TIMU ya soka ya Toto Afrika ya Mwanza jioni ya leo inatarajiwa kushuka dimba la CCM Kirumba, jijini humo kupepetana na wageni wao Abuja FC ya Nigeria katika pambano la kirafiki la kimataifa la kujiandaa na duru la pili la Ligi Kuu Tanzania Bara.
Pambano hilo la Mwanza ni kati ya mechi mbili zitakazochezwa baina ya timu hizo mbili ambazo zimeanzisha ushirikiano wa pamoja.
Kwa mujibu wa Katibu Mipango wa Toto, Hassani Kiraka, pambano jingine la timu hizo mbili litachezwa kesho kwenye dimba la Kambarage, mkoani Shinyanga.
Kiraka alisema, mbali na mechi hizo mbili kutumiwa na timu yao kukiandaa kikosi chao kwa ajili ya duru la pili litakaloanza Januari 21, pia zitatumiwa kukusanya fedha kwa za kuiwezesha Toto kushiriki vema ligi hiyo kutokana na kuwa na hali mbaya kiuchumi.
"Tunawahimiza mashabiki wa soka wa jijini Mwanza na Shinyanga ambao kwa muda mrefu hawajapata burudani ya kimataifa kujitokeza kwa wingi katika mechi hizo ikiwa sehemu yao ya kuichangia timu yetu, ili ishiriki vema katika duru lijalo," alisema Kiraka.
Alisema, uongozi wao umepania kuona Toto Afrika katika duru la pili, ikifanya vema tofauti na ilivyokuwa duru lililopita kwa nia ya kuiokoa timu yao isishuke daraja, ndio maana wameialika Abuja Fc ambayo wameanzisha ushirikiano wa pamoja baina yao.
Aliongeza, katika mechi hizo mbili benchi la ufundi la Toto lililopo chini ya John Tegete na msaidizi wake, Choki Abeid, watatafuta wachezaji wanne kutoka kikosi cha Abuja Fc, ili ikiwezekana mwakani wawasajili katika timu yao.
Toto iliyoanza duru la kwanza kwa makeke kabla ya kutetereka na kumaliza mzunguko huo ikiwa nafasi ya 11 katika msimamo wa ligi, katika kikosi chake inao nyota wawili wa Kinigeria, akiwemo kinara wao wa mabao, Enyima Darlington na Chika Chimaobi Chukwu.
Mwisho
STRIKA

USILIKOSE

Tuesday, December 27, 2011
Simba, Yanga zaumwa sikio

BEKI wa zamani wa timu za Ushirika-Moshi, Simba na Yanga, Willy Martin 'Gari Kubwa', amezitaka klabu za Simba na Yanga na kufanya maandalizi kwa vitendo badala ya maneno ili kujiandaa na mechi za kimataifa mwakani.
Aidha amelitaka Shirikisho la Soka Tanzania, TFF, kumsaidia kocha Jan Poulsen wa Taifa Stars kuitafutia timu mechi za kutosha za kimataifa kabla ya kushiriki wa mechi za kuwania Fainali za Afrika za 2013 na Kombe la Dunia la 2014.
Akizungumza kwenye mahojiano maalum, Gari Kubwa, alisema ili Simba na Yanga ziweze kufanya vema katika mechi zake za Ligi ya Mabingwa Afrika na Kombe la Shirikisho ni lazima zijipange vya kutosha badala ya kupiga 'blabla' huku muda ukienda.
Gari Kubwa, aliyewahi kuzichezea pia timu ya Majimaji-Songea, Bandari-Mtwara na Taifa Stars kwa nyakati tofauti, alisema maandalizi ya kutosha na kupata mechi nyingi za kirafiki za kimataifa zinaweza kuzibeba Simba na Yanga mwakani.
Alisema kinyume cha hapo ni kwamba timu hizo zisubiri kung'olewa mapema kama ilivyozoeleka na kuishia kutoa visingizio visivyo na maana.
"Naamini Simba na Yanga zikijipanga vema zinaweza kufanya vizuri katika uwakilishi wao, lakini zikiendelea kupiga blabla wakati muda ukizidi kwenda basi watarajie kuendelea kuwasononesha mashabiki wao kwa kung'olewa mapema," alisema.
Aidha, alilishauri Shirikisho la Soka nchini, TFF, kuanza maandalizi ya kuitafutia mechi za kirafiki za kimataifa, timu ya taifa, Taifa Stars, ili ijiweke vema kabla ya kukabiliana na wapinzani wao katika kuwania Fainali za Afrika na zile za Dunia.
Alisema amegundua Kocha Mkuu, Jan Poulsen amekuwa na wakati mgumu kwa matokeo mabaya ya timu yake kwa makosa yanayofanywa na TFF kwa kutoitafutia Stars mechi za kutosha kumpa nafasi kocha kurekebisha makosa.
"TFF lazima ibadilike na kuitafutia Stars mechi nyingi za kimataifa mapema, ili kumsaidia Poulsen, ni vigumu timu kufanya vema kama haipati mechi za maana za kujipima nguvu kabla ya kuingia kwenye ushindani," alisema.
Stars imepangwa kundi C katika makundi ya kuwania Fainali za Dunia zitakazofanyika Brazil, huku pia ikiwa na kibarua cha kuumana na Msumbiji katika mechi za mchujo za kuingia makundi ya kufuzu Fainali za Afrika 2013 zitakazochezwa nchini Afrika Kusini.
mwisho
Mchaki 'aula' VIlla Squad
KLABU ya soka ya Villa Squad, imemteua aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Soka wilaya ya Kinondoni, KIFA, Frank Mchaki kuwa Kaimu Katibu Mkuu baada ya Katibu Mkuu wao, Idd Godigodi kuwa mgonjwa.
Makamu Mwenyekiti wa klabu hiyo, Ramadhani Uledi, aliiambia MICHARAZO kuwa, wamelazimika kumuomba Mchaki awashikie nafasi hiyo ya Ukatibu kuitokana na Katibu wao kuwa mgonjwa na huku wakikabiliwa na majukumu kabla ya kuanza kwa ligi.
Uledi, alisema kamati yao ya utendaji ililazimika kuhitisha kikao cha dharura na kufanya maamuzi hayo, kwa nia ya kuifanya Villa isitetereke wakati ikijiandaa na duru la pili la Ligi Kuu Tanzania bara litakaloanza Januari 21.
"Tumemundikia barua kumuomba akaimu ukatibu mkuu, kutokana na uzoefu alionao na ametukubalia kwani kabla ya uteuzi alikuwa ndiye Katibu wa Kamati ya Usajili ya klabu yetu ambayo alifanya kazi nzuri kwa kuimarisha kikosi," alisema Uledi.
MICHARAZO iliwasiliana na Mchaki, ambaye alikiri kuombwa na uongozi wa klabu hiyo kushikilia cheo hicho na kudai haoni sababu ya kuikataa ilihali ni mmoja wa wadau wakubwa wa klabu hiyo.
"Ni kweli kuhusu jambo hilo na nimeshawajibu kuafiki uteuzi huo na kuwahidi wana Villa wanipe ushirikiano kuiwezesha timu yetu ifanye vema kwenye ligi hiyo na kuondokanan na janga la kushuka daraja pamoja na ukata uliopitiliza," alisema.
Villa Squad iliyorejea Ligi Kuu msimu huu, ndiyo inayoshikilia mkia katika msimamo wa ligi hiyo yenye timu 14.
Mwisho
Makamu Mwenyekiti wa klabu hiyo, Ramadhani Uledi, aliiambia MICHARAZO kuwa, wamelazimika kumuomba Mchaki awashikie nafasi hiyo ya Ukatibu kuitokana na Katibu wao kuwa mgonjwa na huku wakikabiliwa na majukumu kabla ya kuanza kwa ligi.
Uledi, alisema kamati yao ya utendaji ililazimika kuhitisha kikao cha dharura na kufanya maamuzi hayo, kwa nia ya kuifanya Villa isitetereke wakati ikijiandaa na duru la pili la Ligi Kuu Tanzania bara litakaloanza Januari 21.
"Tumemundikia barua kumuomba akaimu ukatibu mkuu, kutokana na uzoefu alionao na ametukubalia kwani kabla ya uteuzi alikuwa ndiye Katibu wa Kamati ya Usajili ya klabu yetu ambayo alifanya kazi nzuri kwa kuimarisha kikosi," alisema Uledi.
