STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, January 18, 2015

Wenyeji AFCON waanza na sare, Gabon yaua 2-0

Nahodha wa Guinea ya Ikweta, Emilio Nsue akiifungia timu yake bao katika mechi dhidi ya Kongo
Pierre-Emerick  Aubameyang akishangilia bao la kuongoza na Gabon wakati akiiongoza timu yake kushinda mabao 2-0 dhidi ya Burkina Faso (Picha:SuperSport)
Mashabiki wa soka nchini Guinea ya Ikweta wakimimika uwanjani kushuhudia ufunguzi wa michuano hiyo mjini Bata
BATA, Guinea ya Ikweta
FAINALI za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) zimeanza kwa kishindo kwa kushuhudiwa wenyeji, Guinea ya Ikweta ikilazimishwa sare ya 1-1 huku Gabon wakiifumua wanafainali zilizopita, Burkina Faso kwa mabao 2-0 katika mechi za ufunguzi zilizochezwa mjini Bata.
Wenyeji wakiwaanikizwa na washangiliaji wao, walitangulia kupata bao katika mechi ya mapema kupitia kwa Nsue aliyefunga katika dakika ya 16 kabla ya Kongo kuchomoa zikiwa zimesalia dakika tatu kupitia kwa Thievy Bifouma na kuwanusuru wakali kuambulia pointi moja katika kundi lao la A.
Katika mechi iliyofuata, Gabon ikiongoza na mshambuliaji nyota anayeichezea Borussia Dortmund, Pierre-Emerick Aubameyang wakipata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Burkina Faso.
Aubameyang alianza kwa kufunga bao la kuomngoza katika dakika ya 19 kabla ya Malick Evouna kuongeza bao la pili lililowakatisha tamaa 'Farasi Weupe' wa Burkinabe baada ya kufunga bao katika dakika ya 72.
Katika mfululizo wa michuano hiyo leo timu za Kundi B zitashika dimba la Ebebiyin kwa  mabingwa mara tatu wa fainali hizo, Tunisia watavaana na Cape Verde huku  Zambia wakitarajiwa kuumana na DR Congo.
Zambia na DR Congo ndiyo watakaoanza kuumizana saa 1 usiku kabla ya Tunisia na Cape Verde kukutana katika mechi ya kisasi baada ya timu hizo kufanyiana mtimanyongo kwenye mechi za kuwania fainali za Kombe la Dunia kwa Tunisia kuichongea Cape Verde waliokuwa wamefuzu hatua ya mwisho kwa madai ya kumtumia mchezaji asiyestahili na Cape Verde kuzikosa fainali hizo, ingawa Tunisia walikwama licha ya kupeta katika rufaa yao baada ya kung'oka kwa Algeria walioenda kufanya maajabu kwa kufika raundi ya 16 Bora.
Jumla ya timu za mataifa 16 zinachuana kwenye fainali hizo ambazo zinachezwa Guinea ya Ikweta baada ya Morocco kugoma kuiandaa kwa madai ya kuhofia maambukizo ya Ugonjwa wa Ebola.
Kitu cha kustaajabisha ni kwamba waliokuwa mabingwa watetezi NIgeria wameshindwa kwenda kwenye fainali hizo zinazochezwa kuanzia jana na kutarajiwa kumalizika Februari 8 ambapo bingwa mpya atafahamika.

Hapatoshi leo England, Man City vs Arsenal

KIVUMBI cha Ligi Kuu ya England kinatarajiwa kuendelea leo kwa mechi mbili likiwamo linalovuta hisia za wengi litakalochezwa kwenye uwanja wa Etihad mjini Manchester kati ya wenyeji Manchester City dhidi ya Arsenal.
Pambano jingine la leo litazikutanisha timu za West Ham Utd watakaokuwa nyumbani kuwakaribisha Hull City katika uwanja wa Boleyn.
Mabingwa watetezi Manchester City wataikaribisha Arsenal wakitoka kulazimishwa sare katika mechi yao ya mwisho, ilihali Arsenal wakitoka kupata ushindi mnono wa mabao 3-0 dhidi ya Stoke City.
Ingawa Arsenal itakosa huduma za beki wake Mathieu Debuchy aliyeumia bega katika mechi yao iliyopita sambamba na kuwakosa wakali wengine ambao ni majeruhi kama ambavyo watetezi Man City watakavyokosa huduma za wakali wake akiwamo Yaya Toure na Wlifried Bony waliopo Afrika kwa sasa..
City itakuwa ikisaka ushindi nyumbani kuweza kuendelea kuwabana Chelsea wanaoongoza msimamo wa ligi hiyo wakati wao wakiwa wapo nafasi ya pili.
Watetezi hao wana pointi 47 wakati wapinzani wao Arsenal wakiwa na pointi 36 wakishika nafasi ya tano.
Ligi hiyo itaendelea kesho kwa pambano moja tu litakalozikutanisha timu za Everton dhidi ya West Bromwich Albion mechi itakayochezwa kwenye uwanja wa Goodson Park.

MTIBWA, JKT RUVU NANI KUIENGUA AZAM?

JKT Ruvu
Mtubwa Sugar
BAADA ya mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Azam kukalia kiti cha uongozi kwa kuiengua Mtibwa Sugar iliyokuwa imeking'ang'ania tangu ligi ianze kufuatia ushindi wake wa bao 1-0 ugenini dhidi ya Stand Utd, Wakata Miwa wa Manungu watajiuliza mbele ya maafande wa JKT Ruvu.
Timu hizo mbili zinatarajiwa kuumana jioni ya leo kwenye moja ya mechi mbili zinazochezwa leo kwenye mfululizo wa ligi hiyo, pambano litakalochezwa uwanja wa Chamazi, huku pambano jingine likiwa ni kati ya Wagosi wa Kaya, Coastal Union dhidi ya Polisi Moro mchezo utakaopigwa uwanja wa Mkwakwani-Tanga.
Mtibwa walifungwa na Simba kwa mikwaju ya penati 5-4 katika pambano la fainali ya Kombe la Mapinduzi na kuwa kipigo cha kwanza katika mechi za mashindano kwa msimu huu, na mchezo wa leo utakuwa na jasho na damu ili kurejea kileleni au kuwapisha maafande hao kukwea kileleni kwani wanalingana nao pointi.
JKT wapo nafasi ya tatu kwenye msimamo wakilingana pointi na Mtibwa sote zikiwa na pointi 16 na timu yoyote itakayoibuka na ushindi itaipiku Azam wenye pointi 17 baada ya ushindi wake wa jana.
Kocha wa Mtibwa Sugar, Mecky Mexime ametamba kuwa michuano ya Mapinduzi imewaivisha vema, licha ya kwamba hakufanikiwa kuitwaa ubingwa kama dhamira yao ilivyokuwa.
"Tunarejea kwenye ligi tukiwa tumekamilika, tuna hasira na dhamira ya kuendelea kulinda rekodi yetu ya kutopoteza mchezo wowote katika ligi hiyo," alisema Mexime.
Naye kocha wa timu ya JKT, Fred Felix Minziro alisema kuwa ameandaa vijana wake kuhakikisha wanaendelea vipigo kwa wapinzani wake ndani ya Ligi Kuu ili kutimiza lengo la kuiweka timu hiyo katika nafasi nzuri zaidi.
"Vijana wangu wapo tayari kwa vita, tunachotaka ni kupata ushindi bila kujali tunacheza na timu ipi," alisema Minziro.
Katika mechi nyingine za ligi hiyo zilizochezwa jana, Simba ikilata ushindi wa mabao 2-0 dhidi Ndanda mjini Mtwara, Yanga iling'anga'niwa na Ruvu Shooting kwa kutofungana kama ilivyokuwa kwa Mgambo JKT dhidi ya Prisons Mbeya na Kagera Sugar ililala nyumbani kwa bao 1-0 toka kwa Mbeya City.

