STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, September 27, 2014

Barua ya wazi kwa Wajumbe wa Bunge la Katiba kutoka Zanzibar

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhOkLsciXf-74G8GIdbS_htvzslWBy8miIPYzTL96vqTVCU_0Tg1cOReOW6eT0QjqSONTsFX3mfXtU9sxZ6p14UIXghJu9H5CZcjNo-wlAeSz-A8BWvps1Lmj_8MrM-CgwAe0rLJ8Kl2LPx/s1600/WABUNGE+WAKIPITIA+RASIMU+YA+MAPENDEKEZO+YATAKAYO+TUMIWA+NA+KIKAO+CHA+BUNGE+LA++KUJADILI++RASIMU+YA+KATIBA.JPG
Assalam alaykum
Natumai hamjambo ndugu, kaka na dada zangu. Inshallah Mwenyenzi Mungu akupeni afya na uzima kuelekea kipindi hiki muhimu cha kupiga kura kuamua Katiba Inayopendezwa na pia Mola akupeni busara na maamuzi mema.
Nakuandikieni barua hii kama Mzanzibari mwenzenu sina zaidi ya hilo. Ni kutokana na Uzanzibari wangu nimeona kuwa nijaribu kukuaidhini, kunasihini, kukushawishini, kukusemeshini, kukuombeni kuwa msiikubali Katiba Inayopendekezwa na muipigie kura ya HAPANA.
Tafadhalini wekeni mbali ushindani, itikadi na mitazamo ambayo inatutenganisha Wazanzibari na muamue kwa maslahi makubwa, mapana na ya muda mrefu ya Zanzibar. Msitizame tulipojikwaa bali tizameni tulipoanguka. Msitizame nyuma mkahesabu visa na mikasa ila nyinyi hapo mlipo ndio wenye fursa ya kuikoa, kuinusuru na kuihuisha Zanzibar.

Naam, ni kura ya HAPANA ndio ambayo itaibakisha, itaiokoa, itaisimamisha Zanzibar. Mjue mkipigia kura ya NDIYO maana yake ni kuwa Zanzibar tuipendayo inazidi kupungua, kuchukuliwa na kumezwa kama ambavyo imekuwa khofu yetu kwa miaka kadhaa ya Muungano huu.
Nataka muamini ndani ya dhati yangu mimi ni muumini wa Muungano. Nataka Muungano wa haki na hadhi sawa baina ya Washirika wa Muungano – Tanganyika na Zanzibar- ili kila nchi ipate fursa sawa za kuhudumia watu wake.
Wengi wenu kwa kauli zenu mara kadhaa mmekuwa mkisema Muungano hauakisi hali ya usawa, haki na hadhi sawa lakini mkawa mnatumia neno KERO kuwasilisha fikra zenu hizo, na wengi tukawa na matumaini kwamba fursa hiiya kuunda upya Katiba yetu itapunguza kama si kuondosha kabisa KERO hizo.
Ila baada ya kuiona Katiba inayopendekezwa nimeona kuwa andiko hilo halina msaada, halina muelekeo na halina wema na Zanzibar. Kulikubali andiko hilo ni kujitia kitanzi wenyewe na sasa imekuwa ni kusokotwa, kubanwa na kudhibitiwa Zanzibar lakini mara hii itakuwa kwa kujitakia wenyewe.

Huko nyuma tumekuwa tukisema kuwa kumekuwa na hadaa, sijui ujanja, sijui ghalat,sijui unyemela wa kuongeza Mambo ya Muungano ambayo yamekuwa yakipunguza madaraka ya Zanzibar, lakini mara hii tunajichinja wenyewe kwa mikono yetu.
Hii ilikuwa ni fursa kubwa kwetu kusimama kama Zanzibar. Zanzibar ilipaswa kusimama kama kundi zima ndani ya Bunge na kukaa na kundi zima la upande wa pili yaani Tanganyika, na watu wa pande mbili hizi kuamua umbo, hadhi na sifa gani tunataka Tanzania iwe.
Hili la pande mbili lilikuwa lisionewe aibu kwa sababu ndio ukweli na uhalisia kwamba tuko pande mbili. Haiwezekani kuwa na Muungano, ambapo upande mmoja una kila sifa za kuwa nchi, halafu upande mwengine uwe na sifa za kuwa dola na nchi ifichwe ndani yake.

Ilikuwa ni nafasi nzuri kwa Zanzibar kudai haki zake, stahiki zake, fursa zake ili iweze kukidhi mahitaji ya watu wake, maana hata kama tumo ndani ya Muungano basi bado tuna chumi mbili zinazoshindana na kwa kweli zinazopigania na kunyang’anyiana rasilmali karibu zile zile.
Ilikuwa ni wakati wa kufanya kila njia ili Zanzibar ijitengenezee fursa ya kuwa na mafanikio kama ya Visiwa vya Seychelles au Mauritius ambavyo wastani wa kipato cha mwananchi wa nchi hizo mbili ni zaidi ya dola 14,000 na dola 15,000 mtawalia.
Najua hoja itakuja basi haya yangefanywa kwa umoja, na mbona umoja huo haukuwepo, nakiri kuwa hilo kweli limetokea, lakini ni kama katika mchezo iwapo mchezaji mmoja ametolewa ama kwa kuonewa na mwamuzi au kwa kitendo chake cha makusudi, haina maana kuwa waliobakia uwanjani wakubali kupoteza mchezo, badala yake hujibidiisha kushinda ili iwe njia moja ya kumsuta mwenzao aliyetolewa na sifa kwa kweli inakuja kwa waliobakia uwanjani.
Kwa kuendelea kujigandisha katika ubavu, kuendelea kuamini kuwa hatuwezi kujitegemea na kwa hivyo mambo kadhaa kuyabakisha katika Muungano ni kujiviza akili, ni kujidhalilisha kimkakati na kujidogosha kihadhi.
Si kweli na si kweli kabisa kuwa Katiba Inayopendekezwa ina maslahi na Zanzibar. Haina, haina katu, haina Abadan, kamwe haina. Ni katiba ambayo inatuweka pabaya na pagumu zaidi na imeendelea kuyachukua mamlaka ya Zanzibar na kuyatia katika Muungano.

Vipi Katiba hii itakuwa na maslahi na sisi? Hebu tutizame mambo machache:
1. Kundosha au kuukataa mfumo wa Shirikisho ina maana
a) Zanzibar haiwezi kuwa na hadhi na haki sawa na Serikali ya Muungano.
b) Tumejibakisha pale pale Zanzibar haina mshirikia mwenziwe kwenye Muungano
c) Tumerudi pale pale mshirika wa Zanzibar ni Tanzania na kwa hivyo hakuna usawa
d) Tumeganda pale pale kuwa Tanganyika inasimamiwa na Serikali ya Muungano
e) Tumesalia papo kuwa Bunge la Muungano linatunga sheria za Tanganyika na tunajua kuwa sheria kama hizo hazina nguvu Zanzibar
f) Tumejizuga vile vile kumwita Waziri wa Muungano hata asiesimamia jambo la Muungano kama kilimo bila ya kuwa na hadhi kama hiyo.
g) Tumekwama pale pale Mahakama Kuu ya Tanganyika inaitwa ya Muungano
h) Tumejidanganya vile vile wafanyakazi wote wa Tanganyika wanabaki ni wa Muungano na wale wa Zanzibar mwisho wao Chumbe.

