STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, September 25, 2014

Mbwa Mwitu wa Kajala azinduliwa, Lamata alalamika

BAADHI ya picha za matukio katika shughuli hiyo ya usiku wa jana
FILAMU ya Mbwa Mwitu ya msanii Kajala Masanja imezinduliwa kwa kishindo usiku wa jana kwenye ukumbi wa Sinema wa Mlimani City, huku mtunzi na muongozaji wake, Leah Richard 'Lamata' akilalamika ukiritimba unaofanywa na wasimamizi wa tasnia ya filamu nchini.
Lamata aliidokeza MICHARAZO mapema kuwa, kabla ya kuzindua filamu hiyo iliyotengenezwa na Kay Entertainment wakikumbana na vikwazo wakipigwa namna simulizi la filamu hiyo ya dakika 15 iliyogusa matukio ya kweli yaliyoikumba jamii hivi karibuni kutoka makundi ya wahalifu yaitwayo 'Mbwa Mwitu', 'Boda kwa Boda', 'Bad Face' na 'Watoto wa Mbwa'.
"Hii inkatisha tamaa lengo letu kuifundisha jamii juu ya kuepuka uhalifu kwani mwisho wake huwa siyo mwema, lakini 'mabosi' wanaosimamia fani hii wanadhani sisi tunaelimisha vibaya katika matukio yaliyopo ndani ya filamu hii ya 'Mbwa Mwitu'.
Lamata alisema bado wataendelea kutunga filamu zinazoigusa jamii sambamba na kuielimisha, kuionya na kuiburudisha kama sifa za fasihi ilivyo.
Ndani ya filamu hiyo wamo Kajala, Hemed Suleiman, Mama Kawele, Quick Racca na Mwinjuma Muumin 'Kocha wa Dunia'.
Nyota mbali walihudhuria onyesho hilo wakiwamo waigizaji Rich Richie, mtoto wa Kajala, Paula, Sandra, Odama na wengineo kibao waliompiga tafu Kajala.

Tuesday, September 23, 2014

Mama Mkwe wa Jennifer Mgendi huyooo Mtaani

FILAMU mpya ya muimbaji wa nyimbo za Injili, Jennifer Mgendi iitwayo 'Mama Mkwe' inatarajiwa kuigizwa sokoni siku ya Alhamisi baada ya kukwama kuachiwa jana Jumatatu kama ilivyokuwa imepangwa.
Aidha Muinjilisti huyo amewataka mashabiki wake wasiikose kupata darasa la kutosha.
Jennifer alisema filamu hiyo itaachiwa rasmi Septemba 25 baada ya jana kukwama kwa sababu zilizo nje ya uwezo wake ikiwa ni wiki kadhaa tangu kumalizika kurekodiwa kwake na kusema kwa ujumbe uliopo ndani yake, mashabiki hawapaswi kuikosa.
Muimbaji huyo alisema, kisa cha Mama anayeingilia ndoa ya mwanae wa kiume akitaka kupatiwa mjukuu ni mambo ambayo yamekuwa yakiwakumba wanajamii wengi na kusambaratisha ndoa zao bila kutaka.
"Ni mambo yanayotokea ndaniya jamii na kuwaachia watu machungu, sasa waigizaji wameonyesha uhalisia wa mambo namna ndoa nyingi zinavyosambaratika kwa sababu ya mambo kama hayo," alisema.
Katika filamu hiyo, Jennifer ameigiza na wasanii wengine wakali kama kina Mussa Banzi, Bahati Bukuku, Christine Matai, Bibi Esther na wengine.
"Itakuwa mtaani Alhamisi, mashabiki wasikose kuona uhondo huu. Mama Mkwe ni zaidi ya kazi zangu za nyuma kwa namna ilivyosukwa na kutendewa haki na wasanii walioigiza," alitamba Jennifer.

ACT Tanzania yakana kuwa mamluki Tanzania

http://www.mtizamohuru.co.tz/wp-content/uploads/2014/03/act.jpgNa Kipimo Abdallah
CHAMA cha Alliance for Change and Transparency (ACT-Tanzania) kimekanusha  tuhuma zinazotolewa na baadhi ya wanasiasa kuwa  ni chama kilichokuja kubomoa vyama vya upinzani hapa nchini.
Hayo yamesemwa na Katibu wa Mawasiliano na Uenezi wa ACT -Tanzania Mohammed Massaga wakati akizungumza na mwandishi wa MICHARAZO ofisi kwake jijini Dar es Salaam.
Massaga aliomba vyama hivyo kuacha kufanya siasa nyepesi na kujikita katika hoja ili kuhakikisha kuwa upinzani unakuwa na nguvu ili viweze kukitoa chama tawala CCM madarakani.
Alitoa wito kwa watanzania kuviunga mkono vyama vya siasa ambavyo vinaonyesha ni madhubuti ya kukabiliana na ubadhirifu wa rasilimali za Taifa ili kufikia malengo ya maisha bora ambayo kwa sasa yamekwama.
Katibu huyo wa Mawasiliano na Uenezi alisema iwapo vyama vya upinzani vitakuwa na umoja na ushirikiano wa dhati zipo dadli tosha za kukiondoa chama tawala madarakani.
Alisema wapo baadhi ya viongozi ambao wanashindwa kufanya siasa na kubakia kulalamika jambo ambalo linachelewesha mabadiliko.
"Ndhani unaona mwenyewe tatizo la siasa za Tanzania ni wanasiasa kushutumiwa na kuacha kufanya siasa za kweli ambazo zinaweza kuleta mabadiliko kwa jamii ya Kitanzania" alisema
Massaga alitolea mfano wa mchakato wa Bunge Maalum la Katiba linaloendelea mjini Dodoma kuwa ni matumizi mabaya ya fedha za Serikali.
Kwa upande mwingine Massaga alisema katika kujenga chama chao cha ACT- Tanzania wamefanikiwa kuvuna wachama wapya zaidi ya 11,800 katika mikoa 12 ya Tanzania Bara kwa kipindi cha mwezi Agosti mwaka huu.
Katibu huyo wa Mawasiliano na Uenezi ACT alisema kwa sasa chama hicho kina wanachama zaidi ya 187,000 nchini kote hivyo juhudi zao ni kuongeza wanachama wengi zaidi kwa kutumia itikadi yao ya demokrasia ya jamii.
Alisema chama hicho kilifanya ziara katika mikoa 12 ambayo Tanga, Singida, Shinyanga, Simiyu, Geita, Tabora, Mara, Mwanza, Lindi, Kigoma, Pwani na Mtwara ambapo wamepokelewa kwa nguvu kubwa.
Massaga alisema pamoja na kuvuna idadi hiyo ya wanachama wamefanikiwa kusimika viongozi wa muda katika majimbo 68 ya Tanzania bara na viongozi wa kata na matawi kwenye majimbo hayo.
"Kwa kifupi tumepata mafanikio makubwa katika kipindi hiki cha miezi minne tangu kupewa usajili wa muda kwani kila tunapopita tunapokelewa kwa nguvu zote jambo ambalo linatupa matumaini ya kufanya vizuri kwenye chaguzi zijazo", alisema.
Katibu huyo wa Mawasiliano na Unezi wa ACT-Tanzania alisema katika kuhakikisha kuwa wanafikia malengo katika medani za siasa Tanzania wataendelea kuwaelimisha wanachama juu ya kujitokeza kushiriki uchaguzi wa serikali za mitaa.

