STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, February 13, 2015

VALENTINE DAY NI KITU GANI, JE UISHEREHEKEE?

KESHO baadhi ya watanzania wataingia kwenye mkumbo wa kusherehekea siku iliyobatizwa jina la 'Valentine Day' wakiitaja kama Siku ya Wapendanao.
Kwa hakika kwa Mcha Mungu ni haramu kwake kuiadhimisha sherehe hiyo kutokana na ukweli ni siku ya KIPAGANI na inayokinzana na MAFUNDISHO YA MUNGU MWENYEEZI iwe kwa Ukristo ama kwa Uislam.
Hata hivyo ni vema tuongelee kidogo nini maana ya Valentine kwa asili yake kisha kila mtu kwa IMANI  yake na mapana yake akatambua na kujiamulia kwa nafsi yake ama kukufuru au kumshukuru aliyemuumba.


Maneno hayo aliyoyasema Mtume Muhammad (SAW) hakika yamethibiti kwa sababu imedhihirika Waislamu kuigizia mila, desturi na tabia za makafiri na kuzisherehekea kama mfano siku hii inayoitwa 'Valentine day' (Siku ya Wapendanao).
Na baya zaidi na la kusikitisha sana ni kwamba sherehe hizi zinaenezwa katika njia mbali mbali za mawasiliano kama kutumiana kadi, barua pepe (e-mail), salamu katika simu za mkono. 
Hakika fitna hii humfanya Muislamu aharibu 'Aqiydah (Iymaan) yake kwa kudhani kuwa anafanya jambo la kawaida na hali ni jambo lisilo katika sheria ya dini yetu bali ni shirki kubwa na upotofu wa kufuata wanayoamini makafiri.
Na Mwenyezi Mungu anasema kuwa "Hawatakuwa Radhi Mayahudi na Manaswara kuwaona mpaka mfuate mila zao"
Baadhi ya Waislam na wasio waislam wapo kwenye harakati za kujiandaa na siku hiyo wajifuata mkumbo bila kujua kile wanachokisherehekea ebu tujifunze;
Historia Ya Sherehe Ya Siku Ya ValentineSherehe hii ya wapendanao ni sherehe ya wapagani  wa Kirumi wakati dini yao ya upagani ilikuwa ni dini iliyotapakaa kwa Warumi karne zaidi ya kumi na saba zilizopita.  
Na fikra zao ilikuwa ni kuelezea hisia ya 'mapenzi ya kiroho'
Kulikuwa na visasili (uongo) zilizohusishwa na sherehe hii ya upagani ya Warumi ambao umeendelea kutoka warithi wa Kikiristo. 

Miongoni mwa uongo huo ni kuamini kwao Warumi kuwa Romulus, aliyevumbua Rome, alinyonyeshwa siku moja na mbwa mwitu mwanamke, hivyo akampa nguvu na hikma.
Warumi walikuwa wakisherehekea tukio hili katikati ya Februari kila mwaka kwa kufanya sherehe kubwa. 

Na mojawapo ya tambiko katika sherehe hii ni kuchinja mbwa au mbuzi. 
Vijana wawili wenye nguvu hujipaka damu ya mbwa au ya mbuzi katika miili yao, kisha huiosha damu hiyo kwa maziwa. 
Baada ya hapo, watu hufanya gwaride wakiwa vijana hawa wawili wako mbele wakiongoza gwaride iliyokuwa ikitembea barabarani. 
Vijana hao wawili walikuwa wakichukua vipande vya ngozi ambavyo waliwapigia watu wanaowavuka. Wanawake wa kirumi walikuwa wakipokea mapigo hayo wakiamini kuwa yatawahifadhi na kutibu utasa.
 

Kufungamana kwa Mt. Valentine na Sherehe Hii

Mtakatifu Valentine (Saint Valentine) ni jina waliopewa mashujaa wawili wakongwe waliokufa ambao ni wana wa kanisa la kikiristo. 

Inasemekena kwamba walikuwa ni wawili au mmoja tu. 
Huyo mmoja alikufa Rome kutokana na mateso ya kiongozi wa Kigothi aliyeitwa Claudius. 
Kanisa la Saint Valentine lilijengwa kwa ajili ya kudumisha kumbukumbu yake.
Warumi walipoingia ukristo, wakaendelea kusherehekea sikukuu ya wapendanao (valentine day) lakini wakabadilisha kutoka fikra ya upagani ya 'mapenzi ya kiroho' (spiritual love) na kuleta fikra nyingine iliyojulikana kama ni 'mapenzi ya mashujaa' yaliyowakilishwa na Saint Valentine ambaye aliuliwa kwa ajili ya kutetea mapenzi na amani. 

Vile vile ikajulikana ni sikukuu ya wapenzi, na Saint Valentine alifanywa kuwa ni mlezi wa mapenzi ya mtakatifu.
Miongoni mwa imani yao inayoambatana na sherehe hii ni kwamba majina ya wasichana waliofika umri wa kuolewa yaliandikwa katika vikaratasi vidogo vilivyokunjwa mviringo kisha vikawekwa katika chombo juu ya meza. 

Kisha wavulana waliotaka kuoa waliitwa na kila mmoja huchagua karatasi moja ikiwa na jina la msichana. Kisha hujiambatanisha naye huyo msichana aliyempata kutokana na kura hiyo aliyochagua kwa muda wa mwaka ili wajuane vizuri kisha tena hufunga ndoa, au kama hawakuelewana hurudia tena kufanya kura inapofika siku hiyo mwaka unaofatia.  
Vile vile imesemekana kwamba chanzo cha sikukuu hii, ni kwamba warumi walipokuwa wakristo baada ya ukristo kutapakaa, Mfalme wa Kirumi Claudius II alitoa hukumu katika karne ya tatu kwamba askari wasioe kwa sababu kuoa kwao kutawashughulisha na vita walivyokuwa wakipigana. 

Hukumu hiyo ilipingwa na Saint Valentine ambaye alianzisha kuozesha maaskari kwa siri. 
Alipokuja kujua mfalme, alimfunga jela na akamhukumu kuuliwa. 
Huko jela akapendana na mtoto wa mkuu wa jela, lakini ikawa ni siri kwani kutokana na sheria ya ukristo, mapadri na makasisi wameharamishwa kuoa au kupenda.
Hata hivyo alipewa heshima yake na wakristo kwa sababu ya kushikilia na kujikita imara katika ukristo wakati mfalme alipotaka kumsamehe kwa sharti aache ukristo na kuabudu miungu ya Kirumi ili awe msiri wake na awe mkwe wake. 

Lakini Saint Valentine alikataa ahadi hiyo na akapendelea ukristo, kwa hiyo akauliwa siku ya tarehe 14 Februari 270 CE. 
Ndio ikaitwa siku hii kwa jina la huyo mtakatifu (Valentine).

Papa (Pope) naye akaifanya siku hiyo ya kufa Saint Valentine tarehe 14 Februari 270 CE kuwa ni sikukuu ya mapenzi. 

Na ni nani alikuwa Papa huyo? Ni Askofu mkuu wa kanisa la 'universal church', ambaye ni mrithi wa mtakatifu Peter.
Ndugu Waislamu tazameni vipi huyo askofu anavyohusika katika kuadhimisha sikukuu hii ambayo ni uzushi katika dini yao ya Kikiristo. 


Hii itukumbushe kauli ya Allaah
"Wamewafanya makuhani wao na wamonaki wao kuwa ni marabi badala ya Mwenyezi Mungu"At-Tawbah: 31

Matendo Yanayotakiwa Kujiepusha Katika Sikukuu Hii  
1- Kuonyeshana bashasha na furaha kama ilivyo katika sikukuu zao nyingine.
2-Kupeana mawaridi mekundu (Red Roses) ambayo ni alama ya kuelezea mapenzi, 'mapenzi ya kiroho' ya wapagani au 'mapenzi' ya Wakristo. Hivyo inajulikana kuwa ni 'Sikukuu Ya Wapendanao'.
3-Kupelekeana kadi. Na kadi nyingine zina picha za 'mungu wa mapenzi wa kirumi' ambaye ana mbawa mbili, akiwa amekamata upinde na mshale. Huyu ndio mungu wa mapenzi wa wapagani warumi. Shirk iliyoje hii ndugu Waislamu?
4-Kubadilishana maneno ya mapenzi na matamanio katika kadi wanazopelekeana, yakiwa katika mfumo wa kimashairi, tenzi na sentensi fupi fupi. 

Kadi nyingine zina picha za kimzaha na maneno ya kuchekesha, na mara nyingi zina maneno ya kusema 'Kuwa Valentine wangu'. 

