STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, July 21, 2014

Diamond, WEma wote Bei Kali bhanaa!



STAA wa nyimbo za 'Bum Bum' na 'Mdogomdogo' Nasibu Abdul 'Diamond' na mpenzie wake, Wema Sepetu 'Madam' wanatarajia kucheza filamu ya pamoja iitwayo 'Bei Kali'.
Filamu hiyo ambayo inatarajiwa kuanza kushutiwa hivi karibuni inazalishwa na kampuni ya Siumulizi African Entertainment ya msanii Simon Mwapagata 'Rado'.
Rado aliliambia MICHARAZO kuwa, filamu hiyo ya mapenzi itaanza kurekodiwa baada ya kuafikia na wenzao hao ambao wamekuwa gumzo kwa mashabiki wa burudani nchini.
Mkali huyo alisema mazungumza na wawili hao yapo katika hatua nzuri na kwamba itakuwa mara ya kwanza kwa nyota hao kuuza sura kwa pamoja katika filamu.
Rado alisema mbali na Diamond na Wema pia, ndani ya filamu hiyo atakuwepo yeye mwenyewe na wasanii wengine.
"Natarajia kutengeneza filamu mpya iitwayo 'Bei Kali' ambayo miongoni mwa washiriki wake ni Diamond na Wema Sepetu na kwa sasa tupo kwenye mazungumzo ya mwisho," alisema.
Rado alisema ushiriki wa nyota hao ndani ya 'Bei Kali' utaifanya filamu hiyo kuendana na uhalisi wa jina lake kwani Diamond na Wema ni wasanii wa kiwango cha kimataifa.
"Kama wenyewe walivyo ghali, filamu ya Bei Kali inawafaa na mashabiki watarajie kumuona Diamond kivingine, kwa Wema hakuna maswali juu ya umahiri wake katika uigizaji," alisema.

Mfungo wakwamisha video ya Shaa

VIDEO ya wimbo mpya unaendelea kutamba hewani wa staa wa zamani wa kundi la Wakilisha, Sarah Kais 'Shaa' uitwao 'Subira' imekwama kutoka na sasa itatoka baada ya Idd.
Meneja wa msanii huyo, Said Fella 'Mkubwa' aliiambia MICHARAZO kuwa, video iliyotayarishwa na Adam Juma wa Next Level Production imeshindwa kuachiwa kupisha Mfungo.
Fella alisema kwa namna 'mauno' yaliyopo ndani ya video hiyo imemfanya asitishe kuiachia hewani kuhofia kuwaharibia 'swaumu' mashabiki wao na itaachiwa baada ya mfungo huo.
"Video ya Shaa iitwayo 'Subira' ambayo ilikuwa itokee na audio yake, tumeisitisha mpaka baada ya kumalizika mfungo kwa sababu ndani ya video hiyo kuna mauno sana," alisema.
Fella alisema hivyo mara baada ya kusherehekewa kwa sikukuu ya Eid el Fitri video hiyo itaachiwa hewani kwenda sambamba na audio yake ambayo imekuwa gumzo kwa sasa.
Wimbo huo wa Subira ni wa pili kwa Shaa tangu awe chini ya lebo ya Mkubwa na Wanaye, awali akitoka na singo iitwayo 'Sugua Gaga'.

Hivi ndivyo Stars ilipobanwa na Mambas Taifa

Mshambuliaji wa timu ya soka ya Tanzania, Taifa Stars, Mbwana Samatta akitafuta mbinu za kuwatoka wachezaji wa Msumbiji katika mchezo uliofanyika
kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Mbwana Samatta akiwatoka mabeki wa timu ya taifa ya Msumbiji.
Mshambuliaji nyota wa Taifa Stars, Mbwana Samatta akiwa katikati ya mabeki wa timu ya taifa ya Msumbiji. 
Mshambuliaji wa timu ya soka ya Tanzania, Taifa Stars, Thomas Ulimwengu akimtoka beki wa Msumbiji, Zainadine Junior katika mchezo uliofanyika kwenye
Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, wa kuwania tiketi ya Fainali za Afrika zitakazofanyika nchini Morocco mwakani. Timu hizo zilitoka sare ya 2-2. 
 Thomas Ulimwengu  akichuana na beki wa Msumbiji, Josemar Machaisse.
 Huniwezi…Mshambuliaji wa Taifa Stars, Thomas Ulimwengu
akimtoka beki wa Msumbiji, Zainadine Junior.
 Mshambuliaji wa Stars, Khamis Mcha akiwa katika harakati za kufunga goli.
 Golikipa wa Stars, Deogratius Munishi akishangilia bao la pili la Taifa Stars kwa kuonyesha fulana yake iliyokuwa ikisomeka ‘Sisi ni Watoto wa Rais Kikwete’.
Picha zote na francisdande

'Kipusa' cha Kaole Kwanza kuleta mapinduzi Bongo'

Mwenyekiti wa Kaole Kwanza, Ndimbagwe Misayo 'Thea'
Baadhi ya wasanii wa Kaile Kwanza katika picha ya pamoja na waalikwa wakati wa uzinduzi wa igizo lao la Kipusa hivi karibuni
Baadhi ya wasanii wa Kaile Kwanza katika picha ya pamoja na waalikwa wakati wa uzinduzi wa igizo lao la Kipusa hivi karibuni
MWENYEKITI wa kundi la Kaole Kwanza linaloundwa na nyota wa zamani wa Kaole Sanaa Group, Ndimbagwe Misayo 'Thea' amelitabiria igizo lao la 'Kipusa' kuleta mapinduzi makubwa katika fani ya uigizaji hasa michezo ya kwenye runinga.
Thea alisema hadithi ya igizo hilo linalotarajiwa kuanza kuonekana hewani hivi karibuni na namna wasanii walioshiriki walivyoitendea haki mbele ya kamera inampa 'jeuri' ya kuamini tamthilia ya 'Kipusa' itafunika sana ikianza kurushwa.
Akizungumza na MICHARAZO, Thea alisema mseto wa wasanii wazoefu na chipukizi chini ya muongozaji mahiri nchini Christant Mhenga na jinsi simulizi la igizo hilo lilivyo ni wazi litafunika na kuleta mapinduzi katika fani ya uigizaji siku za usoni.
Thea alisema Kaole Kwanza hawakukurupuka kuamua kuandaa kazi hiyo ambayo tayari ipo katika hatua ya mwisho kabla ya kurushwa na kituo kimojawapo nchini cha runinga baada ya mazungumzo ya pande mbili kwenda vizuri mpaka sasa.
"Hakukurupuka, tulikaa chini na kufikiria namna ya kusaidia kupeleka mbele gurudumu la fani ya uigizaji na kuibuka na 'Kipusa' tunataka kuwaonyesha wengine uwezo tulionao, pamoja na kusaidia kuingia kwenye ushindani wa kimataifa," alisema Thea.
Mwenyekiti huyo pia alifafanua kuwa wameamua kutumia jina la Kaole Kwanza kwa sababu asilimia kubwa ya wasanii waliibukia na kutamba kupitia Kaole Sanaa na hawakufanya hivyo kwa lengo la kuibua malumbano na wasanii wengine.
"Sisi ni Kaole Kwanza, chimbuko letu ni Kaole Sanaa...Wanaolalamika kuhusu sisi labda wana yao na hatuko kwa ajili ya kulumbana na mtu sisi kazi yetu kuwapa burudani mashabiki wa sanaa," alisema Thea baada ya kuulizwa swali kuhusu uongozi wa Kaole Sanaa kulalamika utambulisho wa kundi hilo jipya kama Kaole.

