STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, September 20, 2014

Tanzania yazidi kuporomoka FIFA, Cameroon yapaa

http://imikinonews.com/files/news_images/1596757601114051870520140716101415.jpgTANZANIA imeendelea kuporomoka tena kwenye viwango vya soka vinavyotolewa kila mwezi na Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa), baada ya kuanguka kwa nafasi tano katika viwango vipya vilivyotolewa.
Tanzania, ambayo ilifungwa 2-0 na Burundi katika mechi ya kimataifa ya kirafiki iliyopita, sasa inakamata nafasi ya 115 duniani na 33 barani Afrika ikiwa nyuma ya Uganda wanaoongoza Afrika Mashariki wakiwa nafasi ya 79 duniani na 19 Afrika, Rwanda walioko nafasi ya 93 duniani na 25 Afrika na Kenya walioporomoka kwa nafasi saba wakiwa nafasi ya 30 Afrika na 111 duniani.
Aligeria waliopanda kwa nafasi nne, wanaongoza barani Afrika wakiwa nafasi ya 20 duniani wakifutwa na Ivory Coast walioshuka kwa nafasi tatu baada ya kukubali kichapo cha mabao 4-1 kutoka kwa Cameroon waliopanda kwa nafasi 12 na kukamata nafasi ya nane Afrika na 42 duniani.
Nafasi ya tatu barani Afrika inakaliwa na Tunisia (31) wakipanda kwa nafasi 11 wakifuatwa na Ghana (33), Senegal (36), Nigeria (37) na Cape Verde (41). Guinea waliopanda kwa nafasi 16 wanakamata nafasi ya tisa barani Afrika na 48 duniani huku Burkina Faso waliopanda kwa nafasi 10 wakifunga pazia la 10 bora barani Afrika wakifungana na Guinea katika nafasi ya 48 duniani.
Uganda pia ni wa kwanza katika Ukanda wa Cecafa wa Afrika Mashariki na Kati wakifuatwa na Rwanda, Kenya, Tanzania, Burundi, Ethiopia (39, 132), Sudan (40, 133), Shelisheli (47, 172), Sudan Kusini (50, 185), Eritrea (52, 202), Somalia (53, 204) huku Djibouti wakifunga mlango Cecafa na Afrika wakiwa 54 Afrika na 205 duniani.
Mabingwa wa dunia, Ujerumani wanaongoza 10 bora ulimwenguni wakifuatwa na Argentina, Colombia waliopanda kwa nafasi moja wakiwashusha Uholanzi, Ubelgiji, Brazil, Uruguay, Hispania, Ufaransa na Uswis.

Spurs walalamikia ubaguzi, wenyeji wao waomba radhi

Roberto Soldado
Patashika baina ya Spurs na Partizan

partizan banner
Bango lililoibua hisia za kibaguzi ambalo Spurs wamelalamikia UEFA
Jan Verthongen (R) challenges Partizan Belgrade"s Danko Lazovic UONGOZI wa klabu ya Tottenham Hotspurs limepeleka malalamiko yao Shirikisho la Soka la Ulaya, UEFA kufuatia kuonyeshwa kwa mabango yenye kulenga ubaguzi na mashabiki wa Partizan Belgrade. 
Meneja wa Spurs Mauricio Pochettino ameelezea bango hilo kama jambo lisilokuwa na heshima na lisilokubalika. 
Spurs walishindwa kutamba ugenini baada ya kulazimishwa suluhu na wenyeji wao katika Uwanja wa Partizani, nchini Serbia.
Maofisa wa Spurs waliwataarifu UEFA juu ya uwepo wa bango hilo kabla ya mapumziko na wajumbe wake walilipiga picha kama ushahidi baada ya mchezo huo. 
Mwaka 2007, Partizan walitolewa katika michuano ya Kombe la UEFA na kutozwa faini kwa vurugu wakati wa mchezo wa mkondo wa kwanza wa michuano hiyo dhidi ya Zrinjski Mostar.
Tayari uongozi wa klabu ya Partizan imeomba radhi kwa kitendo hicho kilichofanywa na mashabiki wao kupitia mabango hayo.

Friday, September 19, 2014

Gareth Bale bado aiwaza Spurs, ahidi kurejea

Gareth Bale alihama Spurs masimu uliopita
http://www.guinnessworldrecords.com/media/6352324/Gareth-Bale-main.jpgWINGA machachari wa Real Madrid, Gareth Bale amezungumzia dokezo la kurejea Tottenham hapo baadaye.
Nyota huyo aliondoka White Hart Lane msimu uliopita kwa rekodi ya dunia ya uhamisho na ameendelea kuimarisha kiwango chake nchini Hispania.
Lakini licha ya kuonekana ametulia ndani ya kikosi akiwa sambamba na Cristiano Ronaldo ndani ya Bernabeu, Bale amesema bado anaipenda Tottenham.
"Tottenham siku zote itaendelea kuwepo ndani ya moyo wangu. Natumaini mashabiki bado wananipenda inagawa nimeondoka," alisema wakati akiongea na BT Sport.
"Nawapenda mashabiki wa Spurs. Huwezi jua ninaweza kurejea siku moja".