MICHARAZO iliwasiliana na Mchaki, ambaye alikiri kuombwa na uongozi wa klabu hiyo kushikilia cheo hicho na kudai haoni sababu ya kuikataa ilihali ni mmoja wa wadau wakubwa wa klabu hiyo.
"Ni kweli kuhusu jambo hilo na nimeshawajibu kuafiki uteuzi huo na kuwahidi wana Villa wanipe ushirikiano kuiwezesha timu yetu ifanye vema kwenye ligi hiyo na kuondokanan na janga la kushuka daraja pamoja na ukata uliopitiliza," alisema.
Villa Squad iliyorejea Ligi Kuu msimu huu, ndiyo inayoshikilia mkia katika msimamo wa ligi hiyo yenye timu 14.
Mwisho
Maneno, Matumla washindwa kutambiana
MABONDIA wakongwe wa ngumi za kulipwa nchini, Maneno Oswald 'Mtambo wa Gongo' na Rashid Matumla 'Snake Man' juzi walishindwa kutambiana baada ya pambano lao la kumaliza ubishi kuisha kwa kutoka sare.
Hata hivyo Oswald, ameyakubali matokeo hayo kwa ushingo upande, akidai kwamba alistahili kutangazwa mshindi kutokana na kumzidi maarifa mpinzani wake aliyeteleza na kuanguka ulingoni mara sita na kujikuta akiumia mguu.
Pambano hilo lisilo la ubingwa lililokuwa na raundi 10 na uzani wa kati lililosimamiwa na Shirikisho la Ngumi za Kulipwa Nchini, PST, lilifanyika kwenye ukumbi wa Heinken Pub, Mtoni Kijichi nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam.
Katika pambano hilo lililochezeshwa na mwamuzi wa kimataifa wa mchezo huo nchini, Anthony Rutta, mabondia wote wawili walipewa pointi 99-99, kitu ambacho Maneno Oswald aliiambia MICHARAZO kuwa ni kama mpinzani wake 'alibebwa' tu.
"Kwa kweli nimeyakubali matokeo hayo kwa shingo upande kwa vile nilistahili kabisa ushindi, ila mpinzani wangu amelindwa, Matumla kaanguka mara sita ulingoni, utetezi wake ulingo ulikuwa unateleza mbona mie sikuteleza," alisema Maneno.
Aliongeza kuwa, licha ya kuambiwa kuna mipango inafanywa ili warudiane tena, yeye binafsi hana mpango wa kufanya hivyo na kudai anataka kupigana na Mada Maugo, aliyedai ndiye anayemuona mpinzani wake wa ukweli.
"Sitarudiana na Matumla hata iweje, nataka kupigana na Maugo kwani namuona ndiye bondia wa kweli kwa sasa nchini katika uzito wetu.," alisema.
MICHARAZO lilijaribu kumsaka Matumla kusikia kauli yake juu ya matokeo ya mchezo huo, lakini simu yake haikuwa hewani.
Hilo lilikuwa ni pambano la nne kwa Maneno na Matumla kuzipiga, kwani walishacheza mechi tatu na mara mbili Matumla aliibuka na ushindi dhidi ya moja la mpinzani wake.
Katika mechi nyingine za utangulizi zilizochezwa kabla ya pambano la wawili, Ubwa
Kabla ya pambano hilo kuchezwa kulifanyika mechi kadhaa za utangulizi, ambapo moja wao lilimkutanisha bondia Ubwa Salum aliyempiga kwa pointi Mustafa Dotto.
Friday, December 2, 2011
Zanzibar mguu ndani mguu nje Kombe la Chalenji 2011

HATMA ya timu ya taifa ya Zanzibar, Zanzibar Heroes kuendelea na michuano ya Kombe la Chalenji, inasubiri majaliwa ya sheria ya kumpata best losser, kufuatia goli la Amissi Cedric lililo wapa ushindi Burundi wa goli 1-0 pala walipowakabili Uganda jana.
Zanzibar ilipata ushindi wake wa kwanza kwenye michuano hiyo inayoendelea jijini jana katika pambano lililochezwa mapema kwenye uwanja wa Taifa kwa kuilazaq Somalia mabao 3-0 na kufikisha pointi nne.
Mabao ya mshambuliaji wao hatari Suleiman Kassim 'Selembe', Ally Badru na nahodha Aggrey Morris yaliisaidia Zanzibar kujiweka katika nafasi nzuri ya kusonga mbele kutegemeana na matokeo ya makundi mengine yanayochezwa leo na kesho.
Kama mambo yatajipa Zanzibar waliopo nafasi ya tatu katika kundi lao la B nyuma ya Burundi wanaoongoza kwa pointi 7 na Uganda wenye pointi sita itafuzu hatua ya robo fainali.
Kwani kama sio ushindi wa bao 1-0 iliyopata Burundi mbele ya Uganda, Zanzibar isingekuwa na wakati mgumu wa kusubiri kapu la hisani kusonga mbele.
Zanzibar itabidi wangoje hekima za CECAFA kama watapata nafasi katika best loser ingawa kwa kuangalia matokeo ya makundi mengine yalivyo moja ya nafasi ya mshindwa bora kwa 'mashujaa' hao wa Zanzibar ni kubwa, ingawa soka halipo hivyo.
Ndugu zao Tanzania kesho nao watakuwa vitani kupigana kutinga robo fainali, kwa kuumana na Zimbabwe wanaolingana nao pointi tatu, huku Rwanda amabyo itacheza leo dhidi ya Djibout ikiwa imeshajihakikishia nafasi mojawapo ya kucheza hatua hiyo ya mtoani itakayoanza Jumatatu.
TMK kuumwa Kichwa Dar mpaka Mwanza
BAADA ya kimya cha miaka mitatu, kundi la muziki wa kizazi kipya la TMK Wanaume Family, limefyatua wimbo na video mpya iitwayo 'Kichwa Kinauma' itakayotambulishwa katika maonyesho maalum jijini Dar na Mwanza.
Kibao hicho kipya kilichorekodiwa 'audio' yake katika studio za MJ Records na video kutolewa na kampuni ya Visual Lab, inatarajiwa kusambazwa kwenye vituo vya redio na runinga wiki hii na kufuatiwa na maonyesho katika majiji hayo.
Meneja wa kundi hilo, Said Fella 'Mkubwa Fella' aliliambia MICHARAZO kuwa, kazi hiyo mpya itatambulishwa kwa wakazi wa Dar katika onyesho litakalofanyika Jumapili ya Desemba 4 kwenye ukumbi wa Maisha Club na kisha kuvaamia Mwanza Desemba 9.
Fella alisema wakiwa jijini Mwanza, kudni lao litakitambulisha kibao hicho na nyimbo nyingine binafsi za wasanii wa TMK Wanaume Family, kwenye ukumbi wa Villa Park.
"Mkubwa tumefyatua kibao kipya na video yake iitwayo Kichwa Kinauma ikiwa ni baada ya ukimya wa miaka mitatu tangu tutoe kazi ya mwisho na tutaitambulisha rasmi kwa mashabiki wetu katika miji ya Dar na Mwanza," alisema.
Fella aliongeza katika maonyesho hayo mawili ya jijini Dar na Mwanza, pia wataonyesha 'trela' la filamu ya kundi hilo ili kuwapa kionjo tu mashabiki wao kabla ya filamu hiyo kuingizwa sokoni katikati ya mwezi ujao.
"Unajua tumefyatua filamu inayohusiana na kundi letu, hivyo katika maonyesho hayo mawili ya utambulisho wa 'Kichwa Kinauma', pia tutaonyesha trela la filamu hiyo ambayo tutaitoa hadharani katikati ya Desemba," alisema Fella.
Kundi hilo la TMK Wanaume Family, linaundwa na wasanii kadhaa nyota wakiwemo Mhe Temba, Said Chegge, Dogo Aslay anayetamba na wimbo wa 'Nakusemea' na wengineo.
Sikinde yajiandaa kukamilisha albmu mpya
BENDI kongwe ya Mlimani Park 'Sikinde' ipo katika maandalizi ya mwisho ya kufyatua albamu yao mpya itakayozinduliwa mwishoni mwa mwezi ujao.