Fainali za Kombe la Dunia 2022 nchini Qatar zayeyuka

https://www.venturesonsite.com/news/wp-content/uploads/2014/06/qatar-chronicle-qatar-2022-stadiums.jpgIMEBAINIKA wazi kuwa ni ndoto kwa Fainali za Soka za Kombe la Dunia za mwaka 2022 kufanyika Qatar.
Mjumbe wa kamati ya utendaji ya Shirikisho la Soka Duniani,FIFA, Theo Zwanziger amefichua kuwa ni vigumu fainali hizo kuchezwa nchini humo kutokana na hali ya joto kali katika nchi hiyo.
Zwanziger ambaye ni raia wa Ujerumani aliliambia jarida la michezo la Bild jana kuwa anadhani mwisho wa siku michuano ya Kombe la Dunia 2022 haitafanyika katika nchi hiyo. 
Mjumbe huypo aliendelea kudai kuwa watabibu wamesema hawatakubalia kuwajibika kama michuano hiyo itafanyika katika hali ya hatari kama hiyo. 
Japo Qatar wamesisitiza ambao ni matajiri wakubwa wa mafuta wamesisitiza kuwa wanaweza kuandaa michuano hiyo majira ya kiangazi kwa kutumia teknolojia ya vipoza hewa katika viwanja vyake, sehemu za mazoezi na mahali watakapofikia mashabiki bado kumekuwa na wasiwasi mkubwa kuhusiana na afya za wachezaji na mashabiki watakaokuja kushuhudia michuano hiyo. 
Zwanziger amesema anajua wanaweza kuweka vipoza hewa viwanjani lakini Kombe la Dunia halichezwi viwanjani pekee kwani mashabiki kutoka duniani kote watakwenda na kusafiri katika hali hiyo ya joto jambo ambalo ni hatari kwa afya na maisha yao. Michuano ya mwaka 2022 imekuwa ikileta mjadala mkubwa huku rais wa FIFA Sepp Blatter akikiri kuwa walifanya makosa kuipa Qatar kuandaa michuano hiyo na kutaka kuangalia uwezekano wa kuamisha michuano hiyo ichezwe katika majira ya baridi.

AS Vita yanusa Fainali za Afrika, yainyuka Sfaxien

http://www.congoplanet.com/pictures/news/as_v_club_congo_kinshasa_football_vita_z.jpgKLABU ya AS Vita ya DR Congo imeanza vema mbio zake za kucheza Fainali za Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya kuinyuka CS Sfaxien ya Tunisia mabao 2-1.
Mabao ya Vita katika mchezo huo uliochezwa katika Uwanja wa Tata Raphael jijini Kinshasa yalitupiwa kimiani na Firmin Ndombe Mubele na Heritier Luvumbu Nzinga huku lile la kufutia machozi la Sfaxien likifungwa na Ali Maaloul. 
Ushindi huo unaiweka katika nafasi nzuri Wakongo hao kwa mechi ya marudiano itakayofanyika wikiendi hii mjini Tunis.
Vita watakwenda katika mchezo wao wa marudiano wakihitaji sare ya aina yoyote inaweza kuwapeleka fainali ambapo watakutakana na aidha ES Setif ya Algeria au TP Mazembe ya DRC. 
Sfaxien ambao ni mabingwa wa Kombe la Shirikisho na Super Cup walionekana kuzimiliki vyema dakika 20 za mwisho katika mchezo huo lakini walishindwa kutafuta nafasi ya kusawazisha. 
Katika mchezo wa kwanza 'ndugu' zao TP Mazembe walichapwa mabao 2-1 na wapinzani wao ambao watarudiana nao wikiendi hii mjini Lubumbashi na kama timu hizo za Kongo zitafuzu fainali itakayopigwa  Octoba 25-26 na Novemba 1-2 itakuwa ni mara ya kwanza kwa timu Chini ya Jangwa la Sahara kukutana pamoja katika hatua hiyo.

Kifo cha Ebosse chaiponza JS Kabylie, lupango miaka miwili

http://i.ytimg.com/vi/nRgfnT26dgY/0.jpg 
KLABU ya JS Kabylie ya Algeria imefungiwa kushiriki katika michuano ya Afrika kwa miaka miwili kufuatia shambulio lililosababisha kifo cha mchezaji wa kimataifa wa Cameroon Albert Ebosse. 
Uamuzi umechukuliwa na Shirikisho la Soka barani Afrika-CAF katika kiakao chake kilichofanyika jijini Addis Ababa, Ethiopia. 
Kabylie ilimaliza katika nafasi ya pili kwenye msimamo wa Ligi Kuu nchini humo hivyo kuwapa nafasi ya kushiriki michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika mwakani. 
Hatua hiyo ya CAF imekuja kufuatia Shirikisho la Soka la Algeria kuitaka Kabylie kucheza mechi zake za nmyumbani bila ya mashabiki katika uwanja huru msimu huu. 
Ebosse alifariki dunia hospitalini mwezi uliopita kutokana na majeraha ya kichwa yaliyosababishwa na kupigwa na kitu kizito na mashabiki wa klabu hiyo ambao walikasirishwa na kipigo cha mabao 2-1 kutoka kwa wapinzani wao USM Algers.

