STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, February 11, 2015

Azam yaifumua Mtibwa Sugar 5-2 warudi kileleni

KLABU ya Azam wamerejea kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara baada ya kuifumua bila huruma Mtibwa Sugar kwa mabao 5-2.
Azam ambao ni mabingwa watetezi wa ligi hiyo wealipata ushindi huo mnono na wa kwanza kushuhudiwa katika mechi za ligi msimu huu katika pambano pekee lililochezwa kwenye uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam.
Frank Domayo 'Chumvi' alifunga mabao mawili moja kila kipindi sawa na alivyofanya Kipre Tchetche na Didier Kavumbagu alifunga moja kuiangamiza Mtibwa ambao hicho ni kipigo chao cha pili mfululizo.
Mtibwa walioanza msimu huu kwa mkwara na kuongoza ligi hiyo kwa muda mrefu kabla ya kuporomoka mara baada ya kurejea kwenye michuano ya Kombe la Mapinduzi, ilifunikwa eneo la kiungo na Azam.
Vijana hao wa Mecky Mexime walipata mabao yao ya kufutia machozi kupitia kwa Juma Nampaka na Ame Ali ambayo hata hivyo hayakusaidia Wakata Miwa hao kufurukuta mbele ya mabingwa watetezi hao.
Kwa ushindi huo umeifanya Azam kurejea tena kileleni wakifungana pointi 25 sawa na Yanga, lakini tofauti na mabao ya kufunga na kufungwa yanawapa nafasi ya kukalia kiti cha uongozi.
Mtibwa wenyewe wameendelea kusalia katika nafasi ya sita wakiwa na pointi 18 sawa na ilizonazo timu za Kagera Sugar na Coastal Union.
Yanga na Azam zinazochuana kieleleni mwishoni mwa wiki zitakuwa kwenye majukumu ya kimataifa wakati Yanga itaikaribisha BDF XI ya Bostwana na wenzao Azam wataumana na El Merreikh wanaotarajiwa kutua nchini kesho tayari kwa pambano hilo litakalochezwa Jumapili.
Pambano la Yanga litacheza Jumamosi na viingilio vimeshjatangazwa kwa kiingilio cha chini kikiwa ni Sh 5000 tu.
Wakati lile la Yanga kiingilio cha chini kabisa ni Sh 2000 na vingine ni VIPB Sh 5000 na VIP A 10000 na tyiketi zitaanza kuuzwa Ijumaa.

Mourinho amchongea Van Persie kwa FA

MENEJA wa vinara wa Ligi Kuu ya England, klabu ya Chelsea, Jose Mourinho amekishambulia Chama cha Soka cha Uingereza(FA) kwa kuamua kutochukua hatua yeyote kwa mshambuliaji wa Manchester United, Robin Van Persie kwa tuhuma za kumtwanga kiwiko mchezaji wa upinzani.
Van Persie alionekana akimpiga kiwiko James Tomkins wakati wa mchezo ambao United ilitoa sare ya bao 1-1 dhidi ya West Ham United Jumapili iliyopita lakini mwamuzi Mark Clattenburg hakuona tukio hilo huku FA nao wakilifumbia macho.
Uamuzi huo unamfanya Mourinho kutowaelewa FA kwani anatarajiwa kumkosa nyota wake Diego Costa katika mchezo wa leo dhidi ya Everton baada ya mshambuliaji wa kimataifa wa Hispania kufungiwa mechi tatu kwa kukutwa na hatia ya kumkanyaga kwa makusudi Emre Can mwezi uliopita.
Akihojiwa Mourinho amesema watu haohao ambao wamemfungia mchezaji wake Costa ndio hao ambao hawataki kumfungia Van Persie kwa kosa lake alilofanya.
Mourinho aliendelea kudai kuwa anajua kama angekuwa mchezaji wake lazima angefungiwa kwani tukio kama hilo lilimtokea Ramires na alilimwa adhabu.

Sanchez, Ramsey wazua hofu Arsenal

http://www3.pictures.zimbio.com/gi/Aaron+Ramsey+Alexis+Sanchez+Leicester+City+N8Hb6G9P6Rgl.jpg
Ramsey, Sanchez



KOCHA wa Arsenal, Arsene Wenger amesema ana wasiwasi kuhusu hali za nyota wake Alex Sanchez na Aaron Ramsey baada ya kupata majeruhi katika mchezo Ligi Kuu walioshinda mabao 2-1 dhidi ya Leicester City.
Ramsey alitolewa nje ikiwa ni dakika tisa tu toka aingie akitokea benchi katika kipindi cha pili baada ya kupata majeruhi ya msuli wa paja, huku winga wa kimataifa wa Chile, Sanchez yeye alitolewa nje kufuatia kuchezewa faulo na Matthew Upson ambayo ilimfanya kushindwa kuendelea na mchezo huo uliochezwa Emirates.
Wenger amesema ana wasiwasi na nyota wake hao kwani hana uhakika watakaa nje ya uwanja kwa kipindi gani wakijiuguza. Mabao yaliyofungwa na Laurent Koscielny na Theo Walcott yalitosha kuwapa Arsenal ushindi huo muhimu baada ya kuchapwa na  Tottenham Hospur
Mabao yaliyofungwa na Laurent Koscielny na Theo Walcott yalitosha kuwapa Arsenal ushindi huo muhimu baada ya kuchapwa na mahasimu wao Tottenham Hotspurs mwishoni mwa wiki iliyopita.

