STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, October 7, 2014

Dk Ndumbaro kuburuzwa Kamati ya Nidhamu kisa...!

http://hivisasa.co.tz/wp-content/uploads/2014/06/ndumbalo1.jpg
Dk Damas Ndumbaro, Mwanasheria wa Klabu 14 za Ligi Kuu zinazopinga agizo la TFF kuwakata asilimia 5 za fedha za wadhamini wao
SAKATA la vilabu 14 vinavyoshiriki Ligi Kuu ya Bara kupitia kwa mwanasheria wao, Dk Damas Ndumbaro, kupingana na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) juu ya kukatwa asilimia tano ya fedha za wadhamini wa ligi hiyo na kutishia kutoshiriki ligi na zitapiga kura ya maoni ya kutokuwa na imani na Rais wa TFF, Jamal Malinzi, ikiwa TFF itatekeleza azma yake, limechukua sura.
Mapema wiki iliyopita, Malinzi aliagiza timu hizo kukatwa kiasi hicho cha pesa kwa ajili ya Mfuko wa Maendeleo ya Soka (FDF) ambapo klabu husika zikiwemo Simba na Yanga zimepinga hatua hiyo na kutishia kutocheza ligi kuu kama agizo hilo litatekelezwa na Bodi ya Ligi.
Sasa kwa mujibu wa vyanzo vya kuaminika inaelezwa kwamba Shirikisho la soka nchini limefikia hatua ya kumpeleka mwanasheria huyo Damas Ndumbaro kwenye Kamati ya Nidhamu ya shirikisho hilo kutokana na kitendo chake alichokifanya mwishoni mwa wiki iliyopita.

Credit:Shafii Daud

CAF yaitosa Tanzania AFCON 2017

http://i2.cdn.turner.com/cnn/dam/assets/140823175408-afcon-trophy-story-top.jpgSHIRIKISHO  la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limefahamishwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) kuwa Tanzania haitaweza kuwa mwenyeji wa Fainali za Afrika- AFCON 2017 kwa kuwa haijawahi kuandaa fainali zozote za vijana Afrika. Fainali hizo ni zile za vijana wenye umri chini ya miaka 17 na 20.
Hivyo, TFF inaelekeza nguvu zote katika kuandaa Fainali za Afrika kwa vijana wenye umri chini ya miaka U17 mwaka 2019.
Tunapenda kuchukua fursa hii kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanazania, Jakaya Kikwete kwa kututia moyo katika kuomba uenyeji wa AFCON 2017.
Pia tunamshukuru Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk Fenella Mukangara kwa juhudi binafsi alizozionyesha katika jitihada za Tanzania kuomba uenyeji wa AFCON 2017.
TFF inaamini kwa dhati kuwa uenyeji wa Afrika U17 2019 utaifungulia Tanzania milango ya kuandaa mashindano makubwa zaidi.

Newz Alert! Mwanasheria Mkuu ZNZ afutwa kazi

HABARI zilizotufikia hivi punde zinasema kuwa Aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar,Othman Masoud amefutwa kazi na Rais wa Zanzibar, Dk Mohammed Ali Shein.
Taarifa kutoka visiwani humo zinasema kuwa Mwanasheria huyo aliyeamua kutumia demokrasia yake katika Bunge la Katiba kwa kupigia kura za ndiyo na hapana vipengele na ibara za Rasimu ya Katiba Mpya amefutwa kazi usiku huu.
Inaelezwa maamuzi hayo ya Dk Shein yamekuja ikiwa imesalia saa chache kabla ya rasimu huyo kukabidhiwa kwa viongozi wakuu wa nchi kesho mjini Dodoma na nafasi yake imeelezwa inazibwa na aliyekuwa Mwansheria Mkuu Msaidizi, Said Hassan Said.
hata hivyo haikuelezwa sababu ya kufutwa kazi kwa Mwanasheria huyo ambaye kwa baadhi ya wajumbe na wananchi wa visiwani humo wanamuona kama 'Msaliti' kwa alichokifanya kwenye Bunge Katiba lililomalizika hivi karibuni.

Mkude, Mgeveke waongezwa Stars


http://hivisasa.co.tz/wp-content/uploads/2014/05/IMG_7000.jpgKATIKA kuhakikisha wanapata ushindi katika mechi yao ya Jumapili dhidi ya Benin, Kocha Mart Nooij ameongeza wachezaji watatu kwenye kikosi cha Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager ili kukiongezea nguvu.
Taifa Stars inajianda kukabiliana na Benin katika mechi ya Kalenda ya Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA)  itakayofanyika Jumapili (Oktoba 12 mwaka huu) jijini Dar es Salaam.
Wachezaji walioongezwa ni kiungo Jonas Mkude na mlinzi Joram Mgeveke kutoka timu ya Simba, pamoja na mlinzi Gadiel Michael wa Azam.

WANYARWANDA KUZIHUKUMU STARS v BENIN

taifa stars 2014

MAREFA kutoka Rwanda ndiyo watakaochezesha mechi ya Kalenda ya Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) kati ya Taifa Stars na Benin itakayofanyika Jumapili jijini Dar es Salaam. Hakizimana Louis ndiye atakayeongoza waamuzi hao wa FIFA kwa kupuliza filimbi kwenye mechi hiyo itakayochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 11 jioni. 
Atasaidiwa na Simba Honore na Niyitegeka Jean Bosco.
Mechi hiyo itatanguliwa na ile ya viongozi wa dini- Kiislamu vs Kikristo kudumumisha upendo, amani na ushirikiano itakayoanza saa 9 kamili alasiri. 

Tiketi za elektroniki zitakazotumika kwa mechi hiyo tayari zimeanza kuuzwa kwa kiingilio cha sh. 4,000 na sh. 10,000.