Rooney, Gerrard wapigwa 'madongo' England

http://www1.pictures.zimbio.com/gi/Wayne+Rooney+Steven+Gerrard+England+v+Ukraine+ygx0xe1DQpXl.jpg

MWANZO mbaya wa msimu kwa klabu za Manchester United na Liverpool unachangiwa na manahodha wao wawili Wayne Rooney na Steven Gerrard, imeelezwa.
Mchambuzi wa soka wa Goal.com, Greg Stobart, amesema "upendeleo" wanaopata Rooney na Gerrard kwa kuwa manahodha na kuachwa waendelee kubaki uwanjani licha ya kucheza chini ya kiwango, kunazigharimu timu hizo hasa katika zama hizi ambazo hata nyota wakubwa wa kimataifa huachwa benchi.
Wakati Juan Mata alianzia benchi na Di Maria na Radamel Falcao nao wakamalizia mechi wakiwa benchi, Rooney aliendelea kunufaika kwa "upendeleo" wa kubaki uwanjani kwa dakika 90 zote, licha ya kupiga shuti moja tu langoni mwa Leicester katika kipigo chao cha 5-3 juzi Jumapili.
Kuna maswali yanayohoji kama Rooney anastahil nafasi kikosi pamoja na wakali kama Falcao, Di Maria na Robin van Persie. Tabia yake ya kupooza mpira haiendani na falsafa ya kocha Louis Van Gaal ya soka la kushambulia.
Van Gaal said alisema Ijumaa iliyopita kwamba Rooney, kwa kuwa nahodha, anatarajia kuendea kunufaika na "upendeleo" wa kuanza katika mechi ngingi zaidi msimu huu na kubaki uwanjani kwa muda mrefu zaidi linapokuja suala la kocha kufanya mabadiliko. Jambo hilo linampa uhakika mchezaji ambaye wengi wanaona kwamba hastahili kuanza katika kikosi chenye sura mpya cha Manchester United. Na kipigo cha 5-3 dhidi ya Leicester juzi ni mfano unaoonyesha ni kwa nini.
Alionekana akiwawakia kwa hasira wachezaji wenzake, ikiwamo kumshukia beki yosso Tyler Blackett (20) kufuatia Leicester kufunga goli la 3-3, lakini Rooney alionyesha kutojielewa kwani yeye ndiye aliyepoteza mpira uliozaa goli hilo.

Bilioni 20 zahitajika kutatua tatizo la Ajiora nchini

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj-F5hwnHLukOOHecjhZ-ghBDejeN6VOEVNIpFPCcLyvhzRQSnpxPJQMoPK0TMjEI6_GHXln6t7ZsHQv5IPO-4lzTHCdxZsY5zg0yjg0u1lXUwCocg-aXzVOF9kMVqArWiwC4b0HCaqkiE/s1600/2.JPG
Dk Kisui (kushoto) akifafanua jambo
Na Kipimo Abdallah
WIZARA ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo imesema inahitaji shilingi bilioni 20 kila mwaka ili iweze kupunguza tatizo la ajira hapa nchini.
Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi Msaidizi wa Uwezeshaji na Uhamasishaji wa Wizara hiyo Dk. Steven Kisui  wakati akijibu swali la mwandishi wa habari hii.
Alisema bajeti wanayotengewa haitoshelezi mahitaji ya vijana jambo ambalo linachelewesha juhudi za kupunguza ukubwa wa tatizo hilo ambalo linatajwa kama janga la Taifa.
Dk. Kisui alisema mahitaji ni makubwa kutoka kwa vijana mbalimbali nchini ambao wamejiunga katika SACCOS ila uwezo wa Serikali ni mdogo hivyo zoezi hilo
linachukua muda kutatuliwa.
"Kusema ukweli bajeti ya shilingi bilioni 6 hatuwezi kufikia malengo lakini tutaenda hivyo hivyo hadi tufikie muafaka,kwani kiukweli ni ndogo mnno", alisema.
Kisui alisema juhudi za Wizara ni kuhakikisha kuwa hicho kidogo kinachopatikana kinawafia walengwa ambao watakuwa wamefikia vigezo pamoja na ukweli kuwa bilioni 20 zingeweza kutatua tatizo.
Kwa upande wake Kaimu Mkuu Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali Concilia Nyibitanga alisema hadi kufikia sasa ni Halimashauri 42 kati ya 169 ambazo vijana wake ndio wametengeneza vikundi vya SACCOS.
Alisema mwamko wa Halimashauri kuhakikisha kuwa vikundi vinakuwepo imekuwa mdogo sana jambo ambalo linakwamisha juhudi za Serikali.
"Pamoja na juhudi za serikali katika kuhakikisha kuwa vijana wanafikiwa bado mwamko ni mdogo sana katika Halimashauri nyingi jambo ambalo linaweza kuwa kikwazo", alisema.
Nyibitanga alisema fedha hizo ambazo zinakopeshwa kwa riba ndogo lengo lake ni kuhakikisha kuwa vijana wanajiajiri ili kuhakikisha kuwa wanakabilianana changamoto zinazowakabili.

Kajala kuzindua Mbwa Mwitu kesho Mlimani City

Kajala katika pozi
Kava la picha hiyo ya Mbwa Mwitu inayozinduliwa kesho Mlimani
NYOTA wa filamu nchini Kajala Masanja 'Kajala' kupitia kampuni yake ya Kay Entertainment inatarajiwa kuzindua filamu ya aina yake kesho usiku.
Filamu hiyo inayofahamika kama 'Mbwa Mwitu' itazinduliwa kwenye ukumbi wa Mlimani City kwa watu maalum walioalikwa kuhudhuria.
Kinachoifanya filamu hiyo kuwa ya kipekee ni muda mfupi iliyonayo wa dakika 15 tu, 10 ikiwa ni filamu yenyewe na tano za 'ducumentary' ya baadhi ya vijana waliokuwa wakiunda kundi la Mbwa Mwitu lililotikisa jiji.
Mtunzi na muongozaji wa filamu hiyo, Leah Richard 'Lamata' aliiambia MICHARAZO kuwa, filamu hiyo inasimulia visa na mikasa ya kundi la Mbwa Mwitu lililohusishwa na uvamizi na uporaji wa watu jijini Dar es Salaam.
"Uzinduzi utafanyika Mlimani Sept 24 (kesho) na ndani ya filamu hiyo ya dakika 10 ina nyongeza ya dakika tano za mahojiano ya waliokuwa vijana wa 'Mbwa Mwitu' ambao wameacha uhalifu huo," alisema Lamata kwa niaba ya Kajala ambaye ni mmoja wa washiriki wa filamu hiyo.
Mbali na Kajala wengine walioicheza ni Hemed Suleiman 'PHD', Grace Mapunda 'Mama Kawele', Mwinjuma Muumin, Abort Rocca, Hassain Hussein na Abdul Karim.
Kundi la Mbwa Mwitu na yake ya Watoto wa Mbwa, Boda kwa Boda na Bad Face yalitikisa jiji kwa vitendo vyao ya kihalifu kabla ya jeshi la Polisi kuyashughulikia huku baadhi ya washirika wao kuuwawa na wananchi.

