STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, February 13, 2015

NASAHA YA IJUMAA- KISA CHA NABII ADAM (AS)

Jinamizi la Sikinde videoni, Valentine wapo Pentagone

BENDI kongwe ya muziki wa dansi ya Mlimani Park 'Sikinde' imerekodi video ya wimbo wao mpya uliobeba jina la albamu ya ijayo iitwayo 'Jinamizi la Talaka',  huku wakiweka bayana kwamba watajumuika na mashabiki wao kusherehekea 'Siku ya Wapendanao' jijini Dar es Salaam.
Mmoja wa viongozi wa Sikinde, Abdallah Hemba, aliiambia MICHARAZO kuwa bendi yao imerekodi video hiyo ambayo ipo hatua za mwisho kukamilishwa kama utambulisha wa ujio wa albamu yao mpya itakayokuwa na nyimbo saba.
Hemba ambaye ni mmoja wa waimbaji nyota nchini alisema kuwa mara video hiyo itakapokamilika wataiachia hewani na kuanza jukumu la kumalizia nyingine za nyimbo zilizosalia kabla ya kufanya uzinduzi baadaye mwaka huu.
"Tumeanza kurekodi video za nyimbo za albamu yetu mpya, tumeanza na 'Jinamizi la Talaka' ikiwa hatua za mwisho na tutaendelea kwa nyingine baadae," alisema Hemba.
Hemba alisema katika kusherehekea Siku ya Wapendanao itakayoadhimishwa kesho, bendi yao itafanya onyesho maalum kwa wakazi wa Kurasini eneo la Mivinjeni katika ukumbi wa Pentagone Pub.
"Tutajumuika na mashabiki wetu eneo la Mivinjeni Kurasini kwa kutambulisha nyimbo mpya na kuwakumbushia za zamani ili kuonyesha tunawapenda katika ukumbi wa Pentagone Pub," alisema Hemba, aliyewahi kutamba na bendi ya Mchinga Sound.

Thursday, February 12, 2015

RATIBA YA MECHI ZA LIGI KUU VPL NDIZO HIZI

JKT Ruvu
Mtibwa Sugar

Ndanda Fc

Ruvu Shooting
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjsiSMyuzw8Scaz_WXLWA8zexyBWABhGV6CxMyERHknqT5Q43BcmRrLvHUNE4oKs2G0hzOPiau9RUA7-sUr7pys-pddVf-7IGaefiwHsTshpDCGxRvAxh3L-kL2Ok3ZtNfCb9E2HTfhftye/s1600/S1.jpg
Simba
Feb 14, 2015
Ndanda vs Mtibwa Sugar
Coastal Union vs Mbeya City
Stand United vs Mgambo Shooting
Feb 15, 2015
Polisi Morogoro vs Simba
Kagera Sugar vs JKT Ruvu
Feb 21, 2015
Mbeya City vs Yanga
Kagera Sugar vs JKT Ruvu
Ndanda vs Coastal Union
Mgambo Shooting vs Mtibwa Sugar
Feb 22, 2015
Stand United vs Simba
Azam vs Tanzania Prisons
Feb 25, 2015
Mbeya City vs Ruvu Shooting

HIVI NDIVYO TFF ILIVYOPANGUA KAMATI ZAKE NDOGO ZA SHERIA

 
JUDICIAL AND STANDING COMMITTEES.

Kamati ya Utendaji iliyoketi tarehe 19 Disemba 2014, ilifanya mabadiliko katika kamati ndogo ndogo na zile za kisheria. Kamati hizo ni kama ifuatavyo

KAMATI YA NIDHAMU
1.   Tarimba Abbas (Mwenyekiti)
2.   Advocate Jerome Msemwa ( Makamu mwenyekiti)
3.    Kassim Dau
4.   Nassoro Duduma
5.   Kitwana Manara 

KAMATI YA RUFANI YA NIDHAMU
1.   Advocate Mukirya Nyanduga (Mwenyekiti)
2.   Advocate Revocatus Kuuli (Makamu mwenyekiti)
3.   Abdala Mkumbura
4.   Dr. Francis Michael
5.   Advocate Twaha Mtengela
 
KAMATI YA MAADILI
1.   Advocate Wilson Ogunde (Mwenyekiti)
2.   Advocate Juma Nassoro (Makamu mwenyekiti)
3.   Advocate Ebenezer Mshana
4.   Geroge Rupia
5.   Mh. Said Mtanda

KAMATI YA RUFANI YA MAADILI
1.   Advocate Walter Chipeta (Mwenyekiti)
2.   Magistrate  George Kisagenta (Makamu-M'Kiti)
3.   Lilian Kitomari
4.   Advocate Abdala Gonzi

KAMATI YA UCHAGUZI
1.   Advocate Melchesedeck Lutema
2.   Advocate Adamu Mambi (Makamu mwenyekiti)
3.   Hamidu Mahmoud Omar
4.   Jeremiah John Wambura
5.   John Jambele

KAMATI YA RUFANI TA UCHAGUZI
1.   Advocate Julius Lugaziya (Mwneyekiti)
2.   Advocate Machare Suguta (Makamu Mwenyekiti)
3.   Idrisa Nassor
4.   Paschal Kihanga
5.   Benister Lugora

KAMATI YA FEDHA NA MIPANGO
1.   Wallace Karia (Mwenyekiti)
2.   Yahya Mohamed (Makamu mwenyekiti)
3.   Goodluck Moshi
4.   Omar Walii
5.   Ellie Mbise
6.    Deo Lubuva

KAMATI YA MASHINDANO
1.   Geofrey Nyange (Mwenyekiti)
2.   Ahmed Mgoyi (Makamu mwenyekiti)
3.   James Mhagama
4.   Stewart Masima
5.   Steven Njowoka
6.   Said Mohamed

KAMATI YA UFUNDI
1.   Kidao Wilfred (Mwenyekiti)
2.   Athumani Kambi (Makamu mwenyekiti)
3.   Vedastus Rufano
4.   Dan Korosso
5.   Pelegriunius Rutahyugwa

KAMATI YA MPIRA WA MIGUU YA VIJANA
1.   Ayoub Nyenzi (Mwenyekiti)
2.    Khalid Abdallah (Makamu mwenyekiti)
3.    Ali Mayay
4.   Mulamu Ngh’ambi
5.   Said Tully

KAMATI YA MPIRA WA MIGUU WANAWAKE
1.   Blassy Kiondo (Mwenyekiti)
2.   Rose Kissiwa (Makamu mwenyekiti)
3.   Zena Chande
4.   Amina Karuma
5.   Zafarani Damoder
6.   Beatrice Mgaya
7.   Sofia Tigalyoma
8.   Ingrid Kimario (Katibu wa Kamati)

