STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, February 19, 2015

Ally Mustafa 'Barthez' ni Nouma sana!

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi2gWCT-X80QbEFaBLH3ow-j-DUBUoiESu7HybsUaOTaiK29nZu8xGcFRQwETVHpw-nbY11UkU2DDjhKczuGFnfxgBd_5QO8ZU6Kvpo1vd4IHZkFNaX3sIoyhhtPOFOXUbpjMPWPETf4lkv/s1600/35.jpg
Barthez mbele kushoto akiwaongoza wachezaji wenzakle wa Yanga
PAMBANO la Yanga dhidi ya Prisons-Mbeya lililochezwa uwanja wa Sokoine, jijini Mbeya kwa vijana wa Jangwani wakiibuka na ushindi wa mabao 3-0 umezidi kumpandisha chati kipa Ally Mustafa 'Barthez' ambaye amedaka mechi sita mfululizo za Ligi Kuu Tanzania Bara bila kuruhusu bao lolote.
Kipa huyo aliyekuwa na wakati mgumu mbele ya kikosi cha Jangwani tangu Yanga ilipolazimishwa sare ya mabao 3-3 na Simba Oktoba mwaka juzi, hajafungwa bao lolote katika muda wa dakika 540 huku kwenye uwanja wa Sokoine akigeuka kuwa shujaa kwa kuokoa michomo mingi ya wachezaji wa Prisons.
Hizo ni mbali na dakika 90 za pambano la kimataifa la Kombe la Shirikisho Afrika ambapo Yanga ilishinda mabao 2-0 na yeye akiwa kwenye milingoni mitatu ya lango ya vijana wa Jangwani.
Barthez aliyesajiliwa na Yanga akitokea Simba, rekodi zake zinaonyesha kuwa ameshuka dimba katika mechi hizo kama ifuatavyo na kuwafunika makipa wote wa timu nyingine 13 zinazoshiriki ligi hiyo.
Jan 17, 2015Yanga vs Ruvu Shooting (0-0)
Jan 24, 2015Polisi Moro vs Yanga (1-0)
Feb 01, 2015Yanga vs Ndanda (0-0)
Feb 4, 2018Coastal Union vs Yanga (0-1)
Feb 08, 2015Yanga vs Mtibwa Sugar (2-0)
 Feb 14, 2015-Kimataifa
Yanga vs BDF XI (2-0)
Feb 19, 2015
Prisons vs Yanga (0-3)

FAINALI ZA DUNIA 2022 KUFANYIKA DESEMBA?

http://www.shalomlife.com/img/2014/12/27573/qatar_.jpg
MTANDAO mmoja barani Ulaya umetoa taarifa kuwa tayari muafaka umeshafikiwa kwa michuano ya Kombe la Dunia itakayofanyika nchini Qatar mwaka 2022 kufanyika katika kipindi cha Novemba na Desemba ili kuwepa joto kali katika kipindi cha kiangazi.
Wakiorodhesha vyanzo mbalimbali mtandao huo umedai kuwa uamuzi umeshafanyika kwani kikosi kazi kilichoteuliwa na Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) kinatarajia kuwasilisha miezi hiyo katika kikao chao kitakachofanyika wiki ijayo jijini Doha kabla ya kamati ya utendaji haijakamilisha mpango huo wakati wa kikao cha mwezi ujao jijini Zurich.
Wiki tatu zilizopita, Katibu Mkuu wa FIFA Jerome Valcke katika mahojiano yake na radio moja nchini Ufaransa alisema Kombe la Dunia nchini Qatar linatakiwa kuandaliwa wakati wa majira ya baridi lakini kugongana na michuano ya Olimpiki ya kwenye baridi Februari mwaka 2022 pia ni hatihati.
Hata hivyo mpango huo haujafafanua kwa undani zaidi kuwa michuano ya Kombe la Shirikisho ambayo huchezwa mwaka mmoja kabla ya Kombe la Dunia kama nayo itasogezwa mbele kuepuka majira ya kiangazi.
Desemba mwaka jana Chama cha Vilabu barani Ulaya na Muungano wa Ligi za Soka barani humo vilipendekeza michuano hiyo ya Qatar kuchezwa kati ya May na Juni ili kutovuruga ratiba zingine za kawaida za msimu.
Uteuzi wa Qatar kuandaa fainali hizo na zile za mwaka 2018 nchini Russia zimeghubikwa na mizengwe na kuelezwa kujaa vitendo vya rushwa, ingawa FIFA imekuwa ikijitetea.

BAHANUZI, MAHUNDI WANG'ARA VPL

http://2.bp.blogspot.com/-ORUnNfNV-xE/VM0wOPMp6vI/AAAAAAABdBc/1sAbma_8dB4/s1600/BAHANUZI.jpg
Said Bahanuzi
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh2NUIe7-6s8hh3LAnWZphC1Sfmct-j1gnFK6vBlYl6-vWAkEms7KvbsXk8lsXx7as54qc9WOVhCaehk3-wlIYA3DXm_G5D2mryGl3IxaJ0IKhGMNNPLYmPUTtm0N9aOnG0wHywciFMsGQ/s1600/IMG_1197.jpg
Mahundi (kulia) akichuana na Niyonzima katika moja ya mechi ya Ligi Kuu
KIUNGO wa timu ya Coastal Union ya Tanga, John Mahundi amechaguliwa kuwa mchezaji bora wa mwezi Desemba 2014 wa Ligi Kuu Tanzania Bara.
Mahundi alitoa mchango mkubwa kwa timu yake ya Coastal Union mwezi huo na kuchaguliwa na jopo la makocha linalofanya kazi ya kuchagua mchezaji bora wa kila mwezi.
Aidha mshambuliaji wa timu ya Polisi Morogoro, Said Bahanuzi 'Spider Man' amechaguliwa kuwa mchezaji bora mwezi Januari 2015.
Bahanuzi anayechezea timu ya Polisi Moro kwa mkopo akitokea timu ya Young Africans amekua na mchango mkubwa kwa timu yake tangu kujiunga nayo mzunguko wa pili wa Ligi Kuu ya Vodacom nchini.
Kwa kuibuka wachezaji bora, Mahundi na Bahanuzi watazawadiwa fedha taslimu Sh. Mil. 1/ kwa kila mmoja kutoka kwa wadhamini wa ligi hiyo kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom.
Jopo maalum la makocha waliopo katika viwanja vyote vinavyotumika kwa mechi za Ligi Kuu ndiyo wanaofanya kazi ya kuchagua mchezaji bora kwa kila mechi kwa kuzingatia vigezo vilivyowekwa.
Baadaye alama zao kujumlishwa ili kumpata mshindi wa mwezi.

Yanga wafanya mauaji Mbeya, Azam yabanwa

Yanga
Msuva na Coutinho walipokuwa wakijiandaa kuiangamiza Prisons-Mbeya

Azam
Azam walishindwa kushangilia kama hivi leo kwa Ruvu Shooting
KLABU ya Yanga imeendeleza rekodi yake ya kugawa dozi kwa wapinzani wao katika Ligi Kuu Tanzania Bara, baada ya kuilaza Prisons-Mbeya kwa mabao 3-0 na kukwea kileleni mwa msimamo wakiiengua Azam.
Azam waliokuwa uwanja wa Mabatini-Mlandizi wameshindwa kutamba kwa kulazimishwa suluhu mbele ya maafande wa Ruvu Shooting na kutoa nafasi kwa Yanga kuwaacha kwa pointi mbili kileleni.
Kwa suluhu iliyopata kwa Ruvu, imeifanya mabingwa watetezi Azam kufikisha pointi 26 na kushuka hadi nafasi ya pili licha ya timu zote mbili kulingana mechi zote zikicheza michezo 14 kila moja.
Yanga ikicheza kwenye uwanja wa Sokoine, Mbeya walipata ushindi huo murua na uliowafanya kufikisha pointi 28 baada ya kupata mabao yake mawili katika kipindi cha kwanza na jingine kipindi cha pili.
Mabao hayo yaliwekwa kimiani na Simon Msuva aliyefunga dakika ya tatu tu ya mchezo kabla ya Coutinho kuongeza la pili.
Msuva alirudi tena kambani kwa kufunga bao la tatu kipindi cha pili na kumfanya afikishe jumla ya mabao sita akibakisha mabao mawili kumkuta Didier Kavumbagu wa Azam mwenye mabao nane.
Yanga wataendelea kusalia jijini humo kwa ajili yua kusubiri pambano lake la Jumapili dhidi ya Mbeya City kabla ya kutimka zao Botswana kuwafuata BDF XI kwa ajili ya mechi ya marudiano ya Kombe la Shirikisho Afrika.
Katika mchezo wao wa kwanza uliochezwa mwishoni mwa wiki, Yanga iliitambia BDF kwa kuilaza mabao mawili yote yakiwekwa kimiani na Mrundi, Amissi Tambwe.

