STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, September 25, 2014

Liverpool yaingia matatani Ulaya

http://cdn3-i.hitc-s.com/69/liverpool_wall_12402.jpgKLABU ya Liverpool ni moja ya vilabu kadhaa vinavyotarajiwa kufanyiwa uchunguzi kama wamekiuka Sheria ya Matumizi ya Fedha-FFP.
Kwa mujibu wa sheria za Shirikisho la Soka barani Ulaya-UEFA vilabu vyote barani humo vinapaswa kuweka kikomo cha hasara kutofikia paundi milioni 35.4 kwa misimu miwili. 
Kuna adhabu hutolewa kwa wasiotimiza masharti hayo ambapo Manchester City tayari wameshakumbana nayo kwa kutozwa faini na kuwekewa kiwango cha matumizi katika usajili na kupunguziwa idadi ya wachezaji katika kikosi chake Mei mwaka huu. 
Lakini pamoja na kupata hasara ya paundi milioni 49.8 katika msimu wa mwaka 2012-2013 na paundi milioni 41 msimu wa mwaka 2011-2012, Liverpool wana uhakika wanaweza kuvuka kikwazo hicho bila adhabu. 
Liverpool sambamba na Monaco, Inter Milan na AS Roma ambazo zote hazikushiriki michuano ya Ulaya msimu uliopita tayari zimepeleka taarifa za akaunti zao Bodi ya Udhibiti wa Fedha ya Klabu-CFCB lakini kuna uwezekano wa kuagizwa kupelekea maelezo zaidi kuhusu fedha hizo. 
Msimu uliopita vilabu 76 viliingia katika uchunguzi wa FFP lakini vilabu tisa pekee ndio vilipewa adhabu kwa kukiuka sheria hiyo.

HAWA NDIYO WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA VYUO VIKUU 2014-2015




CHUNGULIA mwenyewe kwa kubofya jina la chuo kupakua faili lenye majina:
  1. BUGANDO BScN_2014.pdf (82.4 KB)
  2. BUGANDO MD.pdf (106.2 KB)
  3. BUGANDO MEDICAL LABORATORY SCIENCES.pdf (79.7 KB)
  4. BUGANDO PHARMACY.pdf (80.0 KB)
  5. BUGANDO NURSING.pdf (76.0 KB)
  6. IFM BACHELOR DEGREE 2014
  7. MAKUMIRA PROPOSED STUDENTS 2014/2015
  8. MUM Undergraduate Selection - Direct.pdf (561.3 KB)
  9. MUM Undergraduate Selection - Equivalent.pdf (202.0 KB)
  10. SAUT Selected Students.pdf (307.3 KB)
  11. ST. AUGUSTINE 2014
  12. ST Franscis MD Batch one (52.3 KB)
  13. ST Franscis MD Batch two (37.2 KB)
  14. ST Franscis MD Batch Three (49.5 KB)
  15. Stella Maris Mtwara.pdf (283.1 KB)
  16. UDSM 2014/2015 
  17. Mwenge Catholic University

Mechi ya Simba Yanga lapeperuka Oktoba 12

http://tff.or.tz/wp-content/uploads/2014/05/taifa-stars-2014.jpg
Stars iliyopeperusha pambano la Simba na Yanga Oktoba 12
PAMBANO la watani wa jadi kati ya Simba na Yanga 'limeota mbawa' Oktoba 12 kutokana na kuwepo kwa pambano la kimataifa kati ya Taifa Stars na Benin.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Shirikisho la Soka Tanzania, TFF, Stars itacheza na Benin katika mechi inayotambuliwa na FIFA.
Taarifa hiyo inaseme mechi hiyo itachezwa Oktoba 12 kwenye uwanja wa Taifa, siku ambayo Simba na Yanga zilikuwa ziumane kilingana na ratiba ya awali ya Ligi Kuu ambayo sasa inatarajiwa kufanyiwa marekebisho yatakayotangazwa kesho Septemba 26.
Taarifa kamili ya TFF inasomeka hivi:
Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) inashuka uwanjani Oktoba 12 mwaka huu kuikabili Benin katika mechi ya kirafiki ya kalenda ya Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA).Mechi hiyo itachezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 10 kamili jioni. Programu ya Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager kwa ajili ya mechi hiyo itatangazwa baadaye na Kocha Mkuu Mart Nooij.Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linaendelea na taratibu nyingine kwa ajili ya mechi hiyo ikiwemo usafiri wa Benin kuja nchini, ambapo timu hiyo inatarajiwa kutua Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), Oktoba 10 mwaka huu ikiwa na msafara wa watu 28.
Pambano la Stars na Benin litatanguliwa na mechi ya kudumisha upendo kati ya viongozi wa dini ya Kikristo na Kiislamu.
 Wakati huo huo, kutokana na mechi hiyo ratiba ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) inafanyiwa marekebisho madogo, na marekebisho hayo yatatangazwa kesho (Septemba 26 mwaka huu).
 RAIS MALINZI KUFUNGA KOZI YA WANAWAKE
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi anatarajia kufunga mafunzo ya uongozi kwa viongozi wa vyama vya mpira wa miguu wa wanawake vya mikoa ya Tanzania Bara.
 Hafla ya kufunga mafunzo hayo itafanyika kesho (Septemba 26 mwaka huu) saa 5 asubuhi kwenye ofisi za TFF, Uwanja wa Karume, Dar es Salaam.
 Mafunzo hayo ya siku tano yalishirikisha viongozi 34 wakiwemo baadhi ya waandishi wa habari na Meneja wa Twiga Stars, na yaliendeshwa na Mkufunzi wa Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA), Henry Tandau.
 BONIFACE WAMBURA
KNY KATIBU MKUU
SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA.

