STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, May 4, 2014

Diamond, Jaydee wafunika tuzo za Kili Music Awards 2014

Diamond aliyeng'ara tuoz za Kill akimpita hata 20 Percent aliyetamba mwaka juzi

Comandoo Jide kama kawa
1. USIKU wa jana kulikuwa na utoaji wa tuzo za muziki ambapo kama kawaida Diamond amerejea kwa kishindo kwa kunyakua tuzo lukuki, sambamba na Jady Jaydee na Mzee Yusuph. Jisomee mwenyewe washindi wa tuzo hiyo kisha upime ukali wa wasanii hao watatu waliotajwa hapo juu.

WIMBO BORA WENYE VIONJO VYA ASILI YA TANZANIA - Bora Mchawi, Dar Bongo Massive
2. MSANII BORA CHIPUKIZI ANAYEIBUKA - Young Killer 
3. WIMBO BORA WA ZOUK - Yahaya, Lady Jaydee
4. WIMBO BORA WA AFRO POP - Number One, Diamond Platnumz
5. WIMBO BORA WA RAGGA / DANCEHALL - Nishai Chibwa Ft Juru
6. WIMBO BORA WA RAGGAE - Niwe na wewe, Dabo
7.WIMBO BORA WA TAARAB - Wasiwasi wako, Mzee Yusuf
8. KIKUNDI CHA MWAKA CHA TAARAB - Jahazi Modern Taarab
9. MWIMBAJI BORA WA KIKE  TAARAB - Isha Ramadhani
10. MWIMBAJI BORA WA KIUME TAARAB - Mzee Yusuf
11. WIMBO BORA WA KISWAHILI BENDI - Ushamba mzigo, Mashujaa Band
12. MWIMBAJI BORA WA KIKE BENDI - Luiza Mbutu
13. MWIMBAJI BORA WA KIUME BENDI - Jose Mara
14. RAPA BORA WA MWAKA BENDI - Furguson


15. BENDI YA MWAKA - Mashujaa Band
16. MWIMBAJI BORA WA KIKE, KIZAZI KIPYA - Lady Jaydee
17. MWIMBAJI BORA WA KIUME, KIZAZI KIPYA - Diamond
18. KIKUNDI CHA MWAKA CHA KIZAZI KIPYA - Weusi
19. WIMBO BORA WA RNB - Closer, Vanessa Mdee
20. WIMBO BORA WA HIP HOP - Nje ya Box, Nick wa Pili Ft Joh Makini & Gnako
21. MSANII BORA WA HIP HOP - Fid Q
22. WIMBO BORA WA KUSHIRIKISHA / KUSHIRIKIANA - Muziki Gani, Nay wa Mitego ft Diamond
23. WIMBO BORA WA AFRIKA MASHARIKI - Tubonge, Jose Chameleone
24. MTUNZI BORA WA MWAKA TAARAB - Mzee Yusuf
25. MTUNZI BORA WA MWAKA BENDI - Christian Bella
26. MTUNZI BORA WA MWAKA KIZAZI KIPYA - Diamond
27. MTUNZI BORA WA MWAKA HIP HOP - Fid Q
28. MTAYARISHAJI BORA WA NYIMBO WA MWAKA, TAARAB - Enrico
29. MTAYARISHAJI BORA WA NYIMBO WA MWAKA, BENDI - Amoroso
30. MTAYARISHAJI BORA WA NYIMBO WA MWAKA, KIZAZI KIPYA - Man Water, Combination Sound
31. HALL OF FAME, INDIVIDUAL - Hassan BItchuka
32. HALL OF FAME, INSTITUTION - Masoud Masoud
33. VIDEO BORA YA MUZIKI YA MWAKA - Number One, Diamond
34.WIMBO WA MWAKA - Number One. Diamond
35. MTUMBUIZAJI BORA WA KIKE WA MUZIKI - Isha Ramadhani
36. MTUMBUIZAJI BORA WA KIUME WA MUZIKI - Diamond

Friday, May 2, 2014

Kiwewe, Matumaini wapona kwa Injili

WACHEKESHAJI Robert Augustino 'Kiwewe' na Tumain Martin 'Matumaini' wameamua kugeukia muziki wa Injili wakijiandaa kuachia albamu yao iitwayo 'Nimepona'.
Akizungumza na MICHARAZO hili, Kiwewe anayetamba na kipindi cha 'Ze Comedy Show' alisema kuwa albamu hiyo itakuwa na nyimbo sita na imeshakamilika ikisubiri kuachiwa mtaani.
Kiwewe alisema wameamua kumtumikia Mungu kwa kuimba kama njia ya kumshukuru kwa yote aliyowatendea tangu walipoanza kujipatia umaarufu kupitia fani ya uigizaji.
"Tumeamua kumtumia Mungu kwa njia ya huduma ya nyimbo na tunaomba mashabiki wetu watuunge mkono mara albamu hiyo itakapoingia sokoni wakati wowote kuanza sasa," alisema.
Hata hivyo Kiwewe aliweka bayana kwamba pamoja  na kuimba muziki wa Injili, yeye hajaokoka kama 'patna' wake Matumaini ambaye kwa sasa ni Mlokole akisali Mito ya Baraka.
"Sijaokoka kwa sababu siyo kila aimbaye muziki wa Injili ameokoka, ila Matumaini yeye kaokoka," alisema.
Matumaini mwenyewe alisema albam,u hiyo wameirekodia katika studuio za Levon, zilizopo Kibamba jijini Dar na kuzitaja nyimbo zilizopo katika albamu hiyo kuwa ni 'Nimepona', 'Amani ya Bwana', 'Msukule', 'Nitakutangaza Bwana', 'Mungu' na 'Anaweza Yesu' na amepanda kuiachia wiki mbili zijazo.

Mabweni Shule ya Sekondari yateketea kwa moto

MABWENI saba ya wavulana wa Shule ya Sekondari Ivumwe, mkoani hapa, inayomilikiwa na Jumuiya ya Wazazi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), yameteketea kwa moto na kuteketeza vifaa mbalimbali vya wanafunzi wa shule hiyo.

Moto huo ulizuka jana majira kati  ya saa tatu na nne asubuhi wakati wanafunzi hao wakiwa madarasani kuendelea na masomo yao.

Akitoa taarifa mbele ya Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi taifa, Abdallah Majura Bulembo, aliyefika mkoani hapa kujionea janga hilo, Mkuu wa shule hiyo, Emmery Muhondwa, alisema mbali na kuteketeza mabweni hayo, hakuna madhara ya kibinadamu.

Mwalimu Muhondwa alisema moto huo uliteketeza vitanda 93, magodoro 186, mashuka 372, blanketi 186, mabegi 186, matranker 186 pamoja na vitabu na madaftari, vyote vikiwa na jumla ya  thamani ya sh milioni 30.

“Katika kukabiliana na hali hiyo, tumewahamishia wanafunzi katika madarasa yaliyokuwa yanatumiwa na kidato cha sita ili walale humo, tumeazima magodoro 169 kutoka Shule ya Sekondari ya Loleza na tunawasiliana na wazazi ili wawanunulie nguo za kushindia na za shule huku tukiendelea kukarabati mabweni,’’ alisema Mwalimu Muhondwa.

Mwenyekiti wa jumuiya hiyo taifa, Bulembo, aliwapa pole wanafunzi na kuwataka wawe wavumilivu katika kipindi hiki.

Pia alitoa mchango aliouita wa dharura wa sh milioni tatu  kwa ajili ya ukarabati wa mabweni na mahitaji mengine ya haraka na kuahidi kuwashirikisha wadau wengine wa elimu ili kuwasaidia wanafunzi hao.

Mbali na mchango huo, alitoa tamko kuzitaka shule zote zinazomilikiwa na jumuiya hiyo kuwa na bima ya moto.