Arsene Wenger apuuzia sakata lake na Mourinho


KOCHA wa Arsenal, Arsene Wenger amesema kamwe hajutii kumsukuma kocha wa Chelsea, Jose Mourinho katika mechi ya juzi zikiwa ni dakika 20 tu tangu mechi hiyo iliyochezwa Uwanja wa Stamford Bridge kuanza kuchezwa.
Wawili hao walitibuana baada Gary Cahill kumchezea rafu mbaya winga mshambuliaji wa Arsenal Alexis Sanchez na Wenger kukasirishwa na uamuzi wa Mourinho wa kuonyesha kumtetea Cahill.
Hata hivyo, kama si juhudi za refa Martin Atkinson na mwamuzi wa akiba Jonathan Moss kujaribu kuwasuluhisha zingepigwa kavu kavu.
"Cha kujutia nini baada ya hilo? Nilitaka kwenda kutoka (pointi) A hadi B na mtu fulani akanitibua bila kuonyesha ishara ya mapokeo," Wenger alisema.
"B ilikuwa ni kuangalia kama Sanchez aliumia. Ilikuwa ni kusukumwa? Kidogo. Unaweza kuona kama ukweli nimejaribu kumsukuma."
Wenger anasema alimsukuma "kidogo" Mourinho.
Hata hivyo walitenganishwa na mwamuzi wa akiba Jon Moss na refa Atkinson, lakini haitarajiwi FA kuwachukulia hatua zaidi.
Mourinho alisema alitaka "kusahau" kuhusu tukio hilo na Mfaransa huyo, na akasisitiza hakufanya lolote baya.
"Inauma kwa sababu hii ni mechi kubwa, klabu kubwa, mpinzani mkubwa,na mechi muhimu kwa timu zote. Hali hii inaufanya mchezo kuwa na hisia,'' alisema.
"Nimefanya makosa mengi sana katika soka, lakini si kipindi hiki kwa sababu nilikuwa katika eneo langu la kiufundi na halikuwa kosa langu. Mchezo umekwisha. Mwisho wa stori."
Uhusiaano wa makocha hao wawili umekuwa wa maneno maneno katika mechi kwa kipindi kilichopita, kwa Mourinho kumpachika Wenger "mtaalam wa kufeli" hiyo ilikuwa Februari mwaka huu.
Mourinho pia alisema hahofii uamuzi wa kitabibu baada ya Thibaut Courtois kuhaha kutokana na kukwaruzana na mshambuliaji wa Kimataifa wa Chile Sanchez na kwamba pengo hilo likiwamo litazibwa na Petr Cech.

Esha Buheti achekelea tuzo mbili kwa mpigo

Esha Buheti akiwa na tuzo yake ya ACVCA-2014
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiVLR6SKy55g1ZgzkaXh0gpsrnv1_T8oa6EBwc7LrSGGG6KbSjBI5WwFEbyB69EgDwDS4spNTr4l3syPUdQ8KGG3x-33z7oUTejlSRFKTZkmTpdbBaYjKLLVlJaOzLLQcpKyKLUYcQM44vG/s1600/2.jpg
Esha Buheti katika pozi
MSHINDI wa Tuzo za filamu za Action & Cuts Viewers Choice (ACVCA-2014) Esha Buheti amesema mafanikio aliyopata kwa kipindi kifupi katika tasnia hiyo imetokana na kipaji cha kuzaliwa, kujituma na kujiheshimu mbele ya jamii.
Esha alisema, amejisikia faraja kuona ndani ya kipindi kisichozidi miezi mitatu akinyakua tuzo ya pili baada ya ile ya ZIFF-2014 (Tamasha la Kimataifa la Filamu la Zanzibar) na katu hatavimba kichwa badala yake kuongeza bidii afike mbali zaidi.
Mrembo huyo alisema kuwashinda nyota wa filamu kama Chuchu Hans, Salma Jabu 'Nisha', Shamsa Ford na Blandina Chagula 'Johari' siyo kazi ndogo na kusisitiza anashukuru wote waliopigia kura za kutosha na kunyakua tuzo hiyo ya pili.
"Kwa kweli nimejisikia faraja kubwa kwa lililonitokea, sikuamini kama ningeweza kuibukia mshindi mbele ya washindani wangu ambao naamini ni wakali. Hii ni changamoto kwangu kundelea kufanya vyema ili nitambe kimataifa," alisema.
Muigizaji huyo alishinda tuzo hiyo wiki iliyopita katika kipengele cha Muigizaji Bora Msaidizi, ikiwa ni miezi mitatu tangu alipotwaa tuo ya Muigizaji Bora wa Kike wa ZIFF-2014 kupitia filamu ya 'Mimi na Mungu Wangu' anayoitaja kama kazi bomba kwake.

Hammer Q kuweka kibakuli chake videoni

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjPuXhtoeR4zztOCIdP7ZAekZVHi6Yl2h8tpe5fFNe4ECtPzhUsg7Z-Na338MBN_tvxM5xrs2kGZ0v9Fn6DnsJSOz75hXNxqqYAL7QbNtlUvMB7tp7ZN4t-71MOswqFm3nnUcz3wFF5r6g/s1600/Hammer+Q.jpgMUIMBAJI mahiri wa muziki wa taarab, Hammer Q ameachiwa wimbo wake binafsi uitwao 'Kibakuli', ambao anajipanga kuutengenezea video yake mapema hivi karibuni.
Hammer Q aliyewahi kutamba kwenye muziki wa kizazi kipya na wimbo wa 'Lady' kabla ya kuhamia kwenye taarab, ameachiwa wimbo huo uliopo kwenye mduara.
Wimbo huo umetengenezwa na mtayarishaji aitwae Anta Nation na  umeanza kutamba kwenye redio na mitandao ya kijamii.
Msanii huyo amesema kwa sasa anafanya mchakato ili kutengeneza video ya wimbo huo mapema kuwapa burudani zaidi mashabiki wake.
Hammer Q mbali na kufanya muziki kama 'solo artist' pia analiimbia kundi maarufu na miondoko ya mduara ya Zanzibar la Offside Trick sambamba na kufanya kazi na mkewe Salha Abdallah 'Salha wa Hammer'

Ligi ikienda mapumziko, Yanga yapumua, Mtibwa Sugar inatisha

Yanga wanaenda mapumziko wakipumua nafasi ya tatu
Coastal Union bado wanajikongoja

Watetezi Azam wakiporomoka hadi nafasi ya pili wakiwapisha Mtibwa kuwaongoza
Mtibwa timu pekee iliyoshinda mechi zake 100%

Ruvu Shooting ndiyo ambayo haijafunga bao hata mmoja mpaka sasa. Ni kwamba pengo la Maguli (kushoto) halijapata mrithi wa kuliziba?
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgboM03iAUZPCYvuYadSX-DrgxLYiOqanpQRh7w9oQyCDx_BclL4a6oF2VrzSbdjwrhAhFHPKlzRnMprs771Eep9DtnpEeGeoC5KrCHMmrC1wfNHGwyf56QiZMMSUqM8AmM2gVywZA6S2I/s1600/HMB_8265.JPG
Simba wataivaa Yanga mechi ijayo ikiandamwa na mdudu wa sare
RAUNDI ya tatu ya Ligi Kuu Tanzania Bara umemalizika  mwishoni mwa wiki na kushuhudia jumla ya mabao 44 yakitinga wavuni, huku mshambuliaji wa Azam Didier Kavumbangu akiongoza kwa kupachika mabao manne kati ya hayo.
Kavumbagu aliyetua Azam akitokea Azam anafuatiwa kwa karibuni na Ally Shomari wa Mtibwa mwenye mabao matatu kiisha kufuatiwa na wachezaji wanne wenye mabao mawili kila mmoja.
Timu yenye fowadi kali mpaka sasa wakati lihi ikienda mapumziko kwa wiki moja ni Mtibwa Sugar na Ndanda FC zenye mabao sita kila moja, kisha kufuatiwa na Azam yenye mabao matano kisha Yanga na Simba zikafuatia zikiwa zimetumbukiza kimiani mabao manne kila moja.
Pamoja na kuwa kinara wa kufunga mabao Ndanda pia ndiyo timu yenye ukuta mwepesi ikiruhusu mabao sita mpaka sasa ikifuatiwa na timu za Stanmd United na Polisi waliopanda pamoja ligi ya msimu huu zikiwa zimeruhusu mabao matano.
Ruvu Shooting ndiyo timu iliyo na safu butu mpaka sasa ikiwa haijafunga bao lolotewakifuatiwa na Mbeya City, Mgambo na JKT Ruvu wenye bao moja moja.
Ukuta wa chuma wa ligi hiyo mpaka sasa ni ule wa klabu ya Mbeya City ambayo haujaruhusu bao lolote kwake huku Mtibwa Sugar na Azam zikifuata kwa kufungwa bao moja tu kila moja.
Yanga ambayo ilianza kwa kipigo katika ligi ya msimu huu imechupa toka maeneo ya kati hadi nafasi ya tatu wakiwaacha watani zao watakaoumana nao katika mechi yao ijayo wakiwa na pointi tatu wakishika nafasi ya 10.