Saturday, January 17, 2015

'MANYIGU' WA KAGAME KUWAPIMA STARS MABORESHO

AMAVUBI watakaokuja nchini Januari 21 kucheza na Stars Maboresho
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhX82vKFmbU_azF2jw6Sh1OefY0VH4MPXgegGJAQLnMmy6vNVnrI-U7UR0pkyKYfPWcecYEI-bvfVbXjelpAhelaeNjL5YqxsymlHKKyZfOv0aYMdCY5xQTD_WZWSuDm41Tr1kDs1jbA_yU/s1600/maboresho.png
Stars maboresho wanaotarajiwa kuvaana na Amavubi Januari 22
KIKOSI cha timu ya taifa ya Rwanda 'Amavubi' (Nyigu) wanatarajia kutua nchi katika kati ya wiki ijayo kuipima ubavu timu ya Taifa Stars Maboresho.
Tayari Kocha Mkuu wa Stars, Mart Nooij ameteua kikosi cha wachezaji 26 wa timu hiyo kwa ajili ya mchezo huo utakaopigwa kwenye uwanja wa CCM, Kirumba Januari 22, mwaka huu.
Nooij alisema kati ya wachezaji hao 10 ambao wanatoka katika mikoa ya kanda ya ziwa wataweka kambi Mwanza na wengine 10 wanaotoka upande wa Dar es Salaam wataweka kambi hapo Dar es Salaam.
Alisema kambi kwa ajili ya michuano hiyo itaanza rasmi kesho Jumapili  na siku inayofuata watakwenda Mwanza kuungana na wengine kwa ajili ya kambi ya pamoja.
“Mechi hiyo ni muhimu kwetu kwani wachezaji ambao watafanya vizuri tutawapandisha kucheza katika kikosi kikubwa,”alisema Nooij.
Nooij aliwataja wachezaji wa kikosi hicho kuwa ni; Aishi Manula, Benedict Tinoko, Miraji Adam, Andrew Vicent, Michael Gadiel, Emmanuel Semwanda, Joram Mgeveke, Edward Charles na Adam Salamba.
Wengine ni; Aboubakary Mohammed, Hassan Dilunga, Hussein Malombe, Shiza Ramadhani, Omari Nyenje, Kelvin Friday, Alfred Masumbakenda, Salim Mbonde, Atupele Green na Rashid Mandawa.
Pia wamo Manyika Peter, Salum Telela, Hassan Banda, Mohammed Hussein, Said Ndemla, Said Makapu na Simon Msuva.
Aidha,  kwa mujibu wa taarifa ya Mjumbe wa Kamati Tendaji ya Shirikisho la Soka Tanzani (TFF), Vedastus Lufano, kiingilio kwenye mechi hiyo itakuwa sh. 20,000 kwa viti maalumu (VIP), viti vya kawaida sh. 10,000 na mzunguko ni sh. 3,000.
Lufano aliwataja baadhi ya wachezaji wa Amavubi wanaotarajia kutua jijini Mwanza Januari 21 kwa ndege ya Rwanda Air, kuwa ni Marcel Nzarora, Olivier Kwizera, Sotel Kayomba, Ismail Nshutiyamagala , Emery Basiyenge na Michel Rushengoga.
Wengine ni Fitina Ombolenga, Janvier Mutijima, Haruna Niyonzima, Tean Baptista, Mugiraneza Savio, Nshuti Dominique, Patrick Sibomano, Jean Claude, Zagabe Andrew, Buteara Ernest , Sugira Danny, Ushengimana Betramed Iladukunda na Blenvue Mugenzi.
Lufano aliongeza kuwa taarifa iliyotumwa TFF kutoka Rwanda, Amavubi itaongozana na viongozi waliotajwa kuwa ni Stephen Costan, Vincent Mashami, Ibrahim Mugisha, Moussa Hakizimana, Nuhu Assouman, Boume Mugabe, Piere Baziki na Mkuu wa Msafara Bandora Felician.
Awali, Mkurugenzi wa Mashindano wa Shirikisho la Soka Tanzania(TFF) Boniface Wambura alisema mechi hiyo ni sehemu ya programu ya Kocha Mart Nooij kuiandaa timu hiyo kwa ajili ya mechi za mchujo michuano ya Afrika kwa  wachezaji wanaocheza Ligi za Ndani (CHAN). 
Mechi za mchujo za michuano hiyo ambayo fainali zake zitafanyika mwakani nchini Rwanda zinaanza Mei mwaka huu.