Simba yapata pigo, Ivo, Kiongera kuikosa Yanga Okt 12

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj8__24SqlWkKjcX7F8kwlm9XNcJcmuX00g5LSeJnhkhyvDdgaA_LOv5ObDUcs7DcWxwbUMiMiTANgKbV434hiewe8cAlv0KlOHhyuP0g6sM4YhdkxIkgyI8l30SjnEcyw_ja49lQ9HlEI/s1600/ivo.jpg 
WIKI mbili kabla ya kuvaana na watani zao, Yanga klabu ya Simba imepata pigo baada ya kipa wake namba moja, Ivo Mapunda kuvunjika kidole na hivyo kuwa nje ya dimba kwa wiki nane.
Kwa mujibu wa taarifa za klabu hiyo Ivo amevunjika kidole mazoezini Zanzibar jana asubuhi na anatakiwa kuwa nje ya uwanja kwa wiki nane.
Kuumia huko kunamfanya asiweze kusimama langoni wakati  wa pambano la watani wa jadi la Simba na Yanga la Oktoba 12.
Daktari wa Simba SC Yassin Gembe amenukuliwa akisema Ivo aliumia wakati anachupia mpira katika mazoezi ya asubuhi na kwa bahati mbaya mpira ukamgonga kwenye kidole kidogo cha mwisho mkono wa kulia.
Gembe amesema Ivo alitoka mazoezini baada ya tukio hilo na baadaye akapelekwa hospitali ya Mnazi Mmoja kisiwani humo ambako baada ya vipimo ikagundulika amevunjika sana.
"Si kuvunjika kwa mzaha, amevunjika sana na anatakiwa kupumzika kwa wiki nane, baada ya hapo aanze taratibu… ina maana makadirio ya kurudi tena uwanjani ni hadi baada ya miezi mitatu" – Gembe.
Kuumia kwa Ivo kunatoa nafasi kwa makipa chipukizi Hussein Sharrif  ‘Cassilas’ na Peter Manyika kujibidiisha ili kuziba pengo lake ambapo sasa Ivo anafanya idadi ya wachezaji majeruhi ambao ni tegemeo Simba kufikia wanne baada ya Paul Kiongera anayetakiwa kuwa nje wiki sita, Haroun Chanongo na Issa Rashid ‘Baba Ubaya’.

Aisha Bui awaandalia mashabiki wake 'Asante' kumpokea

Aisha Bui katika pozi tofauti
NYOTA wa filamu nchini, Aisha Fat'hi  a.k.a Aisha Bui, yupo kwenye maandalizi ya kufyatua kazi mpya baada ya filamu yake ya 'Mshale wa Kifo' kufanya vyema sokoni.
Akizungumza na MICHARAZO, Aisha alisema anashukuru namna mashabiki walivyoipokea filamu yake hiyo ya kwanza kuitengeneza mwenyewe kupitia kampuni ya Bad Girl Entertainment na katika kuonyesha shukrani zake anajiandaa kuwatengenezea filamu nyingine kali zaidi.
Aisha alisema ingawa ni mapema kwa sasa kutaja jina la filamu hiyo, lakini alisema itawashirikisha wasanii kadhaa nyota kama alivyofanya katika 'Mshale wa Kifo' aliowashirikisha kina Mzee Chillo, Gabo na wengine.
"Nipo katika maandalizi ya kutengeneza filamu nyingine mpya, hii kama 'Mshale wa Kifo' itashirikisha pia wakali mbalimbali wa filamu nchini, lengo ni kuwapa burudani mashabiki wangu walioniunga mkono kupitia kazi yangu ya kwanza kuizalisha mwenyewe," alisema Aisha.
Kabla ya kutengeneza filamu yake mwenyewe, alishafanya vema katika filamu za wenzake zikiwamo za 'Saturday Morning', 'The Second Wife', 'Better Days', 'Not Without My Son', 'Continous Love', 'Revenge of Love', 'Mirathi', 'Pain of Love' na 'Crazy Love'.

Mashetani Wekundu kumpigia misele Gerard Pique

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjuyvOqEQPRTd8rb3TwgCrdwrkJv25RIrKO5tVEc69etf1RqMa9oRZknqbCqG35plalZ5O0rf0aHR1cMgKHEd_pd8Lj8yuoEqhsZrMY-HvGZKiXjbbOmdo3n2XiN6O5S24WwaeAbCk-xgKL/s1600/gerard+pique+wallpaper+barca+barcelona+photo+gallery+barcablog+barca+blog+2.jpg
IMEFAHAMIKA kuwa klabu ya Manchester United wana mpango wa kumrejesha Gerard Pique Old Trafford akitokea Barcelona.
Mlinzi huyo aliondoka United mwaka 2008 kwa uhamisho uliogharimu pauni milioni £5 ambapo amekuwa mchezaji wa kutumainiwa Katalunya tangu wakati huo ambapo ameisaidia kutwaa mataji manne ya ligi ya Hispania 'La Liga' mataji mawili ya ligi ya mabingwa Ulaya na mawili ya Copa del Reys.
Hata hivyo nyota huyo wa kimataifa wa Hispania mpaka sasa ameitumikia timu yake michezo mitatu tu huku bosi mpya wa Barcelona Luis Enrique akionekana kupendelea zaidi kumtumia Javier Mascherano na Jeremy Mathieu katika sehemu ya ulinzi.
Kwa mujibu wa gazeti moja la nchini Hispania la AS limearifu kuwa Manchester United inataka kutumia mwanya huo kuweka pendekezo la kutaka kumsajili Pique kurejea Old Trafford, licha ya kwamba mlinzi huyo mwenye umri wa miaka 27 akiwa ndio kwanza amesaini mkataba wa nyongeza na Barca.
Bosi Louis van Gaal kwasasa analazimika kusaka namna ya kuimarisha eneo la ulinzi katika kikosi chake mwezi Januari wakati huu ambapo United ikiwa imekusanya alama tano tu katika michezo mitano tangu kuanza kwa msimu mpya wa Premier League huku ikiwa tayari imeshatolewa katika kombe la Capital One na MK Dons.

Algeria yajaribu bahati yake AFCON 2017

http://en.starafrica.com/football/files/2014/07/alg%C3%A9rie1.jpgNCHI ya Algeria imeamua kujitosa kuwania uenyeji wa Fainali za Afrika, AFCON 2017 baada ya kukosa nafasi ya uandaaji wa fainali za  2019, 2021 na 2023.
Shirikisho la Soka la Algeria limetangaza kutuma maombi ya kutaka uenyeji wa michuano hizo za 2017. 
Taifa hilo la kaskazini mwa Afrika litachuana na nchi za Ethiopia, Ghana, Kenya, Tanzania, Mozambique, Zimbabwe na Misri katika kugombea nafasi hiyo. 
Libya ilishindwa kuandaa michuano hiyo kufuatia vita vya wenyewe kwa wenyewe vinavyoendelea nchini humo toka uondolewe utawala wa Muamar Gaddafi. 
Mshindi katika kinyang’anyiro hicho anatarajiwa kutangazwa mapema mwakani na Shirikisho la Soka barani Afrika-CAF. 
Cameroon wao walishinda haki za kuandaa michuano hiyo mwaka 2019 wakati Ivory Coast na Guinea wao walipata nafasi ya kuandaa michuano ya mwaka 2021 na 2023.

