STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, September 21, 2014

Manchester United bado sana, yagongwa 5, Spurs yafa nyumbani

Emmanuel Adebayor
Adebayor akipaparika kuisaidia Spurs isife nyumbani bila mafanikio
Esteban Cambiasso
Hivi ndivyo Mashetani Wekundu walivyonyonyolewa leo ugenini na Leicester City
Etienne Capoue (left) and Stephane SessegnonHALI bado tete kwa klabu ya Manchester United baada ya jioni hii kubamizwa mabao 5-3 na klabu iliyorejea kwenye ligi kuu ya England, Leicester City katika pambano la ugenini, huku Tottenham Hotspur ikifa nyumbani mbele ya West Bromwich Albion kwa bao 1-0.
Manchester iliyofanya 'mauaji' ya kutisha wiki iliyopita kwa kuifumua timu kibonde ya QPR kwa mabao 4-0 ilionekana kama ingeendeleza ushindi kwa Leicester City baada ya kutangulia kupata mabao mawili ya haraka.
Mabao hayo yaliyofungwa na Robin van Persie katika dakika ya 13 ya mchezaji akimalizia kazi nzuri ya Radamel Falcao na Angel di Maria kuongeza la pili dakika tatu baada ya kumegewa pande na Wayne Rooney.
Hata hivyo hilo la pili halikudumu kwani dakika moja baadaye Ulloa aliifungua wenyeji bao na kufanya matokeo kuwa 2-1  hadi wakati wa mapumziko.
Kipindi cha pili Mashetani Wekundu ambao wana pengo katika nafasi ya ulinzi tangu walipowauza Rio Ferdinand na Namanja Vidic, waliongeza bao la tatu dakika ya 57 na kiungo Ander Herrera kwa kazi nzuri ya Di Maria.
Wenyeji walicharuka na kurejesha bao la pili dakika ya 62 kwa mkwaju wa penati kupitia Nugent kabla ya Cambiasso kusawazisha bao dakika mbili baadaye, huku pia Mashetani Wekundu wakimpoteza beki wao Blackett kwa kadi nyekundu.
Magoli yaliyoizamisha vijana wa Louis Van Gaal, yalitumbukizwa wavuni katika dakika ya 79 na Vardy na Ulloa akahitimisha kwa mkwaju wa penati katika dakika ya 83.
Katika mechi nyingine iliyochezwa mapema sambamba na pambano hilo, Spurs ikiwa nyumbani iliendeleza uteja baada ya kulazwa bao 1-0 na wageni wao West Brom.
Bao lililoiua Spurs lilifungwa na James Morrison katika dakika ya 74, licha ya wenyeji kucharuka kutaka kuondokana na aibu ya kulala nyumbani.
Ligi inaendelea kwa mechi mbili kati ya Crystal Palace dhidi ya Everton na Manchester City dhidi ya Chelsea.

Simba, Coastal hapatoshi leo, Ndanda Kuchele!

Simba watapona kwa Coastal
Yusuf Chippo, Kocha wa Coastal Union (mwenye kofia) ataendeleza ubabe kwa vijana wake dhidi ya Simba leo Taifa?
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgSvHwYqtPQMuzPoWUu4QCWVjjgvVwLySqdBYExhW-LxDkl-tjqI3X__y-_vwNzmO6A72piQEbxsK79AqJ8vub5o2bTvjx1VL8FqSFT_-uMryVYDTOmZZVv18G_WiMV4YrQE_D_be0p_aWy/s1600/20140913_160438.jpg
Ndanda Fc waliokaa kileleni baada ya ushindi wake wa kishindo jana dhidi ya Stand Utd
WAKATI mabingwa wa zamani wa soka nchini, Simba na Coastal Union zikishuka dimbani leo katika mechi ya kisasi baina ya 'wanandugu' hao, wageni wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Ndanda wameanza na mguu mzuri kwa kukaa kileleni mwa msimamo wa ligi.
Ushindi wa mabao 4-1 iliyopata ugenini dhidi ya Stand United ya Shinyanga imeiweka Ndanda kileleni ikiwazxidi mabingwa watetezi Azam kwa uwiano wa bao moja la kufunga.
Azam wanakamata nafasi ya pili na kufuatiwa na Mtibwa Sugar waliowatoa nishai Yanga na Marcio Maximo wao pamoja na Jaja, kisha Prisons waliowakong'ota maafande wa Ruvu Shooting wakifuatia mbele ya Mgambo JKT walioshinda jana nyumbani mjini Tanga.
Ingawa ni mapema mno kuijadili ligi kwa sasa, lakini kwa kuwa asubuhi njema huonekana asubuhi, Ndanda, Azam, Mtibwa na Prisons zimesafisha 'nyota' kwa ushindi katika mechi zao za ufunguzi, huku Mbeya City na JKT Ruvu wenyewe wakikusanya pointi moja moja.
Raundi ya kwanza ya mechi hizo za ufunguzi itakamilika leo wakati Simba na Coastal Union zitakazpovaana kwenye dimba la Taifa, huku Simba ikitaka kulipa kisasi na Coastal wakitafuta rekodi ya kuendeleza ubabe kwa vijana wa Msimbazi.
Katika mechi ya mwisho ya msimu uliopita baina ya timu hizo, Simba ilikubali kipigo cha bao 1-0, goli lililofungwa na beki kinda wa Coastal Hamad Juma dakika chache kabla ya mapumziko na kulizamisha jahazi la Wekundu wa Msimbazi waliokuwa chini ya Kocha Zdravkov Logarusic ambaye kwa sasa hayupo na timu hiyo.
Simba itawakabili Coastal wakiwa chini ya Mzambia Patrick Phiri na ikiundwa na kikosi imara, hali inayofanya pambano hilo kuwa la kusubiriwa kwa hamu kwani hata Coastal nao siyo ya kubezwa kwa usajili iliyofanywa chini ya kocha Mkenya, Yusuf Chippo.
Je ni Simba itakayolipa kisasi au Coastal itakayoendeleza ubabe katika mechi ya leo? Jibu ni baada ya dakika 90 ya mchezo huo. Tusubiri tuone.