“Kuanzia sasa, suala la bima ya moto ni la lazima kwa shule zote za jumuiya ya wazazi wa CCM. Baraza Kuu tutakutana kwa dharura mjini Dodoma Mei 17, mwaka huu na tutakachokipata tutakileta haraka kwenu ili kusaidia janga hili la moto,’’ alisema Bulembo.

Mwenyekiti wa bodi ya shule hiyo, Dk. Victoria Kanama, alimshukuru mwenyekiti huyo kwa mchango wake.

“Tutahakikisha tunakarabati mabweni haya ndani ya mwezi mmoja na kufanya jitihada za kuongeza ufanisi wa ufaulu katika shule yetu,” alisema Dk. Kanama.

Ivumwe, ni kati ya shule zenye sifa ya kufaulisha ambapo katika mtihani wa utamilifu (Mock), kidato cha sita mwaka huu, shule hiyo imeshika nafasi ya pili kati ya shule 26 zilizokuwa na watahiniwa 30 Kanda ya Nyanda za Juu Kusini.
Udaku Special

Bomu lingine laua watu 10 Nigeria


mlipuko
USIKU wa kuamkia leo Maafisa nchini Nigeria wametoa taarifa kuhusu mlipuko uliotokea na kuua watu 19 katika kituo cha basi katika mji mkuu wa taifa hilo Abuja.
Kwa mujibu wa mkurugenzi wa idara ya kushughulikia mikasa na hali ya dharura- FEMA- Abbas G Idriss, watu 60 walijeruhiwa vibaya lakini 6 kati yao wametibiwa na kuruhusiwa kwenda nyumbani pia magari sita yameharibiwa katika mlipuko huo.
Mlipuko huo umetokea katika eneo la Nyanya ambao uko karibu na kituo cha basi ambako zaidi ya watu sabini waliuwawa katika shambulizi la tarehe14 mwezi Aprili.
nyanya 
Ripoti za awali zimesema kuwa watu kadhaa wameuwawa na wengine wengi kujeruhiwa,Waandishi wanasema kuwa mlipuko huo umesababishwa na bomu lililotegwa ndani ya gari,Mmoja wa walioshuhudia kisa hicho amesema aliona miili 20 ya watu waliouwawa.
Mpaka sasa hakuna kundi lililodai kuhusika katika shambulizi hilo lakini kundi la wanamgambo wa kiislamu la Boko Haram limewahi kutekeleza mashambulizi kama hayo mjini Abuja,Mengi ya mashambulizi ya Boko Haram yamekuwa yakitokea katika maeneo ya kaskazini mashariki mwa Nigeria.
Bomu la tarehe 14 Aprili lilizua hofu kwamba huenda wanamgambo hao wameanza kupanua maeneo wanayoendeleza harakati zao.

Yanga yatoa ufafanuzi sakata la usajili wa akina Domayo Azam

Didier-Kavumbagu-na-Frank-Domayo-wakisaini-kuichezea-klabu-ya-Azam-FCUongozi wa klabu ya Young Africans unapenda kuwajulisha wanachama wake, wapenzi wa soka na wadau kwa ujumla kuwa taarifa za kuhama kwa wachezai wake Didier Kavumbagu na Frank Domayo kwenda kujiunga na Azam FC zisiwakatishe tamaa, ni mapenzi ya wachezaj wenyewe kwani walishakubaliana na uongozi kila kitu juu ya kuendelea kuitumikia Yanga kabla ya siku mbili hizi kuonekana wakiwa wamejiunga na wana ramba ramba.
Yanga tayari ina wachezaji watatu wenye mikataba inayoendelea na kama kanuni za VPL kwa wachezai wa kimataifa kuwa watatu zitatumika wachezaji Haruna Niyonzima, Hamisi Kizza na Emmanuel Okwi ndio watakaoendelea, hivyo uongozi uliomba mwongozo kwa TFF juu ya taratibu zitakazotumika kwa msimu ujao kabla ya kuwasainisha Kavumbagu na Twite.
Awali uongozi wa Yanga ulikuwa kwenye mazungumzo na wachezaji hao tangu mwanzoni mwa msimu wa 2013/2014 juu ya kuongezewa muda wa mikataba yao ili waweze kuendelea kuitumika Yanga kwa ajili msimu mpya ujao 2014/2015.
Didier Kavumbagu na Mbuyu Twite ambao mikataba yao ilikuwa mwishoni waliongea na uongozi tangu mapema mwaka jana mwezi wa Septemba juu ya kuweka sahihi zao na kuendelea kuitumikia Yanga na kukubaliana mambo yote ya msingi kikubwa kilichokuwa kinasubiriwa ni maamuzi ya TFF juu ya usajili wa wachezaji wa kigeni msimu mpya wa 2014/2015 kwani Azimio la Bagamoyo linapaswa kuanza kutekelezwa msimu huu
Uongozi wa Yanga uliandikia TFF barua mapema kuomba kupewa mwongozo wa kanuni zitakazotumika kwenye usajli kwa wachezaji wa kimataifa kwa msimu mpya kufuatia Azimio la Bagamoyo kuelekeza msimu huu kila timu inapasa kuwa na wachezaji watatu wa kigeni, mpaka sasa uongozi wa Yanga haujapata majibu juu ya utaratibu utakaotumika kwenye msimu wa Ligi Kuu ijayo.
Hivyo makubaliano ya wachezaji Didier Kavumbagu, Mbuyu Twite na uongozi wa Yanga SC yalikua yakisubira majibu ya TFF juu ya kanuni zipi zitakazotumika kwenye usajili msimu wa 2014/2015 kwa wachezaji wa kigeni na katika hali ya kushangaza Kavumbagu akaonekana tayari ameshasaini kuichezea timu ya Azam FC.
Kuhusu Frank Domayo aliyeripotiwa jana kujiunga na Azam FC pia alikuwa katika makubaliano ya kuongeza mkataa tangu mwezi Julai 2013, alikubaliana na uongozi juu ya mambo yote ya msingi na kilichobakia ilikuwa ni kuweka sahihi kwenye mkataba mpya, lakini Domayo alisema hawezi kusaini mpaka siku atakapokuja mjomba wake ambaye ndie wakala wake na ahadi hiyo iliendelea kwa muda wa mwaka mzima kabla ya jana kusikia ameshasaini timu nyngine.
Habari hizi zimewashitua wapenzi, wanachama na washabiki wa Young Africans lakini ukweli ni kuwa wachezaji wenyewe walishindwa kuwa wakweli kwa viongozi na mwisho wa siku walikua na mipango yao ya kuondoka, hivyo uongozi ulijtahid kadri ya uwezo wake lakini wachezaji wanaonekana hawakua tayari kuendelea kuichezea Yanga SC.
Taarifa kamili kuhusu mipango ya timu kwa msimu ujao pamoja na ripoti ya kocha mkuu Hans pamoja na benchi lake la Ufundi zitatolewa hivi karibuni baada ya benchi la ufundi na uongozi kukaa kwa pamoja na kuafikiana mipango ya msimu ujao.
Aidha uongozi wa Yanga SC unawaomba wanachama wake, wapenzi na washabiki wasiwe na wasi wasi juu ya kuondoka kwa wachezaji hao kwani Yanga bado ina nafasi wachezaji wengi wenye vipaji na itaendelea kuboresha kikosi chake kwa kuzingatia maelekezo ya kocha mkuu Hans katika usajli wa msimu ujao