Katibu wa bendi hiyo, Hamis Milambo, alisema kuwa tayari wameshafyatua vibao kadhaa kwa ajili ya albamu hiyo itakayokuwa na nyimbo sita na watamalizia nyimbo zilizosalia kabla ya katikati ya Desemba.
Milambo, alisema katika harakati za kuitambulisha albamu hiyo wamefyatua video ya kibao chao cha 'Jinamizi la Talaka' ambao unatesa kwenye vituo kadhaa vya redio nchini.
"Sikinde tupo katika maandalizi ya kukamilisha kurekodi albamu yetu mpya itakayokuwa na nyimbo sita, ambayo tutaitoa hadharani mwishoni mwa Desemba," alisema.
Katibu huyo alivitaja baadhi ya vibao vitakavyokuwa katika albamu hiyo itakayochukua nafasi ya 'Supu Imetiwa Nazi' kuwa ni; 'Jinamizi la Talaka', 'Bundi', 'Mihangaiko ya Kazi' na 'Asali na Shubiri'.
Sikinde, kwa muda wa miaka miwili sasa haijatoa albamu yoyote tangu ilipotamba na Supu Imetiwa Nazi ambayo ilifyatuliwa wakati ikiwa chini ya Shirika na Maendeleo Dar es Salaam, DDC iliyowatema rasmi mapema mwaka uliopita.
Katibu wa bendi hiyo, Hamis Milambo, alisema kuwa tayari wameshafyatua vibao kadhaa kwa ajili ya albamu hiyo itakayokuwa na nyimbo sita na watamalizia nyimbo zilizosalia kabla ya katikati ya Desemba.
Milambo, alisema katika harakati za kuitambulisha albamu hiyo wamefyatua video ya kibao chao cha 'Jinamizi la Talaka' ambao unatesa kwenye vituo kadhaa vya redio nchini.
"Sikinde tupo katika maandalizi ya kukamilisha kurekodi albamu yetu mpya itakayokuwa na nyimbo sita, ambayo tutaitoa hadharani mwishoni mwa Desemba," alisema.
Katibu huyo alivitaja baadhi ya vibao vitakavyokuwa katika albamu hiyo itakayochukua nafasi ya 'Supu Imetiwa Nazi' kuwa ni; 'Jinamizi la Talaka', 'Bundi', 'Mihangaiko ya Kazi' na 'Asali na Shubiri'.
Sikinde, kwa muda wa miaka miwili sasa haijatoa albamu yoyote tangu ilipotamba na Supu Imetiwa Nazi ambayo ilifyatuliwa wakati ikiwa chini ya Shirika na Maendeleo Dar es Salaam, DDC iliyowatema rasmi mapema mwaka uliopita.
Poulsen bado hajaniamini-Jabu

BEKI mahiri wa Simba anayezichezea pia timu za taifa, Juma Jabu, amekiri kwamba kocha wa sasa wa timu ya taifa (Taifa Stars), Jan Poulsen hajamuamini ndiyo maana amekuwa haitwi mara kwa mara katika kikosi hicho.
Hata hivyo, alisema kutoaminiwa huko kunatokana na kuwepo majeruhi kwa muda mrefu tangu Mdenmark huyo alipoitwaa timu hiyo toka kwa Mbrazil, Marcio Maximo.
Jabu maarufu kama 'JJ', alisema amekuwa akipata nafasi ndogo ndani ya kikosi cha Stars kwa vile Poulsen hajaridhika naye, tofauti na ilivyo kwa Maximo ambapo panga pangua hakukosekana kikosini.
"Sio siri sijapata nafasi kubwa ndani ya kikosi cha Stars tangu iwe chini ya Poulsen, hii inatokana na kocha kutoniamini pengine kwa vile nilikuwa majeruhi na hivyo kutoonekana dimbani, ila naamini michuano ya Chalenji itanirejesha Stars," alisema.
Alisema kuitwa kwake katika kikosi cha Kilimanjaro Stars ambayo leo inamaliza mechi zake za makundi dhidi ya Zimbambwe, ni fursa nzuri ya kumshawishi Poulsen ampe nafasi ya kudumu katika Stars inayokabiliwa na mechi za kuwania kufuzu CAN 2013 na WC 2014.
Katika hatua nyingine beki huyo alisema mipango yake ya kwenda kucheza soka la kulipwa nchini Afrika Kusini inaendelea vema, ingawa hakupenda kuweka bayana kwa madai suala lake linasimamiwa na wakala wake.
"Mipango yangu ya kwenda Afrika Kusini ipo pazuri, ila mwenye nafasi ya kuliongelea kwa undani ni wakala wangu," alisema Jabu.
Mkenya Kariuki kutua nchini Kesho kupiogana na Nassib Ramadhan
MPINZANI wa Bingwa wa Dunia anayetambuliwa na World Boxing Forum, Nassib Ramadhan 'Manny Pacquiao', Mkenya Anthony Kariuki, anatarajia kutua nchini kesho kwa pambano lao litakalofanyika Desemba 9 jijini Dar es Salaam.
Kariuki na Nassib watapigana katika pambano lisilo la ubingwa la raundi 10 uzani wa Fly kwenye ukumbi wa DDC Keko, ambapo watasindikizwa na michezo kadhaa ya utangulizi.
Akizungumza na MICHARAZO, mratibu wa pambano hilo, Pius Agathon, alisema Kariuki atatua nchini leo mchana akiambatana na kocha wake tayari kwa pambano lake ambalo litaenda sambamba na maadhimisho ya Miaka 50 ya Uhuru.Agathon, alisema kambi ya Mkenya huyo itakuwa eneo la Keko, wakati mpinzani wake ipo eneo la Mabibo chini ya kocha wake, Christopher Mzazi.
"Mkenya atakayepigana na Nassib Ramadhan atatua nchini Jumamosi (kesho)na moja kwa moja ataingia kambini eneo la Keko, tayari kuvaana na mpinzani wake aliyejichimbia Mabibo," alisema Agathon.
Agathon aliongeza kuwa maandalizi kwa ujumla ya pambano hilo litakalohudhuriwa pia na nyota wa zamani wa mchezo huo walioliletea sifa Tanzania katika miaka 50 ya Uhuru yamekamilika na inasubiriwa siku ya kufanyika kwa mchezo huo.
Alisema siku hiyo kutakuwa na michezo mitano ya utangulizi kabla ya Nassib Ramadhan kupeperusha bendera ya Tanzania mbele ya Mkenya.
BREAKING NEWS: Mr Ebbo hatunaye


Taarifa zilizotufikia muda huu zinasema kwamba aliyekuwa msanii wa muziki wa kizazi kipya, Abel Loshilaa Motika 'Mr Ebbo' amefariki alfajiri ya leo na anatarajiwa kuzikwa huko kwao Arusha siku ya Jumapili.
Mr Ebbo aliyetamba na staili yake ya kuimba 'kiswahili cha kimasai', arakumbukwa kwa nyimbo matata kama Mi Mmasai Bana, Maneno Mbofu Mbofu, 'Pombe' na nyinginezo.
Kwa taarifa za awali zinasema alikuwa akiugua kitambo, ingawa haikuwahi kuripotiwa mapema hadi leo tulipopenyezewa taarifa hizi.
Mungu Aiweke Roho ya Mr Ebbo Mahali Pema. Amin
Friday, November 18, 2011
Mabondia 10 kuwasindikiza Nassib vs Kariuki
BINGWA wa zamani wa Dunia wa World Boxing Forum, Juma Fundi na Rashid Ally ni miongoni mwa mabondia watakaolisindikiza pambano la kimataifa kati ya Nassib Ramadhan 'Manny Pacquiao wa Tz' dhidi ya Anthony Kariuki kutoka Kenya.
Nassib anayeshikilia kwa sasa taji la dunia la World Boxing Forum baada ya kumvua Juma Fundi Mei mwaka huu, atapigana na Karikuki katika pambano litaklofanyika siku ya kuadhimisha miaka 50 ya Uhuru, Desemba 9 kwenye ukumbi wa DDC Keko, jijini Dar es Salaam.
Mratibu wa pambano hilo, Pius Agathon, aliiambia MICHARAZO kwamba Fundi na Ally ni kati ya mabondia 10 watakaopanda ulingoni kusikindikiza pambano hilo la raundi 10 lisilo la ubingwa kati ya Nassib na Kariuki.