TP Mazembe yafa ugenini kwa ES Setif

http://www.groupelavenir.org/IMG/arton1718.jpg
TP Mazembe
KLABU ya TP Mazembe ya DR Congo imepewa kipigo cha mabao 2-1 ugenini na ES Setif ya Algeria, lakini bao la kujifunga ,a wenyeji limewasaidia kuwaweka katika nafasi nzuri ya kusonga mbele kama itashinda angalao bao 1-o nyumbani wiki ijayo.
Said Aroussi alijifunga kattika dakika 52 kwenye harakati za kuokoa mpira wa krosi uliopigwa na Rainford Kalaba na kuwapa uongozi TP Mazembe.
Hata hivyo wenyeji walirudisha bao hilo dakika chache baadaye kupitia kwa Younes akimalizia krosi pasi huku waamuzi wa poambano hilo wakijichanganya, refga wa kati akisema goli wakati msaidizi wake akionyesha kibendera cha kuotea cha mpiga krosi.
Refa Neant Alioum alikubali goli hilo baada ya kuzongwa na wachezaji wa ES Setif wakipinga maamuzi ya mshika kibendera, japo TP Mazembe waliamua kucheza soka.
Dakika chache kabla ya kumalizika kwa pambano hilo wenyeji walipata bao la ushindi kupitia kwa Abdulmalek Ziaya aliyemtungua kipa mwenye mbwembwe Robert Kidiaba.

Tevez aiangamiza AC Milan Italia

Carlos Tevez
Carlos Tevez akitupia kitu nyavuni na kuwaacha kipa na mabeki wa Milan wakiwa katika simanzi
BAO pekee lililofungwa na Muargentina, Carlos Tevez katika dakika ya 71 akimalizia kazi ya Paul Pogba lilitosha kuwapa ushindi mujarabu mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Italia, Seria A Juventus dhidi ya AC Milan katika pambano lililochezwa uwanja wa San Sirro, mjini Milan.
Kipigo hicho kimeishusha Milan mpaka nafasi ya tatu ikisaliwa na pointi zake 6 na kuwapisha Juventus kukaa kileleni ikiwa na pointi 9 na mabao manne ya kufungwa ikiwa haijafungwa bao lolote mpaka sasa.
AS Roma waliokuwa nafasi ya tatu wamepanda hadi nafasi ya pili katika msimamo wa ligi hiyo kwa uwiano wa mabao ya kufunga na kufungwa dhidi yake na Milan ambao wamefunga mabao nane na kuruhusu mabao sita.
Ligi hiyo inatarajiwa kuendelea leo kwa michezo mbalimbali ambapo mapame saa saba mchana huu, Chievo Verona itakuwa nyumbani kuialika Parma, Genoa itaialika Lazio na AS Roma watakuwa nyumbani kuikaribisha Cagliari.
Mechi nyingine za leo ni kati ya Sassuolo dhidi ya Sampdoria, Atalanta itaikaribisha Fiorentina, Udinese itaialika Napoli, Palermo itakuwa wenyeji wa Inter Milan na Hellas Verona watakuwa wageni wa Torino.

Saturday, September 20, 2014

Liverpool majanga! Yazamishwa 3-1 na West Ham

Winston Reid (r)
West Ham wakiiadhibu Liverpool

Winston Reid
Bao la kwanza la West Ham likitumbukizwa wavuni na Winston Reid kwa kichwa
Diafro Sakho (second on the left)
West Ham wakishangilia bao lao la pili lililofungwa na Diafro Sakho
Mario Balotelli and Adrian
Balotelli akikoromewa na kipa wa West Ham
Raheem Sterling (l)
Sterling akipongezwa baada ya kufunga bao la kufutia machozi la Liverpool
TIMU ya Liverpool wameendelea kuwa urojo katika Ligi Kuu ya England baada ya mudfa mfupi uliopita kunyukwa mabao 3-1 na West Ham United katika pambano kali lililochezwa Upton Park.
Liverpool ambayo wiki iliyopita ilinyukwa nyumbani na Aston Villa kwa bao 1-0, ilishindwa kupata dawa ya kurejea kwenye makali yake ikiwa haina Luis Suarez baada ya kwenda mapumziko wakiwa nyuma kwa mabao 2-1.
Winston Reid aliwaandikia wenyeji bao dakika ya pili tu ya mchezo akimalizia kazi ya Tomkins kabla ya Diafro Sakho kuongeza la pili dakika tano baadaye na kuwapa presha vijana wa Branden Rodgers kuepuka kipigo ugenini.
Juhudi zao zilizaa matunda dakika ya 26 wakati Raheem Starling kufunga bao la pekee la timu yake, hata dakika za lala salama wenyeji waliandika bao la tatu lililowafanya Liverpool iliyotoka kupata ushindi wa mabao 2-1 katika Ligi ya Mabingwa Ulaya kushindwa kuepuka kipigo hicho kwa West Ham baada ya  Morgan Amalfitano kusukumua mpira wavuni akimalizia kazi nzuri ya Stewart Downing.