Arsene Wenger apumua Arsenal wakijiandaa kuivaa Spurs

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhLx4Ctj5fXJAnEPWAnPQLE87dYZzsslg675yLAakU1-WpskYn3CW0mbJ2CIKGeRf5M4Yqi-eVxM6Pyv_R7oLwacXTN6v0ML9tDqP3gR9TEUBNLUbo6FhO2brnwFUrixY0Has-XeGIPRHE/s1600/guar.jpgMENEJA wa klabu ya Arsenal, Arsene Wenger amesema anategemea Per Martesacker na Kieran Gibbs kurejea katika kikosi chake katika mchezo wa Jumamosi dhidi ya mahasimu wao wa kaskazini mwa London Tottenham Hotspurs. 
Majeraha madogo madogo yalipelekea Martersacker na Gibbs kukosa mchezo wa Kombe la Ligi dhidi ya Southampton na kupelekea Wenger kuwatumia mabeki wasio wazoefu akiwemo Hector Bellerin na Isaac Hayden. 
Kukosekana kwa Nacho Monreal kunamaanisha Calum Chambers ndio mchezaji pekee katika safu ya ulinzi mwenye uzoefu aliyechezeshwa na Wenger lakini kinda huyo amecheza katika mechi saba pekee za Arsenal toka alipojiunga akitokea Southampton. 
Katika mchezo huo Arsenal walitandikwa nyumbani mabao 2-1 na Southampton lakini Wenger ana uhakika kuwa mabeki wake wazoefu Matersacker na Gibbs watakuwa fiti kwa ajili ya mchezo wa Jumamosi. 
Safu ya ulinzi ya Arsenal ilizidi kupungua baada ya taarifa za Jumatatu kuwa beki wa kimataifa wa Ufaransa Mathieu Debuchy atakosekana dimbani kwa miezi mitatu kufuatia kufanyiwa upasuaji wa kifundo cha mguu wake wa kushoto.

Ronaldo akaribia rekodi ya Di Stephano Real Madrid

http://assets2.sportsnet.ca/wp-content/uploads/2014/01/ronaldo_cristiano.jpgCRISTIANO Ronaldo alifunga magoli manne katika ushindi wa Real Madrid wa 5-1 dhidi ya Elche katika Ligi Kuu ya Hispania juzi na kuwa 'hat-trick' yake ya 25 kwa Real Madrid.
Ilikuwa ni 'hat-trick' ya pili katika siku tatu baada ya kufunga magoli matatu katika ushindi wa 8-2 dhidi ya Deportivo la Coruna Jumamosi.
Ronaldo ndiye aliyesababisha penalti iliyowapa Elche goli la kuongoza baada ya kuukosa mpira na kumpiga teke Pedro Musquera wakati akijaribu kuokoa kutokea ndani ya boksi la Madrid. "Licha ya kwamba nililalamika kwa refa, ilikuwa ni penalti. Ni lazima niwe mkweli. Alikuja ghafla, lilikuwa ni shambulio ambalo sikulitarajia. Yalikuwa ni maamuzi sahihi ya refa," alisema Ronaldo.
"Nimefunga magoli manne katika mechi moja mara mbili ama tatu. Nina furaha mpira (wa 'hat-trick' nampelekea mwanangu," alisema.
'Hat-trick' hiyo ya 25 inamfanya kubakisha tatu kumfikia Alfredo di Stefano anayeshikilia rekodi ya Real Madrid ya kufunga 'hat-trick' 28. Pia ilikuwa ni ya 21 katika La Liga pekee, moja nyuma ya vinara wanaoshikilia rekodi, Di Stepano na Telmo Zarra, gwiji wa Athletic Bilbao.
Ronaldo tayari msimu huu amefunga magoli 13 katika michuano yote na kufikisha mabao 264 tangu ajiunge na Madrid, hivyo kubakisha magoli 59 kumfikia mshikarekodi wa zama zote klabuni hapo Raul aliyefunga magoli 323. Na kwa kuwa Madrid wana mechi 56 zilizobaki msimu huu, huenda akaivunja rekodi hiyo 2014-15. 

Hammer Q ana Kibakuli cha Mduara

MUIMBAJI mahiri wa muziki wa taarab, Hammer Q ameachiwa wimbo wake binafsi uitwao 'Kibakuli', wakati Rich Mavoko akiwaonyesha mashabiki wake video ya wimbo wake mpya uitwao 'Pacha Wangu'.
Hammer Q aliyewahi kutamba kwenye muziki wa kizazi kipya na wimbo wa 'Lady' kabla ya kuhamia kwenye taarab, ameachiwa wimbo huo uliopo kwenye mduara.
Wimbo huo umetengenezwa na mtayarishaji aitwae Anta Nation na  umeanza kutamba kwenye redio na mitandao ya kijamii.
Katika hatua nyingine Staa wa Roho Yangu, Rich Mavoko ameonjesha kionjo cha video yake mpya ya Pacha Wangu ambayo anatarajia kuachia siku ya leo pamoja na ngoma nyingine mpya.

Mbwa Mwitu wa Kajala azinduliwa, Lamata alalamika

BAADHI ya picha za matukio katika shughuli hiyo ya usiku wa jana
FILAMU ya Mbwa Mwitu ya msanii Kajala Masanja imezinduliwa kwa kishindo usiku wa jana kwenye ukumbi wa Sinema wa Mlimani City, huku mtunzi na muongozaji wake, Leah Richard 'Lamata' akilalamika ukiritimba unaofanywa na wasimamizi wa tasnia ya filamu nchini.
Lamata aliidokeza MICHARAZO mapema kuwa, kabla ya kuzindua filamu hiyo iliyotengenezwa na Kay Entertainment wakikumbana na vikwazo wakipigwa namna simulizi la filamu hiyo ya dakika 15 iliyogusa matukio ya kweli yaliyoikumba jamii hivi karibuni kutoka makundi ya wahalifu yaitwayo 'Mbwa Mwitu', 'Boda kwa Boda', 'Bad Face' na 'Watoto wa Mbwa'.
"Hii inkatisha tamaa lengo letu kuifundisha jamii juu ya kuepuka uhalifu kwani mwisho wake huwa siyo mwema, lakini 'mabosi' wanaosimamia fani hii wanadhani sisi tunaelimisha vibaya katika matukio yaliyopo ndani ya filamu hii ya 'Mbwa Mwitu'.
Lamata alisema bado wataendelea kutunga filamu zinazoigusa jamii sambamba na kuielimisha, kuionya na kuiburudisha kama sifa za fasihi ilivyo.
Ndani ya filamu hiyo wamo Kajala, Hemed Suleiman, Mama Kawele, Quick Racca na Mwinjuma Muumin 'Kocha wa Dunia'.
Nyota mbali walihudhuria onyesho hilo wakiwamo waigizaji Rich Richie, mtoto wa Kajala, Paula, Sandra, Odama na wengineo kibao waliompiga tafu Kajala.