PSPF kudhamini Siku ya Msanii Tanzania kwa Sh Mil 10

http://www.8020fashionsblog.com/wp-content/uploads/2013/09/pspf.pngNa Kipimo Abdallah
MFUKO wa Pensheni wa PSPF  umetoa shilingi milioni 10 kwa ajili ya kudhamini siku ya Msaani Tanzania.
Hayo yamesemwa na Afisa Uhusiano Mwandamizi wa PSPF Abdul Njaidi wakati akizungmza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.
Alisema lengo la PSPF kujitolea kudhamini siku hiyo na katika kuangalia sekta nzima ya sanaa kwa kuwawezesha, kuwapa mafunzo wasanii ili waweze kujikwamua kiuchumi hapa nchini.
Njaidi alisema PSPF imekuwa ikijikita katika kuwapatia mafao watumishi wa sekta mbalimbali zilizo rasmi kwa miaka mingi ila kwa kipindi cha hivi karibuni hata sekta isiyo rasmi inahusishwa wakiwepo wasanii.
"Kwa kuanza sisi PSPF tumeamua kudhamini siku ya Msanii Tanzania kwa kutoa milioni 10 ambapo tunaamini zitasaidia mchakato huo", alisema.
Aidha Njaidi alisema pamoja na kudhamini siku hiyo PSPF inaendelea na kupokea wanachama kutoka sekta mbalimbali ambao wapo tayari kwa malengo yao baadae.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Haak Neel Production Company Limited Geofrey Katulo alisema  siku ya Msanii ni mradi uliobuniwa na Baraza la SanaaTaifa (BASATA) na utaendeshwa kwa ubiia wa Haak Neel  Production Company Limited.
Alisema mradi huo ulibuniwa ili kuungana na wenzao duniani kuadhimisha siku siku ya kimataifa ya Msanii ambayo huadhimishwa kila ifikapo Oktoba 25 kwa lengo la kumtambua msaani, kazi zake pamoja na mchango wake katika jamii.
Katula alisema kauli mbiu ya siku ya msaanii mwaka 2014 ni "Sanaa ni Kazi" ambapo fani zitakazohusika katika maadhimisho hayo ni taarabu, muziki wa dansi, ngoma za asili, muziki wa msanii kutoka nje ya nchi.
Fani zingine ni uchezaji shoo, dansi za mitaani, bongo fleva, maonyesho ya mitindo ya mavazi, sanaa kwa watoto na maonyesho ya sanaa za ufundi pamoja na semina.

Sunday, September 21, 2014

Simba yashindwa kulipa kisasi kwa Coastal Taifa

simba
MASHABIKI wa klabu ya Simba wametoka uwanja wa Taifa wakiwa hawana furaha baada ya kikosi cha timu yao kushindwa kulinda mabao mawili waliyoyafunga kipindi cha kwanza na kuwaachia Coastal Union warejeshe kipindi cha pili na kufanya mchezo huo kumalizika kwa sare ya mabao 2-2 katika Ligi Kuu.
Mabao mawili ya Shaaban Kisiga na Amissi Tambwe yaliwafanya vijana wa Msimbazi kuwa na furaha na kuamini wangepata nafasi ya kuwacheka wapinzani wao Yanga waliozabuliwa mabao 2-0 na Mtibwa Sugar jana mjini Morogoro baada ya kwenda mapumziko wakiwa mbele.
Hata hivyo kipindi cha pili kilipoanza Coastal waliingia kivingine na kucharuka na kurejesha bao moja baada ya jingine kupitia wa Lutimba Yayo na Ramadhani Salim kufungwa kwa faulo na kuifanya matokeo kusomeka mabao 2-2 na kuwafanya mashabiki wa Simba kuwa wanyonge, licha ya timu ya kupata pointi moja.
MSIMAMO LIGI KUU TANZANIA BARA 2014-2015
                                          P  W  D  L  F  A  Pts
1. Ndanda Fc                    1   1    0   0  4   1    3
2. Azam                             1   1    0   0  3   1   3
3. Mtibwa Sugar                1   1    0   0  2    0  3
4. Prisons                           1   1   0   0   2   0   3
5. Mgambo JKT                1    1   0   0   1   0   3
6. JKT Ruvu                      1    0   1   0   0   0   1
7. Coastal Union                1    0   1   0   2   2   1
8. Simba                            1    0   1   0   2   2   1
9.Mbeya City                     1    0   1    0   0  0  1
10. Kagera Sugar               1    0   0   1    0   1   0
11. Ruvu Shooting              1    0   0   1    0   2  0
12.Yanga                            1    0   0   1    0   2  0
13. Polisi Moro                  1    0   0   1    1    3  0
14.Stand Utd                     1    0   0   1    1    4  0

Manchester United bado sana, yagongwa 5, Spurs yafa nyumbani

Emmanuel Adebayor
Adebayor akipaparika kuisaidia Spurs isife nyumbani bila mafanikio
Esteban Cambiasso
Hivi ndivyo Mashetani Wekundu walivyonyonyolewa leo ugenini na Leicester City
Etienne Capoue (left) and Stephane SessegnonHALI bado tete kwa klabu ya Manchester United baada ya jioni hii kubamizwa mabao 5-3 na klabu iliyorejea kwenye ligi kuu ya England, Leicester City katika pambano la ugenini, huku Tottenham Hotspur ikifa nyumbani mbele ya West Bromwich Albion kwa bao 1-0.
Manchester iliyofanya 'mauaji' ya kutisha wiki iliyopita kwa kuifumua timu kibonde ya QPR kwa mabao 4-0 ilionekana kama ingeendeleza ushindi kwa Leicester City baada ya kutangulia kupata mabao mawili ya haraka.
Mabao hayo yaliyofungwa na Robin van Persie katika dakika ya 13 ya mchezaji akimalizia kazi nzuri ya Radamel Falcao na Angel di Maria kuongeza la pili dakika tatu baada ya kumegewa pande na Wayne Rooney.
Hata hivyo hilo la pili halikudumu kwani dakika moja baadaye Ulloa aliifungua wenyeji bao na kufanya matokeo kuwa 2-1  hadi wakati wa mapumziko.
Kipindi cha pili Mashetani Wekundu ambao wana pengo katika nafasi ya ulinzi tangu walipowauza Rio Ferdinand na Namanja Vidic, waliongeza bao la tatu dakika ya 57 na kiungo Ander Herrera kwa kazi nzuri ya Di Maria.
Wenyeji walicharuka na kurejesha bao la pili dakika ya 62 kwa mkwaju wa penati kupitia Nugent kabla ya Cambiasso kusawazisha bao dakika mbili baadaye, huku pia Mashetani Wekundu wakimpoteza beki wao Blackett kwa kadi nyekundu.
Magoli yaliyoizamisha vijana wa Louis Van Gaal, yalitumbukizwa wavuni katika dakika ya 79 na Vardy na Ulloa akahitimisha kwa mkwaju wa penati katika dakika ya 83.
Katika mechi nyingine iliyochezwa mapema sambamba na pambano hilo, Spurs ikiwa nyumbani iliendeleza uteja baada ya kulazwa bao 1-0 na wageni wao West Brom.
Bao lililoiua Spurs lilifungwa na James Morrison katika dakika ya 74, licha ya wenyeji kucharuka kutaka kuondokana na aibu ya kulala nyumbani.
Ligi inaendelea kwa mechi mbili kati ya Crystal Palace dhidi ya Everton na Manchester City dhidi ya Chelsea.

