STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, October 16, 2014

Algeria yafuzu Fainali za AFCON 2015 yaitungua Malawi 3-0

Algeria prove why they are the top ranked side in AfricaTIMU ya taifa ya Algeria imeweka rekodi ya kuwa nchi ya kwanza kufuzu katika Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika zitakazofanyika mwakani nchini Morocco baada ya kupata ushindi murua wa mabao 3-0 dhidi ya Malawi katika mechi za kundi D.
Vijana wa kocha Christian Gourcuff wameweka rekodi ya kushinda mechi zake zote mpaka sasa kukiwa kumesaliwa mechi mbili kabla ya mechi za makundi kumalizika.
Mabao ya washindi hao waliong'olewa kwenye raundi ya pili ya Fainali za Kombe la Dunia za 2014 na waliokuja kuwa Mabingwa wapya, Ujerumani yaliwekwa kimiani naYasine Brahimi  dakika ya pili, Riyad Mahrez dk ya 45 na Islam Slimani Dk ya 55.
Katika mechi nyingine ya michuano hiyo kundi B lilishuhudiwa Ethiopia ikiwa ugenini mjini Bamako iliicharaza wenyeji Mali kwa mabao 3-2 na kujiweka pazuri kabla ya mechi mbili za mwisho dhidi ya Algeria na Malawi.
Bakary Sako alianza kufungua milango ya pambano hilo kwa kuwafungia wenyeji bao la kuongoza dakika ya 31 kabla ya wageni kurejesha na kuongeza la pili kupitia kwa wachezaji wao Oumed Oukri na Getaneh Kebede na Mali kuchomoa na kufanya matokeo kuwa 2-2 kwa bao la Mustapha Yatabare dakika dakika ya 69.

Bao la ushindi la Ethiopia lilifungwa na Abebaw Butako Bune, huku Angola ikiwa nyumbani ilipata ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Lesotho katika mechi ya Kundi C.
Bastos alianza kuwaandikia wenyeji bao dakika ya pili kabla ya Ary Papel kuongeza la pili dakika ya 33 na kufanya hadi mapumziko matokeo kuwa 2-0 na kwenye kipindi cha pili Tsoanelo Koetle alijifunga katika dakika ya 47 na Love akapigilia msumari wa mwisho kw akuifungia Palancas Negras bao dakika ya 57.
nazo timu za Burkina Faso na Gabon zilitoshana nguvu kwa kufungana bao 1-1 Jonathan Pitroipa akiifungia Burkinabe na wageni kuchomoa kupitia kwa Malick Evouna dakika ya 76.
Cape Verde waliendelea kuweka ugumu katika Kundi F baada ya kupata ushindi mwembamba wa bao 1-0 dhidi ya Msumbiji kwa bao la Heldon katika dakika ya 75 na kuifanya wenyeji kufikisha pointi 9, huku Msumbiji wakisalia kwenye nafasi ya tatu ikiwa na pointi 5 sawa na Zambia walioshinda nyumbani mabao 3-0 dhidi ya Niger.
Nayo timu ya Tunisia ilifuata nyayo za majirani zao Misri walioishinda Botswana kwa mabao 2-0 nyumbani baada ya kuilaza Senegal bao 1-0 bao lilifungwa 'jioni' na Ferjani Sassi na kuifanya Tunisia kuongoza msimamo wa kundi hilo wakiwa na pointi 10 wakifuatiwa na Senegal wanaokamata nafasi ya pili wamiwa na pointi saba wakiitangulia Misri wenye pointi 6 wakiwa nafasi ya tatu.

Breaking Newz! Nigeria yamtimua Stephen Keshi, Amodu amrithi

http://ynaija.com/wp-content/uploads/2013/10/Nigerias-coach-Stephen-Ke-011.jpg
Stephen Keshi akiwa amebebwa alipotwaa ubingwa wa Afrika
https://thetbjoshuafanclub.files.wordpress.com/2009/12/amodu1.jpg
Shaibu Amodu anayemrithi Keshi kartika Super Eagles

SHIRIKISHO la Soka la Nigeria, NFF, kimetangaza kumfuta kazi aliyekuwa kocha Mkuu wa Super Eagles, Stephen Keshi ikiwa ni saa chache tangu aiongoze timu hiyo kupata ushindi wa mabao 3-1 nyumbani dhidi ya Sudan katika mechi ya kuwania Fainali za Kombe la Afrika za 2015.
Kocha za zamani wa timu hiyo Shaibu Amodu ndiye aliyepewa mikoba ya kuuiongoza Super Eagles katika mechi zilizosalia za kundi lake.
Keshi, nyota wa zamani wa timu hiyo amekuwa kocha wa Nigeria tangu mwaka 2011 na alifanikiwa  kuipeleka Super Eagles kwenye Fainali za Kombe la Dunia na kuishia nao raundi ya pili na inaelezwa tangu fainali hizo hakuwa na mkataba wowote licha ya kuendelea kuinoa timu hiyo aliyoipa ubingwa wa Afrika fainali za mwaka jana zilizofanyika nchini Afrika Kusini.
Kwa mujibu wa NFF, maamuzi ya kutimuliwa kwa Keshi yamekuja baada ya Kamati ya Utendaji ya Shirikisho hilo kukutana jana.
"Kwa manufaa ya soka la Nigeria na kiu kubwa ya kushiriki fainali za mwaka 2015 kamati imeamua kuachana na Keshi na benchi lake lote la ufundi," taarifa ya NFF ilisomeka hivyo.
Badala ya keshi NFF imemtaja Amodu aliyewahi kuinoa timu hiyo katika vipindi vinne tofauti mara ya mwisho ikiwa ni mwaka 2008-2010.
Vipindi vingine ambayo Shaibu Amodu aliwahi kuiongoza timu hiyo ni mwaka 1994-95, 1998-99, 2001-2002, Mei Mwaka jana alikuwa Mkurugenzi wa Ufundi wa Soka nchini humo kabla ya kupata kazi kama hiyo katika klabu na kutema nafasi yake hadi alipoitwa leo na NFF kuwa Kocha Mkuu kwa mara ya tano.

Maafa makubwa Misri! Bomu lalipuliwa Mahakamani jiji Cairo

An injured man arrives at the Helal hosp 
BOMU lililotengenezwa kienyeji huko Cairo, Misri limelipuka karibu na mahakama kuu siku ya Jumanne tarehe 14 mwaka huu na kujeruhi watu 12 ambapo gari na maduka yaliliyokuwa karibu ya eneo hilo la tukio yameharibika.
Haikufahamika vizuri kama lengo lilikuwa ni la kumuua mtu mmoja au kufanya tu uharibifu kwa sababu hii ni mara ya pili tukio kama hili limetokea huko Cairo chini ya mwezi mmoja.
Ripoti zinasema bomu ambalo lililipuka mwezi uliopita karibu na wizara ya mambo ya nje lililoua polisi watatu, lilisababisha uhalifu mkubwa ambao haukutokea kwa muda mrefu mjini Cairo.
Shambulizi hilo la bomu lilianzishwa na kundi la Jeshi la Kiislamu liitwalo Ajnad Misr ambapo inasemekana ongezeko la mashambulizi ya majeshi ya Kiislamu yamezidi kwenye nchi hiyo toka mkuu wa jeshi aitwae Abdel Fattah al-Sisi ampindue Rais Mohamed Morsi mwaka jana baada ya wananchi kupinga utawala wake.
Baada ya kumpindua Rais Mohamed Morsi mkuu huyo wa jeshi Abdel Fattah alivunja udugu wa Kiislamu uliokuwa chini ya Mohamed Morsi ambapo serikali ililitangaza kuwa ni kundi la kigaidi.