Tuesday, September 23, 2014

Mama Mkwe wa Jennifer Mgendi huyooo Mtaani

FILAMU mpya ya muimbaji wa nyimbo za Injili, Jennifer Mgendi iitwayo 'Mama Mkwe' inatarajiwa kuigizwa sokoni siku ya Alhamisi baada ya kukwama kuachiwa jana Jumatatu kama ilivyokuwa imepangwa.
Aidha Muinjilisti huyo amewataka mashabiki wake wasiikose kupata darasa la kutosha.
Jennifer alisema filamu hiyo itaachiwa rasmi Septemba 25 baada ya jana kukwama kwa sababu zilizo nje ya uwezo wake ikiwa ni wiki kadhaa tangu kumalizika kurekodiwa kwake na kusema kwa ujumbe uliopo ndani yake, mashabiki hawapaswi kuikosa.
Muimbaji huyo alisema, kisa cha Mama anayeingilia ndoa ya mwanae wa kiume akitaka kupatiwa mjukuu ni mambo ambayo yamekuwa yakiwakumba wanajamii wengi na kusambaratisha ndoa zao bila kutaka.
"Ni mambo yanayotokea ndaniya jamii na kuwaachia watu machungu, sasa waigizaji wameonyesha uhalisia wa mambo namna ndoa nyingi zinavyosambaratika kwa sababu ya mambo kama hayo," alisema.
Katika filamu hiyo, Jennifer ameigiza na wasanii wengine wakali kama kina Mussa Banzi, Bahati Bukuku, Christine Matai, Bibi Esther na wengine.
"Itakuwa mtaani Alhamisi, mashabiki wasikose kuona uhondo huu. Mama Mkwe ni zaidi ya kazi zangu za nyuma kwa namna ilivyosukwa na kutendewa haki na wasanii walioigiza," alitamba Jennifer.

ACT Tanzania yakana kuwa mamluki Tanzania

http://www.mtizamohuru.co.tz/wp-content/uploads/2014/03/act.jpgNa Kipimo Abdallah
CHAMA cha Alliance for Change and Transparency (ACT-Tanzania) kimekanusha  tuhuma zinazotolewa na baadhi ya wanasiasa kuwa  ni chama kilichokuja kubomoa vyama vya upinzani hapa nchini.
Hayo yamesemwa na Katibu wa Mawasiliano na Uenezi wa ACT -Tanzania Mohammed Massaga wakati akizungumza na mwandishi wa MICHARAZO ofisi kwake jijini Dar es Salaam.
Massaga aliomba vyama hivyo kuacha kufanya siasa nyepesi na kujikita katika hoja ili kuhakikisha kuwa upinzani unakuwa na nguvu ili viweze kukitoa chama tawala CCM madarakani.
Alitoa wito kwa watanzania kuviunga mkono vyama vya siasa ambavyo vinaonyesha ni madhubuti ya kukabiliana na ubadhirifu wa rasilimali za Taifa ili kufikia malengo ya maisha bora ambayo kwa sasa yamekwama.
Katibu huyo wa Mawasiliano na Uenezi alisema iwapo vyama vya upinzani vitakuwa na umoja na ushirikiano wa dhati zipo dadli tosha za kukiondoa chama tawala madarakani.
Alisema wapo baadhi ya viongozi ambao wanashindwa kufanya siasa na kubakia kulalamika jambo ambalo linachelewesha mabadiliko.
"Ndhani unaona mwenyewe tatizo la siasa za Tanzania ni wanasiasa kushutumiwa na kuacha kufanya siasa za kweli ambazo zinaweza kuleta mabadiliko kwa jamii ya Kitanzania" alisema
Massaga alitolea mfano wa mchakato wa Bunge Maalum la Katiba linaloendelea mjini Dodoma kuwa ni matumizi mabaya ya fedha za Serikali.
Kwa upande mwingine Massaga alisema katika kujenga chama chao cha ACT- Tanzania wamefanikiwa kuvuna wachama wapya zaidi ya 11,800 katika mikoa 12 ya Tanzania Bara kwa kipindi cha mwezi Agosti mwaka huu.
Katibu huyo wa Mawasiliano na Uenezi ACT alisema kwa sasa chama hicho kina wanachama zaidi ya 187,000 nchini kote hivyo juhudi zao ni kuongeza wanachama wengi zaidi kwa kutumia itikadi yao ya demokrasia ya jamii.
Alisema chama hicho kilifanya ziara katika mikoa 12 ambayo Tanga, Singida, Shinyanga, Simiyu, Geita, Tabora, Mara, Mwanza, Lindi, Kigoma, Pwani na Mtwara ambapo wamepokelewa kwa nguvu kubwa.
Massaga alisema pamoja na kuvuna idadi hiyo ya wanachama wamefanikiwa kusimika viongozi wa muda katika majimbo 68 ya Tanzania bara na viongozi wa kata na matawi kwenye majimbo hayo.
"Kwa kifupi tumepata mafanikio makubwa katika kipindi hiki cha miezi minne tangu kupewa usajili wa muda kwani kila tunapopita tunapokelewa kwa nguvu zote jambo ambalo linatupa matumaini ya kufanya vizuri kwenye chaguzi zijazo", alisema.
Katibu huyo wa Mawasiliano na Unezi wa ACT-Tanzania alisema katika kuhakikisha kuwa wanafikia malengo katika medani za siasa Tanzania wataendelea kuwaelimisha wanachama juu ya kujitokeza kushiriki uchaguzi wa serikali za mitaa.