Hii inaashiria maana ya kikiristo ya sikukuu hii baada ya kuwa asili yake ni kutokana na fikra za upagani.
5-Katika nchi nyingi za kimagharibi, hufanyika sherehe siku hiyo ambayo kunakuweko kuchanganyika wanaume na wanawake, kuimba, na kucheza dansi. Na wengi wanapelekeana zawadi kama mawaridi, maboksi ya chokoleti kwa wake zao, marafiki na wanaowapenda.
Kutokana na maelezo yote hayo ya chanzo cha sikukuu hii, tunaona kwamba siku hiyo haina uhusiano wowote katika Uislamu, bali yana uhusiano na washirikina mapagani, hata wakristo katika dini yao nao pia ni uzushi, sasa itakuwaje sisi Waislamu tuwaigize kusherehekea?
Basi ndugu Waislamu tutambue kuwa jambo hili ni ovu mno, haimpasi Muislamu kuharibu 'Aqiydah (iymaan) yake kwani kuna hatari kubwa kushiriki katika sherehe hii nayo ni kuingia katika kumshirikisha Allaah na kama tunavyojua kuwa Allaah Hamsamehe mtu anayefanya shirki pindi akifariki bila ya kutubu kama ilivyo katika aya ifuatayo:
"Hakika Mwenyezi Mungu Hasamehe kushirikishwa, na Husamehe yaliyo duni ya hilo kwa Amtakaye. Na anayemshirikisha Mwenyezi Mungu basi hakika amezua dhambi kubwa" (An-Nisaa: 48).
Hivyo ni kuharamishwa na Pepo na kupata makazi ya moto, tunajikinga na Allaah kwa hayo.
"Kwani anayemshirikisha Mwenyezi Mungu, hakika Mwenyezi Mungu Atamharimishia Pepo, na mahala pake ni Motoni. Na waliodhulumu hawatakuwa na wa kuwanusuru"-Al-Maaidah: 72.
Tunamuomba Allaah  Atuepushe na kila aina ya shirk na Atuonyeshe yaliyo ya haki tuyafuate, na yaliyo ya batili tujiepushe nayo na Atuajaalie ni miongoni mwa wale wanaosikiliza kauli (nyingi) wakafuata zile zilizo njema.  Aamiyn