Agathon, alisema Fundi atapigana siku hiyo na Juma Seleman katika pambano la raundi sita la uzani wa kilo 51, Fred Sayuni dhidi ya Bakar Dunda na Ramadhani Kumbele ataonyeshana kazi na Shabaan Madilu.
"Mipambano mingine siku hiyo itakuwa ni kati ya Rashid Ally atakayepigana na Daud Mhunzi katika uzito wa kilo 57 na Faraji Sayuni ataumizana na Alfa George ndipo Nassib atakapopanda ulingoni kupigana na Kariuki katika uzani wa Fly," alisema.
Mratibu huyo alisema maandalizi ya jumla ya mapambano hayo yanaendelea vema ikiwemo kumalizana na mabondia wote ambao kwa sasa wanaendelea kujifua kwa mazoezi tayari kuonyeshana ubabe siku hiyo kwenye ukumbi huo wa DDC Keko.
Aliongeza lengo la michezo hiyo mbali na kuwaweka fiti mabondia hususani Nassib ambaye mwakani atalitetea taji lake la World Boxing Forum, pia ni maalum kwa ajili ya kuadhimisha miaka 50 ya Uhuru.
"Tumeandaa michezo hii ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha miaka 50 ya Uhuru sambamba na kumuandaa vema Nassib kabla ya kulitetea taji lake mwakani," alisema.
Mwisho
Niyonzima aikana Simba, awatroa hofu Jangwani

KIUNGO nyota wa kimataifa wa klabu ya Yanga, Haruna Niyonzima 'Fabregas' amewatoa hofu wanayanga kwa kuweka wazi kwamba hana mpango wa kujiunga na mahasimu wao Simba kwa kile alichodai anaridhika na maisha yake Jangwani.
Pia, kiungo huyo alisema kama ni kuondoka Yanga, basi sio kwa kujiunga na klabu nyingine ya Tanzania, bali ni kwenda kucheza soka la kulipwa Ulaya, ikiwa ni kati ya ndoto anazoota kila siku maishani mwake.
Akizungumza moja na kipindi cha michezo cha Radio One 'Spoti Leo', Niyonzima, amedai kushangazwa na taarifa kwamba Simba inamnyemelea wakati hajawahi kufanya mazungumzo yoyote na uongozi wa klabu hiyo au mtu yeyote.
Kiungo huyo aliyetua Jangwani akitokea klabu ya APR ya Rwanda, alisema mbali na kutowahi kuzungumza na mtu yeyote ili kujiunga Simba, lakini yeye binafsi hana mpango huo kwa vile anaridhika na maisha yake ndani ya klabu yake ya sasa.
"Aisee sina mpango wa kuihama Yanga na hivyo nawataka wanayanga wasiwe na hofu nadhani yanayosemwa yanatokana na kuvutiwa na soka langu, lakini sijawahi kuzungumza na mtu yeyote kujiunga Simba," alisema.
"Pia kwa namna mambo yangu yanayotekelezwa ndani ya Yanga na mie kuitumikia klabu hiyo kwa mafanikio, sioni sababu ya kutaka kuhama na kama ikitokea hivyo basi ni kwenda zaidi ya Tanzania, lakini sio kujiunga Simba," alinukuliwa Niyonzima.
Nyota huyo anayeichezea pia timu ya taifa ya nchi yake ya Rwanda 'Amavubi' alisema ingawa yeye ni mchezaji na lolote linaweza kutokea, lakini hadi wakati akizungumza hakuwa amewaza lolote juu ya kuiacha Yanga aliyosaini nayo mkataba wa miaka miwili.
Kwa wiki kadhaa sasa kumekuwa na taarifa kwamba Simba imekuwa ikimwinda kiungo huyo ambaye soka lake limewakuna wengi tangu atue Jangwani, ikiwa kama jibu la watani zao, Yanga kudaiwa kumnyatia mshambuliaji wao, Felix Sunzu.
Tetesi hizo za Yanga na Simba kubadilishana wachezaji zimekuja wakati mbio za usajili wa dirisha dogo nchini likizidi kupambana moto.
Mwisho
Mkwasa, Julio wambeep Poulsen kwa Boban

MAKOCHA wapya wa timu ya taifa ya Tanzania Bara, Kilimanjaro Stars, Charles Boniface Mkwasa na Jamhuri Kihwelu 'Julio' wamembeep, kocha mkuu wa timu ya taifa, Taifa Stars, Jan Poulsen bada ya kumuita kikosi kiungo wa wa Simba, Haruna Moshi 'Boban'.
Boban na mshambuliaji mpya wa Azam, Gaudence Mwaikimba, wameitwa katika kikosi cha Kilimanjaro Stars kitakachotetea ubingwa wake katika mashindano ya Kombe la Chalenji yatakayoanza Novemba 25 jijini Dar es Salaam.
Baada ya Boban kusajiliwa na Simba na kuanza kuitumikia kwenye fainali zilizopita na Kombe la Kagame mwaka huu, kocha wa Taifa Stars, Jan Poulsen, alimuita katika kikosi cha vijana wa umri chini ya miaka 23 kilichokuwa na mechi mbili za kirafiki na Shelisheli jijini Arusha lakini kiungo huyo alikacha wito huo na hivyo kuendelea kuwa nje ya timu hiyo kwa muda mrefu.
Akitangaza kikosi cha nyota 28 jana, kocha msaidizi wa Kili Stars, Jamhuri Kihwelu 'Julio' alisema kuwa kikosi chake kitaanza mazoezi leo kwenye Uwanja wa Karume na lengo la kuita wachezaji hao ni kuwapima zaidi na baadaye watachujwa na kubaki 20 kama kanuni za usajili wa mashindano hayo zinavyoeleza.
Julio alisema kuwa ameita wachezaji wengi chipukizi ili kuwapa nafasi zaidi ya kujifunza na kuitumikia nchi yao kwa bidii huku pia akiwaita wazoefu ili waweze kupambana na changamoto kutoka kwa timu pinzani kwenye michuano hiyo.
"Tunawaomba Watanzania wajue kuwa hii ni timu yao, watupe ushirikiano, waipende na kuishangilia ili sisi wazawa tuweze kulitetea kombe, tunaahidi kupambana na kukibakisha kikombe," alisema kocha huyo.
Alisema kuwa wanaahidi kupambana na wachezaji wasio na nidhamu ili wajirekebishe na hatimaye kuitumikia vyema nchi yao kutokana na uwezo wa kucheza soka walionao.
"Hii ni timu ya wote na kwa kuwa mpira hauchezwi chumbani, hata Saidi Maulidi (SMG) kama anaweza kuja aje katika mazoezi apambane na akionyesha anaweza tutamchukua katika kikosi cha watu 20," aliongeza Julio kuhusiana na uteuzi wa wachezaji wanaocheza nje ya nchi.
Kikosi kamili cha timu hiyo kilichoitwa jana ambacho nahodha wake atakuwa ni kipa Juma Kaseja kutoka Simba ni pamoja na Deo Munishi 'Dida' kutoka Mtibwa Sugar, Shabani Kado (Yanga), huku mabeki wa pembini wakiwa ni Shomari Kapombe (Simba), Godfrey Taita (Yanga), Juma Jabu (Simba) na Paul Ngelema (Ruvu Shooting).
Mabeki wa kati walioitwa ni Juma Nyoso (Simba), Said Murad (Azam), Erasto Nyoni (Azam) na Salum Telela (Moro United) huku viungo wakiwa ni Shabani Nditi (Mtibwa Sugar), Ibrahim Mwaipopo (Azam), Nurdin Bakari (Yanga), Mwinyi Kazimoto (Simba), Boban, Ramadhan Chombo (Azam), Rashid Yusuf (Coastal Union), Jimmy Shogi (JKT Ruvu Stars) na Mohamed Soud (Toto Africans).
Washambuliaji walioitwa ni Mrisho Ngassa (Azam), Mbwana Samatta (TP Mazembe, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo), Mwaikimba (Moro United), John Bocco (Azam), Thomas Ulimwengu (TP Mazembe ), Hussein Javu (Mtibwa Sugar), Daniel Reuben (Coastal Union) na Nizar Khalfan wa Vancouver Whitecaps ya Canada.
Kilimanjaro Stars itaanza kampeni ya kutetea ubingwa wake siku moja baada ya kwanza ya michuano hiyo kwa kuumana na Rwanda 'Amavubi' kwenye Uwanja wa Taifa.