Fainali za Kombe la Dunia 2022 nchini Qatar zayeyuka

https://www.venturesonsite.com/news/wp-content/uploads/2014/06/qatar-chronicle-qatar-2022-stadiums.jpgIMEBAINIKA wazi kuwa ni ndoto kwa Fainali za Soka za Kombe la Dunia za mwaka 2022 kufanyika Qatar.
Mjumbe wa kamati ya utendaji ya Shirikisho la Soka Duniani,FIFA, Theo Zwanziger amefichua kuwa ni vigumu fainali hizo kuchezwa nchini humo kutokana na hali ya joto kali katika nchi hiyo.
Zwanziger ambaye ni raia wa Ujerumani aliliambia jarida la michezo la Bild jana kuwa anadhani mwisho wa siku michuano ya Kombe la Dunia 2022 haitafanyika katika nchi hiyo. 
Mjumbe huypo aliendelea kudai kuwa watabibu wamesema hawatakubalia kuwajibika kama michuano hiyo itafanyika katika hali ya hatari kama hiyo. 
Japo Qatar wamesisitiza ambao ni matajiri wakubwa wa mafuta wamesisitiza kuwa wanaweza kuandaa michuano hiyo majira ya kiangazi kwa kutumia teknolojia ya vipoza hewa katika viwanja vyake, sehemu za mazoezi na mahali watakapofikia mashabiki bado kumekuwa na wasiwasi mkubwa kuhusiana na afya za wachezaji na mashabiki watakaokuja kushuhudia michuano hiyo. 
Zwanziger amesema anajua wanaweza kuweka vipoza hewa viwanjani lakini Kombe la Dunia halichezwi viwanjani pekee kwani mashabiki kutoka duniani kote watakwenda na kusafiri katika hali hiyo ya joto jambo ambalo ni hatari kwa afya na maisha yao. Michuano ya mwaka 2022 imekuwa ikileta mjadala mkubwa huku rais wa FIFA Sepp Blatter akikiri kuwa walifanya makosa kuipa Qatar kuandaa michuano hiyo na kutaka kuangalia uwezekano wa kuamisha michuano hiyo ichezwe katika majira ya baridi.

AS Vita yanusa Fainali za Afrika, yainyuka Sfaxien

http://www.congoplanet.com/pictures/news/as_v_club_congo_kinshasa_football_vita_z.jpgKLABU ya AS Vita ya DR Congo imeanza vema mbio zake za kucheza Fainali za Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya kuinyuka CS Sfaxien ya Tunisia mabao 2-1.
Mabao ya Vita katika mchezo huo uliochezwa katika Uwanja wa Tata Raphael jijini Kinshasa yalitupiwa kimiani na Firmin Ndombe Mubele na Heritier Luvumbu Nzinga huku lile la kufutia machozi la Sfaxien likifungwa na Ali Maaloul. 
Ushindi huo unaiweka katika nafasi nzuri Wakongo hao kwa mechi ya marudiano itakayofanyika wikiendi hii mjini Tunis.
Vita watakwenda katika mchezo wao wa marudiano wakihitaji sare ya aina yoyote inaweza kuwapeleka fainali ambapo watakutakana na aidha ES Setif ya Algeria au TP Mazembe ya DRC. 
Sfaxien ambao ni mabingwa wa Kombe la Shirikisho na Super Cup walionekana kuzimiliki vyema dakika 20 za mwisho katika mchezo huo lakini walishindwa kutafuta nafasi ya kusawazisha. 
Katika mchezo wa kwanza 'ndugu' zao TP Mazembe walichapwa mabao 2-1 na wapinzani wao ambao watarudiana nao wikiendi hii mjini Lubumbashi na kama timu hizo za Kongo zitafuzu fainali itakayopigwa  Octoba 25-26 na Novemba 1-2 itakuwa ni mara ya kwanza kwa timu Chini ya Jangwa la Sahara kukutana pamoja katika hatua hiyo.

Kifo cha Ebosse chaiponza JS Kabylie, lupango miaka miwili

http://i.ytimg.com/vi/nRgfnT26dgY/0.jpg 
KLABU ya JS Kabylie ya Algeria imefungiwa kushiriki katika michuano ya Afrika kwa miaka miwili kufuatia shambulio lililosababisha kifo cha mchezaji wa kimataifa wa Cameroon Albert Ebosse. 
Uamuzi umechukuliwa na Shirikisho la Soka barani Afrika-CAF katika kiakao chake kilichofanyika jijini Addis Ababa, Ethiopia. 
Kabylie ilimaliza katika nafasi ya pili kwenye msimamo wa Ligi Kuu nchini humo hivyo kuwapa nafasi ya kushiriki michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika mwakani. 
Hatua hiyo ya CAF imekuja kufuatia Shirikisho la Soka la Algeria kuitaka Kabylie kucheza mechi zake za nmyumbani bila ya mashabiki katika uwanja huru msimu huu. 
Ebosse alifariki dunia hospitalini mwezi uliopita kutokana na majeraha ya kichwa yaliyosababishwa na kupigwa na kitu kizito na mashabiki wa klabu hiyo ambao walikasirishwa na kipigo cha mabao 2-1 kutoka kwa wapinzani wao USM Algers.

Rooney, Gerrard wapigwa 'madongo' England

http://www1.pictures.zimbio.com/gi/Wayne+Rooney+Steven+Gerrard+England+v+Ukraine+ygx0xe1DQpXl.jpg

MWANZO mbaya wa msimu kwa klabu za Manchester United na Liverpool unachangiwa na manahodha wao wawili Wayne Rooney na Steven Gerrard, imeelezwa.
Mchambuzi wa soka wa Goal.com, Greg Stobart, amesema "upendeleo" wanaopata Rooney na Gerrard kwa kuwa manahodha na kuachwa waendelee kubaki uwanjani licha ya kucheza chini ya kiwango, kunazigharimu timu hizo hasa katika zama hizi ambazo hata nyota wakubwa wa kimataifa huachwa benchi.
Wakati Juan Mata alianzia benchi na Di Maria na Radamel Falcao nao wakamalizia mechi wakiwa benchi, Rooney aliendelea kunufaika kwa "upendeleo" wa kubaki uwanjani kwa dakika 90 zote, licha ya kupiga shuti moja tu langoni mwa Leicester katika kipigo chao cha 5-3 juzi Jumapili.
Kuna maswali yanayohoji kama Rooney anastahil nafasi kikosi pamoja na wakali kama Falcao, Di Maria na Robin van Persie. Tabia yake ya kupooza mpira haiendani na falsafa ya kocha Louis Van Gaal ya soka la kushambulia.
Van Gaal said alisema Ijumaa iliyopita kwamba Rooney, kwa kuwa nahodha, anatarajia kuendea kunufaika na "upendeleo" wa kuanza katika mechi ngingi zaidi msimu huu na kubaki uwanjani kwa muda mrefu zaidi linapokuja suala la kocha kufanya mabadiliko. Jambo hilo linampa uhakika mchezaji ambaye wengi wanaona kwamba hastahili kuanza katika kikosi chenye sura mpya cha Manchester United. Na kipigo cha 5-3 dhidi ya Leicester juzi ni mfano unaoonyesha ni kwa nini.
Alionekana akiwawakia kwa hasira wachezaji wenzake, ikiwamo kumshukia beki yosso Tyler Blackett (20) kufuatia Leicester kufunga goli la 3-3, lakini Rooney alionyesha kutojielewa kwani yeye ndiye aliyepoteza mpira uliozaa goli hilo.