Bonite Bottlers wagawa runinga kwa wateja wao

KAMPUNI ya vinywaji baridi ya Bonite Bottlers Ltd jana ilikabidhi zawadi za luninga mpya za kisasa aina ya Sony LED zenye upana wa inchi 32 kwa washindi 29 wa shindano la Jionee Mwenyewe Kombe la FIFA la Dunia.
Katika promosheni hiyo iliyozinduliwa mapema mwezi uliopita, Coca-Cola itapeleka Watanzania 14 kwenda kushuhudia mechi ya robo fainali ya Kombe la FIFA la Dunia nchini Brazil mwezi Julai. Vile vile Coca-Cola itatoa mipira 8,000 yenye nembo ya FIFA World Cup na fulana 30,000.
Waliobahatika kushinda luninga na kukabidhiwa zawadi zao jana ni Paulina Mushi, Gabriel Warance (mwanafunzi), Moun Johnson (IT Technician), Rispa Waziri, Sophia Paulo, Abela Solomon, Chediel G. Mziray, Asha Ramadhan, Godfrey Mollel na Jackson Shayo (wafanyabiashara) na Simon Mrema (mchimba madini).
Washindi wengine ni Faidha Elidaima, Costantine Urio, Magreth Mshana, Enna Mbwambo, Emmanuel Tarimo, Julius Kimaro, Amir Ali, Emmanuel Mwasha, Gerald Swai, Joseph Mushi na Martine Temu wakazi wa mji wa Moshi.
Akizungumzia ushindi wake Gabriel Warance ambaye ni mwanafunzi jijini Arusha alishukuru Mungu kwa kumuwezesha kushinda luninga. Vile vile aliishukuru kampuni ya Bonite kwa kuleta promosheni hiyo ambayo imewawezesha wale watakaobahatika kushinda kubadili maisha yao kwa namna fulani.
Washindi wengine pia hawakusita kuonyesha furaha yao na kusema kwamba wataendelea kushiriki kwa lengo la kuendelea kushinda zawadi zaidi. “Hii ni nyota njema kwangu na naamini Mungu aliyeniwezesha kushinda zawadi hii ana uwezo wa kunipa tiketi ya kwenda Brazil kushuhudia 'laivu' fainali za Kombe la FIFA la Dunia,” alisema Godfrey Mollel ambaye ni mfanyabihashara.
Akizungumza baada ya kukabidhi zawadi kwa washindi, Meneja Mkuu wa Mauzo wa Bonite Bottlers, Christopher Loiruk aliwashukuru wateja wa Coca-Cola na wananchi kwa ujumla kwa kuendelea kuburudika na vinywaji vya Coca-Cola.
“Kombe la FIFA la Dunia ndiyo mchezo wenye mashabiki wengi zaidi duniani. Kwa kushirikisha wateja wetu katika promosheni hii, Coca-Cola itawawezesha mashabiki wa soka nchini Tanzania kuungana na wengine duniani kote kusherehekea kwa pamoja burudani ya Kombe la Dunia 2014,” anasema Loiruk
Washindi wamepatikana kwa kunywa vinywaji vya Coca-Cola na kupata vizibo viwili vyenye kutengeneza neno Brazil pamoja na kizibo cha ushindi. Kizibo cha ushindi kina picha ya kitu ambacho mteja ameshinda (TV, mpira au fulana) wakati kizibo cha ushindi wa zawadi ya tiketi kina nembo ya ndege kikiashiria safari ya kwenda Brazili kushuhudia moja kwa moja mechi ya Kombe la Dunia.

Sevilla, Benfica zafuzu fainali za UEFA Ueropa League

Stephen M'Bia akiifungia Sevilla bao muhimu lililowapeleka fainali za Europa League
Wachezaji wa Benfica wakifurahia kufuzu fainali za Europa kwa mara ya pili mfululizo
KLABU za Benfica ya Ureno na Sevilla zimefanikiwa kufuzu fainali za Ligi Ndogo ya Ulaya (UEFA Ueropa League) baada ya kupata matokeo ya kusisimua ugenini dhidi ya Juventus na Valencia.
Benfica imepenya hatua hiyo kwa mara ya pili mfululizo baada ya kuidindia Juventus mjini Turin na kutoka suluhu ya kutofungana na kufuzu kwa jumla ya mabao 2-1 yaliyopatikana kwenye mechi yao ya kwanza wiki iliyopita nchini Ureno.
Wareno hao ambao waliokuwa pungufu wachezaji wawili baada ya Enzo Perez  kupewa kadi ya pili ya njano na kufuatiwa na nyekundu dakika ya 67 na baadaye na Markovic kupewa nyekundu ya moja kwa moja dakika ya 89 sambamba na Vucinic wa Juventsu, hawajawahi kunyakua taji hilo licha ya kucheza fainali mbili za michuano hiyo sasa itavaana na Sevilla ya Hispania ambayo iliwaduwaza wenyeji wao Valencia kwa kufunga bao dakika za jioni wakati wenyeji wakionekana wameshatinga fainali za michuano hiyo.
Stephen M'Bia alifunga kwa kichwa bao muhimu kwa timu yake dakika chache kabla ya pambano hilo kumalizika na kuivusha Sevilla katika fainali hizo zitakazofanyika Mei 14 mjini Turin, Italia ambazo zitakuwa za tatu kwa timu hiyo baada ya kufanya hivyo mara mbili 2006 ilipotwaa ubingwa na na 2007.
Kabla ya hapo matumaini ya Sevilla yaliyeyuka baada ya wenyeji kuongoza kwa mabao matatu mpaka zikiwa zimesalia dakika 20 za mwisho.
Mabao ya Sofiane Feghouli katika dakika ya 14 na jingine la kujifunga kwa kipa wa Sevilla Beto katika dakika ya 26na lililowanyong'onyesha wageni katika dakika ya 70 kupitia kwa Jemery Flamin, liliwapa matumaini wageni kutinfa fainali hizo kabla ya M'bia kuwakata maini kwa bao hilo la jioni.
Matokeo ya mwisho yalikuwa 3-3, lakini Sevilla imefuzu kutokana na kupata ushindi wa mabao 2-0 nyumbani na hivyo bao la ugenini ilililopata limekuwa na faida kwao na sasa itavaana na Benfica.

Thursday, May 1, 2014

Msajili airejesha katiba ya Simba irekebishwe

Mkurugenzi wa Michezo, Leonard Thadeo
Na: Genofeva Matemu – Afisa Mawasiliano Serikalini (WHVUM)
SERIKALI kupitia Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo imemaliza kupitia Rasimu ya Katiba ya klabu ya Simba kwa ajili ya kuidhinisha katiba hiyo na kuifanya klabu hiyo kuendelea na taratibu za uchaguzi mkuu.
Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Michezo Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bw. Leonard Thadeo alipokutana na waandishi wa habari kujibu hoja mbalimbali za waandishi leo jijini Dar es Salaam.
Akijibu moja ya hoja iliyomtaka kufafanua Wizara imefikia wapi katika upatikanaji wa Katiba ya Klabu ya Simba Bw. Thadeo amesema kuwa upitiaji wa Katiba umemelizika na kuonekana kuwa na mapungufu machache yanayohitaji kurekebishwa ili Wizara iweze kuidhinisha katiba hiyo.
“Mchakato wa upitiaji wa Katiba ya klabu ya Simba umemalizika jana lakini kumekuwepo na mapungufu machache yanayohitaji kurekebishwa ili Wizara iweze kuidhinisha Katiba hiyo” amesema Bw. Thadeo.
Akifafanua zaidi Bw. Thadeo amesema kuwa mapungufu hayo yanalenga zaidi upande wa kisheria ambapo mtu anaweza kutafsiri neno vibaya hivyo kupata maana tofauti na Katiba ilivyokusudia hivyo kuitaka klabu hiyo kufanya marekebisho hayo mapema na kurejesha Katiba hiyo Wizarani kwa ajili ya kuidhinishwa.
Aidha Bw. Thadeo amewataka waandishi wa habari pamoja na wanachama wa klabu ya Simba kuwa na subira ili waweze kupata Katiba itakayokidhi malengo ya klabu yao kwani mchakato wa upitiaji wa Katiba ulihitaji umakini.