KIVUMBI CHA AFCON KUTIMKA HIVI KUANZIA LEO

MASHINDANO ya Mataifa ya Afrika, AFCON 2015, yanaanza rasmi leo nchini  Guinea ya Ikweta kwa nchi 16 wakiwamo wengine kuanza kuichuana kuwania taji lisilo na mwenyewe baada ya Nigeria kushindwa kufuzu.
Michuano hiyo iliyohamishiwa Guinea ya Ikweta baada ya waliokuwa wawe wenyeji wa fainali za 2015, Morocco kuchomoa kwa kisingizio cha kuhofia ugonjwa Ebola ina makundi manne yenye timu 4 kila mmoja.
Timu mbili za juu ndizo zitakazofanikiwa kufuzu robo fainali na miji minne ndiyo inayotumika katika fainali hizo ambayo ni mjini mkuu Malabo, Bata, Mongomo na Ebebitin.
Makundi yapo kama ilivyo hapo chini;
http://www.diskifans.com/wp-content/uploads/2014/12/CAF-620x274.jpg
VIWANJA:
-Estadio de Bata, Mjini Bata, Watazamaji 37,500
-Nuevo Estadio de Malabo, Malabo, Watazamaji 15,250
-Estadio de Mongomo, Mongomo, Watazamaji 10,000
-Nuevo Estadio de Ebebiyín, Ebebitin, Watazamaji 5,000

Leo Jumamosi kutakuwa na michezo miwili ya ufunguzi ya Kundi A ambapo mechi ya awali itawakutanisha wenyeji Guinea ya Ikweta (Equatorial Guinea) dhidi ya mabingwa wa mwaka 1972, Congo Brazzaville watakapocheza kwenye uwanja wa Bata Mjini Bata na kufuatia Mechi ya Burkina Faso na Gabon Uwanjani hapo hapo.
Kesho Jumapili ratiba inaonyesha ni zamu ya timu za Kundi B ambapo mabingwa wa mwaka 2012 Zambia wataumana na DR Congo na usiku itakuwa zamu ya mabingwa mara tatu wa fainali hizo Tunisia dhidi ya wageni wa michuano hiyo Cape Verde.
Ratiba inaonyesha kila siku kuanzia leo kutakuwa na michezo mwili  na Fainali zake zitachezwa Februari 8 kwenye uwanja wa Bata, mjini Bata ambapo Afrika itashuhudia na kumtambua bingwa mpya wa AFCON.
Wenyeji Guinea ya Ikweta hii ni mara yao ya pili kuanza fainali hizo kwani mwaka 2012 waliziandaa kwa kushirikiana na majirani zao Gabon ambao safari hii wamepangwa kundi moja pamoja nao.
AFCON 2015:RATIBA
Jumamosi Januari 17

19:00 Equatorial Guinea v Congo [Estadio de Bata]
22:00 Burkina Faso v Gabon [Estadio de Bata]

Jumapili Januari 18
1900 Zambia v Congo DR [Nuevo Estadio de Ebebiyín]
2200 Tunisia v Cape Verde Islands [Nuevo Estadio de Ebebiyín]

Jumatatu Januari 19
1900 Ghana v Senegal [Estadio de Mongomo]
2200 Algeria v South Africa [Estadio de Mongomo]

Jumanne Januari 20
1900 Côte d'Ivoire v Guinea [Nuevo Estadio de Malabo]
2200 Mali v Cameroon [Nuevo Estadio de Malabo]

Jumatano Januari 21
1900 Equatorial Guinea v Burkina Faso [Estadio de Bata]
2200 Gabon v Congo [Estadio de Bata]

Alhamisi Januari 22
1900 Zambia v Tunisia [Nuevo Estadio de Ebebiyín]
2200 Cape Verde Islands v Congo DR [Nuevo Estadio de Ebebiyín]

Ijumaa Januari 23
19:00 Ghana v Algeria [Estadio de Mongomo]
22:00 South Africa v Senegal [Estadio de Mongomo]

Jumamosi Januari 24
1900 Côte d'Ivoire v Mali [Nuevo Estadio de Malabo]
2200 Cameroon v Guinea [Nuevo Estadio de Malabo]

Jumapili Januari 25
21:00 Gabon v Equatorial Guinea [Estadio de Bata]
21:00 Congo v Burkina Faso [Nuevo Estadio de Ebebiyín]

Jumatatu Januari 26
21:00 Congo DR v Tunisia [Estadio de Bata]
21:00 Cape Verde Islands v Zambia [Nuevo Estadio de Ebebiyín]

Jumanne Januari 27
21:00 South Africa v Ghana [Estadio de Mongomo]
21:00 Senegal v Algeria [Nuevo Estadio de Malabo]
Jumatano Januari 28
21:00 Cameroon v Côte d'Ivoire [Nuevo Estadio de Malabo]
21:00 Guinea v Mali [Estadio de Mongomo]

ROBO FAINALI
Jumamosi Januari 31

19:00 Mshindi Kundi A v Mshindi wa Pili Kundi B [Estadio de Bata]==RF1
22:00 Mshindi Kundi B v Mshindi wa Pili Kundi A [Nuevo Estadio de Ebebiyín]==RF2

Jumapili Februari 1
19:00 Mshindi Kundi C v Mshindi wa Pili Kundi D [Estadio de Mongomo]==RF3
22:00 Mshindi Kundi D v Mshindi wa Pili Kundi C [Nuevo Estadio de Malabo]==RF4
NUSU FAINALI
Jumatano Februari 4

22:00 RF 1 v RF4 [Estadio de Bata]==NF1

Alhamisi Februari 5
22:00 RF2 v RF3 [Nuevo Estadio de Malabo]==NF2

MSHINDI WA 3
Jumamosi Februari 7

21:00 Aliefungwa NF1 v Aliefungwa NF2 [Nuevo Estadio de Malabo]

FAINALI
Jumapili Februari 8

22:00 Mshindi NF1 v Mshindi NF2 [Estadio de Bata]

Monday, January 12, 2015

Messi azikata maini zinazomnyemelea, adai haiendi kokote

http://news.bbcimg.co.uk/media/images/72166000/jpg/_72166204_hi020543910.jpg
Siendi Kokote
NYOTA wa klabu ya Barcelona, Lionel Messi amesisitiza kuwa haendi kokote wakati kukiwa na taarifa za kuhusishwa kunyemelewa na Chelsea na Manchester City.
Messi alisema klabu hizo zinazodaiwa kutaka kumnyakua 'wote ni waongo' na kwamba atasalia katika klabu yake ya Barcelona.
Mshambuliaji huyo wa Argentina ambaye jana alifunga bao la tatu wakati timu yake ikishinda nyumbani 3-1 dhidi ya Mabingwa watetezi alidai taarifa zote kwamba anataka kuondoka Nou Camp ni uzushi.
"Sijaulizwa chochote kuhusu kusalia hapa kwa sababu sitaki kwenda kokote kwa sasa," alisema Messi.
Aliongeza kuwa anasikia kwamba amefanya mazungumzo na klabu za Chelsea na Manchester City kwa ajili ya kujiunga na Ligi Kuu tya England na kudai 'klabu zote hizo ni waongo'.
Akihojiwa na kituo cha TV ya klabu hiyo katika kipindi cha El Marcador alisema
"Nimesikia kwamba nimefanya mazungumzo na Chelsea na (Manchester) City....lakini ni uongo mtupu."
Taarifa kwamba kuna ufa mkubwa baina ya Messi na Kocha wake, Luis Enrique zimechochea taarifa za ama Messi au kocha huyo kung'oka Nou Camp.
Messi amekanusha pia taarifa kwamba amekuwa sehemu ya kutimuliwa kwa majkocha na wachezaji ndani ya klabu hiyo kwa kudai hakuna kitu kama hicho.
"Kuna taarifa nyingi juu ya mahusiano mabovu baina ya (Pep) Guardiola, (Samuel) Eto'o, (Zlatan) Ibrahimovic Bojan (Krkic) hakuna ukweli wowote," alisema.
Mchezaji huyo alisema amechoka kusikia habari za uzushi kuhusu yeye.