KAMATI YA WAAMUZI
1.   Saloum Umande Chama (Mwenyekiti)
2.   Nassoro Said (Makamu mwenyekiti)
3.   Charles Ndagala (Katibu)
4.   Kanali Issaro Chacha
5.   Soud Abdi

KAMATI YA HABARI NA MASOKO
1.   Athuman Kambi (Mwenyekiti)
2.   Alms Kasongo (Makamu Mwenyekiti)
3.   Rose Mwakitangwe
4.   Amir Mhando
5.   Haroub Selemani

KAMATI YA UKAGUZI WA FEDHA
1.   Ramadhan Nassib (Mwenyekiti)
2.   Epaphra Swai (Makamu mwenyekiti)
3.   Jackson Songora
4.   Golden Sanga
5.   Francis Ndulane
6.   Cyprian Kwiyava

KAMATI YA TIBA
1.   Dr. Paul Marealle (Mwenyekiti)
2.   Dr. Fred Limbanga (Makamu mwenyekiti)
3.   Dr. Mwanandi Mwankewa
4.   Dr. Eliezer Ndelema
5.   Asha Mecky Sadik

KAMATI YA FUTSAL NA BEACH SOCCER
1.   Ahmed Idd Mgoyi (Mwenyekiti)
2.   Hussein Mwamba (Makamu mwenyekiti)
3.   Samson Kaliro
4.   Shaffih Dauda
5.   Boniface Pawassa
6.   Apollo Kayugi

PRESIDENTIAL COMMISSION FOR AFFAIRS
1.   Omar Abdulkadir (Mwenyekiti)
2.   Emmanuel Chaula (Makamu mwenyekiti)
3.   Victor Mwandiki
4.   Riziki Majala
5.   Zahra Mohamed
6.   David Nyandu

PRESIDENTIAL COMMISSION ON BUSINESS AND INVESTMENTS
1.   William Erio (Mwenyekiti)
2.   Mbaraka Igangula
3.   Advocate Iman Madega
4.   Lt. Col Charles Mbuge
5.   Philemon Ntalihaja

TIMU ya Taifa ya Beach Soccer kuwafuata Wakenya kesho

TIMU ya Taifa ya Tanzania ya mpira wa ufukweni (beach soccer) inatarajia kurusha karata yake ya kwanza Jumapili kwa kucheza na Kenya katika raundi ya kwanza ya michuano ya Afrika kwa ajili ya fainali za Afrika za michuano hiyo zitakazofanyika Aprili mwaka huu nchini Shelisheli.
Mchezo huo utachezwa Mombasa nchini Kenya na mchezo wa marudiano utachezwa nchini kati ya Februari 20 na 22 mwaka huu
Akizungumza jijini, Kocha wa timu hiyo John Mwansasu, alisema maandalizi ya kwa ajili ya mchezo huo yanaendelea vema na wamecheza michezo miwili ya kirafiki na timu ya Zanzibar na kusema walipoteza mmoja na kushinda mmoja.
 “Maandalizi yanaendelea na kiwango cha wachezaji kinaimarika kila siku na nawaahidi watanzania kurudi na ushindi japo sikupata michezo ya kirafiki ya kimataifa lakini nina imani na timu yangu”, alisema Mwansasu.
Kocha John Mwansasu anasaidiwa na Ali Shariff 'Adolf' kutoka Zanzibar, na Meneja wa timu ni George Lucas na kikosi cha timu ya Taifa ya Tanzania ya mpira wa ufukweni (beach soccer) kinaundwa na wachezaji  15, saba toka Zanzibar na nane Tanzania bara
Iwapo timu ya Tanzania itasonga mbele, katika raundi ya pili itacheza na Misri ikianzia nyumbani kati ya Machi 13 na 15 mwaka huu.
Timu hiyo inayofanya mazoezi kwenye ufukwe wa Escape One inatarajiwa kuondoka nchini kesho Ijumaa.

Mama Muuza wa Shamsa bado kidogo tu

SHAMSA Ford, mmoja wa nyota wa filamu wa kike nchini, amewataka mashabiki wake wakae tayari kuipokea filamu yake mpya ya 'Mama Muuza' ambayo ipo hatua za mwisho ikirekebishwa kabla ya kuachiwa mtaani.
Akizungumza na MICHARAZO, Shamsa alisema filamu hiyo iliyotungwa na kutayarishwa na yeye mwenyewe ikiwa imewashirikisha wasanii kadhaa nyota akiwamo Haji Adam 'Baba Haji', itatoka Aprili.
"Nipo katika marekebisho ya mwishomwisho na nitaiachia 'Mama Muuza' miezi miwili ijayo kulingana na foleni iliyopo kwa wasambazaji," alisema.
Shamsa alisema kama ilivyokuwa kwa 'Chausiku' moja ya filamu iliyofanya vema kwa mwaka 2014, ndivyo 'Mama Muuza' itakavyokuwa kutokana na simulizi lake kubeba uhalisia wa maisha ya uswahili.
"Kama ilivyokuwa 2014 napenda mwaka 2015 uwe wenye raha na burudani kwa mashabiki wangu kupitia 'Mama Muuza'," alisema Shamsa.