Azam yazidi kuibomoa Yanga, yambeba Domayo

Kavumbagu na Domayo walitotua Azam baada ya mikataba yao Yanga kumalizika
BAADA ya kufanikiwa kumnyakua mshambuliaji wa kimataifa wa Yanga, Didier Kavumbagu, klabu ya Azam imeendelea kuibomoa Yanga kwa kumsajili kiungo wa klabu hiyo ya Jangwani, Frank Domayo.
Domayo ambaye pia ni kiungo wa timu ya Taifa (Taifa Stars) ameingia mkataba wa miaka miwili na mabingwa hao wa Ligi Kuu ya Bara.
Kiungo huyo aliyejijengea umaarufu mkubwa klabuni hapo msimu huu akimuweka benchi nahodha wa timu ya taifa ya Rwanda, Haruna Niyonzima, amesajiliwa kutokana na kupendekezwa na kocha wa Azam, Mcameroon Joseph Omog.
"Domayo ameshasaini. Ni katika kukamilisha maelekezo ya kocha," alisema Katibu Mkuu wa Azam, Nasoro Idrisa.
Kusajiliwa kwa Domayo, kijana mdogo mwenye kipaji, kumekuwa ni pigo kubwa kwa Yanga, ambayo tayari msimu huu imevuliwa taji lake la ubingwa wa Tanzania Bara kwa matajiri hao wa Chamazi.
Azam ambao wametwaa ubingwa wa Bara kwa mara ya kwanza msimu huu wameanza usajili mapema ili kuunda kikosi cha kitakachoshiriki mashindano ya Ligi ya Klabu Bingwa Afrika mapema mwakani.
Wachezaji wengine wanaotajwa kutakiwa na Azam ni pamoja na washambuliaji wa Simba, Amissi Tambwe na Ramadhani Singano.
Hata hivyo, nyota hao wawili bado wana mikataba na klabu yao ambayo mwakani haitashiriki tena michuano ya kimataifa.
Katika hatua nyingine Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limeanza uchunguzi juu ya kitendo cha viongozi wa Azam kuvamia kambi ya Stars mjini Mbeya na kumsainisha Domayo kwa kilichoelezwa ni kwenda kinyume na taratibu za usajili.
Hata hivyo Azam siyo ya kwanza kufanya hivyo kwani Yanga na Simba walishawahi kufanya misimu iliyopita na haikufanywa uchunguzi wowote kwa nia ya kuchukulia hatua waliohusisha na ukiukwaji huo.

Atletico Madrid moto, yaiua Chelsea kwao yaifuata Real fainali Ulaya

Chelsea wakishangilia bao lao lililofungwa na Fernanndo Torres
Atletico wakipambana kuwania kutinga fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya
MEI 24 mjini Lisbon, Ureno itakuwa Fainali ya timu za jiji la Madrid, baada ya Atletico Madrid kuwafuata wapinzani wao wa jiji hilo Real Madrid kufuatia kutoa kipigo cha mabao 3-1 kwa Chelsea katika pambano la marudiano la Nusu Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Chelsea ikiwa kwenye uwanja wake wa nyumbani wa Stanford Bridge ilishindwa kuhimili makali ya wapinzani wao na kukubali kuondolewa kwa mara ya kwanza na timu za Hispania katika hatua hiyo baada ya kutandikwa huku wakishuhudiwa na gwiji wa zamani wa Argentina, Diego Maradona.
Vijana wa Mourinho walitangulia kupata bao la kuongoza lililofugwa na nyota wa zamani wa Atletico, Fernando Torres katika dakika ya 36 kabla ya wageni kusawazisha kupitia kwa Adrian dakika moja kabla ya kwenda mapumziko.
Kipindi cha pili kilikuwa kibaya kwa Chelsea baada ya Atletico kupata bao la pili lililofungwa kwa penati na Diego Costa katika dakika ya 60 kabla ya Tuiran kuongeza bao la tatu dakika ya 72 na kuihakikishia Atletico kutinga fainali za michuano hiyo kwa mara ya kwanza baada ya miaka 20 iliyopita.
Timu hiyo sasa itakutana na mahasimu wao, Real Madrid iliyowavua taji Bayern Munich juzi kwa kuicharaza mabao 4-0 nyumbani kwao na kufuzu hatua hiyo kwa jumla ya mabao 5-0 baada ya mechi ya kwanza mjini Madrid kupata ushindi wa bao 1-0.

Wednesday, April 30, 2014

Miili ya waliokufa ajali ya Singida waanza kutambuliwa

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj3HAzgI5ejXZIyNcqMJaTT85XjZvOu2bov0tWDiQnia54biJdpoDHHWW0xYFF75HuMykuls7TOCKVf843bs4_U_60SbULAnYrqhsrxDbBOguGfwBnOHWDTHZRWU8-CxwzgdZkBPuTnO7o/s1600/1.jpg
Baadhi ya miili ya watu waliokufa kwenye ajali iliyosababishwa na basi la Sumry
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEicj2zByf8m-xK1qel4ADrQklEgUEenqOL_dhOswXFx3_FS3FE-RfUGdKF6RvS0-8JPmbot7v-ZvJp6amixQ029lnaoZFqBmhCoDrQ-r7TxE-2l8fsPCRVsJd1DYmAUce3Lu2ffVOYf5Yg/s1600/2.jpg
Ndugu, jamaa na familia za marehemu wa ajali iliyosababishwa na basi la Sumry wakiwa nje ya hospitali kusubiri kutambua miili ya ndugu zao
MIILI ya watu waliofariki kwenye ajali iliyosababishwa na basi la Sumry, iliyoaua watu 19 wakiwamo trafiki wanne imeanza kutambuliwa.
Ajali hiyo ilitokea juzi kwa basi la Sumry lililokuwa linatokea Kigoma kwenda Dar baada ya kuwaparamia watu waliokuwa wakitoa msaada ya mwendesha baiskeli aliyekuwa amekufa kwa kugongwa katika kijiji cha kijiji cha Utaho, wilayani Ikungi, barabara kuu ya Singida- Dodoma.
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa Singida, Geofrey Kamwela, alisema siku ya tukio hilo wananchi wakiwa na askari polisi wa doria walikuwa wamekusanyika pembezoni mwa barabara kuupakia mwili wa mwendesha baiskeli, Gerald Zefania, aliyegongwa na lori na kufa papo hapo siku hiyo saa 1:30 jioni.
Alisema wakati wakiupakia mwili huo kwenye gari la polisi namba PT 1424 huku likiwa limeegeshwa pembeni mwa barabara, basi hilo lilitokea ghafla kwa kasi na kuwagonga watu 15 na kufariki dunia papo hapo, wengine wanne walikata roho wakati wakipelekwa hospitalini.
Kamanda Kamwela alisema dereva wa basi hilo, Paulo Njilo, mkazi wa jijini Dar es Salaam baada ya kukaribia eneo hilo aliliona gari la polisi likiwa limeegeshwa pembeni kushoto mwa barabara, lakini wakati akijaribu kulikwepa ndipo alipoliparamia kundi la watu waliokuwa na askari.
 Aidha, alisema dereva wa basi hilo baada ya ajali hiyo aliendelea na mwendo hadi aliposimama kilomita 25 katika makao makuu ya Wilaya ya Ikungi na kutokomea kusikojulikana, lakini juhudi za kumtafuta zinaendelea.
Kamanda huyo aliwataja askari waliokufa kuwa ni F.849 D/CPL Boniface Magubika wa CID Wilaya ya Singida, F.6837 Pc Jumanne Mwakihaba wa FFU Singida, G.7993 Pc, Novatus Tarimo wa ofisi ya RCO na G.8948 Pc, Michael Mwakihaba wa FFU Singida.
Wengine ni Ofisa Mtendaji Kijiji cha Utaho, Ramadhan Mjengi; Mwenyekiti wa Kijiji Utaho, Paul Hamis; Mwenyekiti wa Kitongoji cha Utaho, Ernest Salanga; Said Rajab, Usirika Itambu, Chima Mughenyi, Salim Juma, Abeid Ramadhan, Mwinyi Hamis na Issa Hussein, wote wakazi wa kijiji cha Utaho.
Kamanda Kamwela alisema miili ya marehemu wengine wanne bado haijatambuliwa na ndugu zao na imehifadhiwa kwenye chumba cha maiti katika Hospitali ya Mkoa wa Singida.
Kamanda Kamwela alisema majeruhi wawili kati ya nane wa ajali hiyo  wamelazwa katika Hospitali ya Mkoa Singida na wengine sita wapo hospitali ya Misheni Malikia wa Ulimwengu iliyopo Puma.
Aliongeza kuwa  miili ya askari polisi inatarajiwa kusafirishwa kwenda katika mikoa wanakotoka wakati wowote baada ya taratibu za kipolisi kukamilika ikiwamo kuwasiliana na ndugu zao walioko mikoa ya Kilimanjaro, Pwani, Mbeya na Iringa.