Fikiria hii ndio Zanzibar tuitakayo?
2. Tunajipa moyo kuwa kumfanya Rais wa Zanzibar kuwa ni Makamo wa Rais wa Muungano kuna manufaa kwa Zanzibar ilhali hakutakuwa na msaada wowote.
Tumewapa watu matumaini kuwa hilo litawezesha Rais wa Zanzibar akitoka nje atakuwa na hadhi ya kimuungano wakati tunajua hilo litaleta utata mkubwa zaidi huko mbele. Kwanza kwa suala la gharama pili kutakuwa na mgongano wa maslahi na majukumu yake kama Rais wa Zanzibar vs Umakamo wa Muungano

3. Haiwezekani Rasimu Inayopendekezwa iwe imenyofoa mamlaka zaidi yaliokuwa yameanza kuikaribia Zanzibar kutokana na Rasimu ya Warioba, halafu isemwe kuwa kuna maslahi kwa Zanzibar.
a) Kuondoa uwezo wa Zanzibar kuunda Benki yake
b) Kurudisha nguvu za kuigawa Zanzibar kwa Rais wa Muungano
c) Kukubali ardhi kurembwa
d) Tumerudisha suala la Tume ya Pamoja ya Fedha ambayo imeshindikana kwa miaka kadhaa toka nia hiyo ilipotiwa kwenye Katiba ya 1977.
4. Uamuzi wa kuyatia madaraka ya Serikali ya Zanzibar ndani ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano ilhali hakuna sehemu yoyote ya Katiba Inayopendekezwa ambapo madaraka ya Serikali ya Tanzania Bara kama inavyoitwa yameainishwa ni kuendelea kujidanganya.

Pili, kwa kufanya hivyo tunarudi tena pale pale ambapo Zanzibar inaonekana inakiuka Katiba ya Jamhuri pale inapotaka kufanya mabadiliko yenye maslahi yake, ilhali jambo kama hilo halionekani na wala halipo kwa upande wa mshirika mwenziwe, maana mshirika ni huyo huyo Serikali ya Jamhuri na Serikali ya Tanzania Bara.
Ndugu, kaka na dada zangu ujue wazi kuwa maamuzi unayotaka kuyafanya ni makubwa na yana athari ya muda mrefu kwa vizazi vingi vya Zanzibar, ambayo pamoja na tofauti zetu, lakini naamini tunakubaliana kuwa Zanzibar tuipendayo iwepo. Na kuwepo kwake lazima iwe na nguvu na matao yake.
Na kwa dalili zote Rasimu Inayopendekezwa inapopotoa nguvu na matao ya Zanzibar. Inaondosha uzuri na haiba yake kwa kuifanya kuwa ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano badala ya kuwa ni nchi moja kamili ndani ya Muungano huu.

Fikirini, pimeni na muvuke nje ya itikadi na mitizamo. Fanya uamuzi ili nafsi yake iwe na amani kwa sababu umefanya uamuzi wako bila ya shindikizo, maelekezo au utashi wa kisiasa, maana wewe kwanza ni Mzanzibari kisha mengine ndio yanafuata.
Nawaomba radhi kwa uamuzi huu wa kuandika barua ya wazi maana isingewezekana kumfika kila mmoja wenu, lakini nataka muamini kuwa barua hii nimeiandika kwa sababu nimeona kuna wajibu kwangu kufanya hivyo.
Unapotaka kupiga kura fikiria, wazia na pimia juu ya uzito wa mchoro wako mmoja tu wa kalamu utavyokuwa na athari kwa nchi yako, watu wako na watoto na wajukuu wako. Fumba macho, rudisha nyuma fikra zako,
kumbubuka wema na ihsani za waliokuzunguka, uliokuwa nao pamoja katika maisha yako na uwafikirie khatma njema ya muda mrefu.

Kumbubuka jukumu lako kwa Mwenyenzi Mungu na fikiria kama hicho ni kitendo cha mwisho cha maisha yako ili ukitie katika mizania nzuri ya maamuzi yako.
Piga HAPANA kwa faida ya Zanzibar na usinitizame mimi kama Ally Saleh, la. 

Mimi ni mtu mmoja tu tena tunaweza kuwa tuna mzigo wa tofauti zetu, lakini pamoja na yote mimi na wewe ndio Zanzibar.
Kwa maslahi ya Zanzibar piga HAPANA.

Ally Saleh
Zanzibar

Kocha Liverpool akiri Balotelli bado sana, japo amemsifu Anfield

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhz4XqJAAKnprDJap4_tn1QZtE-90nE7JVa1KXPPSo34ulgKddta1D1UPbRVLDhilRX1FxRY0gMqnVBAMwH97o56EtYPXHAVmH_AE1iGygVEZivYIp7SRNaIE-ui9fyJ4BEMaiUxyiG8m5u/s1600/baloooooooooo.jpgMENEJA wa klabu ya Liverpool, Brendan Rodgers amekiri kuwa Mario Balotelli bado hajafikia hadhi ya kiwango cha dunia lakini amemuunga mkono kuwa anaweza kuvaa viatu vya Luis Suarez na kufanya vitu vikubwa Anfield. 
Suarez aliuzwa Barcelona kwa kitita cha euro milioni 88 katika usajili wa kiangazi huku nafasi yake ikizibwa na Balotelli aliyesajiliwa akitokea AC Milan kwa kitita cha euro milioni 20. 
Rodgers anaamini kuwa nyota huyo wa kimataifa wa Italia anapswa kufuata nyayo za Suarez akiwa hapo na kuonyesha thamani yake akiwa kama mshambuliaji. 
Rodegrs amesema pamoja na kwamba Balotelli hajafikia hadhi ya kiwango cha dunia lakini hana shaka na kipaji chake kwani ana uwezo wa kufikia huko kama akitilia maanani kazi yake hiyo.

