo.
Pambano hilo lilichezwa kwenye uwanja wa Chamazi na washindi walienda mapumziko wakiongoza kwa bao 1-0 lililofungwa na Hassani Kabunda, huku Oljoro wakipoteza penati katika dakika ya tano tu ya mchezo huo.
Kipindi ca pili wenyeji walipata bao la pili lililofungwa kwa mkwaju wa penati na Hassani Kabunda kabla ya Oljoro kujipatia bao la kufutria machozi lililotokana pia kwa mkwaju wa penati kupitia kwa Shaibu Nayopa.
Ushindi huo uliokuwa ukihitajiwa mno na Ashanti umeiwezesha timu hiyo inayonolewa na kocha mahiri, King Abdallah Kibadeni, kufikisha jumla ya pointi 21 kutokana na mechi 23 na kushika nafasi ya 11.
Oljoro ambayo inapigana kuepuka kushuka daraja kama ilivyo kwa wapinzani wao, imeendelea kusota kwenye nafasi ya 13 ikiwa na pointi 16, tatu zaidi ya wanaoburuza mkia Rhino Rangers ambayo kesho itakuwa wageni wa JKT Ruvu kwenye uwana wa Chamazi.
Mechi nyingine zitakazopigwa kesho ni kati ya vinara wa ligi hiyo, Azam itakayokwaruzana na Simba kwenye uwanja wa Taifa, Yanga watakuwa ugenini kuumana na Mgambo JKT, huku mabingwa wa zamani Mtibwa Sugar na Coastal Union watapepetana uwanja wa Manungu, Morogoro na Kagera Sugar itaialika Ruvu Shooting na jiji la Mbeya litashuhudia Mbeya City na Prisons-Mbeya zitaumana uwanja wa Sokoine.

Redd's Miss Tanzania washtuliwa na BASATA

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiB6UvYNwcMvfbMpSAtHa7GLsvdfWtGpQLb5MLk4MqnfoTgqET4znJNnHr3E5ikuD8-0OC6Bijb_j8KcvhCz-S0VLvzqKubxrGrL4T17tVKQPKse6-QWm7tPc2Dqw5-F5NgojtP5rFYWaFS/s1600/IMG_9116.JPG
BARAZA la Sanaa la Taifa (BASATA), limeitaka Kamati ya Miss Tanzania kutohusisha burudani zinazokiuka maadili ya Mtanzania wakati wa mashindano yao ya urembo mwaka huu.
Akizungumza wakati wa kikao cha tathmini ya mashindano ya Miss Tanzania 2013 kilichofanyika kwenye ukumbi wa baraza hilo, Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa Idaya ya Ukuzaji Sanaa BASATA, Vivian Shalua, alisema kuwa maadili ni muhimu kuzingatiwa katika mashindano hayo ili kuepukana na dhana potofu kuwa yanahusiana na uhuni.

“Maadili yazingatiwe katika mashindano ya mwaka huu, kuanzia kwa washiriki hadi burudani zitakazohusishwa, kama ‘vigodoro’, ‘kanga moja mbendembende’ na nasikia siku hizi kuna ‘tisheti ndembendembe’,” alisema Mkurugenzi huyo.
Alisema kuwa BASATA ipo tayari kuyapigania mashindano ya Miss Tanzania kuhakikisha yanakuwa katika ubora wa hali ya juu kwa kushirikiana na Kampuni ya Lino International Agency ambao ndio waandaaji wa mashindano hayo.
Mkurugenzi huyo pia aliitaka Lino kuwaelimisha mawakala wanaoandaa mashindano hayo juu ya umuhimu wa kuwa na vibali kutoka BASATA, ikiwa ni pamoja na kutowavumilia watovu wa nidhamu bila kujali ukongwe wao katika tasnia hiyo.
Kwa upande wake, Ofisa Sanaa Kitengo cha Matukio, Kurwijira Maregesi, aliitaka Lino kujipanga kujiweka tayari kufanya mashindano hata pale inapokosa mdhamini, huku mjumbe mwingine katika kikao hicho ambaye ni Ofisa Sanaa BASATA, Philemon Mwasanga, akisisitiza mawakala kuwekeana mikataba na warembo kabla ya mashindano kuanza.
“Lino isiwafumbie macho mawakala wasiojali mikataba na warembo, na warembo waisome na kuielewa ili kuepusha migogoro inayoweza kutokea,” alisema.
Akijibu hoja kadhaa zilizoibuliwa katika kikao hicho, Mkurugenzi wa Lino International Agency, Hashimu Lundenga, alisema kuwa wamejipanga ili kuweza kufanya mashindano yao bila kutegemea wadhamini, huku akiitaka BASATA kuwasaidia katika hilo.
“Tatizo mashindano yetu gharama yake ni kubwa sana, nasi hatupendi kuona ubora wake ukishuka kutokana na kushindwa kumudu gharama, ndio maana tumekuwa tukihangaika kuomba udhamini kutoka katika makampuni mbalimbali makubwa hapa nchini,” alisema.
Juu ya mikataba baina ya warembo na mawakala, Lundenga alisema: “Mwaka huu tumesisitiza mawakala waingie mikataba na washiriki kabla ya mashindano na tutakuwa makini katika kufuatilia hilo na changamoto nyinginezo zilizoibuliwa katika kikao hiki.”
Mmoja wa warembo walioshiriki mashindano ya mwaka jana ambaye ni Miss Sinza 2013, Prisca Clement, alisema kuwa kuna umuhimu wa kuongezwa kwa zawadi katika ngazi za chini ili kumwezesha mshiriki kujivunia na kujitosa kwake katika mashindano hayo bila kujali kama ameshinda au la.
Mashindano ya Miss Tanzania 2014 yamezinduliwa mapema wiki hii ambapo fainali zake zinatarajiwa kuwa kati ya Septemba na Novemba mwaka huu chini ya udhamini wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), kupitia kinywaji chake cha Redd’s Orirginal.