Simba, Coastal hapatoshi leo, Ndanda Kuchele!

Simba watapona kwa Coastal
Yusuf Chippo, Kocha wa Coastal Union (mwenye kofia) ataendeleza ubabe kwa vijana wake dhidi ya Simba leo Taifa?
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgSvHwYqtPQMuzPoWUu4QCWVjjgvVwLySqdBYExhW-LxDkl-tjqI3X__y-_vwNzmO6A72piQEbxsK79AqJ8vub5o2bTvjx1VL8FqSFT_-uMryVYDTOmZZVv18G_WiMV4YrQE_D_be0p_aWy/s1600/20140913_160438.jpg
Ndanda Fc waliokaa kileleni baada ya ushindi wake wa kishindo jana dhidi ya Stand Utd
WAKATI mabingwa wa zamani wa soka nchini, Simba na Coastal Union zikishuka dimbani leo katika mechi ya kisasi baina ya 'wanandugu' hao, wageni wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Ndanda wameanza na mguu mzuri kwa kukaa kileleni mwa msimamo wa ligi.
Ushindi wa mabao 4-1 iliyopata ugenini dhidi ya Stand United ya Shinyanga imeiweka Ndanda kileleni ikiwazxidi mabingwa watetezi Azam kwa uwiano wa bao moja la kufunga.
Azam wanakamata nafasi ya pili na kufuatiwa na Mtibwa Sugar waliowatoa nishai Yanga na Marcio Maximo wao pamoja na Jaja, kisha Prisons waliowakong'ota maafande wa Ruvu Shooting wakifuatia mbele ya Mgambo JKT walioshinda jana nyumbani mjini Tanga.
Ingawa ni mapema mno kuijadili ligi kwa sasa, lakini kwa kuwa asubuhi njema huonekana asubuhi, Ndanda, Azam, Mtibwa na Prisons zimesafisha 'nyota' kwa ushindi katika mechi zao za ufunguzi, huku Mbeya City na JKT Ruvu wenyewe wakikusanya pointi moja moja.
Raundi ya kwanza ya mechi hizo za ufunguzi itakamilika leo wakati Simba na Coastal Union zitakazpovaana kwenye dimba la Taifa, huku Simba ikitaka kulipa kisasi na Coastal wakitafuta rekodi ya kuendeleza ubabe kwa vijana wa Msimbazi.
Katika mechi ya mwisho ya msimu uliopita baina ya timu hizo, Simba ilikubali kipigo cha bao 1-0, goli lililofungwa na beki kinda wa Coastal Hamad Juma dakika chache kabla ya mapumziko na kulizamisha jahazi la Wekundu wa Msimbazi waliokuwa chini ya Kocha Zdravkov Logarusic ambaye kwa sasa hayupo na timu hiyo.
Simba itawakabili Coastal wakiwa chini ya Mzambia Patrick Phiri na ikiundwa na kikosi imara, hali inayofanya pambano hilo kuwa la kusubiriwa kwa hamu kwani hata Coastal nao siyo ya kubezwa kwa usajili iliyofanywa chini ya kocha Mkenya, Yusuf Chippo.
Je ni Simba itakayolipa kisasi au Coastal itakayoendeleza ubabe katika mechi ya leo? Jibu ni baada ya dakika 90 ya mchezo huo. Tusubiri tuone.

TP Mazembe yafa ugenini kwa ES Setif

http://www.groupelavenir.org/IMG/arton1718.jpg
TP Mazembe
KLABU ya TP Mazembe ya DR Congo imepewa kipigo cha mabao 2-1 ugenini na ES Setif ya Algeria, lakini bao la kujifunga ,a wenyeji limewasaidia kuwaweka katika nafasi nzuri ya kusonga mbele kama itashinda angalao bao 1-o nyumbani wiki ijayo.
Said Aroussi alijifunga kattika dakika 52 kwenye harakati za kuokoa mpira wa krosi uliopigwa na Rainford Kalaba na kuwapa uongozi TP Mazembe.
Hata hivyo wenyeji walirudisha bao hilo dakika chache baadaye kupitia kwa Younes akimalizia krosi pasi huku waamuzi wa poambano hilo wakijichanganya, refga wa kati akisema goli wakati msaidizi wake akionyesha kibendera cha kuotea cha mpiga krosi.
Refa Neant Alioum alikubali goli hilo baada ya kuzongwa na wachezaji wa ES Setif wakipinga maamuzi ya mshika kibendera, japo TP Mazembe waliamua kucheza soka.
Dakika chache kabla ya kumalizika kwa pambano hilo wenyeji walipata bao la ushindi kupitia kwa Abdulmalek Ziaya aliyemtungua kipa mwenye mbwembwe Robert Kidiaba.

Tevez aiangamiza AC Milan Italia

Carlos Tevez
Carlos Tevez akitupia kitu nyavuni na kuwaacha kipa na mabeki wa Milan wakiwa katika simanzi
BAO pekee lililofungwa na Muargentina, Carlos Tevez katika dakika ya 71 akimalizia kazi ya Paul Pogba lilitosha kuwapa ushindi mujarabu mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Italia, Seria A Juventus dhidi ya AC Milan katika pambano lililochezwa uwanja wa San Sirro, mjini Milan.
Kipigo hicho kimeishusha Milan mpaka nafasi ya tatu ikisaliwa na pointi zake 6 na kuwapisha Juventus kukaa kileleni ikiwa na pointi 9 na mabao manne ya kufungwa ikiwa haijafungwa bao lolote mpaka sasa.
AS Roma waliokuwa nafasi ya tatu wamepanda hadi nafasi ya pili katika msimamo wa ligi hiyo kwa uwiano wa mabao ya kufunga na kufungwa dhidi yake na Milan ambao wamefunga mabao nane na kuruhusu mabao sita.
Ligi hiyo inatarajiwa kuendelea leo kwa michezo mbalimbali ambapo mapame saa saba mchana huu, Chievo Verona itakuwa nyumbani kuialika Parma, Genoa itaialika Lazio na AS Roma watakuwa nyumbani kuikaribisha Cagliari.
Mechi nyingine za leo ni kati ya Sassuolo dhidi ya Sampdoria, Atalanta itaikaribisha Fiorentina, Udinese itaialika Napoli, Palermo itakuwa wenyeji wa Inter Milan na Hellas Verona watakuwa wageni wa Torino.