Monday, February 9, 2015

HII NDIYO SHOW TIME YA H-BABA

http://www.bongo5.com/wp-content/uploads/2012/10/H-baba.jpg
H-Baba


IVORY COAST NDIYO VIDUME AFRIKA, YARUDI YA 1992

The Ivory Coast team and staff pose with their Africa Cup of Nations trophy having defeated Ghana 9-8 on penalties on Sunday night
Waflame wa soka Afrika, Ivory Coast
The Ivory Coast team celebrate landing the Africa Cup of Nations on penalties, their first AFCON title since 1992
Oyooooooooooooooooo!
Ivory Coast captain and Manchester star Yaya Toure is presented with the Africa Cup of Nations trophy on Sunday evening
Nahodha Yaya Toure akipokea Kombe toka kwa Rais  Nguema
HISTORIA imejirudia tena nchini Guinea ya Ikweta baada ya Ivory Coast kufanikiwa kutwaa ubingwa wa Fainali za Mataifa ya Afrika 2015  kwa kuichapa Ghana kwa mikwaju ya penati kama ilivyokuwa katika fainali za mwaka 1992.
Katika fainali za mwaka huo, Ghana maarufu kama Black Stars walikufa kwa mikwaju ya penati 11-10 na usiku wa kuamkia leo walikubali tena kipigo cha penati 9-8 kwa wapinzani wao na kuliacha taji likienda kwa Ivory Coast ikiwa ni mara ya pili kwao.
Timu hizo zililazimika kupigiana penati baada ya kumaliza dakika 120 bila ya kufungana na katika upigaji wa penati, Ivory Coast walianza vibaya kwa Wilfried Bony kukosa penati, lakini haikuweza kuwakatisha tamaa Tembo wa Afrika kumaliza udhia na ukame wa miaka zaidi ya 20 tangu wanyakue taji la kwanza 1992.
Ghana wanaweza kujilaumu kwa kushindwa kuibuka mabingwa kwa mara ya tano kutokana na kipindi cha pili cha dakika 90 kutawala sehemu kubwa ya pambano hilo lililosisimua kutokana na lilivyokuwa kali.
Katika hatua ya mikwaju ya penati Black Stars walianza kwa Mubarak kufunga kabla ya Bony kukosa, Jordan Ayew akapata penati ya pili ya Ghana na Tallo wa Ivory Coast naye akaikosa penati yake na kufanya matokeo kuwa 2-0.
Hata hivyo Acquah na Acheampong walikosa penati  zilizofuata za Ghana, wakati Aurierna Doumbia walifunga zao na matokeo kuwa 2-2.
Andre Ayew alifunga mkwaju wake na Yaya Toure akasawazisha, John Mensah akafunga na Solomon Kalou akasawazisha kabla ya Agyemang-Badu kufunga mkwaju wake na Koro Toure kusawalisha.
Afful aliifungia Ghana na Kanon kusawazisha zoezi likawa piga nikupige hadi katika penati ya tisa ambapo Ghana kupitia kipa wake Razak Brimah ilikosa na Ivory Coast kutumbukiza yao iliyowapa ubingwa wa pili katika historia za michuano hiyo kupitia kwa Boubacar Barry aliyegeuka kuwa shujaa kabla ya nahodha Yaya Toure kukabidhiwa taji na Rais wa Guinea ya Ikweta, Nguema kwenye uwanja wa Bata.

Irene Uwoya awataka mashabiki wake kupokea Kisoda

Na Rahma White
MUIGIZAJI nyota wa filamu nchini, Irene Uwoya 'Oprah' amewataka mashabiki wake kujiandaa kuipokea kazi yake mpya iitwayo 'Kisoda' akidai ni kazi kali kuliko hata filamu yake ya awali iitwayo 'Apple' aliyoitoa mwaka jana.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, Irene alisema 'Kisoda' ni moja ya kazi zitakazoleta mapinduzi makubwa katika fani ya uigizaji nchini kwa namna ilivyoandaliwa ikishirikisha wasanii wa ndani na nje ya nchi.
Irene alisema filamu hiyo iliyomtafuna fedha nyingi ipo katika hatua ya uhariri na itaachiwa wakati wowote zoezi hilo likikamilika akiwataka mashabiki wajiandae kuipokea kwa mikono miwili.
"Kama kuna waliodhani nilibahatisha kwenye 'Apple', wamekosea safari hii naja na 'Kisoda', moja kati ya filamu kali ambayo imewashirikisha wasanii wa Tanzania na Afrika Kusini, chini ya kampuni yangu ya Apple Entertainment," alisema Irene.
Msanii huyo alisema amekusudia ndani ya mwaka 2015 awape burudani ya kutosha mashabiki wake na kwa kuanza ameanza na Kisoda kabla ya kufuatiwa na mambo mengine makubwa zaidi.
Irene aliwataja baadhi ya wasanii walioshiriki filamu nchini wa hapa nchini ukiondoa yeye (Irene) ni Islam, Mariam Ismail na Msami.
Kimwana huyo aliyewahi kunyakua tuzo ya Muigizaji w Kike Chipukizi wa tuzo za Kinara kupitia filamu ya Diversion of LOve' kabla ya kuanza kuzalisha filamu zake na kuwahi  kuendesha kipindi cha kwenye runinga cha 'Paradise Show' ameshiriki filamu zaidi ya 30 zilizomjengea umaarufu mkubwa ndani na nje ya nchi.
Baadhi ya kazi hizo ni; 'Ngumi ya Maria', 'Nyati',  'Zawadi Yangu', 'Aliyemchokoza Kaja', 'Figo','Rosemary', 'Snitch', 'The Return of Omega', 'Money Talk', 'Omega Confusion', 'Question Mark', 'Safari', 'Innocent Case', 'Nyota Yangu', 'Last Card', 'Doa la Ndoa', 'Offside' na 'Oprah'.