Wednesday, February 18, 2015

Yanga, Azam vitani tena viwanja tofauti kesho

https://hivisasa.co.tz/wp-content/uploads/2014/09/DSC02166.jpg
Yanga
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhdDjGKemN2sVnPU1l723rHo-UtuVjBZ673i-L4ZgSmKzLiH8dPrkov8VclFd1qQYP1c48z_omeSmeZFlSwvlBweJ0Ous2ja2z3bmlzGANL_dA-GQmz780dcej0AwtKL-Z13vKA-TDyjsQ/s1600/HERM5672-1.JPG
Azam
MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Azam pamoja na wapinzani wao wakuu katika mbio za kuwania ubingwa wa msimu wa 2014-2015, Yanga kesho wanatarajiwa kushuka viwanja tofauti kusaka nafasi ya kujiimarisha kileleni mwa msimu wa ligi hiyo.
Yanga waliopo Mbeya wanatarajiwa kuvaana na Prisons katika pambano litakalochezwa kwenye uwanja wa Sokoine, wakati Azam watakabiliana na maafande wa Ruvu Shooting katika pambano linalotarajiwa kuwa kali litakalochezwa kwenye uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.
Timu hizo mbili zilizotoka kwenye majukumu yao ya kuiwakilisha taifa katika michezo ya kimataifa ya Ligio ya Mabingwa Afrika na Kombe la Shirikisho zote zipo kileleni zikiwa na pointi 25, Azam akitangulia kwa kuwa na uwiano mzuri wa mabao ya kufunga na kufungwa kulinganisha na wapinzani wao.
Azam wanarejea kwenye ligi hiyo wakiwa na kumbukumbu ya ushindi mnono wa mabao 5-2 kwenye uwanja wa Chamazi dhidi ya Mtibwa Sugar, wakati Yanga ikitoka kuwafyeka Mtibwa mabao 2-0.
Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa Yanga, Jerry Muro alinukuliwa mapema jana kuwa kikosi chao kipo tayari jijini Mbeya kugawa dozi kwa maafande hao wa Magereza kabla ya kumalizia kazi kwa Mbeya City Jumapili na kuanza safari ya kuwafuata Wabotswana wa BDF XI kwa mechi ya marudiano ya kimataifa.
Azam wenyewe kupitia Meneja wao, Jemedari Said imetamba kuitoa nishai Ruvu Shooting kabla ya mechi yao ya mwisho ya ligi kuanza safari kuelekea Sudan kurudiana na El Merreikh katika Ligi ya Mabingwa Afrika ambapo katika mchezo wa kwanza uliochezwa Jumapili walishinda mabao 2-0.
Licha ya Yanga na Azam kutamba kujiandaa kugawa dozi kwa wapinzani, timu za Ruvu Shooting na Prisons inayoburuza mkia nazo zimetamba hawatakubali kufa kikondoo katika mechi hizo za kesho kwani hata wao wanazihitaji pointi tatu toka kwa vigogo hao.
Msemaji wa Ruvu Masau Bwire na Kocha wa Prisonsa, David Mwamaja walisema kwa nyakti tofauti kuwa wanahitaji ushindi kuliko kitu kingine katika mechi hizo za kesho kwa lengo la kujiweka katika nafasi nzuri ndani ya ligi hiyo iliyoanza  kushika kasi kwa mechi za duru la pili.

Bingwa wa FDL kujulikana J2 Taifa

http://shaffihdauda.co.tz/wp-content/uploads/2015/01/DSC_4165.jpg
Mwadui Shinyanga
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhX4CPi_gLzDiNDFJxODqQK-bun_Lz_-fqogmOSBafonpNyQztxKsciMrA9kx7T2CAkfa14juJT5WVK1BxZPxkqTuD40uPWHMTtpatpKUHMvQpdWau2Aw3yYJfbYrgwYFAnwHWaIEFpT7c/s1600/sports.JPG
Aficans Sports 'Wana Kimanumanu
KLABU za African Sports  ya Tanga na Mwadui FC ya Shinyanga zinatarajiwa kucheza mchezo wa fainali  kusaka Bingwa wa Ligi Daraja la Kwanza (FDL) siku ya Jumapili kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
African Sports waliibuka washindi wa kwanza katika Kundi A, na Mwadui FC washindi wa kwanza Kundi B watacheza mchezo huo wa fainali ambapo Bingwa atapewa zawadi ya Kombe na medali, hali kadhalika kwa msindi wa pili.
Akizungumza na waandishi wa habari jana Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) Baraka Kizuguto alisema kwa mujibu wa Kanuni, ni lazima apatikane mshindi mmoja ambaye ni bingwa.
“Ligi Daraja la Kwanza (FDL) ilimalizika mwishoni mwa wiki kwa timu nne kupanda Ligi Kuu kwa kila kundi kutoa timu mbili, Kundi A ni African Sports na Majimaji FC, Kundi B ni timu za Mwadui FC na Toto Africans,”alisema.
Alisema  timu za Green Worriors na Villa Squad zimeteremka  Daraja la pili baada ya kushika nafasi za mwisho kwenye msimamo wa Ligi Daraja la Kwanza, Villa Squad kutoka Kundi A na Green Warriors Kundi B.
Katika hatua nyingine, Rais wa TFF  Jamal Malinzi ametuma salamu za pongezi kwa Wenyekiti wa klabu ya African Sports (Tanga) , Majimaji (Ruvuma),  Mwadui (Shinyanga) na Toto Africans ya Mwanza kwa timu zao kupanda Ligi Kuu ya Vodacom (VPL).
 Katika salamu zake  Malinzi alisema klabu hizo zinapaswa kujipanga na kufanya maandalizi kwa ajili ya msimu mpya wa Ligi Kuu ya Vodacom 2015/2016, kwani VPL ni ngumu kutokana na timu zote kuwa na ushindani mkubwa wa kutafuta matokeo mazuri kuepeuka kushuka daraja.
 Kwa niaba ya TFF, familia ya mpira na watanzania kwa ujumla wanawapa pongezi timu za African Sports, Majimaji, Mwadui na Toto Africans kwa kupanda Ligi Kuu ya Vodacom na kuwatakia maandalizi mema ya VPL 2015/2016,” alisema.

KWA UCHAFU HUU ELIMU TANZANIA ITAPANDA KWELI?!



Haifahamiki ni wanafunzi wa shule gani ya Sekondari, lakini hii ni taswira ya kitu gani kinachoendelea katika shule zenu nyingi na sababu ya kupatikana kwa division ziro lukuki

Rais wa FIFA alaani ubaguzi wa mashabiki wa Chelsea

http://i.telegraph.co.uk/multimedia/archive/02939/sepp-blatter_2939007b.jpg
Rais wa FIFA, Sepp Blatter aliyekerwa na kitendo chga kibaguzi kilichofanywa na amshabiki wa Chelsea dhidi ya mtu mweusi mjini Paris.
PARIS, Ufaransa
RAIS wa Shirikisho la Kimataifa la Soka Sepp Blatter amewalaumu mashabiki wa klabu ya Chelsea, kwa kitendo chao cha kumzuia mtu mweusi kuingia ndani ya treni huku wakiimba nyimbo za kibaguzi jijini hapa.
Blatter amelaaini kitendo hicho kilichofanywa na baadhi ya mashabiki hao wa Chelsea cha ubaguzi wa rangi dhidi ya mtu huyo mweusi na kumzuia kuingia katika treni jana Jumanne.
Baadhi ya mashabiki wa Chelsea wameonekana katika mkanda wa video wakizuia mlango wa treni kabla hawajamsukuma mtu huyo huku wakiimba nyimbo za kibaguzi: 
"Sisi wabaguzi, sisi wabaguzi na hicho ndicho tunachokitaka."
Tukio hilo lilitokea baada ya mchezo wa Ligi ya Mabingwa wa Ulaya uliofanyika jijini hapa na Chelsea kutoka sare ya kufungana bao 1-1 na Paris Saint-Germain kwenye uwanja wa Parc des Princes, huku klabu hiyo ikijibu haraka kuwa kitendo hicho sio cha kiungwana.
Ni wiki moja tu baada ya kocha wa zamani wa AC Milan Milan Arrigo Sacchi kutoa kauli kuwa "kuna weusi wengi" katika ligi ya vijana ya Italia, ambapo Blatter akijibu matukio yote hayo katika mtanda wake wa kijamii wa Twitter.
Matukio ya kibaguzi katika michezo yamekuwa kama ugonjwa sugu, huku adhabu dhidi ya wahusika yakielezwa kuruhusu kuendelea kuyahamasisha.

Jeshi Nigeria ladai kuua Boko Haram 300

http://d.ibtimes.co.uk/en/full/1418176/nigeria-boko-haram-2000-feared-killed-after-baga-attacked-second-time-days.png
baadhi ya wapiganaji wa Boko haram wakiwa 'kamili' na zana zao
ABUJA, Nigeria
ZAIDI ya wanamgambo 300 wa kundi la Boko Haram wameuawa katika zoezi la kijeshi huko Kaskazini-Mashariki ya Nigeria, limesema jeshi la Nigeria.
Baadhi ya askari wamekamatwa na silaha kadhaa zimeharibiwa, alisema msemaji wa jeshi hilo, Chris Olukolade.
Pia katika tukio hilo askari wawili walipoteza maisha yao na wengine 10 walijeruhiwa wakati wa zoezi hilo la siku mbili huko katika jimbo la Borno, aliongeza.
Hatahivyo, vifo hivyo havijathibitishwa.
Jeshi la Nigeria lilituhumiwa katika siku zilizopita kuwa limekuwa likitoa taarifa za uongo kuhusu kujeruhiwa kwa maadui.
Boko Haram wamevamia raia huku wakiwaua maelfu wa askari tangu kundi hilo lianzishe vurugu kwa ajili ya kuanzisha taifa lao la kiislamu mwaka 2008.
Nigeria, Chad, Cameroon na Niger hivi karibuni vimeunda jeshi la muungano na kudai kuwa limekuwa likifanya vizuri dhidi ya Boko Haramu.
Tisho la kundi hilo linaelezwa ndiyo sababu ya kuahirishwa kwa Uchaguzi Mkuu wa nchini huo uliokuwa ufanyike Jumamosi iliyopita na kupelekwa mbele hadi majuma sita yaani Machi 28.