Waziri Mahanga azindua kitabu cha Marehemu Steven Kanumba

NAIBU Waziri wa Kazi na Maendeleo ya Vijana, Makongoro Mahanga,  jana amezindua rasmi kitabu cha marehemu Steven Charles Kanumba, Kinachoitwa ''Steven Charles Kanumba: The Great Fallen Tree''  kilichoandikwa na Emmanuel Zirimwabagabo, raia wa Congo anayeishi nchini Canada.
Akizungumza na wadau waliohudhuria hafla hiyo alisema vijana wanapaswa kutumia vipaji vyao kwa kujituma, kuthubutu na kufanya kazi kwa nguvu kama marehemu Kanumba na si kulalamika kila siku,  jambo linalopelekea kuibuka kwa makundi mbalimbali kama vile Panya Road na mengineyo.
Aidha mwandishi huyo amewataka wadau mbalimbali kumuunga mkono katika kukinunua kitabu hicho cha Kanumba, ambacho pia amekiandika kwa lugha ya Kiswahili na Kiingereza ili kuweza kukisambaza dunia nzima.
Alisisitiza kwamba vizazi vijavyo ambavyo havikumuona vitamfahamu muigizaji huyo nguli wa Tanzania kupitia kitabu hicho kilichozungumzia maisha yake yote ya enzi za uhai.
Wasanii mbalimbali wa filamu walihudhuria uzinduzi huo huku bendi ya Malaika chini ya Christian Bella ilitumbuiza kusindikiza uzinduzi huo.
(Na Gabriel Ng'osha/GPL).

Nani kuwa Mwanasoka Bora wa FIFA leo, Ni Ronaldo au Messi?

http://static.goal.com/672500/672581_herol.jpg 
KITENDAWILI cha Nani kuwa Mwanasoka Soka wa Dunia wa Shirikisho la Soka Duniani (FIFA Ballon d'Or 2014 kinatarajiwa kutenguliwa leo wakati mshindi atakapotangazwa.
Nyota wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo kutoka Ureno, Lionel Messi Muargentina anayeichezea Barcelona na kipa Manuel Neuer Mjerumani wa klabu ya Bayern Munich ndiyo wanaochuana kwenye tuzo hizo.
Messi anayeshikilia rekodi ya kunyakua tuzo hizo mara nne safari hapewi nafasi kubwa kama Ronaldo ambaye anaishikilia kwa sasa tuzo hiyo.
Hata hivyo kitendo cha kuvunja rekodi mbalimbali na kuifikisha timu yake kwenye fainali inampa nafasi ya kumuangusha Ronaldo, ingawa haitegemewi.
Wafuatiliaji wa soka wanaamini wachezaji wote watatu walioingia kwenye fainali wanastahili kunyakua tuzo hiyo, huku kipa Neuer akipigiwa chapuo kwa kuiwezesha timu yake ya taifa kutwaa ubingwa wa Dunia katika fainali za Kombe la Dunia za Brazil.
Je ni Messi, Ronaldo au Neuer atakayenyakua tuzo hiyo hiyo leo huko Uswisi zitakapotolewa.

Mwana Mfalme aahidi makubwa FIFA atakapochaguliwa

http://www2.pictures.zimbio.com/gi/Ali+Bin+Al+Hussein+FIFA+Ballon+Gala+2012+NI3gHmXp6hll.jpgMGOMBEA Urais katika uchaguzi ujao wa Shirikisho la Soka Duniani-FIFA, Prince Ali bin Al Hussein amejinadi kuwa atakuwa atalifanya shirikisho hilo kuwa la uwazi na uwajibikaji kama atachaguliwa kugombea kumshinda rais wa sasa Sepp Blatter katika Uchaguzi huo.
Prince Ali mwenye umri wa miaka 39 alitangaza mipango yake ya kugombania nafasi hiyo mapema wiki hii na kuapa kusafisha jina la shirikisho hilo ambalo hivi sasa limechaguzi kwa tuhuma mbalimbali za ufisadi. Mwana mfalme huyo wa Jordan amesema kama taasisi FIFA imekuwa ikifanya mambo yake kwa siri hivyo anadhani wakati umefika wa kubadilisha suala hilo na kulileta kwa wakati tunaoishi sasa wa ukweli na uwazi. Uchaguzi wa FIFA unatarajiwa kufanyika Mei 29 mwaka huu
Shirikisho la Soka Duniani, FIFA limekuwa likighubikwa na kashfa ya rushwa juu ya mchakato wa upatikanaji wa wenyeji wa fainali mbili za Kombe la Dunia za 2018 zitakazofanyika Russia na zile za 2022 zitakazochezwa Qatar.
Copy and WIN : http://bit.ly/copy_win

Wakala wa Ronaldo atwaa tuzo kwa mara ya 5 mfululizo

http://globesoccer.wpengine.netdna-cdn.com/wp-content/uploads/2014/05/Globe-Soccer-Awards-2371.jpgWAKALA wa mshambuliaji nyota wa kimataifa wa Ureno na klabu ya Real Madrid, Cristiano Ronaldo amefanikiwa kunyakuwa tuzo ya wakala bora kwa mara ya tano mfululizo ijulikanayo kama Globe Soccer Awards.
Wakala huyo Jorge Mendes amepewa tuzo hiyo kwa kutambua mafanikio yake kama wakala wa wachzaji mojawapo akiwa Ronaldo.
Mendes ambaye kwa mara kwanza kunyakuwa tuzo hiyo ilikuwa mwaka 2010 amekuwa akiwasimamia wachezaji bora kabisa duniani ambapo mbali ya Ronaldo mwingine ni James Rodriguez na hata meneja wa Chelsea Jose Mourinho.
Ronaldo ndio aliyenyakuwa tuzo ya mchezaji bora wa mwaka inayotolewa na Globe Soccer huku meneja wa Madrid Carlo Ancelotti akinyakuwa tuzo ya kocha bora.