Nasibu Ramadhani, Moh' Matumla kumaliza ubishi leo Manzese

  MABONDIA Nasibu Ramadhani na Mohammed Matumla wakitunishiana misuli jana wakati wakipimwa uzito. Mabondia hao wanatarajiwa kuonyeshana kazi leo kwenye ukumbi wa Friends Corner -Manzese Dar.
Mratibu wa mpambano wa ngumi Ibrahimu Kamwe katikati akiwangalia mabondia wa kike Lulu Kayage kushoto na Fatuma Yazidu wanavyo tunishiana misuli baada ya kupima uzito kwa ajili ya mpambano wao
Lulu Kayage na Fatuma Yazidu wakitambiana baada ya kupima uzito
Bondia Nassibu Ramadhani akipima uzito kwa ajili ya mpambano wake na Mohamedi Matumla

Mohamed Matumla akipima uzito
Bondia Nassibu Ramadhani na Mohamed Matumla wakinuliwa mikono juu na Mratibu wa mpambano huo Ibrahimu Kamwe katikati  mpambano utakaofanyika leo Jumamosi hii katika ukumbi wa Friends Corner Manzese
Bondia Juma Fundi na Issa Omari wakinuliwa mikono juu na Mratibu wa mpambano huo Ibrahimu Kamwe katikati  mpambano utakaofanyika jumamosi hii katika ukumbi wa Friends Corner Manzese
Bondia Lulu Kayage akipimwa na Daktari baada ya kupima uzito kushoto ni mpinzani wake Fatuma

Kocha Mkwasa apata ulaji TFF baada ya kurejea umangani

ALIYEKUWA kocha wa Yanga, Charles Boniface Mkwasa 'Master' ameteuliwa kuwa Ofisa Mtaalamu wa Elimu ya Mafunzo wa Shirikisho la Soka Tanzania, TFF.
Katibu wa TFF, Selestine Mwesigwa ameithibitisha juu ya Mkwasa kupewa nafasi hiyo baada ya kurejea kutoka Uarabuni, alipokwenda kufundisha klabu.  
Kwa upande wake, Mkwasa, amesema kuwa amekwishaanza kazi yake hiyo mpya TFF na anatarajia kuifanya kwa ufanisi kwa sababu ana utaalamu nayo.
Juu  ya mkataba wake na Yanga, Mkwasa alisema kwamba wakati anakwenda Uarabuni alipewa likizo ya mwaka mmoja, kwa sababu amerudi kabla ya muda huo ameona bora kukubali kazi hiyo ya TFF kuliko kukaa bure.  
“Kama Yanga SC watanihitaji kurudi kazini kabla ya muda huo, ni suala la kuzungumzika tu, kwa sababu TFF ipo kwa ajili ya maendeleo ya soka hapa nchini na Yanga ni klabu ya Tanzania,” amesema Mkwasa.
Mkwasa alijiunga na Yanga Desemba mwaka jana akitokea Ruvu Shooting ya Pwani, lakini baada ya msimu Mei mwaka huu akaondoka pamoja na aliyekuwa kocha Mkuu wa klabu hiyo, Mholanzi Hans va der Pluijm kwenda Uarabuni.  
Hata hivyo, baada ya muda mfupi wa kufanya kazi huko, Pluijm aliyemchukua Mkwasa kwenda naye huko- akatofautiana na uongozi wa timu na kusitishiwa mikataba.

Jackson Chove apigwa 'stop' VPL, kisa....!

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhygAN_AuPouzgtENYfVB6K9r_XT4puGs9mNJfCn6tOCsHGCVRWrpBA-fODZAj9nLzU1DQRHdz56xrsadm5UVEe7NZs7nqK16sVVLf7g2SXrk7nryIBpvpkO0zc541qNmiTEWXe83XFzXY/s640/Chove.jpg
Chove (Kulia) wakati akiichezea Coastal Union. TFF imemzuia kucheza mpaka ithibitishwe usalama wa afya yake
SHIRIKISHO la Soka Tanzania, TFF, limetangaza kumpiga 'stop' kipa wa JKT Ruvu, Jackson Chove 'Mandanda' kushuka dimbani kwa usalama wake.
Mandanda aliumia na kuzimia kwa zaidi ya dakika 10 katika mechi ya kwanza kati ya JKT Ruvu ilipokuwa ikiivaa Mbeya City mjini Mbeya.
Katika mechi hiyo ya ufunguzi wa Ligi Kuu Bara, timu hizo zilimaliza kwa sare ya bila kufunga.
Rais wa TFF, Jamal Malinzi amesema hadi Chove atakapowasilisha vipimo vyake kwa shirikisho hilo nalo kuviwasilisha kwa wataalamu ili kujiridhisha kama yuko sawa.
“Kitendo cha mtu kuzimia kwa dakika 15 si kidogo, tungependa kuhijirisha.
“Lakini tunawashauri wenzetu wa klabu kuhakikisha wanalizingatia suala la kuwapima wachezaji wao kwa kuwa mchezo wa soka si kitu lahisi,” alisema Malinzi.
Timu nyingi za Ligi Kuu Bara na hata ligi nyingine, zimekuwa hazifanyi vipimo vya uhakika kwa wachezaji wake kabla ya kuanza kwa ligi hiyo.

Kivumbi VPL, Simba 'gonjwa' kujiuliza kwa Polisi leo, Yanga kesho


Simba itavuna nini kwa Polisi Moro leo ikiwa na mapengo ya nyota wake
Mbeya City kubanana na Coastal

Mtibwa Sugar itavuna nini kwa Ndanda leo Jamhuri!

Ndanda kuendeleza undava hata kwa Mtibwa Sugar?
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiSj4wlWkv-2AQE3IvC1lX7uW_YO4cl9SxwZ5CWEb_t6__r6sDF2d3ovOJWyqVLDiwy-L-rNeVRe-yAbQRMvxc_V9CnsdKwnuFbVntE9lWfsQhXGQRqoM1ip_aLhfFCQnaSsb1U4ve9bYY/s1600/AZAM+FC.JPG
Mabingwa watetezi Azam watakaovaana na Ruvu Shooting
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg3IlGghMl999NBu1mDQnXx12kxWnPimfDRgGEQ3V4-WggiKqkjyA4pqjRh3EqwZW7Ec6uQpM6R_oUmTgNptp87AxXdjOHieFee6ZG0UmDU-9_DRxDGCYYobQzKOQBLdTPBiOgTbAFu4FM/s1600/cb4a0-1375766_581274061909694_1850204431_n-Copy.jpg
Prisons-Mbeya kuendeleza ubabe wa Yanga

Simba itawamudu maafande wa Polisi Moro?
JKT Ruvu nao kibarua chao kipo kesho kwa Kagera Sugar