Saturday, September 20, 2014

Liverpool majanga! Yazamishwa 3-1 na West Ham

Winston Reid (r)
West Ham wakiiadhibu Liverpool

Winston Reid
Bao la kwanza la West Ham likitumbukizwa wavuni na Winston Reid kwa kichwa
Diafro Sakho (second on the left)
West Ham wakishangilia bao lao la pili lililofungwa na Diafro Sakho
Mario Balotelli and Adrian
Balotelli akikoromewa na kipa wa West Ham
Raheem Sterling (l)
Sterling akipongezwa baada ya kufunga bao la kufutia machozi la Liverpool
TIMU ya Liverpool wameendelea kuwa urojo katika Ligi Kuu ya England baada ya mudfa mfupi uliopita kunyukwa mabao 3-1 na West Ham United katika pambano kali lililochezwa Upton Park.
Liverpool ambayo wiki iliyopita ilinyukwa nyumbani na Aston Villa kwa bao 1-0, ilishindwa kupata dawa ya kurejea kwenye makali yake ikiwa haina Luis Suarez baada ya kwenda mapumziko wakiwa nyuma kwa mabao 2-1.
Winston Reid aliwaandikia wenyeji bao dakika ya pili tu ya mchezo akimalizia kazi ya Tomkins kabla ya Diafro Sakho kuongeza la pili dakika tano baadaye na kuwapa presha vijana wa Branden Rodgers kuepuka kipigo ugenini.
Juhudi zao zilizaa matunda dakika ya 26 wakati Raheem Starling kufunga bao la pekee la timu yake, hata dakika za lala salama wenyeji waliandika bao la tatu lililowafanya Liverpool iliyotoka kupata ushindi wa mabao 2-1 katika Ligi ya Mabingwa Ulaya kushindwa kuepuka kipigo hicho kwa West Ham baada ya  Morgan Amalfitano kusukumua mpira wavuni akimalizia kazi nzuri ya Stewart Downing.

Al Ahly yaifyatua Coton Sport kwao, Sewe, Leopards 0-0

http://english.ahram.org.eg/Media/News/2014/9/20/2014-635468104658720940-872.jpg
Al Ahly
WALIOKUWA mabingwa watetezi wa Ligi ya Mabingwa Afrika Al Ahly ya Misri imeanza vyema mechi yake ya Nusu Fainali ya Kombe la Shirikisho baada ya kuizabua Coton Sport ugenini kwa  bao 1-0.
Bao pekee lililowazamisha wenyeji mjini Goroua Cameroon liliwekwa kimiani na  Waleed Soliman dakika ya 72. Timu hizi zitarudiana wiki ijayo kujua itakayotinga Fainali ya michuano hiyo.
Katika mechi nyingine ya Kombe hilo timu za Sewe Sport ya Ivory Coast na AC Leopards ya Kongo zilitoshana nguvu kwa kutoka suluhu.

Arsenal yaua ugenini, Welbeck atisha, Cisse aikoa Newcastle, Wanyama aizamisha Swansea akiangusha chozi uwanjani

Arsenal striker Danny Welbeck scores his first goal for the club
Alan Pardew
Kocha Allan Pardew akionyeshwa vipeperushi vya kutaka atimuliwe Newcastle kanbla ya Cisse kumuokoa kwa kufunga mabao mawili na kuambulia sare nyumbani
Papiss Cisse celebrates his second goal
Cisse akishangilia mabao yake jioni ya leo
Victor Wanyama (centre) celebrates his goal at the Liberty Stadium
Victor Wanyama akipongezqwa na wenzaake baada ya kuifungia Southampton bao pekee lililowapa ushindi ugenini dhidi ya Swansea City
ARSENAL wakiwa katika kiwango kizuri kabisa na kusahau kichapo chao cha Ligi ya Mabingwa Ulaya wameisambaratisha Aston Villa nyumbani kwao kwa kuwalaza mabao 3-0, huku Danny Welbeck akifunga moja ya mabao hayo.
Welbeck ambaye alikosa nafasi nyingi za kufungwa wakati Ze Gunners wakifa 2-0 nchini Ujerumani mbele ya Borussia Dortmund, alifunga bao la pili akimalizia pasi ya Mesut Ozil ambaye alitangulia kufunga bao la kwanza katika dakika ya 32.
Mshambuliaji huyo aliyesajiliwa toka Manchester United ndiye aliyemtengenezea bao hilo Ozil kabla na yeye kumtengenezea dakika mbili baadaye na kuifanya Arsenal kuwa mbele kwa mabao mawili.
Bao la tatu na la ushindi la vijana wa Arsene Wenger lilitokana na kijifunga kwa mchezaji wa Aston Villa, Ali Cissokho dakika ya 36.
Katika mechi nyingine za Ligi ya Engalnd, QPR ikiwa nyumbani ililazimisha sare ya mabao 2-2 na  Stoke City, sawa  na ilivyokuwa kwa Newcastle United iliyosubiri mtokea benchi Pappis Demba Cisse kufunga mabao mawili na kuepuka kipigi cha nyumbani dhidi ya Hull City, huku mashabiki wa Newcastle wakibeba vipeperushi vikitaka kocha Allan Pardew atimuliwe
Burnley ikiwa nyumbani ililazimishwa suluhu na Sunderland na Swansea ikijikuta ikipokea kipigo cha pili mfululizo baada ya kufungwa na Southampton ikiwa ni wiki moja tangu Chelsea walipowatoa nishai.
Bao pekee lililoizamisha Swansea iliyotoka kunyukwa mabao 4-2 liliwekwa kimiani na Mkenya Victor Wanyama dakia ya 80 huku nyota wa Swanseas Winfried Bony akilimwa kadi nyekundu baada ya kupata kadi za njano mbili katika pambano hilo.
Ushindi huo umeipaleka Southampton hadi kwenye nafasi ya pili nyuma ya Chelsea itakayoshuka dimbani kesho kuwakabili Manchester City uwanja wa ugenini.