Mchungaji auwawa Kanisani akiendesha ibada

Security officers examin the lifeless body of an assistant pastor George Karidhimba Muriki of the Maximum Revival Ministries Church after he was shot dead by...
maafisa wa Polisi wakimsaidia msaidizi wa mchungaji aliyeuwawa nje ya kanisa hilo (Picha:AP)
WATU wenye silaha wasiofahamika walimfyatulia risasi na kumuuwa mchungaji mmoja wakati wa ibada kanisani siku ya jumapili katika mji wa Mombasa nchini Kenya  maahala ambako polisi wanapambana na vijana wa ki-islam wenye msimamo mkali.
Mauaji hayo yalitokea ndani ya mlango mkuu wa kuingilia kwenye kanisa la Maximum Revival Centre katika mtaa wa majengo. 
Mashahidi wanasema polisi waliwazuia watu wenye silaha kuingia ndani ya kanisa na kuuwa waathirika Zaidi. Watu hao wenye silaha hawajafahamika  lakini kundi la wanamgambo wa Al-Shabab kutoka nchi jirani ya Somalia limeshambulia malengo kadhaa nchini Kenya. Kundi hilo la Al-Shabab liliapa kulipiza kisasi kwa majeshi ya Kenya kuwepo nchini Somalia kwa ajili ya kusaidia  wanajeshi wa serikali dhidi ya wanamgambo hao.
VOA

Messi, Suarez, Neymar wafunga Barca wakiua Atletico Madrid

Lionel Messi, Neymar and Luis Suarez
Nyota wa Barcelona wakishangilia ushindi wao
Lionel Messi, Neymar and Luis Suarez
Furaha tupu kwa wakali wa Nou Camp
WASHAMBULIAJI nyota wa Barcelona Lionel Messi, Luis Suarez na Neymar wote walifunga wakati timu yao ikiiadhibu mabingwa watetezi wa La Liga, Atletico Madrid kwa mabao 3-1 kwenye mchezo wa ligi hiyo ya Hispania.
Neymad alianza kufungua karamu ya mabao kwa wenyeji waliokuwa uwanja wa Nou Camp katika dakika ya 12 baada ya kumalizia kazi nzuri ya  Suarez kabla ya Suarez kufunga b ao la pili dakika ya 35 kwa kazi nzuri ya Messi.
Wenyeji walipata bao la kufutia machozi lililofungwa na Mario Mandzukic katika dakika ya 57 kwa mkwaju wa penati baada ya Messi kucheza madhambi langoni mwake dhidi ya Jesus Gamez.
Hata hivyo mshambuliaji huyo anayenyemelewa na Chelsea, alisahihisha makosa kwa kutumbukiza wavuni bao la tatu dakika tatu kabla ya pambano hilo kumalizika na kuifanya Barcelona kuwapumulia Real Madrid kwa tofauti na pointi moja, wenyewe wakiwa na 41 wakati Real wakiwa na 42.
Atletico Madrid wameendelea kusalia nafasi ya tatu wakiwa na pointi 38 baada ya kucheza mechi  18 kama Barcelona, huku Real Madrid akiwa na mecho moja mkononi kwani imecheza mechi 17 tu.
Katika mechi nyingine za ligi hiyo, Athletic Bilbao ilikubali kipigo cha 2-1 nyumbani dhidi ua Elche, Granada ililazimishwa sare ya 1-1 nyumbani na Real Sociedad inayonolewa na kocha David Moyes na leo usiku Rayo vallecano itakuwa wenyeji wa Cordoba katika mfululizo wa ligi hiyo inayozidi kushika kasi.

Juventus yaifyatua Napoli 3-1, yazidi kujikita kileleni

Paul Pogba akishangilia na wenzake
VINARA wa Ligi Kuu ya Italia, Serie A, Juventus imeendelea kujiimarisha kileleni mwa msimamo wa ligi hiyo baada ya kuikung'uta Napoli wakiwa ugenini kwa mabao 3-1.
Bao la Paul Pogba katika dakika ya 29 akimalizia kazi nzuri ya Llorente liliwashtua wenyeji ambao walienda mapumziko wakiwa nyuma kabla ya kuzinduka kipindi cha pili baada ya iguel Britos kusawazisha dakika ya 64.
Dakika ya 69 wageni waliongeza bao la pili kupitia Martin Cacerea aliyemaliza pande la Andrea Pirlo na katika dakika za lala salama Arturo Vidal aliifungia Juventus bao la tatu na kuifanya timu hiyo kufikisha pointi 43 na kuzidi kuwakimbia wapinzani wa AS Roma waliomalizishwa sare ya 2-2 nyumbani na Lazio mapema jana.
Katika mchezo mwingine wa ligi hiyo Sampdoria ilikubali kichapo cha bao 1-0 toka kwa Empoli.

Ali Baucha, Ney wa Mitego waja na Vululu

BAADA ya kutamba na 'Chimpododo' na 'Zumzum' aliomshirikisha K-One, dansa wa zamani na mtayarishaji mkongwe wa muziki nchini, Ali Baucha anajiandaa kuachia wimbo wake mpya uitwao 'Vululu'.
Baucha aliiambia MICHARAZO kuwa wimbo huo mpya ambao umerekodiwa katika studio za Baucha Records, ameimba akishirikiana na Ney wa Mitego.
"Katika kuukaribisha mwaka mpya wa 2015, nipo mbioni kuiachia kazi yangu mpya iitwayo 'Vululu' niliyoimba na msanii Ney wa Mitego, kila kitu kimekamilika kilichobakia ni siku ya kutoka hadharani," alisema Baucha.
Baucha alisema wimbo huo wa 'Vululu' ni miongoni mwa kazi mpya zilizotengenezwa na studio zake za Baucha Records.
Alisema kazi nyingine zitakazoachiwa ni pamoja na wimbo mpya wa K-One alioimba na Suma Lee na kazi mpya ya Fizzo aliyesumbua mwaka jana na '24 Hours' ambaye safari hii ataimba na Walter Chilambo

Rama Pentagone wa Twanga Pepeta Tajiri Penzi

MUIMBAJI mahiri wa bendi ya African Stars 'Twanga Pepeta', Ramadhan Mhoza 'Pentagone' amefyatua wimbo wake binafsi uitwao 'Tajiri Penzi'.
Wimbo huo uliorekodiwa kwa mtayarishaji Amaroso ni utambulisho wa albamu binafsi ya muimbaji huyo wa zamani wa bendi ya Double M Sound, Levent Musica na Extra Bongo.
Akizungumza na MICHARAZO, Pentagone alisema wimbo huo ulio katika mahadhi ya rhumba ni kati ya nyimbo zitakazokuwa katika albamu yake aliyopanga kuitoa baadaye mwaka huu.
"Katika kutimiza ahadi yangu kwa mashabiki, nimetengeneza wimbo mpya uitwao 'Tajiri Penzi' ambao upo katika miondoko ya rhumba na ni kazi yangu binafsi nje ya Twanga Pepeta," alisema.
Pentagone alisema kwa sasa anajipanga kwa ajili ya kutengeneza video ya wimbo huo kabla ya kuanza kurekodi nyimbo nyingine kukamilisha albamu yake ya kwanza itakayokuwa na jumla ya nyimbo sita au nane