Chelsea wapata afueni, Terry, Cech warejea dimbani

http://www2.pictures.zimbio.com/gi/Petr+Cech+John+Terry+Blackburn+Rovers+v+Chelsea+jBW-c2W_Ow3l.jpg
Terry na Cech wakipongezana katika moja ya michezo yao
KIPA tegemeo wa Chelsea Petr Cech na nahodha John Terry wanatarajiwa kucheza mechi ya leo na nusu fainali ya Ligi ya mabingwa Ulaya kati yao na Atletico Madrid baada ya wachezaji hao kufanya mazoezi ya timu hiyo tangu juzi.
Ilisemekana Cech asingeweza kucheza tena msimu huu baada ya kuteua bega lake katika mchezo wa kwanza wakati Terry alitolewa nje kutokana na kuumia kifundo cha mguu katika mchezo huo uliomalizika kwa sare ya 0-0. 
Eden Hazard na Samuel Eto’o ambao walikuwa majeruhi wao pia walionekana kuwa fiti kwa kufanya mazoezi  jana, huku viungo John Mikel Obi na Frank Lampard wote hawatakuwepo katika mchezo huo wa marudiano utakaofanyika katika Uwanja wa Stamford Bridge kutokana na kutumikia adhabu ya mechi moja.
Kwa sasa imebaki maamuzi ya kocha Jose Mourinho kuona kama anaweza kuwatumia wachezaji waliorejea toka kwenye majareha kwa ajili ya mechi hiyo kuwania nafasi ya kutinga fainali kuifuata Real Madrid iliyotangulia usiku wa jana kwa kuizabua waliokuwa watetezi, Bayern Munich kwa kwa mabao 4-0.

Malawi yatua kuifuata Stars Mbeya

http://www.malawidemocrat.com/wp-content/uploads/2012/06/Flames-e1339493490888.jpg
Malawi the Flames wanaotua leo kuivaa Taifa Stars
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhXy4DjvygUby0tzSChTVErun58_E3LDqa5xJ_i2zWfMLszWFaSyC9gFEfrYDK13Z3ay7OtaoFftdVKgyeW0ng6kOwB9SLKwda42hmSDnjKljVaRMR3dk2Wg9ugd3lFENkSbBF8-a-GegEK/s1600/FKB_1718.JPG
Taifa Stars itakayoikaribisha Malawi ikiwa na kocha mpya Mart Nooij
TIMU ya soka ya taifa ya Malawi (Flames) inatarajiwa kuwasili nchini kesho kwa ajili ya mechi ya kirafiki dhidi ya Taifa Stars itakayochezwa Jumapili hii kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine mjini Mbeya.
Boniface Wambura, Ofisa Habari na Mawasiliano wa Shirikisho la Soka nchini (TFF), alisema jijini Dar es Salaam  kuwa Flames yenye msafara wa watu 31 utakaoongozwa na mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Chama cha Soka cha Malawi (FAM) itaingia Mbeya kwa usafiri wa barabara. Wachezaji katika msafara huo watakuwa 20.
Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager ikiwa chini ya Kocha mpya, Mart Nooij tayari ipo jijini Mbeya tangu juzi kujiwinda kwa mechi hiyo ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya mechi ya mashindano ya kuwania kufuzu fainali zijazo za Afrika (AFCON) dhidi ya Zimbabwe itakayochezwa jijini Dar es Salaam kati ya Mei 16 na 18 mwaka huu.
Mwishoni mwa wiki Taifa Stars iliyofinyangwa na TFF, ilitia doa sherehe za miaka 50 ya uwapo wa Tanzania baada ya kuchapwa  magoli 3-0 dhidi ya timu ya taifa ya Burundi (Intamba Murugamba) kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

As Vita, Mazembe wapangwa kundi moja Afrika

http://www.adunagow.net/main/wp-content/uploads/Mazembe.jpg
Tp Mazembe

Al Ahly
KLABU za TP Mazembe na AS Vita za DR Congo zimepangwa kundi moja la  A katika Ligi ya Mabingwa Afrika ikiwa pamoja Al Hilal ya Sudan na Zamalek ya Misri.
Kundi B la michuano hiyo limezikutanisha timu za waarabu watupu, Esperance na C.S Sfaxien za Tunisia  E.S Setif ya Algeria na Ahly Benghazi ya Libya.
Katika droo iliyotolewa inaonyesha michezo za makundi hayo zitaanza kuchezwa kati ya Mei 16 na 18 na 23 na 25, Juni 6 na 8, Julai 25 na 27, Agosti 8 na 10 na  22 na 24 huku timu zitakazoshika nafasi mbili za juu kwenye makundi zikisonga Nusu Fainali.

Wakati huo huo ratiba ya makundi kwa michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika nayo imepangwa ambapo wababe wa Yanga, Al Ahly ya Misri imepangwa kundi B linalotajwa kama la kifo.
Kundi hilo linajumuisha timu za  Sewe Sport ya Ivory Coast, Etoile du Sahel ya Tunisia na Nkana Red Devils ya Zambia.
Kundi A lenyewe lina timu za Coton Sport ya Cameroon, ASEC Mimosas ya Ivory Coast, AS Real ya Mali na AC Leopards ya Kongo Brazzaville.
Mechi za michuano hiyo zinatarajiwa kuchezwa kuanzia kati ya Mei 16 na 18 na Juni 23 na 25, Juni 6 na 8, Julai 25 na 27, Agosti 8 na 10 na 22-24 na washindi wawili wa kila kundi watasonga Nusu Fainali.
Makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika
Kundi A: TP Mazembe (DRC), Al-Hilal (Sudan), Zamalek (Misri) na AS Vita (DRC)
Kundi B: Esperance (Tunisia), CS Sfaxien (Tunisia), Entente Setif (Algeria) na Al-Ahly Benghazi (Libya).
Makundi Kombe la Shirikisho Afrika:
Kundi A: Coton Sport (Cameroon), ASEC Mimosa (Ivory Coast), AS Real Bamako (Mali) na AC Leopards (Congo)
Kundi B: Al Ahly (Misri), Sewe Sport (Ivory Coast) Etoile du Sahel (Tunisia) na Nkana Red Devils (Zambia)

Bayern chali yapigwa 4-0 kwao na kuvuliwa taji

* Leo zamu ya Chelsea na Atletico Madrid

UNAWEZA usiamini ila ndivyo ilivyo, mabingwa watetezi wa Ligi ya Ulaya Bayern Munich wamevuliwa taji hilo baada ya kukandikwa mabao 4-0 na Real Madrid na kuwafanya wababe hao wa Hispania kutinga fainali.
Mpango wa kocha Carlo Ancelotti wa kuwapanga washambuliaji wake watatu Karim Benzema, Gareth Bale na Cristiano Ronaldo ulizaa mpango baada ya Real kuisambaratisha Bavarians nyumbani kwao bila kutarajiwa na kuzima ndoto za Pep Guardiola kubadilisha matokeo ya kipigo cha bao 1-0 ilichopewa timu yake katika  mechi ya kwanza.
Mabao mawili ya Sergio Ramos na mengine ya Cristiano Ronaldo yalitosha kukwamisha safari ya wababe hao wa Ujerumani kwenye uwanja wao wa Allianz Arena na kukubali kulitema taji hilo.
Ramos alianza kufunga bao la kwanza dakika ya 16 kwa pasi ya Luka Modric kabla ya kuongeza jingine dakika nne baadaye akimalizia pasi ya Pepe na Ronaldo alikuja kupigilia msumari katika dakika ya 34 kwa pasi ya Bale na kumalizia udhia dakika ya 90 kufunga bao la nne.
Real Madrid sasa inasubiri mshindi kati ya Chelsea ya England na Atletico Madrid wanaoumana leo katika mechi ya marudiano nyingine ya nusu fainali, mechi itakayochezwa mjini London.
Katika mechi ya kwanza timu hizo ziliotoka suluhu ya kutofungana na yeyeote eatakayetumia vyema karata yake ataifuata Real kwenye fainali ya Mei 24 mjini Lisbon Ureno.