MSIMAMO KAMILI WA LIGI KUU TANZANIA BARA 2014-2015
                               P   W    D    L    F    A   GD   Pts

01. Mtibwa Sugar     03  03   00  00  06   01  +5   09
02. Azam                 03  02   01  00  05   01  +4   07
03.Yanga                  03  02   00  01  04   04  00   06
04. Mbeya City          03  01  02  00  01   00  +1   05
05.Kagera Sugar       03  01  01   01  03   02 +1   04
06. Prisons                03  01  01   01  03  02  +1  04
07.Coastal Union       03  01  01   01  04  04   00  04
08.Stand Utd             03  01  01   01  03   05  -2   04
09. Ndanda Fc           03  01  00   02  06    06  00  03
10.Simba                  03  00  03   00  04    04  00  03
11. Mgambo JKT       03  01  00   02   01    02  -1  03
12. Polisi Moro          03  00   02  01   03    05   -2  02
13.JKT Ruvu             03  00   01  02   01   04   -3  01
14. Ruvu Shooting     03  00  01   02  00   04   -4  01

http://static.goal.com/462500/462526_heroa.jpg
Didier Kavumbangu  (kushoto) akipongezwa na wenzake
Wafungaji Bora:
4- Didier Kavumbagu(Azam)


3-
Ally Shomari (Mtibwa)


2-
Shaaban Kisiga (Simba), Nassor Kapama (Ndanda), Ame Ally (Mtibwa), Rashind Mandawa (Kagera)


1- Emmanuel Okwi, Amissi Tambwe (Simba), Coutinho, Kelvin Yondan, Haruna Niyonzima, Simon Msuva (Yanga), Deo Julius (Mbeya City), Danny Mrwanda, Nicolaus Kabipe, Bakari (Polisi-Moro),  Salum Kanoni,  (Kagera), Aggrey Morris  (Azam), Ernest Joseph, Paul Ngalema, (Ndanda), Jacob Mwaitalako, Ibrahim Kihaka, Laurian Mpalile (Prisons), Lutimba Yayo, Rama Salimu, Joseph Mahundi, Hussein Sued, (Coastal), Ramadhani Pella (Mgambo), Mussa Mgosi (Mtibwa), Jabir Aziz (JKT Ruvu), Salum Kamana, Heri Mohammed, Mussa Said(Stand Utd)

Baby Madaha 'ala shavu' Ujerumani

STAA wa 'Amore' na 'Summer Holliday', Baby Madaha amekula shavu baada ya kuteuliwa kwenda kushiriki filamu ya kimataifa nchini Ujerumani iitwayo 'Saint & Ghost'.
Muigizaji huyo aliliambia MICHARAZO kuwa, anajiandaa kupaa kwenda Ujerumani kushiriki filamu hiyo itakayotengenezwa na mtayarishaji maarufu Dittiman.
Baby Madaha alisema filamu hiyo itawashirikisha pia waigizaji wengine kutoka nchini Ujerumani na kutamba ni nafasi yake ya kujitangaza zaidi kimataifa.
"Nashukuru Mungu nimepata bahati ya kuteuliwa kwenda kushiriki katika filamu inayotengenezwa na Prodyuza Dittiman iitwayo 'Saint and Ghost' kazi hiyo itafanyika nchini Ujerumani," alisema Baby Madaha.
Msanii huyo anayepanda farasi wawili kwa wakati mmoja kwa maana ya kuimba muziki na kucheza filamu, alisema uteuzi wake umekuja baada ya kuwavutia waratibu wa filamu hiyo kupitia kazi mbalimbali alizocheza ambazo zimekuwa zikifanya vyema kimataifa.
Baadhi ya filamu alizocheza mwanadada huyo ni 'Desperado', 'Ray of Hope', 'The Gal Bladder', 'The Lost' na 'House No. 44'.

SHIWATA kuadhimisha Miaka 10 kwa sherehe la nguvu

Mwenyekiti wa SHIWATA, Cassim Twalib 'Teacher' akifafanua jambo kwenye mkutano na wanahabari hivi karibuni
MTANDAO wa Wasanii Tanzania (Shiwata) wenye maskani yake Ilala jijini Dar es Salaam, unatarajia kufanya sherehe ya kutimiza miaka kumi tangu ulipoanzishwa Desemba mwaka 2004.
Kwa mujibu wa mwenyekiti wa mtandao huo, Cassim Talib, sherehe hizo zitafanyika Desemba mwaka huu katika kijiji cha wasanii kilichopo Mwanzega wilaya ya Mkuranga mkoani Pwani.
Talib alisema kuwa katika sherehe hizo ambazo zitapambwa na burudani za mpira wa miguu, ngumi, ngoma za asili na nyingine nyingi kutoka kwa wasanii ambao ni wanachama wa Shiwata.
"Katika sherehe yetu hiyo ya kutimiza miaka kumi tangu tulipoanzisha mtandao huu kutakuwa na zoezi la kugawa nyumba kwa wasanii ambazo zitakuwa zimekamilika wakati huo wa Desemba," alisema Talib.
Alisema kuwa mtandao huo una wanachama 8,000 ambao baadhi yao wamekuwa wakichangia fedha kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za wasanii na sasa Shiwata imegawa 66 ambazo tayari zimekamilika..
Mwenyekiti huyo alisema kuwa kuna nyumba 45 ambazo zinaendelea kujengwa hadi sasa na kwamba ana uhakika kufikia Desemba zitakuwa zimekamilika na kugawiwa kwa wahusika wakati huo wa sherehe za kutimiza miaka kumi.
 "Tunatarajia kusherekea miaka kumi ya kuanishwa kwa mtandao wetu tukiwa tumepitia changamoto nyingi zikiwamo za kuzushiwa kuwa sisi ni matapeli na kila aina ya uzushi, lakini tumeshinda hizo njama za kutuhujumu na sasa tunaendelea kusonga mbele," alisema.