Jahazi la timu ya Babi lazidi kuzama Malaysia

Kikosi cha UiTM anayoichezea Abdi Kassim (wa kwanza kulia mbele)
JAHAZI la timu ya UiTM anayoichezea kiungo wa kimataifa wa Tanzania, Abdi Kassim 'Babi' limezidi kuzama kwenye Ligi Kuu ya nchini Malaysia baada ya jana kufungwa kwa mara ya pili mfululizo.
UiTM iliyokuwa ugenini, ilikumbana na kipigo cha bao 1-0 toka kwa wenyeji wao Negeri Sembilan,  waliowafuata kwenye uwanja Tuanku Abdulrahaman, mjini Seremban ikiwa ni siku chache tangu idunguliwe nyumbani kwa mabao 4-1 na Felda United.
Kipigo hicho cha jana ni cha sita katika michezo 9 iliyocheza timu hiyo na kuifanya izidi kuporomoka kwenye msimamo wa ligi hiyo ikienda nafasi ya 11, nafasi moja toka mkiani.
UiTM iliyomsajili Babi kwa mkataba wa mwaka mmoja akitokea KMKM imesaliwa na pointi zake 7 kutokana na kushinda mechi mbili tu na kuambulia sare moja na kupoteza mechi zilizosalia.
Timu hiyo inatarajiwa kushuka dimbani Ijumaa ijayo kwa kuvaana na Kedah kwenye uwanja wao wa nyumbani.

PSG yazidi kupeta Ufaransa

Paris Saint Germain's Zlatan Ibrahimovic of Sweden, center, controls the ball past Nice's Mathieu Bodmer of France, left, during their French League One soccer match, in Nice stadium,southeastern France, Friday, March 28, 2014. (AP Photo/Lionel Cironneau)
Zlatan Ibrahimovic akichuana na wachezaji wa Nice wakati PSG ilipopata ushindi wa ugenini
BAO la kujifunga la Timothee Kolodziejczak wa Nice usiku wa jana liliisaidia mabingwa watetezi wa Ligue 1, PSG kuendeleza wimbi la ushindi katika ligi hiyo na kujichimbia kileleni.
Wenyeji walijifunga bao hilo katika dakika ya 52 wakati Kolodziejczak akiwa katika harakati za kuokoa mpira na kuisaidia PSG ambayo Jumatano itavaana na Chelsea katika mchezo wa mkondo wa kwanza wa Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa  Ulaya kujikita kileleni.
Timu hiyo kwa ushindi wa jana imefikisha jumla ya pointi 76 kutokana na michezo 31 na kuwaacha wanaowafukuzia Monaco kwa pointi 13 hata Monaco itakayoshuka dimbani leo dhidi ya Evian TG.