Staina, Ney wa Mitego Kwenu Vipi?


MSANII mkali wa hip hop, Stamina, kutoka mji wa Morogoro, ameachia wimbo wake mpya uitwao 'Kwenu Vipi' ambao amemshirikisha mkali mwingine wa 'michano', Ney wa Mitego.
Wimbo huo tayari umeanza kusikika hewani kupitio vituo vya redio na mitandao ya kijamii ikiwa ni kazi mpya kwa Stamina tangu alipoachia wimbo wa mwisho uitwao 'Mguu Pande Mguu Sawa' alioimba na mshindi wa BSS, Walter Chilambo.
Kwa mujibu wa Stamina, wimbo huo umetengenezwa katika studio za Seductive Records chini ya mtayarishaji mkali wa nyimbo za 'Muziki Gani' na 'Salam Zao'.
Msanii huyo anasifika kwa umahiri wa kutunga mistari 'mitamu' katika nyimbo zake na amejipatia umaarufu mkubwa kupitia nyimbo zake kadhaa zinazoendelea kutamba kwa sasa nchini.
Baadhi ya nyimbo za Stamina alizoimba mwenyewe na kushirikisha wasanii wengine ni 'Kabwela', 'Alisema', 'Najuta Kubalehe', 'Wazo la Leo', 'Mwambie Mwenzio', 'Mke wa Baba', 'Jamvi la Wageni' na 'Mapenzi'.

Saturday, July 19, 2014

HII NDIYO RATIBA YA LIGI KUU YA ENGLAND 2014-2015

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEicwtVs9kbizNkYY1qiZ27IWHZQNrcJpMm4hcWwbisc0Y9bQG-mTmarf5FzSpaOQBY-HqHwZCySf6iQ0j2lnCeqsRwwuZqoJM6xcXxLfu4qugLL0JC9fWgdtcxu7Hh0G0Rir0aKBAYDfDs/s1600/english_premier_league_2013-2014.png
KIPUTE cha Ligi Kuu ya England inatarajiwa kuanza kutimua vumbi lake kuanzia Agosti 16 mwaka huu ambapo tayari Chama cha Soka cha nchini hiyo, FA kimetoa ratiba ya awali ya ligi hiyo.
Inaitwa ratiba ya awali kwa sababu itakuwa ikiboreshwa kutegemeana na matakwa ya watangazaji wa televisheni na michuano mingine ya vikombe nchini humo.
MICHARAZO inawaletea ratiba hiyo hapo chini namna klabu 20 zitakapokuwa zikichuana kuwania taji hilo linaloshikiliwa kwa sasa na klabu ya Manchester City.

AGOSTI 16
Arsenal         v Palace
Burnley         v Chelsea
Leicester    v Everton
Liverpool    v Southampton
Man United    v Swansea
Newcastle    v Man City
QPR            v Hull City
Stoke        v Aston Villa
West Brom    v Sunderland
West Ham        v Tottenham

AGOSTI 23
Aston Villa    v Newcastle
Chelsea        v Leicester
Palace        v West Ham
Everton        v Arsenal
Hull City    v Stoke City
Man City        v Liverpool
Southampton    v West Brom
Sunderland    v Man United
Swansea        v Burnley
Tottenham    v QPR

AGOSTI 30
Aston Villa    v Hull City
Burnley        v Man United
Everton        v Chelsea
Leicester    v Arsenal
Man City        v Stoke City
Newcastle    v Palace
QPR            v Sunderland
Swansea        v West Brom
Tottenham    v Liverpool
West Ham        v Southampton

SEPTEMBA 13
Arsenal        v Man City
Chelsea        v Swansea
Palace        v Burnley
Hull City    v West Ham
Liverpool    v Aston Villa
Man United    v QPR
Southampton    v Newcastle
Stoke City    v Leicester
Sunderland    v Tottenham
West Brom    v Everton

SEPTEMBA 20
Aston Villa    v Arsenal
Burnley        v Sunderland
Everton        v Palace
Leicester    v Man United
Man City        v Chelsea
Newcastle    v Hull City
QPR            v Stoke City
Swansea        v Southampton
Tottenham    v West Brom
West Ham        v Liverpool

SEPTEMBA 27
Arsenal        v Tottenham
Chelsea        v Aston Villa
Palace        v Leicester
Hull City    v Man City
Liverpool    v Everton
Man United    v West Ham
Southampton    v QPR
Stoke City    v Newcastle
Sunderland    v Swansea
West Brom    v Burnley

OKTOBA 4
Aston Villa    v Man City
Chelsea        v Arsenal
Hull City    v Palace
Leicester    v Burnley
Liverpool    v West Brom
Man United    v Everton
Sunderland    v Stoke City
Swansea        v Newcastle
Tottenham    v Southampton
West Ham        v QPR

OKTOBA 18
Arsenal        v Hull City
Burnley        v West Ham
Palace        v Chelsea
Everton        v Aston Villa
Man City        v Tottenham
Newcastle    v Leicester
QPR            v Liverpool
Southampton    v Sunderland
Stoke City    v Swansea
West Brom    v Man United

OKTOBA 25
Burnley        v Everton
Liverpool    v Hull City
Man United    v Chelsea
QPR            v Aston Villa
Southampton    v Stoke City
Sunderland    v Arsenal
Swansea        v Leicester
Tottenham    v Newcastle
West Brom    v Palace
West Ham        v Man City

NOVEMBA 1
Arsenal        v Burnley
Aston Villa    v Tottenham
Chelsea        v QPR
Palace        v Sunderland
Everton         v Swansea
Hull City     v Southampton
Leicester    v West Brom
Man City        v Man United
Newcastle    v Liverpool
Stoke City    v West Ham

NOVEMBA 8
Burnley         v Hull City
Liverpool     v Chelsea
Man United     v Palace
QPR            v Man City
Southampton     v Leicester
Sunderland     v Everton
Swansea        v Arsenal
Tottenham    v Stoke City
West Brom    v Newcastle
West Ham        v Aston Villa

NOVEMBA 22
Arsenal         v Man United
Aston Villa     v Southampton
Chelsea         v West Brom
Palace         v Liverpool
Everton         v West Ham
Hull City     v Tottenham
Leicester    v Sunderland
Man City     v Swansea
Newcastle    v QPR
Stoke City     v Burnley

NOVEMBA 29
Burnley         v Aston Villa
Liverpool     v Stoke City
Man United     v Hull City
QPR            v Leicester
Southampton     v Man City
Sunderland     v Chelsea
Swansea        v Palace
Tottenham    v Everton
West Brom    v Arsenal
West Ham        v Newcastle

DESEMBA 2
Arsenal        v Southampton
Burnley         v Newcastle
Palace         v Aston Villa
Leicester    v Liverpool
Man United     v Stoke City
Swansea        v QPR
West Brom    v West Ham

DESEMBA 3
Chelsea         v Tottenham
Everton         v Hull City
Sunderland     v Man City

DESEMBA 6
Aston Villa     v Leicester
Hull City     v West Brom
Liverpool     v Sunderland
Man City     v Everton
Newcastle    v Chelsea
QPR            v Burnley
Southampton     v Man United
Stoke City     v Arsenal
Tottenham    v Palace
West Ham        v Swansea City