Baby J kutanguliza Katapila lake videoni

http://www.bongo5.com/wp-content/uploads/2014/01/baby-J.jpg
NYOTA wa muziki wa kizazi kipya kutoka visiwani Zanzibar, Jamila Abdullah 'Baby J' amesema ameamua kubadili mawazo ya kuachia 'audio' ya 'Katapila' na badala yake ataanza na video.
Akizungumza na MICHARAZO, Baby J alisema ameamua kutoa video kabla ya 'audio' kwa nia ya kuwapa ladha tofauti mashabiki wake.
Baby J alisema video hiyo inayoendelea kurekodiwa na kampuni ya Visual Lab (Next Level) chini ya mtaalam Adam Juma na ataiachia hewani mara baada ya kukamilika kurekodiwa.
"Badala ya kuanza kuachia 'audio' ya 'Katapila' nimeamua nitoe kwanza video ambayo inaendelea kutengenezwa na Adam Juma,' alisema Baby J.
Wimbo huo mpya unaokuja baada ya 'Nimempenda Mwenyewe' kufanya vema hewani, umetengenezwa na maprodyuza wawili tofauti, Shirko na Lil Ghetto.

Wasanii wahimiza kuhudhuria semina ya Haki Miliki

Kama wanavyopeana sapoti kwenye tuzo wasanii wanapaswa pia kuhudhuria semina mbalimbali kupata uelewa na wa mambo yanayowakwaza
Na Kipimo Abdallah
UMOJA wa Mashirikisho ya Sanaa Tanzania umewaomba wasanii nchini kujitokeza katika semina ambayo inatarajia kufanyaka Oktoba mwaka huu katika Ukumbi wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Umoja huo Godfrey Ndimbo wakati akizunumza na waandishi wa habari  jijini Dar es Salaam.
Alisema umoja wao unatoa pongezi kwa taasisi hiyo ya Haki Neel Production Company ambayo imetambua msanii wa Tanzania.
Ndimbo alisema semina hiyo itajikita katika kuwaelimisha wasanii kuhusu mafao ya uzeeni, matibabu kupitia bima ya afya, Haki Miliki, Haki Shiriki na Kodi.
“Napenda kuwaomba wasanii wa Tanzania kujitokeza kwa wingi katika semina hiyo kwani itawajengea uwezo mzuri katika kutambua haki zao nyingi ambazo zinakiukwa, ” alisema.
Ndimbo alisema katika semina hiyo wanatarajia kuwahusisha watumishi kutoka taasisi mbalimbali kama Poilisi, Uhamiaji na Mahakimu.
Katibu Mkuu huyo alisema lengo la kushirikisha sekta hizo ni kuhakikisha kuwa wanakuwa na ufahamu dhidi ya kazi hizo za wasanii nchini ili wajione kuwa wana haki ya kutetea kazi hizo.
Alisema lengo ni kuhakikisha kuwa sheria inayotumika kutoa hukumu kwa husika inakuwa na tija kwani kwa sasa ni ndogo jambo ambalo linakwamisha maendele ya tasnia hiyo.
Katibu Mkuu huyo alisema pia wanawakaribisha waandishi wa habari katika semina hiyo ili kuhakikisha kuwa wanakuwa na ufahamu mzuri wa kutosha kuhusiana na tasnia hiyo.
Alitoa wito kwa wadau wengine kujitokeza kwa wingi ili kusaidia na taasisi ya Haak Neel Production Company ambayo imeonyesha jitihada za kutambua nafasi ya msanii.
mwisho

Monday, October 6, 2014

Kassim Selembe achekelea kunolewa na Rishard Adolph

KIUNGO mshambuliaji mpya wa Polisi Moro, Kassim Suleiman 'Selembe' amesema anajisikia faraja kubwa kufanya kazi chini ya nyota wa zamani wa kimataifa wa Tanzania Mohammed Rishard 'Adolph'.
Aidha mchezaji huyo aliyekuwa akiichezea Coastal Union, alisema kusuasusa kwa Polisi kwa sasa kunatokana na 'ugeni' wao wa Ligi Kuu, ila kadri watakavyokuwa wakiizoea watawashangaza watu.
Akizungumza na MICHARAZO, Selembe, alisema anajisikia furaha kufanya kazi na kocha Adolph, nyota wa zamani wa Yanga, Pan Africans na Taifa Stars ikizingatiwa ni moja wa nyota wa Tanzania waliojijengea jina kubwa Afrika.
"Kwa mchezaji yeyote anayejitambua kufanya kazi na mtu kama Adolph ni fahari kwa sababu alijijengea jina kubwa ndani na nje ya Tanzania enzi za uchezaji wake, wachezaji tunamfurahia," alisema.
Kiungo wa zamani wa Azam alisema kocha Adolph ni bonge la kocha na anawafanya wachezaji wa Polisi kujiamini na kurejea Ligi Kuu kabla ya yeye kuungana nao akitokea Coastal Union.
Juu ya mwenendo wa kikosi chao, Selembe alisema wanazidi kuimarika kadri wanavyoizoea ligi na kwamba hawana hofu ya kurejea walikotoka akidai ni mapema mno kujadili jambo hilo.
Timu hiyo ilipanda daraja sambamba na Ndanda na Stand United na ilianza kwa kufungwa mechi moja na kuambulia sare mbili katika mechi zao tatu za awali ya ligi hiyo inayoenda mapumziko.
Ligi hiyo itakuwa likizoni kwa wiki moja kupisha mchezo ya kimataifa ya kirafiki unaotambuliwa FIFA Taifa Stars itakapovaana na Benin na itaendelea tena kuanzia Oktoba 18.

Jahazi la QPR lazidi kutota, wapigwa 2-0 na West Ham

QPR  defender Rio Ferdinand
Rio Ferdinand akiwajibika na QPR akifikisha mechi ya 500 katika miaka ya 18 ya kucheza kwake
West Ham United v QPR
Ooh kitu! Wachezaji wa QPR hawaamini wakitunguliwa bao na West Ham
West Ham v QPR
Yebaaa! Wachezaji wa West Ham wakipongeza kwa kupata ushindi wa mabao 2-0 kwa vibonde QPR
JAHAZI la timu ya QPR linaloongozwa na kocha Harry Redknapp limezidi kuzama baada ya jana kucharazwa mabao 2-0 na West Ham United katika mfululizo wa Ligi Kuu ya England.
QPR wenye pointi na kuburuza mkia walianza vibaya mchezao huo baada ya beki wake kutoka Nigeria Chinedum Onuoha, aliyewahi kuichezea Mancjester City kujifunga bao dakika ya tano tu ya mchezo huo uliochezwa Uptown Park.
Kipindi chja pili kilikuwa majanga zaidi kwa wageni baada ya Diafra Sakho kuongeza bao la pili kwa West Ham kwa kuunganisha mpira wa kichwa katika dakika ya 55 na kuifanya West Ham kuchupa toka nafasi ya tisa katika msimamo wa ligi hiyo hadi ya saba, wakati QPR wakiendelea kung'ang'ania mkiani.
QPR haijawahi kushinda mechi yoyote ya uwanja wa ugenini tangu Machi 2, 2013.