Kocha Hispania aanza kuaga, kutema timu baada ya Euro Cup

http://i.dailymail.co.uk/i/pix/2014/10/01/1412176952043_wps_10_Spain_s_head_coach_Vicent.jpg
Kocha Del Bosque
KOCHA wa Hispania, Vicente Del Bosque amesema ataachia ngazi ya kukinoa kikosi hicho cha timu ya taifa baada ya michuano ya Euro 2016 itakayofanyika nchini Ufaransa.
Del Bosque (63), ameshuhudiwa akipata mafanikio ya dhahabu kwa umri wake huo katika soka la Hispania, baada ya kushinda Kombe la Dunia  2010 na michuano ya Ulaya (Euro 2012) katika historia ya jina lake kwenye timu ya taifa.
Hata hivyo, Hispania ilianza kudorora katika Kombe la Dunia 2014 nchini Brazil na kipigo cha mabao 2-1 dhidi ya Slovakia ilichokipata Alhamisi ni cha kwanza katika mechi 36 za kuwania kufuzu kuanzia 2006 -- kimemfanya Del Bosque kuanza kukosolewa kwa mara ya kwanza tangu alipotwaa mikoba ya kuinoa timu hiyo mwaka 2008 kutoka kwa Aragones.
Baada ya kutolewa kwenye Kombe la Dunia, kocha huyo mkuu wa Hispania, Del Bosque alionekana kuzama zaidi katika vipaji vya timu ya taifa ya makinda kwa kuviandaa kwa ajili ya Euro 2016. Tayari Del Bosque ameiongoza Hispania katika michuano mikubwa ya kimatifa mitatu na kushinda miwili tangu alipoanza kuinoa 2008.
"Nadhani Euro 2016 itakuwa michuano yangu ya mwisho kama kocha mkuu wa Hispania," aliiambia  Redio Nacional de Espana.
"Tutaona nini kitatokea wakati tutakapokwenda Ufaransa. Kinadharia, hii ni michuano yangu ya mwisho."
Del Bosque si mtu pekee ambaye yupo katika presha kubwa katika kikosi hicho cha 'La Roja', pia kipa wa Real Madrid, Iker Casillas amepoteza nafasi yake ambayo imetwaliwa na mlinda mlango wa Manchester United, David De Gea wakati  walipoibuka na ushindi wa 4-0 dhidi ya Luxembourg Jumapili.
Casillas (33), amekuwa akikosolewa na vyombo vya habari vya Hispania kutokana na kiwango chake katika Kombe la Dunia na dhidi ya Slovakia, huku pia uwezo wake ndani ya klabu ukizua mjadala, jambo linalomfanya kipa wa kimataifa wa Costa Rica Keylor Navas kuanza kuivizia nafasi yake.

Paul Scholes ampigia 'salute' Jack Welshere

http://i1.mirror.co.uk/incoming/article2168562.ece/alternates/s2197/England-v-Scotland-International-Friendly.jpg
Jack Welshere
KIUNGO nyota wa zamani wa England aliyewahi kutamba na klabu ya Manchester United, Paul Scholes anaamini kwamba Jack Wilshere ameongezeka ubora na sasa ndiye mchezaji bora zaidi katika kikosi cha timu ya taifa ya England.
Welshere, 22, ambaye alicheza kwa dakiia zote 180 za mechi mbili za timu ya taifa ya England za kuwania kufuzu kwa fainali za Euro 2016 ambazo walishinda dhidi ya San Marino na Estonia, alipata kukosolewa na gwiji huyo wa Manchester United kwa kushindwa kuongezeka ubora tangu alipoingia katima kikosi cha kwanza cha Arsenal.
Lakini Scholes sasa amemsifu Wilshere, ambaye alipewa jukumu la kucheza katikati ya kiungo na kocha Roy Hodgson, na gwiji huyo wa Man U mwenye umri wa miaka 39 amefurahishwa na pasi zilizokuwa zikitolewa na kiungo huyo.
“Nadhani Jack Wilshere alikuwa na mechi mbili nzuri sana za England wiki iliyopita,” Scholes aliandika kwenye gazeti la Independent. “Naweza kwenda hatua moja mbele na kusema kwamba, kwa sasa, Wilshere ndiye mchezaji bora wa England.
“Amebadilika na ameongeza kitu katika uchezaji wake. Alikuwa ni mtu wa pasi fupi tu, lakini sasa anaweza kupiga pasi ndefu pia.”

Hivi ndivyo Suzuki Sauti ya Malaika alivyozikwa jana jijini Dar

https://fbcdn-sphotos-h-a.akamaihd.net/hphotos-ak-xpf1/v/t34.0-12/10735860_387830028030788_699106094_n.jpg?oh=4a4a71a5e704c6de8d13b86213f578a6&oe=544077E5&__gda__=1413518840_3735b6aa646908122422cde63a7ff273
Waombolezaji wakifukia kaburi ya marehemu Suzuki wakati wa mazishi yake jana kwenye makaburi ya Magomeni Kagera
Mwili wa marehemu Suzuki ulipokuwa ukihifadhiwa jana
Mwili wa Suzuki ukihifadhiwa katika makaburi ya Kagera

Waombolezaji wakiwa makini kufuatilia mazishi ya Suzuki

Baadhi ya woambolezaji walioshiriki mazishi ya Suzuki
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhFhXutATUb6_ogGzQhP1FoqA9uKARlTfPORgEC6yTP-kCm0Wggg8WAt_Ne5GzHPzDDHbaEikGcRE9B53AYkJ-gMmL1fkvt6KkDpCYYUY_zS9m_vVA16ZWnOLkQV38zDGrRyVxrngyVxX8/s400/P1211580.jpg
Suzuki Sauti ya Marehemu enzi za uhai wake
MWILI wa mwanamuziki nyota wa zamani wa bendi za Tabora Jazz, Mikumi Sound, Levent Musica na Extra Bongo, Suleiman Ramadhan 'Suzuki' au Sauti ya Malaika hatimaye umepumzishw akatika mazishi yaliyofanyika jana jioni kwenye makaburi yaliyopo eneo la Kagera.
Mwili huo ulizikwa saa 10:30 mara baada ya kuswaliwa kwenye Msikiti wa Rahman Kagera Mikoroshini na kusindikizwa na wanamuziki wenzake wachache na waumini wengine ambao wlaifurika kumhifadhi muimbaji huyo aliyefariki usiku wa juzi kutokana na kusumbuliwa na ugonjwa wa Kisukari.
MICHARAZO iliwashuhudia wanamuziki wachache waliojitokeza kumsindikiza mwenzao huku baadhi ya waliokuwa mabosi wake wa zamani wakiwa wameingia mitini.
Miongoni mwa wanamuziki walioshiriki mazishi hayo mwanzo mwishoni ni Ramadhan Mhoza 'Pentagone', Athanas Montanabe, Adam Mbombole, Frank Kaba 'Kaba Tano' Redock Sura ya Mauzo, Hosea Mgohachi, dansa wa zamani wa Chino Loketo, Bob Kissa na wengine.
Aidha kulikuwa na wasanii wengine mbalimbali wa muziki ambao walishiriki kumsindikiza mwenzao, huku majina makubwa ya wasanii ambao waliwahi kufanya kazi na marehemu Suzuki wakiwa wameingia mitini.