Manchester United yapigwa nyumbani, yaporomoka EPL

Dusan Tadic (second right) pounces upon the rebound and converts coolly to hand Southampton the lead against Manchester United
Dusan Tadic akifunga bao pekee la Southampton
Southampton captain Jose Fonte led from the back for Southampton and kept Robin van Persie from having any impact on the game
van Persie akiwania mpira na Jose Fonte
Juan Mata (right) missed a number of good chances to level the scores shortly after Southampton went ahead against United
Juan Mata akijaribua kufunga bao
United captain Wayne Rooney cut a dejected figure as he left the pitch after the full time whistle was blown
Nahodha Wayne Rooney akiwa haamini kama wamepigwa kidude nyumbani
KLABU ya Manchester United licha ya kucheza uwanja wa nyumbani na ikiwa imefarijika kwa kurejea dimbani kwa baadhi ya nyota wake waliokuwa majeruhi imeshindwa kufurukuta baada ya kuchapwa bao 1-0 na Southampton katika mechi ya Ligi Kuu ya England.
Bao pekee la wageni ambao ni maarufu kama 'Watakatifu' lililowanyong'onyesha Mashetani Wekundu liliwekwa kimiani katika dakika ya 69 na Dusan Tadic na kuwafanya Southampton kukwea hadi nafasi ya tatu katika msimamo wa ligi hiyo wakiiengua Manchester United.
Ushindi umeifanya Southampton ambayo imelipa kisasi cha kufungwa nyumbani mwezi uliopita kwa mabao 2-1 na wapinzani wao kufikisha pointi  39, mbili zaidi ya ilizonazo vijana wa Luis Van Gaal licha ya zote kucheza mechi 21 kila moja.
Pia ni ushindi wa kwanza wa vijana wa Ronald Koeman katika uwanja wa Old Trafford tangu miaka 27 iliyopita kitu ambachop kimempa faraja kubwa koxcha huyo Mholanzi aliyewahi kuwa msaidizi wa Van Gaal.

Sunday, January 11, 2015

Sevilla yazidi kuchanja mbuga La Liga

http://videosdelbetis.com/wp-content/themes/Video/thumb.php?src=http://videosdelbetis.com/wp-content/uploads/2013/11/sfc.jpg&w=630&zc=1&q=80&bid=1TIMU ya Sevilla ikiwa uwanja wa ugenini ilipata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Almeria na kujiweka katika nafasi nzuri katika mbio zao kwenye Ligi Kuu ya Hispania, La Liga.
Sevilla ilijikuta ikisubiri hadi kwenye kipindi cha pili kuweza kupata mabao yake hayo ambayo yalifungwa na Iborra katika dakika ya 58 kabla ya Coke kuongeza jingine dakika tano baadaye na kuifanya timu hiyo kufikisha pointi 36 na kushika nafasi ya nne.
Mashabiki wa soka wanatarajia kupata burudani baadaye wakati Barcelona itakayokuwa nyumbani itaikaribisha mabingwa watetezi wa ligi hiyo, Atletico Madrid zinazofukuzana nyuma ya vinara Real Madrid ambayo jana ilizinduka katika ligi hiyo klwa kushinda mabao 3-0 dhidi ya Espanyol.

Mgambo JKT yaitoa nishai Ruvu Shooting Mkwakwani


http://tplboard.co.tz/assets/uploads/files/273f8-63.jpg
Mgambo JKT waliopata ushindi dhidi ya Ruvu Shooting
TIMU ya Mgambo JKT imeitoa nishai Ruvu Shooting katika mfululizo wa Ligi Kuu Tanzania Bara mchezo pekee uliochezwa  leo kwenye uwanja wa Mkwakwani Tanga baada ya kuicharaza bao 1-0.
Ruvu Shooting inayonolewa na kocha Mkenya, Tom Oloba ilishindwa kuhimili vishindo vya maafande wenzao licha ya tambo zilizokuwa zikitolewa na uongozi wa klabu hiyo chini ya Msemaji wao, Masau Bwire.
Bao hilo la wenyeji liliwekwa kimiani na Full Maganga katika dakika ya 44, likiwa ni bao la kwanza kwa mchezaji huyo ambaye amekuwa na kismati cha kuzitungua Simba na Yanga.
Kwa ushindi huo Mgambo imefikisha pointi 12 na kuchupa kutoka nafasi ya 12 hadi nafasi ya nane wakiing'oa Ruvu Shooting ambayo imesaliwa na 11.
Msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara baada ya mchezo wa leo:
                                 P   W    D    L    F    A   GD   Pts
01. Mtibwa Sugar       08  04  04  00  11  04  07   16
02. JKT Ruvu             10  05  01  04  10  09   01  16
03. Yanga                  08  04  02  02  11  07   04  14
04.  Azam                  08  04  02  02  10  06   04  14
05.  Kagera Sugar      09  03  05  01  07  04   03  14
06.  Polisi Moro          10  03  05  02  09  08   01  14
07. Coastal Union      09  03  03   03  09  08   01  12
08.  Mgambo JKT      09  04  00  05   05    09  -4  12
09. Ruvu Shooting    10  03  02   05   05   08  -3  11
10. Stand Utd           10  02  05   03   07   12  -5  11
11. Ndanda Fc          10  03  01   06  10    14  -4  10
12. Simba                08  01  06   01   07   07  00  09
13. Mbeya City         08   02  02   04  03   06  -3   08
14. Prisons               09  01  04   04  06   08  -2   07

Wafungaji Bora:
5-
Didier Kavumbagu(Azam)
4-
Rama Salim (Coastal), Danny Mrwanda, Simon Msuva (Yanga) Ame Ally (Mtibwa), Samuel Kamuntu (JKT Ruvu)