Rooney aomba radhi kwa kujirusha

http://a2.fssta.com/content/dam/fsdigital/fscom/Soccer/images/2015/02/18/021815-Soccer-Manchester-United-Rooney-PI-CD.vadapt.620.high.0.jpgGOLIKIPA wa klabu ya Preston, Thorsten Stuckmann amesema Wayme Rooney alimuomba radhi kwa jinsi alivyodanganya na kupata penati katika mchezo wao dhidi ya Manchester United waliofungwa mabao 3-1. Rooney alianguka katika eneo la hatari baada ya kile kilichoonekana kama kuguswa na Stuckmann. Stuckmann alikaririwa na gazeti la The Sun akidai kuwa Rooney alimfuata na kumuomba radhi kwani ilikuwa nafasi yake ya kupata penati na alilazimika kuitumia.
Nyota huyo wa kimataifa wa Uingereza alifunga penati hiyo na kuihakikishia nafasi United ya kucheza hatua ya robo fainali ya michuano ya Kombe la FA dhidi ya Arsenal.
Kitendo hicho cha Rooney kilizua mjadala mkubwa miongoni mwa wachambuzi wa soka lakini aliungwa mkono na kocha wa timu ya taifa ya nchi hiyo Roy Hodgson na mchezaji mwenzake wa zamani Phil Neville ambao walidai alijirusha ili kumkwepa golikipa.
Stuckmann mwenye umri wa miaka 33 amesema suala hilo liko wazi kuwa ile haikuwa penati lakini walipewa kwa sababu wenyewe ni United na kama ingekuwa mchezaji wao ndiye angefanya vile hadhani kama angepewa mkwaju huo.

Copy and WIN : http://bit.ly/copynwin

Mourinho akiri sare ilikuwa kama zali kwa PSG

http://images.dailystar-uk.co.uk/dynamic/58/photos/879000/161879.jpg
Kipa aliyeibeba Chelsea jana ugenini dhidi ya PSG
MENEJA wa klabu ya Chelsea, Jose Mourinho amekiri kikosi cha kilikuwa na bahati kupata sare ya bao 1-1 katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya hatua ya timu 16 bora dhidi ya Paris Saint-Germain. 
Katika mchezo huo Branislav Ivanovic ndiye aliyeifungia Chelsea bao la kuongoza kabla ya Edinson Cavani hajasawazisha. 
Akihojiwa mara baada ya mchezo huo, Mourinho amesema ukiona jinsi golikipa wake Thibaut Courtois alivyokuwa akiokoa michomo mingi ya wapinzani hakuna shaka kuwa ilikuwa bahati kwao kuibuka na ushindi. 
Mourinho amesema sasa karata iko upande wao kwani mchezo huo utaamuliwa katika Uwanja wa Stamford Bridge baada ya wiki mbili zijazo.

Rais Kikwete apangua Ma-DC, Mwakalebela, Kisu waula!

https://pamelamollel.files.wordpress.com/2013/02/frederick-mwakalebela.jpg
Mwakalebela

http://www.thehabari.com/wp-content/uploads/2011/12/kiss.jpg
Shaaban Kissu (kulia)

Na Rahim Junior, Dodoma 
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk Jakaya Kikwete ameendelea kufanya panga pangua katika serikali yake baada ya kufanya mabadiliko ya Wakuu wa Wilaya kwa kuwateua Ma-DC wapya 27, kuwahamisha vituo vya kazi 64 na wengine 42 amewabakisha kwenye vituo vyao vya awali.
Akizungumza na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa Ofisi ya Waziri Mkuu-TAMISEMI, leo mchana, Waziri Mkuu Mizengo Pinda amesema mabadiliko hayo yamesababishwa na kuwepo kwa nafasi wazi 27 ambazo zilitokana na wakuu wa wilaya watatu kufariki dunia; kupandishwa cheo wakuu wa wilaya watano, kupangiwa majukumu mengine wakuu wa wilaya saba na kutenguliwa kwa uteuzi wa wakuu wa wilaya 12.
Hata hivyo, Waziri Mkuu alisema, Rais  Kikwete amewabadilisha vituo vya kazi wakuu wa wilaya 64 na kuwabakiza kwenye vituo vyao vya zamani wakuu wa wilaya 42.
Wakuu wa Wilaya wapya 27 walioteuliwa ni; Mariam Ramadhani Mtima anayeenda Ruangwa; Dk. Jasmine B. Tiisike anayeenda Mpwapwa; Pololeti Mgema (Nachingwea); Fadhili Nkurlu anayeenda Misenyi; Felix Jackson Lyaniva anayeenda Rorya na Katibu Mkuu wa zamani wa TFF, Fredrick Wilfred Mwakalebela anayeenda wilaya ya Wanging’ombe.
Wengine na vituo vyao kwenye mabano ni Zainab Rajab Mbussi (Rungwe); Francis K. Mwonga (Bahi); Kanali Kimiang’ombe Samwel Nzoka (Kiteto), Husna Rajab Msangi (Handeni), Emmanuel J. Uhaula (Tandahimba); Mboni Mhita (Mufindi); Hashim S. Mgandilwa (Ngorongoro); Mariam M. Juma (Lushoto); Thea Medard Ntara (Kyela); Ahmad H. Nammohe (Mbozi); Mtangazaji wa TBC, Shaaban Kissu (Kondoa) na Stephen Zelothe (Musoma).
Wengine ni Pili Moshi (Kwimba); Mahmoud A. Kambona (Simanjiro); Glorius B. Luoga (Tarime); Zainab R. Telack (Sengerema); Bernard Nduta (Masasi); Zuhura Mustafa Ally (Uyui); Paulo Makonda (Kinondoni); Mwajuma Nyiruka (Misungwi) na na Maftah Ally Mohamed (Serengeti).
Waliotenguliwa uteuzi wao lakini watapangiwa majukumu mengine ni'; Brig. Jenerali Cosmas Kayombo aliyekuwa Simanjiro; Kanali Ngemela E. Lubinga (aliyekuwa Mlele); Juma S. Madaha (aliyekuwa Ludewa); Mercy E. Silla (aliyekuwa Mkuranga); Ahmed R. Kipozi (aliyekuwa Bagamoyo); Mrisho Gambo (aliyekuwa Korogwe) na Elinas A. Pallangyo (aliyekuwa Rombo).
Waziri Mkuu pia aliwataja Wakuu wa Wilaya 12 ambao uteuzi wao umetenguliwa kutokana na sababu za umri, kiafya na kuimarisha utendaji Serikaini na wilaya zao kwenye mabano kuwa; ni James K. Ole Millya (Longido); Elias Wawa Lali (Ngorongoro); Alfred Ernest Msovella (Kongwa); Danhi Beatus Makanga (Kasulu); Fatma Losindilo Kimario (Kisarawe); Elibariki E. Kingu (Igunga); Dk. Leticia Moses Warioba (Iringa); Evarista N. Kalalu (Mufindi); Abihudi M. Saideya (Momba); Martha J. Umbulla (Kiteto); Khalid J. Mandia (Babati) na Elias Goroi (Rorya).

Monday, February 16, 2015

Polisi Zanzibar, KMKM yaendeleza uteja Afrika

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi59R0MYcrxWHLeSNnC_vM50rvpo6pW4S079-xz073BM1qMzHu78BZ3M2A6-Rcffg0AKuCNlGJTx77XuEspNUQTYpSZxeIwClivBXmTswWbLyuGBKDZoXuu3mnXKpUwrCIZ62qjbxpxVhkw/s640/4.jpg
KMKM waliokufa 2-0 Sudan
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiLCWb5BqldkVTcFvaO8san-9Nhbw4RdsAVAbuN1u3556K_TvVv67OvOYjoXCPZ7VpusnafOOpJiS6SLaDK-7wNEixcgcnDUbt54qaR2jof0UEU-xKJdBd0IUmCqdrNsyokdr0MSy0kmIY/s1600/IMG_3886.JPG
Polisi waliopigwa 'mkono' nchini Gabon
WAKATI wawakilishi wa Tanzania Bara, Azam na Yanga wakiwapa raha mashabiki wao, KMKM na Polisi Zanzibar zimeendelea kuwasononesha mashabiki wa soka wa visiwa hivyo baada ya kugeuzwa 'urojo' katika mechi zao za kimataifa zilizochezwa mwishoni mwa wiki.
Polisi wanaoiwakilisha Zanzibar kwenye Kombe la Shirikisho Afrika kama Yanga, ilikutana na kipigo cha mabao 5-0 toka kwa Moumana ya Gabon wakati mabingwa wa visiwani, KMKM wakilala 2-0 nchini Sudan kwa Al Hilal na kujiweka katika mazingira magumu ya kusonga mbele kwenye michuano hiyo.
Tangu Zanzibar ilipopata uanachama wa Shirikisho la Soka Afrika CAF, 2004, imekuwa ikifanya vibaya kwenye uwakilishi wa klabu kwa timu zao kuondolewa hatua za awali.
KMKM na Polisi maarufu kama Wazee wa Tunisia' watakuwa na mtihani mgumu swa na kupanda mlima mrefu kuweza kuzitoa Mounana na Al Hilal katika mechi zao za marudiano wakati wakiwa nyumbani.
Hiyo ni tofauti na wawakilishi wa Tanzania Bara, Yanga na Azam wenye kazi nyepesi kwenye mechi zao za marudiano wiki mbili zijazo ugenini dhidi ya timu za BDF XI ya Botswana na El Merreikh ya Sudan.
Yanga ilianza kwa kuizabua BDF kwa mabao 2-0 juzi kwenye Kombe la Shirikisho, kabla ya Azam kufuata mkumbo huo kwa kuilaza El Merreikh kwa idadi kama hiyo jana kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika.
Matokeo mengine ya michuano ya hiyo ya Ligi ya Mabingwa Afrika yapo hivi;
Al Ahli Tripoli     1 - 0     Smouha
COB     2 - 0     Moghreb Tétouan        
Raja Casablanca     4 - 0     Diables Noirs
St Michel United     1 - 1     Mamelodi Sundowns       
KCCA     1 - 0     Cosmos de Bafia        
Gor Mahia     1 - 0     CNaPS Sport        
Al-Malakia     0 - 2     Kano Pillars  
Recreativo do Libolo  3 - 1     Sanga Balende      