Yanga wenyewe kazi yao ni kesho kwa Prisons
KLABU ya Simba ikiwa  bila ya nyota wake wanne, Paul Kiongera, Haruna Chanongo, Issa Rashid 'Baba Ubaya' na kipa Ivo Mapunda inatarajiwa kushuka dimba la Taifa jioni ya leo kupepetana na Polisi Morogoro, huku kocha wake Patrick Phiri akichekelea pambano lao na Yanga kusogezwa mbele wiki moja.
Simba iliyoanza na sare ya 2-2 dhidi ya Coastal Union wiki iliyopita wakati wakiwa mbele kwa mabao 2-0 watawakosa wachezaji hao muhimu katika kikosi cha kwanza kutokana na kuwa majeruhi, hata hivyo kocha Phiri ametamba wachezaji waliosalia kikosini wapo tayari kuisambaratisha Polisi waliorejea ligi kuu tena.
Polisi inayonolewa na nyota wa zamani wa Yanga, Pan Afrika na Taifa Stars, Mohammed Rishard Adolph, ilikaribishwa ligi hiyo kwa kipigo cha mabao 3-1 na Azam wiki iliyopita na leo itakuwa ikitaka kurekebisha makosa, licha ya ukweli pambano hilo ni gumu kwao.
Phiri alinukuliwa wasingependa kurejea makosa ya wiki iliyopita kwa kuhakikisha wanapata ushindi leo ili kujiweka pazuri kabla ya mechi yao ya mwisho kuisubiri Yanga ambapo aliongelea kusogezwa mbele kwa pambano hilo la watani kutoka Oktoiba 12 hadi Oktoba 18 ni faraja na nafuu kubwa kwao.
Pambano la watani limesogezwa mbele kwa wiki moja toka ratioba ya awali ili kupisha mechi ya kirafiki ya kimataifa kati ya timu ya taifa, Taifa Stars dhidi ya Benin.
Ukionoa pambano la Simba na Polisi ratiba ya ligi hiyo inaonyesha kuwa, Coastal Union baada ya kuidindia Simba itasafiri hadi mjini Mbeya kupepetana na wenyeji wao Mbeya City, huku Azam itaialika Ruvu Shooting uwanja wa Chamazi, wakati Ndanda Fc itakuwa wageni wa Mtibwa Sugar mjini Morogoro.
Mechi nyingine ni Mgambo JKT baada ya kuizabua Kagera Sugar itakuwa tena nyumbani kuwakaribisha Stand United iliyoanza ligi hiyo kwa kichapo cha amabo 4-0.
Kipute cha pili hiyo kitaendelea tena kesho kwa mechi mbili zitakazochezwa jijini Dar es Salaam kwenye uwanja wa Taifa, Yanga iliyoanza kwa 'mkosi' wa kubamizwa mabao 2-0 na Mtibwa mjini Morogoro itaialika Prisons-Mbeya na JKT Ruvu ya Fred Felix Minziro itaikaribisha Kagera Sugar uwanja wa Chamazi.

Msechu, Vanessa, Diamond katika tuzo za AFRIMA-2014

Peter Msechu, Vanessa Mdee na Diamond watakaowanmia tuzo za AFRIMA
DIAMOND Platnumz, Vanessa Mdee na Peter Msechu wametajwa kuwania tuzo za AFRIMA za nchini Nigeria.
Wimbo wa Come Over imemuwezesha Vanessa kutajwa kuwania tuzo katika vipengele viwili vya Best African RnB Soul na Best Female Artist in Eastern Africa.
Peter Msechu kupitia wimbo wake Nyota na Diamond kupitia Number One wametajwa kuwania tuzo ya Best Male Artiste In Eastern Africa.
Diamond naye amepata nafasi mbili katika kinyang’anyiro kupitia wimbo wake wa Number One unawania pia tuzo ya Best African Collaboration.


Bofya hapa kuangalia orodha kamili

Hapatoshi England, Liver vs Eveton, Arsenal v Spurs

http://tvnewsroom.org/wp-content/uploads/2013/09/Sky-Sports-1-NAR-Live-Ford-Super-Sunday-09-01-15-41-28-600x339.jpg




http://i.dailymail.co.uk/i/pix/2008/01_03/arsenalspursccG_468x306.jpg
Nani atakayecheka kati ya Arsenal na Spurs
http://www.theevertonforum.co.uk/wp-content/uploads/2013/05/lolza.jpg
http://static.guim.co.uk/sys-images/Football/Clubs/Club_Home/2010/2/7/1265568899742/Tempers-flare-between-Liv-001.jpg
Presha ya pambano la mji wa Merseyside huwa hivi. Leo itaakuwaje? Tusubiri tuone
 KIVUMBI cha Ligi Kuu ya England kinatarajiwa kuendelea kutimka leo kwa kushuhudiwa mechi za watani wa jadi wa miji ya London Kaskazini na Merseyside wakati Arsenal itakapoumana na Tottenham Hotspur na Liverpool kuwakaribisha Everton uwanja wa Anfield.
Klabu hizo zote nne yenye upinzani wa jadi katika miji yao, zitashuka dimbani zikiwa hazina mwenendo mzuri kulinganisha na msimu uliopita na kuwafanya mashabiki wao kuwa roho juu kujua wataibuka vipi.
Mbali na mechi hiyo, pia kwa mujibu wa ratiba ya ligi hiyo timu nyingine 12 wakiwamo Manchester United na Chelsea watakuwa dimbani kusaka pointi tatu muhimu.
Mashetani WEkundu wanaouguza kipigo cha mabao 5-3 toka kwa Leicester City itakuwa uwanja wa nyumbani wa Old Trafford kuwakaribisha West Ham United na Chelsea watakuwa darajani kuivaa Aston Villa.
Ratiba kamili ya ligi hiyo kwa leo ni kama ifuatavyo;
Liverpool    v Everton   
Chelsea        v Aston Villa       
Crystal Palace       v Leicester
Hull City    v Manchester City
Manchester United    v West Ham 
Southampton    v QPR
Sunderland    v Swansea City
Arsenal        v Tottenham