Al Ahly yaifyatua Coton Sport kwao, Sewe, Leopards 0-0

http://english.ahram.org.eg/Media/News/2014/9/20/2014-635468104658720940-872.jpg
Al Ahly
WALIOKUWA mabingwa watetezi wa Ligi ya Mabingwa Afrika Al Ahly ya Misri imeanza vyema mechi yake ya Nusu Fainali ya Kombe la Shirikisho baada ya kuizabua Coton Sport ugenini kwa  bao 1-0.
Bao pekee lililowazamisha wenyeji mjini Goroua Cameroon liliwekwa kimiani na  Waleed Soliman dakika ya 72. Timu hizi zitarudiana wiki ijayo kujua itakayotinga Fainali ya michuano hiyo.
Katika mechi nyingine ya Kombe hilo timu za Sewe Sport ya Ivory Coast na AC Leopards ya Kongo zilitoshana nguvu kwa kutoka suluhu.

Arsenal yaua ugenini, Welbeck atisha, Cisse aikoa Newcastle, Wanyama aizamisha Swansea akiangusha chozi uwanjani

Arsenal striker Danny Welbeck scores his first goal for the club
Alan Pardew
Kocha Allan Pardew akionyeshwa vipeperushi vya kutaka atimuliwe Newcastle kanbla ya Cisse kumuokoa kwa kufunga mabao mawili na kuambulia sare nyumbani
Papiss Cisse celebrates his second goal
Cisse akishangilia mabao yake jioni ya leo
Victor Wanyama (centre) celebrates his goal at the Liberty Stadium
Victor Wanyama akipongezqwa na wenzaake baada ya kuifungia Southampton bao pekee lililowapa ushindi ugenini dhidi ya Swansea City
ARSENAL wakiwa katika kiwango kizuri kabisa na kusahau kichapo chao cha Ligi ya Mabingwa Ulaya wameisambaratisha Aston Villa nyumbani kwao kwa kuwalaza mabao 3-0, huku Danny Welbeck akifunga moja ya mabao hayo.
Welbeck ambaye alikosa nafasi nyingi za kufungwa wakati Ze Gunners wakifa 2-0 nchini Ujerumani mbele ya Borussia Dortmund, alifunga bao la pili akimalizia pasi ya Mesut Ozil ambaye alitangulia kufunga bao la kwanza katika dakika ya 32.
Mshambuliaji huyo aliyesajiliwa toka Manchester United ndiye aliyemtengenezea bao hilo Ozil kabla na yeye kumtengenezea dakika mbili baadaye na kuifanya Arsenal kuwa mbele kwa mabao mawili.
Bao la tatu na la ushindi la vijana wa Arsene Wenger lilitokana na kijifunga kwa mchezaji wa Aston Villa, Ali Cissokho dakika ya 36.
Katika mechi nyingine za Ligi ya Engalnd, QPR ikiwa nyumbani ililazimisha sare ya mabao 2-2 na  Stoke City, sawa  na ilivyokuwa kwa Newcastle United iliyosubiri mtokea benchi Pappis Demba Cisse kufunga mabao mawili na kuepuka kipigi cha nyumbani dhidi ya Hull City, huku mashabiki wa Newcastle wakibeba vipeperushi vikitaka kocha Allan Pardew atimuliwe
Burnley ikiwa nyumbani ililazimishwa suluhu na Sunderland na Swansea ikijikuta ikipokea kipigo cha pili mfululizo baada ya kufungwa na Southampton ikiwa ni wiki moja tangu Chelsea walipowatoa nishai.
Bao pekee lililoizamisha Swansea iliyotoka kunyukwa mabao 4-2 liliwekwa kimiani na Mkenya Victor Wanyama dakia ya 80 huku nyota wa Swanseas Winfried Bony akilimwa kadi nyekundu baada ya kupata kadi za njano mbili katika pambano hilo.
Ushindi huo umeipaleka Southampton hadi kwenye nafasi ya pili nyuma ya Chelsea itakayoshuka dimbani kesho kuwakabili Manchester City uwanja wa ugenini.

Real Madrid 'yachinja' mtu 8 ugenini La Liga

Real Madrid
James Bond akishangilia moja ya mabao ya Real Madrid
REAL Madrid wamezidnuka kwenye Ligi Kuu ya Hispania baada ya kupata ushindi mnono ugenini wa mabao 8-2  dhidi ya Deportivo la Coruna.
Hat trick ya Cristiano Ronaldo na mabao mawili mawili toka kwa Gareth Bale na Javier Harnandez 'Chicharito na jingine la James Rodgriuez yalitosha kuwapa ushindi huo Madrid dhidi ya wenyeji wao.
Ronaldo alianza kufunga bao dakika ya 29 akimalizia kazi nzuri ya Arbeloa kabla ya James Bond kufunga la pili dakika ya 36 akimalizia pande la Karim Benzema na dakika nne kabla ya mapumziko Ronaldo alirudi tena nyavuni kwa kufunga bao la tatu kwa pasi ya Benzema.
Kipindi cha pili ndicho kilichokuwa kiama kwa wenyeji ambao licha ya kupata bao la kujifutia machozi lililofungwa dakika ya 51 na Medunjanin kwa mkwaju wa penti haikusaidia kitu kwani Bale alifunga bao la nne dakika ya 66 na kuongeza jingine dakika nane baadaye.
Ronaldo alitimiza hat trick yake dakika ya 78 kabla ya Toche wa Deportivo kufunga bao la pili dakika ya 84 na mtokea benchi Chicharito kufunga mabao mawili ya haraka haraka dakika za 88 na 90 na kuifanya vijana wa Carlo Ancelont kuvuna ushindi wa mabao 8-2.

Yanga domo tupu yafa Moro, Azam yaua, Ruvu yalala, Ndanda dah!