TFF yapangua kiduchu ratiba Ligi Daraja la Kwanza (FDL)

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiXBt0R5Pi-ynZE0lUwMuVOoucOGlhDsPIsBIaGAiajuQXwnnQ3ouUqzqLpkbGZdozVZKBB0vK7XL15pWWM0MF2OQWhhvfPiIxQw-fpCI7V6a5Jbi8Fy89wLz6es-PsG5pO3dt0uQLfunnH/s640/Wambura1_2_339a2.jpg
MECHI nne za Kundi A la Ligi Daraja la Kwanza (FDL) zimefanyiwa marekebisho ili kutoa fursa ya matumizi ya Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume jijini Dar es Salaam.


Timu za African Lyon na Kimondo ambazo awali zilikuwa zicheze Oktoba 25 mwaka huu kwenye Uwanja wa Mabatini mkoani Pwani, sasa zitacheza Oktoba 26 mwaka huu Uwanja wa Karume, Dar es Salaam.


Nayo mechi ya Polisi Dar es Salaam na Majimaji ya Songea iliyokuwa ichezwe Oktoba 26 mwaka huu Uwanja wa Karume, Dar es Salaam, sasa itachezwa Oktoba 27 mwaka huu kwenye uwanja huo huo.


Mechi ya Friends Rangers na Ashanti United iliyokuwa ichezwe Mabatini mkoani Pwani, Oktoba 26 mwaka huu, sasa itachezwa Uwanja wa Karume, Oktoba 28 mwaka huu.

Pia mechi ya Lipuli na JKT Mlale iliyokuwa ichezwe Oktoba 25 mwaka huu kwenye Uwanja wa Samora mjini Iringa, imesogezwa mbele kwa siku moja. Mechi hiyo sasa itachezwa Oktoba 26 mwaka huu kwenye uwanja huo huo.

Uchaguzi mdogo Bodi ya Ligi Nov 15

https://hivisasa.co.tz/wp-content/uploads/2014/10/DSC03338.jpgMKUTANO  Mkuu wa Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) utafanyika Novemba 15 mwaka huu jijini Dar es Salaam ambapo moja ya ajenda ni uchaguzi mdogo wa kujaza nafasi moja ya uongozi kwenye bodi hiyo.


Nafasi hiyo ya ujumbe kwenye Kamati ya Uendeshaji ya TPLB iliyokuwa ikishikiliwa na Kazimoto Muzo imebaki wazi baada ya klabu yake ya Pamba ya Mwanza kushuka daraja kutoka la Kwanza hadi la Pili.

Hivyo, wagombea wa nafasi hiyo ni kutoka kwenye klabu za Ligi Daraja la Kwanza (FDL). 
Klabu hizo zina nafasi mbili kwenye Kamati ya Uendeshaji ya TPLB ambapo nyingine inashikiliwa na Omari Mwindadi wa klabu ya Mwadui ya Shinyanga.

Nigeria yazinduka, Ivory Coast hoi, Cameroon wanusa AFCON 2015

http://images.performgroup.com/di/library/Goal_Nigeria/e0/cf/nigeria-vs-sudan-abuja_1ro9umbg2xq9b1qgpib297xiqm.jpg?t=349299433&w=940
Nigeria walipoisulubu Sudan mjini Abuja
http://www.goal-news.com/wp-content/uploads/2014/10/Asamoah-Gyan-Ghana-e1413339163729.jpg
Ghana wakishangilia moja ya mabao yao
http://nilsenreport.ca/wp-content/uploads/2014/06/Ivory-Coast-World-Cup-tea-010.jpg
Ivory Coast iliyokufa kwa DR Congo
http://www.goolfm.net/wp-content/uploads/2014/10/s64.jpg
Cameroon walionusa fainali za AFCON 2015

MABINGWA watetezi wa Kombe la Afrika, Nigeria imelipiza kisasi kwa Sudan kwa kuilaza mabao 3-1, wakati Ivory Coast ikifumuliwa mabao 4-3, huku Uganda ikigawa pointi tena kwa Togo kwa kukubali kipigo cha bao 1-0 kwenye mechi za kuwania kucheza Fainali za Kombe la Afrika zitakazofanyika mwakani nchini Morocco.
Nigeria mabyo ilitoka kupigwa mabao 2-0 na Sudan kwenye mechi iliyochezwa wikiendi iliyopita, ikiwa mjini Abuja waliwakomalia wapinzani wao na kupata ushindi huo muhimu na kufufua matumaini yao ya kwenda kutetea taji hilo Morocco kwa mabao ya Ahmed Mussa aliyefunga mawili dakika ya 48 na 90 na jingine la Aaron Olanare.
Bao la kufutia machozi la Sudan lilifungwa na Mohammed Salah Ibrahim dakika ya 56.
Katika mechi nyingine za mashindano hao Ghana ilipata ushindi mnono nyumbani dhidi ya Guinea waliotoka nao sare siku chache zilizopita.
Mabao ya washindi yalifungwa na Asamoh Gyan aliyefunga dakika ya 16 kabla ya Ander Ayew 'Pele' kuongeza la pili kwa mkwaju wa penati dakika ya 58 na Agyemang-Badu kufunga la tatu dakika za jioni, huku wapinzani wao wakipata bao kupitia kwa Mohammed Yattara.
Uganda ikiwa mjini Lome Togo, ilishinda kulip[a kisasi kwa wenyeji wao kwa kukubali tena kicvhapo cha bao 1-0 na kuzidi kuwaweka pabaya katika mbio za kwenda Morocco.
Bao lililoiangamiza Uganda The Cranes lilifungwa na Serge Akakpo dakika ya 70 na kuifanya Togo kupanda hadi nafasi ya pili katika kundi hilo la E ikiwa na pointi 6, ikishusha Uganda inayosaliwa na pointi zake nne.
Katika mechi za kundi F, Zambia iliendeleza ubabe kwa kuinyuka Niger mabao 3-0 katika pambano lililiochezwa mjini Lusaka kupitia mabao ya Rainford Kalaba, Emmanuel Mayuka na Kenned Mweene aliyefungwa kwa penatui.
Nayo Misri ilipata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Botswana wakirejea ushindi kama huo walioupata katika mechi iliyopita siku chache zilizopita wakiwa ugenini.
Mabao ya washindi yalifungwa na Amr Gamal na Mohammed Salah, huku Cameroon ikizinduka na kuinyuka Sierra Leone kwa mabao 2-0 kupitia mabao ya mapema ya Leonard Kweuke na Stephane Mbia na kuifanya tuimu hiyo inuse fainali hizo za mwakani kwa kufikisha pointi 10 ikifuatiwa na Ivory Coast ambayo walikung'utwa mabao 4-3 na DR Congo katika mechi iliyosisimua.
Magoli ya DR Congo yalifungwa na Neeskens Keban dk ya 21, Junior Kabananga dk ya 35 na Jeremy Bokila dakika ya 36 na 89 huku magoli ya wageni waliocheza pungufu baada ya kumpoteza Yannick Kessie aliyetolewa kwa kadi nyekundu dakika ya 47, yalipachikwa wavuni na Mwanasoka Bora wa Afrika Yaya Toure na Solomon Kalou aliyefunga mawili.