Suarez aitwa 'Stars' ya Uruguay, akitwa Bonge Hispania

http://i.dailymail.co.uk/i/pix/2014/08/18/1408396240290_wps_5_Barcelona_s_Luis_Suarez_f.jpgWAKATI akitajwa kwenye kikosi cha timu ya taifa ya Uruguay, Mshambuliaji nyota wa Barcelona, Luis Suarez amejikuta akibatizwa jina la Bonge, jina ambalo hakuwahi kuitwa hata alipokuwa Liverpool.
Televisheni ya jijini Madrid imemtaja mshambuliaji kuwa ni mwenye uzito kupindukia na kulalamikiwa kuwa anaonekana ni kama mchezaji mstaafu katika taarifa iliyorushwa mchana wa alhamisi siku ambayo Suarez alifunga magoli mawili katika mchezo wa kirafiki akiichezea Barcelona B dhidi ya kikosi cha Indonesian U19.
Ikiwa imesalia mwezi mmoja kabla ya mchezo wa watani wa jadi Clasico katika msimu huu mchezo ambao utakuwa unaashiria kumalizika kwa adhabu ya mshambuliaji huyo kufuatia kumng'ata mlinzi wa timu ya taifa ya Italia mambo yanaonekana kumuendelea kombo nchini Hispania.
Bosi wa Barcelona Luis Enrique amejibu lawama hizo katika mkutano wake na waandishi wa habari akionekana kushangazwa na tuhuma hizo kwa Suarez.
Katika hatua nyingine mshambuliaji huyo amejumuishwa katika kikosi cha awali cha timu ya taifa ya hapa Uruguay kwa ajili ya mechi za kirafiki za mwezi ujao dhidi ya Saudi Arabia na Oman, shiriksiho la soka (AUF) limesema juzi.
Mshambuliaji mwenye matata wa Barcelona huyo amefungiwa kucheza kwa miezi minne, pamoja na mechi tisa za mashindano za timu ya taifa, baada ya kituko chake cha kumng'ata beki wa Italia Giorgio Chiellini kwenye fainali za Kombe la Dunia.
Anaweza kucheza kwenye mechi za kirafiki, hata hivyo, baada ya Mahakama ya Michezo (CAS) kuondoa kipengele ambacho kilimfungia kujihusisha na "jambo lolote la kisoka" katika kifungo chake cha miezi minne.
Baada ya kuachwa kwenye kikosi cha mechi za kirafiki za mwezi huu dhidi ya Japani na Korea Kusini, Suarez ameitwa na kocha Oscar Tabarez katika kikosi cha wachezaji 29 kwa ajili ya mechi hizo za ugenini Saudi Arabia Oktoba 10 na Oman siku tatu baadaye.

Simba, Yanga sasa kutifuana Oktoba 18

PAMBANO la watani wa jadi wa soka nchini, Simba na Yanga ambalo lilikuwa lichezwe Oktoba 12, sasa litafanyika Oktoba 18 baada ya mabadiliko ya ratiba.
Mabadiliko hayo yamekuja kutokana na kuwepo kwa pambano la kirafiki la kimataifa linalotambulishwa na Shirikisho la Soka Duniani, FIFA kati ya Taifa Stars dhidi ya Benin litakalochezwa Oktoba 12 jijini Dar.
Kwa mujibu wa marekebisho madogo yaliyofanywa na Shirikisho la Soka nchini, TFF, ni kwamba mechi zote zilizokuwa zichezwe Oktoba 12 na 13 sasa zitachezwa Oktoba 18 na 19 sambamba na pambano la watani wa Jadi.

Coutinho, Tegete wampa jeuri Maximo akiikabili Prisons Taifa kesho

Kocha Maximo wa Yanga akiwa na Jerson Tegete aliyerejea kikosini baada ya kufanikiwa kuponya majeraha yake
KOCHA Marcio Maximo ametamba kuibuka na ushindi kesho wakati kikosi chake kitakaposhuka dimbani kuwakabili Prisons-Mbeya hii ni baada ya nyota wake waliokuwa majeruhi kupona.
Nyota hao ni pamoja na Mshambuliaji matata, Jerry Tegete na Mbrazil mwenzake Andrey Coutihno ambao huenda wakawepo kikosi katika mechi hiyo ya Jumapili itakayochezwa kwenye uwanja wa Taifa.
Akiongea na tovuti rasmi ya klabu ya Yanga mara baada ya mazoezi, kocha Maximo amesema vijana wake wako fit kuelekea mchezo huo huku wakiwa wamejipanga kuhakikisha wanaondoka na pointi tatu.
Maximo amesema baada ya kupoteza mchezo wa awali dhidi ya wakata miwa wa Mtibwa Sugar, kikosi chake kimekua kikiendelea na mazoezi kila siku katika uwanja wa shule ya sekondari Loyola huku wakiyafanyia marekebisho makosa yaliyojitokeza katika mchezo huo wa awali.
Kuhusu timu ya Tanzania Prisons mbrazil Maximo amesema anatambua walishinda mchezo wa awali dhidi ya Ruvu Shooting hivyo wana morali bado ya kuendeleza ushindi siku ya jumapili, lakini pia kikosi changu kipo fit kwa mchezo huo kwa kusaka pointi tatu muhimu.
Aidha Maximo amesema habari njema kwa wana Yanga ni kurejea dimbani kwa kiungo Andrey Coutinho pamoja na mshambuliaji Jerson Tegete ambao wanatarajiwa kuonekana kwenye mchezo huo na kuhakikisha wanaisaidia timu yao kupata ushindi.
Wachezaji watakaoukosa mchezo wa siku ya jumapili ni Oscar Joshua na Hussein Javu ambao wote ni majeruhi, wakisumbuliwa na maumivu ya nyama za paja, na jumatatu wanatarajiwa kuanza mazoezi mepesi baada ya kuwa kwenye matibabu chini ya usimamizi wa daktari wa timu Dr Suphian Juma.
Mwisho kocha Marcio Maximo amewaomba wapenzi, washabiki, wanachama na wadau wa soka kwa ujumla kujitokeza kwa wingi siku ya jumapili katika mechi dhidi ya Prisons kuja kuwapa sapoti vijana na kuwashangilia muda wote wa mchezo.

Liverpool wapewa Swansea, Man City v Newcastle Capital One


Suso wa Liverpool akishangilia bao lililosaidia kuivusha timu yao katika michuano ya Kombe la Ligi (Capital One)


Frank Lampard akishangilia goli lake la tatu katika mechi mbili dhidi ya Sheffield jana

SHREWSBURY Town, timu pekee ya daraja la chini zaidi iliyosalia katika michuano ya kombe la ligi 'Capital One Cup' amepangwa kukutana na timu ngumu ya ligi kuu ya England, Chelsea kwenye mechi ya raundi ya nne.
Raundi iliyopita Shrews inayocheza daraja la pili iliwaondoa mabingwa wa Championship, Norwich na sasa itawakaribisha Chelsea walioshinda 2-1 dhidi ya Bolton jana usiku.
Mabingwa watetezi, Manchester City, walioitoa Sheffield jana kwa kuifunga mabao 7-0 katika dimba la Etihad watachuana na Newcastle inayocheza ligi kuu.
Liverpool waliosonga mbele kwa penati 14-13 dhidi ya Middlesbrough jumanne usiku, watachuana na Swansea City, zote zinacheza ligi kuu.
Stoke wataikaribisha Southampton , wakati Tottenham watakuwa nyumbani dhidi ya Brighton.
Mechi nyingine za raundi ya nne zitawakutanisha Sheffield United watakaosafiri kuifuata MK Dons na Fulham watakabiliana na Derby.