Mengi kumtangaza Mshindi wa Wazo la Biashara 3N leo

http://blogs-images.forbes.com/mfonobongnsehe/files/2014/04/reginald-mengi.jpg
Mfanyabishara maarufu nchini Dk Reginald Mengi
 Na Rahma Junior
MSHINDI wa Januari 2015 wa Shindano la Wazo la Biashara 3N' anatarajiwa kutangazwa leo Alhamisi ya Februari 12 kuanzia saa tano asubuhi jijini Dar es salaam.
Kwa mujibu wa Dk. Reginald Mengi kupitia kurasa wake wa twitter, alitangazia umma kuwa Shindano hilo jipya lijulikanalo kwa kifupi -3N, ikiwa ni kifupisho cha ‘Nitabuni wazo la biashara, Nitatekeleza, na Nitafanikiwa’, ambapo mshindi wa kwanza wa mwezi Januari anatarajiwa kutangazwa siku hiyo ya alhamisi Februari 12.
Dk. Mengi aliweka ujumbe huo twittter : “Kutokana na sababu zisizozuilika mshindi wa Januari wa shindano la 3N atatangazwa Februari 12 saa 5 asubuhi. Samahani kwa usumbufu wowote”.
Kwa mujibu wa Dk. Mengi awali mshind I alitakiwa kutangazwa Jumatano ya leo ya Februari 11, kabla ya kusogeza mbele hiyo Februari 12.
Shindano hilo litakuwa linafanyika kila mwezi kwa muda wa miezi sita kuanzia Januari Mosi 2015, hadi Juni 30, 2015, na mshindi wa kila mwezi atajishindia ruzuku ya shilingi milioni 10 atakazozitumia kutekeleza kwa vitendo wazo lake la biashara.
Shindano hilo, linawashirikisha Watanzania pekee, litaendeshwa kwa njia ya mtandao wa kompyuta ambapo mshiriki atatuma wazo lake la biashara kwa anuani ya twita @regmengi Shindano la Wazo la Biashara. Katika mchujo wa kwanza jopo la wataalamu litateua mawazo 10 bora Zaidi na waliotoa mawazo hayo watafanyiwa usaili kwa njia ya simu ili jopo hilo lijiridhishe kama mawazo waliyoyotuma ni yao binafsi, na kama wamejipanga vizuri kutekeleza kibiashara.
Kutokana na mawazo hayo 10 teule, jopo litachagua wazo moja kuwa mshindi. Hii ni mara ya tatu kwa Dkt. Mengi kuendesha shindano kwa kutumia mtandao wa kompyuta wa twitter kwa kuamini kwake kuwa mitandao ya kijamii ina nguvu kubwa katika kuchochea ujasiriamali hasa kwa kizazi cha sasa.
Shindano la kwanza na la pili lililoendeshwa mwaka jana lilikusudiwa kushawishi mawazo ya kuondoa umaskini katika taifa lenye utajiri mkubwa, lakini watu wake wengi wakiwa bado wametopea katika lindi la umaskini.
Awali akizungumza katika uzinduzi wa shindano hilo, Dkt. Mengi alisema shindano hilo limelenga kuhimiza watu kuwa na upeo mkubwa wa kuona fursa za kibiashara na kuzitumia kujikwamua kiuchumi. Pia alisema shindano hilo ni mchango wake binafsi wa kuunga mkono jitihada za serikali na sekta binafsi za kuwakomboa wananchi kiuchumi kwa njia za ujasirimali, kwani amesema Sera zote mbili za kitaifa za Elimu ya juu na maendeleo ya viwanda vya kati na vidogo zina vipengele vya kuchochea na kuendeleza utamaduni wa ujasirimali wa mtu mmoja mmoja.
“Kwa muda mrefu nimekuwa nikishawishi uwepo wa moyo wa ujasirimali miongoni mwa wa Watanzania na hasa kwa vijana. Ni ndoto yangu kuona uchumi wetu unakua kwa kasi kiasi cha kuzalisha zaidi ya mamilionea 100 kila mwaka wanaoendesha biashara halali,” alisema.
Alisema kuwa na wazo sahihi la biashara, katika muda muafaka na eneo sahihi ni muhimu zaidi kuliko ruzuku ya fedha.
“Nataka vijana watambue kwamba wanaweza kuanza na kitu kidogo na kukua kufikia kampuni kubwa kabisa ya kimataifa unayoweza kufikiria,” alisema na kusisitiza kwamba anaamini siku moja mazingira ya ujasirimali nchini Tanzania yakuwa miongoni mwa mazingira bora kabisa barani Afrika.
Amesisitiza kuwa Shindano hilo liko wazi kwa watanzania wote na wanachotakiwa kufanya ni kuhakikisha wanapeleka wazo lao la biashara kwa Dk Mengi kupitia mtandao wa kompyuta wa twita, kwa kumtag Dk Mengi kwenye @regmengi.
Aidha amesema ni wale tu watakaomtag ndio watafikiriwa na jopo la wataalamu, na kusisitiza kuwa maamuzi ya jopo la Wataalamu yatakuwa ni ya mwisho.
Washindi wa kila mwezi wataarifiwa kwa kutumiwa ujumbe mfupi kwa kupitia akaunti zao za twita (DM) na kupewa ruzuku yao katika sherehe fupi itakayohudhuriwa na waandishi wa habari.

Wednesday, February 11, 2015

Azam yaifumua Mtibwa Sugar 5-2 warudi kileleni

KLABU ya Azam wamerejea kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara baada ya kuifumua bila huruma Mtibwa Sugar kwa mabao 5-2.
Azam ambao ni mabingwa watetezi wa ligi hiyo wealipata ushindi huo mnono na wa kwanza kushuhudiwa katika mechi za ligi msimu huu katika pambano pekee lililochezwa kwenye uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam.
Frank Domayo 'Chumvi' alifunga mabao mawili moja kila kipindi sawa na alivyofanya Kipre Tchetche na Didier Kavumbagu alifunga moja kuiangamiza Mtibwa ambao hicho ni kipigo chao cha pili mfululizo.
Mtibwa walioanza msimu huu kwa mkwara na kuongoza ligi hiyo kwa muda mrefu kabla ya kuporomoka mara baada ya kurejea kwenye michuano ya Kombe la Mapinduzi, ilifunikwa eneo la kiungo na Azam.
Vijana hao wa Mecky Mexime walipata mabao yao ya kufutia machozi kupitia kwa Juma Nampaka na Ame Ali ambayo hata hivyo hayakusaidia Wakata Miwa hao kufurukuta mbele ya mabingwa watetezi hao.
Kwa ushindi huo umeifanya Azam kurejea tena kileleni wakifungana pointi 25 sawa na Yanga, lakini tofauti na mabao ya kufunga na kufungwa yanawapa nafasi ya kukalia kiti cha uongozi.
Mtibwa wenyewe wameendelea kusalia katika nafasi ya sita wakiwa na pointi 18 sawa na ilizonazo timu za Kagera Sugar na Coastal Union.
Yanga na Azam zinazochuana kieleleni mwishoni mwa wiki zitakuwa kwenye majukumu ya kimataifa wakati Yanga itaikaribisha BDF XI ya Bostwana na wenzao Azam wataumana na El Merreikh wanaotarajiwa kutua nchini kesho tayari kwa pambano hilo litakalochezwa Jumapili.
Pambano la Yanga litacheza Jumamosi na viingilio vimeshjatangazwa kwa kiingilio cha chini kikiwa ni Sh 5000 tu.
Wakati lile la Yanga kiingilio cha chini kabisa ni Sh 2000 na vingine ni VIPB Sh 5000 na VIP A 10000 na tyiketi zitaanza kuuzwa Ijumaa.

Mourinho amchongea Van Persie kwa FA

MENEJA wa vinara wa Ligi Kuu ya England, klabu ya Chelsea, Jose Mourinho amekishambulia Chama cha Soka cha Uingereza(FA) kwa kuamua kutochukua hatua yeyote kwa mshambuliaji wa Manchester United, Robin Van Persie kwa tuhuma za kumtwanga kiwiko mchezaji wa upinzani.
Van Persie alionekana akimpiga kiwiko James Tomkins wakati wa mchezo ambao United ilitoa sare ya bao 1-1 dhidi ya West Ham United Jumapili iliyopita lakini mwamuzi Mark Clattenburg hakuona tukio hilo huku FA nao wakilifumbia macho.
Uamuzi huo unamfanya Mourinho kutowaelewa FA kwani anatarajiwa kumkosa nyota wake Diego Costa katika mchezo wa leo dhidi ya Everton baada ya mshambuliaji wa kimataifa wa Hispania kufungiwa mechi tatu kwa kukutwa na hatia ya kumkanyaga kwa makusudi Emre Can mwezi uliopita.
Akihojiwa Mourinho amesema watu haohao ambao wamemfungia mchezaji wake Costa ndio hao ambao hawataki kumfungia Van Persie kwa kosa lake alilofanya.
Mourinho aliendelea kudai kuwa anajua kama angekuwa mchezaji wake lazima angefungiwa kwani tukio kama hilo lilimtokea Ramires na alilimwa adhabu.