Sunday, February 8, 2015

Manchester Utd chupuchupu kufa ugenini

Falcao akijaribu kufunga
Kouyate akishangilia bao lake
Pilikapilika uwanjani
KLABU ya Manchester United imeponea chupu chupu kufa ugenini baada ya kupata sare ya 1-1 mbele yua West Ham United.

Bao la kusawazisha lililofungwa dakika za lala salama na Daley Blind liliwaokoa Mashetani Wekundu kufa katika uwanja wa Boleyn Ground.
Blind alifunga bao hilo katika dakika mbili za nyongeza na kumnusuru kocha Luis Van Gaal kuumbuka kama alivyonusurika kocha wa Manchester City jana dhidi ya Hull City baada ya vijana wake kusawazisha bao dakika za jioni.
Wenyeji walitangulia kupata bao dakika ya 49 kupitia kwa Cheikhou Kouyaté na kulikuwa na kila dalili kwa Mashetani Wekundu kufa ugenini, lakini Blind kuchomoa na kuifanya Manchester United kufikisha pointi 44 na kukomalia nafasi ya nne nyuma ya Southampton waliorejea katika Tatu Bora.
Hata hivyo dakika mbili za nyongeza baada ya Man kupata bao ilijikuta ikimpoteza beki wake, Luke Shaw kwa kupewa kadi nyekundu ilifuatia kutokana na kadi ya pili ya njano kwa kumchezea vibaya Stewart Downing.
Vikosi vilikuwa hivi; 
West Ham: Adrian, Jenkinson, Song, Tomkins, Cresswell, Kouyate, Noble, Downing, Nolan, Valencia, Sakho.
Sub: Jarvis, O'Brien, Amalfitano, Jaaskelainen, Cole, Oxford, Lee
Manchester United: De Gea, Valencia, Jones, Rojo, Shaw, Blind, Rooney, Januzaj, Di Maria, van Persie, Falcao
Sub: Mata, Smalling, Ander Herrera, Fellaini, Valdes, McNair, Wilson

Kocha Redknapp kurejea soka kama mwanahisa

http://talksport.com/sites/default/files/tscouk_old_image/blog/Harry-Redknapp_21.jpg
Kocha Harry Redknapp
MENEJA wa zamani wa klabu ya QPR, Harry Redknapp amebainisha anaweza kurejea katika ulimwengu wa soka akiwa sehemu ya mwanahisa.
Redknapp mwenye umri wa miaka 67 ambaye alijiuzulu kuinoa QPR wiki iliyopita kutokana na matatizo ya mguu anahusishwa na kikundi kinachotaka kununua klabu karibu na nyumbani kwake katka Pwani ya Dorset.
Akihojiwa Redknapp amesema jambo hilo linamvutia hivyo anataka kujihusha nalo, kwani mchezo wa soka bado uko katika damu yake.
Redknapp ambaye amewahi kuipeleka Tottenham Hotspurs katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya na pia kuzinoa klabu za Portsmouth na West Ham United aliongeza kuwa wana matumaini ya kupata klabu ya kuinunua.

Jose Mourinho aanza mbwembwe zake England

http://static.guim.co.uk/sys-images/Observer/Columnist/Columnists/2013/6/7/1370621593808/jose-mourinho-010.jpg
Jose Mourinho
KOCHA wa vinara wa Ligi Kuu ya England Chelsea, Jose Mourinho amesema hadhani kama tofauti ya pointi saba walionayo kileleni mwa msimamo wa Ligi hiyo ni faida katika mbio zao za kugombea taji hilo. Chelsea imeitandika Aston Villa kwa mabao 2-1 jana, wakati Manchester City wanaowafuata katika nafasi ya pili wakipotoka sare na Hull City wanaokamata nafasi ya tatu toka mkiani.
Akihojiwa Kocha Mourinho, amesema ingekuwa nchi nyingine angeweza kuanza kushangilia katika kwa Uingereza tofauti ya alama saba sio chochote.
Mourinho aliendelea kudai kuwa bado kuna mechi 14 na alama 42 za kupigania hivyo kila mchezo unakuwa mgumu na chochote kinaweza kutokea.
Kocha huyo pia alisisitiza hakushtushwa kuona City wakitoa sare nyumbani na Hull ambao wako mstari wa kushuka daraja lakini amefurahi kuona matumaini ya kunyakuwa taji yakiwa mikononi mwao.
Ligi hiyo iliendelea tena jioni ya leo kwa timu za Newcastle United wakipata sare ya 1-1 na timu ya Stoke City wakati West Bromwich Albion wakiwa ugenini walipata sare ya 2-2 dhidi ya timu ya Burnley.

Sepp Blatter aponda vyombo vya habari vurugu AFCON

http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/4/44/Sepp_Blatter_at_signing_of_agreement_creating_FIFA_Ballon_d%E2%80%99Or_in_Johannesburg_2010-07-05_1.jpg
Rais wa FIFA, Sepp Blatter
RAIS wa Shirikisho la Soka la Dunia (FIFA) Sepp Blatter, ameponda vyombo vya habari kuonyesha vurugu zilizozuka katika mchezo wa nusu fainali ya michuano ya Mataifa ya Afrika kati ya wenyeji Guinea ya Ikweta na Ghana.
Mchezo huo uliochezwa Malabo ulisimamishwa kwa dakika 30 baada ya mashabiki kurusha vitu kwa wachezaji na mashabiki wa timu pinzani hali iliyosababisha polisi kutumia helikopta na mabomu ya machozi kuwatawanya mashabiki hao.
Vurugu hizo zilikuwa zikirushwa moja kwa moja duniani kote, lakini Blatter anadhani pamoja na vurugu hizo lakini kuna mazuri mengi ya kusifiwa katika michuano hiyo inayotarajiwa kumalizika leo.
Blatter amesema siku zote habari nzuri huwa sio habari ila habari mbaya ndio habari akimaanisha kuwa siku zote watu wamekuwa wakizungumzia mabaya.
Rais huyo amesema dosari ndogo kama iliyotokea katika mchezo wa nusu fainali haipaswi kupewa nafasi ya kusahau mafanikio yaliyopata katika michuano hiyo ambayo imendaliwa kwa kipindi kifupi kuliko ilivyopangwa.