DESEMBA 13
Arsenal         v Newcastle
Burnley         v Southampton
Chelsea         v Hull City
Palace         v Stoke City
Everton         v QPR
Leicester    v Man City
Man United     v Liverpool
Sunderland     v West Ham
Swansea        v Tottenham
West Brom    v Aston Villa

DESEMBA 20
Aston Villa     v Man United
Hull City     v Swansea City
Liverpool     v Arsenal
Man City     v Palace
Newcastle    v Sunderland
QPR             v West Brom
Southampton     v Everton
Stoke City     v Chelsea
Tottenham    v Burnley
West Ham        v Leicester

DESEMBA 26
Arsenal         v QPR
Burnley         v Liverpool
Chelsea         v West Ham
Palace         v Southampton
Everton         v Stoke City
Leicester    v Tottenham  
Man United     v Newcastle
Sunderland     v Hull City
Swansea        v Aston Villa
West Brom    v Man City

DESEMBA 28
Aston Villa     v Sunderland
Hull City     v Leicester
Liverpool     v Swansea
Man City     v Burnley
Newcastle    v Everton
QPR             v Palace
Southampton     v Chelsea
Stoke City     v West Brom
Tottenham    v Man United
West Ham        v Arsenal

2015
JANUARI 1
Aston Villa     v Palace
Hull City     v Everton
Liverpool     v Leicester
Man City     v Sunderland
Newcastle    v Burnley
QPR             v Swansea
Southampton     v Arsenal
Stoke City     v Man United
Tottenham    v Chelsea
West Ham        v West Brom

JANUARI 10
Arsenal         v Stoke City
Burnley         v QPR
Chelsea         v Newcastle
Palace         v Tottenham
Everton         v Man City
Leicester    v Aston Villa
Man United     v Southampton
Sunderland     v Liverpool
Swansea City     v West Ham
West Brom    v Hull City

JANUARI 17
Aston Villa     v Liverpool
Burnley         v Palace
Everton         v West Brom
Leicester    v Stoke City
Man City     v Arsenal
Newcastle    v Southampton
QPR             v Man United
Swansea        v Chelsea
Tottenham    v Sunderland
West Ham        v Hull City

JANUARI 31
Arsenal         v Aston Villa
Chelsea         v Man City
Palace         v Everton
Hull City     v Newcastle
Liverpool     v West Ham
Man United     v Leicester
Southampton     v Swansea
Stoke City     v QPR   
Sunderland     v Burnley
West Brom    v Tottenham

FEBRUARI 7
Aston Villa     v Chelsea
Burnley         v West Brom
Everton         v Liverpool
Leicester    v Palace
Man City     v Hull City
Newcastle    v Stoke City
QPR             v Southampton
Swansea        v Sunderland
Tottenham    v Arsenal
West Ham        v Man United

FEBRUARI 10
Arsenal         v Leicester
Palace         v Newcastle
Hull City     v Aston Villa
Liverpool     v Tottenham
Man United     v Burnley
Southampton     v West Ham
West Brom    v Swansea

FEBRUARI 11
Chelsea         v Everton
Stoke City     v Man City
Sunderland     v QPR

FEBRUARI 21
Aston Villa     v Stoke City
Chelsea         v Burnley
Palace         v Arsenal
Everton         v Leicester
Hull City     v QPR
Man City     v Newcastle
Southampton     v Liverpool
Sunderland     v West Brom
Swansea        v Man United
Tottenham    v West Ham

FEBRUARI 28
Arsenal         v Everton
Burnley         v Swansea
Leicester    v Chelsea
Liverpool     v Man City
Man United     v Sunderland
Newcastle    v Aston Villa
QPR             v Tottenham
Stoke City    v Hull City
West Brom    v Southampton
West Ham        v Palace

MACHI 3
Aston Villa     v West Brom
Hull City     v Sunderland
Liverpool     v Burnley
QPR             v Arsenal
Southampton     v Palace
West Ham        v Chelsea

MACHI 4
Man City     v Leicester
Newcastle    v Man United
Stoke City     v Everton
Tottenham    v Swansea

MACHI 14
Arsenal         v West Ham
Burnley         v Man City
Chelsea         v Southampton
Palace         v QPR
Everton         v Newcastle
Leicester    v Hull City
Man United     v Tottenham
Sunderland     v Aston Villa
Swansea        v Liverpool
West Brom    v Stoke City

MACHI 21
Aston Villa     v Swansea
Hull City     v Chelsea
Liverpool     v Man United
Man City     v West Brom
Newcastle    v Arsenal
QPR             v Everton
Southampton     v Burnley
Stoke City     v Palace
Tottenham    v Leicester
West Ham        v Sunderland

MACHI 4
Arsenal         v Liverpool
Burnley         v Tottenham
Chelsea         v Stoke City
Palace         v Man City
Everton         v Southampton
Leicester    v West Ham
Man United     v Aston Villa
Sunderland     v Newcastle
Swansea        v Hull City
West Brom    v QPR

MACHI 11
Burnley         v Arsenal
Liverpool     v Newcastle
Man United     v Man City
QPR             v Chelsea
Southampton     v Hull City
Sunderland     v Palace
Swansea        v Everton
Tottenham    v Aston Villa
West Brom    v Leicester
West Ham        v Stoke City

APRILI 18
Arsenal         v Sunderland
Aston Villa     v QPR
Chelsea         v Man United
Palace         v West Brom
Everton         v Burnley
Hull City     v Liverpool
Leicester    v Swansea
Man City     v West Ham
Newcastle    v Tottenham
Stoke City     v Southampton

APRILI 25
Arsenal         v Chelsea
Burnley         v Leicester
Palace         v Hull City
Everton         v Man United
Man City     v Aston Villa
Newcastle    v Swansea
QPR             v West Ham
Southampton     v Tottenham
Stoke City     v Sunderland
West Brom    v Liverpool

MEI 2
Aston Villa     v Everton
Chelsea         v Palace
Hull City     v Arsenal
Leicester    v Newcastle
Liverpool     v QPR
Man United     v West Brom
Sunderland     v Southampton
Swansea        v Stoke City
Tottenham    v Man City
West Ham        v Burnley

MEI 9
Arsenal         v Swansea
Aston Villa     v West Ham
Chelsea         v Liverpool
Palace         v Man United
Everton         v Sunderland
Hull City     v Burnley
Leicester    v Southampton
Man City     v QPR
Newcastle    v West Brom
Stoke City     v Tottenham

MEI 16
Burnley         v Stoke City
Liverpool     v Palace
Man United     v Arsenal
QPR             v Newcastle
Southampton     v Aston Villa
Sunderland     v Leicester
Swansea City     v Man City
Tottenham    v Hull City
West Brom    v Chelsea
West Ham        v Everton

MEI 24
Arsenal         v West Brom
Aston Villa     v Burnley
Chelsea         v Sunderland
Palace         v Swansea
Everton         v Tottenham
Hull City     v Man United
Leicester    v QPR
Man City     v Southampton
Newcastle    v West Ham
Stoke City     v Liverpool