Allan Kamote, Thomas Mashali mabingwa wapya wa UBO

Allan Kamote (kulia) akionyeshana umwamba na Osgood Kayuni wa Malawi katika pambano lao la kuwania Mkanda wa Dunia wa UBO na Kamote kushinda kwa pointi.
Thomas Mashali akimrushia konde Ramadhani Ali 'Alibaba' katika pambano lao lililochezwa jana kwenye uwanja wa Mkwakwani na Mashali kushindwa kwa TKO ya raundi ya tatu na kutwaa ubingwa wa UBO Afrika
MABONDIA Allan Kamote na Thomas Mashali wametawazwa kuwa mabingwa wa UBO baada ya kushinda mapambano yao ya ngumi za kulipwa yaliyofanyika jana uwanja wa Mkwakwani-Tanga.
Kamote alifanikiwa kutwaa ubingwa wa Dunia wa UBO baada ya kumshinda kwa pointi bondia Osgood Kayuni kutoka Malawi katika pambano la raundi 12 la uzani wa Light.
Naye bondia Thomas Mashali alimchapa kwa TKO ya raundi ya tatu Mtanzania mwenzake Ramadhani Ali 'Alibaba' na kutwaa mkanda wa UBO Afrika katika pambano lao la raundi 10 na uzito wa kati. Michezo hiyo iliratibiwa na Shirikisho la Ngumi za Kulipwa Tanzania (PST) na ilishuhudiwa pia Francis Miyeyusho akimshinda kwa pointi bondia wa Tanzania anayeishi Kenya Emilio Norfat.
Bondia Kamote licha ya kufanikiwa kutwaa mkanda huo wa Dunia wa UBO, lakini pia amefanikiwa kulipa kisasi kwa mpinzani wake kutoka Malawi aliyewahi kupigana naye mara mbili na kupigwa.
Katika pambano hilo mabondia wote walikuwa wakiviziana na kutupiana makonde kwa ufundi, hali ambayo iliwafanya mashabiki kuwa roho juu kwa kutojua nani atakayeibuka na ushindi hadi jaji alipotangaza matokeo yaliyompa ushindi Kamote.
Katika mechi nyingine za utangulizi, bondia Francis Miyeyusho alimshinda kwa pointi Emilio Norfat, huku Jacob Maganga na Said Mundi wakishindwa kutambiana kwa kutoka sare.

Ronaldo azidi kutesa La Liga, Messi abakisha 2 tu!

Cristiano Ronaldo
Ronaldo akishangilia moja ya mabao yake matatu usiku wa jana
Lionel Messi of Barcelona
Messi akifunga bao lake la 349 katika La liga dhidi ya Rayo Valecano
WAKATI Lionel Messi akiwa amesaliwa na mabao mawili tu ili kufikia rekodi ya mabao katika Ligi Kuu ya Hispania, mpinzani wake Cristiano Ronaldo usiku wa jana alifunga hat-trick yake ya 22 wakati akiisaidia Real Madrid kushinda nyumbani kwa mabao 5-0 dhidi ya Athletic Bilbao.
Ronaldo alifunga mabao hayo katika dakika za 2, 55 na 88 akisaidiwa na Gareth Bale na Pepe, huku mabao mengine yakiwekwa kimiani na Karim Benzema katika dakika za 41 na 69 na kuifanya Madrid kufikisha jumla ya pointi 15, nne nyuma ya vinara Barcelona ambao wameendelea kushinda mfululizo katika ligi hiyo.
Mabao hayo yamemfanya Ronaldo kufikia rekodi ya ha trick nyingi za gwiji wa Madrid Alfredo de Stephano na Telmo Zarra waliowahi kufunga pia hat trick 22 akimtangulia Messi mwenye ha trick 19 akikamata nafasi ya tano.
Hata hivyo Messi aliisaidia Barcelona kushinda mechi yao ya sita na kuweka rekodi ya kutoruhusu kufungwa bao lolote katika mechi saba mfululizo wakati wakiizamisha Rayo Valecano kwao kwa mabao 2-0.
Messi alifunga bao lililomfanya afikishe jumla ya mabao 349 katika La Liga na kushika nafasi ya pili nyuma ya  gwiji wa zamani wa Athletic Bilbao, Telmo Zarra aliyetamba miaka ya 1940-50 aliyefunga mabao 351, ikiwa na maana akifunga mabao mawili tu atamfikia na kuifukizia rekodi mpya katika ligi hiyo maarufu.
Bao jingine la wababe hao wa Nou Camp liliwekwa kimiani na Neymar na kuwafanya wachezaji hao wawili wanaotoka mataifa hasimu katika soka Amerika ya Kusini, Argentina na Brazil kufikisha jumla ya mabao 13 wakicheza pamoja..
Katika mechi nyingine za ligi hiyo Atletico Madrid iokiwa ugenini ilikumbana na kipigo cha mabao 3-1 kutoka kwa Valencia, huku Cordoba na Getafe walitoka sare ya 1-1 na Eibar kulazimishwa sare ya mabao 3-3 na Levante.
Almeria na Elche zilitoshana nguvu kwa sare ya 2-2 na Malaga ikaifumua 2-1 Grenada waliwafuata nyumbani kwao, huku Sevilla ikipata ushindi mnono nyumbani dhidi ya Deportivo la Coruna waliowafumua mabao 4-1 na Celta Viro ililala nyumbani 3-1 kwa Villarreal na Espaniol ilitaka nyumbani kwa kuilaza Real Sociedad kwa mabao 2-0.
ANGALIA WAKALI WA HAT TRICK LA LIGA
Cristiano Ronaldo 22
Alfredo Di Stefano 22
Telmo Zarra 22
Edmundo Suarez 19
Lionel Messi 19
Barcelona's Lionel Messi and Neymar
Neymar na Messi wakishangilia mabao yao wakati wakishinda ugenini na timu iliyopoteza wachezaji wao wawili uwanjani kw akandi nyekundu Rayo Valecano.






























































Sunday, October 5, 2014

Juventus yaizamisha As Roma, Tevez moto chini!