Asamoah Gyan bado alia na Yattara

http://img.modernghana.com/images/content/bgwi04lyx6_asamoahgyan580.jpg
Asamoah Gyan
NAHODHA wa kikosi cha timu ya taifa ya Ghana, Asamoah Gyan ambay anajiandaa kushuka dimbani kuiongoza timu yake katika mechi ya Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika dhidi ya Ivory Coast, amedai hatomsamehe golikipa wa Guinea Naby Yattara kutokana na faulo aliyomchezea timu zao zilipokutana.
Golikipa huyo alimkanyaga Gyan kwa teke la tumboni katika dakika za mwisho za mchezo wa robo fainali uliokutanisha timu hizo.
Yattara alilimwa kadi nyekundu lakini hajapewa adhabu yeyote nyingine mpaka sasa kiasi cha Gyan katika mahojiano yake alisema bado analitaka Shirikisho la Soka la Afrika(CAF) kumtwanga adhabu Yattara kwa sababu anadhani alidhamiria kufanya tukio lile.
Gyan aliendelea kudai kuwa ilikuwa ni faulo mbaya ambayo ingeweza kumsababisha asicheze tena soka ndio maana hataki kumsamehe kwa hilo.
Hata hivyo kipa huyo alinukuliwa juzi akisema kuwa hawezi kumuomba radhi Gyan kwa sababu hakukusudia kumuumiza na kusisitiza kuwa hilo ni tukio la bahati mbaya katika harakati za mchezo.

YANGA YALIPA KISASI, NGASSA AKIONDOA 'GUNDU'

http://shaffihdauda.co.tz/wp-content/uploads/2015/02/NGASSA-MRISHO.jpg
Mrisho Ngassa aliyefunga mabao yote mawili Yanga ikiizamisha Mtibwa uwanja wa Taifa
MABAO mawili ya winga machachari Mrisho Ngassa aliyetokea benchi yameiwezesha Yanga kulipa kisasi kwa Mtibwa Sugar na kurejea kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.
Yanga ambayo awali ilionekana kuugaya mchezo huo uliochezwa kwenye uwanja wa Taifa, ulishuhudiwa dakika 45 za kwanza mambo yakiwa magumu kwa klabu zote baada ya kutofungana bao lolote.
Hata hivyo mabadiliko yaliyofanywa na kocha Hans van der Pluijm ya kumtoa Kpah Sherman na kumuingiza Mrisho Ngassa yalizaa matunda baada ya mkali huyo kufunga mabao hayo muda mchache tangu awepo uwanjani na kuifanya Yanga kurudi katika nafasi ya kwanza.
Yanga imefanikiwa kufikisha pointyi 25 baada ya mechi 13 na kuiengua Azam ambao jana walilazimishwa sare ya 2-2 na Polisi Morogoro ikiwa na pointi 22 baada ya kucheza mechi 12.
Azam inatarajiwa kushuka dimbani siku ya Jumatano kwa ajili ya kucheza na Mtibwa Sugar katika mechi ya kiporo itakayochezwa uwanja wa Chamazi.
Magoli hayo mawili yamemwezesha Ngassa kuondoa 'gundu' baada ya kutoweza kufunga bao lolote msimu huu, kitu ambacho hakikuwa cha kawaida kwa mchezaji huypo aliyewahi kuwa Mfungaji Bora.
Wakati Azam wakiingia kambini kujiandaa na pambano lao na Mtibwa, Yanga wanatarajiwa kuelekea visiwani Zanzibar ili kuweka kambi kusubiri  mchezo wao wa Kombe la Shirikisho utajkaocheza Jumamosi.
Yanga itashuka dimbani Jumamosi kuumana na BDF XI ya Botswana katika mechi ya mkondo wa kwanza wa raundi ya kwanza ya michuano hiyo kabla ya kurudiana nao wiki mbil baadaye.
MSIMAMO LIGI KUU TANZANIA BARA 2014-2015
                              P   W   D    L    F    A   GD   Pts
01.  Yanga              13  07  04  02  15   07  08  25
02.  Azam               12  06  04  02  17   10  07   22
03. Polisi Moro         14  04  07  03  12   11  01  19
04. JKT Ruvu           14  05  04  05  14   14  00  19
05. Ruvu Shooting   14  05  04  05   10  11   -1  19
06. Mtibwa Sugar     12  04  06  02   13  09  04  18
07. Coastal Union     14  04  06  04  11   10  01  18
08. Kagera Sugar      14 04  06  04   11   11  00  18
09. Simba                 13  03  08  02  13   11  02  17
10. Mbeya City          13   04  04  05  09  11   -2  16
11. Ndanda Fc           14  04  03   07  13  18   -5  15
12. Mgambo JKT        12  04  02  06   06  11   -5  14
13. Stand Utd            14  02  06   06   09  17   -8  12
14. Prisons                13  01  08   04   10   12   -2  11
 