Shule ya Joyland yasaidia yatima msaada wa thamani ya Sh. Mil.5

Mkuruigenzi wa Shule ya Joyland Pre & Primary, Fred Otieno (wa pili kulia) na mmoja wa walimu wa shule hilo wakikabidhi sehemu ya msaada wao kwa Baba Mlezi wa Kityo cha Kulelea Yatima cha Yatima Trust Fund, Haruna Mtandika (kushoto) huku wakisaidiwa na baadhi ya yatima wa kituo hicho.
Mmoja wa walimu wa Shule ya Joyland, Madam Anna akiwa amempakata mmoja wa yatima wanaolelewa kwenye kituo cha Yatima Trust Fund, mara baada ya kukabidhi msaada wao kwa kituo hicho kilichopo Chamazi.
Mmoja wa yatima, Halima Seif akitoa shukrani zake na kuililia serikali na watu wengine kuwasaidia kuwaendeleza kielimu.
Viongozi wa Shule ya Joyland wakiongozwa na Mkurugenzi wao, Fred Otieno (wa nne toka kulia) wakikabidhi sehemu ya msaada walioutoa leo kwa kituo cha Yatima Trust Fund
Ngojeni tuwasaidie kupeleka ndani! Baadhi ya wasaidia wa kituo cha Yatima Trust Fund wakipelekea misada waliyopewa ndani ya stoo yao
Huu ni mwanzo tu, tutawaletea zaidi
Mkurugenzi wa Joyland Pre& Primary, Fred Otieno akizungumza na vyombo vya habari baada ya kukabidhi msaada wao kwa yatima leo jijini Dar es Salaam.
Baba Mlezi na mmoja wa waasisi wa Yatima Trust Fund, Haruna Mtandika akitoa shukrani zake wakati akizungumza na wanahabari
 UONGOZI wa Shule ya Joyland Pre & Primary ukishirikiana na wazazi wa watoto wanaosoma shule iliyopo Tuangoma, Kigamboni umetoa msaada wa vyakula na vitu mbalimbali wenye thamani ya zaidi ya Sh. Mil. 5 kwa kituo cha kulelea yatima cha Yatima Trust Fund.
Msaada huo ulikabidhiwa leo mchana na uongozi wa Shule hiyo kwa viongozi wa kituo hicho kilichopo Chamazi, nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam katika hafla fupi iliyofanyika kwenye kituoni hapo.
Mkurugenzi wa shule hiyo, Fred Otieno alisema uongozi wa shule yao ambayo haina muda mrefu tangu ianzishwe ukishirikiana na wazazi waliamua kujitolea msaada huo kama sehemu ya kuonyesha namna wanavyoguswa na yatima nchini.
Otieno alisema ingawa walichokitoa ni kidogo, lakini anaamini kitawasaidia yatima hao na kutoa wito kwa watu wengine kujitolea kwa hali na mali kuwasaidia yatima sehemu yoyote walipo.
"Kama sehemu ya jamii tunaguswa na matatizo ya yatima na ndiyo maana tukaamua kuchangishana kuanzia walimu, uongozi wa shule, wazazi na hata wanafunzi ili kuja kuwafariji yatima hawa." alisema.
Otieno alisema yatima hawapaswi kuachwa, hawakupenda kuwapoteza wazazi, hivyo wafarijiwe kwa kusaidia kwa hali na mali na wao wameonyesha mfano ili wengine waige.
Naye Baba mlezi na muasisi wa kituo hicho, Haruna Mtandika aliyepokea msaada huo kwa niaba ya uongozi na yatima wanaolelewa kituoni hapo waliushukuru uongozi wa shule ya Joyland.
Mtandika alisema Yatima Trust Fund iliyoasisiwa mwaka 1996 na kusajiliwa rasmi mwaka 2001 wamefariji kwa kukumbukwa kwa msaada huo na kuwaomba watu waige mfano wa shule hiyo.
"Tunawashukuru sana Joyland kwa kuonyesha moyo wa huruma kwa yatima hawa, na Mungu awabariki zaidi kwani nimesikia shule yenu haina muda mrefu tangu muianzishe lakini umeonyesha mfano wa kuigwa," alisema
Pia alidokeza kwenye risala yao changamoto wanayokabiliana nayo ikiwamo uhaba wa samani kwa ajili ya malazi, chakula, ada na sare kwa watoto wanaowasomesha, ambapo Mkurugenzi wa Joyland, aliahidi kuwasomesha watoto wawili toka kituoni hapo.
Otieno, alisema watoto hao mmoja mmoja wa kike na mwingine wa kiume watasomeshwa kwa kugharamiwa na uongozi wa shuleni kuanzia chekechea hadi darasa la saba.
Naye mmoja wa watoto wanaolelewa kituoni hapo, Halima Seif (16) pamoja na kuushukuru uongozi wa Joyland, pia alitoa wito kwa watu wengine wenye uwezo kuwasaidia kusomeshwa.
"Nilikuwa naomba watu watusaidie, kwa mfano mimi napenda shule, lakini sijaendelea na masomo ya sekondari kwa sababu sina wa kunilipia ada hiyo nawaomba watu wengine watuangalie sisi yatima," alisema Halima huku akimwaga chozi la uchungu.
Mara baada ya makabidhiano hayo, uongozi wa shule, walimu na waalikwa wengine walijumuika kula na kuburudika na muziki na yatima hao kama njia ya kuwafariji jambo lililonekana kufurahiwa na watoto hao.

Manchester Utd yaua Old Trafford

Wayne Rooney heads home Manchester United's equaliser
Rooney akifunga bao la kwanza la Man Utd
Inside out: As Mata turns inside Bacuna the defender takes the Spanish midfielders legs out
'Fundi' Juan Mata akiwajibika uwanjani
KLABU ya Manchester United leo wakiwa kwenye uwanja wao wa nyumbani wa Old Trafford wameifumua bila huruma Aston Villa kwa kuikandika mabao 4-1 katika mchezo wa Ligi Kuu ya England.
Mashetani Wekundu waliotoka kuchezea kichapo cha aibu cha mabao 3-0 toka kwa Mahasimu wao, Manchester City, leo ilionekana wamekuja kivingine na hasa kocha wao David Moyes kuwachezesha kwa pamoja mafundi, Shinji Kagawa na Juan Mata.
Wageni walianza kuwashtua vijana wa Moyes kwa kufunga bao katika dakika ya 13 kupitia kwa Ashley  Westwood kabla Wayne Rooney kusawazisha dakika saba baadaye kwa pasi ya Mjapan Kagawa.
Rooney alirejea tena kimiani kwa kuifungia Man Utd bao dakika ya 45 kwa mkwaju wa penati baada ya Mata kuchezewa faulu na kufanya Mashetani hao kwenda mapumziko wakiwa mbele kwa 2-1
Kipindi cha pili Man walizidi kuonyesha wamedhamiria kuwatia adabu Villa walioiangusha Chelsea wiki iliyopita baada ya Juan Mata kufunga bao la tatu katika dakika ya 57.
Mtokea benchi Javier Hernández 'Chicharito' alihitimisha karamu ya mabao kwa kupachika bao la nne katika dakika ya nyongeza kabla ya mpira kwisha na kumpa Moyes afueni toka kwa mashabiki kwa ushindi huo mnono uliowafanya wafikishe jumla ya pointi 54.
Hata hivyo ushindi huo bado umeiacha Red Devils kwenye nafasi ya saba baada ya kucheza meci 32 na Aston Villa wamebaki nafasi ya 12 kwenye msimamo wa ligi inayoendelea kwa sasa kwa mechi kadhaa.