Jaja hakufua dafu kwa vijana wa Mtibwa kwani alikosa penati

Watetezi Azam walioanza kwa kishindo kwa kuilaza Polisi Moro
Yanga iliyokufa Morogoro na Jaja wao
JKT Ruvu walioanza kwa suluhu dhidi ya Mbeya City
Prisons walioanza kwa ushindi wa mabao 2-0 ugenini mbele ya Ruvu Shooting
IMG-20140920-WA0053
Mbeya City
MSHAMBULIAJI Didier Kavumbagu ameifungia Azam mabao mawili na kuwasaidia mabingwa watetezi hao kuanza vyema Ligi Kuu Tanzania Bara, huku timu yake ya zamani, Yanga ikifa Morogoro kwa mabao 2-0 kutoka kwa Mtibwa Sugar.
Kavumbagu aliyekuwa mfungaji tegemeo wa Yanga kwa misimu miwili akiwa na kikosi hicho alifunga mabao yake katika dakika ya 14 na 90 wakati Azam wakiizamisha Polisi Morogoro kwa mabao 3-1 katika mechi iliyochezwa uwanja wa Chamazi.
Bao jingine la watetezi hao waliotoka kunyukwa mabao 3-0 na Yanga kwenye mechi ya Nago ya Jamii liliwekwa kimiani na nahodha wa zamani wa Azam, Aggrey Morris dakika ya 23 wakati Polisi walipata bao lao la kufutia machozi dakika ya 60.
Katika mechi nyingine iliyokuwa inasubiriwa kwa hamu kubwa nchini iliyochezwa uwanja wa jamhuri, Morogoro, Yanga ilishindwa kutamba mbele ya Mtibwa Sugar kwa kukandikwa mabao 2-0, huku nyota wake mpya, Jaja akikosa penati na mabo mawili ya Yanga yakikataliwa na mwamuzi kwa madai wafungaji Simon Msuva na Mrisho Ngassa wameotea.
Mussa Hassan Mgosi alianza kuitia aibu Yanga kwa kufunga bao la kuongoza dakika ya 16 kabla ya Ame Ali kuongeza bao la pili dakika ya 82 na kuifanya Yanga kushindwa kuamini kama kwa miaka minne mfululizo wameshindwa kupata ushindi kwenye dimba la Jamhuri mbele ya Mtibwa inayonolewa na nahodha wa zamani wa Stars Mecky Mexime.
Mwamuzi Dominick Nyamisana wa Dodoma, alitoa adhabu ya penati kwa Yanga dakika ya 46, lakini Genilson Santana Jaja alikosa baada ya mkwaju wake kupanguliwa na kipa wa zamani wa Yanga, Said Mohammed.
Mwamuzi huyo aliyakataa mabao mawili ya Yanga katika dakika ya 47 na 49 kwa madai washambuliaji wa Yanga Simon Msuva aliyetokea benchi na Ngassa kuotea.
Katika mechi nyingine Mbeya City na JKT Ruvu zimetoshana nguvu kwa kutoka suluhu, huku maafande wa Ruvu Shooting wakifa nyumbani kwao Mlandizi kwa mabao 2-0, huku Ndanda Fc ikianza ligi kwa kishindo kwa kuilaza wageni wenzao Stand United kwa mabao 4-1 mjini Shinyanga.
Nayo Mgambo ilianza vema ligi hiyo kwa kupata ushindi mwembamba nyumbani dhidi ya Kagera Sugar baada ya kuwazamisha wakata miwa hao bao 1-0. Bao pekee la mchezo huo lilifungwa na ramadhani Pela na kuifanya Mgambo kuanza tofauti iliyovyokuwa msimu uliopita ilipopigana kuepuka kushuka daraja.

HIVI NDIVYO VUMBI LA LIGI TANO ZA ULAYA LITAKAVYOTIMKA

http://hd.wallpaperswide.com/thumbs/barclays_premier_league_2014_2015-t2.jpghttp://luckybardc.com/files/Soccer-LuckyBar-v2-2013.jpg
LIGI tano zenye mvuto barani Ulaya inatarajiwa kutimka vumbi leo na MICHARAZO inakuletea baadahi ya ratiba zake kwa wikiendi hii na muda wa kurushwa kwa mechi zenye mvuto kwa saa za Afrika Mashariki.
Ratiba ya EPL:
QPR            v Stoke        (8:45) 
Aston Villa    v Arsenal    (11:00) 
Burnley        v Sunderland
Newcastle    v Hull City
Swansea        v Southampton
West Ham        v Liverpool    (1:30)
 
La Liga LEO:
Deportivo    v Real Madrid    (11:00) 
Athletic        v Granada CF
Atletico        v Celta Vigo
Espanyol        v Malaga

Seria A LEO:
Cesena        v Empoli
AC Milan        v Juventus    (3:45)

Bundesliga LEO:  
FC Augsburg    v Werder Bremen
Hamburg SV    v Bayern Munich
Paderborn    v Hanover 96
Schalke 04    v Frankfurt
Stuttgart    v Hoffenheim
Mainz        v Dortmund

Ligue 1 LEO:

Marseille    v Stade Rennes
FC Lorient    v Stade Reims
Metz            v Bastia
Nantes        v Nice
Toulouse        v Caen
Reuters