Wafungaji:
7-
Didier Kavumbagu(Azam)
6- Samuel Kamuntu (JKT Ruvu), Rashida Mandawa (Kagera Sugar)
5-
Ame Ali (Mtibwa), Danny Mrwanda (Yanga)
4-
Rama Salim (Coastal),  Simon Msuva (Yanga),  Emmanuel Okwi (Simba), Nassor Kapama (Ndanda)
3- Ally Shomari (Mtibwa),  Jacob Massawe (Ndanda), Kipre tchetche (Azam)
2-
Shaaban Kisiga, Dan Sserunkuma(Simba),  Salum Kanoni, Atupele Green (Kagera Sugar) Aggrey Morris (Azam),  Najim Magulu, Jabir Aziz (JKT Ruvu), Amissi Tambwe, Jerry Tegete, Mrisho Ngassa (Yanga), Ibrahim Kihaka (Prisons), Mussa Mgosi (Mtibwa), Heri Mohammed, Mussa Said (Stand Utd), Ally Nassor,  Malimi Busungu (Mgambo), Nicolaus Kabipe (Polisi),Yahya Tumbo (Ruvu Shooting)

Yanga kulipa kisasi kwa Mtibwa leo Taifa?!

Wakata Miwa wa Manungu, Mtibwa Sugar
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjD1DkH-KANYfSP-lMJIrFLhkzjqB0KhC2HRInBtLOg-GaupvdQqEA5_bgI-mH-UIyzUAItfzKFQQrOWcqfRRa8UBWoaXdQk1K7ESNnytqX3XOT2wNo7RpSWAvXOYRRhw10rgajuMQIjnnn/s1600/IMG_6036.JPG
Kikosi cha Yanga kitatoka vipi leo Taifa?
BAADA ya ombi lao la kutaka mechi yao dhidi ya Mtibwa Sugar kuahirishwa kugonga mwamba kwa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Yanga leo watashuka dimba la Taifa kwa nia ya kulipa kisasi cha mabao 2-0 walichopewa na wapinzani wao kwenye mechi ya mkondo wa kwanza.
Yanga ilikumbana na kipigo hicho katika mechi ya ufunguzi wa ligi hiyo kwenye uwanja wa Jamhuri Morogoro na iliiomba TFF iwaahirishie mechi yao ili kutoa nafasi ya kujiandaa vizuri kwa mchezo wao wa Kombe la Shirikisho dhidi ya BDF XI ya Botswana siku ya Jumamosi ijayo.
TFF imewachomolea na kuwataka washuke dimbani leo na kuwa na muda wa wiki moja ya kuvaana na wageni wao watakaowafuata Alhamisi wiki hii kwa ajili ya mchezo huo wa Jumamosi.
Ikiwa imetoka kupata ushindi mwembamba wa bao 1-0 uliovunja mwiko wa kushindwa kushinda katika uwanja wa Mkwakwani kwa karibu misimu miwili sasa, Yanga itawashukia Mtibwa Sugar kama mwewe kutokana na hasira za 'kubaniwa' na TFF.
Hata hivyo Yanga isitarajie mteremko kwani wapinzani wao, kwani msimu huu timu hiyo imeonekana kuimarika zaidi kuliko misimu miwili iliyopita na isingependa kulala tena jijini Dar kama ilivyokuwa katika msimu uliopita walipochapwa mabao 2-0.
Ikiwa chini ya nahodha wa zamani wa Taifa Stars, Mecky Mexime, Mtibwa ilikaa muda mrefu kileleni kabla ya kuteleza baada ya kuruhusu kipigo chake cha kwanza toka kwa maafande wa Ruvu  Shooting na leo ingependa kupata ushindi ili kujirejesha nafasi za juu.
Mtibwa Sugar imeporomoka toka nafasi ya tatu hadi ya sita ikiwa na pointi 18 wakati watani zao wapo nafasi ya pili baada ya Azam kuwaporomosha kufuatia sare ya mabao 2-2 iliyoapa mjini Morogoro dhidi ya Polisi Moro.
Kocha Mexime waliolazimishwa suluhu ya 0-0 na Coastal Union katika mechi yao ya mwisho, alisisitiza kuwa lengo lao ni kuona wanamaliza katika nafasi mbili za juu na hivyo wamerekebisha makosa yaliyowafanya washindwe kupata ushindi katika mechi  nne zilizopita za ligi hiyo.
Timu hiyo katika mechi hizo iliambulia sare tatu na kipigo kimoja na kuwwafanya waporomoke kileleni waliokoongoza kwa muda mrefu tangu kuanza kwa msimu huu.
Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano wa Yanga, Jerry Muro alisema kikosi chao kipo tayari kwa vita ya leo ili kuweza kuendeleza ubabe wao na kujiweka katika mazingira mazuri ya kuchukua ubingwa baada ya kurejea kileleni.
Muro alisema Yanga itawakosa baadhi ya nyota wake ambao ni majeruhi, lakini bado wachezaji waliosalia wataiongoza timu hiyo kulipa kisasi cha mabao 2-0 ilichopewa mjini Morogoro katika mechi ya mkodno wa kwanza kabla ya kuingia kambini kuwasubiri BDF XI ya Botswana kwenye mchezo wa kimataifa.