Special Al Hidaya

Copy and WIN : http://bit.ly/copynwin
Friday, 13 February 2015 VALENTINE NI NINI? Leo nimeona niongelee kidogo nini maana ya Valentine kwa asili yake kisha kila mtu kwa Imani yake na mapana yake akatambua kuwa anapokuwa sehemu ya Valentine Day anakuwa ana adhimisha nini na kwa sababu gani wengi tunasheherekea kama sio kuadhimisha Valetine Pasipo kujua asili yake. Valentine’s Day kama Sikukuu Ya Kipagani: Valentine’s Day si siku ya Sikuu ya Kikristo, hata kama jina lake asili yake inatokana na Ukristo haiwezi kuhalalisha sasa Valentine kuwa Siku Ya Kikristo. Tukiangalia suala sikukuu hii kwa jicho la tatu, hatuoni uhusiano mkubwa kati ya watu wa Mungu na Malove dove yaani mapenzi. Kuna mambo mengi yanaweza ibua mjadala na kutokuelewana miongoni mwa jamii ya wakristo na wasomi juu ya chimbuko ya Siku ya wapendanao al maarufu Valentine’s Day. Hatutaweza kamwe kuwa na uwezo wa kuwa na jibu muafaka kuhusu uhalali wa kusheherekea valentine kwa namna moja ama nyingine kutokana na tofauti za kitamaduni na kidini ili mwisho wa siku tujenga upya hadithi kamili na madhubuti, lakini uhusiano kipagani hadi sasa na nguvu zaidi kuliko wale wa Kikristo kwa namna yoyote ile. Februari 14 & Juno Fructifier au Juno Februata (February 14th & Juno Fructifier or Juno Februata) Enzi hizo Warumi walikuwa wakisheherekea kwa kupumzika kabisa kama sikukuu ya muungano ama sikukuu zozote za hapa bongo kila Februari 14 kama siku ya kutoa heshima kwa Juno Fructifier. Huyu Juno Fructifier alikuwa nani?huyu alikuwa Malkia wa miungu ya Kirumi ambaye alikuwa Mungu mke kama mmoja wapo wa miungu ya ndoa kama ndo zilikuwa zinasua sua basi tarehe 14 February ndo ilikuwa kama siku ya kufanya matambiko. Enzi hizoilikuwa Katika sherehe moja, wanawake walikuwa wakiwasilisha majina yao na kuweka kwenye kisanduku na baadae wanaume wangepita mbele ya kisanduku hicho na kila mmoja kujitwalia jina moja. Kilichokuwa kinatokea katika sherehe kila aliyejiokotea jina hulitaja na kujitwalia huyo mwanamke kuwa mwanandoa kwa muda wote wa sikukuu wakati mwingine ilikuwa ni mwanandoa wako kwa mwaka mzima mpaka Valentine nyingine akaweke jina pale kwenye kibox. Mila hii ilitumika kukuza Jamii ya Kirumi kwa maana ya uzazi na maisha mengine kwa ujumla, kasheshe kama ulibeba ile ya mwaka mzima then Valentine imefika kisha unataka kubadilisha halafu uliyembeba mwaka jana mjamzito tehe tehe imekula kwako. St Valentine, Padri Wa Kikristo (St. Valentine, Christian Priest) Kulingana na hadithi za zamani, Mfalme wa Kirumi mwenye jina Claudius II ilipiga marufuku juu ya ndoa kwa sababu enzi hizo vijana wengi walikuwa wakiojitwalia wake mapema ili kukimbia jeshi maana amri ilikuwa mtu ambaye hana mke hana familia ndo alikuwa anapaswa kuingia jeshini maana hana cha kupoteza yuko mwenyewe tuy tehe tehe. Sasa kuna Padri mmoja wa Kikristo aitwaye Valentinus yeye ndo alikuwa kazi yake kufungisha hizo harusi kisirisiri maana inaonekana walikiuwa wakimpoza na mwisho wa siku huyu padri akahukumiwa kunyongwa. Wakati akisubiri kunyongwa, Wapenzi Vijana (Couples) walimtembelea na kumwandikia kitu kama barua kama sio waraka kuwa ni namna gani ndo ni tamu kuliko Vita ya kwanza vya dunia na vya pili. Valentine Mwingine. Valentinus mwingine alikuwa Padri nae alifungwa jela kwa ajili ya kusaidia Wakristo. Wakati akiwa bado yuko jela huyu kuhani aka fall in love na binti mlinzi wa gereza na wakati karibu anakwenda kunyongwa akaandika ujumbe “From Your Valentine” . Habari zake zikahifadhiwa na kuripotiwa Papa Julius I na baadae alijenga nakshi nakshi juu ya kaburi lake. Wakristo Wajibinafsishia Valentine’s Day: Katika mwaka wa 469 wa kutawala kwake Gelasius alitangaza Februari 14 siku takatifu kwa heshima ya Valentinus tajwa hapo juu badala ya kuwa siku ya kipagani ya mungu Lupercus wa Kirumi. Hapa ndo Wakristo wa enzi hizo wakachakachua sikukuu hiyo na kuruhusu kuchukua baadhi ya maadhimisho ya siku ya mapendo na ngono ambapo awali mambo hayo yalikuwa katika mazingira ya upagani. Si ajabu kwenye Valentine hii ukaona Guest House zimejaa, madukani watu wananunua condom hawajui kuwa kuadhimisha huko hawajaanza wao ila ni zile imani za kipagani. Maadhimisho ya kipagani yalikuwa lazima yaitimishwe kwa tendo la ngono ili kuonesha kilele cha upendo. Na njia rahisi iliyokuwa ikitumika katika kusheherekea siku hii ni ile ya kuweka majina kwenye kibox kisha kilaini unajibebea huku “mungu” Shahidi akisimamia zoezi zima. Kwa maana ya kwamba hakuna mtu atakaye okota jina bahati mbaya kuna roho inayomuongoza mtu kuchagua jina fulani. Valentine Day Yageuka kuwa Siku Ya Wapendanao. Kama ambavyo tumeitazama siku ya Valentine wala haikuwa siku ya wapendanao ilikuwa sikukuu ya Kipagani, ila baadae ikachakachuliwa hapo ikawa ya Kikristo lakini ni kama upagani ndani yake. Ilipokuwa Wakati wa Uamsho kwente Karne ya 14 ambapo tamaduni zikaanza kupewa tena shamrashamra za Kitaifa, ndipo Valentine ikapewa shavu la kuwa siku ya wapendanao. Ndipo katika kipindi hiki watu wakaachana na makatazo ya kidini wakati huo na yale mafundisho ya msingi katika dini yakapewa kisogo na watu wakageukia matamanio yao.Nyaraka na nyimbo mbali mbali za kuhusu mapenzi, ngono na kujamiiana vikaenea katika kizazi hicho kama ilivyo sasa kila nyimbo ni mapenzi hata picha za mabango ya barabarani ni mapenzi kwenda mbele. Valentine na Kibiashara Zaidi. We utaona tu valentine hii ubepari unavyoshika hatamu yake katika kutumia ili tu “Wapenzi” Wakolezee eti Valentine Day. Kuna watu watanunua nguo mpya nyekundu ili mradi tu watupie kitu chekundu, mijihela mingine itapelekwa kununulia zawadi za wapenzi, hapo sijahesabu maua yatakayonunuliwa siku ya valentine, hapo sijaongelea chakula cha usiku cha wapenzi, hapo sijaongelea wale watakao amua kwenda kulala. Kama kuna siku nzuri ya biashara basi Valentine inakaribiana na Christimas. Mtazamo Wangu na Valentine Za Kibongo. Nakubaliana na wale ambao siku hiyo watatumia kuwapongeza ndugu zao wazazi wao na wapenzi wao. Swali la kujiuliza hapa “tuna adhimisha” ama “tunasheherekea” Valentine?kama tuna adhimisha siku hii, lazima ujue unachoadhimisha, kipi kati yapo juu unachoadhimisha?kama unasheherekea unashehereka nini?otherwise tunakuwa busy na sikukuu tusiyoijua. Ukitaka lawama valentine we usinunue zawadi, usimtoe mtu dinner, jikaushe kama jumanne zingine tu za kawaida. Kwa Mtazamo wangu mdogo nimebaini “Valentine Day” Wanawake ndo wako excited nayo kuliko Wanaume. Kwanini?Kwa wale wanaume wasio waaminifu siku hiyo wengi hu opt kupumzika nyumbani ili kuondoa lawama. How?Unajua wanaume wengi ndio wanao cheat sasa anapotaka kwenda outing anajua msala unaweza kutokea. Ila kwa wale wanao tazamia kusheherekea ama kuadhimisha siku hii kwa namna yoyote ile basi nina wasiwasi wa baadhi ya watu kukimbiwa kidizaini siku hii, na wengi pasipo kujua kuwa kuna roho nyuma yake watajikuta wakiadhimisha kwa ngono kama ishara ya upendo kumbe ni ile ibada ya kipagani tuliyoisoma hapo juu. Abiria chunga mzigo wako kwenye Valentine. Swali la Kujiuliza Kuna madhara yoyote ya Mkristo kusheherekea Sikukuu Ya Valentine? SPECIAL THANKS TO SAM SASALI. Posted by Sophia Mbeyu at 00:36 Email ThisBlogThis!Share to TwitterShare to FacebookShare to Pinterest No comments: Post a Comment Links to this post Create a Link Older Post Home Translate Powered by Translate PLACE YOUR ADS HERE PLACE YOUR ADS HERE TANGAZO: UNAHITAJI VIATU WASILIANA NASI HAPA TANGAZO: UNAHITAJI VIATU WASILIANA NASI HAPA UNAHITAJI BOFYA PICHA HII KUONA PICHA ZAIDI About Me My Photo Sophia Mbeyu View my complete profile Blog Archive Popular Posts MATOKEO YA DARASA LA SABA MWAKA 2014 YAMETOKA, INGIA HUMU KUONA DK. CHARLES E. MSOND E AKITANGAZA MATOKEO YA DARASA LA SABA MAPEMA HII LEO OFISINI KWAKE,MSONDA AMESEMA MATOKEO YA MWAKA HUU UFAURU WAKE ... MITINDO YA VITENGE KWA WANAWAKE NA WANAUME... KAMA INAVYYONYESHA PICHA! VAZI LAKITENGE LAWEZA KUTUMIWA KAMA VAZI LA OFISI AMA CASUAL SIO LAZIMA KITENGE KIWE N... MITINDO YA VITENGE KWA WOTE,.... WADAU WA VITENGE KILA WIKI KUNA POST YA VITENGE FUATILIA POST ZA NYUMA KUPATA MITINDO MBALIMBALI ZAIDI... MITINDO YA VITENGE KWA AKINA DADA NA WATOTO.. MITINDO YA VITENGE Mitindo ya Vitenge inaweza kushonwa katika dizain mbalimbali, hii inaonyesha mitindo kwa vijana ni katika kuonyesha kuwa kitenge si lazima ... MITINDO BOMBA YA VITENGE! Huhitaji nguo za majina kupendeza, kitu cha kitenge tosha kabisa kukutoa bomba! MITINDO MBALIMBALI YA VITENGE, VIATU NA HANDBAG ZA KITENGE.... MITINDO YA VITENGE KWA AKINA DADA NA WATOTO! MITINDO YA VITENGE KATIKA MATUKIO TOFAUTI... MITINDO YA VITENGE Labels African day 2008 may AMUUA BABA YAKE KUMUOKOA SHANGAZI YAKE ALIYEKUWA ANABAKWA- NACHINGWEA ARIEL SHARON AFARIKI ASEMA YADHOOFISHA UCHUMI AFRIKA aswira Kutoka Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar:Rais wa Comoro Awasili Zanzibar Kuhudhuria Maadhimisho ya Sherehe za Miaka 50 ya Mapinduzi BAADA YA BASI KUGONGA NA KUUA WATATU BABA NA MWANA JAY-Z NA MWANAE BLUE IVY.. Biza mupulu artist Biza mupulu Botswana BREAKING NEWS: FIFA YAHAMISHA MUDA WA KOMBE LA DUNIA MWAKA 2022 HUKO QATAR HABARI ZA KIMATAIFA/ WAUMINI WAUAWA MSIKITINI NCHINI NIGERIA HABARI ZA UMBEYA/. WAKATI WEMA AKITUMA VIDEO YA DIAMOND AKIWA KITANDANI HAKUNA KAMA MWANAMKE HAPO NAPO SASA IGP ATANGAZA MABADILIKO MAKUBWA JESHI LA POLISI. IJUMAA NJEMA WADAU WA SOPHIEMBEYU BLOG.... IMETANGAZWA RASMI KESHO NI SIKU YA MAPUMZIKO KUSHEHEREKEA MAPINDUZI: Kundi la FM Academia KUTWAA TUZO YA MWANASOKA BORA WA AFRIKA NJE YA AFRIKA Machael Jackson kuaga dunia MADAWA YA KULEVYA YAINGIZWA SUPERMARKET KATIKA MAKASHA YA NDIZI MAGAZETI YA LEO IJUMAA 10 JANUARY 2014 Magonjwa ya mlipuko yanukia jijini Dar MAN UNITED YAZINDUKA Mariam bongo MAWAZIRI WAPYA WATANO WATAJWA TANZANIA MITINDO YA NYWELE MITINDO YA VITENGE MKAPA AIPONDA MISAADA KUTOKA NJE MSIKIE JOKATE AKIONGELEA MUZIKI NA FILAMU....... Mwekezaji abomoa nyumba za wananchi wa Mkuyuni-Morogoro ili kupisha ujenzi wa Majosho.11 jan mgogoro Nondoz wa Bongo waliokamilisha kisomo chao Data India. Pablo Machine Familia dar Pablo Machine na watoto Pablo Machine na wakenya kwenye festival Pablo Machine Sabiti PENNY NAE ANENA "HAITATOKEA KAMWE NIKAMDHARAU DIAMOND PICHA ZA WATUHUMIWA WALIOKAMATWA WAKISAFIRISHA SILAHA ZA KIVITA KATAVI PICTURE OF THE DAY..KWA RAHA ZAO Rais wa Zanzibar Dr Ali Shein Aendelea Kutunuku Nishani Rihanna out in Barbados RWANDA YAKANUSHA UVUMI KUHUSU KIFO CHA KAGAME SABABU YA KIFO CHA MPENDWA WETU ZAINAB BUZOHERA TASWIRA MBALI MBALI KATIKA SHEREHE YA MIAKA 50 YA MAPINDUZI ZANZIBAR LEO 12/01/2014 UNAKANDAMIZA ... VAZI LA LEO Wa Bongo WAFANYABIASHARA WA DAR WAGOMEA MASHINE ZA KODI ZA TRA WAFUNGA MADUKA LEO Wakali bongo hawo WANANCHI WALITEKETEZA BASI KWA MOTO WAZIRI KIGODA : MFUMO MASHINE EFDs NI MBOVU WEEKEND NJEMA WADAU WA SOPHIEMBEYU BLOG....NAWAPENDAAA MINGIIII. WEMA NI MAMA KIJACHO? SOMA ALICHOANDIKA HAPO Wizara ya maliasili na utalii imewasimamisha kazi watumishi wake 22 wa idara ya wanyama pori YAICHAPA 2-0 SWANSEA CITY Yatima Dar walilia madarasa yakujisomea PLACE YOUR ADS HERE PLACE YOUR ADS HERE powered by Slideshow Sikiliza clouds radio SIKILIZA KWANZA JAMII RADIO Followers Google+ Followers Total visitors Total Pageviews Sparkline 1515131 CLOCK & CALENDAR buy research paper custom essay writing answering service care February 2015 S M T W T F S 1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 11 12 13 14 15 16 17 18 19 20 21 22 23 24 25 26 27 28 Free Counter Counter Free PLACE YOUR ADS HERE PLACE YOUR ADS HERE WEBSITES & BLOGS MICHUZI JIACHIE BONGOBLOGS TanzMED Wavuti Allyshams Myummah76 Francis Godwin Globalpublishers Full Shangwe Ladyjaydee Swahili TV TMF Haki Ngowi Mimi na Tanzania Mo Blog Chadema Blog CCM Blog January Makamba Zitto kabwe Habari Leo Daily News Mwananchi Mtanzania Tanzania Daima Raia Mwema Majira Mwanaspoti The Citizen Daraja Letu IPP Media Bashir Nkoromo BBC Swahili Sauti ya Amerika Jamii Forums BLOG DEVELOPMENT BLOG DEVELOPMENT AUDIO BAR SIKILIZA BRAND NEW TRACK HAPA!! VIDEO BAR UNATAKA KUPUNGUA UZITO!! CLICK THIS IMAGE Contact Form Name