Tuesday, April 29, 2014

UEFA yazitia hatiani Man City, PSG

KLABU za Manchester City ya Uingereza na Paris Saint-Germain ya Ufaransa watakabiliwa na adhabu baada ya kukiuka maadili ya sheria ya matumizi ya fedha ya Shirikisho la Soka barani Ulaya-UEFA. 
Mbali na hao vilabu vingine vipatavyo 20 vinaaminika kukutwa na hatia ya kuvunja sheria hiyo. 
UEFA itatoa ofa maalumu kwa vilabu hivyo vilivyokiuka sheria hiyo kuelekea katika mkutano wao utakaofanyika Alhamisi. 
Adhabu kubwa ambayo ni timu husika kuenguliwa katika michuano ya Ulaya haitarajiwi kuwepo ingawa pia hawakuweka wazi ni adhabu zipi zitaazotolewa kwa timu hizo.

Rais wa Brazil amuunga mkono Dani Alves Hispania

Dani Alves aliebaguliwa Hispania na shabiki wa Villarreal
Rais wa Brazil  Dilma akiwa na Rais wa FIFA
RAIS Dilma Rousseff, amesifu kitendo cha mchezaji wa kimataifa wa Brazil, na Barcelona Dani Alves kutokana na tukio la ubaguzi wa rangi wakati wa mechi ya ligi kuu ya Uhispania, La Liga kati ya Barcelona na Villareal .
Mchezaji huyo wa Barcelona aliokota ndizi aliyokuwa ametupiwa na kuila kabla ya kuitupa na kuendelea na mchezo.
Bi Rousseff aliandika katika mtandao wake wa twitter kuwa Dani Alves alionyesha ujasiri wa kukabiliana na ubaguzi wa rangi katika kandanda na kuwa ni tukio la kuigwa .
Klabu ya Villarreal inasema kuwa imempiga marufuku mwanaume ambaye alitupa ndizi hiyo uwanjani na kuwa hatohudhuria mechi zote za nyumbani za klabu hiyo maishani.
Mamia ya watu na wachezaji maarufu duniani wameonyesha upendo wao kwa mchezaji huyo kwa kuweka picha zao kwenye mitandao wa kijamii wakila ndizi.
Mchezaji wa Manchester City Sergio Aguero alipachika picha akila ndizi sawa na nyota ya soka ya wanawake Marta .
Wengine ni Luiz Suarez wa Liverpool,Oscar, David Luiz na Willian wote wa Chelsea .
Rais wa Fifa sepp Blatter ameongezea sauti yake katika tukio la hivi punde akisema ni vibaya kwa dhulma hizo kuendelea katika karne hii.
BBC

Elias Maguli ajinadi Simba, Yanga, Azam

Elias Maguli
MSHAMBULIAJI nyota wa Ruvu Shooting, Elias Maguli amesema yupo tayari kutua klabu yoyote kati ya Simba, Yanga au Azam, iwapo ataridhishwa na dau atakalowekewa mezani na klabu hizo.
Maguli aliyeshika nafasi ya pili kwa ufungaji sambamba na Kipre Tchjetche na Mrisho Ngassa, wakiwa nyuma ya Amissi Tambwe aliyeibuka Mfungaji Bora, alisema haoni tatizo kuihama Ruvu Shooting kama kuna klabu inayomhitaji.
Alisema, ingawa mpaka sasa hakuna timu yoyote iliyomfuata kumshawishi kujiunga nayo kwa msimu ujao, lakini amekuwa akisoma na kusikia tetesi tu kuwa Simba inamnyemelea na kusema milango i wazi kwao kama wanamtaka.
Maguli, alisema siyo Simba tu bali hata kama ni Yanga, Azam au Mbeya City inamhitaji yupo tayari kujiunga nayo mradi taratibu zifuatwe na masilahi yawe ya kuridhisha kwa sababu maisha yake yanategemea soka kama ajira.
"Nisiwe muongo zijafuatwa na klabu yoyote mpaka sasa, lakini nasikia tu tetesi za kuhitaji na moja ya klabu kubwa nchini, ila mimi nategemea soka klabu yoyote iliyoridhishwa nami milango i wazi waje tuzungumze," alisema.
Kuhusu kushindwa kuendelea na kasi ya ufungaji kama ilivyokuwa kwenye msimu wa kwanza, Maguli alisema matatizo aliyokuwa nayo kwenye duru la pili ikiwamo kuuguliwa na mama yake na sakata lake la kutimka umangani kusaka soka la kulipwa lilichangia kumfanya aachwe mbali na Tambwe.
Maguli aliyekuwa akishika nafasi ya pili nyuma ya Tambwe katika duru la kwanza wakitofautiana bao moja, Tambwe akiwa na 10 yeye akiwa na 9 alijikuta akiachwa mbali na mpinzani wake huyo aliyefunga bao 19 huku yeye na wenzake wawili wakimaliza msimu na mabao 13 tu.
Aidha Maguli amesema anamshukuru Mungu kwa kuweza kuitwa kwenye kikosi cha timu ya taifa, chini ya kocha mpya kutoka Uholanzi, Mart Nooij, akidai ni furaha kwake na kuahidi kutomuangusha.
"Namshukuru Mungu, nilikuwa likizo nyumbani Mara na sasa naelekea Mbeya kwenye kambi, nimefurahi sana kocha mpya kunijumuisha kikosini.

Muumin & Double M Sound kujitambulisha Kigoma

Muumin
BAADA ya kukonga nyoyo za mashabiki wa mikoa ya Shinyanga na Kagera wakati wa sikukuu ya Pasaka, bendi iliyorejeshwa upya ya Double M Sound mwezi ujao inatarajiwa kwenda kujitambulisha kwa wakazi wa Kigoma.
Mkurugenzi wa bendi hiyo, Prince Mwinjuma Muumini aliiambia MICHARAZO kuwa, wanatarajia kwenda kuitambulisha bendi yao katika miji ya Kibondo na Kasulu iliyopo mkoani Kigoma.
Muumin alisema onyesho la kwanza mkoani humo watalifanya Mei 9 mjini Kibondo kabla ya siku inayofuata watahamia Kasulu kabla ya kurejea maskani kwao Kahama-Shinyanga kwa ajili ya kufanya mazoezi za uzinduzi rasmi.
"Tunashukuru tumerejea salama kutoka kwenye maonyesho yetu wakati wa sikukuu ya Pasaka kwa kutambulisha bendi eneo la Kakola, Ushirombo, Ruzewe, Ngara na Katoro. Kwa sasa tupo kambini mjini Kahama kujiandaa na ziara ya mkoani Kigoma mapema mwezi ujao," alisema Muumin.
Muumin aliongeza kuwa uongozi wao unajipanga kufanya uzinduzi na onyesho la kwanza kuitambulisha na kuizindua Double M Sound mjini Kahama mwishoni mwa mwezi ujao.
"Pamoja na watu kujua Double M Sound ipo Kahama, lakini hawajawahi kuiona hadharani kwa sababu tunapanga kuizindua rasmi mwishoni mwa Mei na kisha ndipo tuanze kuifanya maonyesho mjini hapa," alisema Muumin.
Double M Sound iliyowahi kutamba na nyimbo mbalimbali ilisambaratika mara baada ya uzinduzi wa albamu yao ya Titanic mwaka 2004 na Muumin ameamua kuifufua upya na kujichimbia Kahama kama maskani yake kwa sasa.