https://s.yimg.com/bt/api/res/1.2/etgxU0ykbfbKLMs4UzzcCw--/YXBwaWQ9eW5ld3M7cT04NTt3PTYzMA--/http://l.yimg.com/os/publish-images/sports/2014-10-03/dba924d0-4b36-11e4-9a01-6d10b444caf4_Totti_Juve_0310.jpgCARLOS Tevez amezidi kung'ara nchini Italia baada ya jioni ya leo kuifungia timu yake ya Juventus mabao mawili wakati 'Kibibi cha Turin' kikiwazima As Roma kwa mabao 3-2 kwenye pambano la kusisimua la Seria A, huku timu zote mbili zikicheza pungufu wa mchezaji mmoja mmoja baada ya wachezaji wao kupewa kadi nyekundu kwa nyakati tofauti kutokana na madhambi.
Tevez ambaye amekuwa akichuniwa kuitwa katika timu ya taifa ya Argentina, alifunga mabao yake yote kwa mikwaju ya penati katika dakika ya 27 na 45 wakati bao jingine likiwekwa kimiani na Bonucci dakika nne kabla ya pambano hilo kumalizika.
Mabao ya wageni yalifungwa na Francisco Totti pia kwa mkwaju wa penati dakika ya 32 na Iturbe dakika ya 44.
Kwa ushindi huo Juventus wamezidi kujichimbia kileleni mwa msimamo wa ligi hiyo wakiwa na pointi 18 tatu zaidi ya wapinzani wao hao waliokuwa wametofautiana mabao ya kufunga na kufungwa kwenue msimamo huo.
Katika mechi nyingine ya ligi hiyo mapema leo mchana Empoli ikiwa nyumbani ilipata ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Palermo, huku Lazio ikiizamisha Sassuolo kwa mabao 3-2 waliowafuata nyumbani kwao, Parma walikubali kipigo cha magoli 2-1 dhidi ya wageni wao Genoa na Atalanta ikafa ugenini kwa bao 1-0 dhidi ya Sampdoria.
Timu za Udinese na Cesena zilitoshana nguvu kwa kufunga bao 1-1 na hivi sasa kuna mechi mbili zinachezwa ambazo hata hivyo haziwezi kubadilisha msimamo wa nafasi za juu za ligi hiyo.











































Mtibwa Sugar ushindi 100%, Shomar ampumulia Kavumbagu

WAKATI Mtibwa Sugar ikikwea kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara kwa kuiengua Azam, Ally Shomari, mshambuliaji huyo wa Mtibwa amemuashia taa ya kijani Didier Kavumbagu kwa kufikisha bao la tatu kwenye orodha ya wafungaji bora wa ligi hiyo.
Shomari ndiye aliyeifungia Mtibwa Suigar bao pekee lililoizamisha Mgmabo JKT katika mfululizo wa mechi za ligi kuu katika pambano lililochezwa kwenue uwanja wa Manungu, Turiani Morogoro.
Mtibwa imeweka rekodi ya kushinda mechi zake zote tatu na kufikisha pointi 9 na kukwea kileleni mwa msimamo wakiizidi mabingwa watetezi Azam kwa zaidi ya pointi mbili baada ya timu hiyo jana kulazimishwa suluhu na Prisons-Mbeya.
Shomari alifunga bao hilo dakika ya 10 ya pambano hilo na kufanya afikishe idadi ya mabao matatu akiwa nyuma ya Kavumbagu kwa bao moja.
Didier anaongoza msimamo akiwa na mabao manne, kisha Shomar na kufuatiwa na wachezaji wanne wenye mabao mawili kila mmoja ambao ni Ami Ali wa Mtibwa Sugar, Shaaban Kisiga wa Simba, Rashid Mandawa wa Kagera Sugar na Nassor Kapama wa Polisi Morogoro.

Chelsea waizima Arsenal, Diego Costa hakamatiki

Chelsea striker Diego Costa
Diego Costa akishangilia bao lake dhidi ya Arsenal
KOCHA Arsene Wenger bao hajapata tiza ya kumuzia Jose Mourinho baada ya timu yake ya Arsenal kulala mabao 2-0 mbele ya vijana wa darajani jioni hii katika mfululizo wa Ligi Kuu ya England.
Chelsea ikiwa chini ya Mourinho imekuwa ikiiadhibu Arsenal itakavyo, kitu ambacho kiliendelea leo kwenye uwanja wa Stanford Bridge wakati Chelsea walipopata ushindi huo kupitia mabao ya Eden Hazard aliyefungwa kwa mkwaju wa penati dakika ya 27 kabla ya kinara wa mabao katika ligi Diego Costa kufunga bao la pili katika dakika ya 78 akimalizia kazi nzuri ya Cesc Fabregas na kumfanya kufikisha jumla ya mabao tisa katika ligi hiyo.
Mechi inayoendelea kwa sasa ni kati ya West Ham ambayo ipo nyumbani kuikaribisha QPR na mpaka sasa ikiwa ni dakika chache tangu kuanza wenyeji waoangoza kwa bao 1-0.

Yanga yaendeleza ubabe kwa JKT, yailaza 2-1

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgG0sWioDjCpGG40C4qUjeSnrZ5lrebFf2rc_lRpb6I6-j-HYwaQ3Nhcesj__-Vf7nKoJMj-thfsQvtm8cL1B08Qx6iA2ddT5UGIZnuAtpihh_U1I_ECWTu1qevGqLpIZVSJIV2OjmX1XE/s640/HERM5680.JPGKLABU ya soka ya Yanga wameendelea kuwapa raha mashabiki wao baada ya jioni hii kupata ushindi muhimu wa mabao 2-1 dhidi ya JKT Ruvu na kuendeleza ubabe kwake kwa maafande hao katika Ligi Kuu Tanzania Bara.
Yanga ilipata ushindi huo kwenye uwanja wa Taifa na kuifanya timu hiyo kuchupa hadi nafasi ya tatu ya msimamo ikizipumulia timu za Mtibwa na Azam waliopo mbele yao.
Beki Kelvin Yondani aliianza kuiandika Yanga bao dakika ya 37 kwa mkwaju mkali ulioifanya timu yake kwenda mapumziko ikiwa mbele kwa bao hilo.
Kiungo wa kimataifa wa Rwanda, Haruna Niyonzima aliiongezea Yanga bao kipindi cha pili kabla ya Jabir Aziz kuifungia JKT Ruvu bao la kufutria machozi dakika chache kabla ya mapumziko.
Kwa ushindi huo Yanga imefikisha pointi sita wakati JKT wamendelea kusalia kwenye nafasi ya pili toka mkiani kutokana na kuwa na pointi mopja sawa na ndugu zao wa Ruvu Shooting Stars.
Mechi ijayo kwa Yanga itakuwa ni kati yao na watani zao Simba ambao wapo katika hali mbaya kwa kutoka sare katika mechi tatu mfululizo kiasi cha kubatizwa jina la wazee wa sare na watani zao.

Manchester Utd, Spurs zaua England, Di Maria achaa bwana!