Mume wa Bobby Kristina kizimbani adaiwa kumpiga

Bobby Kristina

Bopbby na mumewe Nick Gordon
NEW YORK, Marekani
MUME wa msanii Bobby Kristina, Nick Gordon, anatarajiwa kupandishwa kizimbani kujibu shitaka la makosa ya uzembe barabarani.
Pia mamalaka nchini hapa zinamchunguza kwa tuhuma za kumjeruhi, Bobbi Kristina ambaye ni mtoto wa mwanamuziki nguli wa zamani, Whitney Houston.
Marehemu Whiyney alizaa mtoto huyo na mwanamuziki mwingine mahiri, Boby Brown, ambaye ni gwiji wa kutumia dawa za kulevya.
Mahakama ya Fulton County State, leo inatarajia kutoa kibali cha kukamaktwa kwa Gordon iwapo atashindwa kuhudhuria kesi ya awali inayomkabili.
Mahakama hiyo inatarajia kutoa kibali hicho ikiwa ni wiki moja tangu Bobbi Kristina, alipokutwa amepoteza fahamu bafuni huku kichwa chake kikiwa ndani ya sinki lililokuwa limejaa maji.
Kwa mujibu wa uchunguzi wa awali, polisi wa mjini hapa wamesema wana imani Gordon alimjeruhi mkewe kabla ya kutokea tukio hilo.
Tayari polisi wameanza kuchunguza mienendo ya uhusiano wa wawili hao, kabla ya Bobbi Kristina, kukutwa na tukio hilo, Jumamosi wiki iliyopita.
Aidha, mamlaka ya kiuchunguzi zimedai wanandoa hao wamekuwa na historia ya kushambuliana ambapo dakika 15 kabla ya tukio hilo walinaswa wakiwa kwenye malumbano makali.
Max Lomas ambaye ni rafiki wa Bobbi Kristina, alidai Gordon alifuta damu katika eneo la tukio zinazosadikiwa kuwa za mkewe.
Lomas alidokeza kuwa alilazimika kuingia nyumbani kwa Bobbi Kristina, baada ya kugonga mlango kwa muda kabla ya kuingia ndani baada ya kukosa mtu wa kumfungulia na kumkuta rafiki yake akiwa amepoteza fahamu bafuni.
Waaguzi katika hospitali aliyolazwa msanii huyo wa vipindi vya televisheni, wanasema hali yake sio nzuri na mjomba wake ameandika kwenye mtandao wa Instagram kuwa hali ya mpwa wake haileti matumaini.
Mjomba huyo alisema madaktari walimwambia ajiandae kupokea taarifa yoyote kwa kuwa hakuna matumaini Bobbi Kristina, kuokoa uhai wake. 
Hatua ya kupoteza fahamu, Bobbi Kristina, limeushtua ulimwengu kwa kuwa linafanana na tukio la kifo cha Whitney aliyefariki Februari 12, 2012.
Whitney alikutwa amefariki bafuni katika Hoteli ya Beverly Hilton huku kichwa chake kikiwa ndani ya maji.
Katika tukio hilo, polisi walikuta chupa za pombe, vyeti vya hospitali vilivyokuwa vikionyesha kusumbuliwa na ugonjwa wa moyo na matumizi ya dawa za kulevya aina ya kokein.
Gordon na Bobby Kristina, walifunga ndoa Januari, mwaka jana licha ya ndoa hiyo kupingwa vikali na Bobby Brown kwa kuwa Godon ni mtoto wa kuasili wa Whitney.

Katika hatua nyingine imeelezwa kuwa mwanadada huyo ameanza kufumbua macho, ikiwa ni kwa mujibu wa shangazi yake.

Mashindano ya Darts kuanza leo Dar

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhVhKfp8h_7sD24sQdW1fxe6itt9YmYbhqVgfkjiu_DA4OxDGKyiOAFD50V8_-ANUr9zuzNVqcLlfoJ7LFfThDq0B_g8qGB_iA4hrLwXtADp89WPM687LH0H_5Sjk-6LfEsGib4q9crHIc/s1600/IMG_4856.jpgMASHINDANO ya mchezo wa vishale (darts) yatakayoshirikisha timu kutoka nchi Tanzania, Kenya na Uganda, yajulikayo kama ‘Kaunje Memoriam Floating Cup’, yanaanza kutimua vumbi leo kwenye Hoteli ya Moshi, Manzese jijini Dar es Salaam.
Mashindano hayo ambayo yameandaliwa na mabingwa wa 2014 wa Afrika Mashariki, Klabu  ya Frendz ya Kinondoni kwa usimamizi wa chama cha mchezo huo Taifa (Tada), yatafanyika kwa siku tatu mfulizo na kufikia kilele chake keshokutwa.
Katibu wa Klabu ya Frendz, Nimesh Katakia alisema kuwa mashindano hayo ni maalum kwa ajili ya kuwaenzi waliokuwa waanzilishi wa klabu hiyo ambao ni marehemu, Kaushik Nariadhara na Said Njenga.
Alisema mashindano hayo yatachezwa kwa mtindo wa timu, wachezaji wawili wawili na mchezaji mmoja mmoja (wanaume), na kwa wanawake yatachezwa kwa mtindo wa timu na mchezaji mmoja mmoja.
Bingwa wa mashindano hayo kwa upande wa timu (wanaume), alisema atajinyakulia fedha taslim Sh. 300,000,  vikombe viwili huku kimoja kikiwa ni cha kushindaniwa kila mwaka, medali sita na cheti. Mshindi wa pili ataibuka na Sh. 200,000, kikombe na cheti wakati mshindi wa tatu ataondoka na Sh.100,000 na cheti.
Aliongeza kuwa, bingwa kwa upande wa wachezaji wawili wawili (wanaume), ataondokana Sh.100,000, medali  na cheti na mshindi wa pili atazawadiwa Sh. 50,000 na cheti, wakati bingwa kwa upande wa mchezaji mmoja mmoja (wanaume) atajinyakulia Sh.100,000, medali, kikombe na cheti na mshindi wa pili atazawadiwa Sh.50,000 na cheti.
Alisema kwa upande wa timu (wanawake),bingwa atazawadiwa Sh.50,000, kikombe, medali na cheti na mshindi wa pili ataibuka na Sh.30,000 na cheti, wakati bingwa kwa upande wa mchezaji mmoja mmoja, atajinyakulia Sh.30,000, kikombe na medali na mshindi wa pili ataambulia Sh.20,000 na cheti.

MOROCCO YAIDINDIA CAF ADHABU AFCON

http://globalvillageextra.com/wp-content/uploads/2014/11/MoroccanNationalTeam.jpg
NCHI ya Morocco imepinga kufungiwa na Shirikisho la Soka Afrika (CAF) baada ya kugoma kuwa mwenyeji wa Fainali za 2015 za Kombe la Mataifa ya Afrika kwa kuhofia mlipuko wa Ebola.
Baada ya kufungiwa kwa nchi hiyo ya Kaskazini mwa Afrika, Shirikisho la Soka la Morocco limepinga vikali adhabu hiyo likidai ni 'ya kushangaza'.
Mwishoni mwa mwaka jana, nchi hiyo ilitaka kusogezwa mbele kwa michuano hiyo kutokana na hofu ya mlipuko wa Ebola kutoka na mashindano hayo kuvuta hisia za watu wengi, kwa mujibu wa Wizara ya Afya ya Morocco.
Equatorial Guinea iliingilia kati na kuomba kuwa mwenyeji wa michuano hiyo na ilifanikiwa, licha ya kuibuka kwa vurugu zilizoharibu mechi ya nusu fainali kati ya wenyeji na Ghana.
CAF ilithibitisha mapema mwezi huu kuwa Morocco itafungiwa kushiriki Afcon mbili zijazo wakati pia ikitozwa faini ya dola za Marekani milioni moja huku pia ikilazimishwa kulipa fidia ya kuharibu mipango €8.5m.
Baada ya kikao cha Kamati ya Wakurugenzi ya Shirikisho la Soka la Morocco (FRMF) Jumanne, imeelezwa kuwa wameshangazwa na uamuzi huo na wanapinga kufungiwa.
"Kikao cha Kamati ya Wakurugenzi kimeeleza kusikitishwa na uamuzi huo mgumu na mkubwa wa CAF," inasomeka taarifa katika mtandao rasmi wa FRMF.
"Kamati ya Wakugenzi wa FRMF inapinga uamuzi wa kufungiwa na kufungiwa kwa misaada ya kifedha, na inaona kuwa maamuzi hayo yaliyochukuliwa na Kamati ya Utendaji ya CAF yanarudisha nyuma maaendeleo ya soka la Afrika, na hayajazingatia kanuni yoyote."

TANZANIA YAPOROMOKA FIFA, IVORY COAST YAPAA

https://media.zenfs.com/en_GB/Sports/Eurosport/1411933-30235371-2560-1440.jpg
Mabingwa wa Afrika, Ivory Coast wamepanda kwa nafasi nane
http://api.ning.com/files/Whapl-f-NAa*ff0QY0nKb-GzXt3OU3W0Um6y3Wv2sdGy1YhHgh3eN4BnXYoFkpa8DdbYB3xmtGU1h7gcY39ru0ECvlOuNWgW/TAIFA1.jpg
Tanzania iliyozidi kuporomoka FIFA
 TANZANIA imeporomoka tena kwa nafasi tatu katika viwango vya kila mwezi vya soka vilivyotolewa Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) jana.
Tanzania sasa inakamata nafasi ya 30 barani Afrika ikiwa nafasi ya 107 duniani.
Ukanda wa Afrika Mashariki na Kati (Cecafa) unaongozwa na Rwanda ambao ni wa 19 barani Afrika na 72 duniani wakifuatwa na Uganda (21 Afrika, 76 duniani), Ethiopia (28,102), Tanzania, Sudan (32, 112), Kenya (36, 116), Burundi (39, 124), Sudan Kusini (50, 189), Eritrea (52, 202), Somalia (53, 204 na Djibouti (54, 206).
Algeria wanashika usukani katika 10 bora barani Afrika wakikamata nafasi ya 18 duniani wakifuatwa na Ivory Coast (20), Ghana (25), Tunisia (26), Cape Verde (35), Senegal (36), Nigeria (42), Guinea ya Ikweta (43), Cameroon (45) na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (46).
Baada ya kutwaa ubingwa wa Afrika, Ivory Coast imepanda kwa nafasi nane huku wanafainali wenzao, Ghana wakipaa kwa nafasi 12.
Ujerumani wanaendelea kuongoza viwango vya dunia wakifuatwa na Argentina, Colombia, Ubelgiji, Uholanzi, Brazil, Ureno, Ufaransa, Uruguay na Hispania wanaofunga 10 bora ulimwenguni

Aston Villa yamtimua Paul Lambert

http://static.guim.co.uk/sys-images/Football/Pix/pictures/2012/10/4/1349390143504/Paul-Lambert-is-suing-Nor-008.jpg
KLABU ya Aston Villa imetangaza kumtimua kocha wake Paul Lambert baada ya kutofurahishwa na mwenendo mzima wa timu hiyo.
Lambert (45), alirithi mikoba ya Alex McLeish Juni 2012 lakini kutokana na matokeo mabovu, ambayo yameifanya Villa kuburuza mkia katika Ligi Kuu kwa sasa, klabu hiyo ilitangaza kuvunja mkataba na Mscotland huyo juzi.
Taarifa kutoka tovuti ya mtandao huo ilisema: "Aston Villa Football Club jioni hii (juzi) imevunja mkataba na kocha Paul Lambert.
"Kocha wa kikosi cha kwanza, Scott Marshall na  kocha wa makipa Andy Marshall wataendelea kukiandaa kikosi kwa ajili ya mechi ya FA Jumapili dhidi ya Leicester City katika Uwaja wa Villa Park.
Klabu pia ingependa kumshukuru  na kuchukua nafasi hii kumtakia mafanikio mema mbeleni.”