Katibu Mkuu Coastal Union 'kizimbani' TFF

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEidwGRi1aPjw1qjpMuqsiRm93wW18DNvNp1gaFYbTH62Y62_VqCRs0oedrMlVZCVHvy_F_78HnKGR-gNSi1rd5OCqL9qGZsX8j08cjXxgxR_ALYQVBcQX7Ph4gHer_s7CxbVAmwr6Q69L_u/s640/DSC04297.JPG
El Siagi (katikati)
KATIBU Mkuu wa Coastal Union, Kassim El Siagi atafikishwa kwenye Kamati ya Maadili ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kwa kushinikiza mkutano wa wanachama wa klabu hiyo ufanyike bila kuandaliwa na Kamati ya Utendaji. Pia El Siagi alitumia vyombo vya habari kuishambulia TFF ambayo haikutambua uamuzi wa mkutano huo ulioelezwa kumdumaza Makamu Mwenyekiti wa klabu hiyo Steven Mnguto. TFF ilimtuma Mkurugenzi wake Msaidizi wa Sheria na Uanachama kufanya uchunguzi wa mgogoro uliokuwa unaendelea katika klabu hiyo. Baada ya kupokea taarifa ya uchunguzi huo, TFF imebaini kuwa Mwenyekiti na Mweka Hazina wa klabu hiyo walishajiuzulu, hivyo uitishwe uchaguzi haraka na kujaza nafasi hizo na nyingine zilizo wazi.
Pia wajumbe wa Kamati ya Utendaji ya Coastal Union, Salim Amir na Albert Peter wameonywa kwa kushiriki katika mkutano ambao wanajua haukuandaliwa na Kamati ya Utendaji.
Vilevile uchunguzi wa TFF umebaini kuwa ushiriki wa Salim Bawazir na Akida Machai kwenye vikao vya Kamati ya Utendaji ya Coastal Union si halali kwa vile wajumbe wa kamati hiyo wanachaguliwa na Mkutano Mkuu na si kuteuliwa na Mwenyekiti.
Kwa vile kutakuwa na uchaguzi wa kujaza nafasi ambazo zipo wazi, uchaguzi huo utasimamiwa na Kamati ya Uchaguzi ya Coastal Union kwa kushirikiana na Kamati ya Uchaguzi ya TFF, na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Tanga na Coastal Union watafanya uhakiki wa reja ya wanachama.

Hujuma mechi ya Stars, Mambas kuchunguzwa

http://shaffihdauda.com/wp-content/uploads/2014/07/10s.jpgSHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) limepokea kwa masikitiko makubwa taarifa zilizoandikwa kwenye baadhi ya Vyombo vya Habari zikielezea tuhuma za hujuma kwa timu ya Taifa (Taifa Stars) katika mechi za kufuzu mashindano ya AFCON. TFF pamoja na kutokuwa na uthibitisho wa tuhuma hizi nzito haliwezi kuzikalia kimya. TFF itateua jopo la kuchunguza tuhuma hizi. Wanafamilia wa mpira wa miguu Tanzania (Members of TFF Family) watakaohitajika kuhojiwa na jopo hilo kwa mujibu wa Ibara ya 37 ya Kanuni za Maadili za TFF watalazimika kutoa ushirikiano. 
Atakayeshindwa kutoa ushirikiano atachukuliwa hatua za kimaadili. 
Pia wadau wa mpira wa miguu ambao sio wanafamilia wa TFF, watakaoitwa na jopo hili wanaombwa watoe ushirikiano kwa nia ya kujenga mpira wetu.

Uongozi Yanga kitanzini, TFF yaipa wiki 2

http://www.eatv.tv/sites/default/files/styles/detailpageimg/public/field/image/yangaa%20clement.JPG?itok=3lkNdTVBSHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) limeitaka klabu ya Yanga kuwasilisha rasimu ya Katiba waliyoipitisha, kwa kuzingatia kuwa Muhtasari wa kikao cha Mkutano Mkuu wao wa Juni 1 mwaka huu umeainisha baadhi ya marekebisho waliyofanya kwa tulivyowaelekeza.
Yanga wanatakiwa kuwasilisha rasimu hiyo kabla ya Oktoba 5 mwaka huu. Ikiwa itakubaliwa na TFF, itapelekwa kwa Msajili wa Klabu na Vyama vya Michezo ili waweze kufanya uchaguzi wa viongozi wao.

Kivumbi England, Arsenal kesho, Man City, Chelse J'pili

http://img.eplmatches.com/2014/06/premier-league.jpg
KIVUMBI cha Ligi Kuu ya England kinatarajiwa kuendelea tena kesho wakati Arsenal watakapokuwa ugenini kuvaana na wenyeji wao Aston Villa, huku kazi nzima ikiwa Jumapili.
Arsenal iliyotoka kukong'otwa mabao 2-0 na Borussia Dortmund katika Ligi ya Mabingwa Ulaya watawafuata Villa ambayo haijapoteza mchezo wowote mpaka sasa ikiwa nafasi ya pili katika msimamo nyuma ya Chelsea wanaoongoza wakiwa na pointi 12, Villa ikiwa na 10.
Arsenal inayokamata nafasi ya saba itahitaji ushindi ili kurejea kwenye mbio zao za kutaka kutwaa ubingwa licha ya kukabiliwa na majeruhi katika kikosi chao.
Mechi nyingine za kesho Jumamosi zitakuwa ni kati ya vibonde QPR waliozabuliwa mabao 4-0 wiki iliyopita na Manchester United itakapokuwa nyumbani kuialika Stoke City, huku Liverpool itaifuata West Ham ikiwa inaugua kipigo ilichopewa wiki iliyopita na Aston Villa.
Ratiba kamili ya kesho ni;
14:45 QPR v Stoke  
17:00 Aston Villa v Arsenal
17:00 Burnley v Sunderland
17:00 Newcastle v Hull
17:00 Swansea v Southampton
19:30 West Ham v Liverpool
Jumapili  
15:30 Leicester v Man United  
15:30 Tottenham v West Brom
18:00 Everton v Crystal Palace
18:00 Man City v Chelsea
Ratiba nyingine ya ligi hiyo;
Jumamosi Septemba 27  
14:45 Liverpool v Everton
17:00 Chelsea v Aston Villa
17:00 Crystal Palace v Leicester
17:00 Hull v Man City
17:00 Man United v West Ham
17:00 Southampton v QPR
17:00 Sunderland v Swansea
19:30 Arsenal v Tottenham
Jumapili Septemba 28
18:00 West Brom v Burnley
Jumatatu Septemba 29  
22:00 Stoke v Newcastle