Kocha Liverpool ajipa matumaini juu ya kikosi chake

http://assets.kompas.com/data/photo/2014/08/31/2107275000-DV1855065780x390.jpgKOCHA wa Liverpool, Brendan Rodgers ametamba kwa kusema kuwa, Liverpool haihitaji fomula maalumu kutwaa ubingwa wa ligi kuu ya soka ya Uingereza na wachezaji wake wapya wameanza kuzoea maisha klabuni Anfield.
Baada ya kuvuka matarajio msimu uliopita na kushika nafasi ya pili nyuma ya mabingwa Manchester City, Liverpool imeanza kwa kusuasua msimu huu, ikifungwa mechi mbili kati ya nne za ligi kuu.
Lakini ikiwa ilisajili wachezaji wengi katika dirisha lililopita, Rodgers hadhani kama itachukua muda mrefu kabla ya kikosi chake kuzoeana na kuanza kupanda kwenye msimamo wa ligi.
"Siku zote tutaangalia namna tofauti tofauti za kushinda mechi. Hakuna fomula moja ya uhakika, ni kufanyia kazi kila siku kwenye uwanja wa mazoezi," Rodgers aliwaambia waandishi wa habari.
"Mwaka mmoja uliopita ningeweza kufukuzwa kazi, 'Tutakuja kufunga magoli?' na kama mtakumbuka tulimaliza na magoli 101 msimu uliopita.
"Tulilazimika kusajili wachezaji wengi katika dirisha lililopita kwa sababu ya Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya. Hili huchukua muda mrefu zaidi kidogo lakini nimeridhishwa na jinsi kila mmoja anavyozoea mazingira. Tuna wachezaji wanaojizoea mazingira ya nchi nyingi tofauti."
Mmoja wa wachezaji wapya wa Rodgers, mshambuliaji Mario Balotelli, aliifungia Liverpool goli lake la kwanza kwenye ushindi wa Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya dhidi ya Ludogorets Jumanne.
Makubwa yanategemewa kutoka kwa Muitalia huyo mwenye hasira za karibu baada ya kuvaa viatu vya mfungaji bora wa msimu uliopita Anfield, Luis Suarez na Rodgers ameridhishwa na ukomavu ambao Balotelli ameonyesha tangu ajiunge kutoka AC Milan.
"Anaifahamu vizuri historia, si tu ya klabu bali ya jiji la Liverpool," Rodgers alisema. "Nitatumia muda mwingi na wachezaji wengi lakini ni kijana mzuri na nadhani unaweza kuona kwamba yupo tayari kwa kazi."
Baada ya kufungwa bila kutarajiwa na Aston Villa mwishoni mwa wiki iliyopita, Liverpool iliyo katika nafasi ya nane ni mgeni wa West Ham United leo ikitaraji kupunguza pengo la pointi sita na viongozi Chelsea.

Tanzania yazidi kuporomoka FIFA, Cameroon yapaa

http://imikinonews.com/files/news_images/1596757601114051870520140716101415.jpgTANZANIA imeendelea kuporomoka tena kwenye viwango vya soka vinavyotolewa kila mwezi na Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa), baada ya kuanguka kwa nafasi tano katika viwango vipya vilivyotolewa.
Tanzania, ambayo ilifungwa 2-0 na Burundi katika mechi ya kimataifa ya kirafiki iliyopita, sasa inakamata nafasi ya 115 duniani na 33 barani Afrika ikiwa nyuma ya Uganda wanaoongoza Afrika Mashariki wakiwa nafasi ya 79 duniani na 19 Afrika, Rwanda walioko nafasi ya 93 duniani na 25 Afrika na Kenya walioporomoka kwa nafasi saba wakiwa nafasi ya 30 Afrika na 111 duniani.
Aligeria waliopanda kwa nafasi nne, wanaongoza barani Afrika wakiwa nafasi ya 20 duniani wakifutwa na Ivory Coast walioshuka kwa nafasi tatu baada ya kukubali kichapo cha mabao 4-1 kutoka kwa Cameroon waliopanda kwa nafasi 12 na kukamata nafasi ya nane Afrika na 42 duniani.
Nafasi ya tatu barani Afrika inakaliwa na Tunisia (31) wakipanda kwa nafasi 11 wakifuatwa na Ghana (33), Senegal (36), Nigeria (37) na Cape Verde (41). Guinea waliopanda kwa nafasi 16 wanakamata nafasi ya tisa barani Afrika na 48 duniani huku Burkina Faso waliopanda kwa nafasi 10 wakifunga pazia la 10 bora barani Afrika wakifungana na Guinea katika nafasi ya 48 duniani.
Uganda pia ni wa kwanza katika Ukanda wa Cecafa wa Afrika Mashariki na Kati wakifuatwa na Rwanda, Kenya, Tanzania, Burundi, Ethiopia (39, 132), Sudan (40, 133), Shelisheli (47, 172), Sudan Kusini (50, 185), Eritrea (52, 202), Somalia (53, 204) huku Djibouti wakifunga mlango Cecafa na Afrika wakiwa 54 Afrika na 205 duniani.
Mabingwa wa dunia, Ujerumani wanaongoza 10 bora ulimwenguni wakifuatwa na Argentina, Colombia waliopanda kwa nafasi moja wakiwashusha Uholanzi, Ubelgiji, Brazil, Uruguay, Hispania, Ufaransa na Uswis.

Spurs walalamikia ubaguzi, wenyeji wao waomba radhi

Roberto Soldado
Patashika baina ya Spurs na Partizan

partizan banner
Bango lililoibua hisia za kibaguzi ambalo Spurs wamelalamikia UEFA
Jan Verthongen (R) challenges Partizan Belgrade"s Danko Lazovic UONGOZI wa klabu ya Tottenham Hotspurs limepeleka malalamiko yao Shirikisho la Soka la Ulaya, UEFA kufuatia kuonyeshwa kwa mabango yenye kulenga ubaguzi na mashabiki wa Partizan Belgrade. 
Meneja wa Spurs Mauricio Pochettino ameelezea bango hilo kama jambo lisilokuwa na heshima na lisilokubalika. 
Spurs walishindwa kutamba ugenini baada ya kulazimishwa suluhu na wenyeji wao katika Uwanja wa Partizani, nchini Serbia.
Maofisa wa Spurs waliwataarifu UEFA juu ya uwepo wa bango hilo kabla ya mapumziko na wajumbe wake walilipiga picha kama ushahidi baada ya mchezo huo. 
Mwaka 2007, Partizan walitolewa katika michuano ya Kombe la UEFA na kutozwa faini kwa vurugu wakati wa mchezo wa mkondo wa kwanza wa michuano hiyo dhidi ya Zrinjski Mostar.
Tayari uongozi wa klabu ya Partizan imeomba radhi kwa kitendo hicho kilichofanywa na mashabiki wao kupitia mabango hayo.