Pigo! Gerrard nje wiki tatu Liverpool

http://i3.mirror.co.uk/incoming/article4735129.ece/alternates/s1227b/Leicester-City-v-Liverpool.jpg
Nahodha Steven Gerrard
LIVERPOOL, England
NAHODHA wa Liverpool, Steven Gerrard anakabiliwa na hatihati ya kuwa nje kwa wiki tatu kutokana na kuwa majeruhi, kwa mujibu wa magazeti mengi ya Uingereza.
Gerrard alitolewa dakika ya 68 wakati Liverpool ikishinda 3-2 dhidi ya Tottenham kwanye Ligi Kuu ya England Jumanne, na magazeti ya The Guardian na Liverpool Echo yameripoti kuwa kiungo huyo anasumbuliwa na misuli ya nyama za paja ambayo yatamfanya kukaa nje kwenye mechi ya Kombe la FA mwishoni mwa wiki dhidi ya Crystal Palace.
Msimu huu Gerrard (34), ameanza mechi 20 za Ligi Kuu na anatarajiwa pia kuikosa mechi ya Europa League nyumbani dhidi Besiktas, nyingine ikiwa dhidi ya Southampton Februari. 22.

NASAHA YA IJUMAA- KISA CHA NABII ADAM (AS)

Jinamizi la Sikinde videoni, Valentine wapo Pentagone

BENDI kongwe ya muziki wa dansi ya Mlimani Park 'Sikinde' imerekodi video ya wimbo wao mpya uliobeba jina la albamu ya ijayo iitwayo 'Jinamizi la Talaka',  huku wakiweka bayana kwamba watajumuika na mashabiki wao kusherehekea 'Siku ya Wapendanao' jijini Dar es Salaam.
Mmoja wa viongozi wa Sikinde, Abdallah Hemba, aliiambia MICHARAZO kuwa bendi yao imerekodi video hiyo ambayo ipo hatua za mwisho kukamilishwa kama utambulisha wa ujio wa albamu yao mpya itakayokuwa na nyimbo saba.
Hemba ambaye ni mmoja wa waimbaji nyota nchini alisema kuwa mara video hiyo itakapokamilika wataiachia hewani na kuanza jukumu la kumalizia nyingine za nyimbo zilizosalia kabla ya kufanya uzinduzi baadaye mwaka huu.
"Tumeanza kurekodi video za nyimbo za albamu yetu mpya, tumeanza na 'Jinamizi la Talaka' ikiwa hatua za mwisho na tutaendelea kwa nyingine baadae," alisema Hemba.
Hemba alisema katika kusherehekea Siku ya Wapendanao itakayoadhimishwa kesho, bendi yao itafanya onyesho maalum kwa wakazi wa Kurasini eneo la Mivinjeni katika ukumbi wa Pentagone Pub.
"Tutajumuika na mashabiki wetu eneo la Mivinjeni Kurasini kwa kutambulisha nyimbo mpya na kuwakumbushia za zamani ili kuonyesha tunawapenda katika ukumbi wa Pentagone Pub," alisema Hemba, aliyewahi kutamba na bendi ya Mchinga Sound.

Thursday, February 12, 2015

RATIBA YA MECHI ZA LIGI KUU VPL NDIZO HIZI

JKT Ruvu
Mtibwa Sugar

Ndanda Fc

Ruvu Shooting
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjsiSMyuzw8Scaz_WXLWA8zexyBWABhGV6CxMyERHknqT5Q43BcmRrLvHUNE4oKs2G0hzOPiau9RUA7-sUr7pys-pddVf-7IGaefiwHsTshpDCGxRvAxh3L-kL2Ok3ZtNfCb9E2HTfhftye/s1600/S1.jpg
Simba
Feb 14, 2015
Ndanda vs Mtibwa Sugar
Coastal Union vs Mbeya City
Stand United vs Mgambo Shooting
Feb 15, 2015
Polisi Morogoro vs Simba
Kagera Sugar vs JKT Ruvu
Feb 21, 2015
Mbeya City vs Yanga
Kagera Sugar vs JKT Ruvu
Ndanda vs Coastal Union
Mgambo Shooting vs Mtibwa Sugar
Feb 22, 2015
Stand United vs Simba
Azam vs Tanzania Prisons
Feb 25, 2015
Mbeya City vs Ruvu Shooting

HIVI NDIVYO TFF ILIVYOPANGUA KAMATI ZAKE NDOGO ZA SHERIA

 
JUDICIAL AND STANDING COMMITTEES.

Kamati ya Utendaji iliyoketi tarehe 19 Disemba 2014, ilifanya mabadiliko katika kamati ndogo ndogo na zile za kisheria. Kamati hizo ni kama ifuatavyo

KAMATI YA NIDHAMU
1.   Tarimba Abbas (Mwenyekiti)
2.   Advocate Jerome Msemwa ( Makamu mwenyekiti)
3.    Kassim Dau
4.   Nassoro Duduma
5.   Kitwana Manara 

KAMATI YA RUFANI YA NIDHAMU
1.   Advocate Mukirya Nyanduga (Mwenyekiti)
2.   Advocate Revocatus Kuuli (Makamu mwenyekiti)
3.   Abdala Mkumbura
4.   Dr. Francis Michael
5.   Advocate Twaha Mtengela
 
KAMATI YA MAADILI
1.   Advocate Wilson Ogunde (Mwenyekiti)
2.   Advocate Juma Nassoro (Makamu mwenyekiti)
3.   Advocate Ebenezer Mshana
4.   Geroge Rupia
5.   Mh. Said Mtanda

KAMATI YA RUFANI YA MAADILI
1.   Advocate Walter Chipeta (Mwenyekiti)
2.   Magistrate  George Kisagenta (Makamu-M'Kiti)
3.   Lilian Kitomari
4.   Advocate Abdala Gonzi

KAMATI YA UCHAGUZI
1.   Advocate Melchesedeck Lutema
2.   Advocate Adamu Mambi (Makamu mwenyekiti)
3.   Hamidu Mahmoud Omar
4.   Jeremiah John Wambura
5.   John Jambele

KAMATI YA RUFANI TA UCHAGUZI
1.   Advocate Julius Lugaziya (Mwneyekiti)
2.   Advocate Machare Suguta (Makamu Mwenyekiti)
3.   Idrisa Nassor
4.   Paschal Kihanga
5.   Benister Lugora

KAMATI YA FEDHA NA MIPANGO
1.   Wallace Karia (Mwenyekiti)
2.   Yahya Mohamed (Makamu mwenyekiti)
3.   Goodluck Moshi
4.   Omar Walii
5.   Ellie Mbise
6.    Deo Lubuva

KAMATI YA MASHINDANO
1.   Geofrey Nyange (Mwenyekiti)
2.   Ahmed Mgoyi (Makamu mwenyekiti)
3.   James Mhagama
4.   Stewart Masima
5.   Steven Njowoka
6.   Said Mohamed

KAMATI YA UFUNDI
1.   Kidao Wilfred (Mwenyekiti)
2.   Athumani Kambi (Makamu mwenyekiti)
3.   Vedastus Rufano
4.   Dan Korosso
5.   Pelegriunius Rutahyugwa

KAMATI YA MPIRA WA MIGUU YA VIJANA
1.   Ayoub Nyenzi (Mwenyekiti)
2.    Khalid Abdallah (Makamu mwenyekiti)
3.    Ali Mayay
4.   Mulamu Ngh’ambi
5.   Said Tully

KAMATI YA MPIRA WA MIGUU WANAWAKE
1.   Blassy Kiondo (Mwenyekiti)
2.   Rose Kissiwa (Makamu mwenyekiti)
3.   Zena Chande
4.   Amina Karuma
5.   Zafarani Damoder
6.   Beatrice Mgaya
7.   Sofia Tigalyoma
8.   Ingrid Kimario (Katibu wa Kamati)

KAMATI YA WAAMUZI
1.   Saloum Umande Chama (Mwenyekiti)
2.   Nassoro Said (Makamu mwenyekiti)
3.   Charles Ndagala (Katibu)
4.   Kanali Issaro Chacha
5.   Soud Abdi

KAMATI YA HABARI NA MASOKO
1.   Athuman Kambi (Mwenyekiti)
2.   Alms Kasongo (Makamu Mwenyekiti)
3.   Rose Mwakitangwe
4.   Amir Mhando
5.   Haroub Selemani