Sanchez, Ramsey wazua hofu Arsenal

http://www3.pictures.zimbio.com/gi/Aaron+Ramsey+Alexis+Sanchez+Leicester+City+N8Hb6G9P6Rgl.jpg
Ramsey, Sanchez



KOCHA wa Arsenal, Arsene Wenger amesema ana wasiwasi kuhusu hali za nyota wake Alex Sanchez na Aaron Ramsey baada ya kupata majeruhi katika mchezo Ligi Kuu walioshinda mabao 2-1 dhidi ya Leicester City.
Ramsey alitolewa nje ikiwa ni dakika tisa tu toka aingie akitokea benchi katika kipindi cha pili baada ya kupata majeruhi ya msuli wa paja, huku winga wa kimataifa wa Chile, Sanchez yeye alitolewa nje kufuatia kuchezewa faulo na Matthew Upson ambayo ilimfanya kushindwa kuendelea na mchezo huo uliochezwa Emirates.
Wenger amesema ana wasiwasi na nyota wake hao kwani hana uhakika watakaa nje ya uwanja kwa kipindi gani wakijiuguza. Mabao yaliyofungwa na Laurent Koscielny na Theo Walcott yalitosha kuwapa Arsenal ushindi huo muhimu baada ya kuchapwa na  Tottenham Hospur
Mabao yaliyofungwa na Laurent Koscielny na Theo Walcott yalitosha kuwapa Arsenal ushindi huo muhimu baada ya kuchapwa na mahasimu wao Tottenham Hotspurs mwishoni mwa wiki iliyopita.

Monday, February 9, 2015

HII NDIYO SHOW TIME YA H-BABA

http://www.bongo5.com/wp-content/uploads/2012/10/H-baba.jpg
H-Baba


IVORY COAST NDIYO VIDUME AFRIKA, YARUDI YA 1992

The Ivory Coast team and staff pose with their Africa Cup of Nations trophy having defeated Ghana 9-8 on penalties on Sunday night
Waflame wa soka Afrika, Ivory Coast
The Ivory Coast team celebrate landing the Africa Cup of Nations on penalties, their first AFCON title since 1992
Oyooooooooooooooooo!
Ivory Coast captain and Manchester star Yaya Toure is presented with the Africa Cup of Nations trophy on Sunday evening
Nahodha Yaya Toure akipokea Kombe toka kwa Rais  Nguema
HISTORIA imejirudia tena nchini Guinea ya Ikweta baada ya Ivory Coast kufanikiwa kutwaa ubingwa wa Fainali za Mataifa ya Afrika 2015  kwa kuichapa Ghana kwa mikwaju ya penati kama ilivyokuwa katika fainali za mwaka 1992.
Katika fainali za mwaka huo, Ghana maarufu kama Black Stars walikufa kwa mikwaju ya penati 11-10 na usiku wa kuamkia leo walikubali tena kipigo cha penati 9-8 kwa wapinzani wao na kuliacha taji likienda kwa Ivory Coast ikiwa ni mara ya pili kwao.
Timu hizo zililazimika kupigiana penati baada ya kumaliza dakika 120 bila ya kufungana na katika upigaji wa penati, Ivory Coast walianza vibaya kwa Wilfried Bony kukosa penati, lakini haikuweza kuwakatisha tamaa Tembo wa Afrika kumaliza udhia na ukame wa miaka zaidi ya 20 tangu wanyakue taji la kwanza 1992.
Ghana wanaweza kujilaumu kwa kushindwa kuibuka mabingwa kwa mara ya tano kutokana na kipindi cha pili cha dakika 90 kutawala sehemu kubwa ya pambano hilo lililosisimua kutokana na lilivyokuwa kali.
Katika hatua ya mikwaju ya penati Black Stars walianza kwa Mubarak kufunga kabla ya Bony kukosa, Jordan Ayew akapata penati ya pili ya Ghana na Tallo wa Ivory Coast naye akaikosa penati yake na kufanya matokeo kuwa 2-0.
Hata hivyo Acquah na Acheampong walikosa penati  zilizofuata za Ghana, wakati Aurierna Doumbia walifunga zao na matokeo kuwa 2-2.
Andre Ayew alifunga mkwaju wake na Yaya Toure akasawazisha, John Mensah akafunga na Solomon Kalou akasawazisha kabla ya Agyemang-Badu kufunga mkwaju wake na Koro Toure kusawalisha.
Afful aliifungia Ghana na Kanon kusawazisha zoezi likawa piga nikupige hadi katika penati ya tisa ambapo Ghana kupitia kipa wake Razak Brimah ilikosa na Ivory Coast kutumbukiza yao iliyowapa ubingwa wa pili katika historia za michuano hiyo kupitia kwa Boubacar Barry aliyegeuka kuwa shujaa kabla ya nahodha Yaya Toure kukabidhiwa taji na Rais wa Guinea ya Ikweta, Nguema kwenye uwanja wa Bata.