Jailan, Matimbwa kuonyeshana kazi Morogoro
BONDIA mahiri wa ngumi za kulipwa wa mkoa wa Morogoro, Mohamed Jeilani anatarajiwa kupanda ulingoni kuonyeshana ubabe na Mohammed Matimbwa wa Dar katika pambano lisilo la mkanda litakalofanyika siku ya Desemba 3, mjini Morogoro.
Pambano hilo la raundi nane litafanyika kwenye ukumbi wa Urafiki na litasindikizwa na michezo kadhaa ya utangulizi.
Mkurugenzi wa kampuni ya BS Promotion, waandaaji wa pambano hilo, Daudi Julian aliiambia MICHARAZO kwamba mchezo huo ni wa uzani wa kilo 60 na lengo lake ni kuhamamisha mchezo wa ngumi mkoani humo.
Julian, alisema maandalizi ya pambano hilo na michezo yote ya utangulizi yanaendelea vema na tayari mabondia wote watakaopigana siku hiyo wanaendelea kujifua kujiweka tayari kuonyeshana kazi ulingoni.
Aliwataja mabondia watakaowasindikiza Jailan na Matimbwa siku ya pambano lao ni pamoja na Maneno William ‘Chipolopolo’, Nassib Msafiri ‘Ngumi Nondo’ na Said Idd ‘Simple Boy’ watachapana na mabondia kutoka Dar es Salaam na Tanga.
"Kampuni yetu imeandaa pambano la ngumi la kirafiki kati ya Mohammed Jailan dhidi ya Mohammed Matimbwa litakalofanyika Desemba 3 mwaka huu na kusindikizwa na michezo mingine kati ya mabondia wa Moro dhidi ya wale wa Dar na Tanga," alisema.
Alisema mbali ya pambano hilo, kampuni hiyo pia inatarajia kuandaa mapambano mengine ya ngumi , siku ya kusherehekea sikukuu ya X-mass ambapo mabondia wa mkoa wa Morogoro, Dar es Salaam, Dodoma na Tanga wataonyeshana kazi.
Julian ametoa wito kwa wafadhili wa michezo kujitokeza na kudhamini mapambano mbalimbali yatakayoandaliwa na kampuni yake kwa lengo la kuhamasisha mchezo huo mkoani humo.
Mwisho
Pambano hilo la raundi nane litafanyika kwenye ukumbi wa Urafiki na litasindikizwa na michezo kadhaa ya utangulizi.
Mkurugenzi wa kampuni ya BS Promotion, waandaaji wa pambano hilo, Daudi Julian aliiambia MICHARAZO kwamba mchezo huo ni wa uzani wa kilo 60 na lengo lake ni kuhamamisha mchezo wa ngumi mkoani humo.
Julian, alisema maandalizi ya pambano hilo na michezo yote ya utangulizi yanaendelea vema na tayari mabondia wote watakaopigana siku hiyo wanaendelea kujifua kujiweka tayari kuonyeshana kazi ulingoni.
Aliwataja mabondia watakaowasindikiza Jailan na Matimbwa siku ya pambano lao ni pamoja na Maneno William ‘Chipolopolo’, Nassib Msafiri ‘Ngumi Nondo’ na Said Idd ‘Simple Boy’ watachapana na mabondia kutoka Dar es Salaam na Tanga.
"Kampuni yetu imeandaa pambano la ngumi la kirafiki kati ya Mohammed Jailan dhidi ya Mohammed Matimbwa litakalofanyika Desemba 3 mwaka huu na kusindikizwa na michezo mingine kati ya mabondia wa Moro dhidi ya wale wa Dar na Tanga," alisema.
Alisema mbali ya pambano hilo, kampuni hiyo pia inatarajia kuandaa mapambano mengine ya ngumi , siku ya kusherehekea sikukuu ya X-mass ambapo mabondia wa mkoa wa Morogoro, Dar es Salaam, Dodoma na Tanga wataonyeshana kazi.
Julian ametoa wito kwa wafadhili wa michezo kujitokeza na kudhamini mapambano mbalimbali yatakayoandaliwa na kampuni yake kwa lengo la kuhamasisha mchezo huo mkoani humo.
Mwisho
Banka afichua kilichompeleka JKT Ruvu

KIUNGO mahiri wa zamani wa klabu za Simba na Yanga, Mohammed Banka ametua JKT Ruvu akisema ni klabu aliyokuwa akiiota kwa muda mrefu kutokana na na kuwa na soka la kuvutia na lenye ushindani uwanjani.
Aidha amekanusha kuwahi kufanya mazungumzo na viongozi wa timu za Coastal Union na Moro United ili ajiunge navyo kama ilivyokuwa ikiripotiwa.
Akizungumza na MICHARAZO Banka, alisema tayari ameshamwaga wino wa kuichezea JKT kwa ajili ya duru la pili la Ligi Kuu Tanzania Bara na amefurahi mno.
Banka, alisema soka la JKT ndilo lililomsukuma kujiunga akiamini namna ya uchezaji wa klabu hiyo na aina ya wachezaji anaoungana nao itamsaidia kurejea upya katika soka la Tanzania baada ya nusu msimu kuwa nje ya dimba kutokana na mzozo wake na Simba.
"Nimemwaga wino wa kuichezea JKT Ruvu, kikubwa kilichonivutia kujiunga na timu hii ni aina ya soka inalocheza na wachezaji iliyonayo, ni kati ya klabu nilizokuwa naota kuzichezea kwa vile ni timu yenye malengo na ushindani wa kweli dimbani," alisema Banka.
Alipoulizwa imekuwaje amezitosa Coastal Union na Moro United ambazo zimekuwa
zikijinasibu kumnyemelea, Banka, alisema zaidi ya kusikia kwenye vyombo vya habari
hakuwahi kufuatwa na kiongozi yeyote wa timu hizo kuzungumza nao.
"Ndugu yangu sijawahi kufuatwa wala kuwasiliana japo kwa simu kuzungumza kuhusu
kujiunga na klabu hizo, zaidi ya kusikia kwenye vyombo vya habari kwamba natakiwa nazo, ila JKT Ruvu kabla ya kujiunga nilishafanya nao mazoezi weakati duru la kwanza likielekea ukingoni," alisema Banka.
Banka, aliyewahi kuichezea Moro United na aliyekuwa mchezaji wa Simba kabla ya kuigomea klabu hiyo kumtoa kwa mkopo kwa klabu ya Villa Squad ni miongoni mwa wachezaji watano wapya waliongezwa katika klabu hiyo ya JKT Ruvu.
Wengine waliotua JKT Ruvu ni George Mketo na Paul Ngahyoma toka Kagera, Said Hamis toka Polisi Morogoro na Bakar Kondo aliyerejeshwa kikosini.
Mwisho
Bondia Moro amtaka Miyeyusho
BONDIA machachari wa ngumi za kulipwa mkoani Morogoro, Maneno William 'Chipolopolo' ameibuka na kudai anamtaka bingwa wa UBO-Mabara, Francis Miyeyusho wa Dar es Salaam, ili apigane nae.
Chipolopolo aliyejipatia umaarufu mkubwa mkoani humo, kutokana na uwezo wake wa kurusha makonde makali ulingoni, hivi sasa yuko katika mazoezi makali chini ya mwalimu Boma Kilangi.
Akizungumza na blog hii kutoka Morogoro, bondia huyo alisema amejipanga vizuri kufanya maajabu katika mchezo wa ngumi huku kiu yake kubwa ikiwa ni kuchapana na Miyeyusho maarufu kama 'Chichi Mawe'.
Chipolpolo, alisema anamuona Miyeyusho ni bondia wa kawaida na kwamba atapigika kirahisi licha ya kufanya vizuri katika mchezo huo katika siku za hivi karibuni.
Alisema, ili kutimiza dhamira yake yupo tayari kupanda ulingoni wakati wowote kuzipiga na Miyeyusho kama atatokea promota wa kuwaandalia pambano hilo.
Bondia huyo wa Morogoro alisema licha ya Miyeyusho kumchapa Mbwana Matumla hivi karibuni katika ukumbi wa Diamond Jubilee Dar es Salaam, ni lakini kwake lazima apate kipigo.
"Nipo fiti, najiamini na nafikiri sasa ni wakati wa kuchapana na Miyeyusho na kizuri zaidi ni bondia wa uzito wangu," alisema.