Bilioni 20 zahitajika kutatua tatizo la Ajiora nchini

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj-F5hwnHLukOOHecjhZ-ghBDejeN6VOEVNIpFPCcLyvhzRQSnpxPJQMoPK0TMjEI6_GHXln6t7ZsHQv5IPO-4lzTHCdxZsY5zg0yjg0u1lXUwCocg-aXzVOF9kMVqArWiwC4b0HCaqkiE/s1600/2.JPG
Dk Kisui (kushoto) akifafanua jambo
Na Kipimo Abdallah
WIZARA ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo imesema inahitaji shilingi bilioni 20 kila mwaka ili iweze kupunguza tatizo la ajira hapa nchini.
Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi Msaidizi wa Uwezeshaji na Uhamasishaji wa Wizara hiyo Dk. Steven Kisui  wakati akijibu swali la mwandishi wa habari hii.
Alisema bajeti wanayotengewa haitoshelezi mahitaji ya vijana jambo ambalo linachelewesha juhudi za kupunguza ukubwa wa tatizo hilo ambalo linatajwa kama janga la Taifa.
Dk. Kisui alisema mahitaji ni makubwa kutoka kwa vijana mbalimbali nchini ambao wamejiunga katika SACCOS ila uwezo wa Serikali ni mdogo hivyo zoezi hilo
linachukua muda kutatuliwa.
"Kusema ukweli bajeti ya shilingi bilioni 6 hatuwezi kufikia malengo lakini tutaenda hivyo hivyo hadi tufikie muafaka,kwani kiukweli ni ndogo mnno", alisema.
Kisui alisema juhudi za Wizara ni kuhakikisha kuwa hicho kidogo kinachopatikana kinawafia walengwa ambao watakuwa wamefikia vigezo pamoja na ukweli kuwa bilioni 20 zingeweza kutatua tatizo.
Kwa upande wake Kaimu Mkuu Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali Concilia Nyibitanga alisema hadi kufikia sasa ni Halimashauri 42 kati ya 169 ambazo vijana wake ndio wametengeneza vikundi vya SACCOS.
Alisema mwamko wa Halimashauri kuhakikisha kuwa vikundi vinakuwepo imekuwa mdogo sana jambo ambalo linakwamisha juhudi za Serikali.
"Pamoja na juhudi za serikali katika kuhakikisha kuwa vijana wanafikiwa bado mwamko ni mdogo sana katika Halimashauri nyingi jambo ambalo linaweza kuwa kikwazo", alisema.
Nyibitanga alisema fedha hizo ambazo zinakopeshwa kwa riba ndogo lengo lake ni kuhakikisha kuwa vijana wanajiajiri ili kuhakikisha kuwa wanakabilianana changamoto zinazowakabili.

Kajala kuzindua Mbwa Mwitu kesho Mlimani City

Kajala katika pozi
Kava la picha hiyo ya Mbwa Mwitu inayozinduliwa kesho Mlimani
NYOTA wa filamu nchini Kajala Masanja 'Kajala' kupitia kampuni yake ya Kay Entertainment inatarajiwa kuzindua filamu ya aina yake kesho usiku.
Filamu hiyo inayofahamika kama 'Mbwa Mwitu' itazinduliwa kwenye ukumbi wa Mlimani City kwa watu maalum walioalikwa kuhudhuria.
Kinachoifanya filamu hiyo kuwa ya kipekee ni muda mfupi iliyonayo wa dakika 15 tu, 10 ikiwa ni filamu yenyewe na tano za 'ducumentary' ya baadhi ya vijana waliokuwa wakiunda kundi la Mbwa Mwitu lililotikisa jiji.
Mtunzi na muongozaji wa filamu hiyo, Leah Richard 'Lamata' aliiambia MICHARAZO kuwa, filamu hiyo inasimulia visa na mikasa ya kundi la Mbwa Mwitu lililohusishwa na uvamizi na uporaji wa watu jijini Dar es Salaam.
"Uzinduzi utafanyika Mlimani Sept 24 (kesho) na ndani ya filamu hiyo ya dakika 10 ina nyongeza ya dakika tano za mahojiano ya waliokuwa vijana wa 'Mbwa Mwitu' ambao wameacha uhalifu huo," alisema Lamata kwa niaba ya Kajala ambaye ni mmoja wa washiriki wa filamu hiyo.
Mbali na Kajala wengine walioicheza ni Hemed Suleiman 'PHD', Grace Mapunda 'Mama Kawele', Mwinjuma Muumin, Abort Rocca, Hassain Hussein na Abdul Karim.
Kundi la Mbwa Mwitu na yake ya Watoto wa Mbwa, Boda kwa Boda na Bad Face yalitikisa jiji kwa vitendo vyao ya kihalifu kabla ya jeshi la Polisi kuyashughulikia huku baadhi ya washirika wao kuuwawa na wananchi.