KAMATI YA UKAGUZI WA FEDHA
1.   Ramadhan Nassib (Mwenyekiti)
2.   Epaphra Swai (Makamu mwenyekiti)
3.   Jackson Songora
4.   Golden Sanga
5.   Francis Ndulane
6.   Cyprian Kwiyava

KAMATI YA TIBA
1.   Dr. Paul Marealle (Mwenyekiti)
2.   Dr. Fred Limbanga (Makamu mwenyekiti)
3.   Dr. Mwanandi Mwankewa
4.   Dr. Eliezer Ndelema
5.   Asha Mecky Sadik

KAMATI YA FUTSAL NA BEACH SOCCER
1.   Ahmed Idd Mgoyi (Mwenyekiti)
2.   Hussein Mwamba (Makamu mwenyekiti)
3.   Samson Kaliro
4.   Shaffih Dauda
5.   Boniface Pawassa
6.   Apollo Kayugi

PRESIDENTIAL COMMISSION FOR AFFAIRS
1.   Omar Abdulkadir (Mwenyekiti)
2.   Emmanuel Chaula (Makamu mwenyekiti)
3.   Victor Mwandiki
4.   Riziki Majala
5.   Zahra Mohamed
6.   David Nyandu

PRESIDENTIAL COMMISSION ON BUSINESS AND INVESTMENTS
1.   William Erio (Mwenyekiti)
2.   Mbaraka Igangula
3.   Advocate Iman Madega
4.   Lt. Col Charles Mbuge
5.   Philemon Ntalihaja

TIMU ya Taifa ya Beach Soccer kuwafuata Wakenya kesho

TIMU ya Taifa ya Tanzania ya mpira wa ufukweni (beach soccer) inatarajia kurusha karata yake ya kwanza Jumapili kwa kucheza na Kenya katika raundi ya kwanza ya michuano ya Afrika kwa ajili ya fainali za Afrika za michuano hiyo zitakazofanyika Aprili mwaka huu nchini Shelisheli.
Mchezo huo utachezwa Mombasa nchini Kenya na mchezo wa marudiano utachezwa nchini kati ya Februari 20 na 22 mwaka huu
Akizungumza jijini, Kocha wa timu hiyo John Mwansasu, alisema maandalizi ya kwa ajili ya mchezo huo yanaendelea vema na wamecheza michezo miwili ya kirafiki na timu ya Zanzibar na kusema walipoteza mmoja na kushinda mmoja.
 “Maandalizi yanaendelea na kiwango cha wachezaji kinaimarika kila siku na nawaahidi watanzania kurudi na ushindi japo sikupata michezo ya kirafiki ya kimataifa lakini nina imani na timu yangu”, alisema Mwansasu.
Kocha John Mwansasu anasaidiwa na Ali Shariff 'Adolf' kutoka Zanzibar, na Meneja wa timu ni George Lucas na kikosi cha timu ya Taifa ya Tanzania ya mpira wa ufukweni (beach soccer) kinaundwa na wachezaji  15, saba toka Zanzibar na nane Tanzania bara
Iwapo timu ya Tanzania itasonga mbele, katika raundi ya pili itacheza na Misri ikianzia nyumbani kati ya Machi 13 na 15 mwaka huu.
Timu hiyo inayofanya mazoezi kwenye ufukwe wa Escape One inatarajiwa kuondoka nchini kesho Ijumaa.

Mama Muuza wa Shamsa bado kidogo tu

SHAMSA Ford, mmoja wa nyota wa filamu wa kike nchini, amewataka mashabiki wake wakae tayari kuipokea filamu yake mpya ya 'Mama Muuza' ambayo ipo hatua za mwisho ikirekebishwa kabla ya kuachiwa mtaani.
Akizungumza na MICHARAZO, Shamsa alisema filamu hiyo iliyotungwa na kutayarishwa na yeye mwenyewe ikiwa imewashirikisha wasanii kadhaa nyota akiwamo Haji Adam 'Baba Haji', itatoka Aprili.
"Nipo katika marekebisho ya mwishomwisho na nitaiachia 'Mama Muuza' miezi miwili ijayo kulingana na foleni iliyopo kwa wasambazaji," alisema.
Shamsa alisema kama ilivyokuwa kwa 'Chausiku' moja ya filamu iliyofanya vema kwa mwaka 2014, ndivyo 'Mama Muuza' itakavyokuwa kutokana na simulizi lake kubeba uhalisia wa maisha ya uswahili.
"Kama ilivyokuwa 2014 napenda mwaka 2015 uwe wenye raha na burudani kwa mashabiki wangu kupitia 'Mama Muuza'," alisema Shamsa.

Mengi kumtangaza Mshindi wa Wazo la Biashara 3N leo

http://blogs-images.forbes.com/mfonobongnsehe/files/2014/04/reginald-mengi.jpg
Mfanyabishara maarufu nchini Dk Reginald Mengi
 Na Rahma Junior
MSHINDI wa Januari 2015 wa Shindano la Wazo la Biashara 3N' anatarajiwa kutangazwa leo Alhamisi ya Februari 12 kuanzia saa tano asubuhi jijini Dar es salaam.
Kwa mujibu wa Dk. Reginald Mengi kupitia kurasa wake wa twitter, alitangazia umma kuwa Shindano hilo jipya lijulikanalo kwa kifupi -3N, ikiwa ni kifupisho cha ‘Nitabuni wazo la biashara, Nitatekeleza, na Nitafanikiwa’, ambapo mshindi wa kwanza wa mwezi Januari anatarajiwa kutangazwa siku hiyo ya alhamisi Februari 12.
Dk. Mengi aliweka ujumbe huo twittter : “Kutokana na sababu zisizozuilika mshindi wa Januari wa shindano la 3N atatangazwa Februari 12 saa 5 asubuhi. Samahani kwa usumbufu wowote”.
Kwa mujibu wa Dk. Mengi awali mshind I alitakiwa kutangazwa Jumatano ya leo ya Februari 11, kabla ya kusogeza mbele hiyo Februari 12.
Shindano hilo litakuwa linafanyika kila mwezi kwa muda wa miezi sita kuanzia Januari Mosi 2015, hadi Juni 30, 2015, na mshindi wa kila mwezi atajishindia ruzuku ya shilingi milioni 10 atakazozitumia kutekeleza kwa vitendo wazo lake la biashara.
Shindano hilo, linawashirikisha Watanzania pekee, litaendeshwa kwa njia ya mtandao wa kompyuta ambapo mshiriki atatuma wazo lake la biashara kwa anuani ya twita @regmengi Shindano la Wazo la Biashara. Katika mchujo wa kwanza jopo la wataalamu litateua mawazo 10 bora Zaidi na waliotoa mawazo hayo watafanyiwa usaili kwa njia ya simu ili jopo hilo lijiridhishe kama mawazo waliyoyotuma ni yao binafsi, na kama wamejipanga vizuri kutekeleza kibiashara.
Kutokana na mawazo hayo 10 teule, jopo litachagua wazo moja kuwa mshindi. Hii ni mara ya tatu kwa Dkt. Mengi kuendesha shindano kwa kutumia mtandao wa kompyuta wa twitter kwa kuamini kwake kuwa mitandao ya kijamii ina nguvu kubwa katika kuchochea ujasiriamali hasa kwa kizazi cha sasa.
Shindano la kwanza na la pili lililoendeshwa mwaka jana lilikusudiwa kushawishi mawazo ya kuondoa umaskini katika taifa lenye utajiri mkubwa, lakini watu wake wengi wakiwa bado wametopea katika lindi la umaskini.
Awali akizungumza katika uzinduzi wa shindano hilo, Dkt. Mengi alisema shindano hilo limelenga kuhimiza watu kuwa na upeo mkubwa wa kuona fursa za kibiashara na kuzitumia kujikwamua kiuchumi. Pia alisema shindano hilo ni mchango wake binafsi wa kuunga mkono jitihada za serikali na sekta binafsi za kuwakomboa wananchi kiuchumi kwa njia za ujasirimali, kwani amesema Sera zote mbili za kitaifa za Elimu ya juu na maendeleo ya viwanda vya kati na vidogo zina vipengele vya kuchochea na kuendeleza utamaduni wa ujasirimali wa mtu mmoja mmoja.
“Kwa muda mrefu nimekuwa nikishawishi uwepo wa moyo wa ujasirimali miongoni mwa wa Watanzania na hasa kwa vijana. Ni ndoto yangu kuona uchumi wetu unakua kwa kasi kiasi cha kuzalisha zaidi ya mamilionea 100 kila mwaka wanaoendesha biashara halali,” alisema.
Alisema kuwa na wazo sahihi la biashara, katika muda muafaka na eneo sahihi ni muhimu zaidi kuliko ruzuku ya fedha.
“Nataka vijana watambue kwamba wanaweza kuanza na kitu kidogo na kukua kufikia kampuni kubwa kabisa ya kimataifa unayoweza kufikiria,” alisema na kusisitiza kwamba anaamini siku moja mazingira ya ujasirimali nchini Tanzania yakuwa miongoni mwa mazingira bora kabisa barani Afrika.
Amesisitiza kuwa Shindano hilo liko wazi kwa watanzania wote na wanachotakiwa kufanya ni kuhakikisha wanapeleka wazo lao la biashara kwa Dk Mengi kupitia mtandao wa kompyuta wa twita, kwa kumtag Dk Mengi kwenye @regmengi.
Aidha amesema ni wale tu watakaomtag ndio watafikiriwa na jopo la wataalamu, na kusisitiza kuwa maamuzi ya jopo la Wataalamu yatakuwa ni ya mwisho.
Washindi wa kila mwezi wataarifiwa kwa kutumiwa ujumbe mfupi kwa kupitia akaunti zao za twita (DM) na kupewa ruzuku yao katika sherehe fupi itakayohudhuriwa na waandishi wa habari.