Chipolopolo alisema hachagui mahali pa kupambana na bondia huyo na kwamba yupo tayari kuvaana naye hata jijini Dar es Salaam.
MIcharazo lilijaribu kumsaka Miyeyusho kwa njia ya simu kupata maoni yake juu ya tambo za bondia huyo wa Morogoro, lakini hakuweza kupatikana.
Mwisho
Chipolopolo aliyejipatia umaarufu mkubwa mkoani humo, kutokana na uwezo wake wa kurusha makonde makali ulingoni, hivi sasa yuko katika mazoezi makali chini ya mwalimu Boma Kilangi.
Akizungumza na blog hii kutoka Morogoro, bondia huyo alisema amejipanga vizuri kufanya maajabu katika mchezo wa ngumi huku kiu yake kubwa ikiwa ni kuchapana na Miyeyusho maarufu kama 'Chichi Mawe'.
Chipolpolo, alisema anamuona Miyeyusho ni bondia wa kawaida na kwamba atapigika kirahisi licha ya kufanya vizuri katika mchezo huo katika siku za hivi karibuni.
Alisema, ili kutimiza dhamira yake yupo tayari kupanda ulingoni wakati wowote kuzipiga na Miyeyusho kama atatokea promota wa kuwaandalia pambano hilo.
Bondia huyo wa Morogoro alisema licha ya Miyeyusho kumchapa Mbwana Matumla hivi karibuni katika ukumbi wa Diamond Jubilee Dar es Salaam, ni lakini kwake lazima apate kipigo.
"Nipo fiti, najiamini na nafikiri sasa ni wakati wa kuchapana na Miyeyusho na kizuri zaidi ni bondia wa uzito wangu," alisema.
Chipolopolo alisema hachagui mahali pa kupambana na bondia huyo na kwamba yupo tayari kuvaana naye hata jijini Dar es Salaam.
MIcharazo lilijaribu kumsaka Miyeyusho kwa njia ya simu kupata maoni yake juu ya tambo za bondia huyo wa Morogoro, lakini hakuweza kupatikana.
Mwisho
Saturday, November 12, 2011
Maugo kuweka kambi Mwanza kumwinda Mjerumani
BONDIA machachari wa ngumi za kulipwa nchini, Mada Maugo anatarajia kuingia kambini jijini Mwanza, kujiandaa na pambano lake la kimataifa la kuwania ubingwa wa IBF dhidi ya Mjerumani Rico Nicovic atakayepigana nae Desemba 26 jijini humo.
Maugo ameiambia MICHARAZO kuwa, anatarajia kuondoka jijini Dar es Salaam wiki ijayo kwenda kuweka kambi jijini Mwanza tayari kumkabili mpinzani wake huyo katika pambano litakalofanyika kwenye uwanja wa CCM Kirumba.
Bondia huyo alisema kambi na pambano hilo la kimataifa litakalosimamiwa na Shirikisho la Ngumi za Kulipwa nchini, vyote vimeandaliwa na kugharamiwa na Mbunge wa Jimbo la Rorya, Lameck Airo 'Obama'.
"Maandalizi ya pambano langu yanaendelea vema nikiwa nimeshanza kuzungumza na mabondia watakaosindikiza siku hiyo na wiki ijayo natarajia kuondoka Dar kuelekea Mwanza kuweka kambi kwa ajili ya pigano hilo," alisema Maugo.
Aliongeza pambano lake na Mjerumani huyo, litakuwa la raundi 12 katika uzani wa kilo 72.5 na watasindikizwa na michezo zaidi ya mitano itakayowahusisha pia mabondia wakongwe nchini akiwemo bingwa wa zamani wa dunia wa WBU, Rashid Matumla.
Maugo alisema Matumla atapigana na bondia kutoka Uganda, huku Emma Kichere na mabondi wengine wa kanda ya Ziwa watapanda ulingoni kuonyeshana kazi sambamba na kuhamasisha mchezo katika kanda hiyo.
"Mkongwe Matumla atakuwepo kunisindikiza siku ya pambano langu na Nicovic, kuba analofanya mfadhili wangu, yaani Mbunge wa Rorya ni kuhamasisha ngumi katika kanda ya ziwa," alisema Mada.
Maugo, hivi karibuni alipata ushindi wa KO kwa kumpiga Joseph Odhiambo katika pambano lisilo la ubingwa ikiwa ni baada ya kutoka kupokea kipigo toka kwa Francis Cheka katika pambano la kuwania taji la UBO-Inter Continental.
Mwisho
Miyeyusho aota ubingwa wa dunia
BONDIA machachari, Francis Miyeyusho anayeashikilia taji la UBO-Mabara baada ya kumvua aliyekuwa akilishikilia, Mbwana Matumla, aliyemtwanga hivi karibuni alisema kiu yake kubwa kwa sasa ni kuona anautwaa ubingwa wa dunia katika mchezo huo.
Miyeyusho anayefahamika zaidi kama 'Chichi Mawe', alisema kumvua taji Mbwana ni furaha kubwa, lakini hajaridhika hadi atakapotwaa ubingwa wa dunia katika mchezo huo kama wanavyofanya mabondia wengine duniani.
Bondia huyo, alisema haitakuwa na maana yoyote ya ushindi wake kwa Mbwana kama ataishia kwenye taji hilo la Mabara, ndio maana anasisitiza angependa kuona anafika mbali katika mchezo huo kwa kutwaa ubingwa wa dunia.
"Kiu yangu kubwa kwa sasa ni kuona natwaa ubingwa wa dunia, itakuwa furaha kubwa kuliko hii ya kumvua taji Golden Boy, ambaye ni mmoja kati ya mabondia ninaowaheshimu kwa mafanikio yao nchini kama ilivyo kwa kaka yake," alisema.
Miyeyusho alimtwanga Mbwana kwa pointi katika pambano lao lililofanyika Oktoba 30 kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee, Dar es Salaam likiwa ni pambano la tatu kati yao kukutana katika mchezo huo.
Katika mapambano yao ya awali yaliyochezwa Februari 21, 2004 na Januari 17, 2009, Miyeyusho alichezea kichapo toka kwa Mbwana.
Wakati huo huo, bingwa anayeshikilia taji la dunia la World Boxing Forum, Nassib Ramadhan anatarajiwa kupanda ulingoni Desemba 9 kuzipiga na mkenya Anthony Kariuki katika pambano litakalofanyika kwenye ukumbi wa DDC Keko.
Mratibu wa pambano hilo, Pius Aghaton alisema pambano hilo la raundi 10 la uzito wa fly, litasindikizwa na michezo kadhaa ya utangulizi na lengo kubwa ni kumuandaa Nassib kwa pambano la kutetea taji lake hilo analoshikilia baada ya kumvua aliyekuwa bingwa wake, Juma Fundi, katika pambano lililofanyika nchini Mei mwaka huu.
Coastal yawafuata Banka, Chuji Dar
UONGOZI wa klabu ya soka ya Coastal Union ya Tanga, imewafuata viungo nyota wa zamani wa Simba na Yanga, Mohammed Banka na Athuman Idd 'Chuji', ikipuuza taarifa kwamba Chuji ameamua kurejea Yanga kwa duru lijalo la Ligi Kuu Tanzania.
Mwenyekiti wa timu hiyo, Ahmed Aurora, alisema wanaamini Chuji ataichezea timu yao kama itakavyokuwa kwa Mohammed Banka na Ally Ahmed Shiboli ambao imekuwa ikiwanyemelea kukiimarish kikosi chao kwa duru hilo lijalo.
Aurora, alisema alikuwa akijiandaa kuja Dar ili kuonana na wachezaji hao watatu inayotaka kuwasajili kwenye dirisha dogo linalotarajiwa kufungwa Novemba 30.
"Klabu yetu bado inawahitaji wachezaji hao ili kuisaidia katika duru la pili na najiandaa kuja huko, licha ya kwamba nimeshtusha kusikia Chuji ametua Yanga, wakati tayari tulishaanza mazungumzo nae," alisema.
Aurora alisema hata kama Chuji atakuwa ametua Yanga (ingawa Yanga imemruka kimanga) bado wao watamfuata kuzungumza nae kabla ya kumsainisha mkataba wa kuicheza Coastal katika duru la Pili litakaloanza Januari mwakani.