Wednesday, October 15, 2014

Suarez akiri ilikuwa vigumu kukiri kosa la kumng'ata Chiellini

http://vertienteglobal.com/wp-content/uploads/2014/06/luis-suarez-anota-gol.jpghttp://img2.timeinc.net/people/i/2014/news/140707/luis-suarez-600.jpgSTRIKA nyota wa Barcelona, Luis Suarez amesema ilikuwa ngumu kukubaliana na ukweli wa kumng’ata beki wa Italia Giorgio Chiellini katika michuano ya Kombe la dunia nchini Brazil. 
Nyota huyo wa kimataifa wa Uruguay aliyejiunga na Barcelona akitokea Liverpool kwa kitita cha Pauni Mil. 75 alifungiwa miezi minne kutokana na tukio hilo. 
Akihojiwa strika huyo amesema alikuwa akiona vigumu kukubali alichokifanya kwani yeye ni binadamu kama walivyo wengine. 
Suarez, 27, amesema alikuwa hataki kumsikiliza yeyote au kuongea na yeyote kwa sababu alikuwa hataki kukubaliana na ukweli. 
Suarez alimuomba radhi Chiellini Juni 30 zikiwa zimepita siku sita toka afanye tukio baada ya Uruguay kushinda bao 1-0 dhidi ya Italia, msamaha ambao ulipokelewa na beki huyo na kueleza matumaini yake kama Shirikisho la Soka Duniani-FIFA lingeweza kumpunguzia adhabu hiyo. 
Kabla kuomba radhi Suarez alikanusha kwa kudai kuwa aliteleza bahati mbaya na usoni mwa Chiellini na kumuangukia jambo ambalo lilikuwa kama vichekesho kwani tukio hilo lote lilionekana katika picha za video.

Ronaldo alibeba Ureno, Ujerumani bado gonjwa Ulaya

http://i.ytimg.com/vi/TevIMI1W8NI/0.jpg
Ronaldo akishangilia bao lake lililoiua Denmark nyumbani kwao
http://www.101greatgoals.com/wp-content/uploads/2014/10/Screen-Shot-2014-10-14-at-23.54.46.png
Wachezaji wa Ireland wakishangilia bao lao la kusawazisha dhidi ya Ujerumani
http://www.theglobeandmail.com/sports/soccer/article21090950.ece/BINARY/w620/510260433_534397343.JPG
Mabingwa wa Dunia, Ujerumani wakihenyeka uwanjani dhidi ya Jamhuri ya Ireland
WAKATI Mabingwa wa Kombe la Dunia Ujerumani wakiwa hawajatulia, Mwanasoka Bora wa Dunia, Cristiano Ronaldo usiku wa jana aliifungia timu yao ya Ureno bao pekee lililowapa ushindi dhidi ya Denmark uwanja wa ugenini katika mbuio za kuwania Fainali za Kombe la Mataifa ya Ulaya Euro 2016.
Ujerumani inayouguza kichapo cha mabao 2-0 ilichopewa na Poland wikiendi iliyopita ilishindwa kulinda bao lake na kujikuta wakilazimishwa sare ya baoa 1-1 nyumbani na Jamhuri ya Ireland waliochomoa bao 'jioni'.
Ton Kroos aliiandikia wenyeji bao la kuongoza dakika ya 71, lakini wageni walikaza msuli na kulirejesha dakika za nyongeza kupitia John O'shea na kufanya timu hizo kugawana pointi huku Poland wakilazimishwa sare ya mabao 2-2 na Scotland ikiwa nyumbani.
Matokeo ya mechi nyingine ni kwamba Ureno ikiwa ugenini iliizabua Denmark kwa bao 1-0 lililofungwa na nahodha wake Cristioano Ronaldo katika dakika ya lala salama mashabiki wakiamini kuwa timu hizo zimetoka suluhu na kuifanya Ureno kufikisha jumla ya pointi tatu na kushika nafasi ya tatu.
Katika mechi nyingine za michuano hiyo, Gibraltar imeendelea kutoa takrima baada ya kugongwa nyumbani mabao 3-0 na Georgia, San Marino kulazwa mabao 4-0 nyumbani na Uswisi, wakati Visiwa vya Faroe walilala nyumbani pia kwa bao 1-0 kutoka kwa Hungary, Finland ikafa pia nyumbani kwa mabaop 2-0 kw akipigo cha Romania na Ugiriki ikaendeleza unyonge kwa timu zilizocheza nyumbani jana kwa kulazwa mabao 2-0 na Ireland ya Kaskazini.

Kivumbi Afrika, Nigeria vs Sudan, Uganda v Togo hapatoshi!!

https://media.premiumtimesng.com/wp-content/files/2014/06/Eagles-Getty-images.jpg
Watetezi Nigeria
http://static.pulse.ng/img/incoming/origs3188111/4750486101-w980-h640/The-Sudanese-national-team.jpg
Sudan
http://www.goal-news.com/wp-content/uploads/2014/10/Guinea-vs-Ghana.jpg
Ghana
http://www.redpepper.co.ug/wp-content/uploads/2014/08/1.-EBOLA-OR-NOT-The-Cranes-are-ready-to-fly-to-Morocco-Picture-by-John-Batanudde-445x350.jpg
Uganda watacheka kama hivi leo kwa Togo
VUMBI la michuano ya kuwania kufuzu Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika, AFCON-2015 linatarajiwa kuendelea kutimka leo wakati mechi kadhaa zitapigwa kwenye mataifa mbalimbali barani Afrika.
Cameroon iliyong'ang'aniwa katika mechi iliyopita na Sierra Leone itakuwa nyumbani kurudiana na majirani zao hao, wakati Togo iliyoiduwaza Uganda The Cranes mjini Kampala itaialikia wapinzani wao hao katika pambano la kusisimua.
Mabingwa watetezi waliofumuliwa mjini Khartoum na wenyeji wao Sudan itajiuliza nyumbani huku Angola na Lesotho zitaonyeshana kazi mjini Luanda.
Mechi nyingine za makundi hayo zitakuwa kama ifuatavyo;
Ghana vs    Guinea
Zambia vs    Niger
Côte d'Ivoire vs    Congo DR   
Egypt vs Botswana   
Cape Verde Islands vs Msumbiji
Mali vs Ethiopia
Burkina Faso vs    Gabon
South Africa vs    Congo
Tunisia vs    Senegal   
Algeria vs    Malawi