Romelu Lukaku kutua jumla Goodson Park

http://worldsoccertalk.com/wp-content/uploads/2013/10/romelu-lukaku.png
KLABU ya Everton inajiandaa kumrejesha tena klabuni mshambuliaji wake nyota Romelu Lukaku alioyekuwa akiichezea timu hiyo kwa mkopo toka Chelsea baada ya dili lake la kwenda kujiunga Atletico Madrid kuota mbawa.
Mbelgiji huyo ni mshambuliaji chaguo la kwanza la kocha Roberto Martinez  majira haya ya kiangazi na anatarajia kukamilisha usajili wake ndani ya saa 48 zijazo.
Martinez, aliyekuwa anamfikiria Demba Ba kama mbadala wa Lukaku, ila hakukubaliana na mshahara aliodai wa paundi elfu 80 kwa wiki, na sasa anataka kumshawishi mbelgiji mwenye miaka 21 kumwaga wino katika kikosi chake cha msimu ujao.
Inafahamika kuwa maandalizi makubwa ya kumrudisha Everton yamekamilika baada ya kurejea kutoka Austria walipoweka kambi.
Lukaku alikuwa anatarajia kusaini Atletico Madrid, lakini kwa bahati mbaya ikawa tofauti kwasababu hakuwa chaguo la kwanza la kocha Diego Simeone.
Wolfsburg  pia walionesha nia kubwa ya kumsajili kama ilivyokuwa kwa Tottenham, lakini Lukaku alifurahia maisha  Goodison na anapenda kuendelea kuisaidia klabu hiyo mpaka kufuzu ligi ya mabingwa.
Martinez pia amefanya mazungumzo ya kumrudisha mchezaji aliyekuwa kwa mkopo, Monaco, Lacina Traore sambamba na kuzungumza na kiungo wa Bosnia ,Muhamed Besic, mwenye miaka 21, anayekipiga klabu ya Ferencvaros.

Yaya Toure akata mzizi wa fitina adai haendi kokote

http://content.mcfc.co.uk/~/media/Images/Shared/Players/Players1213/First%20Team%20Player%20Profiles/Yaya_Toure.ashx?h=700&mh=700&mw=800&w=800LICHA ya awali kuelezwa hafurahii maisha ndani ya Manchester City hasa baada ya kukerwa na viongozi wake kuipuuza sikua yake ya kuzaliwa, Kiungo nyota wa mabingwa hao wa soka wa England, Yaya Toure amesema hana mpango wa kuondoka katika timu hiyo.
Awali kulikuwa na tetesi kwamba mahasimu wa City, Mashetani Wekundu Manchester United walikuwa wakimvizia ili kumnyakua, lakini mchezaji huyo ameweka bayana kwamba atasalia klabuni hapo kwa msimu mwingine ujao.
Toure alinukuliwa na kituo cha Sky Sport kuwa mashabiki wa timu hiyo wamekuwa wema kwake na kwa familia hivyo ameona ni bora abaki kwa ajili yao. 
Vyombo vya habari vimekuwa vikimhusisha kiungo huyo kuhamia katika vilabu mbalimbali toka wakala wake Dimitry Seluk alipoandika katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa twitter kuwa nyota huyo hajatulia. 
Seluk alitoa madai kuwa nyota huyo wa kimataifa wa Ivory Coast hakupewa utambulisho rasmi na klabu katika siku yake ya kuzaliwa wakati wa safari yao ya Abu Dhabi huku Toure mwenyewe akiunga mkono kauli hiyo. 
Toure amesema kwa sasa mambo yote yako sawa na baada ya tetesi nyingi kuzungumziwa juu yake anajipanga kufanya kitu kwa ajili ya mashabiki. 
Nyota huyo alijiunga na City akitokea Barcelona mwaka 2010 na haraka alijitengenezea jina na kuwa mchezaji tegemeo akiisaidia City Kombe la FA mwaka 2011 na mataji mawili ya Ligi Kuu mwaka 2012 na 2014.

Kuziona Stars na Mambas ni Sh 7,000 tu

http://kandanda.galacha.com/wp-content/themes/LondonLive/thumb.php?src=http://kandanda.galacha.com/wp-content/uploads/2014/06/TAIFA1.jpg&w=467&h=278&zc=1&q=100
MASHABIKI wa soka watazishuhudia timu za taifa za Tanzania, Taifa Stars na Mambas ya Msumbiji kwa Kiingilio cha Sh. 7,000 tu katika pambano hilo litakalochezwa kwenye uwanja wa Taifa kesho kuwania nafasi ya kutinga kwenye makundi ya kwenda kwenye Fainali za Kombe la Afrika 2015 zitakazofanyika nchini Morocco.

Kwa mujibu wa Afisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania, TFF, Boniface Wambura, viingilio kwa mechi hiyo vitakuwa bni sh. 7,000 na sh. 30,000 kwa viti maalumu 4,500 tu.
Kuanzia asubuhi ya leo Jumamosi tiketi za kielektroniki zimeanza kuuzwa pia katika magari maalumu kwenye vituo vya Buguruni Shell, Dar Live Mbagala, Ferry Magogoni, Kigamboni, OilCom Chang’ombe, OilCom Ubungo, Shule ya Sekondari Benjamin Mkapa (Kariakoo), TCC Club Chang’ombe na Uwanja wa Taifa.

 Aidha tiketi zinapatikana kupitia M-PESA kwa kupiga *150*00# kisha bonyeza 4, bonyeza tena 4 kisha weka namba ya kampuni 173399 kisha ingiza 7000 kama namba ya kumbukumbu ya malipo, kisha andika tena 7000 kwenye weka kiasi, kasha weka namba ya siri na baadaye bonyeza  1 kukubali.

 Utapokea ujumbe wenye orodha ya vituo vya MaxMalipo vya kuchukua tiketi ukiwa na namba ya uhakiki wa malipo yako.

 Vituo vya MaxMalipo vya kuchukulia tiketi ni mgahawa wa Steers uliopo mtaa wa Samora/Ohio, maduka makubwa ya Uchumi Supermarket (Quality Centre, Tabata Segerea na kituo cha daladala Makumbusho), Sheer Illussions (Millennium Tower na Mlimani City), maduka makubwa ya TSN Supermarket (City Centre, Kibo Tegeta na Upanga).

 Vodashop (Ubungo na Mill Pamba), Shop Mwenge (Born to Shine), Puma Petrol Station (Mwenge na Uwanja wa Ndege), Engen Petrol Station (Mbezi Beach), Big Bon Petrol Station (Kariakoo, Sinza Mori, Mbagala na Temeke), YMCA (Posta Mpya), City Sports Lounge (Posta), Uwanja wa Taifa) na Uwanja wa Karume.

Hatari! Kijana aua mtoto na kula ubongo wake


Askari kanzu wa kituo cha Polisi Himo wakiwa wamemkamata Lawrence Mramba anayetuhumiwa kumuua mtoto wa miaka 9 na kula ubongo wake. PICHA | DIONIS NYATO.

Moshi.  

MKAZI mmoja wa Moshi amemuua mwanafunzi wa darasa la 3 kule Samanga leo na kisha 'kula ubongo' wa mtoto huyo katika tukio la kutisha lililostua wakazi wa mji huu.

Kijana huyu aliyefahamika kwa jina la Lawrence Mramba, 20, alimshambulia mtoto huyo mwenye umri wa miaka 9 kwa panga wakati akienda shule mnamo saa 1 asubuhi Ijumaa, akampasua kichwa na kisha akaanza kutafuna ‘vipande vya ubongo wake.’