Irene Uwoya awataka mashabiki wake kupokea Kisoda

Na Rahma White
MUIGIZAJI nyota wa filamu nchini, Irene Uwoya 'Oprah' amewataka mashabiki wake kujiandaa kuipokea kazi yake mpya iitwayo 'Kisoda' akidai ni kazi kali kuliko hata filamu yake ya awali iitwayo 'Apple' aliyoitoa mwaka jana.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, Irene alisema 'Kisoda' ni moja ya kazi zitakazoleta mapinduzi makubwa katika fani ya uigizaji nchini kwa namna ilivyoandaliwa ikishirikisha wasanii wa ndani na nje ya nchi.
Irene alisema filamu hiyo iliyomtafuna fedha nyingi ipo katika hatua ya uhariri na itaachiwa wakati wowote zoezi hilo likikamilika akiwataka mashabiki wajiandae kuipokea kwa mikono miwili.
"Kama kuna waliodhani nilibahatisha kwenye 'Apple', wamekosea safari hii naja na 'Kisoda', moja kati ya filamu kali ambayo imewashirikisha wasanii wa Tanzania na Afrika Kusini, chini ya kampuni yangu ya Apple Entertainment," alisema Irene.
Msanii huyo alisema amekusudia ndani ya mwaka 2015 awape burudani ya kutosha mashabiki wake na kwa kuanza ameanza na Kisoda kabla ya kufuatiwa na mambo mengine makubwa zaidi.
Irene aliwataja baadhi ya wasanii walioshiriki filamu nchini wa hapa nchini ukiondoa yeye (Irene) ni Islam, Mariam Ismail na Msami.
Kimwana huyo aliyewahi kunyakua tuzo ya Muigizaji w Kike Chipukizi wa tuzo za Kinara kupitia filamu ya Diversion of LOve' kabla ya kuanza kuzalisha filamu zake na kuwahi  kuendesha kipindi cha kwenye runinga cha 'Paradise Show' ameshiriki filamu zaidi ya 30 zilizomjengea umaarufu mkubwa ndani na nje ya nchi.
Baadhi ya kazi hizo ni; 'Ngumi ya Maria', 'Nyati',  'Zawadi Yangu', 'Aliyemchokoza Kaja', 'Figo','Rosemary', 'Snitch', 'The Return of Omega', 'Money Talk', 'Omega Confusion', 'Question Mark', 'Safari', 'Innocent Case', 'Nyota Yangu', 'Last Card', 'Doa la Ndoa', 'Offside' na 'Oprah'.

Sunday, February 8, 2015

Manchester Utd chupuchupu kufa ugenini

Falcao akijaribu kufunga
Kouyate akishangilia bao lake
Pilikapilika uwanjani
KLABU ya Manchester United imeponea chupu chupu kufa ugenini baada ya kupata sare ya 1-1 mbele yua West Ham United.

Bao la kusawazisha lililofungwa dakika za lala salama na Daley Blind liliwaokoa Mashetani Wekundu kufa katika uwanja wa Boleyn Ground.
Blind alifunga bao hilo katika dakika mbili za nyongeza na kumnusuru kocha Luis Van Gaal kuumbuka kama alivyonusurika kocha wa Manchester City jana dhidi ya Hull City baada ya vijana wake kusawazisha bao dakika za jioni.
Wenyeji walitangulia kupata bao dakika ya 49 kupitia kwa Cheikhou Kouyaté na kulikuwa na kila dalili kwa Mashetani Wekundu kufa ugenini, lakini Blind kuchomoa na kuifanya Manchester United kufikisha pointi 44 na kukomalia nafasi ya nne nyuma ya Southampton waliorejea katika Tatu Bora.
Hata hivyo dakika mbili za nyongeza baada ya Man kupata bao ilijikuta ikimpoteza beki wake, Luke Shaw kwa kupewa kadi nyekundu ilifuatia kutokana na kadi ya pili ya njano kwa kumchezea vibaya Stewart Downing.
Vikosi vilikuwa hivi; 
West Ham: Adrian, Jenkinson, Song, Tomkins, Cresswell, Kouyate, Noble, Downing, Nolan, Valencia, Sakho.
Sub: Jarvis, O'Brien, Amalfitano, Jaaskelainen, Cole, Oxford, Lee
Manchester United: De Gea, Valencia, Jones, Rojo, Shaw, Blind, Rooney, Januzaj, Di Maria, van Persie, Falcao
Sub: Mata, Smalling, Ander Herrera, Fellaini, Valdes, McNair, Wilson

Kocha Redknapp kurejea soka kama mwanahisa

http://talksport.com/sites/default/files/tscouk_old_image/blog/Harry-Redknapp_21.jpg
Kocha Harry Redknapp
MENEJA wa zamani wa klabu ya QPR, Harry Redknapp amebainisha anaweza kurejea katika ulimwengu wa soka akiwa sehemu ya mwanahisa.
Redknapp mwenye umri wa miaka 67 ambaye alijiuzulu kuinoa QPR wiki iliyopita kutokana na matatizo ya mguu anahusishwa na kikundi kinachotaka kununua klabu karibu na nyumbani kwake katka Pwani ya Dorset.
Akihojiwa Redknapp amesema jambo hilo linamvutia hivyo anataka kujihusha nalo, kwani mchezo wa soka bado uko katika damu yake.
Redknapp ambaye amewahi kuipeleka Tottenham Hotspurs katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya na pia kuzinoa klabu za Portsmouth na West Ham United aliongeza kuwa wana matumaini ya kupata klabu ya kuinunua.

Jose Mourinho aanza mbwembwe zake England

http://static.guim.co.uk/sys-images/Observer/Columnist/Columnists/2013/6/7/1370621593808/jose-mourinho-010.jpg
Jose Mourinho
KOCHA wa vinara wa Ligi Kuu ya England Chelsea, Jose Mourinho amesema hadhani kama tofauti ya pointi saba walionayo kileleni mwa msimamo wa Ligi hiyo ni faida katika mbio zao za kugombea taji hilo. Chelsea imeitandika Aston Villa kwa mabao 2-1 jana, wakati Manchester City wanaowafuata katika nafasi ya pili wakipotoka sare na Hull City wanaokamata nafasi ya tatu toka mkiani.
Akihojiwa Kocha Mourinho, amesema ingekuwa nchi nyingine angeweza kuanza kushangilia katika kwa Uingereza tofauti ya alama saba sio chochote.
Mourinho aliendelea kudai kuwa bado kuna mechi 14 na alama 42 za kupigania hivyo kila mchezo unakuwa mgumu na chochote kinaweza kutokea.
Kocha huyo pia alisisitiza hakushtushwa kuona City wakitoa sare nyumbani na Hull ambao wako mstari wa kushuka daraja lakini amefurahi kuona matumaini ya kunyakuwa taji yakiwa mikononi mwao.
Ligi hiyo iliendelea tena jioni ya leo kwa timu za Newcastle United wakipata sare ya 1-1 na timu ya Stoke City wakati West Bromwich Albion wakiwa ugenini walipata sare ya 2-2 dhidi ya timu ya Burnley.

Sepp Blatter aponda vyombo vya habari vurugu AFCON

http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/4/44/Sepp_Blatter_at_signing_of_agreement_creating_FIFA_Ballon_d%E2%80%99Or_in_Johannesburg_2010-07-05_1.jpg
Rais wa FIFA, Sepp Blatter
RAIS wa Shirikisho la Soka la Dunia (FIFA) Sepp Blatter, ameponda vyombo vya habari kuonyesha vurugu zilizozuka katika mchezo wa nusu fainali ya michuano ya Mataifa ya Afrika kati ya wenyeji Guinea ya Ikweta na Ghana.
Mchezo huo uliochezwa Malabo ulisimamishwa kwa dakika 30 baada ya mashabiki kurusha vitu kwa wachezaji na mashabiki wa timu pinzani hali iliyosababisha polisi kutumia helikopta na mabomu ya machozi kuwatawanya mashabiki hao.
Vurugu hizo zilikuwa zikirushwa moja kwa moja duniani kote, lakini Blatter anadhani pamoja na vurugu hizo lakini kuna mazuri mengi ya kusifiwa katika michuano hiyo inayotarajiwa kumalizika leo.
Blatter amesema siku zote habari nzuri huwa sio habari ila habari mbaya ndio habari akimaanisha kuwa siku zote watu wamekuwa wakizungumzia mabaya.
Rais huyo amesema dosari ndogo kama iliyotokea katika mchezo wa nusu fainali haipaswi kupewa nafasi ya kusahau mafanikio yaliyopata katika michuano hiyo ambayo imendaliwa kwa kipindi kifupi kuliko ilivyopangwa.