Radamel Falcao
Falcao akishangilia bao lake lililokuwa la pili kwa Mashetani Wekundu mapema leo
Angel di Maria celebrates
Di Maria akishangilia bao la kwanza la Man Utd ambalo ni la tatu kwake tangu ajiunge na timu hiyo
Tottenham playmaker Christian Eriksen (left) rifles in a shot to put his side in front against Southampton
Erikson akiifungia Spurs bao dhidi ya Southampton

Radamel Falcao akishangilia bao lake la kwanza tangu ajiunge Old Trafford
Angel Di Maria celebrates scoring Manchester United's first goal against Everton on 27 minutes - it was his third goal in a United shirt
Angel Di Maria akishangilia baada ya kufunga goli la uongozi la Manchester United dhidi ya Everton kunako dakika ya 27 hili likiwa ni goli lake la tatu tangu kujiunga United
Di Maria celebrated by replicating the heart-shaped celebration of his former Real Madrid colleague Gareth Bale
MABAO mawili kutoka kwa wachezaji waliosajiliwa hivi karibuni, Angel di Maria na Radamel Falcao yameisaidia Manchester United kuchupa hadi nafasi ya nne ya msimamo wa Ligi Kuu England baada ya kuilaza timu ya Everton kwa mabao 2-1.
Wakiwa kwenye uwanja wao wa nyumbani wa Old Trafford, Mashetani Wekundu walionyesha dhamira ya ushindi kwa kuandika bao la kwanza lililofungwa na Di Maria dakika ya 27 akimalizia pasi ya Juan Mata.
Bao hilo lililodumu hadi mapumziko kabla ya wageni kuchomoa kupitia kwa Naismith katika dakika ya 55 kama ya nyota wa zamani wa Atletico Madrid na Monaco Falcao kufunga bao la ushindi dakika ya 62 kwa kazi nzuri iliyofanywa na di Maria na kuwapa ushindi muhimu vijana wa Luis Van Gaal.
Katika pambano jingine la ligi hiyo Tottenham Hotspur ikiwa uwanja wa nyumbani wa White Hartlane walipata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Southampton.
Bao pekee la pambano hilo lilifungwa na Christian Eriksen dakika ya 40 na kuwafanya Spurs kupata ushindi muhimu na pointi tatu zilizowafanya kufikisha jumla ya pointi 11 na kuchupa hadi nafasi ya sita.

HILI NDILO BANGO LA TFF SIKU YA LEO

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEijr9kkxAeelCLIoQDTDWazSPHrj9DPBX1uk9mq_cWwffJecJpO5SimMeqNKlsoXYrao2j9DZ3-fPjcRnpcNFuvRrKHCJIOs9smSGK8yNMGsKep-uVyJwBJyCxrvDjki5M8BDTM5Qqdxbo/s1600/tff_LOGO1.jpg
STARS KAMBINI, WACHEZAJI WA NJE WATUATimu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) inaingia kambini kesho (Oktoba 6 mwaka huu) kujiwinda kwa mechi ya Kalenda ya Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) dhidi ya Benin itakayochezwa Oktoba 12 mwaka huu jijini Dar es Salaam.

Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager inaingia kambini kwenye hoteli ya Accomondia jijini Dar es Salaam ikiwa na kikosi cha wachezaji 26 walioitwa na Kocha Mart Nooij kwa ajili ya mechi hiyo itakayochezwa kuanzia saa 11 jioni.

Kwa mujibu wa Kocha Nooij, timu hiyo itakuwa na vipindi (sessions) 11 vya mazoezi kabla ya kucheza na Benin (Squirrels). Stars itafanya mazoezi asubuhi na jioni kuanzia Jumatatu hadi Ijumaa ambapo baadhi yatafanyika Uwanja wa Taifa, na mengine kwenye uwanja mwingine.


Wachezaji Thomas Ulimwengu na Mbwana Samata wanaochezea timu ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC) pamoja na Mwinyi Kazimoto anayechezea timu ya Al Markhiya ya Qatar wanawasili nchini kesho (Oktoba 6 mwaka huu).

Naye mshambuliaji Juma Liuzio anayechezea timu ya Zesco ya Zambia atawasili nchini keshokutwa (Oktoba 7 mwaka huu) kwa ndege ya Kenya Airways akitokea Ndola.

MAFUNZO YA USAJILI LIGI DARAJA LA PILIShirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) litaendesha mafunzo ya usajili kwa klabu za Ligi Daraja la Pili (SDL) yatakayofanyika kesho na keshokutwa (Oktoba 6 na 7 mwaka huu) kwenye hosteli ya TFF iliyopo Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume kuanzia saa 3 asubuhi.

Mafunzo hayo yatahusu usajili wa mtandao ambao ndiyo klabu hizo zitautumia kwa ajili ya Ligi hiyo itakayoanza baadaye mwezi ujao katika makundi manne ya timu sita sita kwa mtindo wa nyumbani na ugenini.

Kesho mafunzo hayo yatakuwa kwa ajili ya maofisa wa usajili wa klabu za Abajalo, Arusha FC, Kiluvya United, Magereza Iringa, Milambo SC, Mji Mkuu (CDA), Mkamba Rangers, Mshikamano, Mvuvumwa FC, Navy, Njombe Mji, Singida United, Transit Camp, Volcano FC na Wenda FC.

Oktoba 7 mwaka huu mafunzo hayo yatahusisha maofisa usajili wa klabu za Bulyanhulu FC, Eleven Stars, JKT Rwamkoma, Kariakoo Lindi, Mbao FC, Mpanda United, Pamba, Town Small Boys na Ujenzi Rukwa.

MABADILIKO YA MECHI ZA FDL KUNDI BShirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limefanya mabadiliko kwa baadhi ya mechi za kundi B Ligi Daraja la Kwanza (FDL) baada ya kupokea barua kutoka Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Mwanza (MZFA) ikieleza kuwa Uwanja wa CCM Kirumba utatumika kwa shughuli za kidini kuanzia Oktoba 16 hadi 19 mwaka huu.

Kutokana na hali hiyo, mechi namba 17 kati ya Toto Africans na Green Warriors iliyokuwa ichezwe kwenye uwanja huo Oktoba 18 mwaka huu sasa itafanyika Oktoba 20 mwaka huu.

Mabadiliko hayo pia yameathiri mechi namba 19 kati ya Green Warriors na Oljoro JKT ambayo sasa itachezwa Uwanja wa Karume, Dar es Salaam, Oktoba 23 mwaka huu badala ya Oktoba 21 mwaka huu.

Vilevile mechi namba 25 kati ya Burkina Faso na Oljoro JKT imesogezwa mbele kwa siku moja kutoka Oktoba 25 mwaka huu hadi Oktoba 26 mwaka huu. Mechi hiyo itachezwa Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.