Wednesday, February 11, 2015

Azam yaifumua Mtibwa Sugar 5-2 warudi kileleni

KLABU ya Azam wamerejea kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara baada ya kuifumua bila huruma Mtibwa Sugar kwa mabao 5-2.
Azam ambao ni mabingwa watetezi wa ligi hiyo wealipata ushindi huo mnono na wa kwanza kushuhudiwa katika mechi za ligi msimu huu katika pambano pekee lililochezwa kwenye uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam.
Frank Domayo 'Chumvi' alifunga mabao mawili moja kila kipindi sawa na alivyofanya Kipre Tchetche na Didier Kavumbagu alifunga moja kuiangamiza Mtibwa ambao hicho ni kipigo chao cha pili mfululizo.
Mtibwa walioanza msimu huu kwa mkwara na kuongoza ligi hiyo kwa muda mrefu kabla ya kuporomoka mara baada ya kurejea kwenye michuano ya Kombe la Mapinduzi, ilifunikwa eneo la kiungo na Azam.
Vijana hao wa Mecky Mexime walipata mabao yao ya kufutia machozi kupitia kwa Juma Nampaka na Ame Ali ambayo hata hivyo hayakusaidia Wakata Miwa hao kufurukuta mbele ya mabingwa watetezi hao.
Kwa ushindi huo umeifanya Azam kurejea tena kileleni wakifungana pointi 25 sawa na Yanga, lakini tofauti na mabao ya kufunga na kufungwa yanawapa nafasi ya kukalia kiti cha uongozi.
Mtibwa wenyewe wameendelea kusalia katika nafasi ya sita wakiwa na pointi 18 sawa na ilizonazo timu za Kagera Sugar na Coastal Union.
Yanga na Azam zinazochuana kieleleni mwishoni mwa wiki zitakuwa kwenye majukumu ya kimataifa wakati Yanga itaikaribisha BDF XI ya Bostwana na wenzao Azam wataumana na El Merreikh wanaotarajiwa kutua nchini kesho tayari kwa pambano hilo litakalochezwa Jumapili.
Pambano la Yanga litacheza Jumamosi na viingilio vimeshjatangazwa kwa kiingilio cha chini kikiwa ni Sh 5000 tu.
Wakati lile la Yanga kiingilio cha chini kabisa ni Sh 2000 na vingine ni VIPB Sh 5000 na VIP A 10000 na tyiketi zitaanza kuuzwa Ijumaa.

Mourinho amchongea Van Persie kwa FA

MENEJA wa vinara wa Ligi Kuu ya England, klabu ya Chelsea, Jose Mourinho amekishambulia Chama cha Soka cha Uingereza(FA) kwa kuamua kutochukua hatua yeyote kwa mshambuliaji wa Manchester United, Robin Van Persie kwa tuhuma za kumtwanga kiwiko mchezaji wa upinzani.
Van Persie alionekana akimpiga kiwiko James Tomkins wakati wa mchezo ambao United ilitoa sare ya bao 1-1 dhidi ya West Ham United Jumapili iliyopita lakini mwamuzi Mark Clattenburg hakuona tukio hilo huku FA nao wakilifumbia macho.
Uamuzi huo unamfanya Mourinho kutowaelewa FA kwani anatarajiwa kumkosa nyota wake Diego Costa katika mchezo wa leo dhidi ya Everton baada ya mshambuliaji wa kimataifa wa Hispania kufungiwa mechi tatu kwa kukutwa na hatia ya kumkanyaga kwa makusudi Emre Can mwezi uliopita.
Akihojiwa Mourinho amesema watu haohao ambao wamemfungia mchezaji wake Costa ndio hao ambao hawataki kumfungia Van Persie kwa kosa lake alilofanya.
Mourinho aliendelea kudai kuwa anajua kama angekuwa mchezaji wake lazima angefungiwa kwani tukio kama hilo lilimtokea Ramires na alilimwa adhabu.

Sanchez, Ramsey wazua hofu Arsenal

http://www3.pictures.zimbio.com/gi/Aaron+Ramsey+Alexis+Sanchez+Leicester+City+N8Hb6G9P6Rgl.jpg
Ramsey, Sanchez



KOCHA wa Arsenal, Arsene Wenger amesema ana wasiwasi kuhusu hali za nyota wake Alex Sanchez na Aaron Ramsey baada ya kupata majeruhi katika mchezo Ligi Kuu walioshinda mabao 2-1 dhidi ya Leicester City.
Ramsey alitolewa nje ikiwa ni dakika tisa tu toka aingie akitokea benchi katika kipindi cha pili baada ya kupata majeruhi ya msuli wa paja, huku winga wa kimataifa wa Chile, Sanchez yeye alitolewa nje kufuatia kuchezewa faulo na Matthew Upson ambayo ilimfanya kushindwa kuendelea na mchezo huo uliochezwa Emirates.
Wenger amesema ana wasiwasi na nyota wake hao kwani hana uhakika watakaa nje ya uwanja kwa kipindi gani wakijiuguza. Mabao yaliyofungwa na Laurent Koscielny na Theo Walcott yalitosha kuwapa Arsenal ushindi huo muhimu baada ya kuchapwa na  Tottenham Hospur
Mabao yaliyofungwa na Laurent Koscielny na Theo Walcott yalitosha kuwapa Arsenal ushindi huo muhimu baada ya kuchapwa na mahasimu wao Tottenham Hotspurs mwishoni mwa wiki iliyopita.

Monday, February 9, 2015

HII NDIYO SHOW TIME YA H-BABA

http://www.bongo5.com/wp-content/uploads/2012/10/H-baba.jpg
H-Baba


IVORY COAST NDIYO VIDUME AFRIKA, YARUDI YA 1992

The Ivory Coast team and staff pose with their Africa Cup of Nations trophy having defeated Ghana 9-8 on penalties on Sunday night
Waflame wa soka Afrika, Ivory Coast
The Ivory Coast team celebrate landing the Africa Cup of Nations on penalties, their first AFCON title since 1992
Oyooooooooooooooooo!
Ivory Coast captain and Manchester star Yaya Toure is presented with the Africa Cup of Nations trophy on Sunday evening
Nahodha Yaya Toure akipokea Kombe toka kwa Rais  Nguema
HISTORIA imejirudia tena nchini Guinea ya Ikweta baada ya Ivory Coast kufanikiwa kutwaa ubingwa wa Fainali za Mataifa ya Afrika 2015  kwa kuichapa Ghana kwa mikwaju ya penati kama ilivyokuwa katika fainali za mwaka 1992.
Katika fainali za mwaka huo, Ghana maarufu kama Black Stars walikufa kwa mikwaju ya penati 11-10 na usiku wa kuamkia leo walikubali tena kipigo cha penati 9-8 kwa wapinzani wao na kuliacha taji likienda kwa Ivory Coast ikiwa ni mara ya pili kwao.
Timu hizo zililazimika kupigiana penati baada ya kumaliza dakika 120 bila ya kufungana na katika upigaji wa penati, Ivory Coast walianza vibaya kwa Wilfried Bony kukosa penati, lakini haikuweza kuwakatisha tamaa Tembo wa Afrika kumaliza udhia na ukame wa miaka zaidi ya 20 tangu wanyakue taji la kwanza 1992.
Ghana wanaweza kujilaumu kwa kushindwa kuibuka mabingwa kwa mara ya tano kutokana na kipindi cha pili cha dakika 90 kutawala sehemu kubwa ya pambano hilo lililosisimua kutokana na lilivyokuwa kali.
Katika hatua ya mikwaju ya penati Black Stars walianza kwa Mubarak kufunga kabla ya Bony kukosa, Jordan Ayew akapata penati ya pili ya Ghana na Tallo wa Ivory Coast naye akaikosa penati yake na kufanya matokeo kuwa 2-0.
Hata hivyo Acquah na Acheampong walikosa penati  zilizofuata za Ghana, wakati Aurierna Doumbia walifunga zao na matokeo kuwa 2-2.
Andre Ayew alifunga mkwaju wake na Yaya Toure akasawazisha, John Mensah akafunga na Solomon Kalou akasawazisha kabla ya Agyemang-Badu kufunga mkwaju wake na Koro Toure kusawalisha.
Afful aliifungia Ghana na Kanon kusawazisha zoezi likawa piga nikupige hadi katika penati ya tisa ambapo Ghana kupitia kipa wake Razak Brimah ilikosa na Ivory Coast kutumbukiza yao iliyowapa ubingwa wa pili katika historia za michuano hiyo kupitia kwa Boubacar Barry aliyegeuka kuwa shujaa kabla ya nahodha Yaya Toure kukabidhiwa taji na Rais wa Guinea ya Ikweta, Nguema kwenye uwanja wa Bata.