Friday, September 19, 2014

Gareth Bale bado aiwaza Spurs, ahidi kurejea

Gareth Bale alihama Spurs masimu uliopita
http://www.guinnessworldrecords.com/media/6352324/Gareth-Bale-main.jpgWINGA machachari wa Real Madrid, Gareth Bale amezungumzia dokezo la kurejea Tottenham hapo baadaye.
Nyota huyo aliondoka White Hart Lane msimu uliopita kwa rekodi ya dunia ya uhamisho na ameendelea kuimarisha kiwango chake nchini Hispania.
Lakini licha ya kuonekana ametulia ndani ya kikosi akiwa sambamba na Cristiano Ronaldo ndani ya Bernabeu, Bale amesema bado anaipenda Tottenham.
"Tottenham siku zote itaendelea kuwepo ndani ya moyo wangu. Natumaini mashabiki bado wananipenda inagawa nimeondoka," alisema wakati akiongea na BT Sport.
"Nawapenda mashabiki wa Spurs. Huwezi jua ninaweza kurejea siku moja".

Katibu Mkuu Coastal Union 'kizimbani' TFF

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEidwGRi1aPjw1qjpMuqsiRm93wW18DNvNp1gaFYbTH62Y62_VqCRs0oedrMlVZCVHvy_F_78HnKGR-gNSi1rd5OCqL9qGZsX8j08cjXxgxR_ALYQVBcQX7Ph4gHer_s7CxbVAmwr6Q69L_u/s640/DSC04297.JPG
El Siagi (katikati)
KATIBU Mkuu wa Coastal Union, Kassim El Siagi atafikishwa kwenye Kamati ya Maadili ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kwa kushinikiza mkutano wa wanachama wa klabu hiyo ufanyike bila kuandaliwa na Kamati ya Utendaji. Pia El Siagi alitumia vyombo vya habari kuishambulia TFF ambayo haikutambua uamuzi wa mkutano huo ulioelezwa kumdumaza Makamu Mwenyekiti wa klabu hiyo Steven Mnguto. TFF ilimtuma Mkurugenzi wake Msaidizi wa Sheria na Uanachama kufanya uchunguzi wa mgogoro uliokuwa unaendelea katika klabu hiyo. Baada ya kupokea taarifa ya uchunguzi huo, TFF imebaini kuwa Mwenyekiti na Mweka Hazina wa klabu hiyo walishajiuzulu, hivyo uitishwe uchaguzi haraka na kujaza nafasi hizo na nyingine zilizo wazi.
Pia wajumbe wa Kamati ya Utendaji ya Coastal Union, Salim Amir na Albert Peter wameonywa kwa kushiriki katika mkutano ambao wanajua haukuandaliwa na Kamati ya Utendaji.
Vilevile uchunguzi wa TFF umebaini kuwa ushiriki wa Salim Bawazir na Akida Machai kwenye vikao vya Kamati ya Utendaji ya Coastal Union si halali kwa vile wajumbe wa kamati hiyo wanachaguliwa na Mkutano Mkuu na si kuteuliwa na Mwenyekiti.
Kwa vile kutakuwa na uchaguzi wa kujaza nafasi ambazo zipo wazi, uchaguzi huo utasimamiwa na Kamati ya Uchaguzi ya Coastal Union kwa kushirikiana na Kamati ya Uchaguzi ya TFF, na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Tanga na Coastal Union watafanya uhakiki wa reja ya wanachama.

Hujuma mechi ya Stars, Mambas kuchunguzwa

http://shaffihdauda.com/wp-content/uploads/2014/07/10s.jpgSHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) limepokea kwa masikitiko makubwa taarifa zilizoandikwa kwenye baadhi ya Vyombo vya Habari zikielezea tuhuma za hujuma kwa timu ya Taifa (Taifa Stars) katika mechi za kufuzu mashindano ya AFCON. TFF pamoja na kutokuwa na uthibitisho wa tuhuma hizi nzito haliwezi kuzikalia kimya. TFF itateua jopo la kuchunguza tuhuma hizi. Wanafamilia wa mpira wa miguu Tanzania (Members of TFF Family) watakaohitajika kuhojiwa na jopo hilo kwa mujibu wa Ibara ya 37 ya Kanuni za Maadili za TFF watalazimika kutoa ushirikiano. 
Atakayeshindwa kutoa ushirikiano atachukuliwa hatua za kimaadili. 
Pia wadau wa mpira wa miguu ambao sio wanafamilia wa TFF, watakaoitwa na jopo hili wanaombwa watoe ushirikiano kwa nia ya kujenga mpira wetu.

Uongozi Yanga kitanzini, TFF yaipa wiki 2

http://www.eatv.tv/sites/default/files/styles/detailpageimg/public/field/image/yangaa%20clement.JPG?itok=3lkNdTVBSHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) limeitaka klabu ya Yanga kuwasilisha rasimu ya Katiba waliyoipitisha, kwa kuzingatia kuwa Muhtasari wa kikao cha Mkutano Mkuu wao wa Juni 1 mwaka huu umeainisha baadhi ya marekebisho waliyofanya kwa tulivyowaelekeza.
Yanga wanatakiwa kuwasilisha rasimu hiyo kabla ya Oktoba 5 mwaka huu. Ikiwa itakubaliwa na TFF, itapelekwa kwa Msajili wa Klabu na Vyama vya Michezo ili waweze kufanya uchaguzi wa viongozi wao.