Friday, March 28, 2014

Ashanti, Oljoro nani kulia Chamazi, vita ipo J'pili

Oljoro JKT
Ashanti United
VIBONDE vya Ligi Kuu Tanzania Bara, Ashanti United na Oljoro JKT kesho zinatarajiwa kupepetana katika pambano pekee kwa siku ya Jumamosi, huku kila moja ikiwa inahitaji ushindi ili kufufua matumaini ya kuendelea kusalia kwenye ligi ya msimu ujao.
Timu hizo zinazofuata toka mkiani zikiwa juu ya Rhino Rangers inayoburuza mkia na pointi zake 13 zitaumana kwenye uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam.
Ni ushindi pekee kwa kila timu utafufua matumaini ya kuendelea kucheza ligi ya msimu ujao, vinginevyo huenda wakajiweka pabaya zaidi kushuka daraja kama walivyo wenzao wa Rhino ambao watashuka dimbani  Jumapili dhidi ya JKT Ruvu.
Ashanti inayonolewa na kocha Abdallah Kibadeni ina pointi 18 ikiwa nafasi ya 12, huku wapinzani wao wakiwa chini yao na pointi 16 kila moja ikiwa imecheza mechi 22.
Kila timu inahitaji ushindi ikizingatiwa zimetoka kuchezea vichapo katika mechi zao zilizopita, Ashanti ikizamishwa mabao 2-0 na Ruvu Shooting na Oljoro ikizabuliwa na Azam.
Timu hizo zilizobadilisha makocha baada ya kuyumba kwenye duru la kwanza, zimekuwa kama homa ya vipindi kwa viwango vyao kupanda na kushuka kulingana na aina ya mechi.
Kivumbi zaidi cha ligi hiyo kitakuwa Jumapili ambapo viwanja sita vitawaka moto kwa kuzikutanisha timu 12 zikiwamo tatu zinazowania taji la ubingwa wa ligi hiyo linaloshikiliwa kwa sasa na Yanga.
Azam watakuwa kwenye uwanja wa Taifa kuivaa Simba, ikihitaji ushindi ili kuujongelea ubingwa huo na pia kuiombea mabaya Yanga watakaokuwa ugenini mjini Tanga kupepetana na Mgambo JKT iteleze katika mechi yake hiyo itakayopigwa uwanja wa Mkwakwani.
Azam ina pointi 50, nne na ilizonazo Yanga licha ya kuwa mbele kwa mchezo mmoja na timu yoyote ikiteleza itatoa nafasi kwa mwenzake kuubeba ubingwa huo kwa msimu wa 2013-2014.
Mbeya City waliopo nafasi ya tatu na pointi 42 wakiwa nao wanauota ubingwa watakuwa uwanjwa wa Sokoine kuumana na ndugu zao Prisons wanmaougulia kipigo cha mabao 5-0 walichopewa na Yanga juzi.
Ushindi wowote kwa Mbeya utamaanisha unaiweka pabaya Simba katika mbio zake kutaka kuambulia angalau nafasi ya tatu kama ilivyokuwa msimu uliopita.
Simba wana pointi 36 na wamesaliwa na mechi nne, ambazo kama watashinda zote itafikisha pointi 48 zilizopitwa na Azam tayari.
Simba itavaana na Azam ikiwa inauguza kipigo cha bao 1-0 ilichopewa na Coastal Union mwishoni mwa wiki iliyopita kqwenye uwanja wa Taifa.
Mabingwa hao wa soka wa 1988 wenyewe watawafuata Mtibwa Sugar kuumana nao katika mchezo utakaochezwa uwanja wa Manungu, huku timu zote zikiwa hazina nafasi ya ubingwa wala hofu ya kushuka daraja.
Michezo nyingine ya Jumapili ni pamoja na Kagera Sugar watakuwa wenyeji wa Ruvu Shooting katika pambano linalosubiriwa kwa hamu kubwa mjini Bukoba, ambapo Msemaji wa Ruvu Masau Bwire ametamba kwamba wanaenda Kaitaba kuvuna pointi tatu.
Hata hivyo Bwire anatamba akitambua wazi kuwa Kagera Sugar huwa wagumu kwene uwanja wao wa nyumbani.
Timu hizo mbili zinafukuzana kwenye nafasi ya tano na sita zikitofautishwa na pointi moja, Kagera wakiwa na pointi 32 na Ruvu wenyewe wana pinti 31.

TMK, Tip Top kuzindua Yamoto

WASANII nyota toka makundi ya Tip Top Connection na TMK Wanaume Family wanatarajiwa kupamba uzinduzi wa video za Yamoto na Inno za kundi jipya linalooundwa na chipukizi toka Kituo cha Mkubwa na Wanawe.
Kundi hilo linaloundwa na wasanii Dogo Aslay, Beka, Maromboso na Bella, litazinduliwa Jumapili Masaki na nyota wa Tip Top wakiongozwa na Madee huku TMK litakuwa chini ya Chegge.
Kwa mujibu wa mmoja wa mabosi wa wasanii hao, Said Fella 'Mkubwa' aliliambia MICHARAZO uzinduzi wa kundi hilo utaenda sambamba na utambulisho wa kazi mpya za wasanii hao.
"Tunatarajiwa kuwatambulisha rasmi na kuzindua kundi la Moto linaloundwa na wasanii wanne walioibuliwa na Mkubwa na Wanae watakaosindikizwa na makundi ya Tip Top na TMK," alisema Fella.
Fella alisema makundi hayo yote yatakuwa na wasanii wao wote nyota na kuwataka mashabiki wa muziki kujitokeza kwa wingi Jumapili ili kupata burudani murua.