Ratiba kamili hii hapa:
Tottenham Hotspur vs Brighton
Stoke City vs Southampton
Bournemouth vs West Brom
Shrewsbury vs Chelsea
Liverpool vs Swansea City
MK Dons vs Sheffield United
Manchester City vs Newcastle United

Friday, September 26, 2014

Mwanamke auwawa kwa SMG Mbeya

http://s3.amazonaws.com/mbc_actionha/uploads/43304/large.jpgMWANAMKE MMOJA ALIYEFAHAMIKA KWA JINA LA NKUSUBILA KAMINYONGE (70) MKAZI WA MTAA WA KATI SOWETO ALIUAWA KWA KUPIGWA RISASI AINA YA SMG MAENEO YA MKONO WAKE WA KUSHOTO CHINI YA BEGA NA KUPELEKEA KIFO CHAKE.

TUKIO HILO LIMETOKEA USIKU WA KUAMKIA LEO MAJIRA YA SAA 03:00 HUKO MAENEO YA SOWETO, MTAA WA KATI, KATA YA RUANDA, TARAFA YA SISIMBA, JIJI NA MKOA WA MBEYA. INADAIWA KUWA, WATU HAO WALIVUNJA GETI LA NYUMBA NA KISHA KUINGIA NDANI NA KUVUNJA MLANGO WA CHUMBA ALICHOKUWA AMELALA MAREHEMU NA KISHA KUMPIGA RISASI.

WAKATI WATU HAO WANAVAMIA NYUMBA HIYO, MAREHEMU ALIKUWA AMELALA NA MUME WAKE AITWAYE OSIA MALAMBUGI (72) MKAZI WA MTAA WA KATI SOWETO AMBAYE ALISHTUKA BAADA YA KUSIKIA MLIO MKUBWA WA RISASI NA KUKUTA MKE WAKE AMEPIGWA RISASI NA WATU HAO AMBAO WALIKIMBIA MARA BAADA YA TUKIO HILO.

 HAKUNA KITU CHOCHOTE KILICHOCHUKULIWA/KUPORWA. CHANZO CHA MAUAJI HAYO BADO KUFAHAMIKA, UPELELEZI UNAENDELEA. MWILI WA MAREHEMU UMEHIFADHIWA KATIKA HOSPITALI YA RUFAA MBEYA. MSAKO UNAENDELEA KUWATAFUTA WALIOHUSIKA KATIKA TUKIO HILI.

KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHINA MSAIDIZI MWANDAMIZI WA POLISI AHMED Z. MSANGI ANATOA WITO KWA YEYOTE MWENYE TAARIFA ZA WATU HAO WALIOHUSIKA KATIKA TUKIO HILO AZITOE KATIKA MAMLAKA HUSIKA ILI HATUA ZA KISHERIA ZICHUKULIWE DHIDI YAO.

Thursday, September 25, 2014

Liverpool yaingia matatani Ulaya

http://cdn3-i.hitc-s.com/69/liverpool_wall_12402.jpgKLABU ya Liverpool ni moja ya vilabu kadhaa vinavyotarajiwa kufanyiwa uchunguzi kama wamekiuka Sheria ya Matumizi ya Fedha-FFP.
Kwa mujibu wa sheria za Shirikisho la Soka barani Ulaya-UEFA vilabu vyote barani humo vinapaswa kuweka kikomo cha hasara kutofikia paundi milioni 35.4 kwa misimu miwili. 
Kuna adhabu hutolewa kwa wasiotimiza masharti hayo ambapo Manchester City tayari wameshakumbana nayo kwa kutozwa faini na kuwekewa kiwango cha matumizi katika usajili na kupunguziwa idadi ya wachezaji katika kikosi chake Mei mwaka huu. 
Lakini pamoja na kupata hasara ya paundi milioni 49.8 katika msimu wa mwaka 2012-2013 na paundi milioni 41 msimu wa mwaka 2011-2012, Liverpool wana uhakika wanaweza kuvuka kikwazo hicho bila adhabu. 
Liverpool sambamba na Monaco, Inter Milan na AS Roma ambazo zote hazikushiriki michuano ya Ulaya msimu uliopita tayari zimepeleka taarifa za akaunti zao Bodi ya Udhibiti wa Fedha ya Klabu-CFCB lakini kuna uwezekano wa kuagizwa kupelekea maelezo zaidi kuhusu fedha hizo. 
Msimu uliopita vilabu 76 viliingia katika uchunguzi wa FFP lakini vilabu tisa pekee ndio vilipewa adhabu kwa kukiuka sheria hiyo.

HAWA NDIYO WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA VYUO VIKUU 2014-2015




CHUNGULIA mwenyewe kwa kubofya jina la chuo kupakua faili lenye majina:
  1. BUGANDO BScN_2014.pdf (82.4 KB)
  2. BUGANDO MD.pdf (106.2 KB)
  3. BUGANDO MEDICAL LABORATORY SCIENCES.pdf (79.7 KB)
  4. BUGANDO PHARMACY.pdf (80.0 KB)
  5. BUGANDO NURSING.pdf (76.0 KB)
  6. IFM BACHELOR DEGREE 2014
  7. MAKUMIRA PROPOSED STUDENTS 2014/2015
  8. MUM Undergraduate Selection - Direct.pdf (561.3 KB)
  9. MUM Undergraduate Selection - Equivalent.pdf (202.0 KB)
  10. SAUT Selected Students.pdf (307.3 KB)
  11. ST. AUGUSTINE 2014
  12. ST Franscis MD Batch one (52.3 KB)
  13. ST Franscis MD Batch two (37.2 KB)
  14. ST Franscis MD Batch Three (49.5 KB)
  15. Stella Maris Mtwara.pdf (283.1 KB)
  16. UDSM 2014/2015 
  17. Mwenge Catholic University

Mechi ya Simba Yanga lapeperuka Oktoba 12

http://tff.or.tz/wp-content/uploads/2014/05/taifa-stars-2014.jpg
Stars iliyopeperusha pambano la Simba na Yanga Oktoba 12
PAMBANO la watani wa jadi kati ya Simba na Yanga 'limeota mbawa' Oktoba 12 kutokana na kuwepo kwa pambano la kimataifa kati ya Taifa Stars na Benin.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Shirikisho la Soka Tanzania, TFF, Stars itacheza na Benin katika mechi inayotambuliwa na FIFA.
Taarifa hiyo inaseme mechi hiyo itachezwa Oktoba 12 kwenye uwanja wa Taifa, siku ambayo Simba na Yanga zilikuwa ziumane kilingana na ratiba ya awali ya Ligi Kuu ambayo sasa inatarajiwa kufanyiwa marekebisho yatakayotangazwa kesho Septemba 26.
Taarifa kamili ya TFF inasomeka hivi:
Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) inashuka uwanjani Oktoba 12 mwaka huu kuikabili Benin katika mechi ya kirafiki ya kalenda ya Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA).Mechi hiyo itachezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 10 kamili jioni. Programu ya Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager kwa ajili ya mechi hiyo itatangazwa baadaye na Kocha Mkuu Mart Nooij.Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linaendelea na taratibu nyingine kwa ajili ya mechi hiyo ikiwemo usafiri wa Benin kuja nchini, ambapo timu hiyo inatarajiwa kutua Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), Oktoba 10 mwaka huu ikiwa na msafara wa watu 28.
Pambano la Stars na Benin litatanguliwa na mechi ya kudumisha upendo kati ya viongozi wa dini ya Kikristo na Kiislamu.
 Wakati huo huo, kutokana na mechi hiyo ratiba ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) inafanyiwa marekebisho madogo, na marekebisho hayo yatatangazwa kesho (Septemba 26 mwaka huu).
 RAIS MALINZI KUFUNGA KOZI YA WANAWAKE
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi anatarajia kufunga mafunzo ya uongozi kwa viongozi wa vyama vya mpira wa miguu wa wanawake vya mikoa ya Tanzania Bara.
 Hafla ya kufunga mafunzo hayo itafanyika kesho (Septemba 26 mwaka huu) saa 5 asubuhi kwenye ofisi za TFF, Uwanja wa Karume, Dar es Salaam.
 Mafunzo hayo ya siku tano yalishirikisha viongozi 34 wakiwemo baadhi ya waandishi wa habari na Meneja wa Twiga Stars, na yaliendeshwa na Mkufunzi wa Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA), Henry Tandau.
 BONIFACE WAMBURA
KNY KATIBU MKUU
SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA.