Mangasport     1 - 0     Bantu         
LLB Académic     0 - 0     Kabuscorp        
Séwé Sport     1 - 2     Kaloum Star
Real de Banjul     1 - 1     BYC
Pikine     1 - 0     Etoile Filante
MC El Eulma     1 - 0     Kedus Giorgis
Kaizer Chiefs     2 - 1     Township Rollers
Fomboni Club     0 - 1     Big Bullets
Azam     2 - 0     Al Merreikh 
Enyimba     3 - 0     Buffles de Borgou
Liga Muçulmana     0 - 0     APR
Mbabane Swallows     1 - 1     ZESCO United
USM Alger     3 - 0     Foullah Edifice
Al Hilal Omdurman     2 - 0     KMKM
Matokeo ya Kombe la Shirikisho Afrika;
Al-Ghazal     0 - 1     Petrojet
URA     3 - 2     Elgeco Plus
Benfica Luanda     2 - 0     Le Messager Ngozi
RSB Berkane     2 - 1     Onze Créateurs
Petite Rivièr…     1 - 2     Ferroviário Beira
Côte d'Or     2 - 3     Dedebit
RC Bobo-Dioulasso     0 - 1     Warri Wolves
Volcan Club     0 - 1     Petro de Luanda
Young Africans     2 - 0     BDF XI
Panthère     0 - 1     Rayon Sports
MC Alger     0 - 0     Sahel 
Leones Vegetar…     1 - 0     Dolphins
Étoile du Congo     1 - 2     FC MK
BV Wits     3 - 0     Royal Leopards
Khartoum 3     1 - 0     Power Dynamos
Sofapaka     1 - 2     Platinum
Al-Ittihad     6 - 1     Elect-Sport
Unisport Bafang     1 - 0     Olympique Ngor
Mounana     5 - 0     Polisi
Hearts of Oak     1 - 0     Police
Togo Port     2 - 0     CARA Brazzaville
ASO Chlef     2 - 0     Kamboi Eagles
Horoya     1 - 0     Fassell

Sikiliza ngoma mpya ya Shaa iitwayo For You


KOCHA JULIO AWAUMBUA WALIOMBEZA

Kocha jamhuri Kihwelu 'Julio'
KOCHA Jamhuri Kihwelu 'Julio' ni maarufu kwa kuwa mzungumzaji na mtu mwenye tambo nyingi zinazokera, lakini kwa kitendo alichofanya cha kuipandisha Ligi Kuu timu ya Mwadui Shinyanga mwaka mmoja baada ya kubaniwa na TFF ni kama amewaumbua wabaya wake.
Waliombeza na kumtimua ndani ya Simba katikati ya msimu uliopita wakati Simba ikiwa nafasi ya nne pamoja na bosi wake Abdallah Kibadeni 'King' huenda sasa wakatafuta mahali pa kuficha sura zao kwa aibu baada ya Julio kufanya kweli kwa kuirejesha Mwadui Ligi Kuu baada ya miaka zaidi ya 30 tangu ishuke daraja.
Msimu uliopita mara baada ya kutemwa na Simba, Julio alipewa mikoba ya kuinoa timu hiyo na kumaliza vinara wa kundi lao na kuonekana kama wamepanda daraja kabla ya TFF kuwaengua kutokana na rufaa ya JKT Kanembwa kuwaacha nafasi ya tatu nma ya pili ikitwaliwa na Stand United kama utani.
Kocha huyo aliyewahi kutamba na klabu mbalimbali ikiwamo Pilsner na Simba na timu ya taifa, akiwa mmoja wa mabeki mahiri wa kati, hakukata tamaa na badala yake alisuka kikosi chake na kuwezesha kupata msimu huu baada ya kumaliza kinara wa kundi lao wakifuatiwa na Toto Africans ambao nao wanarejea ligi chinio ya kocha John Tegete.
Akihojiwa mara baada ya kupata ushindi wa mabao 4-3, Julio alituma salamu zake kwa vigogo vya Ligi Kuu kuwa wajiandae kupata upinzani mkali msimu wa 2015-2016 kwani Mwadui haitacheza chini ya Nafasi ya Tatu Bora.
"Wajiandae tunakuja, tunajipanga kuhakikisha tunakuwa miongoni mwa timu Tatu Bora," alisema Julio hata ikiwa ligi yenyewe bado haijaanza.
Julio mmoja wa makocha wenye elimu ya juu ya ukocha na ambaye amekuwa akipata mafanikio licha ya utamaduni wa kupuuzwa kwa makocha wazalendo wanaotumiwa kama 'spea tairi' ameuthibitishia umma kwamba makocha Wazalendo wanaweza.
Mbali na kutwaa mataji kama mchezaji wa Simba, Julio pia ameshatwaa ubingwa wa Kombe la taifa kama kocha wa timu ya soka ya Ilala iliyoundwa na nyota wa Simba na Yanga kama ambavyo kikosi chake cha Mwadui kilivyoundwa na wakali wa timu hizo ambao walipigana na kuibeba kurudi Ligi Kuu msimu ujao.
MICHARAZO inampongeza Julio na timu yake sambamba na kuzipongeza timu zote nne za Majimaji Songea, Africans Sports na Totyo Africans kwa kurejea tena ligi kuu baada ya muda mrefu kuwa nje ya lifgi hiyo kubwa nchini.
Jambo la muhimu jipangeni mapema sasa ili msije mkainusa na kurejea tena ligi daraja la kwanza kama ambavyo imekuwa ikishuhudiwa kwa baadhi ya timu zinazopanda ligi hiyo na kudumu kwa msimu mmoja.

Yamoto Band kwenda kutumbuiza kwa Malkia Elizabeth II

Kundi la Yamoto Band
Bango la onyesho hilo la Yamoto kwa Malkia
KUNDI linalofanya vizuri katika muziki wa kizazi kipya nchini, Yamoto Band, linatarajiwa kwenda nchini Uingereza kwa ajili ya kutumbuiza.
Mkurugenzi wa kundi hilo, Said Fella, alisema Yamoto itaondoka nchini kesho kwa ajili ya kufanya onyesho lao siku ya Jumamosi.
Fella alisema onyesho lao litafanyika kwenye ukumbi wa Royal Regency, jijini London ikiwa ni mara ya kwanza kwa Yamoto kutua kwenye nchi hiyo ya Malkia.
Fella alisema ziara yao imeandaliwa na baadhi ya Watanzania wanaoishi Uingereza na taarifa walizonazo watafanya onyesho Februari 21 na kama kutakuwa na onyesho jingine la ziada watafahamu huko huko.
"Bendi itaondoka Febaruari 17 na onyesho litafanyika Februari 21 mjini London kwenye ukumbi wa Royal Regency," alisema Fella.
Kundi la Yamoto linaundwa na wasanii wanne wakali ambao ni Aslay, Maromboso, Enock Bella na Beka na limekuwa likitamba na nyimbo mbalimbali zikiwamo 'Yamoto', 'Nitajuta', 'Niseme', 'Tulia' na sasa wanatingisha na 'Nitakupwelepweta'

Shamsa Ford 'awauma' sikio wenzie, msikie...!

Kimwana Shamsa Ford
SHAMSA Ford ambaye ameufungua mwaka kwa kuuza sura ndani ya filamu ya 'Kudra' amewataka wasanii wenzake wa kike kujipanga mwaka 2015 ili kuhakikisha wanafika mbali kimataifa.
Shamsa anayejiandaa kupakua filamu yake mpya ya 'Mama Muuza' alisema kuwa mwaka 2015 uwe mwaka wa mipango kwa wasanii wa filamu nchini hasa wa kike kwa kuhakikisha wanakuwa namba moja badala ya kuridhika na nafasi walizonazo.
Mwanadada huyo alisema kwa upande wake amejipanga kuhakikisha anafanya kila jitihada ili kung'ara ikiwamo kunyakua tuzo kwa vile uwezo na sababu ya kufanya hivyo anayo.
"Ningependa kuwakumbusha wasanii wenzangu wa kike kuamka na kuufanya mwaka 2015 uwe wa mwaka wa mafanikio kwao, tujipange tuweze kuona tunatamba kimataifa," alisema.
Shamsa aliyekimbiza mwaka jana kupitia filamu kadhaa ikiwamo 'Hukumu ya Ndoa Yangu' na ile yake ya 'Chausiku', alisema imefika wakati wasanii nchini waelekeze nguvu zao kwenye soko la kimataifa badala na kuridhika na mafanikio ya nyumbani