Man Utd, West Ham vita kali England

http://www.whufc.com/javaImages/86/a4/0,,~11445382,00.jpg

KLABU ya Manchester United ikiwa na furaha ya kufuzu Raundi ya Tano ya Kombe la FA, leo watakuwa dimba la ugenini kupepeta na West Ham Utd katika moja ya michezo minne ya Ligi Kuu ya England.
Vijana wa Luis Van Gaal, wanaifuata Wagonga Nyundo wa London wakitoka kuitoa nishai Cambridge United walionekana kutaka kuwatoa nishai kama vigogo vingine vilivyofanyiwa kwenye michuano hiyo ya FA.
Mashetani Wekundu waliichapa timu hiyo ya Daraja la Pili mabao 3-0 baada ya mechi ya kwanza wiki iliyopita kuisha kwa suluhu ya 0-0, hivyo watatua uwanja wa Boleyn Ground kwa nia ya kuendeleza furaha yao.
Wakiwa na kumbukumbu ya kushinda katika mechi ya kwanza msimu huu dhidi ya wapinzani wao ambao kwa misimu mitatu sasa hajaonja ushindi mbele ya Mashetani Wekundu, Manchester isitarajie mteremko.
West Ham wamekuwa na msimu mzuri safari hii wakishinda mechi 10 kati ya 23 walizocheza wakikamata nafasi ya nane na pointi zao 36,  saba pungufu na ilizonazo Man Utd waliopo nafasi ya tatu katika msimamo.
Mbali na mechi hiyo pia katika ligi hiyo leo kutakuwa na michezo mingine miwili wa mapoema ukizikutanisha timu za Burnley dhidi ya West Bromwich kabla ya Newcastle United kukikaribisha Stoke City.

NI GHANA AU IVORY COAST LEO

* Zinakutana katika fainali ya kisasi

http://www.ghanatoghana.com/wp-content/uploads/2015/01/Ghana-black-stars-players-group-picture.jpg
Ghana Black Stars
https://nbcprosoccertalk.files.wordpress.com/2013/11/ivory-coast-oct.jpg
Kikosi cha Ivory Coast
MALABO, Guinea ya Ikweta
AFRIKA inatarajiwa kufahamu Bingwa Mpya wa soka wakati Ivory Coast na Ghana zitakapoumana kwenye mchezo wa fainali za michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika 2015.
Pambano hilo litakalopigwa kwenye uwanja wa Estadio de Bata, linakumbushia fainali za mwaka 1992 wakati Tembo wa Afrika, Ivory Coast na Black Stars ya Ghana zilipokutana nchini Senegal.
Katika fainali hiyo ya aina yake, Ivory Coast waliwazidi kete wapinzani wao hao na kutwaa taji hilo kwa mikwaju ya penati 11-10 baada ya kumaliza dakika 120 milango ya timu zote ikiwa migumu.
Ivory Coast wamefuzu hatua hiyo baada ya kuing'oa timu ya DR Congo kwa kuwachapa mabao 3-1 katika mechi ya nusu fainali iliyochezwa Jumatano, huku kocha wake Herve Renald 'akizuga; kuwa walipenya kibahati kutokana na timu yake kucheza ovyo.
Wenyewe Ghana walifanikiwa kuwatoa wenyeji Guinea ya Ikweta kwa kuwabangua mabao 3-0 katika mechi iliyojaa vurugu za mashabiki waliokuwa wakishinikiza mwamuzi 'kuwabeba' tena kama ilivyokuwa katika mechi ya robo fainali dhidi ya Tunisia iliyomponza refa wa Mauritius kufungiwa.
Wenyeji hao walitarajiwa jana kuvaana na DR Congo kwa ajili ya kuwania nafasi ya mshindi wa tatu na nne wa fainali hizo za 30 ambazo zilianza kutimua vumbi lake tangu Januari 17.
Mchezo huo wa fainali unasubiriwa kwa hamu kutokana na umahiri wa vikosi vya timu hizo za Afrika Magharibi na washiriki wa Fainali zilizopita za Kombe la Dunia zilizofanyika nchini Brazili.
Tembo wa Afrika wanajivunia kikosi kinachoundwa na nahodha wake Yaya Toure ambaye ndiye Mchezaji Bora wa Afrika, sambamba na mwanasoka ghali wa Afrika, Wilfried Bony na wakali wengine.
Wakati wapinzani wao wanatambia nahodha wake, Asamoah Gyan,  Andre Ayew na nduguye Jordan Ayew, Kwame Appiah na wengine wanaochezaji soka la kulipwa katika klabu mbalimbali za Ulaya.
Kikosi cha Ghana kinachonolewa na kocha wa zamani wa Chelsea,  Avram Grant ambaye atakuwa akitaka kuwapa waajiri wake taji la tano  baada ya kulikosa kwa muda mrefu tangu walipotwaa mara ya mwisho mwaka 1982 na kulikosa kwenye fainali za mwaka 2010 mbele ya Misri.
Ivory Coast wenyewe watakuwa wakisaka taji la pili la michuano hiyo baada ya fainali za mwaka 2012 zilizofanyika nchini Guinea ya Ikweta ikishirikiana na Gabon kulikosa kwa kufungwa na Zambia.
Cha kuvutia ni kwamba kocha aliyewapa taji Zambia mwaka huo, Herve Renald ndiye anayeinoa timu hiyo kwa sasa na kama timu yake itashinda leo ataweka rekodi ya aina yake Afrika ya kuw kocha wa kwanza kuchukua taji hilo akiwa na nchi mbili tofauti.
Je ni Tembo wa Afrika au Nyota Weusi watakaoibuka na ushindi katika mchezo huo wa leo? Tusubiri tuone baada ya kumalizika wa fainali hizo zilizohamishiwa Guinea ya Ikweta baada ya waliokuwa wenyeji wa awali Morocco kuchomoa kwa kisingizio cha hofu ya ugonjwa wa Ebola.
Kitendo hicho kimesababisha nchi hiyo ya Morocco kuadhibiwa kwa kufungiwa fainali mbili za Afrika za 2017 na 2019.