Mara baada ya kitendo hicho cha kushtusha, Mramba, aliyeonekana kuwa na matatizo ya akili, alianza kujikatakata sehemu zake za siri na wembe, huku akitafuna vipande vya mwili wake mwenyewe, kimoja baada ya kingine.

Baadhi ya mashuhuda wanadai kijana huyo ‘alionyesha kuwa na nguvu za ajabu’, huku wanakijiji wenzake wakishindwa kabisa kumdhibiti.

Wengi walilazimika kuketi kando wakimtazama jinsi anavyojikata wakishindwa kujua cha kufanya.

Iliwabidi polisi waingilie kati sakata hilo na hatimaye wakifanikiwa kumthibiti kijana huyo.

Hata hivyo, Mramba alifariki dunia muda mfupi baadaye katika hospitali ya Kilema wakati akipewa matibabu ya dharura kutokana na kupoteza damu nyingi.

MWANANCHI

Phillip Lahm atangaza kustaafu soka baada ya taji

http://www.dfb.de/fileadmin/Image_Archive/News/145498756-1_02_34170_p880722.jpg
NAHODHA wa timu ya taifa ya Ujerumani, Philipp Lahm ametangaza kustaafu kutoka soka la kimataifa ikiwa ni siku chache tangu alipoiongoza nchi yake kunyakua taji la nne la Kombe la Dunia katika Fainali zilizofanyika nchini Brazil.
Kwa mujibu wa taarifa zilizothibitishwa na Shirikisho la Soka Ujerumani – DFB, beki huyo wa Bayern Munich mwenye umri wa miaka 30 amefanya uamuzi huo, baada ya kumpigia simu rais wa DFB Wolfgang Niersbach.
Niersbach alimshukuru kwa mchango wake wa miaka kumi katika timu ya Ujerumani ambapo pia aliibuka kuwa kielelezo kwa chipukizi wengine. Kushinda Kombe la Dunia ni kama kilele cha kazi yake ya kandanda kufikia sasa, ambayo inajumuisha pia taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya, mataji sita ya Bundesliga na sita ya Kombe la Shirikisho la Soka Ujerumani.
Lahm alianza kazi yake ya kandanda mnamo Februari 2004 katika ushindi wao wa mabao mawili kwa moja dhidi ya Croatia. Kisha akaichezea Ujerumani mechi 113 na kufunga magoli matano. Kabla ya kushinda Kombe la Dunia la 2014, Lahm na timu yake waliibuka washindi wa tatu Kombe la Dunia mwaka wa 2006 na 2010, na wakawa makamu bingwa wa dimba la Euro 2008. Pia alicheza katika Euro 2004 na 2012.
Mkataba wa Lahm na mabingwa wa Bundesliga Bayern ulirefushwa kabla ya Kombe la Dunia na utakamilika mwaka wa 2018.

Pacquiao kuzipiga na Chris Algieri

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg893Gr1QfgTI6wsqE0zCvIUweOOMP-5aNTy5PpKPKp8iwEAwUDWdOAz48TAB8Rn4-LmlFt2mvdw_Um8VpEclGO8hM08oW9Dk5gS9MDvzrSiAgl05r0cGmsdQRn3a0UKyfERey7WO1AJgo/s1600/manny+pacquiao.jpg
Manny Pacquiao
http://fightnews.ru/files/u12355/algieri_01_0.jpg
Chris Algieri
BONDIA Mfilipino Manny Pacquiao (35) atarejea ulingoni Nov. 22 kutetea taji lake la World Boxing Organisation (WBO) uzani wa welterweight dhidi ya bondia wa Marekani ambaye hajawahi kupoteza pambano Chris Algieri litakalofanyika Macau, promota wake Bob Arum amesema.
Ukumbi wa Venetian Macao, ambao Pacquiao mwenye rekodi ya kushinda mapambano 56 kupigwa matano na sare 2 alipata ushindi wa pointi dhidi ya Bondia Mmarekani Brandon Rios Novemba mwaka jana, ndiyo utakaofanyikia pambano hilo.
Aprili mwaka huu, Pacquiao alipata ushindi wa pointi dhidi ya Timothy Bradley na kutetea taji lake la WBO welterweight na kulipa kisasi cha kupigwa kiutata dhidi ya Mmarekani huyo Juni 2012.
"Tumesaini dili. Kwa upande wangu, halikuwa dili gumu hata kidogo," Arum aliambia ESPN.com.
Algieri (30), ambaye ni mpiganaji wa 'kick-boxing', ana rekodi ya kupigana mapambano 20 na kushinda yote na alitwaa taji la WBO light-welterweight mwezi uliopita kwa pointi dhidi ya Mrusi Ruslan Provodnikov

Friday, July 18, 2014

Maximo ashikilia hatma ya wachezaji wa3 Yanga

Kocha Marcio Maximo
Kikosi cha Yanga
IMEFAHAMIKA kuwa wachezaji watatu wa kigeni wa klabu ya Yanga kiungo Haruna Noyinzima na washambuliaji wawili wa kimataifa wa Uganda Hamisi Kiiza Diego na Emmanuel Okwi hatima yao ya kuendelea kuitumikia klabu hiyo yenye maskani yake katika makutano ya mitaa ya Twiga na Jangwani iko mikononi mwa kocha mpya wa klabu hiyo Mbrazil Marcio Maximo. 
Habari zilizoifikia rockersports kutoka kwa mmoja wa viongozi wa klabu hiyo ambaye hakutaka jina jina lake kutajwa mtandaoni humu, amesema ujio wa wachezaji wawili kutoka nchini Brazil mshambuliaji Geilson Santos Santana "Jaja" na Kiungo mshamabuliaji Andrey Marcel Ferreira Coutinho kunawaondoa mmoja wa wachezaji wa kigeni kutoka ukanda huu wa Afrika mashariki kwa kuwa wachezaji hao wa Brazil walioletwa na Maximo si wa majaribio bali wamekuja kufanya kazi.
Chanzo hicho kimesema kwa mujibu wa kanuni za usajili za shirikisho la soka nchini TFF ni dhahiri wachezaji wa kigeni wanatakiwa watano na mpaka sasa Yanga imefikisha idadi ya wachezaji saba hivyo basi kuna hatari kati ya Niyonzima na Okwi mmoja akaondoka Jangwani msimu huu.
Taarifa zaidi zinasema kumekuwepo na mazungumzo yanayo endelea baina ya wachezaji hao na kamati ya usajili ya klabu hiyo ambayo kimsingi yanagusa juu ya namna ya kumalizana nao huku zoezi hilo likikumbwa na presha kubwa kutoka kwa mashabiki wa klabu hiyo.
Rockersports

Jose Mourinho amchokonoa Wenger kuhusu Sami Khedira

Sami Khedira
KLABU ya Chelsea imepata nguvu mpya ya mapambano ya kupata saini ya Sami Khedira kufuatia wakala wake kudai kuwa hakuna mazungumzo yoyote yaliyofikiwa mpaka sasa na Arsenal.
Meneja wa 'The Blues' Jose Mourinho amefanikisha usajili wa mlinzi wa kushoto Filipe Luis akitokea Atletico Madrid kwa ada ya uhamisho ya pauni milioni £18 na sasa anajipanga kwa ajili ya kiungo wa kimataifa wa Ujerumani Khedira.
Hapo kabla ilikuwa imefahamika kuwa Arsenal imekamilisha dili la uhamisho wa kiungo huyo mwenye umri wa miaka 27 kwa ada ya pauni milioni £20, lakini walikwama kufikia makubaliano ya mshahara wake wa wiki ambao nyota huyo alikuwa akitaka zaidi ya pauni £180,000.
Amekaririwa wakala wa Khedira, Jorg Neubauer akisema 
 ‘Hatuko kwenye mazungumzo na Arsenal. Sidhani kama ada itakubalika, vinginevyo wange kwisha kunipatia taarifa.’
Khedira amekuwa akimpendeza Mourinho tangu wakati huo akiwa bosi wa Real na inaelezwa kuwa huenda Mourinho akamvuta Stamford Bridge.
Recruit: Chelsea boss Jose Mourinho has already acquired Diego Costa and Filipe Luis
Usajili: Bosi wa Chelsea Jose Mourinho amesha msajili Diego Costa na Filipe Luis