PSPF kudhamini Siku ya Msanii Tanzania kwa Sh Mil 10

http://www.8020fashionsblog.com/wp-content/uploads/2013/09/pspf.pngNa Kipimo Abdallah
MFUKO wa Pensheni wa PSPF  umetoa shilingi milioni 10 kwa ajili ya kudhamini siku ya Msaani Tanzania.
Hayo yamesemwa na Afisa Uhusiano Mwandamizi wa PSPF Abdul Njaidi wakati akizungmza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.
Alisema lengo la PSPF kujitolea kudhamini siku hiyo na katika kuangalia sekta nzima ya sanaa kwa kuwawezesha, kuwapa mafunzo wasanii ili waweze kujikwamua kiuchumi hapa nchini.
Njaidi alisema PSPF imekuwa ikijikita katika kuwapatia mafao watumishi wa sekta mbalimbali zilizo rasmi kwa miaka mingi ila kwa kipindi cha hivi karibuni hata sekta isiyo rasmi inahusishwa wakiwepo wasanii.
"Kwa kuanza sisi PSPF tumeamua kudhamini siku ya Msanii Tanzania kwa kutoa milioni 10 ambapo tunaamini zitasaidia mchakato huo", alisema.
Aidha Njaidi alisema pamoja na kudhamini siku hiyo PSPF inaendelea na kupokea wanachama kutoka sekta mbalimbali ambao wapo tayari kwa malengo yao baadae.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Haak Neel Production Company Limited Geofrey Katulo alisema  siku ya Msanii ni mradi uliobuniwa na Baraza la SanaaTaifa (BASATA) na utaendeshwa kwa ubiia wa Haak Neel  Production Company Limited.
Alisema mradi huo ulibuniwa ili kuungana na wenzao duniani kuadhimisha siku siku ya kimataifa ya Msanii ambayo huadhimishwa kila ifikapo Oktoba 25 kwa lengo la kumtambua msaani, kazi zake pamoja na mchango wake katika jamii.
Katula alisema kauli mbiu ya siku ya msaanii mwaka 2014 ni "Sanaa ni Kazi" ambapo fani zitakazohusika katika maadhimisho hayo ni taarabu, muziki wa dansi, ngoma za asili, muziki wa msanii kutoka nje ya nchi.
Fani zingine ni uchezaji shoo, dansi za mitaani, bongo fleva, maonyesho ya mitindo ya mavazi, sanaa kwa watoto na maonyesho ya sanaa za ufundi pamoja na semina.

Sunday, September 21, 2014

Simba yashindwa kulipa kisasi kwa Coastal Taifa

simba
MASHABIKI wa klabu ya Simba wametoka uwanja wa Taifa wakiwa hawana furaha baada ya kikosi cha timu yao kushindwa kulinda mabao mawili waliyoyafunga kipindi cha kwanza na kuwaachia Coastal Union warejeshe kipindi cha pili na kufanya mchezo huo kumalizika kwa sare ya mabao 2-2 katika Ligi Kuu.
Mabao mawili ya Shaaban Kisiga na Amissi Tambwe yaliwafanya vijana wa Msimbazi kuwa na furaha na kuamini wangepata nafasi ya kuwacheka wapinzani wao Yanga waliozabuliwa mabao 2-0 na Mtibwa Sugar jana mjini Morogoro baada ya kwenda mapumziko wakiwa mbele.
Hata hivyo kipindi cha pili kilipoanza Coastal waliingia kivingine na kucharuka na kurejesha bao moja baada ya jingine kupitia wa Lutimba Yayo na Ramadhani Salim kufungwa kwa faulo na kuifanya matokeo kusomeka mabao 2-2 na kuwafanya mashabiki wa Simba kuwa wanyonge, licha ya timu ya kupata pointi moja.
MSIMAMO LIGI KUU TANZANIA BARA 2014-2015
                                          P  W  D  L  F  A  Pts
1. Ndanda Fc                    1   1    0   0  4   1    3
2. Azam                             1   1    0   0  3   1   3
3. Mtibwa Sugar                1   1    0   0  2    0  3
4. Prisons                           1   1   0   0   2   0   3
5. Mgambo JKT                1    1   0   0   1   0   3
6. JKT Ruvu                      1    0   1   0   0   0   1
7. Coastal Union                1    0   1   0   2   2   1
8. Simba                            1    0   1   0   2   2   1
9.Mbeya City                     1    0   1    0   0  0  1
10. Kagera Sugar               1    0   0   1    0   1   0
11. Ruvu Shooting              1    0   0   1    0   2  0
12.Yanga                            1    0   0   1    0   2  0
13. Polisi Moro                  1    0   0   1    1    3  0
14.Stand Utd                     1    0   0   1    1    4  0

Manchester United bado sana, yagongwa 5, Spurs yafa nyumbani

Emmanuel Adebayor
Adebayor akipaparika kuisaidia Spurs isife nyumbani bila mafanikio
Esteban Cambiasso
Hivi ndivyo Mashetani Wekundu walivyonyonyolewa leo ugenini na Leicester City
Etienne Capoue (left) and Stephane SessegnonHALI bado tete kwa klabu ya Manchester United baada ya jioni hii kubamizwa mabao 5-3 na klabu iliyorejea kwenye ligi kuu ya England, Leicester City katika pambano la ugenini, huku Tottenham Hotspur ikifa nyumbani mbele ya West Bromwich Albion kwa bao 1-0.
Manchester iliyofanya 'mauaji' ya kutisha wiki iliyopita kwa kuifumua timu kibonde ya QPR kwa mabao 4-0 ilionekana kama ingeendeleza ushindi kwa Leicester City baada ya kutangulia kupata mabao mawili ya haraka.
Mabao hayo yaliyofungwa na Robin van Persie katika dakika ya 13 ya mchezaji akimalizia kazi nzuri ya Radamel Falcao na Angel di Maria kuongeza la pili dakika tatu baada ya kumegewa pande na Wayne Rooney.
Hata hivyo hilo la pili halikudumu kwani dakika moja baadaye Ulloa aliifungua wenyeji bao na kufanya matokeo kuwa 2-1  hadi wakati wa mapumziko.
Kipindi cha pili Mashetani Wekundu ambao wana pengo katika nafasi ya ulinzi tangu walipowauza Rio Ferdinand na Namanja Vidic, waliongeza bao la tatu dakika ya 57 na kiungo Ander Herrera kwa kazi nzuri ya Di Maria.
Wenyeji walicharuka na kurejesha bao la pili dakika ya 62 kwa mkwaju wa penati kupitia Nugent kabla ya Cambiasso kusawazisha bao dakika mbili baadaye, huku pia Mashetani Wekundu wakimpoteza beki wao Blackett kwa kadi nyekundu.
Magoli yaliyoizamisha vijana wa Louis Van Gaal, yalitumbukizwa wavuni katika dakika ya 79 na Vardy na Ulloa akahitimisha kwa mkwaju wa penati katika dakika ya 83.
Katika mechi nyingine iliyochezwa mapema sambamba na pambano hilo, Spurs ikiwa nyumbani iliendeleza uteja baada ya kulazwa bao 1-0 na wageni wao West Brom.
Bao lililoiua Spurs lilifungwa na James Morrison katika dakika ya 74, licha ya wenyeji kucharuka kutaka kuondokana na aibu ya kulala nyumbani.
Ligi inaendelea kwa mechi mbili kati ya Crystal Palace dhidi ya Everton na Manchester City dhidi ya Chelsea.