Mashali, Kaseba kupima uzito leo

Kaseba na Mashali wakishoo
MABONDIA Japhet Kaseba na Thomas Mashali na wengine watakaowasindikiza katika pambano lao la kuwania ubingwa wa UBO Afrika wanatarajiwa kupima uzito wao siku ya Ijumaa jijini Dar.
Kwa mujibu wa taarifa ya mmoja wa waratibu wa pambano hilo, Ibrahim Kamwe mabondia hao watapima uzito kuanzia saa 3 asubuhi kwenye ukumbi wa hoteli ya National iliyopo eneo la Keko.
Mbali na Mashali na Kaseba watakaopambana katika pambano la raundi 10 uzito wa LightHeavy (kilo 79), pia mabondia wengine watakaopima uzito na afya zao ni Allan Kamote ambaye atapigana na Karage Suba katika pambano la kuwania taji la kimataifa ya UBO.
"Mabondia wote wameshataarifiwa na wanatakiwa kuwahi mapema siku ya Ijumaa, National Hotel ili kupima afya na uzito wao kabla ya Jumamosi kuonyeshana kazi kwenye ukumbi wa PTA," alisema.
Kamwe aliwataja wengine watakaochuana katika michezo hiyo iliyoandaliwa na promota Ally Mwazoa, ni pamoja na Fredy Sayuni dhidi ya Rajab Mahoja watakaowania ubingwa wa taifa wa PST.
Baina Mazola atacheza na Bakari Dunda,Issa Omar ataonyeshana kazi na Zuberi Kitandula, Juma Fundidhidi ya Haji Juma, Shabaan Mtengela vs Jumanne Mohamed, Jocky Hamis dhidi ya Said Chaku

Subira ya Shaa mwezi ujao

Shaa katika pozi
'AUDIO' na VIDEO ya wimbo mpya wa msanii, Sarah Kais 'Shaa' unaofahamika kama 'Subira' unatarajiwa kuachiwa rasmi mapema mwezi ujao.
Wimbo huo uliobadilishwa jina kutoka 'Sifa Ujinga' hadi kuwa 'Subira' ni kazi ya pili ya mshindi huyo wa zamani wa Coca Cola Pop Star chini ya familia ya Mkubwa na wanae inayongozwa na Said Fella.
Akizungumza na MICHARAZO, Fella alisema wamepanga kutoa 'audio' na video ya wimbo huo mwezi ujao baada ya kurekodiwa mapema tangu Februari mwaka huu.
Fella alisema waliamua kuuzuia wimbo huo kutoka mapema ili kutoa nafasi ya kazi ya msanii huu iitwayo 'Sugua Gaga' kuendelea kutamba kwenye soko la muziki kutokana na ukali wake.
"Kazi mpya ya Shaa tutaiachia rasmi mapema mwezi ujao ikiwa ni 'audio' na video yake, hivyo mashabiki wajiandae kupata uhondo," alisema Fella waliyeingia mkataba na Shaa kwa muda wa miezi sita.
Kabla ya kutua Mkubwa na Wanae, Shaa alikuwa akifanya kazi chini ya umeneja wa Master J.

Ac Milan yazinduka, Juve moto chini

http://news.bbcimg.co.uk/media/images/73837000/jpg/_73837135_carlos-tevez-getty.jpg
Tevez akishangilia moja ya mabao yake

KLABU ya AC Milan imezinduka nchini Italia baada ya juzi kuikwanyua Fiorentina kwa mabao 2-0 nyumbani kwao, huku usiku wa jana wapinzani wao wa jiji la Milan, InterMilan walilazimishwa sare ya 0-0 na Udinese.
Milan ambaye imekuwa na matokea mabaya kwenye Ligi Kuu ya Seria A, walipata ushindi huo kupitia magoli yaliyofyungwa na Mexes dakika ya 23 kabla ya Mario Balotelli kufunga kipindi cha pili katika dakika ya 64 na kuipaa pointi tatu mabingwa hao wa zamani wa Ulaya.
Katika mechi nyingine za ligi hiyom, Juventus wakiwa nyumbani walipata ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Parma na kuzidi kujiweka karibu na kutetea taji la ubingwa wa ligi hiyo.
Magoli  yote mawili yalitupiwa kambani na Carlos Tevez katika dakika ya 25 na 32 na kuwapa pointi zinazowafanya wafikishe 81 na kusaliwa na mechi nane mkononi ambapo kama akishinda mechi tatu ikiwamo ya Jumapili dhidi ya Napoli atatawaza kuwa bingwa. Wageni walimpoteza Amauri aliyeonyesha kadi nyekundu.
Matokeo ya mechi nyingine za ligi hiyo;