Sikiliza ngoma mpya ya Diamond f P Square

Diamond

Sunday, February 15, 2015

Kagera Sugar wazipumulia Azam, Yanga

http://api.ning.com/files/cPakA0chAEyfyqjZRP3k2djpZ9GyxNW23W69D7FY4fYhsuNz2vmH6gr7yEITcci18IdnTvIgOej4xydmYu8LtJiXW0uQDhCL/16.jpg
Kagera Sugar walioifyatua JKT Ruvu
BAO pekee la dakika ya 38 lililofungwa na kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga na Coastal Union, Atupele Green limeiwezesha Kagera Sugar kuichapa JKT Ruvu na kuchupa hadi nafasi ya tatu ikizipumulia timu za Azam na Yanga zinazoongoza msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.
Kagera ilipata ushindi huo kwenye uwanja wa Kambarage-Shinyanga baada ya kuilaza maafande hao wa JKT kwa bao 1-0.
Ushindi huo ni wa pili mfululizo kwa timu hiyo kwenye uwanja huo tangu walipohamia wakitokea CCM Kirumba walipokuwa wakiambulia vipigo mfululizo.
Kwa ushindi huo Kagera imefikisha pointi 21 na kushika nafasi ya tatu, pointi nne nyuma ya Azam na Yanga wanaongoza wakiwa na pointi 25 ingawa timu hizo mbili zina michezo miwili mikononi zaidi ya Kagera.
Kagera wenyewe wamecheza michezo 15 wakati Azam na Yanga wamecheza mechi 13 tu ingawa katikati ya wiki hii watakuwa viwanja kucheza viporo vyao.
Simba wamechupa nafasi ya nne baada ya kuisulubu Polisi Moro mabao 2-0 uwanja wa Jamhuri Morogoro kwa kufikisha pointi 20 baada ya mechi 14.
MSIMAMO LIGI KUU TZ BARA 2014-2015
                              P   W   D    L    F    A   GD  Pts
01.  Yanga              13  07  04  02  15  07  08   25
02.  Azam               13  07  04  02  22  12  10   25
03. Kagera Sugar    15  05  06  04  12  11  01   21
04. Simba               14  04  08  02  15  11  04   20
05. Mtibwa Sugar    14  04  07  03  15  14  01   19
06. Polisi Moro        15  04  07  04  12  13   -1   19
07. Coastal Union   15  04  07  04  11   10  01   19
08. JKT Ruvu          15  05  04  06  14   15  -1   19
09. Ruvu Shooting  14  05  04  05  10   11  -1   19
10. Mbeya City       14  04  05  05   09   11  -2   17
11. Ndanda Fc        15  04  04  07   13   18  -5   16
12. Stand Utd         15  03  06  06   13   18  -5   15
13. Mgambo JKT     13  04  02  07   07   15  -8   14
14. Prisons             13  01  08   04   10   12  -2  11
Wafungaji:

 8- Didier Kavumbagu(Azam)
6-
Samuel Kamuntu (JKT Ruvu), Ame Ali (Mtibwa), Rashid Mandawa (Kagera Sugar)
 

5-Danny Mrwanda (Yanga), Kipre Tchetche (Azam)
 

4- Rama Salim (Coastal),  Simon Msuva (Yanga),  Emmanuel Okwi (Simba), Nassor Kapama (Ndanda), Heri Mohammed (Stand Utd)
 

3- Ally Shomari (Mtibwa),  Jacob Massawe (Ndanda),Frank Domayo (Azam), Malimi Busungu (Mgambo), Achidilele (Stand Utd), Atupele Green (Kagera)

Toto Afrika, Mwadui zarudi Ligi Kuu 2005-2016

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgaPRe88ZbguLMay9hq8z-MrwZbKRJuuDlKpnOd2wtCCvgsjqCFEWatffl7Dv95XsNWxsZcZutmnogqEcrMxCmWUYaFQlW7HdciyoGr9TrkJealnP3YNu3bp8bM8-sqrTXkYziW61qIkaiy/s1600/TFF+Toto+Africans.jpg
Toto Africans
http://taarifa.co.tz/wp-content/uploads/2015/01/DSC_4165.jpg
Mwadui Shinyanga waliopanda Ligi Kuu
TIMU za Toto Africans na Mwadui Shinyanga zimeungana na timu za Majimaji-Songea na Africans Sports kurejea Ligi Kuu Tanzania Bara msimu ujao baada ya kupata ushindi katika mechi zao za kufungia msimu wa Ligi Daraja la Kwanza Tanzania Bara zilizochezwa mikoa ya Mwanza na Shinyanga.
Toto ilipata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Rhino Rangers ya Tabora wakati Mwadui imeishindilia Burkina Faso kwa mabao 4-3 na kuungana na Majimaji Songea na Africans Sports zilizotangulia mapema kurejea ligi kuu.
Timu hizo zote nne zilizopanda daraja ziliwahi kucheza Ligi Kuu kwa nyakati tofauti, huku Majimaji na Africans Sports zikiwahi kuwa mabingwa miaka tofauti kabla ya kuporomoka hadi madaraja ya chini.

AZAM YAIFYATUA EL MERREIKH 2-0

Azam waliowapa raha Watanzania leo Chamazi
MABINGWA wa soka nchini Azam wameanza vyema michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya kuifumua El Merreikh ya Sudan kwa mabao 2-0 katika pambano la awali la mkondo wa kwanza lililochezwa uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam.
Ushindi huo umekuwa siku moja tu baada ya wawakilishi wengine wa Tanzania katika Kombe la Shirikisho Yanga, kupata ushindi kama huo dhidi ya BDF XI ya Botswana, shukrani zikienda kwa Mshambuliaji wa Kirundi, Amissi Tambwe aliyefunga mabao yote mawili katika kila kipindi jana.
Mabao ya washindi yalifungwa na Didier Kavumbagu na John Bocco Ádebayor' katika kila kipindi na kuifanya Azam kuendeleza rekodi yake katika michuano ya kimataifa kwa kutoruhusu kipigo katika uwanja wa nyumbani dhidi ya wapinzani wao.
Ushindi huo pia kumeiweka Azam katika nafasi nzuri kwa mechi ya marudiano wiki mbili zijazo, inagwa Azam haipaswi kubweteka kwa ushindi huo.

Simba yaifumua Polisi na kupaa 4 Bora

Simba waliotakata Jamhuri, Morogoro
Polisi Moro walionyoolewa leo uwanja wa nyumbani
MAGOLI mawili ya kila kipindi yameiwezesha Simba kuchupa toka maeneo ya chini na kuikamata nafasi ya nne ya msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara baada ya kuifunga Polisi Moro mabao 2-0 kwenye uwanja wa Jamhuri.
Goli la dakika ya 10 lililofungwa na Ibrahim Ajibu na jingine la kipindi cha pili l;a Elias Maguri aliyetumia uzembe wa kipa wa Polisi Tony Kavishe kutoka langoni bila umakini liliisaidia Simba kufikisha jumla ya pointi 20 na kukamata nafasi ya nne baada ya kitambo kirefu kulowea eneo la kati ya namba 8-10.
Katika pambano hilo, Simba iliwafunika kabisa Polisi Moro ambao ni hivi karibu ilitoka kuilaza Mbeya City waliyoinyuka Simba mabao 2-1 kabla ya kuwabana mabingwa watetezi Azam na kutoka nao sare ya 2-2.
Ushindi huo umepokelewa kwa furaha kubwa na mashabiki wa Simba ambao kwa muda mrefu walikuwa hawana furaha.
Kwenye pambano hilo Simba ilimpoteza kipa wake, Ivo Mapunda baada ya kuumia macho na kukimbizwa hospitalini kwa matibabu zaidi na nafasi yake kuchukuliwa na Peter Manyika Jr na kwa sasa klabu hiyo itakuwa ikianza mipango ya kuwafuata Stand United kwenye pambano lijalo mjini Shinyanga.
Katika hatua nyingine baadhi ya wanachama wanaodaiwa kuwa wa Simba Ukawa wamenaswa na POlisi mjini Morogoro baada ya kukamatwa wakitaka 'kuwanga''.

BREAKING NEWZZ! BABA WA DULLY SYKES AFARIKI DUNIA



BABA wa msanii nyota wa muziki wa kizazi kipya nchini, Dully Sykes, Mzee Ebby Sykes (63) amefariki dunia leo.

Kwa mujibu wa taarifa  ambazo MICHARAZO imezipata zinasema kuwa Mzee Sykes ambaye pi ni msanii wa muziki akiimba miondoko ya reggae na mingine alifariki leo mchana katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, Jijini Dar es Salaam.
Taarifa zaidi mtaletewa, ila MICHARAZO inampa pole Prince Dully Sykes na ndugu, jamaa na familia ya marehemu kwa msiba huo mzito kwa kukumbuka kuwa Kila Nafsi itaonja mauti.

Friday, February 13, 2015

VALENTINE DAY NI KITU GANI, JE UISHEREHEKEE?

KESHO baadhi ya watanzania wataingia kwenye mkumbo wa kusherehekea siku iliyobatizwa jina la 'Valentine Day' wakiitaja kama Siku ya Wapendanao.
Kwa hakika kwa Mcha Mungu ni haramu kwake kuiadhimisha sherehe hiyo kutokana na ukweli ni siku ya KIPAGANI na inayokinzana na MAFUNDISHO YA MUNGU MWENYEEZI iwe kwa Ukristo ama kwa Uislam.
Hata hivyo ni vema tuongelee kidogo nini maana ya Valentine kwa asili yake kisha kila mtu kwa IMANI  yake na mapana yake akatambua na kujiamulia kwa nafsi yake ama kukufuru au kumshukuru aliyemuumba.


Maneno hayo aliyoyasema Mtume Muhammad (SAW) hakika yamethibiti kwa sababu imedhihirika Waislamu kuigizia mila, desturi na tabia za makafiri na kuzisherehekea kama mfano siku hii inayoitwa 'Valentine day' (Siku ya Wapendanao).
Na baya zaidi na la kusikitisha sana ni kwamba sherehe hizi zinaenezwa katika njia mbali mbali za mawasiliano kama kutumiana kadi, barua pepe (e-mail), salamu katika simu za mkono. 
Hakika fitna hii humfanya Muislamu aharibu 'Aqiydah (Iymaan) yake kwa kudhani kuwa anafanya jambo la kawaida na hali ni jambo lisilo katika sheria ya dini yetu bali ni shirki kubwa na upotofu wa kufuata wanayoamini makafiri.
Na Mwenyezi Mungu anasema kuwa "Hawatakuwa Radhi Mayahudi na Manaswara kuwaona mpaka mfuate mila zao"
Baadhi ya Waislam na wasio waislam wapo kwenye harakati za kujiandaa na siku hiyo wajifuata mkumbo bila kujua kile wanachokisherehekea ebu tujifunze;
Historia Ya Sherehe Ya Siku Ya ValentineSherehe hii ya wapendanao ni sherehe ya wapagani  wa Kirumi wakati dini yao ya upagani ilikuwa ni dini iliyotapakaa kwa Warumi karne zaidi ya kumi na saba zilizopita.  
Na fikra zao ilikuwa ni kuelezea hisia ya 'mapenzi ya kiroho'
Kulikuwa na visasili (uongo) zilizohusishwa na sherehe hii ya upagani ya Warumi ambao umeendelea kutoka warithi wa Kikiristo. 