Asamoah Gyan bado alia na Yattara

http://img.modernghana.com/images/content/bgwi04lyx6_asamoahgyan580.jpg
Asamoah Gyan
NAHODHA wa kikosi cha timu ya taifa ya Ghana, Asamoah Gyan ambay anajiandaa kushuka dimbani kuiongoza timu yake katika mechi ya Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika dhidi ya Ivory Coast, amedai hatomsamehe golikipa wa Guinea Naby Yattara kutokana na faulo aliyomchezea timu zao zilipokutana.
Golikipa huyo alimkanyaga Gyan kwa teke la tumboni katika dakika za mwisho za mchezo wa robo fainali uliokutanisha timu hizo.
Yattara alilimwa kadi nyekundu lakini hajapewa adhabu yeyote nyingine mpaka sasa kiasi cha Gyan katika mahojiano yake alisema bado analitaka Shirikisho la Soka la Afrika(CAF) kumtwanga adhabu Yattara kwa sababu anadhani alidhamiria kufanya tukio lile.
Gyan aliendelea kudai kuwa ilikuwa ni faulo mbaya ambayo ingeweza kumsababisha asicheze tena soka ndio maana hataki kumsamehe kwa hilo.
Hata hivyo kipa huyo alinukuliwa juzi akisema kuwa hawezi kumuomba radhi Gyan kwa sababu hakukusudia kumuumiza na kusisitiza kuwa hilo ni tukio la bahati mbaya katika harakati za mchezo.

YANGA YALIPA KISASI, NGASSA AKIONDOA 'GUNDU'

http://shaffihdauda.co.tz/wp-content/uploads/2015/02/NGASSA-MRISHO.jpg
Mrisho Ngassa aliyefunga mabao yote mawili Yanga ikiizamisha Mtibwa uwanja wa Taifa
MABAO mawili ya winga machachari Mrisho Ngassa aliyetokea benchi yameiwezesha Yanga kulipa kisasi kwa Mtibwa Sugar na kurejea kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.
Yanga ambayo awali ilionekana kuugaya mchezo huo uliochezwa kwenye uwanja wa Taifa, ulishuhudiwa dakika 45 za kwanza mambo yakiwa magumu kwa klabu zote baada ya kutofungana bao lolote.
Hata hivyo mabadiliko yaliyofanywa na kocha Hans van der Pluijm ya kumtoa Kpah Sherman na kumuingiza Mrisho Ngassa yalizaa matunda baada ya mkali huyo kufunga mabao hayo muda mchache tangu awepo uwanjani na kuifanya Yanga kurudi katika nafasi ya kwanza.
Yanga imefanikiwa kufikisha pointyi 25 baada ya mechi 13 na kuiengua Azam ambao jana walilazimishwa sare ya 2-2 na Polisi Morogoro ikiwa na pointi 22 baada ya kucheza mechi 12.
Azam inatarajiwa kushuka dimbani siku ya Jumatano kwa ajili ya kucheza na Mtibwa Sugar katika mechi ya kiporo itakayochezwa uwanja wa Chamazi.
Magoli hayo mawili yamemwezesha Ngassa kuondoa 'gundu' baada ya kutoweza kufunga bao lolote msimu huu, kitu ambacho hakikuwa cha kawaida kwa mchezaji huypo aliyewahi kuwa Mfungaji Bora.
Wakati Azam wakiingia kambini kujiandaa na pambano lao na Mtibwa, Yanga wanatarajiwa kuelekea visiwani Zanzibar ili kuweka kambi kusubiri  mchezo wao wa Kombe la Shirikisho utajkaocheza Jumamosi.
Yanga itashuka dimbani Jumamosi kuumana na BDF XI ya Botswana katika mechi ya mkondo wa kwanza wa raundi ya kwanza ya michuano hiyo kabla ya kurudiana nao wiki mbil baadaye.
MSIMAMO LIGI KUU TANZANIA BARA 2014-2015
                              P   W   D    L    F    A   GD   Pts
01.  Yanga              13  07  04  02  15   07  08  25
02.  Azam               12  06  04  02  17   10  07   22
03. Polisi Moro         14  04  07  03  12   11  01  19
04. JKT Ruvu           14  05  04  05  14   14  00  19
05. Ruvu Shooting   14  05  04  05   10  11   -1  19
06. Mtibwa Sugar     12  04  06  02   13  09  04  18
07. Coastal Union     14  04  06  04  11   10  01  18
08. Kagera Sugar      14 04  06  04   11   11  00  18
09. Simba                 13  03  08  02  13   11  02  17
10. Mbeya City          13   04  04  05  09  11   -2  16
11. Ndanda Fc           14  04  03   07  13  18   -5  15
12. Mgambo JKT        12  04  02  06   06  11   -5  14
13. Stand Utd            14  02  06   06   09  17   -8  12
14. Prisons                13  01  08   04   10   12   -2  11
 

Wafungaji:
7-
Didier Kavumbagu(Azam)
6- Samuel Kamuntu (JKT Ruvu), Rashida Mandawa (Kagera Sugar)
5-
Ame Ali (Mtibwa), Danny Mrwanda (Yanga)
4-
Rama Salim (Coastal),  Simon Msuva (Yanga),  Emmanuel Okwi (Simba), Nassor Kapama (Ndanda)
3- Ally Shomari (Mtibwa),  Jacob Massawe (Ndanda), Kipre tchetche (Azam)
2-
Shaaban Kisiga, Dan Sserunkuma(Simba),  Salum Kanoni, Atupele Green (Kagera Sugar) Aggrey Morris (Azam),  Najim Magulu, Jabir Aziz (JKT Ruvu), Amissi Tambwe, Jerry Tegete, Mrisho Ngassa (Yanga), Ibrahim Kihaka (Prisons), Mussa Mgosi (Mtibwa), Heri Mohammed, Mussa Said (Stand Utd), Ally Nassor,  Malimi Busungu (Mgambo), Nicolaus Kabipe (Polisi),Yahya Tumbo (Ruvu Shooting)

Yanga kulipa kisasi kwa Mtibwa leo Taifa?!