Chievo     3 - 0     Bologna
Cagliari     1 - 0     Hellas Verona
Genoa     2 - 0     Lazio
Atalanta     2 - 0     Livorno   
Fiorentina     0 - 2     Milan
Catania     2 - 4     Napoli  
Juventus     2 - 1     Parma
Sassuolo     1 - 2     Sampdoria
Inter Milan 0-0 Udinese

Askofu Mhogolo afariki dunia

ASKOFU wa Dayosisi ya Central Tanganyika, Godfrey Mhogolo amefariki dunia nchini Afrika Kusini, alikokuwa amekwenda kwa matitabu. 
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kanisa la Angilikana Dodoma jana, ilisema kuwa Askofu Mhogolo kabla ya kufikwa na mauti alikuwa akitibiwa katika hospitali ya Milpark huko Johanesburg, Afrika Kusini. Askofu Mhogolo alikuwa askofu wa tano wa dayosisi ya Central Tanganyika na atazikwa katika viwanja vya kanisa Kuu la Roho Mtakatifu Mjini Dodoma.  
Hata hivyo Mchungaji Michael Nchimbi alisema mipango ya mazishi inaendelea na taarifa zitatolewa baadaye. 
matukio na vijana

Golden Bush kupeleka makali yao Kilombero

Kikosi cha Golden Bush
Makocha wa Golden Bush, Madaraka Seleman na Herry Morris waliosimama wakiteta na wachezaji wao katika moja ya mechi zao
 MABINGWA wa kandanda wa soka la maveterani, Golden Bush Veterani inatarajiwa kupeleka makali yake wilaya ya Kilombero Morogoro kumenyana na Kilombero Veterani katika mechi inayochezwa kesho.
Kwa mujibu wa Msemaji wa klabu hiyo, Onesmo Waziri 'Ticotico' kikosi cha Golden Bush kitaondoka kesho asubuhi kikiwa na wachezaji 25 wakiongozwa na mkuu wa msafara,  Waziri Mahadh 'Mandieta'.
Ticotico alisema kikosi chao kitashuka dimbani jioni ya kesho kwenye uwanja wa Ruaha kuumana na wenyeji wao watakaokuwa wakiongozwa na nahodha wa zamani wa Simba, Mustafa Hozza.
Ticotico alitamba kuwa wanaenda Kilombero kuendeleza ubabe wao ambao umewafanya kukimbiwa na wapinzani na kwamba wenyeji wao wajiandae kwa kipigo.
Alisema kikosi chao chini ya kocha Madaraka Seleman 'Mzee wa Kiminyio' kitaongozwa na nahodha wao Wisdom Ndhlovu a.k.a Mwakalinga.

TFF kuuendeleza uwanja wao wa Tanga

SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) limeanza mchakato wa kuendeleza uwanja wake uliopo eneo la Mnyanjani jijini Tanga.
Rais wa TFF, Jamal Emil Malinzi alisema shughuli inayoendelea kwa sasa ni kupima udongo (soil test) na kuandaa michoro kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha michezo (Sports Complex) ukiwemo uwanja wa mpira wa miguu na majukwaa yake.
Amesema TFF imetuma maombi rasmi kwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro kuomba eneo la kujenga kituo cha michezo ikiwemo uwanja wa mipira wa miguu na majukwaa yake.
“Pia Mkuu wa mkoa ameombwa kuingilia kati kuwaondoa wafanyabiashara waliovamia uwanja wa mpira wa miguu wa Jamhuri (King George Memorial ground) mjini Moshi,”amesema Malinzi.
Amesema TFF inawakumbusha viongozi wa vyama vya mikoa ambao hawajaomba maeneo ya kujenga vituo vya michezo vikiwemo viwanja vya mpira wa miguu, waongeze jitihada za kufanya hivyo na shirikisho hilo litawaunga mkono.
“TFF inachukua fursa hii kuvipongeza vyama vya mpira wa miguu ambavyo ama tayari vimeshachukua hatua au viko mbioni kuchukua hatua kutafuta na kuendeleza maeneo kwa ajili ya matumizi ya mpira wa miguu. TFF inaahidi kuunga mkono juhudi hizi na pale itakapohitajika kuongeza nguvu haitasita kufanya hivyo,”amesema.

Wednesday, March 26, 2014

Beki Coastal achekelea kuidungua Simba Taifa


Hamad Juma akichuana na Messi siku ya pambano la Coastal na Simba Taifa
MFUNGAJI wa bao pekee la Coastal Union ya Tanga lililoizamisha Simba kwenye uwanja wa Taifa, Hamad Juma anasema mpaka sasa haamini kama ni yeye aliyewalaza mapema vijana hao wa Msimbazi.
Hata hivyo beki huyo wa pembeni, aliyepandishwa kikosi cha kwanza toka timu ya vijana msimu huu, amesema anajisikia fahari kubwa kuwalaza mapema mashabiki wa Simba walioamini wangeshinda.
Akizungumza na MICHARAZO, Hamad alisema kila akikaa na kufikiria alichokifanya kwenye uwanja wa Taifa, hushindwa kujiamini kama ni yeye kutokana na ukweli wapinzani wao walisheheni nyota watupu.
Hamad alisema maamuzi aliyoyafanya mara baada ya beki wa Simba, Omar Salum kuzembea kuokoa mpira hakutarajia, lakini yaliweza kuwapa bao pekee lililoipa Coastal pointi tatu muhimu.
"Huwa nashindwa kuamini kama ni mimi niliyefunga bao lile na kuizamisha Simba, hata hivyo nashukuru kwa kusaidia Coastal na kuweka rekodi ya kuifunga timu kubwa kama ya Simba," alisema.
Alisema ushindi huo ulikuwa muhimu kwao ikizingatiwa kocha wao Yusuph Chipo aliwaamini vijana na kuwapanga katika pambano hilo timu yao ikitoka kufungwa mabao 4-0 na Azam.
Beki huyo alifunga bao hilo dakika ya 44 na kudumu hadi mwisho na kuifanya Simba ipoteze mechi ya nne katika ligi ya msimu huu na kuiacha ikibakia kwenye nafasi ya nne ya msimamo wa ligi hiyo.
Simba pia ilishapoteza mechi nyingine tatu mbele ya Azam, Mgambo JKT na JKT Ruvu na kutishia kukosa uwakilishi wa nchi kwa mara ya pili mfululizo kutokana kutanguliwa na Azam, Yanga na Mbeya City.