Miongoni mwa uongo huo ni kuamini kwao Warumi kuwa Romulus, aliyevumbua Rome, alinyonyeshwa siku moja na mbwa mwitu mwanamke, hivyo akampa nguvu na hikma.
Warumi walikuwa wakisherehekea tukio hili katikati ya Februari kila mwaka kwa kufanya sherehe kubwa. 

Na mojawapo ya tambiko katika sherehe hii ni kuchinja mbwa au mbuzi. 
Vijana wawili wenye nguvu hujipaka damu ya mbwa au ya mbuzi katika miili yao, kisha huiosha damu hiyo kwa maziwa. 
Baada ya hapo, watu hufanya gwaride wakiwa vijana hawa wawili wako mbele wakiongoza gwaride iliyokuwa ikitembea barabarani. 
Vijana hao wawili walikuwa wakichukua vipande vya ngozi ambavyo waliwapigia watu wanaowavuka. Wanawake wa kirumi walikuwa wakipokea mapigo hayo wakiamini kuwa yatawahifadhi na kutibu utasa.
 

Kufungamana kwa Mt. Valentine na Sherehe Hii

Mtakatifu Valentine (Saint Valentine) ni jina waliopewa mashujaa wawili wakongwe waliokufa ambao ni wana wa kanisa la kikiristo. 

Inasemekena kwamba walikuwa ni wawili au mmoja tu. 
Huyo mmoja alikufa Rome kutokana na mateso ya kiongozi wa Kigothi aliyeitwa Claudius. 
Kanisa la Saint Valentine lilijengwa kwa ajili ya kudumisha kumbukumbu yake.
Warumi walipoingia ukristo, wakaendelea kusherehekea sikukuu ya wapendanao (valentine day) lakini wakabadilisha kutoka fikra ya upagani ya 'mapenzi ya kiroho' (spiritual love) na kuleta fikra nyingine iliyojulikana kama ni 'mapenzi ya mashujaa' yaliyowakilishwa na Saint Valentine ambaye aliuliwa kwa ajili ya kutetea mapenzi na amani. 

Vile vile ikajulikana ni sikukuu ya wapenzi, na Saint Valentine alifanywa kuwa ni mlezi wa mapenzi ya mtakatifu.
Miongoni mwa imani yao inayoambatana na sherehe hii ni kwamba majina ya wasichana waliofika umri wa kuolewa yaliandikwa katika vikaratasi vidogo vilivyokunjwa mviringo kisha vikawekwa katika chombo juu ya meza. 

Kisha wavulana waliotaka kuoa waliitwa na kila mmoja huchagua karatasi moja ikiwa na jina la msichana. Kisha hujiambatanisha naye huyo msichana aliyempata kutokana na kura hiyo aliyochagua kwa muda wa mwaka ili wajuane vizuri kisha tena hufunga ndoa, au kama hawakuelewana hurudia tena kufanya kura inapofika siku hiyo mwaka unaofatia.  
Vile vile imesemekana kwamba chanzo cha sikukuu hii, ni kwamba warumi walipokuwa wakristo baada ya ukristo kutapakaa, Mfalme wa Kirumi Claudius II alitoa hukumu katika karne ya tatu kwamba askari wasioe kwa sababu kuoa kwao kutawashughulisha na vita walivyokuwa wakipigana. 

Hukumu hiyo ilipingwa na Saint Valentine ambaye alianzisha kuozesha maaskari kwa siri. 
Alipokuja kujua mfalme, alimfunga jela na akamhukumu kuuliwa. 
Huko jela akapendana na mtoto wa mkuu wa jela, lakini ikawa ni siri kwani kutokana na sheria ya ukristo, mapadri na makasisi wameharamishwa kuoa au kupenda.
Hata hivyo alipewa heshima yake na wakristo kwa sababu ya kushikilia na kujikita imara katika ukristo wakati mfalme alipotaka kumsamehe kwa sharti aache ukristo na kuabudu miungu ya Kirumi ili awe msiri wake na awe mkwe wake. 

Lakini Saint Valentine alikataa ahadi hiyo na akapendelea ukristo, kwa hiyo akauliwa siku ya tarehe 14 Februari 270 CE. 
Ndio ikaitwa siku hii kwa jina la huyo mtakatifu (Valentine).

Papa (Pope) naye akaifanya siku hiyo ya kufa Saint Valentine tarehe 14 Februari 270 CE kuwa ni sikukuu ya mapenzi. 

Na ni nani alikuwa Papa huyo? Ni Askofu mkuu wa kanisa la 'universal church', ambaye ni mrithi wa mtakatifu Peter.
Ndugu Waislamu tazameni vipi huyo askofu anavyohusika katika kuadhimisha sikukuu hii ambayo ni uzushi katika dini yao ya Kikiristo. 


Hii itukumbushe kauli ya Allaah
"Wamewafanya makuhani wao na wamonaki wao kuwa ni marabi badala ya Mwenyezi Mungu"At-Tawbah: 31

Matendo Yanayotakiwa Kujiepusha Katika Sikukuu Hii  
1- Kuonyeshana bashasha na furaha kama ilivyo katika sikukuu zao nyingine.
2-Kupeana mawaridi mekundu (Red Roses) ambayo ni alama ya kuelezea mapenzi, 'mapenzi ya kiroho' ya wapagani au 'mapenzi' ya Wakristo. Hivyo inajulikana kuwa ni 'Sikukuu Ya Wapendanao'.
3-Kupelekeana kadi. Na kadi nyingine zina picha za 'mungu wa mapenzi wa kirumi' ambaye ana mbawa mbili, akiwa amekamata upinde na mshale. Huyu ndio mungu wa mapenzi wa wapagani warumi. Shirk iliyoje hii ndugu Waislamu?
4-Kubadilishana maneno ya mapenzi na matamanio katika kadi wanazopelekeana, yakiwa katika mfumo wa kimashairi, tenzi na sentensi fupi fupi. 

Kadi nyingine zina picha za kimzaha na maneno ya kuchekesha, na mara nyingi zina maneno ya kusema 'Kuwa Valentine wangu'. 

Hii inaashiria maana ya kikiristo ya sikukuu hii baada ya kuwa asili yake ni kutokana na fikra za upagani.
5-Katika nchi nyingi za kimagharibi, hufanyika sherehe siku hiyo ambayo kunakuweko kuchanganyika wanaume na wanawake, kuimba, na kucheza dansi. Na wengi wanapelekeana zawadi kama mawaridi, maboksi ya chokoleti kwa wake zao, marafiki na wanaowapenda.
Kutokana na maelezo yote hayo ya chanzo cha sikukuu hii, tunaona kwamba siku hiyo haina uhusiano wowote katika Uislamu, bali yana uhusiano na washirikina mapagani, hata wakristo katika dini yao nao pia ni uzushi, sasa itakuwaje sisi Waislamu tuwaigize kusherehekea?
Basi ndugu Waislamu tutambue kuwa jambo hili ni ovu mno, haimpasi Muislamu kuharibu 'Aqiydah (iymaan) yake kwani kuna hatari kubwa kushiriki katika sherehe hii nayo ni kuingia katika kumshirikisha Allaah na kama tunavyojua kuwa Allaah Hamsamehe mtu anayefanya shirki pindi akifariki bila ya kutubu kama ilivyo katika aya ifuatayo:
"Hakika Mwenyezi Mungu Hasamehe kushirikishwa, na Husamehe yaliyo duni ya hilo kwa Amtakaye. Na anayemshirikisha Mwenyezi Mungu basi hakika amezua dhambi kubwa" (An-Nisaa: 48).
Hivyo ni kuharamishwa na Pepo na kupata makazi ya moto, tunajikinga na Allaah kwa hayo.
"Kwani anayemshirikisha Mwenyezi Mungu, hakika Mwenyezi Mungu Atamharimishia Pepo, na mahala pake ni Motoni. Na waliodhulumu hawatakuwa na wa kuwanusuru"-Al-Maaidah: 72.
Tunamuomba Allaah  Atuepushe na kila aina ya shirk na Atuonyeshe yaliyo ya haki tuyafuate, na yaliyo ya batili tujiepushe nayo na Atuajaalie ni miongoni mwa wale wanaosikiliza kauli (nyingi) wakafuata zile zilizo njema.  Aamiyn