Mbali na kuwawinda wachezaji hao, timu hiyo pia imetangaza kuwarudisha kundi nyota wake wa kimataifa, Mkenya Edwin Mukenya na Wanigeria wawili, Felix Amechi na Felix Amechi na Samuel Temi ambao walikuwa kwenye orodha ya usajili wa timu hiyo kabla ya kukwamba kutokana na sababu zilizokuwa nje ya uwezo wa pande mbili.
Coastal iliyorejea Ligi Kuu msimu huu ikitokea Daraja la Kwanza na timu nyingine tatu za Oljoro JKT, Moro United na Villa Squad, imemaliza duru la kwanza ikiwa katika nafasi tatu za kwanza toka mkiani baada ya kujikusanyia pointi 11 kwa michezo 13.
Taifa Stars yatakata Chad
Na Maulidi Kitenge, Chad
USHIRIKIANO wa wachezaji waliotokea benchi, Nurdin Bakari na Thomas Ulimwengu katika dakika za lala-salama uliipa Taifa Stars mwanzo mzuri wa mechi za hatua ya mchujo za kuelekea kwenye hatua ya makundi ya kufuzu kwa fainali zijazo za Kombe la Dunia 2014 kufuatia ushindi wa 2-1 ugenini kwa Chad jana.
Kiungo wa Yanga, Nurdin, aliyeingia katika kipindi cha pili kuchukua nafasi ya Abdi Kassim anayecheza soka la kulipwa nchini Vietnam, aliifungia Stars goli la ushindi katika dakika ya 82 akitumia pasi ya mshambuliaji wa TP Mazembe ya DRC, Ulimwengu, ambaye pia aliingia katika kipindi cha pili kuchukua nafasi ya nyota mwenzake wa klabu hiyo ya Congo, Mbwana Samatta.
Katika mechi hiyo iliyofanyika kwenye Uwanja wa Idriss Mahamat Ouya mjini N'djamena, Stars walitangulia kupata bao la mapema katika dakika ya 11 kupitia kwa Ngassa aliyemalizia kiufundi pasi ya kiungo anayecheza soka la kulipwa nchini Canada, Nizar Khalfan.
Hata hivyo, wenyeji walihitaji dakika moja tu kusawazisha goli hilo walilopata kupitia kwa mshambuliaji wao anayecheza soka la kulipwa katika Ligi Daraja la Pili Ufaransa (Ligue 2) ya Club Laval B, Mahamat Labbo katika dakika ya 12 na kufanya matokeo ya 1-1 hadi wakati wa mapumziko.
Wakati mechi ikielekea ukingoni na wenyeji wakiamini kwamba wangeweza kupata angalau sare, Nurdin aliifungia Stars goli la pili na la ushindi katika dakika ya 80 lililoeafanya mashabiki wa Chad waliokuwa wamejaa uwanjani kuanza kuondoka kimyakimya.
Stars itarejea kifua mbele kesho kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere lakini itahitaji kutoruhusu kipigo katika mechi yao ya marudiano Jumanne kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Kama Stars itasonga mbele, itatinga katika Kundi C la kuwania kufuzu kwa fainali zijazo za Kombe la Dunia zitakazofanyika mwaka 2014 nchini Brazil, ambapo watajumuika timu ngumu za Ivory Coast, Morocco na Gambia.
Kocha wa Stars, Jan Poulsen aliwapongeza wachezaji wake baada ya mechi hiyo lakini alisema kazi bado haijamalizika na wanahitaji umakini mkubwa ili kusonga mbele.
Kikosi cha Stars jana kiliundwa na Juma Kaseja, Shomari Kapombe, Idrisa Rajab, Agrey Morris, Juma Nyoso, Shaban Nditi, Henry Joseph, Abdi Kassim/ Nurdin Bakari, Nizar Khalfan, Mrisho Ngassa, Mbwana Samatta/ Thomas Ulimwengu.
BFT yapiga 'dochi' kozi ya makocha

KOZI ya ukocha wa ngumi ngazi ya kimataifa, iliyoandaliwa na Shirikisho la Ngumi za Ridhaa nchini, BFT ikishirikiana na Kamati ya Olimpiki Tanzania, TOC, imekwama kuanza leo Jumamosi kama ilivyopangwa badala yake sasa ifanyika Alhamisi ijayo.
Kozi hiyo itakayoshirikisha washiriki 30 watakaonolewa na Mkufunzi wa Kimataifa kutoka Algeria, ilikuwa imepangwa kuanza leo mjini Kibaha, lakini BFT imetoa taarifa kwamba imesogezwa mbele kutokana na kuchelewa kwa mkufunzi huyo.
Katibu Mkuu wa BFT, Makore Mashaga, alisema mkufunzi huyo, Azzedin Aggoune, aliwatumia taarifa za kupatwa na dharura na hivyo kutoweza kuwasili jana Ijumaa kama alivyokuwa amepanga ambapo sasa ameahidi kuwasili siku ya Jumatano..
Mashaga alisema kutoka na dharura hiyo iliyompata mkufunzi huyo wameona ni vema kuahirisha kozi hiyo na kutoa fursa kwa makocha walioteuliwa kushiriki kozi hiyo kushuhudia michuano ya ngumi ya Kova inayoendelea jijini Dar es Salaam.
"Ile kozi ya kimataifa ya ukocha wa ngumi iliyokuwa ianze Novemba 12-18 mjini Kibaha, imekwama kuanza kutokana na mkufunzi wa kimataifa toka Algeria kupatwa na dharura na kuchelewa kuja, sasa itaanza Novemba 17 huko huko Kibaha," alisema.
Mashaga alisema kozi hiyo inayotambuliwa na Shirikisho la Ngumi la Kimataifa, AIBA, itafungwa rasmi Novemba 25, ambapo washiriki watatunukiwa vyeti pamoja na wasifu wao kuwekwa kwenye database ya shirikisho hilo ili kuwaweza kutumika na kushiriki michuano yoyote ya kimataifa ya ngumi popote duniani.
Mmoja wa washiriki wa kozi hiyo, Rajab Mhamila 'Super D' alisema amefurahi kuteuliwa kushiriki kozi hiyo, akiamini itamsaidia kumpa ujuzi na kumjenga zaidi katika taaluma hiyo ya ukocha aayoifanya katika klabu za Ashanti na Amana zote za Ilala.
Mwisho
Matumla, Oswald kula X-mass ulingoni

MABONDIA wakongwe wa ngumi za kulipwa nchini, Rashid Matumla 'Snake Man' na Maneno Oswald 'Mtambo wa Gongo' wanatarajia kula Xmass wakiwa ulingoni watakapochapana katika pambano lisilo la ubingwa litakalochezwa jijini Dar es Salaam.
Wakongwe hao watapigana kwenye pambano la uzani wa Middle la raundi 10 litakalofanyika kwenye ukumbi wa Heinkein, Mtoni Kijichi na kusindikiwa na michezokadhaa ya utangulizi.
Kwa mujibu wa waratibu wa pambano hilo kampuni ya Adios Promotion kupitia afisa habari wao, Mao Lofombo ni kwamba kabla ya Matumla na Oswald kupanda ulingoni kuonyeshana kazi, mabondia Rashidi Ally na Hassan Sweet watapimana ubavu.
Lofombo alisema michezo mingine itawakutaniosha Kalulu Bakari dhidi ya Athuman Kalekwa na Shabani Kazinga ataonyeshana kazi na Kashinde.
Pambano la la nne kuwakutanisha mabondia mabingwa wa zamani, litafanyika huku kila mmoja akiwa na matokeo tofauti katika michezo yao ya mwisho ambapo Oswald alipigwa na Mada Maugo, wakati Matumla alimshinda Mkenya Ken Oyolo.
Katika michezo yao mitatu iliyopita, Matumla alimshinda Oswald mara mbili moja akimpiga kwa KO mnamo Oktoba 3, 2001 na jingine kwa pointi Oktoba 28, 2006 huku alikubali kichapo cha pointi mbele ya mpinzani wake Februari 4, 2001.
Tayari mabondia wote wameshaanza kutambiana juu ya pambano hilo, kila mmoja akijinasibu kutaka kuibuka na ushindi ili kulinda hadhi yake pamoja na kudhihirisha bado wamo katika mchezo huo licha ya umri kuwatupa mkono.