Jose Mourinho aanza mikwara yake England

http://cdn2.crhoy.com/wp-content/uploads/2014/06/Mou1.jpg 
SAA chache kabla ya kuvaana na mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya England, Jose Mourinho a.k.a Only Special' ameanza zake.
Meneja huyo wa Chelsea amedai hana tatizo katika kikosi chake na kwamba wapo kamili gado kuivaa  Manchester City Jumapili katika mchezo utakaochezwa katika Uwanja wa Etihad. 
Mourinho ameshuhudia kikosi chake kikishinda kila mchezo wa Ligi Kuu msimu huu lakini waligonga mwamba kwa Schalke Jumatano wakati walipolazimishwa sare. 
Hata hivyo, Mourinho anaamini Chelsea ina uwezo wa kuwafunga mahasimu wao hao katika mbio za ubingwa na kusisitiza wanajiamini kwa uwezo wao kuelekea katika mchezo huo. 
Kocha huyo kutoka Ureno, 51 amesema siku zote ni jambo zuri kucheza dhidi ya timu kubwa kwani inafanya kazi yake kuwa rahisi. 
Kocha huyo aliendelea kudai kuwa wanaiheshimu City kwasababu wanastahili lakini wao pia wanajiamini kufanya vyema katika mchezo huo.

MCT yalaani 'uhuni' wa Polisi kwa waandishi wa Habari

We unajifanya mjuaji eeh?
Hivi ndivyo baadhi ya askari wetu wanavyoshindwa kuthamini kazi za watu wengine. Hapa wakimsulubu mwandishi wa habari katika tukio la jana ambalo MCT limelilaani.

Kumekucha Ligi Kuu Tanzania Bara 2014-2015

Watetezi Azam watakuwa nyumbani kuialika Polisi Moro


Yanga wenyewe watakuwa Moro kucheza na Mtibwa, watatoka salama?
Simba wataanza kibarua chao Jumapili dhidi ya Coastal Union
JKT Ruvu wenyewe watakuwa Mbeya kupepetana na Mbeya City
FILIMBI ya kuanza kwa kivumbi cha Ligi Kuu Tanzania Bara 2014-2015 kinatarajiwa kupulizwa rasmi kesho wakati viwanja sita vitakapowaka moto kwa kushuhudia timu 12 kati ya 14 zitakapoanza mbio za kuufukuzia ubingwa wa ligi hiyo.
Kuanza kwa ligi hiyo kutatoa picha halisi ya tambo na mbwembwe za timu wakati wa usajili kwani kwa kuwa soka ni mchezo wa hadharani mashabiki watajua mbivu na mbichi juu ya vikosi hivyo.
Kwa miezi minne klabu 14 za ligi hiyo zimekuwa zikitambiana kuhusu vikosi ilivyosajili na kujigamba kwa matokeo ya mechi kadhaa za kirafiki za kujiandaa na ligi hiyo, hata hivyo tija na ukweli wa ufanisi wa usajili huo utafahamika baada ya kuanza kwa ligi hiyo kesho.
Kwa mujibu wa ratiba ya ligi hiyo, mabingwa watetezi Azam ambao wiki iliyopita walishindwa kufurukuta mbele ya Yanga katika mechi ya Ngao ya Jamii, itakuwa dimba la nyumbani kupepetana na maafande wa Polisi-Moro waliorejea kwenye ligi hiyo katika pambano litakalochezwa uwanja wa Chamazi.
Yanga wenyewe wakiwa na kocha mpya Marcio Maximo kutoka Brazili watakuwa uwanja wa Jamhuri Morogoro kupepetana na wenyeji wao, Mtibwa Sugar ambao hawajawahi kupoteza mchezo wowote kwenye dimba hilo mbele ya Yanga tangu mwaka 2009.
Ratiba Kamili ya kesho;
Septemba 20,2014.
Azam FC vs Polisi Moro [Azam Dar es Salaam] Mtibwa Sugar vs Yanga [Jamhuri, Morogoro] Stand United vs Ndanda FC [Kambarage, Shinyanga] Mgambo JKT vs Kagera Sugar [Mkwakwani, Tanga] Ruvu Shooting vs  Prisons [Mabatini, Mlandizi] Mbeya City vs JKT Ruvu [Sokoine, Mbeya] JUMAPILI:
Simba v Coastal Union [Taifa, Dar es Salaam]

Wembley kutumika Nusu Fainali Ulaya 2020

https://www.daytona.co.uk/news_images/WEM_007936.jpgSHIRIKISHO la Soka Ulaya, UEFA limethibitisha kuwa Uwanja wa Wembley uliopo jijini London Uingereza ndiyo utakaotumika kwa mchezo wa nusu fainali na fainali ya michuano ya Ulaya 2020. 
Viwanja vya Hampden Park na Dublin Aviva vilivyopo jijini Glasgow, Scotland vinatarajiwa kutumika kwa ajili ya mechi za hatua ya 16 bora na mechi tatu za hatua ya makundi. 
Chama cha Soka nchini Uingereza,FA kilishinda nafasi hiyo baada ya Shirikisho la Soka la Ujerumani-DFB kujitoa muda mchache kabla ya kura za UEFA na kuamua kuhamishia nguvu zao katika kutafuta nafasi ya kuandaa michuano hiyo mwaka 2024. 
Michuano ya mwaka 2020 UEFA imefanya kuwa maalamu hivyo itaandaliwa katika viwanja 13 kutoka miji tofauti barani Ulaya. 
Mechi za robo fainali na tatu za hatua ya makundi zitaandaliwa jijini Munich, (Ujerumani), Baku (Azerbaijan), Roma (Italia) na St Petersburg (Urusi). 
Miji mingine itakayoandaa mechi 3 za makundi na moja ya mkondo wa pili ni Copenhagen (Denmark), Bucharest (Romania), Amsterdam (Uholanzi), Bilbao (Uhispania), Budapest (Hungary) na Brussels (Ubeljiji).