Special Al Hidaya

Copy and WIN : http://bit.ly/copynwin
Friday, 13 February 2015 VALENTINE NI NINI? Leo nimeona niongelee kidogo nini maana ya Valentine kwa asili yake kisha kila mtu kwa Imani yake na mapana yake akatambua kuwa anapokuwa sehemu ya Valentine Day anakuwa ana adhimisha nini na kwa sababu gani wengi tunasheherekea kama sio kuadhimisha Valetine Pasipo kujua asili yake. Valentine’s Day kama Sikukuu Ya Kipagani: Valentine’s Day si siku ya Sikuu ya Kikristo, hata kama jina lake asili yake inatokana na Ukristo haiwezi kuhalalisha sasa Valentine kuwa Siku Ya Kikristo. Tukiangalia suala sikukuu hii kwa jicho la tatu, hatuoni uhusiano mkubwa kati ya watu wa Mungu na Malove dove yaani mapenzi. Kuna mambo mengi yanaweza ibua mjadala na kutokuelewana miongoni mwa jamii ya wakristo na wasomi juu ya chimbuko ya Siku ya wapendanao al maarufu Valentine’s Day. Hatutaweza kamwe kuwa na uwezo wa kuwa na jibu muafaka kuhusu uhalali wa kusheherekea valentine kwa namna moja ama nyingine kutokana na tofauti za kitamaduni na kidini ili mwisho wa siku tujenga upya hadithi kamili na madhubuti, lakini uhusiano kipagani hadi sasa na nguvu zaidi kuliko wale wa Kikristo kwa namna yoyote ile. Februari 14 & Juno Fructifier au Juno Februata (February 14th & Juno Fructifier or Juno Februata) Enzi hizo Warumi walikuwa wakisheherekea kwa kupumzika kabisa kama sikukuu ya muungano ama sikukuu zozote za hapa bongo kila Februari 14 kama siku ya kutoa heshima kwa Juno Fructifier. Huyu Juno Fructifier alikuwa nani?huyu alikuwa Malkia wa miungu ya Kirumi ambaye alikuwa Mungu mke kama mmoja wapo wa miungu ya ndoa kama ndo zilikuwa zinasua sua basi tarehe 14 February ndo ilikuwa kama siku ya kufanya matambiko. Enzi hizoilikuwa Katika sherehe moja, wanawake walikuwa wakiwasilisha majina yao na kuweka kwenye kisanduku na baadae wanaume wangepita mbele ya kisanduku hicho na kila mmoja kujitwalia jina moja. Kilichokuwa kinatokea katika sherehe kila aliyejiokotea jina hulitaja na kujitwalia huyo mwanamke kuwa mwanandoa kwa muda wote wa sikukuu wakati mwingine ilikuwa ni mwanandoa wako kwa mwaka mzima mpaka Valentine nyingine akaweke jina pale kwenye kibox. Mila hii ilitumika kukuza Jamii ya Kirumi kwa maana ya uzazi na maisha mengine kwa ujumla, kasheshe kama ulibeba ile ya mwaka mzima then Valentine imefika kisha unataka kubadilisha halafu uliyembeba mwaka jana mjamzito tehe tehe imekula kwako. St Valentine, Padri Wa Kikristo (St. Valentine, Christian Priest) Kulingana na hadithi za zamani, Mfalme wa Kirumi mwenye jina Claudius II ilipiga marufuku juu ya ndoa kwa sababu enzi hizo vijana wengi walikuwa wakiojitwalia wake mapema ili kukimbia jeshi maana amri ilikuwa mtu ambaye hana mke hana familia ndo alikuwa anapaswa kuingia jeshini maana hana cha kupoteza yuko mwenyewe tuy tehe tehe. Sasa kuna Padri mmoja wa Kikristo aitwaye Valentinus yeye ndo alikuwa kazi yake kufungisha hizo harusi kisirisiri maana inaonekana walikiuwa wakimpoza na mwisho wa siku huyu padri akahukumiwa kunyongwa. Wakati akisubiri kunyongwa, Wapenzi Vijana (Couples) walimtembelea na kumwandikia kitu kama barua kama sio waraka kuwa ni namna gani ndo ni tamu kuliko Vita ya kwanza vya dunia na vya pili. Valentine Mwingine. Valentinus mwingine alikuwa Padri nae alifungwa jela kwa ajili ya kusaidia Wakristo. Wakati akiwa bado yuko jela huyu kuhani aka fall in love na binti mlinzi wa gereza na wakati karibu anakwenda kunyongwa akaandika ujumbe “From Your Valentine” . Habari zake zikahifadhiwa na kuripotiwa Papa Julius I na baadae alijenga nakshi nakshi juu ya kaburi lake. Wakristo Wajibinafsishia Valentine’s Day: Katika mwaka wa 469 wa kutawala kwake Gelasius alitangaza Februari 14 siku takatifu kwa heshima ya Valentinus tajwa hapo juu badala ya kuwa siku ya kipagani ya mungu Lupercus wa Kirumi. Hapa ndo Wakristo wa enzi hizo wakachakachua sikukuu hiyo na kuruhusu kuchukua baadhi ya maadhimisho ya siku ya mapendo na ngono ambapo awali mambo hayo yalikuwa katika mazingira ya upagani. Si ajabu kwenye Valentine hii ukaona Guest House zimejaa, madukani watu wananunua condom hawajui kuwa kuadhimisha huko hawajaanza wao ila ni zile imani za kipagani. Maadhimisho ya kipagani yalikuwa lazima yaitimishwe kwa tendo la ngono ili kuonesha kilele cha upendo. Na njia rahisi iliyokuwa ikitumika katika kusheherekea siku hii ni ile ya kuweka majina kwenye kibox kisha kilaini unajibebea huku “mungu” Shahidi akisimamia zoezi zima. Kwa maana ya kwamba hakuna mtu atakaye okota jina bahati mbaya kuna roho inayomuongoza mtu kuchagua jina fulani. Valentine Day Yageuka kuwa Siku Ya Wapendanao. Kama ambavyo tumeitazama siku ya Valentine wala haikuwa siku ya wapendanao ilikuwa sikukuu ya Kipagani, ila baadae ikachakachuliwa hapo ikawa ya Kikristo lakini ni kama upagani ndani yake. Ilipokuwa Wakati wa Uamsho kwente Karne ya 14 ambapo tamaduni zikaanza kupewa tena shamrashamra za Kitaifa, ndipo Valentine ikapewa shavu la kuwa siku ya wapendanao. Ndipo katika kipindi hiki watu wakaachana na makatazo ya kidini wakati huo na yale mafundisho ya msingi katika dini yakapewa kisogo na watu wakageukia matamanio yao.Nyaraka na nyimbo mbali mbali za kuhusu mapenzi, ngono na kujamiiana vikaenea katika kizazi hicho kama ilivyo sasa kila nyimbo ni mapenzi hata picha za mabango ya barabarani ni mapenzi kwenda mbele. Valentine na Kibiashara Zaidi. We utaona tu valentine hii ubepari unavyoshika hatamu yake katika kutumia ili tu “Wapenzi” Wakolezee eti Valentine Day. Kuna watu watanunua nguo mpya nyekundu ili mradi tu watupie kitu chekundu, mijihela mingine itapelekwa kununulia zawadi za wapenzi, hapo sijahesabu maua yatakayonunuliwa siku ya valentine, hapo sijaongelea chakula cha usiku cha wapenzi, hapo sijaongelea wale watakao amua kwenda kulala. Kama kuna siku nzuri ya biashara basi Valentine inakaribiana na Christimas. Mtazamo Wangu na Valentine Za Kibongo. Nakubaliana na wale ambao siku hiyo watatumia kuwapongeza ndugu zao wazazi wao na wapenzi wao. Swali la kujiuliza hapa “tuna adhimisha” ama “tunasheherekea” Valentine?kama tuna adhimisha siku hii, lazima ujue unachoadhimisha, kipi kati yapo juu unachoadhimisha?kama unasheherekea unashehereka nini?otherwise tunakuwa busy na sikukuu tusiyoijua. Ukitaka lawama valentine we usinunue zawadi, usimtoe mtu dinner, jikaushe kama jumanne zingine tu za kawaida. Kwa Mtazamo wangu mdogo nimebaini “Valentine Day” Wanawake ndo wako excited nayo kuliko Wanaume. Kwanini?Kwa wale wanaume wasio waaminifu siku hiyo wengi hu opt kupumzika nyumbani ili kuondoa lawama. How?Unajua wanaume wengi ndio wanao cheat sasa anapotaka kwenda outing anajua msala unaweza kutokea. Ila kwa wale wanao tazamia kusheherekea ama kuadhimisha siku hii kwa namna yoyote ile basi nina wasiwasi wa baadhi ya watu kukimbiwa kidizaini siku hii, na wengi pasipo kujua kuwa kuna roho nyuma yake watajikuta wakiadhimisha kwa ngono kama ishara ya upendo kumbe ni ile ibada ya kipagani tuliyoisoma hapo juu. Abiria chunga mzigo wako kwenye Valentine. Swali la Kujiuliza Kuna madhara yoyote ya Mkristo kusheherekea Sikukuu Ya Valentine? SPECIAL THANKS TO SAM SASALI. Posted by Sophia Mbeyu at 00:36 Email ThisBlogThis!Share to TwitterShare to FacebookShare to Pinterest No comments: Post a Comment Links to this post Create a Link Older Post Home Translate Powered by Translate PLACE YOUR ADS HERE PLACE YOUR ADS HERE TANGAZO: UNAHITAJI VIATU WASILIANA NASI HAPA TANGAZO: UNAHITAJI VIATU WASILIANA NASI HAPA UNAHITAJI BOFYA PICHA HII KUONA PICHA ZAIDI About Me My Photo Sophia Mbeyu View my complete profile Blog Archive Popular Posts MATOKEO YA DARASA LA SABA MWAKA 2014 YAMETOKA, INGIA HUMU KUONA DK. CHARLES E. MSOND E AKITANGAZA MATOKEO YA DARASA LA SABA MAPEMA HII LEO OFISINI KWAKE,MSONDA AMESEMA MATOKEO YA MWAKA HUU UFAURU WAKE ... MITINDO YA VITENGE KWA WANAWAKE NA WANAUME... KAMA INAVYYONYESHA PICHA! VAZI LAKITENGE LAWEZA KUTUMIWA KAMA VAZI LA OFISI AMA CASUAL SIO LAZIMA KITENGE KIWE N... MITINDO YA VITENGE KWA WOTE,.... WADAU WA VITENGE KILA WIKI KUNA POST YA VITENGE FUATILIA POST ZA NYUMA KUPATA MITINDO MBALIMBALI ZAIDI... MITINDO YA VITENGE KWA AKINA DADA NA WATOTO.. MITINDO YA VITENGE Mitindo ya Vitenge inaweza kushonwa katika dizain mbalimbali, hii inaonyesha mitindo kwa vijana ni katika kuonyesha kuwa kitenge si lazima ... MITINDO BOMBA YA VITENGE! Huhitaji nguo za majina kupendeza, kitu cha kitenge tosha kabisa kukutoa bomba! MITINDO MBALIMBALI YA VITENGE, VIATU NA HANDBAG ZA KITENGE.... MITINDO YA VITENGE KWA AKINA DADA NA WATOTO! MITINDO YA VITENGE KATIKA MATUKIO TOFAUTI... MITINDO YA VITENGE Labels African day 2008 may AMUUA BABA YAKE KUMUOKOA SHANGAZI YAKE ALIYEKUWA ANABAKWA- NACHINGWEA ARIEL SHARON AFARIKI ASEMA YADHOOFISHA UCHUMI AFRIKA aswira Kutoka Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar:Rais wa Comoro Awasili Zanzibar Kuhudhuria Maadhimisho ya Sherehe za Miaka 50 ya Mapinduzi BAADA YA BASI KUGONGA NA KUUA WATATU BABA NA MWANA JAY-Z NA MWANAE BLUE IVY.. Biza mupulu artist Biza mupulu Botswana BREAKING NEWS: FIFA YAHAMISHA MUDA WA KOMBE LA DUNIA MWAKA 2022 HUKO QATAR HABARI ZA KIMATAIFA/ WAUMINI WAUAWA MSIKITINI NCHINI NIGERIA HABARI ZA UMBEYA/. WAKATI WEMA AKITUMA VIDEO YA DIAMOND AKIWA KITANDANI HAKUNA KAMA MWANAMKE HAPO NAPO SASA IGP ATANGAZA MABADILIKO MAKUBWA JESHI LA POLISI. IJUMAA NJEMA WADAU WA SOPHIEMBEYU BLOG.... IMETANGAZWA RASMI KESHO NI SIKU YA MAPUMZIKO KUSHEHEREKEA MAPINDUZI: Kundi la FM Academia KUTWAA TUZO YA MWANASOKA BORA WA AFRIKA NJE YA AFRIKA Machael Jackson kuaga dunia MADAWA YA KULEVYA YAINGIZWA SUPERMARKET KATIKA MAKASHA YA NDIZI MAGAZETI YA LEO IJUMAA 10 JANUARY 2014 Magonjwa ya mlipuko yanukia jijini Dar MAN UNITED YAZINDUKA Mariam bongo MAWAZIRI WAPYA WATANO WATAJWA TANZANIA MITINDO YA NYWELE MITINDO YA VITENGE MKAPA AIPONDA MISAADA KUTOKA NJE MSIKIE JOKATE AKIONGELEA MUZIKI NA FILAMU....... Mwekezaji abomoa nyumba za wananchi wa Mkuyuni-Morogoro ili kupisha ujenzi wa Majosho.11 jan mgogoro Nondoz wa Bongo waliokamilisha kisomo chao Data India. Pablo Machine Familia dar Pablo Machine na watoto Pablo Machine na wakenya kwenye festival Pablo Machine Sabiti PENNY NAE ANENA "HAITATOKEA KAMWE NIKAMDHARAU DIAMOND PICHA ZA WATUHUMIWA WALIOKAMATWA WAKISAFIRISHA SILAHA ZA KIVITA KATAVI PICTURE OF THE DAY..KWA RAHA ZAO Rais wa Zanzibar Dr Ali Shein Aendelea Kutunuku Nishani Rihanna out in Barbados RWANDA YAKANUSHA UVUMI KUHUSU KIFO CHA KAGAME SABABU YA KIFO CHA MPENDWA WETU ZAINAB BUZOHERA TASWIRA MBALI MBALI KATIKA SHEREHE YA MIAKA 50 YA MAPINDUZI ZANZIBAR LEO 12/01/2014 UNAKANDAMIZA ... VAZI LA LEO Wa Bongo WAFANYABIASHARA WA DAR WAGOMEA MASHINE ZA KODI ZA TRA WAFUNGA MADUKA LEO Wakali bongo hawo WANANCHI WALITEKETEZA BASI KWA MOTO WAZIRI KIGODA : MFUMO MASHINE EFDs NI MBOVU WEEKEND NJEMA WADAU WA SOPHIEMBEYU BLOG....NAWAPENDAAA MINGIIII. WEMA NI MAMA KIJACHO? SOMA ALICHOANDIKA HAPO Wizara ya maliasili na utalii imewasimamisha kazi watumishi wake 22 wa idara ya wanyama pori YAICHAPA 2-0 SWANSEA CITY Yatima Dar walilia madarasa yakujisomea PLACE YOUR ADS HERE PLACE YOUR ADS HERE powered by Slideshow Sikiliza clouds radio SIKILIZA KWANZA JAMII RADIO Followers Google+ Followers Total visitors Total Pageviews Sparkline 1515131 CLOCK & CALENDAR buy research paper custom essay writing answering service care February 2015 S M T W T F S 1 2 3 4 5 6 7 8 9 10 11 12 13 14 15 16 17 18 19 20 21 22 23 24 25 26 27 28 Free Counter Counter Free PLACE YOUR ADS HERE PLACE YOUR ADS HERE WEBSITES & BLOGS MICHUZI JIACHIE BONGOBLOGS TanzMED Wavuti Allyshams Myummah76 Francis Godwin Globalpublishers Full Shangwe Ladyjaydee Swahili TV TMF Haki Ngowi Mimi na Tanzania Mo Blog Chadema Blog CCM Blog January Makamba Zitto kabwe Habari Leo Daily News Mwananchi Mtanzania Tanzania Daima Raia Mwema Majira Mwanaspoti The Citizen Daraja Letu IPP Media Bashir Nkoromo BBC Swahili Sauti ya Amerika Jamii Forums BLOG DEVELOPMENT BLOG DEVELOPMENT AUDIO BAR SIKILIZA BRAND NEW TRACK HAPA!! VIDEO BAR UNATAKA KUPUNGUA UZITO!! CLICK THIS IMAGE Contact Form Name