Msiba! Muimbaji wa zamani Extra Bongo afariki dunia

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgQc1H5GJ4HwdiXPaWbq-vVhWG0Bm2Vi87Ia9OXMQL5oKZR41D0Hvg8X4TGWY439EgCeIYuWHEJPboaoLwTISvctf3TKJVmvXtVjQFjLJQQRltQP02J05yvMNyCViL0_9LwVpTL8swJgrs/s400/P1191212.JPG
Suzuki enzi za uhai wake
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhFhXutATUb6_ogGzQhP1FoqA9uKARlTfPORgEC6yTP-kCm0Wggg8WAt_Ne5GzHPzDDHbaEikGcRE9B53AYkJ-gMmL1fkvt6KkDpCYYUY_zS9m_vVA16ZWnOLkQV38zDGrRyVxrngyVxX8/s400/P1211580.jpg
Seleman Ramadhan Suzuki Sauti ya Malaika enzi za uhai wake
MWANAMUZIKI nyota wa zamani wa bendi za Mikumi Sound, Levent Musica na Extra Bongo 'Wana Next Level', Suleiman Ramadhani 'Suzuki Sauti ya Malaika' amefariki dunia usiku wa kuamkia leo baada ya kuugua muda mrefu.
Kwa mujibu wa mwanamuziki mwenzake ambaye alikuwa akifuatilia afya yake kipindi akiugua, Ramadhani Mhoza 'Pentagone' ameiambia MICHARAZO, Suzuki amefariki akiwa nyumbani eneo la Magomeni Kagera, jijini Dar es Salaam na huenda akazikwa leo au kesho.
Pentagone aliyefanya kazi na mwanamuziki huyo aliyekuwa na uwezo wa kutunga, kuimba na kurapu  katika bendi za Levent Musica 'Wazee wa Kumuvuzisha' na Extra Bongo, alisema Suzuki alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa Kisukari na alikuwa akitibiwa nyumbani kwa dawa za kienyeji.
"NIlitaka kukutaarifu kubwa swahiba yetu Suzuki hatunaye kwani amefariki usiku wa leo na kwa sasa tunaangalia mipango ya mazishi kwa kuwasiliana na ndugu zake wa karibu," alisema Pentagone ambaye kwa sasa anaiimbia African Stars 'Twnaga Pepeta'.
Enzi za uhai wake, Suzuki anayetokea Kigoma alitamba na bendi za Tabiora Jazz kabla ya kutua Morogoro katika bendi ya Mikumio Sound iliyowahi kutamba na albamu ya Mlinzi wa Godown kabla ya kuitua Levent Musica na baadaye yeye na wanamuziki wenzake watatu, Bob Kissa, Pentagone na Athanas Montanabe walihamia kwa mpigo Extra Bongo na kupakua albamua ya Mjini Mipango.
Mungu Ailaze Roho ya Marehemu Mahali Pema Peponi na MICHARAZO inatoa pole kwa wote walioguswa kwa namna moja au nyingine na msiba huio na kuwaomba kuwa na moyo wa Subira kwa kukumbuka kuwa 'Kila Nafsi Itaonja Mauti' na Sisi ni wa Mola na Kwake Hakika Tutarejea'.

Tuesday, October 14, 2014

Argentina yaiangamiza Hong Kong, Messi aanzia benchi

International friendlies - Argentina stroll to seven-goal victory over Hong Kong
Wachezaji wa Argentina wakipongeza kwa kuinyoa Hong Kong mabao 7-0
ARGENTINA iliyotoka kukung'utwa mabao 2-0 na Brazil mwishoni mwa wiki nchini China, leo imezinduka kwenye mechi zake za kirafiki za kimataifa baada ya kuinyoa Hong Kong mabao 7-0.
Ever Banega alianza kuiandika wageni bao dakika ya 19 kabla Gonzalo Higuan kuongeza la pili katika dakika 42 kwa pasi ya Vangioni na Nicolas Gaitan kuongeza la tatu sekunde chache kabla ya mapumziko.
Kipindi cha pili Higuan alikianza kwa kuongeza bao la tatu dakika ya 54 akimalizia kazi ya Gaitan na baada ya Messi kuingia dimbani aliongeza bao la tano dakika ya 66 kwa kazi nzuri ya Banega.
Gaitan hakutosheka kwa kufunga bao jingine lililokuwa la sita kwa Wanafainali hao wa Kombe la Dunia kwenye dakika ya 72 na Messi kuongeza bao la mwisho  dakika sita kabla a filimbi ya mwisho.

Neymar 4 Japan 0, China yaigonga Paraguay, Costa Rica ikiiua Korea

International friendlies - Four-goal Neymar destroys Japan to reach 40 for Brazil
Akishangilia bao lake la tatu
Neymar célèbre sa prestation exceptionnelle avec le Brésil contre le Japon
Neymar akishangilia moja ya mabao yake mchana huu wakati wanaizamisha Japan kwa mabao 4-0
MSHAMBULIAJI nyota wa Barcelona, Neymar amethibitisha kuwa yeye ndiye kila kitu Brazil baada ya kuifungia timu yake mabao manne wakati timu yake ya taifa ikiiadhibu Japan katika mechi ya kurafiki ya kimataifa.
Neymar alifunga mabao hayo wakati wakipata ushindi wa mabao 4-0 kwenye uwanja wa Singapore ambapo Japan walikuwa kama hawapo uwanjani kwa jinsi alivyothibitiwa.
Mkali huyo alianza kuandika bao dakika ya 18 akimalizia kazi nzuri ya Diego Tardelli kabla ya kuongeza jingine dakika chache baada ya kuanza kipindi cha pili akimalizia kazi nzuri ya Coutinho.
Neymar aliongeza bao la tatu dakika ya 77 kabla ya kupigilia msumari wa mwisho katika dakika ya 81 kwa mpira wa kichwa akiunganisha krosi pasi ya Kaka na kuzidi kumpa raha kocha Dunga anayeinoa Brazil kwa sasa.
Katika mechi nyingine ya kirafiki ya kimataifa, China iliiduwaza Paraguay kwa kuwacharaza mabao 2-1. Mabao ya washindi yalifungwa dakika 20 za awali na Zheng Zi na Wu Lei kabla Ortigoza kuipatia Paraguay bao la kufutia machozi dakika za jioni.
Nayo timu ya Costa Rica Iliiadhibu Jamhuri ya Korea kwa mabao 3-1 katika mchezo mwingine mkali wa kirafiki wa kimataifa uliochezwa mapema mchana wa leo.
Katika mechi nyingine inayoendelea kwa sasa nchini Hongkong, wenyeji wameshakandikwa mabao 6-0 na Argentina na bado dakika kama 15 kabla ya mchezo huo kuisha, Messi akifunga moja na mengine yakiwekwa kimiani na Higuan mawili na Gaitan pia mawili na Banega













Walcott aleta faraja Emirates, arejea dimbani

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi7rsOPqad07I0-k-H9Wizxmhn3SadOqRP-R8t_WrVlo9OuD_iKPU-5OrSvwOjl7ep-fECxEgRe76HGH3E813ae1BNR-w-C9Q2n7-kgAj7OJ9wvRHEa9Jqllo3WVvlDEy7ddyizp79fZBea/s1600/Theo+Walcott+wallpaper+13.jpgWINGA machachari, aliye nyota wa Uingereza, Theo Walcott ameleta faraja kwa mashabiki wa Arsenal baada ya kurejea dimbani kutoka kwenye hali ya majeruhi kwa muda wa miezi 10 iliyopita kwa kujiumiza vibaya goti lake.
Walcott, 25, hajacheza tangu kukata mishipa ya goti lake la kushoto kwenye ushindi wao wa 2-0 dhidi ya wapinzani wao wa London Kaskazini, Tottenham Hotspurs katika Kombe la FA Januari.
“Ni shangwe kukukaribisha tena @theowalcott!” Arsenal waliandika kwenye anwani yao rasmi ya mtandao wa kijamii wa Twitter pamoja na picha yake akipasha misuli na wenzake.
Arsenal watakaribisha Hull City Jumamosi kwenye pambano la Ligi Kuu ya England akiungana na kiungo mwenzake wa pembeni, Serge Gnabry aliyekuwa akiuguza pia goti tangu Machi.
Wawili hao wameinua mioyo ya Ze Gunnerz ambayo itawakosa nyota wake kadhaa waliopo kwenye 'wadi' ya majeruhi viunga vya Emirates akiwamo Mesut Ozil.