Mchujo wa mabondia wa All African Games kuanza kesho

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgKf3j_9lbtaLQyaz_zQF0flGoPDNwRHy3gQ4ONfElr_vig3q8o4Qz8FPYmcPqZ0gMZDYrQgTaoGCdBXuRzDb3SOhXV60xTZTtAozbghUpubPSY0R6H4oYZPX0-B6AMkqUQhs2jWXY7oUw/s1600/antony.JPG
Mchujo kama huu unatarajiwa kuanza kesho Uwanja wa Ndani wa Taifa
http://www.thisday.co.tz/media/picture/large/BFTsecretary%20genera%20Makore%20Mashaga1.jpg
Katibu Mkuu wa BFT, Makore Mashaga
MCHUJO wa kusaka mabondia wa kuingia kambini kwa ajili ya ushiriki wa michuano ya Michezo ya Afrika (All African Games) unatarajiwa kuanza kesho jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa BFT, Makore Mashaga alisema mashindano ya mchujo huo utafanyika kwenye Uwanja wa Ndani ya Taifa na utamalizika Siku ya Wapendanao Februari 14.
Mashaga alisema mashindano hayo maalum yatashirikisha walifanya vizuri katika mashindano ya wazi ya taifa yaliyofanyika hivi karibuni katika Uwanja wa Taifa.
"Mashindano maalum kwa ajili ya kusaka mabondia watakaotuwakilisha kwenye michezo ya Afrika yataanza Februari 9-14 Uwanja wa Ndani wa Taifa na utashirikisha waliofanye vema kwenye michuano ya wazi," alisema.
Kwa mujibu wa Mashanga mabondia 39 watachujana ili kupatikana 15 ili kuunda timu ya taifa ya mchezo huo wa ngumi.
Mashindano hao ya Mataifa ya Afrika yanatarajiwa kutimua vumbi lake kati ya Septemba 4-19 mjini Brazzaville, Congo na Tanzania ni miongoni mwa nchi shiriki.

Saturday, February 7, 2015

Ngoma mpya ya AT-Sijazoea isikilize

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjehOkmJRxMxdVCIy6FjKjZXft65LgwAa2VvK1EW5G5Zc-IjB4jnAEfzogfhC9Xqw9qsHU2nWAxMY-6ZNbQDHCsjDQT_Nsbs4h2IPKNHVXD0GEbFUvQR-3UTk9POsZ2tAUGhNEsQrTYkqTr/s1600/DSC_1141.JPG
Msanii AT akiwa jukwaani
 

Everton, Liverpool hakuna mbabe, zashindwa kutambiana

Utemi na kutunishiana kifua ulikuwapo katika pambano hilo
Raheem Sterling akichuana na Aaron Lennon
Nahodha Steven Gerrard akijaribu kufunga mbele ya lango la Everton bila mafanikio
WAPINZANI wa jadi wa Merseyside, Everton na Liverpool zimeshindwa kutambiana baada ya kutoka suluhu katika pambano kali lililomalizika hivi punde.
Licha ya kushambuliana kwa zamu na kuwepo kwa kosa kosa za hapa na pale katika pambano hilo lililochezwa kwenye uwanja wa nyumbani wa Everton wa Goodison timu hizo zilimaliza dakika 90 zikiwa 0-0 na kugawana pointi moja moja.
Katika pambano hilo Liverpool ilipata pigo mapema baada ya kiungo wak Lucas Leiva kuumia katika dakika ya 15 na nafasi yake kuchukuliwa na Joe Allen, huku Aaron Lennon akishuhudiwa akishuka dimbani kwa mara ya kwanza akiwa na jezi za Everton akitokea Spurs.

Torino yashinda ugenini, Juve, Milan hapatoshi!

http://www1.pictures.zimbio.com/gi/Amauri+Torino+FC+v+Hellas+Verona+FC+Serie+ysKatQlJvdhl.jpgTORINO ikiwa uwanja wa ugenini hivi punde katika Ligi Kuu ya Italia, Serie A, imetoa kipigo kwa wenyeji wao Hellas Verona kwa kuikandika mabao 3-1.
Mabao ya Joseph Martinez katika dakika ya 32 , Fabio Quagliarella kwa mkwaju wa penati dakika ya 50 na bao la dakika 80 kupitia kwa El Kaddouri huku bao la kufutia machozi likifungwa na Luca Toni dakika ya 83.
Muda mchache ujao watetezi Juventus watakuwa uwanja wa nyumbani mjini Turin kuvaana na AC Milan katika pambano la kukata na shoka la ligi hiyo ya Italia.

Cannavaro aomba radhi askari aliyemkumbatia Mkwakwani

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjxAIpa7UbxBV97dfQaSq7VvymKFT0dmquJG4f0lMOxJ7fU0RIzZedDeit-mM7Bu8QPd8wzWN76JNlQdC_HpYL4z2uHLCM0GNqNKsAu5xnqbzInGCMFZ_B6x7Hn-nqeDH8_3MDJ1JufboLP/s1600/CANNA.tif
Nadir Haroub 'Cannavaro'
NAHODHA wa klabu ya Yanga na mfungaji wa bao pekee la Yanga wakati wanaizamisha Coastal Union nyumbani Mkwakwani Tanga, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, amemuomba radhi askari aliyemkimbilia na kumkumbatia dakika chache baada ya kufunga.
Cannavaro alifunga bao hilo katika dakika ya 11, Jumatano iliyopita na kufanya kitendo hicho ambacho kilikuwa gumzo.
Cannavaro alisema alimuomba askari huyo msamaha muda mfupi baada ya mechi hiyo ambapo aliamua kumfuata na kumueleza kuwa hakuwa na nia mbaya.
Cannavaro alisema anamshukuru askari huyo kwa kukubali maombi yake ya msamaha aliyoyatoa kwani hakutarajia hali hiyo kutokea kutokana na furaha aliyoipata baada ya kufunga bao hilo.
“Kiukweli nilifanya kosa kukimbia na kwenda kumkumbatia askari wakati nashangilia bao nililolifunga, nilijikuta ghafla nafanya kitendo kile bila kutarajia, sikukitarajia kabisa wala sikupanga iwe hivyo.