Yanga yaiua Prisons Taifa, Azam haishikiki

Yanga
Azam wanaozidi kuukomalia ubingwa unaoshikiliwa na Yanga
MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga imezidi kufufua matumaini ya kutetea taji hilo baada ya jioni hii kuibugiza Prisons-Mbeya kwa mabao 5-0.
Pambano hilo lililochezwa kwenye uwanja wa Taifa, lilishuhudia Yanga wakienda mapumziko wakiongoza kwa mabao 2-0.
Bao la kwanza la Yanga liliwekwa kimiani na Mganda Emmanuel Okwi kwa mkwaju wa faulo katika dakika ya 21 kabla ya Mrisho Ngassa kuongeza la pili dakika ya 38 akimalizia krosi ya Husseni Javu.
Kipindi cha pili Yanga ilicharuka na hasa baada ya kufanya mabadiliko ya wachezaji na kuweza kujiandikia bao la tatu lililofungwa dakika 68 na mtokea benchi, Hamis Kiiza 'Diego'.
Kiiza alifunga bao hilo akiuwahi mpira uliotemwa na kipa wa Prisons baada ya Simon Msuva kumimina krosi murua langoni mwa 'Wajelajela' na Mganda huyo kufunga kilaini.
Nahodha Nadir Haroub 'Cannavaro' aliiandikia Yanga bao la nne katika dakika ya 78 kwa mkwaju wa penati baada ya mabeki wa Prisons kumuangusha Husseni Javu, aliyeng'ara katika mchezo huo aliyoingia kipindi cha kwanza kuchukua nafasi ya Jerryson Tegete.
Dakika chache kabla ya kumalizika kwa pambano hilo, Kiiza kwa mara nyingine aliiongezea Yanga bao la tano baada ya Hussen Javu kufanya kazi nzuri kwa kufumua shuti langoni mwa wapinzani wao.
Kwa ushindi huo Yanga wamefikisha pointi 46 kutokana na kucheza mechi 21, wakiendelea kusalia nafasi ya pili nyuma ya Azam ambao jioni hii wameibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Mgambo JKT katika pambano lililochezwa jijini Tanga.
taarifa toka Tanga zinasema kuwa Azam walipata mabao yake kupitia kwa John Bocco na Brian Umony na kuifanya timu hiyo kuendeleza rekodi yao ya kutopoteza mchezo wowote katika ligi ya msimu huu na kukaa kileleni wakiwa na pointi 51 licha ya kucheza mchezo 22.

Tuzo za Wanamichezo Bora Juni 27

http://www.fullshangweblog.com/wp-content/uploads/2013/02/kapo4.jpg
Shomari Kapombe Mwanamichezo Bora wa 2012
 TUZO za Wanamichezo Bora Tanzania zinazotolewa Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA) zitafanyika Juni 27, mwaka huu katika ukumbi ambao utatajwa baadaye mjini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Kamati ya tuzo, Rehure Nyaulawa amesema leo kwamba baada ya kikao cha juzi cha Kamati yake juhudi za pamoja baina ya Kamati yake na Kamati ya Utendaji kuzungumza na wadhamini mbalimbali wakubwa na wadogo kwa nia ya kufanikisha tuzo hizo zimeanza.
“Kamati yetu kwanza inawaomba radhi viongozi wa vyama vyote vya michezo kutokana na tuzo kushindwa kufanyika mwaka jana na hilo kwa mujibu wa taarifa ya uongozi wa TASWA iliyowasilishwa kwenye kikao chetu, ilitokana na sababu mbalimbali lakini kubwa ni kujitoa dakika za mwisho kwa baadhi ya kampuni zilizokuwa zimethibitisha kudhamini tuzo hizo,”. Hata hivyo, Nyaulawa ameomba wendelee kutoa ushirikiano mwaka huu na kwa kuanzia watawatumia barua rasmi za kuomba majina ya wanamichezo wao waliofanya vizuri kuanzia Januari 2013 hadi Aprili mwaka huu, ambapo matarajio yao wanamichezo wasiopungua 40 watapewa tuzo. Amesema kwamba kamati pia imeamua kwamba kila mwaka tuzo hizo zijena ujumbe maalum kwa wanamichezo, ambapo kwa kuanzia tuzo za mwaka huu ujumbe wake utakuwa ni: ‘Wanamichezo Tupige Vita Ujangili’. “Tunaamini wale wote wataowania, wale watakaoshinda tuzo hizo na wanamichezo wote wakiwemo waandishi wa habari za michezo tutashirikiana na jamii kwa ujumla kwa kuwa mstari wa mbele kuhamasisha vita dhidi ya ujangili kwa namna tutakavyomudu,”amesema. Amesema pia katika kuhakikisha tuzo za mwaka huu zinakuwa bora kwa maslahi ya wanamichezo wote hapa nchini, kamati imeteua baadhi ya viongozi wa kiserikali kuwa washauri wa kamati katika masuala mbalimbali na sasa wanasubiri majibu yao ili waweze kuwatangaza rasmi.