Real Madrid 'yachinja' mtu 8 ugenini La Liga

Real Madrid
James Bond akishangilia moja ya mabao ya Real Madrid
REAL Madrid wamezidnuka kwenye Ligi Kuu ya Hispania baada ya kupata ushindi mnono ugenini wa mabao 8-2  dhidi ya Deportivo la Coruna.
Hat trick ya Cristiano Ronaldo na mabao mawili mawili toka kwa Gareth Bale na Javier Harnandez 'Chicharito na jingine la James Rodgriuez yalitosha kuwapa ushindi huo Madrid dhidi ya wenyeji wao.
Ronaldo alianza kufunga bao dakika ya 29 akimalizia kazi nzuri ya Arbeloa kabla ya James Bond kufunga la pili dakika ya 36 akimalizia pande la Karim Benzema na dakika nne kabla ya mapumziko Ronaldo alirudi tena nyavuni kwa kufunga bao la tatu kwa pasi ya Benzema.
Kipindi cha pili ndicho kilichokuwa kiama kwa wenyeji ambao licha ya kupata bao la kujifutia machozi lililofungwa dakika ya 51 na Medunjanin kwa mkwaju wa penti haikusaidia kitu kwani Bale alifunga bao la nne dakika ya 66 na kuongeza jingine dakika nane baadaye.
Ronaldo alitimiza hat trick yake dakika ya 78 kabla ya Toche wa Deportivo kufunga bao la pili dakika ya 84 na mtokea benchi Chicharito kufunga mabao mawili ya haraka haraka dakika za 88 na 90 na kuifanya vijana wa Carlo Ancelont kuvuna ushindi wa mabao 8-2.

Yanga domo tupu yafa Moro, Azam yaua, Ruvu yalala, Ndanda dah!

Jaja hakufua dafu kwa vijana wa Mtibwa kwani alikosa penati

Watetezi Azam walioanza kwa kishindo kwa kuilaza Polisi Moro
Yanga iliyokufa Morogoro na Jaja wao
JKT Ruvu walioanza kwa suluhu dhidi ya Mbeya City
Prisons walioanza kwa ushindi wa mabao 2-0 ugenini mbele ya Ruvu Shooting
IMG-20140920-WA0053
Mbeya City
MSHAMBULIAJI Didier Kavumbagu ameifungia Azam mabao mawili na kuwasaidia mabingwa watetezi hao kuanza vyema Ligi Kuu Tanzania Bara, huku timu yake ya zamani, Yanga ikifa Morogoro kwa mabao 2-0 kutoka kwa Mtibwa Sugar.
Kavumbagu aliyekuwa mfungaji tegemeo wa Yanga kwa misimu miwili akiwa na kikosi hicho alifunga mabao yake katika dakika ya 14 na 90 wakati Azam wakiizamisha Polisi Morogoro kwa mabao 3-1 katika mechi iliyochezwa uwanja wa Chamazi.
Bao jingine la watetezi hao waliotoka kunyukwa mabao 3-0 na Yanga kwenye mechi ya Nago ya Jamii liliwekwa kimiani na nahodha wa zamani wa Azam, Aggrey Morris dakika ya 23 wakati Polisi walipata bao lao la kufutia machozi dakika ya 60.
Katika mechi nyingine iliyokuwa inasubiriwa kwa hamu kubwa nchini iliyochezwa uwanja wa jamhuri, Morogoro, Yanga ilishindwa kutamba mbele ya Mtibwa Sugar kwa kukandikwa mabao 2-0, huku nyota wake mpya, Jaja akikosa penati na mabo mawili ya Yanga yakikataliwa na mwamuzi kwa madai wafungaji Simon Msuva na Mrisho Ngassa wameotea.
Mussa Hassan Mgosi alianza kuitia aibu Yanga kwa kufunga bao la kuongoza dakika ya 16 kabla ya Ame Ali kuongeza bao la pili dakika ya 82 na kuifanya Yanga kushindwa kuamini kama kwa miaka minne mfululizo wameshindwa kupata ushindi kwenye dimba la Jamhuri mbele ya Mtibwa inayonolewa na nahodha wa zamani wa Stars Mecky Mexime.
Mwamuzi Dominick Nyamisana wa Dodoma, alitoa adhabu ya penati kwa Yanga dakika ya 46, lakini Genilson Santana Jaja alikosa baada ya mkwaju wake kupanguliwa na kipa wa zamani wa Yanga, Said Mohammed.
Mwamuzi huyo aliyakataa mabao mawili ya Yanga katika dakika ya 47 na 49 kwa madai washambuliaji wa Yanga Simon Msuva aliyetokea benchi na Ngassa kuotea.
Katika mechi nyingine Mbeya City na JKT Ruvu zimetoshana nguvu kwa kutoka suluhu, huku maafande wa Ruvu Shooting wakifa nyumbani kwao Mlandizi kwa mabao 2-0, huku Ndanda Fc ikianza ligi kwa kishindo kwa kuilaza wageni wenzao Stand United kwa mabao 4-1 mjini Shinyanga.
Nayo Mgambo ilianza vema ligi hiyo kwa kupata ushindi mwembamba nyumbani dhidi ya Kagera Sugar baada ya kuwazamisha wakata miwa hao bao 1-0. Bao pekee la mchezo huo lilifungwa na ramadhani Pela na kuifanya Mgambo kuanza tofauti iliyovyokuwa msimu uliopita ilipopigana kuepuka kushuka daraja.

HIVI NDIVYO VUMBI LA LIGI TANO ZA ULAYA LITAKAVYOTIMKA

http://hd.wallpaperswide.com/thumbs/barclays_premier_league_2014_2015-t2.jpghttp://luckybardc.com/files/Soccer-LuckyBar-v2-2013.jpg
LIGI tano zenye mvuto barani Ulaya inatarajiwa kutimka vumbi leo na MICHARAZO inakuletea baadahi ya ratiba zake kwa wikiendi hii na muda wa kurushwa kwa mechi zenye mvuto kwa saa za Afrika Mashariki.
Ratiba ya EPL:
QPR            v Stoke        (8:45) 
Aston Villa    v Arsenal    (11:00) 
Burnley        v Sunderland
Newcastle    v Hull City
Swansea        v Southampton
West Ham        v Liverpool    (1:30)
 
La Liga LEO:
Deportivo    v Real Madrid    (11:00) 
Athletic        v Granada CF
Atletico        v Celta Vigo
Espanyol        v Malaga

Seria A LEO:
Cesena        v Empoli
AC Milan        v Juventus    (3:45)

Bundesliga LEO:  
FC Augsburg    v Werder Bremen
Hamburg SV    v Bayern Munich
Paderborn    v Hanover 96
Schalke 04    v Frankfurt
Stuttgart    v Hoffenheim
Mainz        v Dortmund

Ligue 1 LEO:

Marseille    v Stade Rennes
FC Lorient    v Stade Reims
Metz            v Bastia
Nantes        v Nice
Toulouse        v Caen
Reuters