Kuziona Simba na Yanga ni Buku 7 tu

Yanga
Simba
SHIRIKISHO la Soka Tanzania, TFF, limetengaza viingilio vya pambano la watani wa jadi Simba na Yanga litakalochezwa Jumamosi ambapo cha chini kabisa ni Sh. 7,000.
Washabiki watakaolipa kiingilio hicho ni wale watakaokaa viti vya rangi ya bluu na kijani ambavyo jumla yake ni 36,693 katika uwanja huo wenye viti 57,558. Viingilio vingine ni sh. 10,000 kwa viti vya rangi ya chungwa, sh. 20,000 kwa VIP B na C wakati VIP A itakuwa sh. 30,000. Tiketi zitakazotumika kwenye mechi hiyo ni za elektroniki, na zimeanza kuuzwa jana (Oktoba 13 mwaka huu). Tiketi zinapatikana kwa mtandao wa M-PESA, CRDB Simbanking na maduka ya CRDB Fahari Huduma ambayo yapo zaidi ya mia moja sehemu mbalimbali jijini Dar es Salaam.
Mechi hiyo namba 27 itakayochezeshwa na mwamuzi Israel Mujuni Nkongo akisaidiwa na John Kanyenye na Ferdinand Chacha itaanza saa 10 kamili jioni. Kamishna wa mechi hiyo ni Salum Kikwamba kutoka mkoani Kilimanjaro.
Washabiki wanatakiwa kununua tiketi mapema, kwani hazitauzwa uwanjani siku ya mechi. Milango yote ukiwemo ule wa upande wa Mbagala (Uwanja wa Ndani) itafunguliwa kwa ajili ya washabiki, na itakuwa wazi kuanzia saa 4 asubuhi.
Magari maalumu tu yenye stika ndiyo yatakayoruhusiwa kuingia uwanjani kwa kupitia Barabara ya Mandela. 
Pia washabiki hawaruhusiwi kuingia uwanjani wakiwa na silaha, vitu vya vyuma na mabegi makubwa. Barabara ya kuingilia upande wa Chang’ombe itafungwa kwa watumiaji wa magari.

Morocco yaigonga Kenya 3-0 kirafiki

http://i.ytimg.com/vi/fkaBqomsiF4/maxresdefault.jpgTIMU ya soka ya taifa ya Morocco imeendelea kutoa dozi kwa wapinzani kwenye mechi za kirafiki baada ya usiku wa jana kuikong'ota Kenya Harambee Stars kwa mabao 3-0 ikiwa ni siku chache tangu iishindilie Jamhuri ya Afrika ya Kati kwa mabao 4-0 siku ya Ijumaa.
Mabao ya dakika 15 za mwisho yalitosha kuwatia adabu Harambee Stars ambao walionyesha kandanda zuri kwa muda mrefu wa mchezo kabla ya kuruhusu mabao hayo matatu.
El Mehdi Karnass, Mbark Boussoufa na Mouhcine Iajour kila mmoja alifunga bao moja ndani ya dakika hizo 15 kabla ya pambano hilo kumalizika na kuwapa wenyeji ushindi huo kwenye uwanja wa Marrakech na kuzidi kumpa CV nzuri kocha Ezzaki Badou ambaye katika mechi tatu za karibuni ameshinda zote kwa idadi ya mabao 10 baada ya awali kuwalaza pia Libya mabao 3-0..
Kwa Harambee inayoniolewa na kocha Adel Amrouche ilikuwa ni mechi ya sita ya kimataifa bila kupata ushindi wowote.

Suarez arejea na mabao Uruguay, afunga mbili wakiiua Oman x3

http://level3.soccerladuma.net/cms2/image_manager/uploads/News/166456/7/default.jpgMSHAMBULIAJI nyota wa Barcelona, Luis Suarez amerejea uwanjani na makali yake yale baada ya usiku wa jana kuisaidia timu yake ya taifa ya Uruguay kupata ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya wenyeji wao Oman.
Pambano hilo la kimataifa la kirafiki lililochezwa kwenye uwanja wa Sultan Qoboos mjini Muscat, Suarez aliyekuwa akicheza mechi yake ya pili ya kimataifa tangu alipotoka kifungoni alifunga mabao mawili.
Suarez alifunga mabao hayo kwenye dakika ya 57 akimalizia kazi nzuri ya Rolan na katika dakika ya 67 kwa pasi ya Ramirez kabla ya Jonathan Rodriguez kufunga la tatu dakika ya 87.
Mshambuliaji huyo wa zamani wa Liverpool alifungiwa na FIFA kutokana na kitendo cha kumng'ata beki wa Italia, Giorgio Chiellini katika michuano ya Kombe la Dunia zilizochezwa nchini Brazil.

WENGER HAJUTII KUTOMSAJILI FABREGAS

http://static.sportskeeda.com/wp-content/uploads/2014/06/104741_heroa-1402851267.jpgKOCHA wa Arsenal, Arsene Wenger, amesisitiza kwamba hajuti kumsajili Cesc Fabregas katika kipindi kilichopita cha usajili.
Kiungo huyo wa kimataifa wa Hispania alijiunga na Chelsea akitokea Barcelona kwa ada ya uhamisho ya paundi milioni 27 mwezi Juni na ametisha chini ya Mourinho akitoa pasi za mwisho zilizozaa magoli 7 katika mechi 7, idadi ambayo ni sawa na pasi za mwisho zote zilizopigwa na timu nzima ya Arsenal hadi sasa.
Fabregas ambaye aliichezea Arsenal kwa miaka nane kabla ya kurejea Barcelona 2011, alibainisha katika barua yake ya wazi kwamba Arsenal walikataa kukitumia kipengele cha mkataba cha kumsajili tena kama wanamhitaji kabla ya klabu nyingine kupewa ofa hiyo.
Lakini, Wenger amesisitiza kwamba ana wachezaji wengi wa eneo la kiungo na anaamini kwamba timu yake itapunguza pengo la pointi dhidi ya Chelsea licha ya kulala 2-0 kwenye Uwanja wa Stamford Bridge kabla ya wikiendi ya mechi za kimataifa. 
"Sijutii kutomchukua Cesc kwa sababu tayari tuna wachezaji wengi wa ubunifu katika eneo letu la kiungo," Wenger aliiambia BeIN Sports.
"Chelsea watatakuwa na kipindi kigumu (katika msimu). Ratiba yetu ilikuwa ngumu mno na ninaamini kwamba tunaweza kuziba pengo dhidi yao."