Wakati hayo yakiwa hivyo, Chelsea imethibitisha makubaliano na mlinzi wa kushoto wa Atletico Fillipe Luis.
Mlinzi huyo mwenye umri wa miaka 28 atakamilisha uhamisho wake baada ya kufanikisha kipimo cha afya na makubaliano ya maslahi binafsi.
Usajili wa Mourinho unaendelea akiwa bado katika ushawishi kwa Khedira, matumaini yake ya kumsajili Antoine Griezmann aliyethaminishwa kwa pauni £20 na klabu yake ya Real Sociedad huenda yakagonga mwamba kufuatia upinzani mkubwa kutoka kwa vilabu vya Monaco na Liverpool.
Blue: Chelsea have confirmed the signing of Brazilian defender Filipe Luis (left)
Chelsea imethibitisha kumsajili mlinzi wa kibrazil Filipe Luis

Serengeti Boys wapo njema kuwavaa Amajimbos U17

KOCHA Mkuu wa Serengeti Boys, Hababuu Ali Omari amesema morali ya wachezaji wake ipo juu kwa ajili ya mechi dhidi ya Afrika Kusini (Amajimbos) itakayochezwa leo.
Mechi hiyo ya kwanza ya raundi ya pili ya michuano ya Afrika kwa vijana wenye umri chini ya miaka 17 itafanyika kwenye Uwanja wa Azam Complex uliopo Chamazi jijini Dar es Salaam kuanzia saa 10 jioni. 
Akizungumza kwenye mkutano na waandishi wa habari kwenye ofisi za TFF jijini Dar es Salaam, Kocha Hababuu amesema nia ya kikosi chake ni kuhakikisha wanafika kwenye fainali za Afrika zitakazofanyika mwakani nchini Niger. 
“Tunaiheshimu Afrika Kusini, lakini hatuiogopi. Morali ya wachezaji ipo juu na wanajiamini. Kimsingi wanajua kuwa hii ndiyo njia ya wao kutokea kwenye mpira wa miguu, kwa hiyo lengo ni kushinda,” amesema Kocha Hababuu. 
Naye Kocha wa Afrika Kusini, Molefi Ntseki amesema anaziheshimu timu za Tanzania, na changamoto aliyonayo ni kuhakikisha kuwa anashinda mechi hiyo kwani mara ya mwisho kwa timu yake kushiriki fainali za Afrika ilikuwa miaka sita iliyopita. Kiingilio katika mechi hiyo ni sh. 2,000 na tiketi zitapatikana uwanjani kwenye magari maalumu.

Mambas kutua mchana huu kuwafuata Stars Taifa

http://cdn1.portalangop.co.ao/angola/pt_pt/files/highlight/2014/2/10/0,278d8f7f-0422-46b1-b24f-eba7dd500a60--r--NjQweDM0Mw==.jpg
Kikosi cha Mambas
KIKOSI cha Mambas toka Msumbiji inatarajiwa kuwasili mchana huu tayari kwa pambano lao dhidi ya timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars litakalochezwa Jumapili, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. 
Mambas itatua Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) saa 7.30 mchana kwa ndege ya LAM ikiwa na msafara wa watu 37 ambapo kati ya hao, 25 ni wachezaji. 
Wachezaji watakaokuwa kwenye msafara huo ni; Almiro Lobo, Apson Manjate, Bone Mario Uaferro, Dario Ivan Khan, Edson Sitoe, Eduardo Jumisse, Gelicio Aurelio Banze, Helder Pelembe, Josemar Machaisse, Elias Pelembe, Isac Carvalho na Jeffrey Constatino. 
Wengine ni Manuel Fernandes, Manuel Uetimane, Mario Sinamunda, Momed Hagi, Reginaldo Fait, Reinoldo Mandava, Ricardo Campos, Saddan Guambe, Simao Mate Junior, Soares Victor Soares, Stelio Ernesto, Vando Justino na Zainadine Junior. 
Timu hiyo itafikia kwenye hoteli ya Accomondia, na itaondoka Jumapili mara baada ya kumalizika kwa mechi hiyo itakayochezeshwa na mwamuzi Mahmoud Ashour.

UJERUMANI YAKWEA KILELE UBORA DUNIANI, TANZANIA HAIJAMBO

Mabingwa wapya wa Dunia, Ujerumani
MABINGWA wapya wa Dunia, Ujerumani imepaa hadi kileleni mwa viwango vya ubora wa soka duniani ikiwa ni mara ya kwanza kwao katika miaka 20, FIFA ilitangaza jana.
Ushindi wa 1-0 katika mechi ya fainali umewainua hadi nafasi ya kwanza katika orodha ya viwango hivyo, nafasi moja juu ya wapinzani wao wa mechi ya fainali, Argentina, ambao wamepanda kwa hatua tatu hadi nafasi ya pili.
Uholanzi wamepaa kwa hatua 12 hadi kushika nafasi ya tatu kufuatia mwendo wao mzuri uliowashuhudia wakimaliza wa tatu katika Kombe la Dunia nchini Brazil.
Hispania wamelipa gharama ua kushindwa kusonga mbele kutoka katika hatua ya makundi nchini Brazil kwa kuanguka kutoka katika nafasi ya kwanza hadi ya nane, huku Colombia, Ubelgiji na Uruguay zikichukua nafasi za juu yao.
Wenyeji Brazil, waliosambaratishwa kwa magoli 7-1 dhidi ya Ujerumani katika nusu fainali katika matokeo yaliyostua zaidi kwenye michuano hiyo, wameanguka kwa hatua nne hadi kushika nafasu ya saba.
England wameanguka kwa hatua 10 hadi kushika nafasi ya 20 katika orodha hiyo ya viwango, nafasi ambayo ni ya chini zaidi kwao tangu Mei 1996, baada ya mwendo mbaya kwenye Kombe la Dunia ambao vipigo katika mechi mbili za ufunguzi ziliwapa rekodi mbaya zaidi katika miaka 50.
Katika orodha hizo Tanzania imejitoa kimasomaso kwa kukwea kwa nafasi saba kutoka nafasi ya 113 mpaka 106 huku kwa upande wa Afrika nako kukiwa na mabadiliko kwa Algeria kuongoza kwa kuwa katika nafasi ya 24 walikufuatiwa na waliokuwa vina Ivory Coast katika nafasi ya 25.
'Top 10' ya Dunia inaongozwa na 1. Ujerumani, 2. Argentina, 3. Uholanzi, 4. Colombia, 5. Ubelgiji, 6. Uruguay, 7. Brazil, 8. Hispania, 9. Uswisi, 10. Ufaransa.
Tanzania imepaa kwa nafasi hatua 7 hadi kushika nafasi ya 106 duniani wakati wapinzani wao wa Jumapili kwenye kuwania kufuzu kwa hatua ya makundi ya kuwania kucheza fainali za Mataifa ya Afrika 2015, Msumbiji nao wakipaa kwa hatua nne hadi kushika nafasi ya 114 duniani.
5-Bora ya Ukanda wa Afrika Mashariki na Kati inaongozwa na Uganda inayoshika nafasi ya 87 duniani, Kenya (95, duniani), Tanzania (106), Rwanda (109) na Ethiopia (110).
'Top 10' ya Afrika inaundwa na Algeria inayoshika nafasi ya 24 duniani, Ivory Coast (25, duniani), Nigeria (34), Misri (36), Ghana (38), Tunisia (42), Guinea (51), Cameroon (53), Burkina Faso (58) na Mali wanaoshika nafasi ya 60 duniani.