Simba yapata pigo, Ivo, Kiongera kuikosa Yanga Okt 12

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj8__24SqlWkKjcX7F8kwlm9XNcJcmuX00g5LSeJnhkhyvDdgaA_LOv5ObDUcs7DcWxwbUMiMiTANgKbV434hiewe8cAlv0KlOHhyuP0g6sM4YhdkxIkgyI8l30SjnEcyw_ja49lQ9HlEI/s1600/ivo.jpg 
WIKI mbili kabla ya kuvaana na watani zao, Yanga klabu ya Simba imepata pigo baada ya kipa wake namba moja, Ivo Mapunda kuvunjika kidole na hivyo kuwa nje ya dimba kwa wiki nane.
Kwa mujibu wa taarifa za klabu hiyo Ivo amevunjika kidole mazoezini Zanzibar jana asubuhi na anatakiwa kuwa nje ya uwanja kwa wiki nane.
Kuumia huko kunamfanya asiweze kusimama langoni wakati  wa pambano la watani wa jadi la Simba na Yanga la Oktoba 12.
Daktari wa Simba SC Yassin Gembe amenukuliwa akisema Ivo aliumia wakati anachupia mpira katika mazoezi ya asubuhi na kwa bahati mbaya mpira ukamgonga kwenye kidole kidogo cha mwisho mkono wa kulia.
Gembe amesema Ivo alitoka mazoezini baada ya tukio hilo na baadaye akapelekwa hospitali ya Mnazi Mmoja kisiwani humo ambako baada ya vipimo ikagundulika amevunjika sana.
"Si kuvunjika kwa mzaha, amevunjika sana na anatakiwa kupumzika kwa wiki nane, baada ya hapo aanze taratibu… ina maana makadirio ya kurudi tena uwanjani ni hadi baada ya miezi mitatu" – Gembe.
Kuumia kwa Ivo kunatoa nafasi kwa makipa chipukizi Hussein Sharrif  ‘Cassilas’ na Peter Manyika kujibidiisha ili kuziba pengo lake ambapo sasa Ivo anafanya idadi ya wachezaji majeruhi ambao ni tegemeo Simba kufikia wanne baada ya Paul Kiongera anayetakiwa kuwa nje wiki sita, Haroun Chanongo na Issa Rashid ‘Baba Ubaya’.

Aisha Bui awaandalia mashabiki wake 'Asante' kumpokea

Aisha Bui katika pozi tofauti
NYOTA wa filamu nchini, Aisha Fat'hi  a.k.a Aisha Bui, yupo kwenye maandalizi ya kufyatua kazi mpya baada ya filamu yake ya 'Mshale wa Kifo' kufanya vyema sokoni.
Akizungumza na MICHARAZO, Aisha alisema anashukuru namna mashabiki walivyoipokea filamu yake hiyo ya kwanza kuitengeneza mwenyewe kupitia kampuni ya Bad Girl Entertainment na katika kuonyesha shukrani zake anajiandaa kuwatengenezea filamu nyingine kali zaidi.
Aisha alisema ingawa ni mapema kwa sasa kutaja jina la filamu hiyo, lakini alisema itawashirikisha wasanii kadhaa nyota kama alivyofanya katika 'Mshale wa Kifo' aliowashirikisha kina Mzee Chillo, Gabo na wengine.
"Nipo katika maandalizi ya kutengeneza filamu nyingine mpya, hii kama 'Mshale wa Kifo' itashirikisha pia wakali mbalimbali wa filamu nchini, lengo ni kuwapa burudani mashabiki wangu walioniunga mkono kupitia kazi yangu ya kwanza kuizalisha mwenyewe," alisema Aisha.
Kabla ya kutengeneza filamu yake mwenyewe, alishafanya vema katika filamu za wenzake zikiwamo za 'Saturday Morning', 'The Second Wife', 'Better Days', 'Not Without My Son', 'Continous Love', 'Revenge of Love', 'Mirathi', 'Pain of Love' na 'Crazy Love'.

Mashetani Wekundu kumpigia misele Gerard Pique

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjuyvOqEQPRTd8rb3TwgCrdwrkJv25RIrKO5tVEc69etf1RqMa9oRZknqbCqG35plalZ5O0rf0aHR1cMgKHEd_pd8Lj8yuoEqhsZrMY-HvGZKiXjbbOmdo3n2XiN6O5S24WwaeAbCk-xgKL/s1600/gerard+pique+wallpaper+barca+barcelona+photo+gallery+barcablog+barca+blog+2.jpg
IMEFAHAMIKA kuwa klabu ya Manchester United wana mpango wa kumrejesha Gerard Pique Old Trafford akitokea Barcelona.
Mlinzi huyo aliondoka United mwaka 2008 kwa uhamisho uliogharimu pauni milioni £5 ambapo amekuwa mchezaji wa kutumainiwa Katalunya tangu wakati huo ambapo ameisaidia kutwaa mataji manne ya ligi ya Hispania 'La Liga' mataji mawili ya ligi ya mabingwa Ulaya na mawili ya Copa del Reys.
Hata hivyo nyota huyo wa kimataifa wa Hispania mpaka sasa ameitumikia timu yake michezo mitatu tu huku bosi mpya wa Barcelona Luis Enrique akionekana kupendelea zaidi kumtumia Javier Mascherano na Jeremy Mathieu katika sehemu ya ulinzi.
Kwa mujibu wa gazeti moja la nchini Hispania la AS limearifu kuwa Manchester United inataka kutumia mwanya huo kuweka pendekezo la kutaka kumsajili Pique kurejea Old Trafford, licha ya kwamba mlinzi huyo mwenye umri wa miaka 27 akiwa ndio kwanza amesaini mkataba wa nyongeza na Barca.
Bosi Louis van Gaal kwasasa analazimika kusaka namna ya kuimarisha eneo la ulinzi katika kikosi chake mwezi Januari wakati huu ambapo United ikiwa imekusanya alama tano tu katika michezo mitano tangu kuanza kwa msimu mpya wa Premier League huku ikiwa tayari imeshatolewa katika kombe la Capital One na MK Dons.