Maskini Arsenal yamkosa Debuchy wiki 6

http://ep.imgci.com/PICTURES/CMS/72200/72245.3.jpgIMETHIBITIKA kuwa, beki wa kulia wa Arsenal, Mathieu Debuchy atakuwa nje ya dimba kwa muda wa wiki sita hali inayozidi kuiweka pabaya klabu hiyo.
Meneja wa Arsenal, Arsene Wenger amesema Debuchy atakaa nje ya uwanja kwa kipindi hicho kutokana na kuumia kwake kifundo cha mguu. 
Beki huyo wa kimataifa wa Ufaransa ambaye alitolewa nje kwa machela katika mchezo dhidi ya Manchester City Jumamosi iliyopita anaweza kukosekana kwa miezi mitatu kama itahitajika kufanyiwa upasuaji. 
Wenger alithibitisha hilo na kudai kuwa matokeo zaidi watayajua katika siku chache zijazo baada ya kufanyiwa vipimo zaidi kuonyesha jinsi eneo hilo lilivyoathirika. 
Calum Chambers,19 anatarajiwa kuchukua nafasi ya nyota huyo mwenye umri wa miaka 28 katika mchezo wa kesho dhidi ya Aston Villa. 
Debuchy aliyejiunga na Arsenal akitokea Newcastle United Julai mwaka huu amecheza katika mechi zote saba za timu hiyo msimu huu ukiwemo mchezo wa Ngao ya Jamii dhidi ya Manchester City. 
Beki mwingine kinda Hector Bellerin,19 ndio aliyeingia kucheza nafasi ya upande wa kulia katika mchezo wa Jumanne waliofungwa na Borussia Dortmund kwa mabao 2-0 katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya.

Hatari! Mke wa mtu afa kwa hawara Dar

MWANAMKE Jane Bhoke (27) amefariki dunia nyumbani kwa hawara yake.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Mary Nzuki alisema kifo hicho kilitokea juzi saa 12 jioni eneo la Zingiziwa Chanika wilayani Ilala.
Kamanda Nzuki alisema mtoa taarifa, Mohamed Kambi (44) mkazi eneo hilo alieleza kwamba alikutana na marehemu Septemba 12 mwaka huu katika kilabu cha pombe za kienyeji huko Chanika.
Kambi alisema baada ya kukubaliana walianza kuishi kama mke na mume na huku akibainisha kwamba walifanya mapenzi mara mbili.
“Septemba 15 saa 11 jioni mtoa taarifa na marehemu walikwenda magengeni kununua mahitaji ghafla marehemu alianguka akawa analalamika mguu wa kulia unamuuma… katika harakati za kupunguza maumivu alimeza dawa aina ya diclopa,” alisema kamanda.
Alisema hali ya mgonjwa haikubadilika na ilipofika Septemba 16 saa 10 jioni alifariki dunia huku akibainisha kwamba haifahamiki marehemu ni mkazi wa wapi.