3- Ally Shomari, Emmanuel Okwi (Simba), Rashid Mandawa (Kagera Sugar), Jacob Massawe (Ndanda)
2- Shaaban Kisiga, (Simba), Nassor Kapama (Ndanda) Salum Kanoni (Kagera), Aggrey Morris (Azam),  Najim Magulu, Jabir Aziz (JKT Ruvu), Amissi Tambwe, Jerry Tegete (Yanga), Ibrahim Kihaka (Prisons), Mussa Mgosi (Mtibwa), Heri Mohammed, Mussa Said (Stand Utd), Ally Nassor (Mgambo),  Malimi Busungu (Mgambo), Nicolaus Kabipe (Polisi)
1- Joseph Owino (Simba), Coutinho, Kelvin Yondan, Haruna Niyonzima, Jaja (Yanga), Deo Julius, Steven Mazanda (Mbeya City), Bakari, Imani Mapunda, Said Bahanuzi (Polisi-Moro), Kipre Tchetche,  Aggrey Morris, SHomar Kapombe, John Bocco  (Azam), Ernest Joseph, Paul Ngalema,  (Ndanda), Jacob Mwaitalako,  Laurian Mpalile, Amir Omary, Hamis Mahingo (Prisons), Lutimba Yayo, Kennedy Masumbuko, Joseph Mahundi, Hussein Sued,Itubu Intembe (Coastal), Ramadhani Pella, Full Maganga (Mgambo), Said Mkopi, Vincent Barnabas (Mtibwa), Amos Mgina, Najim Magulu, (JKT Ruvu), Salum Kamana, Shaaban Kondo (Stand Utd), Paul Ngwai, Atupele Green(Kagera Sugar), Juma Nade, Abdulrahman Mussa, Thomas Mathayo , Hamis Kasanga ,Zubeiry Dabi (Ruvu Shooting)

Inter Milan yatamba nyumbani,

Nemanja Vidic
Vita ya Inter Milan dhidi ya Genoa leo
KLABU ya Inter Milan imefanikiwa kuifumia Genoa kwa kuicharaza mabapo 3-1 katika mechi kali ya Ligi Kuu ya Italia, Serie A, wakati AS Roma na mahasimu wao Lazio wametoshana nguvu ya maba0 2-2.
Inter ikiwa nyumbani ilipata ushindi huo kupitia mabao ya Palacio katika dakika ya 12, Mauro Icardi dakika ya 39 na Nimanja Vidic dakika mbili kabla ya mechi kumalizika, huku bao la wageni lilifungwa na Izzo dakika ya 85.
Katrika mechi nyingine za ligi hiyo,
Atlanta ikiwa nyumbani imelazimishwa sare ya 1-1 na Chievo Verona, Cagliari ikainyoa Cesena mabao 2-1 na Fiorentina ikipata ushindi mtamu nyumbani dhidi ya Palermo baada ya kuinyoa mabao 4-3.
Nayo Hellas Verona ikiitafuna Parma waliowafuata kwao kwa mabao 3-1 na Mahasimu wa jiji la Roma, AS Roma na Lazio zilishindwa kutambiana kwa kutoka sare ya 2-2 na Sampdoria iliilaza Empoli kwa bao 1-0 baadaye Napoli watakuwa wenyeji wa vinara Juventus.

Arsenal yaitoa nishai Stoke City Sanchez azidi kung'ara

The Arsenal players join star man Sanchez in celebration of his second goal of the afternoon
Wachezaji wa Arsenal wakipongezana
Arsenal defender Koscielny (6) heads the north London club into an early lead at the Emirates after just six minutes
Laurent Koscielny akifunga bao la kwanza la Arsenal kwa kichwa
MABAO mawili kutoka kwa Alexis Sanchez na jingine la beki Laurent Koscielny yameiwezesha Arsenal kupata ushindi mujarabu nyumbani dhidi ya 'wagumu' Stoke City katika mfululizo wa mechi za Ligi Kuu ya England.
Ushindi  huo umekuja wakati Arsenal ikitoka kupokea kipigo cha mabao 2-0 toka kwa Southampton, ambapo kiungo Mesut Ozil, alirejea uwanjani katika pambano hilo la Emirates baada ya kuwa nje miezi mitatu.
Wenyeji walianza kuandika bao dakika ya 6 kupitia Koscielny kabla ya Sanchez kuongeza la pili dakika ya 33 na kuja kuongeza jingine dakika nne tangu kuanza kwa kipindi cha pili.
Katika pambano hilo Arsenal ilijikuta ikimpoteza beki wake Mathieu Debuchy aliyeumia bega mapema na nafasi yake kuchukuliwa na Bellerin dakika chache baada ya Koscielny kufunga bao la kuongoza kwa kichwa akimaliza krosi ya Sanchez ambaye kwa mabao mawili ya leo amefikisha mabao 12 katika ligi hiyo anayoicheza kwa msimu wa kwanza.

Kwa ushindi hio Arsenal imefikisha pointi 36 na kulingana na Southampton na kukamata nafasi ya tano wakati wapinzani wao wamesaliwa na pointi26 na kusalia kwenye nafasi ya 11.
Muda mchache ujao Manchester United watakuwa uwanja wa Old Trafford kupepetana na Southampton katika mechi nyingine ya ligi hiyo ambayo baadhi ya nyota wa Man Utd waliokuwa nje kwa majeraha watarejea dimbani.
Wachezaji hao ni Daley Blind na Angel di Maria  ambao wapo kwenye kikosi cha kwanza cha kocha Louis Van Gaal.


Saturday, January 10, 2015

Ozil arejea Arsenal, Rojo, Blind waipa furaha Man Utd

Kipa Valdes akiwa na wachezaji wenzake wapya wa Manchester United

Daley Blind akifanya mazoezi hapa akiwa na Dogo Andreas Pereira
Rojo naye alipasha na wenzake
WAKATI Manchester United wakichelekea kurejea tena dimbani kwa nyota wake Marcos Rojo na Daley Blind, Kiungo Mesut Ozil wa Arsenal naye amepona na huenda akarejea uwanjani kesho wakati Arsenal inakipiga dhidi ya Stoke City.
Mashetani Wekundu wanatarajiwa kuwa nyumbani kuwavaa Southampton baada ya kupata sare mbili mfululizo ugenini katika Ligi Kuu ya England, lakini ikiwa na furaha kurejea kwa nyota hao sambamba na kumnasa kipa wa zamani wa Barcelona, Victor Valdes waliyemsainisha.
Kama ilivyo kwa Manchester, Arsenal wenyewe wanafurahi baada ya Ozil kurejea Ligi Kuu England baada ya kukaa nje miezi mitatu kutokana na maumivu ya goti.
Kocha Arsene Wenger amesema Ozil amekuwa akifanya mazoezi na wenzake na sasa yuko fiti, hata hivyo inaonekana ataanzia benchi.
Mjerumani huyo aliyejiunga na Arsenal akitokea Madrid aliumia katika mechi dhidi ya Chelsea, Oktoba mwaka jana.
Ozil ndiye mchezaji ghali zaidi Arsenal iliyompata kwa kitita cha pauni milioni 42.5.