Kocha Liverpool ajipa matumaini juu ya kikosi chake

http://assets.kompas.com/data/photo/2014/08/31/2107275000-DV1855065780x390.jpgKOCHA wa Liverpool, Brendan Rodgers ametamba kwa kusema kuwa, Liverpool haihitaji fomula maalumu kutwaa ubingwa wa ligi kuu ya soka ya Uingereza na wachezaji wake wapya wameanza kuzoea maisha klabuni Anfield.
Baada ya kuvuka matarajio msimu uliopita na kushika nafasi ya pili nyuma ya mabingwa Manchester City, Liverpool imeanza kwa kusuasua msimu huu, ikifungwa mechi mbili kati ya nne za ligi kuu.
Lakini ikiwa ilisajili wachezaji wengi katika dirisha lililopita, Rodgers hadhani kama itachukua muda mrefu kabla ya kikosi chake kuzoeana na kuanza kupanda kwenye msimamo wa ligi.
"Siku zote tutaangalia namna tofauti tofauti za kushinda mechi. Hakuna fomula moja ya uhakika, ni kufanyia kazi kila siku kwenye uwanja wa mazoezi," Rodgers aliwaambia waandishi wa habari.
"Mwaka mmoja uliopita ningeweza kufukuzwa kazi, 'Tutakuja kufunga magoli?' na kama mtakumbuka tulimaliza na magoli 101 msimu uliopita.
"Tulilazimika kusajili wachezaji wengi katika dirisha lililopita kwa sababu ya Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya. Hili huchukua muda mrefu zaidi kidogo lakini nimeridhishwa na jinsi kila mmoja anavyozoea mazingira. Tuna wachezaji wanaojizoea mazingira ya nchi nyingi tofauti."
Mmoja wa wachezaji wapya wa Rodgers, mshambuliaji Mario Balotelli, aliifungia Liverpool goli lake la kwanza kwenye ushindi wa Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya dhidi ya Ludogorets Jumanne.
Makubwa yanategemewa kutoka kwa Muitalia huyo mwenye hasira za karibu baada ya kuvaa viatu vya mfungaji bora wa msimu uliopita Anfield, Luis Suarez na Rodgers ameridhishwa na ukomavu ambao Balotelli ameonyesha tangu ajiunge kutoka AC Milan.
"Anaifahamu vizuri historia, si tu ya klabu bali ya jiji la Liverpool," Rodgers alisema. "Nitatumia muda mwingi na wachezaji wengi lakini ni kijana mzuri na nadhani unaweza kuona kwamba yupo tayari kwa kazi."
Baada ya kufungwa bila kutarajiwa na Aston Villa mwishoni mwa wiki iliyopita, Liverpool iliyo katika nafasi ya nane ni mgeni wa West Ham United leo ikitaraji kupunguza pengo la pointi sita na viongozi Chelsea.

Tanzania yazidi kuporomoka FIFA, Cameroon yapaa

http://imikinonews.com/files/news_images/1596757601114051870520140716101415.jpgTANZANIA imeendelea kuporomoka tena kwenye viwango vya soka vinavyotolewa kila mwezi na Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa), baada ya kuanguka kwa nafasi tano katika viwango vipya vilivyotolewa.
Tanzania, ambayo ilifungwa 2-0 na Burundi katika mechi ya kimataifa ya kirafiki iliyopita, sasa inakamata nafasi ya 115 duniani na 33 barani Afrika ikiwa nyuma ya Uganda wanaoongoza Afrika Mashariki wakiwa nafasi ya 79 duniani na 19 Afrika, Rwanda walioko nafasi ya 93 duniani na 25 Afrika na Kenya walioporomoka kwa nafasi saba wakiwa nafasi ya 30 Afrika na 111 duniani.
Aligeria waliopanda kwa nafasi nne, wanaongoza barani Afrika wakiwa nafasi ya 20 duniani wakifutwa na Ivory Coast walioshuka kwa nafasi tatu baada ya kukubali kichapo cha mabao 4-1 kutoka kwa Cameroon waliopanda kwa nafasi 12 na kukamata nafasi ya nane Afrika na 42 duniani.
Nafasi ya tatu barani Afrika inakaliwa na Tunisia (31) wakipanda kwa nafasi 11 wakifuatwa na Ghana (33), Senegal (36), Nigeria (37) na Cape Verde (41). Guinea waliopanda kwa nafasi 16 wanakamata nafasi ya tisa barani Afrika na 48 duniani huku Burkina Faso waliopanda kwa nafasi 10 wakifunga pazia la 10 bora barani Afrika wakifungana na Guinea katika nafasi ya 48 duniani.
Uganda pia ni wa kwanza katika Ukanda wa Cecafa wa Afrika Mashariki na Kati wakifuatwa na Rwanda, Kenya, Tanzania, Burundi, Ethiopia (39, 132), Sudan (40, 133), Shelisheli (47, 172), Sudan Kusini (50, 185), Eritrea (52, 202), Somalia (53, 204) huku Djibouti wakifunga mlango Cecafa na Afrika wakiwa 54 Afrika na 205 duniani.
Mabingwa wa dunia, Ujerumani wanaongoza 10 bora ulimwenguni wakifuatwa na Argentina, Colombia waliopanda kwa nafasi moja wakiwashusha Uholanzi, Ubelgiji, Brazil, Uruguay, Hispania, Ufaransa na Uswis.

Spurs walalamikia ubaguzi, wenyeji wao waomba radhi

Roberto Soldado
Patashika baina ya Spurs na Partizan

partizan banner
Bango lililoibua hisia za kibaguzi ambalo Spurs wamelalamikia UEFA
Jan Verthongen (R) challenges Partizan Belgrade"s Danko Lazovic UONGOZI wa klabu ya Tottenham Hotspurs limepeleka malalamiko yao Shirikisho la Soka la Ulaya, UEFA kufuatia kuonyeshwa kwa mabango yenye kulenga ubaguzi na mashabiki wa Partizan Belgrade. 
Meneja wa Spurs Mauricio Pochettino ameelezea bango hilo kama jambo lisilokuwa na heshima na lisilokubalika. 
Spurs walishindwa kutamba ugenini baada ya kulazimishwa suluhu na wenyeji wao katika Uwanja wa Partizani, nchini Serbia.
Maofisa wa Spurs waliwataarifu UEFA juu ya uwepo wa bango hilo kabla ya mapumziko na wajumbe wake walilipiga picha kama ushahidi baada ya mchezo huo. 
Mwaka 2007, Partizan walitolewa katika michuano ya Kombe la UEFA na kutozwa faini kwa vurugu wakati wa mchezo wa mkondo wa kwanza wa michuano hiyo dhidi ya Zrinjski Mostar.
Tayari uongozi wa klabu ya Partizan imeomba radhi kwa kitendo hicho kilichofanywa na mashabiki wao kupitia mabango hayo.