Monday, October 13, 2014

'HATUITAKI KATIBA MPYA PENDEKEZWA'

CHAMA cha Wananchi (CUF) kimesema hakiikubali Katiba inayopendekezwa kwa kuwa haina maslahi ya wananchi wa Zanzibar.
Badala yake chama hicho kimewataka Wazanzibari waikatae Katiba iliyopendekezwa na Bunge Maalum la Katiba (BMK).
Kauli hiyo ilitolewa jana na Katibu Mkuu wa CUF ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad, wakati akihutubia mkutano mkubwa wa hadhara katika viwanja vya Demokrasia vya Kibanda Maiti, mjini Zanzibar.
“Wananchi, Katiba haikubaliki kwa Wazanzibari, mimi mwenzenu siikubali, sijui nyinyi wenzangu?” alihoji Maalim Seif na wananchi kuitikia kuwa nao hawaikubali.
Alisema kuwa miongoni mwa mambo yanayoipokonya Zanzibar hadhi yake ni Katiba inayopendekezwa kumpokonya Rais wa Zanzibar mamlaka ya kugawa mikoa, tofauti na Katiba ya Zanzibar ya sasa. 
Alisema kwa maana hiyo Rais wa Muungano anachukua mamlaka ya Rais wa Zanzibar na anaweza kuteuliwa wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya wa Zanzibar. 
“Kwa mabadiliko hayo ya rasimu ya Chenge, Rais wa Muungano anaweza kututeulia Sheha wa Shehia ya Mtoni Zanzibar kutoka Bukoba,” alisema Maalim Seif huku akishangiliwa na wanachama na wafuasi wa CUF.
Maalim Seif alisema Katiba ya Zanzibar na marekebisho yake ya mwaka 2010 iko sahihi kabisa na inazingatia matakwa ya Makubaliano ya Muungano.
Alisema hayuko tayari kuona rasimu hiyo inakubalika na kwamba Wazanzibari hawataki kuiona.
Alisema hakubaliani na kauli za baadhi ya watu waliosema kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) inaridhishwa na mchakato wa Katiba mpya.
“Nataka kuwambia hakuna kikao chochote cha SMZ kilichokaa na kusema tunaijadili rasimu, kama kuna mtu anataka kusema eti Smz imeridhishwa aseme mwenyewe binafsi na siyo Serikali ya Umoja wa Kitaifa,” alisema Maalim Seif.
Maalim Seif aliisifu Rasimu ya Jaji Joseph Warioba ambayo ndiyo ilizingatia matakwa ya Watanzania walio wengi na kwamba pamoja na awali Wazanzibari kupendekeza muundo wa Muungano wa mkataba, lakini kwa busara ya tume hiyo waliikubali muundo wa serikali tatu.
Maalim Seif alisema anahutubia mkutano huo akiwa na furaha kubwa kutokana na umma ulioteremka katika viwanja vya Kibandamaiti, na hiyo ni sababu tosha na ujumbe kuwa hawaitaki Katiba inayopendekezwa.
“Ndugu yangu, rafiki yangu Rais Jakaya Kikwete ufahamu kuwa umma huu uliohudhuria Kibandamaiti ni ujumbe tosha kuwa Katiba hiyo hawaitaki, na mwambia Rais Kikwete kuwa Katiba hii hatuikubali,” alisema Maalim Seif. 
Maalim Seif alisema Katiba bora ni ile inayozingatia maoni ya wananchi. 
“Lakini Rais (Rais Jakaya Kikwete), Katiba yenu mmeweka upande maoni ya wananchi, mmejifungia wenyewe, mmeipitisha wenyewe na mmeichezea ngoma wenyewe”, alisema. 
Naibu Katibu Mkuu wa CUF, Nassor Ahmed Mazrui, alisema wajumbe saba wa Bunge Maalum la Katiba waliopiga kura ya Hapana hadharani kukataa rasimu hiyo ni mashujaa wa Zanzibar na Wazanzibari wote wanapaswa kuwapa heshima kubwa.
Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa CUF, Salum Bimani, alisema wananchi wa Zanzibar wameshaamua na hawatarejea nyuma zaidi ya kuiondoa CCM mwaka 2015 na kuipa Zanzibar mamlaka kamili.
Bimani alisema msiwape kura viongozi wa CCM ambao wanauza nchi ya Zanzibar huku wakicheza ngoma.
“Kwa Shilingi 300,000 watu hawa wanadiriki kuuza nchi, hawa waliopiga kura za ndiyo ni madalali wa Zanzibar, hata wale waliopiga kura za siri pia ni madalali,” alisema Bimani.
Alisema wanasheria wawili wameitetea Zanzibar na wakafikwa na masahiba mazito.
Aliwataka wanasheria hao kuwa Jaji Walfgong Dourado na Mwanasheria Mkuu wa Serikali aliyefutwa kazi, Masoud Othman Masoud.
Bimani alisema Wazanzibari wapo pamoja nao katika kuhakikisha Zanzibar inabaki na wale wenye nia mbaya wajue kwamba Zanzibar wataitapika watake wasitake. 
Mansour alisema naendelea kuwa muumini wa Maridhiano ya Zanzibar. Katiba hii ni yao wenyewe si ya Wazanzibari.
“Baada ya kuona umma huu uliohudhuria katika mkutano huu tunapaswa kumhofia Mwenyezi Mungu,” alisema.
“Naendelea kumuunga mkono Maalim Seif Sharif Hamad, ni kiongozi asiyekuwa mnafiki anajitambua na hatawaliwi na utawala wa Dodoma, anatawaliwa na Wazanzibari wenyewe na matakwa na matumaini yao,” alisema na kuwataka Wazanzibari wasiwe na hofu kwani hawawezi kufungwa wote wako wengi sana, wakati umefika. 
“Tumeungana kwa hiari yetu, tukakubali kwa hiari yetu, sisi si watumwa wa mtu yoyote, tumefungwa tumefukuzwa makazini kwa sababu ya nchi hii, hatuwezi kurudi nyuma,” alisema.
Alieleza kuwa watu wasishangae kumuona Mwenyekiti wa Kamati ya Maridhiano, Mzee Nassoro Moyo, amesimama kwenye jukwa anatetea nchi yake.
Mzee Moyo alisema Wazanzibari hawakubalini kuona watu wanataka kuichukua nchi yao ovyo ovyo.
Mkutano huo ambao ni wa kwanza kuhutubia na Maalim Seif tangu BMK limalize kazi yake na kuwasilisha rasimu kwa Rais Jakaya Kikwete na Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohammed Shein, ulihudhuriwa na maelefu ya wananchi huku baadhi yao wakibeba mabango.
Baadhi ya mabango hayo yalibeba ujumbe usemao “Wapige mabomu rasimu yao hatuitaki, Hongera Othman Masoud, Katiba ya vijisenti (Chenge) hatuitaki”. 
Katika hatua nyingine, Maalim Seif alikanusha taarifa kwenye mitandao kuwa hatajiuzulu wadhifa huo na ataendelea kukiongoza CUF kushika madaraka na kushika Serikali ya Umoja wa Kitaifa katika uchaguzi mkuu wa mwakani, akiwa kwenye nafasi hiyo.
Maalim alisema taarifa zilizoenezwa kwenye mitandao ya kijamii kuwa baada ya kufukuzwa Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar, Masoud Othman Masoud, naye amejiuzulu Umakamu wa Kwanza ni uzushi mtupu.
CHANZO: NIPASHE