Matumla aliyewahi kuwa bingwa wa dunia wa WBU, kwa sasa ana umri wa miaka 43 miaka miwili zaidi ya mpinzani wake mwenye miaka 41 na mwenye rekodi ya kucheza mechi 64 akishinda 37, 26 kwa KO, akipigwa mara 24, 9 kwa KO na kupata sare tatu.
Mpinzani wake rekodi yake pia inaonyesha kapanda ulingoni mara 64 ameshinda mara 46 (33 kwa KO) amepoteza 16 (5 kwa KO) na kupata sare mbili.
Kwa kuangalia rekodi za mabondia hao ni wazi pambano lao lijalo litakuwa lenye mpinzani mkali kila mmoja akipenda kushinda ili kuendeleza rekodi aliyonayo katika mchezo huo wanaoendelea kuucheza karibu miaka 30 sasa.
Mwisho
Jumbe, atambia Shoka la Bucha
UONGOZI wa bendi ya Talent umedai kuwa, albamu yao mpya inayoendelea kuandaliwa itakuwa moto kuliko ile ya kwanza ya 'Subiri Kidogo' ambayo inaendelea kubamba sokoni.
Mkurugenzi wa bendi hiyo, Husseni Jumbe, alisema maandalizi wanayofanya kuipika albamu yao ya pili itakayofahamika kama 'Shoka la Bucha' ni ya aina yake kitu kinachompa jeuri kwamba itafunika kuliko ile ya awali.
Jumbe, alisema tayari wamesharekodi nyimbo nne kati ya sita za albamu hiyo katika studio za Sound Crafters na mara watakapomaliza mbili za mwisho wataanza kurekodi video kabla ya kufanya uzinduzi na kuziingiza sokoni mapema mwakani.
"Nadhani Shoka la Bucha itafunika zaidi kuliko Subiri Kidogo kwa namna tunavyoiandaa kwa sasa tukiwa tumesharekodi nyimbo nne kati ya sita," alisema.
Jumbe, alisema tayari baadhi ya nyimbo hizo zilizorekodiwa zimeshasambazwa kwenye vituo vya redio ili kurushwa hewani.
Alizitaja nyimbo zilizorekodiwa hadi sasa ni Kilio cha Swahiba, Shoka la Bucha, Kiapo Mara Tatu na Jipu la Moyo.
Aliongeza, wapo kwenye mipango ya kufanyta ziara mikoani kwa nia ya kujitangaza zaidi sambamba na kuitambulisha albamu zao mbili, ikiwemo hiyo inayomaliziwa kurekodiwa.
Mkurugenzi wa bendi hiyo, Husseni Jumbe, alisema maandalizi wanayofanya kuipika albamu yao ya pili itakayofahamika kama 'Shoka la Bucha' ni ya aina yake kitu kinachompa jeuri kwamba itafunika kuliko ile ya awali.
Jumbe, alisema tayari wamesharekodi nyimbo nne kati ya sita za albamu hiyo katika studio za Sound Crafters na mara watakapomaliza mbili za mwisho wataanza kurekodi video kabla ya kufanya uzinduzi na kuziingiza sokoni mapema mwakani.
"Nadhani Shoka la Bucha itafunika zaidi kuliko Subiri Kidogo kwa namna tunavyoiandaa kwa sasa tukiwa tumesharekodi nyimbo nne kati ya sita," alisema.
Jumbe, alisema tayari baadhi ya nyimbo hizo zilizorekodiwa zimeshasambazwa kwenye vituo vya redio ili kurushwa hewani.
Alizitaja nyimbo zilizorekodiwa hadi sasa ni Kilio cha Swahiba, Shoka la Bucha, Kiapo Mara Tatu na Jipu la Moyo.
Aliongeza, wapo kwenye mipango ya kufanyta ziara mikoani kwa nia ya kujitangaza zaidi sambamba na kuitambulisha albamu zao mbili, ikiwemo hiyo inayomaliziwa kurekodiwa.
TMK waumwa kichwa videoni

KUNDI la muziki wa kizazi kipya la TMK Wanaume Family, limeachia mtaani video yake mpya ya 'Kichwa Kinauma', ikiwa ni maandalizi ya kupakuliwa albamu mpya ya kundi hilo.
Aidha, kundi la Tip Top Connection kesho linatarajia kuadhimisha miaka 10 tangu kuanzishwa kwake kwa wasanii waliowahi kupitia katika kundi hilo na waliopo sasa kujumuika pamoja katika onyesho litakalofanyika Maisha Club Masaki, jijini Dar es Salaam.
Meneja wa kundi la TMK Wanaume Family, Said Fella 'Mkubwa Fella', alisema video ya wimbo huo ulioimbwa na wasanii Mheshimiwa Temba na Said Chegge, ni kati ya maandalizi ya kundi lao.
Mkubwa Fella alisema kukamilika kwa video ya wimbo huo ni mwanzo wa maandalizi ya upigwaji video wa nyimbo nyingine zitakazokamilisha albamu yao itakayokuwa na vibao 10 ambayo hata hivyo, hakuweza kuitaja jina lake.
"Mkubwa tumekamilisha video ya wimbo wetu mpya wa 'Kichwa Kinauma' tukiwa mbioni kufyatua video za nyimbo zetu nyingine za kukamilisha albamu ijayo ya TMK," alisema.
Mkubwa aliongeza sambamba na hilo, upande wake albamu yake ya miondoko ya taarab ya 'Kunguni Kunguni', ipo katika hatua ya mwisho kuachiwa hadharani ikiwa na nyimbo sita.
Nyimbo za albamu hiyo ya Mkubwa Fella ni 'Kusonakusonona', 'Simuachi', 'Midomo Imewashuka', 'Mchakamchaka', 'Sijapopoa Dodo' na 'Kimodern Modern'.
Nalo kundi la Tip Top Connection, moja ya makundi yanayotamba nchini, kesho litafanya onyesho maalum la kuadhimisha miaka 10 tangu kuanzishwa kwake ambalo litapambwa na burudani mbalimbali ikiwemo soka na muziki utakaotumbuizwa na wasanii mbalimbali.
Onyesho hilo litawajumuisha wasanii wote waliowahi kupitia kundi hilo na wale waliopo sambamba na wengine walioalikwa kuwapiga tafu katika maadhimisho hayo yatakayofanyika kwenye ukumbi wa Maisha Club, Masaki jijini Dar es Salaam.
Young D, Aslay wote boda kwa boda


WASANII wanaokuja juu katika anga la muziki wa kizazi kipya nchini, Aslay Isiaka 'Dogo Aslay' na David Genz Mwanjela 'Young D' wanatarajia kuonyesha kazi watakapoungana na wakali wengine wa miondoko hiyo kwenye onyesho maalum litakalofanyika leo jijini Dar.
Dogo Aslay na Young D, wanaowatishia wakongwe wa muziki huo kwa namna ya kasi yao tangu walipoibuka, watashiriki tamasha lililopewa jina la 'Boda kwa Boda Beach Concert' ambalo litafanyikia kwenye ufukwe ya Mbalamwezi.
Mbali na wasanii hao wanaochuana kimuziki sambamba na chipukizi mwingine, Abdulaziz Chende 'Dogo Janja', pia tamasha hilo litawahusisha wakali kama msanii kutoka Kenya, Jaguar anayetamba na nyimbo za 'Kigeugeu' na 'Nimetoka Mbali' alioimba na nyota wa Tanzania, Ambwene Yesaya 'AY'.
Wengine watakaoshiriki tamasha hilo la 'Bodaboda' ni 'Mzee wa Hakunaga' Sumalee, Godzilla wa Salasala, Beca, Reycho, Country Boy & Stamina, na wengineo huku wakinakshiwa muziki huo na DJ Zero.
Kwa mujibu wa waratibu wa onyesho hilo, G5 Click, wakali hao watashirikiana pamoja kuangusha moja moja kuanzia saa moja jioni hadi 'kuchwee' ili kuwapa burudani mashabiki wa muziki wa kizazi kipya watakaoungana kwenye ufukwe huo.
"Ni tamasha la aina yake siku ya Jumamosi (leo) ambapo wasanii chipukizi na wakali wengine akiwemo Mkenya Jaguar watafanya vitu vyao katika ukumbi wa Mbalamwezi Beach Club."
Subscribe to:
Posts (Atom)