Thursday, September 18, 2014

Tamasha la Magari kufanyika Leaders

http://swahili.cri.cn/mmsource/images/2008/12/10/20080718094020385b.jpg 
Na Suleiman Msuya
KAMPUNI ya  Jast Tanzania Limited kwa kushirikiana na Jossekazi Auto Garage and General supplier wameandaa tamasha la kwanza la Magari la aina yake, linalojulikana kwa jina la Automobile Clinic, ambalo linatarajiwa kufanyika kwa siku mbili mfululizo katika viwanja vya Leaders jijini Dar es salaam.
Tamasha hilo limelenga katika kutoa huduma ya kitaalamu ya kiufundi kwa wenye magari (Checkup and Fix) kutoka kwa mafundi stadi ambao wamebobea katika fani ya ufundi wa makenika katika aina tofauti tofauti za magari.
Akizungumza na vyombo vya habari, kwenye ukumbi wa habari Maelezo, Joseph Mgaya mmiliki wa Jossekazi Auto garage amesema tamasha hili lina lengo kuwakutanisha mafundi stadi na wenye magari, kwa gharama nafuu sana ya shillingi elfu ishirini tu.
Mgaya alisema huduma hizo ambazo zilipaswa kugharimu kiasi kikubwa sana cha pesa kwa wenye magari, kitatolewa kwa bei nafuu ili kwa makusudi tu ya kukutanisha mafundi hao na wenye magari,.
Alisema pamoja na Wateja kutengenezewa Air condition na kujaziwa gesi, kufanyiwa Electronical scan diagnosis, Kuchekiwa Matairi, kuchekiwa Battery, na kupata ushauri wa kiufundi kuhusu gari zao, pia tamasha hilo litakuwa ni sehemu ya kukutanisha watu na kupata burudani. 
Mgaya alisema, Mafundi wapatao 50 waliobobea katika fani ya ufundi magari, wamepatikana baada ya kufanyiwa usaili wa kina na kupitia mchujo na semina elekezi ili kuweza kuhudumia magari yanayokadiriwa kufika zaidi ya 6000 kwa siku hizo mbili.
Pamoja na hayo, Mgaya alisema “ Tumeandaa warsha maalum kwa kina dada, tunatambua kuwa asilimia kubwa ya waendesha magari barabarani hivi sasa ni kina dada, tunataka waelewe ni nini cha kufanya pindi atakapopatwa na hitilafu kwenye gari mabarabarani. “
Elimu hii ambayo wameiita ‘Auto First Aid’, alisema itasaidia kupunguza uharibifu zaidi kwenye magari yao,  alisema wakati mwingine kwenye deshboord ya gari kuna kuwa na alama za hatari, lakini kwa kuwa gari inatembea wanawake wengi wamekua wakipuuzia alama hizo na matokeo yake wanasababisha hasara kubwa zaidi.
“Pamoja na kuwafundisha alama za hatari na nini cha kufanya pindi waonapo alama hizo pia Tutawafundisha kubadilisha matairi, na nini chakufanya na kuwa nacho ikitokea gari limewaharibikia njiani. “ alisema Mgaya.
Mgaya ambaye amefanikiwa sana katika ufundi wa AC za magari, Ndege, na Meli, aliongeza kuwa fani ya ufundi makenika ni kazi ya kuheshimika kama zilivyo kazi nyingine, na kuongeza kuwa anaiona fursa kubwa kwa vijana wanaomaliza elimu ya juu.
“Siku hizi magari yote kuanzia Mwaka 2005 kwenda juu yanatumia vifaa maalum vya computer na internet, pamoja na kuwa maelezo yanakuja kwa lugha ya kingereza, ufundi spana wa kurithishwa hivi sasa hauna nafasi,”alisema.
“Tofauti na zamani ukifeli form 4, unapelekwa kwenye ufundi hali hivi sasa imebadiliilka fani hii inahitaji wasomi na watu wanaoweza kubadilika na kurudi shuleni kila mara, kama computer matoleo ya magari kila mwaka yanakuja na vitu tofauti, hivi sasa break hazina annoying sound, break zikiisha utaona kwenye dashboard, kutengeneza lazima useme user manual ya kingereza na u download soft ware kwenye internet,” alisema Mgaya na kusistiza vijana waingie kwenye fani hii. 
Aidha Mkurugenzi wa Jast Tanzania Limited, Jahu Mohammed Kessy, Mratibu wa Tamasha hilo walisema kuwa, Automobile Clinic litakuwa zaidi ya Tamasha.
“Katika kuhakikisha tunautumia muda wa wateja wetu vizuri, wakati gari inafanyiwa ufundi, kutakuwa na huduma nyingine za ziada zitakazo patikana siku hizo mbili, kutakuwa na vinywaji, vyakula kama nyama choma, na michezo ya watoto, kutakuwa na huduma ya kulipia ya kuoshewa magari, kusafishiwa taa, na baadhi ya vifaa kama Fire extinguisher, manukato ya gari, Triangle na kadhalika vitauzwa hapo uwanjani,” 
Jahu alisema Tiketi zitauza kabla, na kwamba tiketi hizo zitakuwa katika mfano wa sticker ya kubandika kwenye magari, na zitapatikana katika vituo vyote vya kuweka mafuta vya TSN, Supermarket zote za TSN, Kwenye ofisi za Millembe insurance, Bon to shine, BM hair cutting salon, na Mlimani City.
“Hakutakuwa na Kiingilio kwa watu, lakini badala yake kwa magari, magari yenye sticker pekee ndiyo yatakayoruhusiwa kuingia na kupata huduma hizo, tunashauri wenye kununua sticker wafike mapema kwani watakao fika kwanza ndio watakao hudumiwa,”
Jahu alisema katika kurudisha kwa jamamii, mafundi hao hamsini baada ya Tamasha watatembelea kwenye hospitali ya CCBRT kusaidia wakina mama wenye matatizo ya fistula.
Tamasha hilo limedhaminiwa na Milembe insurance, Wambi lube oil distributor, TSN, Binslum tires company Limited, I view, Cocacola, Dreams Limited, Hugo Domingo, Olduvai Bay Wash, 0-60 autogarage, Meku Auto spear part, Dick Sound, Brand Tiger, Clouds FM, Auto Beats, Neh Catering, Pamoja na Lim Painting and decorating.

Sunday, September 14, 2014

Manchester United yaanza Ligi yaifumua QPR

Di Maria akishangilia bao lake
1410710470161_lc_galleryImage_14th_September_2014_Barcl
Furaha ya ushindi Manchester wakifurahia baada ya kuypata moja ya mabao yao
Mata akishangilia bao lake
NYOTA wapya wa Manchester United, Ander Herrera na Angel di Maria walithibitisha thamani yao baada ya kuiwezesha timu yao kupata ushindi wa kwanza msimu huu katika mashindano kwa kuilaza QPR kwa mabao 4-0 katika mfululizo wa Ligi Kuu ya England.
Di Maria aliwainua mashabiki wa Old Trafford kwa kufunga bao la kwanza katika dakika ya 24 kabla ya Herrera kupachika la pili katika dakika ya 36 akimalizia kazi ya nahodha Wayne Rooney.
Dakika moja kabla ya mapumziko, nahodha huyo Rooney alifunga bao la tatu akimalizia kazi murua ya Herrera na bao la mwisho la vijana wa Luis Van Gaal lilifungwa na Juan Mata katika dakika ya 58 kwa kazi safi ya Di Maria aliyeonyesha ubora wake na kuifanya Mashetani Wekundu kupumua baada ya kuanza vibaya ligi na msimu mzima kwa ujumla.
Radamel Falcao aliingia uwanjani katika kipindi cha pili na kuonyesha makeke yake ikiwa ni mara ya kwanza tangu asajiliwe kutoka Monaco.