 

Miili 100 yaokotwa ajali ndege 'iliyodunguliwa' Ukraine


Mabaki ya miili zaidi ya 100 yameokotwa jirani na eneo ilipoanguka ndege ya Malaysian Airlines kule Grabovo jirani na mpaka wa Ukraine na Urusi . 

 
Reuters iliripoti mapema Alhamisi kuwa ndege hiyo yenye namba MH17 ilianguka jimboni Donetsk ikiwa njiani kuelekea Kuala Lumpur ikitokea mjini Amsterdam, Uholanzi.
 
Kuna taarifa zisizo rasmi kuwa ndege hiyo ‘imetunguliwa’ na aidha majeshi ya Ukraine, ama waasi wanaoiunga mkono Urusi, vyanzo mbalimbali vya habari vimeripoti.
 
Waokoaji wamesema miili imeokotwa katika eneo la umbali unaozidi kilometa 15 toka ndege ilipoanguka.
 
“Hatuwezi kuthibitisha kama ndege hiyo imetunguliwa ama la,” alisema Rais wa Ukraine Petro Poroshenko.
 
“Hata hivyo, tunasisitiza kuwa Ukraine haijarusha makombora yoyote angani leo,” aliongeza.
 
Katika taarifa iliyotolewa mapema leo, Malaysian Airlines ilidai ilipoteza mawasiliano na ndege hiyo mnamo saa 8 na dakika 15 GMT.
 
Tovuti ya The Guardian inaripoti kuwa vyanzo toka ndani ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Ukraine vinadai ndege hiyo ilitunguliwa na kombora toka mfumo wa kurusha roketi hewani unaojulikana kama BUK.
 
Teknolojia ya BUK ilikuwa maarufu sana Urusi miaka ya 1970, na ilirithiwa na bado yaendelea kutumika na zile zilizokuwa Jamhuri za Kisovieti, ikiwamo Ukraine.
 
Wachambuzi sasa wanahoji walorusha kombora hilo wamelipataje, huku baadhi wakidai hiyo ni uthibitisho tosha kuwa waasi wanaoiunga mkono Urusi wako nyuma ya ‘shambulizi’ hilo.
 
Kati ya watu 295 walokuwa ndani ya ndege hiyo aina ya Boeing 777, 280 walikuwa abiria na walobaki ni wahudumu na marubani.
 
Picha zilizotupwa katika mitandao ya kijamii na tovuti mbalimbali zinaonyesha masalia ya ndege hiyo yenye rangi za bluu na nyekundu yakifuka moshi.


Picha hizo zimeamsha hisia kali, zikiukumbusha umma kuhusu ajali nyingine inayohusisha ndege ya Malaysia namba MH370 ilopotea toka Machi, huku ikiwa haijaonekana.
 
Mataifa mbalimbali yanaendelea na jitihada za kutathmini kama raia wake walikuwamo ndani ya ndege ‘ilotunguliwa,’ huku baadhi ya mashirika ya ndege, ikiwemo Emirates, Lufthansa, British Airways na Aeroflot, yakisitisha safari zote kwenya anga la Ukraine.

Chanzo: Mwananchi

Hii ndiyo idadi ya waliokufa ajali kati ya Januari-Juni 2014

mpinga
Kamanda Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Mohammed Mpinga akiweka mambo hadharani
  TATHIMINI YA MATUKIO YA AJALI ZA
 BARABARAN JAN-JUNE 2013/2014

Takwimu zinaonyesha kuwa juhudi zetu zimefanikiwa kwa kupunguza ajali na majeruhi, ingawa kuna ongezeko la watu waliofarika katika ajali kwa Jan – June 2014.
S/N0
JAN-JUNE 2013 JAN –JUNE 2014 ONG/PUNG (%)
1 IDADI YA AJALI 11,311 8,405 -          2,906     (26%)
2 VIFO 1,739 1,743                  4   (0.2%)
3 MAJERUHI 9,889 7,523 -          2,366     (24%)


 MIKOA ILIYOONGOZA KWA AJALI ZA BARABARANI KIPINDI JAN-JUNE 2014:-

i)        Kinondoni   – idadi ya ajali      2,140 (25.5%)
ii)      Ilala              - idadi ya ajali – 1,561 (18.6%)
iii)    Temeke      - idadi ya ajali – 1,351 (16.1%)
iv)    Morogoro     –  idadi ya ajali – 514 (6.1%)
v)      Kilimanjaro – idadi ya ajali – 332 (4%)

Kwa mkoa wa DSM peke yake ni ajali 5,052 ( 60.2%)

MIKOA ILIYOONGOZA KATIKA KUPUNGUZA IDADI
YA AJALI ZA BARABARANI KIPINDI JAN-JUNE 2013/2014

MKOA Jan-June 2013 Jan-June 2014 Punguzo

Kinondoni 3059 2140      919 (30%)

Pwani 738 303      435 (59%)

Arusha 563 164      399 (71%)
4 Kilimanjaro 697 332      365 (52%)
5 Morogoro 631 514      117 (19%)

    TAKWIMU ZA MAKUNDI YALIYOATHIRIKA
NA AJALI ZA BARABARANI KIPINDI JAN-JUNE 2013/2014.

     JAN-JUNE 2013 JAN- JUNE 2014      TOFAUTI
KUNDI VIFO MAJERUHI VIFO MAJERUHI VIFO MAJERUHI
MADEREVA 124 725 117 527 -7 -198
ABIRIA 476 4,112 529 3,135 53 -977
W/PIKIPIKI 359 2,460 358 1,928 -1 -532
W/BAISKELI 202 560 177 304 -25 -256
W/MIGUU 550 1,926 548 1,603 -2 -323
W/MIKOKOTENI 28 106 14 26 -14 -80
JUMLA 1,739 9,889 1,743 7,523 4 -2,366
AJALI ZA PIKIPIKI- JAN-JUNE 2013/2014.
 Takwimu zinaonyesha kuwa tumeweza kupunguza ajali, vifo na majeruhi katika ajali za Pikipiki kwa kipindi cha Jan-June 2013 ikilinganishwa na Jan- June 2014.
Jan-June       2013 Jan-June 2014 ONG/PUNG
IDADI YA PIKIPIKIZILIZOHUSIKA 3,720 3,170 -          550 (15%)
IDADI YA AJALI 3016 2402 -          614 (20%)
VIFO 457 423 -          34 (7%)
MAJERUHI 2963 2301 -          662 (22%)