Kivumbi England, Arsenal kesho, Man City, Chelse J'pili

http://img.eplmatches.com/2014/06/premier-league.jpg
KIVUMBI cha Ligi Kuu ya England kinatarajiwa kuendelea tena kesho wakati Arsenal watakapokuwa ugenini kuvaana na wenyeji wao Aston Villa, huku kazi nzima ikiwa Jumapili.
Arsenal iliyotoka kukong'otwa mabao 2-0 na Borussia Dortmund katika Ligi ya Mabingwa Ulaya watawafuata Villa ambayo haijapoteza mchezo wowote mpaka sasa ikiwa nafasi ya pili katika msimamo nyuma ya Chelsea wanaoongoza wakiwa na pointi 12, Villa ikiwa na 10.
Arsenal inayokamata nafasi ya saba itahitaji ushindi ili kurejea kwenye mbio zao za kutaka kutwaa ubingwa licha ya kukabiliwa na majeruhi katika kikosi chao.
Mechi nyingine za kesho Jumamosi zitakuwa ni kati ya vibonde QPR waliozabuliwa mabao 4-0 wiki iliyopita na Manchester United itakapokuwa nyumbani kuialika Stoke City, huku Liverpool itaifuata West Ham ikiwa inaugua kipigo ilichopewa wiki iliyopita na Aston Villa.
Ratiba kamili ya kesho ni;
14:45 QPR v Stoke  
17:00 Aston Villa v Arsenal
17:00 Burnley v Sunderland
17:00 Newcastle v Hull
17:00 Swansea v Southampton
19:30 West Ham v Liverpool
Jumapili  
15:30 Leicester v Man United  
15:30 Tottenham v West Brom
18:00 Everton v Crystal Palace
18:00 Man City v Chelsea
Ratiba nyingine ya ligi hiyo;
Jumamosi Septemba 27  
14:45 Liverpool v Everton
17:00 Chelsea v Aston Villa
17:00 Crystal Palace v Leicester
17:00 Hull v Man City
17:00 Man United v West Ham
17:00 Southampton v QPR
17:00 Sunderland v Swansea
19:30 Arsenal v Tottenham
Jumapili Septemba 28
18:00 West Brom v Burnley
Jumatatu Septemba 29  
22:00 Stoke v Newcastle

Jose Mourinho aanza mikwara yake England

http://cdn2.crhoy.com/wp-content/uploads/2014/06/Mou1.jpg 
SAA chache kabla ya kuvaana na mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya England, Jose Mourinho a.k.a Only Special' ameanza zake.
Meneja huyo wa Chelsea amedai hana tatizo katika kikosi chake na kwamba wapo kamili gado kuivaa  Manchester City Jumapili katika mchezo utakaochezwa katika Uwanja wa Etihad. 
Mourinho ameshuhudia kikosi chake kikishinda kila mchezo wa Ligi Kuu msimu huu lakini waligonga mwamba kwa Schalke Jumatano wakati walipolazimishwa sare. 
Hata hivyo, Mourinho anaamini Chelsea ina uwezo wa kuwafunga mahasimu wao hao katika mbio za ubingwa na kusisitiza wanajiamini kwa uwezo wao kuelekea katika mchezo huo. 
Kocha huyo kutoka Ureno, 51 amesema siku zote ni jambo zuri kucheza dhidi ya timu kubwa kwani inafanya kazi yake kuwa rahisi. 
Kocha huyo aliendelea kudai kuwa wanaiheshimu City kwasababu wanastahili lakini wao pia wanajiamini kufanya vyema katika mchezo huo.

MCT yalaani 'uhuni' wa Polisi kwa waandishi wa Habari

We unajifanya mjuaji eeh?
Hivi ndivyo baadhi ya askari wetu wanavyoshindwa kuthamini kazi za watu wengine. Hapa wakimsulubu mwandishi wa habari katika tukio la jana ambalo MCT limelilaani.

Kumekucha Ligi Kuu Tanzania Bara 2014-2015

Watetezi Azam watakuwa nyumbani kuialika Polisi Moro


Yanga wenyewe watakuwa Moro kucheza na Mtibwa, watatoka salama?
Simba wataanza kibarua chao Jumapili dhidi ya Coastal Union
JKT Ruvu wenyewe watakuwa Mbeya kupepetana na Mbeya City
FILIMBI ya kuanza kwa kivumbi cha Ligi Kuu Tanzania Bara 2014-2015 kinatarajiwa kupulizwa rasmi kesho wakati viwanja sita vitakapowaka moto kwa kushuhudia timu 12 kati ya 14 zitakapoanza mbio za kuufukuzia ubingwa wa ligi hiyo.
Kuanza kwa ligi hiyo kutatoa picha halisi ya tambo na mbwembwe za timu wakati wa usajili kwani kwa kuwa soka ni mchezo wa hadharani mashabiki watajua mbivu na mbichi juu ya vikosi hivyo.
Kwa miezi minne klabu 14 za ligi hiyo zimekuwa zikitambiana kuhusu vikosi ilivyosajili na kujigamba kwa matokeo ya mechi kadhaa za kirafiki za kujiandaa na ligi hiyo, hata hivyo tija na ukweli wa ufanisi wa usajili huo utafahamika baada ya kuanza kwa ligi hiyo kesho.
Kwa mujibu wa ratiba ya ligi hiyo, mabingwa watetezi Azam ambao wiki iliyopita walishindwa kufurukuta mbele ya Yanga katika mechi ya Ngao ya Jamii, itakuwa dimba la nyumbani kupepetana na maafande wa Polisi-Moro waliorejea kwenye ligi hiyo katika pambano litakalochezwa uwanja wa Chamazi.
Yanga wenyewe wakiwa na kocha mpya Marcio Maximo kutoka Brazili watakuwa uwanja wa Jamhuri Morogoro kupepetana na wenyeji wao, Mtibwa Sugar ambao hawajawahi kupoteza mchezo wowote kwenye dimba hilo mbele ya Yanga tangu mwaka 2009.
Ratiba Kamili ya kesho;
Septemba 20,2014.
Azam FC vs Polisi Moro [Azam Dar es Salaam] Mtibwa Sugar vs Yanga [Jamhuri, Morogoro] Stand United vs Ndanda FC [Kambarage, Shinyanga] Mgambo JKT vs Kagera Sugar [Mkwakwani, Tanga] Ruvu Shooting vs  Prisons [Mabatini, Mlandizi] Mbeya City vs JKT Ruvu [Sokoine, Mbeya] JUMAPILI:
Simba v Coastal Union [Taifa, Dar es Salaam]