Simba, Coastal hapatoshi leo, Ndanda Kuchele!

Simba watapona kwa Coastal
Yusuf Chippo, Kocha wa Coastal Union (mwenye kofia) ataendeleza ubabe kwa vijana wake dhidi ya Simba leo Taifa?
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgSvHwYqtPQMuzPoWUu4QCWVjjgvVwLySqdBYExhW-LxDkl-tjqI3X__y-_vwNzmO6A72piQEbxsK79AqJ8vub5o2bTvjx1VL8FqSFT_-uMryVYDTOmZZVv18G_WiMV4YrQE_D_be0p_aWy/s1600/20140913_160438.jpg
Ndanda Fc waliokaa kileleni baada ya ushindi wake wa kishindo jana dhidi ya Stand Utd
WAKATI mabingwa wa zamani wa soka nchini, Simba na Coastal Union zikishuka dimbani leo katika mechi ya kisasi baina ya 'wanandugu' hao, wageni wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Ndanda wameanza na mguu mzuri kwa kukaa kileleni mwa msimamo wa ligi.
Ushindi wa mabao 4-1 iliyopata ugenini dhidi ya Stand United ya Shinyanga imeiweka Ndanda kileleni ikiwazxidi mabingwa watetezi Azam kwa uwiano wa bao moja la kufunga.
Azam wanakamata nafasi ya pili na kufuatiwa na Mtibwa Sugar waliowatoa nishai Yanga na Marcio Maximo wao pamoja na Jaja, kisha Prisons waliowakong'ota maafande wa Ruvu Shooting wakifuatia mbele ya Mgambo JKT walioshinda jana nyumbani mjini Tanga.
Ingawa ni mapema mno kuijadili ligi kwa sasa, lakini kwa kuwa asubuhi njema huonekana asubuhi, Ndanda, Azam, Mtibwa na Prisons zimesafisha 'nyota' kwa ushindi katika mechi zao za ufunguzi, huku Mbeya City na JKT Ruvu wenyewe wakikusanya pointi moja moja.
Raundi ya kwanza ya mechi hizo za ufunguzi itakamilika leo wakati Simba na Coastal Union zitakazpovaana kwenye dimba la Taifa, huku Simba ikitaka kulipa kisasi na Coastal wakitafuta rekodi ya kuendeleza ubabe kwa vijana wa Msimbazi.
Katika mechi ya mwisho ya msimu uliopita baina ya timu hizo, Simba ilikubali kipigo cha bao 1-0, goli lililofungwa na beki kinda wa Coastal Hamad Juma dakika chache kabla ya mapumziko na kulizamisha jahazi la Wekundu wa Msimbazi waliokuwa chini ya Kocha Zdravkov Logarusic ambaye kwa sasa hayupo na timu hiyo.
Simba itawakabili Coastal wakiwa chini ya Mzambia Patrick Phiri na ikiundwa na kikosi imara, hali inayofanya pambano hilo kuwa la kusubiriwa kwa hamu kwani hata Coastal nao siyo ya kubezwa kwa usajili iliyofanywa chini ya kocha Mkenya, Yusuf Chippo.
Je ni Simba itakayolipa kisasi au Coastal itakayoendeleza ubabe katika mechi ya leo? Jibu ni baada ya dakika 90 ya mchezo huo. Tusubiri tuone.

TP Mazembe yafa ugenini kwa ES Setif

http://www.groupelavenir.org/IMG/arton1718.jpg
TP Mazembe
KLABU ya TP Mazembe ya DR Congo imepewa kipigo cha mabao 2-1 ugenini na ES Setif ya Algeria, lakini bao la kujifunga ,a wenyeji limewasaidia kuwaweka katika nafasi nzuri ya kusonga mbele kama itashinda angalao bao 1-o nyumbani wiki ijayo.
Said Aroussi alijifunga kattika dakika 52 kwenye harakati za kuokoa mpira wa krosi uliopigwa na Rainford Kalaba na kuwapa uongozi TP Mazembe.
Hata hivyo wenyeji walirudisha bao hilo dakika chache baadaye kupitia kwa Younes akimalizia krosi pasi huku waamuzi wa poambano hilo wakijichanganya, refga wa kati akisema goli wakati msaidizi wake akionyesha kibendera cha kuotea cha mpiga krosi.
Refa Neant Alioum alikubali goli hilo baada ya kuzongwa na wachezaji wa ES Setif wakipinga maamuzi ya mshika kibendera, japo TP Mazembe waliamua kucheza soka.
Dakika chache kabla ya kumalizika kwa pambano hilo wenyeji walipata bao la ushindi kupitia kwa Abdulmalek Ziaya aliyemtungua kipa mwenye mbwembwe Robert Kidiaba.

Tevez aiangamiza AC Milan Italia

Carlos Tevez
Carlos Tevez akitupia kitu nyavuni na kuwaacha kipa na mabeki wa Milan wakiwa katika simanzi
BAO pekee lililofungwa na Muargentina, Carlos Tevez katika dakika ya 71 akimalizia kazi ya Paul Pogba lilitosha kuwapa ushindi mujarabu mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Italia, Seria A Juventus dhidi ya AC Milan katika pambano lililochezwa uwanja wa San Sirro, mjini Milan.
Kipigo hicho kimeishusha Milan mpaka nafasi ya tatu ikisaliwa na pointi zake 6 na kuwapisha Juventus kukaa kileleni ikiwa na pointi 9 na mabao manne ya kufungwa ikiwa haijafungwa bao lolote mpaka sasa.
AS Roma waliokuwa nafasi ya tatu wamepanda hadi nafasi ya pili katika msimamo wa ligi hiyo kwa uwiano wa mabao ya kufunga na kufungwa dhidi yake na Milan ambao wamefunga mabao nane na kuruhusu mabao sita.
Ligi hiyo inatarajiwa kuendelea leo kwa michezo mbalimbali ambapo mapame saa saba mchana huu, Chievo Verona itakuwa nyumbani kuialika Parma, Genoa itaialika Lazio na AS Roma watakuwa nyumbani kuikaribisha Cagliari.
Mechi nyingine za leo ni kati ya Sassuolo dhidi ya Sampdoria, Atalanta itaikaribisha Fiorentina, Udinese itaialika Napoli, Palermo itakuwa wenyeji wa Inter Milan na Hellas Verona watakuwa wageni wa Torino.