Yanga ya Maximo kiwangoo! yaiua Azam x3

Mrisho Ngassa akijaribu kumtoka Erasto Nyoni wa azam (Picha zote kwa hisani ya Habari Mseto )
Kikosi cha Azam kilichozimwa Taifa leo
Kikosi ch Yanga kilichotwaa Ngao ya Hisani leo kwa kuilzaza Azam
 KLABU ya Yanga iliyo chini ya kocha Marcio Maximo wa Brazil, jioni ya leo imetuma salamu kwa klabu nyingine za Ligi Kuu Tanzania Bara baada ya kuifumua bila huruma watetezi wa ligi hiyo, Azam mabao 3-0 katika pambano la Ngao ya Hisani lililochezwa kwenye uwanja wa Taifa.
Yanga ikiwa katika kiwango cha juu na kuwafunika wapinzani wao, walithibitisha kuwa bado ni wababe wa Azam katika mechi ya Ngao ya Hisani baada ya kuifdunga kwa msimu wa pili mfululizo kwani msimu uliopita waliitambia kwa bao 1-0.
Mabao yaliyoizamisha Azam waliotwaa ubingwa wa ligi msimu uliopita bila ya kupoteza mchezo wowote yalitumbikizwa wavuni na Gelinson Santana 'Jaja' aliyefunga mabao mawili na kuzima ngebe za mashabiki waliokuwa wakimzomea kabla ya Simon Msuva kufunga jingine akitokea benchi kumpokea Nizar Khalfan.
Kipigo hicho cha Azam kimevunja rekodi ya kocha Joseph Omog pamoja na vijana wao ambao walikuwa wakifurahia kushinda au kutoka sare bila kupoteza mchezo wowote tangu mwaka jana katika mashindano nchini Tanzania.

Hofu yatanda Arsenal kuumia kwa Debuchy

Gunners manager Arsene Wenger has admitted that Mathie Debuchy's injury 'doesn't look good'
Arsenal defender Mathieu Debuchy screams in pain after injuring his ankle against Manchester CityKLABU ya Arsenal ipo katika hofu kubwa baada ya beki wake wa kulia Mathieu Debuchy ameumia vibaya na haijajulikana bado  atakaa nje ya kiwanja  kwa muda gani  .
Kocha  Arsene Wenger amesema majeraha ya  Debuchy’s  ‘Hayaonyeshi' kupona upesi na kuna hitajika kufanyika uchunguzi wa kina zaidi waweze kugundua atakaa nje kwa muda gani .
Mchezaji huyo alianguka vibaya na kukanyaga kifundo chake cha mguu wa kushoto katika kipindi cha pili cha mchezo kati ya Arsenal na Manchester City ulioisha kwa sare ya 2-2.
Debuchy, 29 alijiunga na  Arsenal katika majira ya kiangazi akichukua nafasi ya Bacary Sagna,aliyejiunga na  Man City, na alicheza vizuri katika mechi na klabu yake ya zamani katika uwanja Emirates.

Yanga, Azam leo hapatoshi Taifa katika Ngao ya Jamii

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj0OMIi84tDpx05S0PI2fuo0AE_ulzrjGm81vlt-VnfTTM5dO-IxD-GT-W5iOY3rW6KOsIt72oAKVP2adJndh_oTt8BMN6leXVkHUnX5tP_KMFYkNc362P0lRT8ck1Iz7KiBY4fWKa1aGKV/s1600/YANGAVSAZAM.jpgMWISHO wa tambo na mikwara baina ya Azam na Yanga ni leo wakati klabu hizo mbili zitakapopepetana kwenye mechi ya Nf\gao ya Jamii kuashiria kuanza kwa msimu mpya wa Ligi Kuu Tanzania Bara.
Timu hizo zitapambana kwenye uwanja wa Taifa, huku zote zikiwakosa baadhi ya nyota wake kutokana na kuwa majeruhi.
Yanga inatarajiwa kumkosa kiungo wake mahiri, Andrey Coutinho aliyeumia katika mechi ya kirafiki dhidi ya Polisi Dar es Salaam kwenye uwanja wa sekondari ya Loyola.
Mshambuliaji huyo alipatwa na maumivu hayo wakati alipokuwa akijaribu kupiga mpira na hivyo kushindwa kuendelea na mchezo. Timu hizo zilitoka suluhu.
Azam ambao walilala bao 1-0 katika mechi kama hiyo kwa msimu uliopita, haitakuwa na huduma ya nahodha wake, John Bocco Adebayor aliye majeruhi pia, kwa mujibu wa Meneja wa Azam Said Jemedari.
“Tunao majeruhi wawili, ambao hawatakuwepo kwenye programu ya mchezo wa Ngao ya Jamii, ambao ni beki Waziri Salum na nahodha wetu, John Bocco,”alisema Jemedari.
Timu hizo zinakutana baada ya mwaka jana kushuhudia Azam wakiipindua Yanga na kuwanyang'anya ubingwa wakiwa hawajapoteza mchezo wowote.
Mechi hiyo itaanza saa 10 kamili jioni, na kiingilio hicho cha sh. 5,000 ni kwa viti vya rangi ya kijani na bluu vitakavyochukua jumla ya watazamaji 36,000 katika uwanja huo wenye viti 57,558.
Viingilio vingine katika mechi hiyo ambayo itatumia tiketi za elektroniki ni sh. 10,000 kwa viti vya rangi ya chungwa, sh. 20,000 kwa viti vya VIP C na B wakati viti vya VIP A kiingilio ni sh. 30,000.

Simba yabanwa na Ndanda Fc Mtwara

Simba SC
Ndanda Fc
SIMBA imeendelea kwenda mwendo wa kusuasua katika mechi zake za kujiandaa kwa michuano ya ligi kuu ya Tanzania Bara baada ya jana kulazimishwa kutoka suluhu na Ndanda FC.
Katika mechi hiyo ya kirafiki iliyochezwa kwenye Uwanja wa Nangwanda Sijaona mjini Mtwara, vijana wa Ndanda waliwabana vyema wapinzani wao katika vipindi vyote viwili.
Sare hiyo imekuja siku chache baada ya Simba kuchapwa bao 1-0 na URA ya Uganda katika mechi ya kirafiki ya kimataifa iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Kama ilivyokuwa katika mechi dhidi ya URA, mshambuliaji Emmanuel Okwi alishindwa kuonyesha makeke yake kutokana na kubanwa vyema na mabeki wa Ndanda. Okwi aliingia kipindi cha pili kuchukua nafasi ya Abdalla Seseme.