Hemed, Senga waonja Pishi la Kajala

MSANII nyota wa filamu nchini Hemed Suleiman anatarajiwa kuonekana katika kazi mpya ya Kajala Masanja iitwayo 'Pishi'.
Filamu hiyo miongoni mwa filamu tatu zilizoandaliwa na mwanadada huyo kupitia kampuni yake ya Kay Entertainment na imewashirikisha wasanii wengine nyota wakiwamo wachekeshaji mahiri nchini Senga, Asha Boko, Tausi na Mzee Onyango.
Akizungumza na MICHARAZO, Kajala alisema tofauti na filamu yake anayotarajia kuiachia hivi karibuni ya 'Laana', ndani ya Pishi ni ucheshi mtupu na yeye mwenyewe akiicheza kikomedi.
"Wengi wanadhani Kajala ni sistaduu aliyezoea kucheza filamu za kimapenzi tu, ndani ya 'Pishi' ni vunja mbavu mwanzo mwisho ikikusanya 'vichwa' adimu kama Asha Boko, Senga, Onyango na wengine," alisema.
Alidokeza filamu hiyo mpya itatoka mwishoni mwa mwezi ujao ili kutoa nafasi ya filamu yake ya 'Laana' iliyoigizwa na wasanii kama Ahmed Salim 'Gabo', Mama Sonia, Mama Kawele na Pastor Myamba kupata nafasi sokoni.

Toni Kroos atambulishwa Real Madrid

Done deal: Kroos holds up his No 8 shirt at his unveiling in Madrid
Toni Kroos akiwa na jezi yake mpya ya Real Madrid

Golden boy: The former Bayern Munich man was integral during Germany's World Cup triumph
Kroos akipiga akionyesha maufundi yake

MCHEZAJI Toni Kroos amekamilisha uhamisho wake wa Pauni Milioni 24 kujiunga na Real Madrid kutokea kwa mabingwa wa Ujerumani, Bayern Munich.
Bayern walitangaza jana usubuhi kuwa wamefikia makubaliano na Real juu ya mchezaji huyo na uhamisho utafanyika mara moja.
Mkataba wa Kroos ilikuwa unamalizika majira ya kiangazi mwakani na mshindi huyo wa Kombe la Dunia amesaini mkataba wa miaka sita katika dimba la Santiago Bernabeu.
Kroos alitambulishwa rasmi jana na hapa chini ni baadhi ya picha zilizopigwa katika utambulisho wake ndani ya dimba la Bernabeu.
Kroos ametua Real akiiacha kwenye mataa klabu ya Manchester United iliyokuwa ikimfukuzia.

DIEGO COSTA AJIFUNGA MITANO DARAJANI

MSHAMBULIAJI wa Atletico Madrid, Diego Costa amekamilisha usajili wa kujiunga na Chelsea kwa kusaini mkataba wa miaka mitano na klabu hiyo ya London.
Ada ya uhamisho ya mshambuliaji huyo inaaminika kuwa ni paundi milioni 32.
"Nina furaha sana kujiunga na Chelsea," alisema Costa. "Kila mmoja anafahamu kwamba hii ni klabu kubwa katika ligi ya ushindani mkubwa na nina furaha sana kuanza maisha mapya nchini England."
Costa anakuwa mchezaji wa tatu kutua Chelsea kufuatia kusajiliwa kwa Cesc Fabregas kutoka Barcelona na Mario Pasalic (19) kutoka klabu ya Croatia ya Hajduk Split.
Mshambuliaji huyo alifunga magoli 36 katika mechi 52 alizochezea Atletico Madrid msimu uliopita ambao walitwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Hispania kwa mara ya kwanza tangu 1996 na walifika hatua ya fainali ya Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya.
BBC

Ze Gunners wazidi kujiimarisha England

Striking a pose: Debuchy said he was excited to be playing Champions League football again
KLABU ya Arsenal imezidi kujiimarisha kwa kumsajili beki wa kulia wa Ufaransa, Mathieu Debuchy kutokea klabu ya Newcastle United.
Debuchy, 28, amesajiliwa kwa nia ya kuziba pengo la beki wa kulia, Mfaransa mwenzake, Bacary Sagna aliyetimka Emirates na kujiunga na mabingwa wa Ligi Kuu, Manchester City majira haya ya kiangazi mwaka huu.
Debuchy alijivunia usajili huo na akasisitiza kuwa umuhimu wa ligi ya mabingwa ndio kichocheo cha yeye kujiunga na Asernal.
“Najivunia kujiunga na klabu kubwa kama hii na kuvaa rangi zake, ni moja ya klabu kubwa zaidi duniani,” beki huyo wa kulia aliuambia mtandao wa Asernal.com.
“Naangalia mbele nikiwa na Aserne Wenger na kuisaidia timu kuendeleza mafanikio ya msimu uliopita ya kutwaa kombe la FA”.
“Kucheza tena ligi ya mabingwa ni furaha kubwa kwangu na nitajitahidi kadri ya uwezo wangu kuisaidia Asernal kushindania kombe”
Debuchy amewasili  Arsenal kurithi mikoba ya Bacary Sagna ambaye hakuonesha kiwango kikubwa katika fainali za Kombe la Dunia akiwa na Ufaransa.
Kutua kwa mcjhezaji huyo kumekuja siku chache baada ya kumnasa mshambuliaji nyota wa Barcelona, Alexis Sanchez kutoka Chile.

Thursday, July 17, 2014

MALINZI KUWAFUTURISHA WADAU LEO KARUME

RAIS wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi ameandaa futari leo (Julai 17 mwaka huu) kwa wadau mbalimbali wa mpira wa miguu.
Shughuli hiyo itafanyika Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Dar es Salaam ambapo waalikwa wataanza kuwasili saa 11.30 jioni.
 Waalikwa katika futari hiyo wametoka katika makundi mbalimbali. Makundi hayo ni wadhamini, klabu za Ligi Kuu na Daraja la Kwanza za Dar es Salaam ambazo zitawakilishwa na watu wawili wawili.
 Viongozi wa zamani wa TFF, Said El Maamry, Leodegar Tenga, Muhidin Ndolanga, Athuman Nyamlani, Mwina Kaduguda, Michael Wambura, Fredrick Mwakalebela na Ashery Gasabile. Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa TFF waliopo Dar es Salaam, Wizara ya Michezo na Ofisa Elimu wa Mkoa wa Dar es Salaam.
 Vyama shiriki; TWFA, TAFCA, TASMA, SPUTANZA, FRAT ambavyo vitawakilishwa na watu watatu watatu, viongozi wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA), Baraza la Michezo la Taifa (BMT), wahariri wa habari za michezo, Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA) na Polisi kanda Maalumu- Dar es Salaam.
 Wajumbe wa kamati ndogondogo za TFF waliopo Dar es Salaam, wazee wa Simba na Yanga- watano kutoka kila klabu, timu ya Serengeti Boys, klabu ya Saigon, Bodi ya Ligi Kuu, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Wakuu wa wilaya za Dar es Salaam, wabunge wa Dar es Salaam, Meya wa Dar es Salaam, Meya wa Kinondoni, Meya wa Ilala na Meya wa Temeke.
 Waalikwa wengine ni Omari Abdulkadir, Amin Bakhresa, Harudiki Kabunju, Hamis Kissiwa, Ismail Aden Rage, Masoud Sanani, Jamal Bayser, Hassan Dalali, Imani Madega na Mbaraka Igangula.