29 waanza kambi ya Stars marekebisho Tukuyu


Na Mwandishi maalumu, Tukuyu
WACHEZAJI 29 kati ya 34 waliochaguliwa katika programu maalumu ya marekebisho ya timu ya Taifa inayoendeshwa na TFF wameshaanza mazoezi makali katika Wilaya ya Rungwe, Mbeya.

Wachezaji hao, ambao wametokea katika mikoa mabali mbali, waliingia kambini siku ya Jumamosi huku wakiongozwa na Mwalimu Salum Mayanga akisaidiwa na Patrick Mwagata, ambaye ni kocha wa makipa, Meja Joakim Mashanga ambaye ni daktari wa team na Fred Chimela ambaye ni Meneja Vifaa.


Timu ya Taifa, Taifa stars, inayodhaminiwa na Bia ya Kilimanjaro Premium Lager kwa mwaka wa pili mfululizo sasa, inatarajiwa kupata mabadiliko makubwa sana ndani ya miezi miwili ijayo ili ipatikane timu bora itakayoshiriki katika mechi za kufuzu kupata tiketi ya kucheza Kombe la Afrika.

Mashetani Wekundu wafa tena, Arsenal yabanwa Everton yapeta

Edin Dzeko
Edin Dzeko akiwatungua Manchester United
Wilfried Bony
Hekaheka langoni mwa Arsenal

Everton's Ross Barkley
Shhhhh!
  JAHAZI la Manchester United limezidi kuzama baada ya usiku wa kuamkia leo kukandikwa mabao 3-0 kwenye uwanja wake wa nyumbani wa Old Trafford na mahasimu wao wa jiji la Manchester, Manchester City.
Mabao ya Edin Dzeko aliyefunga mawili katika sekundu chache baada ya kuanza kwa mchezo huo na jingine la dakika 26 na lile la Yaya Toure dakika za 'jioni' yaliwafanya vijana wa David Moyes kushindwa kujua wamekumbwa na nini msimu huu.
Ushindi huo umeipeleka City hadi nafasi ya pili ikiiengua Liverpool itakayoshuka dimbani leo kuumana na Sunderland, kutokana na kufikisha pointi 66 baada ya kucheza mechi 29, mechi mbili pungufu na vinara wa ligi hiyo Chelsea wanaoongoza wakiwa na pointi 69.
Katika mechi nyingine, Arsenal ikiwa nyumbani ilinyang'anywa tonge mdomoni baada ya kulazimishwa sare ya 2-2 na Swansea City kwenye uwanja wa Emirates.
Wageni walitangulia kupata bao dakika ya 11 kupitia kwa Wilfried Bony kabla ya wenyeji kuja kusawazisha katika kipindi cha pili kupitia kwa Lucas Podolski katika dakika ya 73 na kuongeza jingine kupitia kwa Olivier Giroud.
Hata hivyo wakati Arsenal ikijiandaa kushangilia ushindi mchezaji wake Mathieu Flamini alijifunga katika harakati za kuokoa shambulizi langoni mwake na kuwapa sare Swansea na kugawa pointi moja moja.
Nao Everton wakiwa ugenini waliwaduwaza wenyeji wao Newcastle Utd kwa kuwakandika mabao 3-0, mabao yaliyowekwa kimiani na Barkley, Lukaku na Osman.
Kwa ushindi huo umeifanya Everton kufikisha pointi 57 na kupanda nafasi ya tano na kuishusha Tottenham Hotspur yenye pointi 56 ambayo inarudi katika nafasi ya sita.
Kivumbi cha ligi hiyo kitaendelea tena usiku wa leo kwa michezo miwili, Liverpool itakayoumana na Sunderland na West Ham Utd itaikaribisha Hull City.

Bayern Munich nouma yatetea taji Ujerumani kwa aina yake

 http://www.sportsarena.com.sg/di/library/omnisport/11/68/bayernmunich_1um7biac60yco14kixp752v0gm.jpg?t=-616441876w=570

MABINGWA watetezi wa Ligi ya Mabingwa Ulaya, Bayern Munich imefanikiwa kutetea taji lake la Ligi Kuu ya Ujerumani (Bundesliga) usiku wa jana baada ya kuwafunga Hertha Berlin kwa mabao 3-1.
Watetezi hao wametwaa taji hilo la 23 wakiwa wameshinda mechi 10 mfululizo na pia wakiwa wamecheza mechi 52 ya mashindano yote bila kupoteza.
Mabo ya washindi katika pambano hilo lililochezwa mjini Berlin, yalifungwa na  Toni Kroos, Mario Goetze na Frank Ribery na kuifanya Bavarians kunyakua taji hilo ikiwa na mechi saba mkononi kabla ya kumaliza msimu wa Bundesliga.