Irene Uwoya awataka mashabiki wake kupokea Kisoda

Na Rahma White
MUIGIZAJI nyota wa filamu nchini, Irene Uwoya 'Oprah' amewataka mashabiki wake kujiandaa kuipokea kazi yake mpya iitwayo 'Kisoda' akidai ni kazi kali kuliko hata filamu yake ya awali iitwayo 'Apple' aliyoitoa mwaka jana.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, Irene alisema 'Kisoda' ni moja ya kazi zitakazoleta mapinduzi makubwa katika fani ya uigizaji nchini kwa namna ilivyoandaliwa ikishirikisha wasanii wa ndani na nje ya nchi.
Irene alisema filamu hiyo iliyomtafuna fedha nyingi ipo katika hatua ya uhariri na itaachiwa wakati wowote zoezi hilo likikamilika akiwataka mashabiki wajiandae kuipokea kwa mikono miwili.
"Kama kuna waliodhani nilibahatisha kwenye 'Apple', wamekosea safari hii naja na 'Kisoda', moja kati ya filamu kali ambayo imewashirikisha wasanii wa Tanzania na Afrika Kusini, chini ya kampuni yangu ya Apple Entertainment," alisema Irene.
Msanii huyo alisema amekusudia ndani ya mwaka 2015 awape burudani ya kutosha mashabiki wake na kwa kuanza ameanza na Kisoda kabla ya kufuatiwa na mambo mengine makubwa zaidi.
Irene aliwataja baadhi ya wasanii walioshiriki filamu nchini wa hapa nchini ukiondoa yeye (Irene) ni Islam, Mariam Ismail na Msami.
Kimwana huyo aliyewahi kunyakua tuzo ya Muigizaji w Kike Chipukizi wa tuzo za Kinara kupitia filamu ya Diversion of LOve' kabla ya kuanza kuzalisha filamu zake na kuwahi  kuendesha kipindi cha kwenye runinga cha 'Paradise Show' ameshiriki filamu zaidi ya 30 zilizomjengea umaarufu mkubwa ndani na nje ya nchi.
Baadhi ya kazi hizo ni; 'Ngumi ya Maria', 'Nyati',  'Zawadi Yangu', 'Aliyemchokoza Kaja', 'Figo','Rosemary', 'Snitch', 'The Return of Omega', 'Money Talk', 'Omega Confusion', 'Question Mark', 'Safari', 'Innocent Case', 'Nyota Yangu', 'Last Card', 'Doa la Ndoa', 'Offside' na 'Oprah'.

Sunday, February 8, 2015

Manchester Utd chupuchupu kufa ugenini

Falcao akijaribu kufunga
Kouyate akishangilia bao lake
Pilikapilika uwanjani
KLABU ya Manchester United imeponea chupu chupu kufa ugenini baada ya kupata sare ya 1-1 mbele yua West Ham United.

Bao la kusawazisha lililofungwa dakika za lala salama na Daley Blind liliwaokoa Mashetani Wekundu kufa katika uwanja wa Boleyn Ground.
Blind alifunga bao hilo katika dakika mbili za nyongeza na kumnusuru kocha Luis Van Gaal kuumbuka kama alivyonusurika kocha wa Manchester City jana dhidi ya Hull City baada ya vijana wake kusawazisha bao dakika za jioni.
Wenyeji walitangulia kupata bao dakika ya 49 kupitia kwa Cheikhou Kouyaté na kulikuwa na kila dalili kwa Mashetani Wekundu kufa ugenini, lakini Blind kuchomoa na kuifanya Manchester United kufikisha pointi 44 na kukomalia nafasi ya nne nyuma ya Southampton waliorejea katika Tatu Bora.
Hata hivyo dakika mbili za nyongeza baada ya Man kupata bao ilijikuta ikimpoteza beki wake, Luke Shaw kwa kupewa kadi nyekundu ilifuatia kutokana na kadi ya pili ya njano kwa kumchezea vibaya Stewart Downing.
Vikosi vilikuwa hivi; 
West Ham: Adrian, Jenkinson, Song, Tomkins, Cresswell, Kouyate, Noble, Downing, Nolan, Valencia, Sakho.
Sub: Jarvis, O'Brien, Amalfitano, Jaaskelainen, Cole, Oxford, Lee
Manchester United: De Gea, Valencia, Jones, Rojo, Shaw, Blind, Rooney, Januzaj, Di Maria, van Persie, Falcao
Sub: Mata, Smalling, Ander Herrera, Fellaini, Valdes, McNair, Wilson

Kocha Redknapp kurejea soka kama mwanahisa

http://talksport.com/sites/default/files/tscouk_old_image/blog/Harry-Redknapp_21.jpg
Kocha Harry Redknapp
MENEJA wa zamani wa klabu ya QPR, Harry Redknapp amebainisha anaweza kurejea katika ulimwengu wa soka akiwa sehemu ya mwanahisa.
Redknapp mwenye umri wa miaka 67 ambaye alijiuzulu kuinoa QPR wiki iliyopita kutokana na matatizo ya mguu anahusishwa na kikundi kinachotaka kununua klabu karibu na nyumbani kwake katka Pwani ya Dorset.
Akihojiwa Redknapp amesema jambo hilo linamvutia hivyo anataka kujihusha nalo, kwani mchezo wa soka bado uko katika damu yake.
Redknapp ambaye amewahi kuipeleka Tottenham Hotspurs katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya na pia kuzinoa klabu za Portsmouth na West Ham United aliongeza kuwa wana matumaini ya kupata klabu ya kuinunua.

Jose Mourinho aanza mbwembwe zake England

http://static.guim.co.uk/sys-images/Observer/Columnist/Columnists/2013/6/7/1370621593808/jose-mourinho-010.jpg
Jose Mourinho
KOCHA wa vinara wa Ligi Kuu ya England Chelsea, Jose Mourinho amesema hadhani kama tofauti ya pointi saba walionayo kileleni mwa msimamo wa Ligi hiyo ni faida katika mbio zao za kugombea taji hilo. Chelsea imeitandika Aston Villa kwa mabao 2-1 jana, wakati Manchester City wanaowafuata katika nafasi ya pili wakipotoka sare na Hull City wanaokamata nafasi ya tatu toka mkiani.
Akihojiwa Kocha Mourinho, amesema ingekuwa nchi nyingine angeweza kuanza kushangilia katika kwa Uingereza tofauti ya alama saba sio chochote.
Mourinho aliendelea kudai kuwa bado kuna mechi 14 na alama 42 za kupigania hivyo kila mchezo unakuwa mgumu na chochote kinaweza kutokea.
Kocha huyo pia alisisitiza hakushtushwa kuona City wakitoa sare nyumbani na Hull ambao wako mstari wa kushuka daraja lakini amefurahi kuona matumaini ya kunyakuwa taji yakiwa mikononi mwao.
Ligi hiyo iliendelea tena jioni ya leo kwa timu za Newcastle United wakipata sare ya 1-1 na timu ya Stoke City wakati West Bromwich Albion wakiwa ugenini walipata sare ya 2-2 dhidi ya timu ya Burnley.

Sepp Blatter aponda vyombo vya habari vurugu AFCON

http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/4/44/Sepp_Blatter_at_signing_of_agreement_creating_FIFA_Ballon_d%E2%80%99Or_in_Johannesburg_2010-07-05_1.jpg
Rais wa FIFA, Sepp Blatter
RAIS wa Shirikisho la Soka la Dunia (FIFA) Sepp Blatter, ameponda vyombo vya habari kuonyesha vurugu zilizozuka katika mchezo wa nusu fainali ya michuano ya Mataifa ya Afrika kati ya wenyeji Guinea ya Ikweta na Ghana.
Mchezo huo uliochezwa Malabo ulisimamishwa kwa dakika 30 baada ya mashabiki kurusha vitu kwa wachezaji na mashabiki wa timu pinzani hali iliyosababisha polisi kutumia helikopta na mabomu ya machozi kuwatawanya mashabiki hao.
Vurugu hizo zilikuwa zikirushwa moja kwa moja duniani kote, lakini Blatter anadhani pamoja na vurugu hizo lakini kuna mazuri mengi ya kusifiwa katika michuano hiyo inayotarajiwa kumalizika leo.
Blatter amesema siku zote habari nzuri huwa sio habari ila habari mbaya ndio habari akimaanisha kuwa siku zote watu wamekuwa wakizungumzia mabaya.
Rais huyo amesema dosari ndogo kama iliyotokea katika mchezo wa nusu fainali haipaswi kupewa nafasi ya kusahau mafanikio yaliyopata katika michuano hiyo ambayo imendaliwa kwa kipindi kifupi kuliko ilivyopangwa.

Asamoah Gyan bado alia na Yattara

http://img.modernghana.com/images/content/bgwi04lyx6_asamoahgyan580.jpg
Asamoah Gyan
NAHODHA wa kikosi cha timu ya taifa ya Ghana, Asamoah Gyan ambay anajiandaa kushuka dimbani kuiongoza timu yake katika mechi ya Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika dhidi ya Ivory Coast, amedai hatomsamehe golikipa wa Guinea Naby Yattara kutokana na faulo aliyomchezea timu zao zilipokutana.
Golikipa huyo alimkanyaga Gyan kwa teke la tumboni katika dakika za mwisho za mchezo wa robo fainali uliokutanisha timu hizo.
Yattara alilimwa kadi nyekundu lakini hajapewa adhabu yeyote nyingine mpaka sasa kiasi cha Gyan katika mahojiano yake alisema bado analitaka Shirikisho la Soka la Afrika(CAF) kumtwanga adhabu Yattara kwa sababu anadhani alidhamiria kufanya tukio lile.
Gyan aliendelea kudai kuwa ilikuwa ni faulo mbaya ambayo ingeweza kumsababisha asicheze tena soka ndio maana hataki kumsamehe kwa hilo.
Hata hivyo kipa huyo alinukuliwa juzi akisema kuwa hawezi kumuomba radhi Gyan kwa sababu hakukusudia kumuumiza na kusisitiza kuwa hilo ni tukio la bahati mbaya katika harakati za mchezo.