Wakata Miwa wa Manungu, Mtibwa Sugar
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjD1DkH-KANYfSP-lMJIrFLhkzjqB0KhC2HRInBtLOg-GaupvdQqEA5_bgI-mH-UIyzUAItfzKFQQrOWcqfRRa8UBWoaXdQk1K7ESNnytqX3XOT2wNo7RpSWAvXOYRRhw10rgajuMQIjnnn/s1600/IMG_6036.JPG
Kikosi cha Yanga kitatoka vipi leo Taifa?
BAADA ya ombi lao la kutaka mechi yao dhidi ya Mtibwa Sugar kuahirishwa kugonga mwamba kwa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Yanga leo watashuka dimba la Taifa kwa nia ya kulipa kisasi cha mabao 2-0 walichopewa na wapinzani wao kwenye mechi ya mkondo wa kwanza.
Yanga ilikumbana na kipigo hicho katika mechi ya ufunguzi wa ligi hiyo kwenye uwanja wa Jamhuri Morogoro na iliiomba TFF iwaahirishie mechi yao ili kutoa nafasi ya kujiandaa vizuri kwa mchezo wao wa Kombe la Shirikisho dhidi ya BDF XI ya Botswana siku ya Jumamosi ijayo.
TFF imewachomolea na kuwataka washuke dimbani leo na kuwa na muda wa wiki moja ya kuvaana na wageni wao watakaowafuata Alhamisi wiki hii kwa ajili ya mchezo huo wa Jumamosi.
Ikiwa imetoka kupata ushindi mwembamba wa bao 1-0 uliovunja mwiko wa kushindwa kushinda katika uwanja wa Mkwakwani kwa karibu misimu miwili sasa, Yanga itawashukia Mtibwa Sugar kama mwewe kutokana na hasira za 'kubaniwa' na TFF.
Hata hivyo Yanga isitarajie mteremko kwani wapinzani wao, kwani msimu huu timu hiyo imeonekana kuimarika zaidi kuliko misimu miwili iliyopita na isingependa kulala tena jijini Dar kama ilivyokuwa katika msimu uliopita walipochapwa mabao 2-0.
Ikiwa chini ya nahodha wa zamani wa Taifa Stars, Mecky Mexime, Mtibwa ilikaa muda mrefu kileleni kabla ya kuteleza baada ya kuruhusu kipigo chake cha kwanza toka kwa maafande wa Ruvu  Shooting na leo ingependa kupata ushindi ili kujirejesha nafasi za juu.
Mtibwa Sugar imeporomoka toka nafasi ya tatu hadi ya sita ikiwa na pointi 18 wakati watani zao wapo nafasi ya pili baada ya Azam kuwaporomosha kufuatia sare ya mabao 2-2 iliyoapa mjini Morogoro dhidi ya Polisi Moro.
Kocha Mexime waliolazimishwa suluhu ya 0-0 na Coastal Union katika mechi yao ya mwisho, alisisitiza kuwa lengo lao ni kuona wanamaliza katika nafasi mbili za juu na hivyo wamerekebisha makosa yaliyowafanya washindwe kupata ushindi katika mechi  nne zilizopita za ligi hiyo.
Timu hiyo katika mechi hizo iliambulia sare tatu na kipigo kimoja na kuwwafanya waporomoke kileleni waliokoongoza kwa muda mrefu tangu kuanza kwa msimu huu.
Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano wa Yanga, Jerry Muro alisema kikosi chao kipo tayari kwa vita ya leo ili kuweza kuendeleza ubabe wao na kujiweka katika mazingira mazuri ya kuchukua ubingwa baada ya kurejea kileleni.
Muro alisema Yanga itawakosa baadhi ya nyota wake ambao ni majeruhi, lakini bado wachezaji waliosalia wataiongoza timu hiyo kulipa kisasi cha mabao 2-0 ilichopewa mjini Morogoro katika mechi ya mkodno wa kwanza kabla ya kuingia kambini kuwasubiri BDF XI ya Botswana kwenye mchezo wa kimataifa.

Man Utd, West Ham vita kali England

http://www.whufc.com/javaImages/86/a4/0,,~11445382,00.jpg

KLABU ya Manchester United ikiwa na furaha ya kufuzu Raundi ya Tano ya Kombe la FA, leo watakuwa dimba la ugenini kupepeta na West Ham Utd katika moja ya michezo minne ya Ligi Kuu ya England.
Vijana wa Luis Van Gaal, wanaifuata Wagonga Nyundo wa London wakitoka kuitoa nishai Cambridge United walionekana kutaka kuwatoa nishai kama vigogo vingine vilivyofanyiwa kwenye michuano hiyo ya FA.
Mashetani Wekundu waliichapa timu hiyo ya Daraja la Pili mabao 3-0 baada ya mechi ya kwanza wiki iliyopita kuisha kwa suluhu ya 0-0, hivyo watatua uwanja wa Boleyn Ground kwa nia ya kuendeleza furaha yao.
Wakiwa na kumbukumbu ya kushinda katika mechi ya kwanza msimu huu dhidi ya wapinzani wao ambao kwa misimu mitatu sasa hajaonja ushindi mbele ya Mashetani Wekundu, Manchester isitarajie mteremko.
West Ham wamekuwa na msimu mzuri safari hii wakishinda mechi 10 kati ya 23 walizocheza wakikamata nafasi ya nane na pointi zao 36,  saba pungufu na ilizonazo Man Utd waliopo nafasi ya tatu katika msimamo.
Mbali na mechi hiyo pia katika ligi hiyo leo kutakuwa na michezo mingine miwili wa mapoema ukizikutanisha timu za Burnley dhidi ya West Bromwich kabla ya Newcastle United kukikaribisha Stoke City.