Mume wa Bobby Kristina kizimbani adaiwa kumpiga

Bobby Kristina

Bopbby na mumewe Nick Gordon
NEW YORK, Marekani
MUME wa msanii Bobby Kristina, Nick Gordon, anatarajiwa kupandishwa kizimbani kujibu shitaka la makosa ya uzembe barabarani.
Pia mamalaka nchini hapa zinamchunguza kwa tuhuma za kumjeruhi, Bobbi Kristina ambaye ni mtoto wa mwanamuziki nguli wa zamani, Whitney Houston.
Marehemu Whiyney alizaa mtoto huyo na mwanamuziki mwingine mahiri, Boby Brown, ambaye ni gwiji wa kutumia dawa za kulevya.
Mahakama ya Fulton County State, leo inatarajia kutoa kibali cha kukamaktwa kwa Gordon iwapo atashindwa kuhudhuria kesi ya awali inayomkabili.
Mahakama hiyo inatarajia kutoa kibali hicho ikiwa ni wiki moja tangu Bobbi Kristina, alipokutwa amepoteza fahamu bafuni huku kichwa chake kikiwa ndani ya sinki lililokuwa limejaa maji.
Kwa mujibu wa uchunguzi wa awali, polisi wa mjini hapa wamesema wana imani Gordon alimjeruhi mkewe kabla ya kutokea tukio hilo.
Tayari polisi wameanza kuchunguza mienendo ya uhusiano wa wawili hao, kabla ya Bobbi Kristina, kukutwa na tukio hilo, Jumamosi wiki iliyopita.
Aidha, mamlaka ya kiuchunguzi zimedai wanandoa hao wamekuwa na historia ya kushambuliana ambapo dakika 15 kabla ya tukio hilo walinaswa wakiwa kwenye malumbano makali.
Max Lomas ambaye ni rafiki wa Bobbi Kristina, alidai Gordon alifuta damu katika eneo la tukio zinazosadikiwa kuwa za mkewe.
Lomas alidokeza kuwa alilazimika kuingia nyumbani kwa Bobbi Kristina, baada ya kugonga mlango kwa muda kabla ya kuingia ndani baada ya kukosa mtu wa kumfungulia na kumkuta rafiki yake akiwa amepoteza fahamu bafuni.
Waaguzi katika hospitali aliyolazwa msanii huyo wa vipindi vya televisheni, wanasema hali yake sio nzuri na mjomba wake ameandika kwenye mtandao wa Instagram kuwa hali ya mpwa wake haileti matumaini.
Mjomba huyo alisema madaktari walimwambia ajiandae kupokea taarifa yoyote kwa kuwa hakuna matumaini Bobbi Kristina, kuokoa uhai wake. 
Hatua ya kupoteza fahamu, Bobbi Kristina, limeushtua ulimwengu kwa kuwa linafanana na tukio la kifo cha Whitney aliyefariki Februari 12, 2012.
Whitney alikutwa amefariki bafuni katika Hoteli ya Beverly Hilton huku kichwa chake kikiwa ndani ya maji.
Katika tukio hilo, polisi walikuta chupa za pombe, vyeti vya hospitali vilivyokuwa vikionyesha kusumbuliwa na ugonjwa wa moyo na matumizi ya dawa za kulevya aina ya kokein.
Gordon na Bobby Kristina, walifunga ndoa Januari, mwaka jana licha ya ndoa hiyo kupingwa vikali na Bobby Brown kwa kuwa Godon ni mtoto wa kuasili wa Whitney.

Katika hatua nyingine imeelezwa kuwa mwanadada huyo ameanza kufumbua macho, ikiwa ni kwa mujibu wa shangazi yake.