Kamanda Kova afunguka vifo vya watoto Bwawa la Kuogolea Dar

Picha haihusiani na habari, ila watoto wakifurahia kuoga kwenye bwawa la kuogolea kama wanavyuoonekana
KAMANDA wa Polisi Kanda Maalum  Suleiman Kova amefafanua juu ya taarifa ya vifo vya watoto watatu
waliofariki wakati wakiongolea kwenye bwawa la hoteli.
Kamanda Kova alisema April 27  kulitokea vifo vya watoto 3 ambao walikua na birthday party nyumbani lakini baada ya kukamilika kwa taratibu za party ya nyumbani waliamua kuimalizia party hiyo hotel ya Landmark,walipofika walienda kuogelea kwenye swimming pool ya watoto lakini baadae watoto hao walitoka kwenye pool ile ya watoto wakaingia kwenye pool ya wakubwa na kwa bahati mbaya waliingia sehemu yenye kina kirefu.
Watoto wenzao walipoona wenzao wanazama walianza kuwavuta kuwatoa nje lakini hali zao tayari zilikua mbaya, mmoja wapo hali yake ilikua kidogo afadhari lakini kwa bahati mbaya nayeye alifia hospital wakati akipatiwa matibabu katika hospitali ya Masana na kufanya Idadi ya watoto waliofariki kuwa 3 majina yao ni Janet Zacharia, Eva na Ndimbuni.
Kamanda Kova amesema; "’Kusema kweli sio mara ya kwanza kutokea, mara nyingi vifo vya watoto vinatokana na uangalifu au uzembe kutoka kwa wale wanaotakiwa kuwaangalia hao watoto wao, hizi hotel zote zenye swimming pool lile eneo la kuogelewa basi wasiruhusiwe watoto wadogo kuogelea au kuwe na mtu ambaye anajua kuogelea au kuokoa ambaye yupo pale’
‘Unajua watoto wana tabia ya kuigana mmoja akiingia akiogelea pengine anafahamu kidogo wengine wote wanafata mkumbo wanaona wanaweza,sisi kama jeshi la Polisi tumeamua hili kosa la uzembe kusababaisha kifo kisheria mtu anaweza kushtakiwa kwa kuzembea kwa kutochukua tahadhari mpaka watoto kama wale ambao hawana hatia uwezo wao mdogo wa kufikiri au kuijiokoa’
‘Tunafatilia kwa umakini lakini jukumu la kufatilia maisha ya watoto ni la wazazi mia kwa mia wasipofanya hivi wakiwa hawapo makini matokeo yake ni haya watoto 3 wamefariki,tunaendelea na uchunguzi na baadae tutatoa taarifa kamili’.

Ubingwa mweupe kwa Juventus, yaifumua Sassuolo 3-1

Wachezaji wa tatu wa Juve (jezi za njano) wakiwania mpiura na beki wa Sassuolo walipoikandika timu hiyo mabao 3-1 ugenini
JUVENTUS imebakisha mechi moja tu kutangazwa tena kuwa mabingwa wa Italia baada ya usiku wa kuamkia leo kupata ushindi mnono wa mabao 3-1 ugenini dhidi ya Sassuolo katika mfululizo wa Ligi Kuu ya nchini hiyo Seria A.
Mabingwa hao watetezi ambao Alhamis hii watakuwa nyumbani kwao kuwakaribisha Benfica ya Ureno kwenye mechi ya marudiano ya Nusu Fainali ya Ligi Ndoigo ya Ulaya (UEFA Europa League) ili kujaribu kupindua matokeo ya kipigo cha mabao 2-1, ilishtukiza kwa bao la mapema la dakika 9 la wenyeji liliwekwa kimiani na Simone Zaza.
Hata hivyo wakati wakitafakari jinsi ya kulirudisha bao hilo wenyeji hao waliwasaidia  kulisawazisha wenyewe baada ya Alessandro
Longhi kujifunga dakika ya 34.
Juventus maarufu kama kibibi kizee cha turin, iliongeza bao la pili katika dakika ya     58 kupitia Claudio Marchisio kabla ya Llorente kufunga bao la tatu katika dakika ya 76 na kuifanya timu hiyo kufikisha pointi 93, nane zaidi na ilizonazo wanaoshikilia nafasi ya pili Roma wenye pointi 85 na kila timu ikiwa imesaliwa na mechi tatu kabla ya kufunga msimu huu.

Arsenal yapumua, yaifumua Newcastle United 3-0

KLABU ya soka ya Arsenal imefufua matumaini yake ya kuwepo kwenye Top 4 na kushiriki moja kwa moja Ligi ya Mabingwa ya Ulaya bada ya usiku wa kuamkia kuitandika Newcastle United kwa mabao 3-0 kwenye uwanja wa wa Emirates, mjini London.
Mabao ya Laurent Koscielny katika dakika ya 26, Mesut Ozil aliyefunga dakika ya 42 na jingine la Olivier Giroud yaliweka Arsenal pazuri ikiwa imepata ushindi wa tatu mfululizo na kuzidi kuikimbia Everton wanaoifukuzia nafasi yao.
Arsenal waliokuwa vinara wa ligi ya England kwa muda mrefu kabla ya kuporomoka, itasubiri kujua hatma yake ya kutwaa nafasi ya nne baada ya pambano la Everton na Manchester City mwishoni mwa wiki, kama Everton itateleza kama ilivyofanya katika mechi zake zilizopita basi vijana wa Gunners watakuwa wamejihakikisha kutwaa nafasi hiyo na kucheza ligi ya mabingwa moja kwa moja.
Vijana hao wa Arsene Wenger wamekusanya jumla ya pointi 73 nne zaidi na iliyonazo Everton waliopo nyuma yao na pointi 69.

Ajali tena! Zaidi ya 15 wafariki ajalini usiku wa kuamkia leo Singida

Picha haihusiani na habari hii, lakini ni miongoni mwa mabasi ya Sumry lililowahi kupata ajali siku za nyuma.
WATU 13 akiwemo askari wa kikosi cha usalama barabarani (Trafiki) wamepoteza maisha baada ya kugongwa na basi la kampuni ya Sumry lililokuwa likitoka Kigoma kwenda Dar katika kijiji cha Ikungi mkoani Singida usiku wa kuamkia leo.
Ajali hiyo ilitokea baada ya ajali ya kwanza iliyolihusisha lori lililomgonga mwendesha baiskeli aliyepoteza maisha papo hapo na wakati wananchi wakiwa wamekusanyika eneo hilo la ajali huku trafiki akiendelea kupima ajali hiyo, lilitokea basi la kampuni ya Sumry na kuwagonga watu hao pamoja na trafiki na kupelekea jumla ya watu 14 kupoteza maisha eneo hilo.
Basi hilo lililokuwa likitokea Kigoma kwenda Dar halikuweza kusimama eneo hilo mpaka dereva wake alipokwenda kujisalimisha kituo cha polisi Ikungi, Singida. 
Miili 14 ya waliopoteza maisha katika ajali hiyo imehifadhiwa katika Hospitali ya Rufaa mkoani Singida pamoja na majeruhi wawili waliopelekwa hospitalini hapo.
MUNGU AZILAZE ROHO ZA MAREHEMU MAHALI PEMA PEPONI. AMEN!