BONIFACE WAMBURA
MKURUGENZI WA MASHINDANO
SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA

AC Milan yazinduka Italia, Muntari aibeba Juve, Roma leo

Sulley Muntari
Sulley Muntari
BAADA ya kucheza mechi tatu bila ushindi hatimaye mabingwa wa zamani wa Italia na Ulaya, AC Milan imezinduka kwenye Ligi Kuu ya Italia Seria A baada ya kupata ushindi mujarabu nyumbani kwao dhidi ya Chievo Verona.
AC Milan inayonolewa na mshambuliaji nyota wa zamani wa timu hiyo na Azzurri timu ya taifa ya Italia, Philip Inzaghi 'Pipo' ilipata ushindiwa mabao 2-0 kwenye uwanja wa Giuseppe Meazza, mjini Milano kupitia mabao ya Sulley Muntari aliyefunga dakika ya 55 na Keisuke Honda aliyeongeza la pili kwa mkwaju wa adhabu ndogo dakika ya 78 na kuifanya Milan kufikisha jumla ya pointi 11 na kuchupa hadi nafasi ya nne ya msimamo wa ligi hiyo unaoongozwa na Juventus.
Katika mechi nyingine iliyochezwa jana katika mfululizo wa ligi hiyo timu Hellas Verona ilipata ushindi mwembamba nyumbani wa bao 1-0 dhidi ya Cagliari.
Kipute cha ligi hiyo kitaendelea leo kwa michezo nan, Empoli itaumana na Palermo, Lazio dhidi ya Sassuolo, Parma itaikaribisha Genoa, Sampodoria itaialika Atalanta, wakati Udinese itaumana na Cesena.
Mechi nyingine ni kati ya vinara wa ligi hiyo Juventus na As Roma zenye pointi 15 kila mmoja zitakapochuana mjini Turin nyumbani kwa Juve, wakati Fiorentina itaumana na Inter Milan na Napoli itaikaribisha Torino.

Mtibwa kuongoza ligi leo, Yanga, JKT ni vita Taifa

Mtibwa Sugar wana nafasi kubwa ya kukalia kiti cha uongozi wa Ligi Kuu msimu huu leo
Mgambo JKT watakubali kufanywa ngazi kwa Mtibwa Sugar leo Manungu?
Kikosi cha JKT Ruvu kinachotarajiwa kuvaana na Yanga leo Taifa, watakuwa mdebwedo tena kama msimu uliopita?
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgG0sWioDjCpGG40C4qUjeSnrZ5lrebFf2rc_lRpb6I6-j-HYwaQ3Nhcesj__-Vf7nKoJMj-thfsQvtm8cL1B08Qx6iA2ddT5UGIZnuAtpihh_U1I_ECWTu1qevGqLpIZVSJIV2OjmX1XE/s640/HERM5680.JPG
Yanga watakaokuwa wakijaribu bahati yao kwa JKT Ruvu leo Taifa, watacheka au kununa kama watani zao Simba?
BAADA ya jana timu ya Azam kushindwa kuwakimbia kwenye msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara kwa kulazimishwa sare ya kutofunga ana Prisons-Mbeya, Mtibwa Sugar leo ina nafasi ya kukalia kiti cha uongozi wa ligi hiyo kama itapata ushindi kwa Mgambo JKT mjini Morogoro.
Mtibwa inaikaribisha Mgambo kwenye uwanja wake wa Manungu, Turiani kati ya mechi mbili zinazopigwa leo kukamilisha raundi ya tatu ya ligi hiyo, pambano jingine likiwa ni kati ya Yanga dhidi ya JKT Ruvu.
Mchezo wa Yanga na JKT Ruvu utapigwa kwenye uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ambapo kila timu itahitaji kupata ushindi ili kujiweka nafasi nzuri katika msimamo kabla ya mechi zao zijazo Oktoba 18 na 19 mwaka huu.
Yanga iliyoifumua Prisons-Mbeya kwa mabao 2-1 katika mechi ya mwisho ipo katika nafasi ya 10 kwa sasa ikiporomoshwa na watani zao Simba ambao jana walilazimishwa sare nyingine ya tatu japo wanalingana pointi tatu kila mmoja, ila uwiano wa mabao unawatenganisha Simba wakiwa juu.
Mtibwa ipo nafasi ya pili ikiwa na pointi sita baada ya kushinda mechi zake mbili na kuwa timu pekee mpaka sasa iliyoshinda mfululizo baada ya Azam jana kulazimishwa sare na Prisons.
Kama itashinda Mtibwa itaweka rekodi ya kushinda kwa asilimia 100 mechi zake na kukwea kileleni kwa kukusanya pointi 9, japo huenda wakata miwa hao wasipate mteremko kwa Mgambo JKt ambayo inauguza kipigo cha bao 1-0 ilichopewa na Stand United mjini Tanga katika mechi yao iliyopita.
Mtibwa inayonolewa na kocha mzawa na nahodha wa zamani wa Taifa Stars, Mecky Mexime inajivunia kuwa na wachezaji vijana wenye vipaji vya soka pamoja na kuongezewa nguvu wa makongwe kama Shaaban Nditi, Mussa Mgosi na Vincent Barnabas.
Kwa Yanga itakayokuwa jijini Dar itakuwa na kazi kubwa mbele ya maafande wa JKT Ruvu wanaonolewa na beki wao wa zamani, Fred Felix Minziro kuweza kuendeleza wimbi lao la ushindi.
Baada ya kunyukwa na Mtibwa katika mechi ya kwanza mjini Morogoro, Yanga ilizinduka kwa kuilaza Prisons na leo ingependa kushinda ili kuchupa hadi kwenye Tatu Bora kwani itafikisha pointi sita na kuivuka hata Mbeya City waliopo nafasi ya tatu kwa sasa na pointi zao tano.
Cha kufurahisha Genlson Santana 'Jaja' na Coutinho, pamoja na wakali wote wa Jangwani wapo fiti na kumpa afueni kocha Marcio Maximo kupanga kikosi anachokitaka kusaka ushindi wao wa pili msimu huu.
Hata hivyo vijana wa Minziro ambao wametoka kupokea kipigo toka kwa Kagera Sugar katika mechi iliyopita hawatataka kufanywa ngazi ya kuipandisha Yanga kwenye Tatu Bora kwani wapo nafasi ya pili toka mkiani wakiwa na pointi moja tu.
Kadhalika bado wanakumbuka katika mechi za msimu uliopita walibugizwa jumla ya mabao 9-2 baada ya mechi ya kwanza kufungwa 4-1 na alipokuja kuipokea timu, Minziro alishindiliwa mabao 5-1.
Ngoja tuone mechi hizo mbili za leo zitatoa matokeo gani ambayo yanaweza kupangua msimamo wa sasa ulivyo kama unavyoonekana hapo chini;
MSIMAMO LIGI KUU TANZANIA BARA 2014-2015
                                            P   W   D    L    F    A   GD   Pts
01. Azam                             03  02  01  00  05  01  +4   07
02. Mtibwa Sugar                02  02  00  00  05  01   +4   06
03. Mbeya City                   03  01  02  00  01   00  +1   05
04. Prisons                          03  01  01   01  03   02  +1   04
05.Kagera Sugar                 03  01  01   01  03   02 +1   04
06.Coastal Union                 03  01  01   01  04   04 00  04
07.Stand Utd                       03  01  01   01  03   05  -2   04
08. Ndanda Fc                    03  01  00   02  06   06  00  03
09.Simba                             03  00  03   00  04   04  00  03
10.Yanga                              02  01  00  01   02   02  00  03
11. Mgambo JKT                 02  01  00  01   01    01  00  03
12. Polisi Moro                     03  00  02  01   03   05   -2  02
13.JKT Ruvu                        02  00  01   01   00   02   -2  01
14. Ruvu Shooting                 03  00  01   02  00   04   -4  01