NI GHANA AU IVORY COAST LEO

* Zinakutana katika fainali ya kisasi

http://www.ghanatoghana.com/wp-content/uploads/2015/01/Ghana-black-stars-players-group-picture.jpg
Ghana Black Stars
https://nbcprosoccertalk.files.wordpress.com/2013/11/ivory-coast-oct.jpg
Kikosi cha Ivory Coast
MALABO, Guinea ya Ikweta
AFRIKA inatarajiwa kufahamu Bingwa Mpya wa soka wakati Ivory Coast na Ghana zitakapoumana kwenye mchezo wa fainali za michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika 2015.
Pambano hilo litakalopigwa kwenye uwanja wa Estadio de Bata, linakumbushia fainali za mwaka 1992 wakati Tembo wa Afrika, Ivory Coast na Black Stars ya Ghana zilipokutana nchini Senegal.
Katika fainali hiyo ya aina yake, Ivory Coast waliwazidi kete wapinzani wao hao na kutwaa taji hilo kwa mikwaju ya penati 11-10 baada ya kumaliza dakika 120 milango ya timu zote ikiwa migumu.
Ivory Coast wamefuzu hatua hiyo baada ya kuing'oa timu ya DR Congo kwa kuwachapa mabao 3-1 katika mechi ya nusu fainali iliyochezwa Jumatano, huku kocha wake Herve Renald 'akizuga; kuwa walipenya kibahati kutokana na timu yake kucheza ovyo.
Wenyewe Ghana walifanikiwa kuwatoa wenyeji Guinea ya Ikweta kwa kuwabangua mabao 3-0 katika mechi iliyojaa vurugu za mashabiki waliokuwa wakishinikiza mwamuzi 'kuwabeba' tena kama ilivyokuwa katika mechi ya robo fainali dhidi ya Tunisia iliyomponza refa wa Mauritius kufungiwa.
Wenyeji hao walitarajiwa jana kuvaana na DR Congo kwa ajili ya kuwania nafasi ya mshindi wa tatu na nne wa fainali hizo za 30 ambazo zilianza kutimua vumbi lake tangu Januari 17.
Mchezo huo wa fainali unasubiriwa kwa hamu kutokana na umahiri wa vikosi vya timu hizo za Afrika Magharibi na washiriki wa Fainali zilizopita za Kombe la Dunia zilizofanyika nchini Brazili.
Tembo wa Afrika wanajivunia kikosi kinachoundwa na nahodha wake Yaya Toure ambaye ndiye Mchezaji Bora wa Afrika, sambamba na mwanasoka ghali wa Afrika, Wilfried Bony na wakali wengine.
Wakati wapinzani wao wanatambia nahodha wake, Asamoah Gyan,  Andre Ayew na nduguye Jordan Ayew, Kwame Appiah na wengine wanaochezaji soka la kulipwa katika klabu mbalimbali za Ulaya.
Kikosi cha Ghana kinachonolewa na kocha wa zamani wa Chelsea,  Avram Grant ambaye atakuwa akitaka kuwapa waajiri wake taji la tano  baada ya kulikosa kwa muda mrefu tangu walipotwaa mara ya mwisho mwaka 1982 na kulikosa kwenye fainali za mwaka 2010 mbele ya Misri.
Ivory Coast wenyewe watakuwa wakisaka taji la pili la michuano hiyo baada ya fainali za mwaka 2012 zilizofanyika nchini Guinea ya Ikweta ikishirikiana na Gabon kulikosa kwa kufungwa na Zambia.
Cha kuvutia ni kwamba kocha aliyewapa taji Zambia mwaka huo, Herve Renald ndiye anayeinoa timu hiyo kwa sasa na kama timu yake itashinda leo ataweka rekodi ya aina yake Afrika ya kuw kocha wa kwanza kuchukua taji hilo akiwa na nchi mbili tofauti.
Je ni Tembo wa Afrika au Nyota Weusi watakaoibuka na ushindi katika mchezo huo wa leo? Tusubiri tuone baada ya kumalizika wa fainali hizo zilizohamishiwa Guinea ya Ikweta baada ya waliokuwa wenyeji wa awali Morocco kuchomoa kwa kisingizio cha hofu ya ugonjwa wa Ebola.
Kitendo hicho kimesababisha nchi hiyo ya Morocco kuadhibiwa kwa kufungiwa fainali mbili za Afrika za 2017 na 2019.

Mchujo wa mabondia wa All African Games kuanza kesho

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgKf3j_9lbtaLQyaz_zQF0flGoPDNwRHy3gQ4ONfElr_vig3q8o4Qz8FPYmcPqZ0gMZDYrQgTaoGCdBXuRzDb3SOhXV60xTZTtAozbghUpubPSY0R6H4oYZPX0-B6AMkqUQhs2jWXY7oUw/s1600/antony.JPG
Mchujo kama huu unatarajiwa kuanza kesho Uwanja wa Ndani wa Taifa
http://www.thisday.co.tz/media/picture/large/BFTsecretary%20genera%20Makore%20Mashaga1.jpg
Katibu Mkuu wa BFT, Makore Mashaga
MCHUJO wa kusaka mabondia wa kuingia kambini kwa ajili ya ushiriki wa michuano ya Michezo ya Afrika (All African Games) unatarajiwa kuanza kesho jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa BFT, Makore Mashaga alisema mashindano ya mchujo huo utafanyika kwenye Uwanja wa Ndani ya Taifa na utamalizika Siku ya Wapendanao Februari 14.
Mashaga alisema mashindano hayo maalum yatashirikisha walifanya vizuri katika mashindano ya wazi ya taifa yaliyofanyika hivi karibuni katika Uwanja wa Taifa.
"Mashindano maalum kwa ajili ya kusaka mabondia watakaotuwakilisha kwenye michezo ya Afrika yataanza Februari 9-14 Uwanja wa Ndani wa Taifa na utashirikisha waliofanye vema kwenye michuano ya wazi," alisema.
Kwa mujibu wa Mashanga mabondia 39 watachujana ili kupatikana 15 ili kuunda timu ya taifa ya mchezo huo wa ngumi.
Mashindano hao ya Mataifa ya Afrika yanatarajiwa kutimua vumbi lake kati ya Septemba 4-19 mjini Brazzaville, Congo na Tanzania ni miongoni mwa nchi shiriki.

Saturday, February 7, 2015

Ngoma mpya ya AT-Sijazoea isikilize

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjehOkmJRxMxdVCIy6FjKjZXft65LgwAa2VvK1EW5G5Zc-IjB4jnAEfzogfhC9Xqw9qsHU2nWAxMY-6ZNbQDHCsjDQT_Nsbs4h2IPKNHVXD0GEbFUvQR-3UTk9POsZ2tAUGhNEsQrTYkqTr/s1600/DSC_1141.JPG
Msanii AT akiwa jukwaani
 

Everton, Liverpool hakuna mbabe, zashindwa kutambiana

Utemi na kutunishiana kifua ulikuwapo katika pambano hilo
Raheem Sterling akichuana na Aaron Lennon
Nahodha Steven Gerrard akijaribu kufunga mbele ya lango la Everton bila mafanikio
WAPINZANI wa jadi wa Merseyside, Everton na Liverpool zimeshindwa kutambiana baada ya kutoka suluhu katika pambano kali lililomalizika hivi punde.
Licha ya kushambuliana kwa zamu na kuwepo kwa kosa kosa za hapa na pale katika pambano hilo lililochezwa kwenye uwanja wa nyumbani wa Everton wa Goodison timu hizo zilimaliza dakika 90 zikiwa 0-0 na kugawana pointi moja moja.
Katika pambano hilo Liverpool ilipata pigo mapema baada ya kiungo wak Lucas Leiva kuumia katika dakika ya 15 na nafasi yake kuchukuliwa na Joe Allen, huku Aaron Lennon akishuhudiwa akishuka dimbani kwa mara ya kwanza akiwa na jezi za Everton akitokea Spurs.