CAF yaichomolea Morocco AFCON 2015

http://static.goal.com/243400/243477_heroa.jpgSHIRIKISHO la Soka Afrika, CAF, limeichomolea Morocco wenyeji wa Fainali za Afrika za mwakani, ambao waliomba kuahirishwa kwa michuano hiyo kwa hofu ya ugonjwa wa EBOLA.
CAF wamesisitiza kuwa fainali hizo za mataifa ya Afrika 2015 itaendelea kama ilivyopanga licha ya hofu ya wenyeji dhidi ya ugonjwa huo hatari.
Morocco waliomba shindano hilo liahirishwa kufuatia mripuko wa ugonjwa huo ambao umeua watu zaidi ya 4,000 baada ya maafisa wa afya nchini humo kuonya kuendelea kwa fainali hizo kwa madai yanaweza kuendeleza uambukizaji zaidi.
Mshauri wa Waziri wa Michezo wa Morocco, Mohammed Ouzzine, alieleza taifa hilo la magharibi mwa bara hilo lina wasiwasi kuandaa shindano hilo linalochukua wiki tatu.
“Matakwa ya Morocco na wakaazi wake pamoja na wale wa bara Afrika yanadunisha linguine lolote. Morocco wamewasilisha ombi hilo kufuatia ushauri muhimu kutoka maafisa wa afya.
“Hatuwezi hatarisha maisha ya watu kwa kuendelea kuandaa shindano hili kwani msingi wa tahadhari unafaa kufuatwa,” mshauri Hamid Faridi aliambia stesheni ya redio, Atlantic Jumamosi.
Kwa majibu, Caf walitoa taarifa wakitofautiana na wenyeji hao huku Afrika Kusini wakilengwa kama waandalizi wa dharura ikiwa Morocco watajiondoa.
“Caf wanadhibitisha hakuna badiliko kwenye ratiba ya shindano hili. Tungependa kukumbusha kwamba tangu dimba la kwanza la 1975, shindano hili halijawahi chelewa au kuhairishwa,” taarifa ya utawala huo wa kandanda ilisema.
Mataifa ya Afrika magharibi, Guinea, Liberia na Sierra Leone yameadhirika zaidi na mkurupuko wa sasa wa Ebola. Guinea na Sierra Leone bado wanawania tiketi za Morocco 2015.
Afrika Kusini waliokoa jahazi la shindano hilo 1996 na mwaka jana.

ARSENAL MAJANGA, MAJERUHI WAZIDI KUONGEZEKA

http://img.bleacherreport.net/img/images/photos/003/042/640/hi-res-a01b8eaefd6aaec9613b24d358507950_crop_north.jpg?w=630&h=420&q=75KLABU ya Arsenal imezidi kupata pigo baada ya nyota wake kadhaa kupata majeraha, kufuatia kuumia kwa beki Laurent Koscielny aliyelazimika kujiondoa kwenye mazoezi ya timu yake ya kitaifa ya Ufaransa.
Beki huyo wa kati amejitoa Les Blues kutokana na maumivu ya ukano wa kisigino.

Meneja Arsene Wenger amepigwa na pigo moja baada ya lingine ikiwa ni mechi saba tu ndani ya msimu mpya huku ambapo sasa Koscielny anajiunga na nyota wenzake Danny Welbeck, Mathieu Debuchy, Mikel Arteta, Olivier Giroud, David Ospina, Aaron Ramsey na Yaya Sanogo kwenye zahanati.

Siku mbili baada ya Ujerumani kutangaza kiungo nyota Mesut Ozil atalazimika kutocheza kati ya wiki 10 na 12, Wenger ameongezewa tumbo joto na habari kuwa beki Koscielny amejiondoa kutoka mechi za Ufaransa dhidi ya Ureno na Armenia kwenye msururu wa kufuzu Kombe la Euro la 2016, huku Danny Welbeck naye akiiumia wakati England ikishinda 1-0.
Shirikisho la Ufaransa limeandika kwenye anwani yao ya mtandao wa kijamii wa Twitter kuwa Koscielny anauguza uvimbe wa ukano wake wa kisigino.

Kocha Nigeria aweweseka kipigo cha Sudan, aomba radhi

http://mobifootball.com/wp-content/uploads/2013/08/B13FEGB0345.jpgKOCHA wa timu ya taifa ya Nigeria, Stephen Keshi bado yuko katika mshangao kufuatia kipigo walichopata kutoka kwa Sudan katika mchezo wa kufuzu michuano ya Mataifa ya Afrika. 
Super Eagles walishindwa kucheza kwa kiwango chao cha juu na kujikuta wakichapwa bao 1-0 katika Uwanja wa Manispaa jijini Khartoum katika mechi za kuwania Fainali za Kombe la Afrika mwakani. 
Keshi amesema kikosi chake kingeweza kuibuka na ushindi katika mchezo huo kama nafasi walizotengeneza zingetumika ipasavyo lakini haraka aliwaomba radhi mashabiki wa Nigeria kwa kupoteza mchezo huo. 
Kocha huyo amesema inabidi aombe radhi kwani mashabiki wa Nigeria walikuwa na imani kubwa na timu yao kuibuka na ushindi. 
Mbali na Keshi lakini pia golikipa na nahodha wa Super Eagles Vincent Enyeama naye aliwaomba radhi mashabiki kwa kipigo hicho na niaba ya wachezaji wenzake na kuahidi kufanya vyema katika michezo yao inayofuata.

Dk Ndumbaro yamkuta, afungiwa miaka 7 katika soka

BAADA ya tetezi zilizokuwa zikizagaa kwamba huenda Mwanasheria wa klabu za Ligi Kuu Tanzania Bara, Dk Damas Ndumbaro yupo kitanzini na huenda akaadhibiwa kwa kauli alizotoa hivi karibuni kuhusiana na makato ya 5% zilizotakiwa na Shirikisho la Soka Tanzania, TFF, hatimaye imethibitika kuwa kweli.
Kamati ya Nidhamu ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), imemfungia Dk Ndumbaro kujihusisha na mambo ya soka kwa muda wa miaka saba na faini ya kiasi cha fedha.
Ndumbaro ambaye aliingia katika mzozo mkubwa na Rais wa TFF, Jamal Malinzi wiki iliyopita baada ya TFF kuagiza kila klabu kukatwa asilimia tano za mapato yatokanayo na udhamini wa klabu hizo wanaoupata kutoka kwa Vodacom, wadhamini wakuu wa ligi kuu ya Tanzania Bara, na Azam TV.
Ndumbaro alikimbilia katika vyombo vya habari na kusema wazi kuwa, klabu zimemuagiza kuwaambia TFF kuwa havipo tayari na havitakubali jambo hilo litokee, huku akijiamini na kuchambua baadhi ya vipengele na mambo ya sheria, Ndumbaro alivuka mipaka pale aliposema kuwa wanatafuta wastani wa wajumbe wa mkutano mkuu wa TFF na kupiga kura ya kutokuwa na imani na rais wa shirikisho, Malinzi.
Kikao cha juzi cha kamati ya nidhamu kimefikia uamuzi wa kumfungia, Ndumbaro na kumlilipisha faini kwa sababu, Ndumbaro ambaye alizungumza kama wakili wa klabu za ligi kuu kupitia,.
TFF imedai Ndumbaro amekanwa na klabu ingawa taarifa zinaeleza si kweli kwa kuwa viongozi wa klabu 12 walisaini kumpitisha kuwa wakili wao.