Ronaldo, Bale, Benzama kuanza pamoja 'kuiua' Bayern, Klopp atabiri

Bale na Ronaldo
WAKATI kocha hasimu wa Bayern Munich, Jurgen Klopp wa Borussia Dortmund akiwapa nafasi kubwa mabingwa watetezi hao kutinga fainali za Ligi ya Mabingwa Ulaya, miamba wa soka wa Hispania, Real Madrid timu yenye mafanikio zaidi katika historia ya michuani hiyo  wakitwaa taji hilo mara tisa wamepania safari hii kuondokana na mzimu wa kulikosa kila mara kwa miaka 12  sasa.
Madrid imeangukia katika hatua ya nusu fainali katika michuano yote mitatu iliyopita, mara mbili ikitolewa dhidi ya timu za Ujerumani.
Borussia Dortmund waliwafunga jumla ya magoli 4-3 katika nusu fainali ya mwaka jana wakati Bayern waliwatoa kwa 'matuta' katika nusu fainali ya msimu wa 2011-12 lakini wanaingia katika mechi ya leo ya marudiano kwenye Uwanja wa Allianz Arena kwa ushindi wa 1-0, kufuatia kiwango cha juu walichoonyesha katika mechi yao ya awali mjini Madrid.
Karim Benzema alifunga goli pekee la mechi hiyo, kuipa timu ya kocha Carlo Ancelotti uongozi, lakini, licha ya hilo, watatakiwa kuwachunga Bayern ambao wamekuwa na mafanikio chini ya kocha wa zamani wa Barcelona, Pep Guardiola.
Mabingwa hao wa Bundesliga wanafukuzia kutwaa makombe matano chini Guardiola baada ya kutwaa Uefa Super Cup na Kombe la Dunia la Klabu, huku pia wakiwasubiri Borussia Dortmund katika fainali ya Kombe la 'FA' la Ujerumani la DFB-Pokal.
Bayern wamepoteza mechi nne tu nyumbani tangu mwanzo wa msimu huu, huku Manchester City na Arsenal zikiwa ni timu pekee za Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya zilizoonja mafanikio kwenye Uwanja wa Allianz Arena katika kipindi hicho, lakini Ancelotti amesisitiza timu yake itakwenda kwenye mechi hiyo ikijiamini wakati wakidhamiria kutwaa makombe matatu katika msimu wa kwanza chini ya kocha huyo Muitalia.
"Nina imani na wachezaji na nadhani kila mmoja anapaswa kuwa hivyo pia," aliuambia mkutano na waandishi wa habari wa Hispania. "Mpango wetu mjini Munich ni kufunga, kuliko kujilinda."
Ancelotti alibainisha kuwa washambuliaji watatu wa Madrid, Benzema, Cristiano Ronaldo na Gareth Bale, wote wataanza mjini Munich.
Alvaro Arbeloa, Jese Rodriguez na Sami Khedira (wote goti) ndiyo wachezaji pekee watakaokosa Real.
Beki Rafinha amerejea kwa Bayern baada ya kutumikia adhabu ya kadi katika mechi ya ligi wikiendi lakini, wakati Thiago amerejea mazoezini, Holger Badstuber (goti), Xherdan Shaqiri (paja) na Tom Starke (kiwiko) wote bado wako nje ya uwanja.
Bayern wamekuwa wakitajwa kama timu inayopewa nafasi kubwa zaidi ya kutwaa taji hilo kwa muda wote wa michuano na Guardiola anaamini kwamba mabingwa hara tano wa Ulaya wanaweza kupindua matokeo ya mechi yao ya awali.
"Ninaiamini kwa asilimia 100 timu yangu," Mcatalunya huyo aliiambia tovuti rasmi ya klabu hiyo ya mjini Munich. "Tunaweza kama tutafanya kazi pamoja."
Mshambuliaji wa Bayern, Mario Mandzukic na nyota wa Madrid, Sergio Ramos, Xabi Alonso na Asier Illarramendi watakosa fainali kama watapigwa kadi za njano katika mechi hiyo ya leo.
Licha ya kuwa bado na nafasi ya kutwaa taji hilo, staili ya uchezaji inayofundishwa na Guardiola imezidi kupoteza umaarufu na haiwavutii wakosoaji wa Bayern.
"Kumiliki mpira hakuna maana yoyote pale mpinzani wako anapotengeneza nafasi bora zaidi yako. Tuna bahati walifunga goli moja tu," alisema rais wa heshima wa Bayern, Franz Beckenbauer katika ukosoaji wake mpya alioutoa karibuni dhidi ya staili ya kucheza ya Guadiola ya tiki-taka la Kijerumani.
Katika hatua nyingine meneja wa klabu ya Borussia Dortmund, Jurgen Klopp ameipa nafasi Bayern Munich kugeuza matokeo ya kufungwa bao 1-0 na Real Madrid katika mchezo wa kwanza wa nusu fainali ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Bao la Karim Benzema lilitenganisha timu hizo mbili katika mchezo huo uliofanyika wiki iliyopita katika Uwanja wa Santiago Bernabeu baada ya Madrid kucheza mchezo wa tahadhari kubwa.
Hata hivyo, Klopp ambaye timu yake ilienguliwa na Madrid katika mzunguko wa mwisho anaamini mahasimu wao Bayern watashinda mchezo huo.
Klopp amesema bado anashawishika kuamini kuwa Bayern wanaweza kushinda hususani kwa mchezo maridadi waliouonyesha mara ya kwanza pamoja na kufungwa. Bayern na Madrid zinatarajiwa kukwaana kesho katika mchezo wa marudiano kutafuta nafasi ya kucheza fainali ya michuano hiyo itakayofanyika jijini Lisbon, Ureno.

Chelsea ilipaki mabasi mawili Anfield, kocha Liver alia

Makocha wanaofukuzana kwenye mbio za ubingwa wa Ligi Kuu ya England
MENEJA wa klabu ya Liverpool, Brendan Rodgers amemtuhumu meneja wa Chelsea Jose Mourinho kwa kupaki mabasi mawili na kuipa ushindi wa mabao 2-0 katika Uwanja wa Anfield. 
Katika mchezo huo mabao ya Chelsea yalifungwa na Demba Ba aliyetumia vyema makosa ya nahodha Steven Gerrard kipindi cha kwanza na lingine la Willian katika majeruhi. 
Kocha Rodgers amesema wapinzani wao walipaki mabasi mawili langoni mwao akimaanisha walikuwa wakizuia kipindi chote cha mchezo huo hivyo kuwapa wakati mgumu kupenya ngome yao ingawa walijitahidi kujaribu. 
Rodgers amesema walijitahidi kushinda mchezo huo lakini walishindwa kupenya ngome ya wapinzani wao ambayo ilikuwa ikilindwa vizuri. 
Pamoja na ushindi huyo Mourinho bado ameendelea kudai kuwa hawana nafasi ya kunyakuwa ubingwa wa Ligi Kuu na kudai kuwa mbio hizo wamewaachia Manchester City na Liverpool. 
Mreno huyo amesema kitu cha msingi alichokuwa akihitaji ni kupata alama tatu hizo muhimu ambazo zitawasaidia kujihakikishia nafasi tatu katika msimamo wa ligi hivyo kufuzu moja kwa moja bila kucheza mechi za mtoano katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu ujao.
Timu hiyo ya Mourinho kesho itakuwa na kibarua kizito mbele ya Atletico Madrid katika mechi ya marudiano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya hatua ya nusu fainali.
Katika mchezo wa kwanza timu hizo zilitoka suluhu bila kufungana mjini Madrid na hivyo Chelsea inapatakiwa kuhakisha inapata ushindi au sare isiyokuwa na mabao iwapo inataka kufuzu hata kwa mikwaju ya penati.