Warembo Miss Tanzania 2014 wawasili kambini

Na Father Kidevu 
Wanyange 30 wanao wanbia taji la Redd's Miss Tanzania 2014 leo wameingia kambini tayari kwa safari ya fainali za Miss Tanzania 2014 zitakazo fanyikia mapema mwezi Oktoba jiji Dar es Salaam.


Warembo hao waliowasdili kwa muda tofauti kuanzaia saa 12 alfajiri ya leo na kupokelewa na waandaaji wa Miss Tanzania katika hoteli ya JB Belmont iliyopo katikati ya jiji la maraha la Dar. 
Warembo kutoka Kanda ya Ziwa walitia fora pale warembo hao walipowasili kambini hapo wakiwa ndani ya gari ya Mshindi wa Kanda ya Ziwa ambayo alizawadiwa hivi kjaribuni katika shindano lao.
 Warembo wa Kanda ya Ziwa wakiteremka katika gari lao baada ya kuwasili na inaelezwa waliendesha kutoka jijini Mwanza.
 Warembo wa Kanda ya Ziwa wakijiandikisha baada ya kuwasili kambini.
 Warembo wakielekea chumba cha mkutano.
 Warembo wakiwa katika chumba cha semina ambapo maelezo mbalimbali ya ka,mbi yao yalitolewa.

Shinji Kagawa aanza na mguu mzuri Borussia Dortmund

Japan international Shinji Kagawa (right) celebrates after his goal at the WestfallonstadionKIUNGO mshambuliaji wa zamani wa Manchester United, Shinji Kagawa amedhihirisha ukali wake baada ya kurejea Borussia Dortmund kwa kishindo kwa kuisaidia timu hiyo kupata ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Freiburg katika Ligi Kuu ya Ujerumani Bundesliga.
Kagawa aliyekaribishwa vyema na mashabiki wa klabu hiyo kwa mabango na bendera ya Japan, alifunga bao moja na kuchangia nyingine lililokuwa la kwanza kwa timu yake lililotumbukizwa wavuni na Adrian Ramos.
Ramos alilipa fadhila kwa kumtengeneza Mjapani huyo aliyepachika bao la pili katika ya 41 na kuifanya wenyeji kwenda mapumziko wakiwa mbele kwa mabao 2-0.
Bao la tatu la Dortmund iliyoimuuza Kagawa kwa Mashetani WEkundu kabla ya kumrudisha hivi karibuni liliwekwa kimiani katika kipindi cha pili na Aubameyang  dakika ya 78 kabla ya wageni kupata bao la kufutia machozi dakika ya 90 kupitia Sorg.

Real Madrid yafa nyumbani, Neymar aibeba Barcelona La Liga


Atletico Madrid's Arda Turan scores
Kitu hicho! Atletico Madrid wakiwaadhibu wenyeji wao
Cristiano Ronaldo
Hawaamini kama ni kweli wamepigwa
Cristiano Ronaldo scored a penalty in Real Madrid's 2-1 defeat against Atletico Madrid on Saturday
Ronaldo akifunga mkwaju wake wa penalti
MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu ya Hispania, Atletico  Madrid wameendeleza ubabe wake kwa Real Madrid baada ya kuinyuka  mabao 2-1 Uwanja wa Bernabeu mjini Madrid, katika mchezo wa ligi hiyo.
Atletico waliwashtukiza wenyeji wao kwa kuandika bao la kuongoza dakika ya 10 tu ya mchezo huo kupitia kwa Tiago.
Wenyeji walicharuka na kusawazisha dakika sita baadaye kupitia kwa Cristiano Ronaldo aliyefunga kwa penalti na kufanya hadi mapumziko mambo yawe 1-1.
Atletico walirejea tena nyavuni mwa wenyeji wao kwa kuandika bao la pili na la ushindi katika dakika ya 76 kupitia kwa Arda Turan aliyemaliza kazi nzuri ya Raul Garcia. 

Katika mechi nyingine za ligi hiyo, Barcelona walipta ushindi nyumbani dhidi ya Athletico Bilbao kwa kuwalaza mabao 2-0.
Mabao yote ya wenyeji wakiwekwa kimiani katika kipindi cha pili na nyota wa Kibrazil, Neymar.
Ijumaa timu za Almeria na Cordoba zilitoshana nguvu kwa kufungana bao 1-1, wakati katika mechi nyingin e za jana,Malaga na Levante zilishindwa kutambiana kwa kutoka suluhu huku Celta Vigo na Real Sociedad zikitoka 2-2.