Real Madrid yazinduka yaipiga Espanol 3-0

Gareth Bale
Bale akishangilia bao lake wakati Real ikiiadhibu Espanyol
Real Madrid v Espanyol
Nacho akishangilia bao lake
LICHA ya kucheza pungufu timu ya Real Madrid imepata ushindi wa mabao 3-0 nyumbani katika  Ligi Kuu ya Hispania dhidi ya Espanyol na kuzidi kujichimbia kileleni mwa msimamo wa ligi hiyo.
Fabio Coentrao alilimwa kadi nyekundu kaytika dakika ya 53, lakini mabao ya James Rodriguez katika dakika ya 12 , Gareth Bale dakika ya 28 na  lile na Nacho la dakika ya 70 yalitosha kuwapa ushindi muhimu Real Madrid iliyoshuhudia nahodha wake, Cristiano Ronaldo akitoka uwanjani bila kufunga bao ikiwa ni mara ya kwanza baada ya muda mrefu msimu huu.
Kwa ushindi hio Madrid wamefikisha pointi 42 na kuiacha Barcelona ikiwa nafasi ya pili na pointi 38 sawa na ilizonazo nazo Atletico Madrid ambazo zinatarajiwa kushuka dimbani kesho.
Katika mechi nyingine ya ligi hiyo iliyochezwa leo, Malaga ikiwa nyumbani ililazimishwa sare ya 1-1 na  Villarreal na hivi sasa Celta Viro ipo dimbani kuumana na Valencia nyumbani kwao na tayari wamekubali bao 1-0.

Haya ndiyo matokeo ya EPL kwa leo

Balotelli akichuana na mchezaji wa Sunderland
City ilipong'ang'aniwa na Everton ugenini leo
Chelsea wakipongezana baada ya kupata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Newcastle Utd
Sunderland     0 - 1     Liverpool
Burnley     2 - 1     Queens Park Rangers
Chelsea     2 - 0     Newcastle United
Everton     1 - 1     Manchester City
Leicester City     1 - 0     Aston Villa
Swansea City     1 - 1     West Ham United
West Bromwich …     1 - 0     Hull City    
Crystal Palace     2 - 1     Tottenham Hotspur

Fainali Mapinduzi ni Simba na Mtibwa

http://taarifa.co.tz/wp-content/uploads/2015/01/simba1.jpg
Simba waliowafuata Mtibwa Fainali za Kombe la Mapinduzi
Mtibwa Sugar (jezi za kijani) watakaoumana na Simba siku ya Jumanne
KLABU ya Simba imefanikiwa kutinga Fainali za michuano ya Kombe la Mapinduzi 2015 baada ya kuing'oa Polisi ya Zanzibar na sasa wanatarajiwa kukutana na Mtibwa Sugar siku ya Jumanne.
Mtibwa ilifanikiwa kufuzu hatua hiyo mapema leo jioni baada ya kuiondosha kwa mikwaju ya penati 4-3 'wababe' wa Yanga, JKU baada ya kumaliza dakika 90 wakiwa sare ya 0-0.
Simba iliyoonyesha mabadiliko makubwa tangu ianze kunolewa na kocha Goran Kopunovic, walipata nafasi hiyo muda mchache uliopita baada ya kupata ushindi wa bao 1-0 katika Nusu Fainali ya pili iliyochezwa uwanja wa Amaan. Zanzibar.
Bao lililoipelekea Simba kwenye hatua hiyo na kurejesha kumbukumbu ya nusu fainali ya mwaka 2010 ambapo timu hizo zilikutana na Mtibwa kuibuka wababe kabla ya kwenda kutwaa taji kwa kuilaza Ocean View bao 1-0.
Pia fainali hizo zinarejesha pia fainali ya ABC Top 8 iliyocvhezwa mwaka juzi na Simba kuilaza Mtibwa kwa mabao 4-3.
Mechi hiyo ya faionali itachezwa usiku wa Jumanne kwenye uwanja wa Amaan huku kila timu ikiwa na matumaini makubwa ya kutwaa taji hilo lililokosa mwenyewe baada ya KCCA ya Uganda kutemeshwa hatua ya Robo Fainali baada ya kufungwa kwa penati na Polisi.

JKT Ruvu waikamata Mtibwa Sugar,, yailaza Stand Utd Ndanda

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjjrGUIMxPw7cdxPgyXtAxRJHOSLFdOsz_Yetg7EBn6y-K7pPB3ToQogwImAjfSZceVrbx9aUL72b0URIua7OK30a6XbaCvr5aiWZXfZNKy95h3Kn2aQ1qmkPYpYSe6mpm7NGtNDBnXSwLZ/s640/DSC_0805.JPG
KIkosi cha JKT Ruvu kilichochupa hadi naasi ya pili ikiziengua Yanga na Azam
MAAFANDE wa JKT Ruvu jioni ya leo wamepata ushindi muhimu wa mabao 2-1 dhidi ya Stand United ya Shinyanga na kuikamata Mtibwa Sugar ambao wapo kwenye michuano ya Kombe la Mapinduzi 2015.
Samuel Kamuntu na Amos Mgina waliifungia mafaande hao mabao hayo na kuifanya timu hiyo inayonolewa na kocha Fred Felix Minziro katika mchezo uliochezwa uwanja wa Chamazi na kuifanya ifikishe pointi 16 sawa na Mtibwa waliosalia kileleni. Bao la wageni Stand lilifungwa na Mussa Said.
JKT waliotangulia michezo miwili mbele dhidi ya Mtibwa inatoautiana na vinara hao mabao ya kufunga na kufungwa, Mtibwa ikiwa na 11 na kuungwa manne ilihali JKT ikiwa na mabao 10 na kufungwa 9.
Katika mechi nyingine iliyochezwa mjini Mtwara, wenyeji Ndanda Fc ililazimishwa sare ya bao 1-1 dhidi ya Polisi Morogoro.
Wageni walitangulia kupata bao kupitia Said Bahanuzi kabla ya wenyeji kuchomoa kupitia Jacob Massawe na kumanya mshambuliaji huyo wa zamani wa Toto African na African Lyon kuikisha bao la tatu msimu huu.
Ligi hiyo itaendelea kesho kwa mechi moja tu itakayowakutanishja wenyeji Mgambo JKT itakayoikaribisha Ruvu Shooting kwenye uwanja wa Mkwakwani Tanga.