Wembley kutumika Nusu Fainali Ulaya 2020

https://www.daytona.co.uk/news_images/WEM_007936.jpgSHIRIKISHO la Soka Ulaya, UEFA limethibitisha kuwa Uwanja wa Wembley uliopo jijini London Uingereza ndiyo utakaotumika kwa mchezo wa nusu fainali na fainali ya michuano ya Ulaya 2020. 
Viwanja vya Hampden Park na Dublin Aviva vilivyopo jijini Glasgow, Scotland vinatarajiwa kutumika kwa ajili ya mechi za hatua ya 16 bora na mechi tatu za hatua ya makundi. 
Chama cha Soka nchini Uingereza,FA kilishinda nafasi hiyo baada ya Shirikisho la Soka la Ujerumani-DFB kujitoa muda mchache kabla ya kura za UEFA na kuamua kuhamishia nguvu zao katika kutafuta nafasi ya kuandaa michuano hiyo mwaka 2024. 
Michuano ya mwaka 2020 UEFA imefanya kuwa maalamu hivyo itaandaliwa katika viwanja 13 kutoka miji tofauti barani Ulaya. 
Mechi za robo fainali na tatu za hatua ya makundi zitaandaliwa jijini Munich, (Ujerumani), Baku (Azerbaijan), Roma (Italia) na St Petersburg (Urusi). 
Miji mingine itakayoandaa mechi 3 za makundi na moja ya mkondo wa pili ni Copenhagen (Denmark), Bucharest (Romania), Amsterdam (Uholanzi), Bilbao (Uhispania), Budapest (Hungary) na Brussels (Ubeljiji).

Maskini Arsenal yamkosa Debuchy wiki 6

http://ep.imgci.com/PICTURES/CMS/72200/72245.3.jpgIMETHIBITIKA kuwa, beki wa kulia wa Arsenal, Mathieu Debuchy atakuwa nje ya dimba kwa muda wa wiki sita hali inayozidi kuiweka pabaya klabu hiyo.
Meneja wa Arsenal, Arsene Wenger amesema Debuchy atakaa nje ya uwanja kwa kipindi hicho kutokana na kuumia kwake kifundo cha mguu. 
Beki huyo wa kimataifa wa Ufaransa ambaye alitolewa nje kwa machela katika mchezo dhidi ya Manchester City Jumamosi iliyopita anaweza kukosekana kwa miezi mitatu kama itahitajika kufanyiwa upasuaji. 
Wenger alithibitisha hilo na kudai kuwa matokeo zaidi watayajua katika siku chache zijazo baada ya kufanyiwa vipimo zaidi kuonyesha jinsi eneo hilo lilivyoathirika. 
Calum Chambers,19 anatarajiwa kuchukua nafasi ya nyota huyo mwenye umri wa miaka 28 katika mchezo wa kesho dhidi ya Aston Villa. 
Debuchy aliyejiunga na Arsenal akitokea Newcastle United Julai mwaka huu amecheza katika mechi zote saba za timu hiyo msimu huu ukiwemo mchezo wa Ngao ya Jamii dhidi ya Manchester City. 
Beki mwingine kinda Hector Bellerin,19 ndio aliyeingia kucheza nafasi ya upande wa kulia katika mchezo wa Jumanne waliofungwa na Borussia Dortmund kwa mabao 2-0 katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya.

Hatari! Mke wa mtu afa kwa hawara Dar

MWANAMKE Jane Bhoke (27) amefariki dunia nyumbani kwa hawara yake.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Mary Nzuki alisema kifo hicho kilitokea juzi saa 12 jioni eneo la Zingiziwa Chanika wilayani Ilala.
Kamanda Nzuki alisema mtoa taarifa, Mohamed Kambi (44) mkazi eneo hilo alieleza kwamba alikutana na marehemu Septemba 12 mwaka huu katika kilabu cha pombe za kienyeji huko Chanika.
Kambi alisema baada ya kukubaliana walianza kuishi kama mke na mume na huku akibainisha kwamba walifanya mapenzi mara mbili.
“Septemba 15 saa 11 jioni mtoa taarifa na marehemu walikwenda magengeni kununua mahitaji ghafla marehemu alianguka akawa analalamika mguu wa kulia unamuuma… katika harakati za kupunguza maumivu alimeza dawa aina ya diclopa,” alisema kamanda.
Alisema hali ya mgonjwa haikubadilika na ilipofika Septemba 16 saa 10 jioni alifariki dunia huku akibainisha kwamba haifahamiki marehemu ni mkazi wa wapi.