Coastal, Mtibwa kuzionolea makali Simba, Yanga

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEih8GIhwPpFvx9y37-dG5TLICcp_KCiphSP1VYgwX79MDr9R3tnTWyceiGkEuX9A89bxtFoklDDQtYSmrAox361CSsxPLNO0QiOzOiXFjYBym8OfCB3s-9GgU3KnI0_8FXHv919Cb0oO1Xk/s640/DSCN0138.jpg
Coastal Union
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgbodZ0IJ3DDDukQkZOD3uBBhFnRyS_36bTNfa2lByCz4hi3do7n2ffnbHwJPZ7M927cjrGC4zHIdMWa_k0r-eR3D8YaAO8lvvkkH17E8Xf7I_WhVKdmiJ87gem7uKakkwoXHDsRcIjqCQC/s640/MTIBWA+SUGAR.jpg
Mtibwa Sugar
MABINGWA wa zamani wa soka nchini Coastal Union ya Tanga na Mtibwa Sugar ya Morogoro zinatarajiwa kupimana ubavu leo katika pambano la kirafiki litakalochezwa kwenye uwanja wa Mkwakwani.
Mechi hiyo ni ya mwisho mwisho kwa klabu hizo kabla ya kujichimbia kambini kujiandaa na msimu mpya wa Ligi Kuu Tanzania Bara itakayoanza rasmi Jumamosi.
Kocha mkuu wa Coastal, Yusuph Chipo ametamba kuwa mchezo huo utakuwa kipimo kizuri kwa timu yake ambayo ilijichimba Pemba, na kugawa dozi nene kwa timu pinzani za Zanzibar ilizocheza nayo ambazo kisoka ni tofauti na timu za Tanzania Bara.
Chipo alisema huo utakuwa ni mchezo kwa kikosi chake kabla ya kuinolea makali Simba watakaofungua nao dimba Jumapili.
Mkenya huyo alisema pia mechi hiyo ni nafasi yake ya kupata kikosi cha kwanza kabla ya kuelekea kwenye Ligi Kuu.
"Baada ya mchezo wa Jumapili na Mtibwa Sugar nitatoa tathmini ya wachezaji, ikiwemo kupata kikosi cha kwanza katika timu,"alisema Chipo.
Kwa upande wa Mtibwa kupitia Msemaji wake, Thobias Kifaru naye alitamba kwamba mechi hiyo ni muhimu kwa benchi lo la ufundi kujiweka tayari kuinza ligi kuikaribisha Yanga kwenye uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro siku ya Jumamosi ijyo.
"Tupo kamili kwa ajili ya kuonyesha burudani kwa mashabiki wa Tanga sambamba na kuipa makali timu yetu kabla ya kuvaana na Yanga," alisema Kifaru.

Nyatawe 'awafunda' wenzake, ataka wajiheshimu

MUIGIZAJI mahiri wa filamu nchini aliyewahi kutamba na makundi ya Shirikisho Msanii Afrika, Happy Mkamwa 'Nyatawe' amewataka wasanii wenzake wa kike kupenda kujiheshimu na kujithamini ili nao waheshimiwa na kuthaminiwa na jamii.
Aidha aliwataka wasanii nchini kwa ujumla kuwa wabunifu na kuumiza vichwa ili kutoa kazi ambazo zitabamba anga la kimataifa.
Akizungumza na MICHARAZO, Nyatawe alisema wasanii wa kike wanapaswa kujitambua wao ni  nani ndani ya jamii na hivyo kuwa mfano bora kuanzia mavazi yao, matendo na hata kwa kauli zao ili kujijengea heshima mbele ya jamii inayowazunguka.
Alisema kuendelea kufanya mambo ya ovyo yanawashushia heshima na kufanya wadharaulike.
"Wasanii wa kike wa leo ndiyo wazazi na walezi wa kesho wa familia hivyo ni wajibu wetu kuwa makini kwa kila tunalofanya au kulitamka, ili kujenga heshima na hadhi zetu," alisema.
Pia aliwakumbusha wasanii kupenda kuwa wabunifu katika kazi zao pamoja na kujituma kwa bidii ili mwishowe waje kutamba kimataifa badala ya kuridhika na mafanikio ya nyumbani.

Sikinde sasa kuzindua Jinamizi lao Oktoba

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgyQvJbNPmPY9Zp7MmXibkXD186MC54L8sZ79WM1IZ_KxdV5R5Wh9ZWSAd3-nx1OZIXAfVweaIncxaslL1wDR3VQuRmdKX2u7M6swKmwLhBJ4W2tcShvII75vxkD5IjN7HNy3v0uowGg6s/s1600/sikinde.JPGBENDI kongwe ya muziki wa dansi nchini, Mlimani Park 'Sikinde' inatarajia kuzindua albamu  yake mpya ya 'Jinamizi la Talaka' mwishoni mwa Oktoba baada ya kushindwa kufanya hivyo  mwezi uliopita.
Aidha bendi hiyo inatarajiwa kufanya ziara ya kimuziki katika mikoa ya Morogoro na Dodoma  wiki ijayo kwa ajili ya kuzitambulisha nyimbo zao mpya za albamu hiyo kwa mashabiki wa mikoa  hiyo.
Msemaji Msaidizi wa Sikinde, Emmanuel Ndege aliiambia MICHARAZO kuwa baada ya kukwama  kufanya uzinduzi wao Agosti kama ilivyokuwa imetangazwa, Sikinde sasa inatarajiwa kuzindua  albamu yao mpya katika maadhimisho ya miaka 38 ya kuanzishwa kwa bendi hiyo.
Ndege alisema kwa sasa wanaendelea kufanya mchakato wa wadhamini kabla ya kutangaza rasmi  tarehe ya jambo hilo, japo alisisitiza itakuwa mwishoni mwa Oktoba.
"Uzinduzi wa albamu yetu mpya utafanyika Oktoba sambamba na maadhimisho ya miaka 38  tangu kuanzishwa kwa Sikinde," alisema Ndege.
Pia aligusia juu ya ziara ya kimuziki wanaotarajia kuifanya wiki ijayo katika mikoa ya Morogoro na  Dodoma ili kutambulisha nyimbo zao mpya kwa mashabiki wa bendi hiyo wa mikoa husika.
"Tupo katika maandalizi ya kwenda kuzitambulisha nyimbo za albamu yetu mpya katika mikoa ya  Dodoma na Morogoro, tukiwa huko pia tutakumbushia nyimbo za zamani za bendi hiyo zilizoipa  Ubingwa wa Muziki wa Dansi Tanzania," alisema Ndege