Algeria yajaribu bahati yake AFCON 2017

http://en.starafrica.com/football/files/2014/07/alg%C3%A9rie1.jpgNCHI ya Algeria imeamua kujitosa kuwania uenyeji wa Fainali za Afrika, AFCON 2017 baada ya kukosa nafasi ya uandaaji wa fainali za  2019, 2021 na 2023.
Shirikisho la Soka la Algeria limetangaza kutuma maombi ya kutaka uenyeji wa michuano hizo za 2017. 
Taifa hilo la kaskazini mwa Afrika litachuana na nchi za Ethiopia, Ghana, Kenya, Tanzania, Mozambique, Zimbabwe na Misri katika kugombea nafasi hiyo. 
Libya ilishindwa kuandaa michuano hiyo kufuatia vita vya wenyewe kwa wenyewe vinavyoendelea nchini humo toka uondolewe utawala wa Muamar Gaddafi. 
Mshindi katika kinyang’anyiro hicho anatarajiwa kutangazwa mapema mwakani na Shirikisho la Soka barani Afrika-CAF. 
Cameroon wao walishinda haki za kuandaa michuano hiyo mwaka 2019 wakati Ivory Coast na Guinea wao walipata nafasi ya kuandaa michuano ya mwaka 2021 na 2023.

Arsene Wenger apumua Arsenal wakijiandaa kuivaa Spurs

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhLx4Ctj5fXJAnEPWAnPQLE87dYZzsslg675yLAakU1-WpskYn3CW0mbJ2CIKGeRf5M4Yqi-eVxM6Pyv_R7oLwacXTN6v0ML9tDqP3gR9TEUBNLUbo6FhO2brnwFUrixY0Has-XeGIPRHE/s1600/guar.jpgMENEJA wa klabu ya Arsenal, Arsene Wenger amesema anategemea Per Martesacker na Kieran Gibbs kurejea katika kikosi chake katika mchezo wa Jumamosi dhidi ya mahasimu wao wa kaskazini mwa London Tottenham Hotspurs. 
Majeraha madogo madogo yalipelekea Martersacker na Gibbs kukosa mchezo wa Kombe la Ligi dhidi ya Southampton na kupelekea Wenger kuwatumia mabeki wasio wazoefu akiwemo Hector Bellerin na Isaac Hayden. 
Kukosekana kwa Nacho Monreal kunamaanisha Calum Chambers ndio mchezaji pekee katika safu ya ulinzi mwenye uzoefu aliyechezeshwa na Wenger lakini kinda huyo amecheza katika mechi saba pekee za Arsenal toka alipojiunga akitokea Southampton. 
Katika mchezo huo Arsenal walitandikwa nyumbani mabao 2-1 na Southampton lakini Wenger ana uhakika kuwa mabeki wake wazoefu Matersacker na Gibbs watakuwa fiti kwa ajili ya mchezo wa Jumamosi. 
Safu ya ulinzi ya Arsenal ilizidi kupungua baada ya taarifa za Jumatatu kuwa beki wa kimataifa wa Ufaransa Mathieu Debuchy atakosekana dimbani kwa miezi mitatu kufuatia kufanyiwa upasuaji wa kifundo cha mguu wake wa kushoto.

Ronaldo akaribia rekodi ya Di Stephano Real Madrid

http://assets2.sportsnet.ca/wp-content/uploads/2014/01/ronaldo_cristiano.jpgCRISTIANO Ronaldo alifunga magoli manne katika ushindi wa Real Madrid wa 5-1 dhidi ya Elche katika Ligi Kuu ya Hispania juzi na kuwa 'hat-trick' yake ya 25 kwa Real Madrid.
Ilikuwa ni 'hat-trick' ya pili katika siku tatu baada ya kufunga magoli matatu katika ushindi wa 8-2 dhidi ya Deportivo la Coruna Jumamosi.
Ronaldo ndiye aliyesababisha penalti iliyowapa Elche goli la kuongoza baada ya kuukosa mpira na kumpiga teke Pedro Musquera wakati akijaribu kuokoa kutokea ndani ya boksi la Madrid. "Licha ya kwamba nililalamika kwa refa, ilikuwa ni penalti. Ni lazima niwe mkweli. Alikuja ghafla, lilikuwa ni shambulio ambalo sikulitarajia. Yalikuwa ni maamuzi sahihi ya refa," alisema Ronaldo.
"Nimefunga magoli manne katika mechi moja mara mbili ama tatu. Nina furaha mpira (wa 'hat-trick' nampelekea mwanangu," alisema.
'Hat-trick' hiyo ya 25 inamfanya kubakisha tatu kumfikia Alfredo di Stefano anayeshikilia rekodi ya Real Madrid ya kufunga 'hat-trick' 28. Pia ilikuwa ni ya 21 katika La Liga pekee, moja nyuma ya vinara wanaoshikilia rekodi, Di Stepano na Telmo Zarra, gwiji wa Athletic Bilbao.
Ronaldo tayari msimu huu amefunga magoli 13 katika michuano yote na kufikisha mabao 264 tangu ajiunge na Madrid, hivyo kubakisha magoli 59 kumfikia mshikarekodi wa zama zote klabuni hapo Raul aliyefunga magoli 323. Na kwa kuwa Madrid wana mechi 56 zilizobaki msimu huu, huenda akaivunja rekodi hiyo 2014-15. 

Hammer Q ana Kibakuli cha Mduara

MUIMBAJI mahiri wa muziki wa taarab, Hammer Q ameachiwa wimbo wake binafsi uitwao 'Kibakuli', wakati Rich Mavoko akiwaonyesha mashabiki wake video ya wimbo wake mpya uitwao 'Pacha Wangu'.
Hammer Q aliyewahi kutamba kwenye muziki wa kizazi kipya na wimbo wa 'Lady' kabla ya kuhamia kwenye taarab, ameachiwa wimbo huo uliopo kwenye mduara.
Wimbo huo umetengenezwa na mtayarishaji aitwae Anta Nation na  umeanza kutamba kwenye redio na mitandao ya kijamii.
Katika hatua nyingine Staa wa Roho Yangu, Rich Mavoko ameonjesha kionjo cha video yake mpya ya Pacha Wangu ambayo anatarajia kuachia siku ya leo pamoja na ngoma nyingine mpya.