“Baada ya mechi kumalizika nilimfuata nikazungumza naye, pia walikuwepo baadhi ya viongozi wangu na wale wa polisi niliwaomba radhi kwa kitendo hicho nilichokifanya, nikashukuru wakanielewa na kulimaliza tatizo hilo,” alisema Cannavaro. 
Saleh Jembe

Bayern Munich, Dortmund zazinduka Bundesliga

David Alaba scores a free-kick for Bayern Munich's second goal against Stuttgart
David Alaba akishangilia bao lake
BAADA ya kuyumba katika mechi zao mbili zilizopita za Bundesliga, Bayern Munich leo imezinduka wakiwa ugenini baada ya kuicharaza Stuttgart kwa mabao 2-0 na kujiimarisha kileleni, lichja ya wapinzani wao wa karibu Wolfsburg wakipata ushindi wa mabao 3-0 nyumbani dhidi ya Hoffenheim.
Arjen Robbin alifunga bao la kuongoza dakika ya 41 kabla ya David Alaba kuongeza la pili dakika ya 51 na kuwafanya Bayern kufikisha pointi 49 na kujichimbia kileleni.
Wapinzani wao Wolfsburg wanawapumulia Bayern baada ya kupata ushindi mnono nyumbani wa mabao 3-0 dhidi ya Hoffeinheim.
Mabingwa wa zamani wa ligi hiyo Borussia Dortmund walizinduka katika hali mbaya waliyonayo baada ya kupata ushindi wa mabao 3-0 ugeninmi dhidi ya Freiburg, ilhali Mainz 05 ilikubali kipigo cha mabao 2-0 nyumbani dhidi ya Hertha Berlin, na timu za Fc Koln na Paderborn zilishindwa kutambiana baada ya kutoka suluhu na hivi sasa  Hamburger SV ipo mbele kwa mabao 2-0 dhidi ya Hannover 96.

DR Congo watwaa nafasi ya 3 AFCON 2015

http://sport360.com/sites/default/files/styles/x644/public/article/462572530.jpg?itok=zFCD8UsM
DR Congo wakishangilia mechi yao ya robo fainali
TIMU ya soka ya DR Congo imefanikiwa kunyakua nafasi ya tatu ya Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika, baada ya kuwanyuka wenyeji Guinea ya Ikweta kwa mikwaju ya penati 4-2 baada ya kumaliza dakika 90 bila kufungana katika mchezo uliochezwa kwenye uwanja wa Nuevo Estadio de Malabo.
Dakika 90 zilishuhudia timu hizo zikishindwa kufungana bao lolote licha ya kosa kosa za hapa na pale nas katika hatua hiyo ya penati wenyeji walipoteza mikwaju miwili ikiwamo nyota wapo Javier Balboa.
DRC walipata penati nne zilizotumbukizwa kimiani na Cedric Mabwati, Lema Mabidi, Chancel Mbemba na  Cedric Mongongu, huku wapinzani wao wakipata penati mbili kupitia kwa Juvenal na Doualla huku Raul Fabiani akifuata nyayo za Balboa.
Kesho ndiyo kesho kwa wanaume wa shoka Ivory Coast na Ghana zitaumana kwenye pambano la Fainali la michuano hiyo litakalochezwa kwenye uwanja wa Estadio de Bata, ikiwa ni mechi ya kisasi kinachorudisha nyuma kumbukumbu ya fainali kama hizo zilizochezwa mwaka 1992.
Katika pambano hilo Ivory Coast iliweka rekodi kwa kuitandika Ghana mabao 11-10 ya mikwaju ya penati baada ya kumaliza dakika 120 bila kufungana, huku timu hiyo ikicheza fainali hizo mwanzo hadi mwisho bila kuruhusu bao lolote katika muda wa kawaida hadi walipotwaa taji mbele ya Ghana.

Prisons yazidi kutaabika, Kagera Sugar yapumua!

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEizcnJ7pJWKJePJhfNmkOr2yBu9fwMkWd7cQe_UETGS3trCWrp-L1l0ibmEWED5gAINsVyz2e9dpQYp5uzBLpCrAH6CPsURTaDxnO43DnahnVVJ-Gur7-j8GB0wRkX-XJHOJQEYZT3o6LbV/s1600/Prisons+Mbeya.JPG
Prisons-Mbeya wanaoburuza mkia
http://shaffihdauda.co.tz/wp-content/uploads/2015/01/10906246_612237655589282_1427524500915532943_n.jpg
Mbeya City waliong'ang'aniwa na JKT Ruvu leo Chamazi
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj_eQMj86MgOTPURUKvU3Dq8WL93GXLLAyYIfSKEVSZCrfBBOYSGRDplhH7mSEXZHwaGtzaQ5RQ-qVr8IRmZV5D7g6EdaUe7ovZEm_AqGOFvKfpK6dEL5FeGNS7nRfeSXHXTd8uX9gtuuk/s1600/IMG_5633.JPG
Kagera Sugar angalau sasa wanapumua baada ya kuondoa gundu Kambarage-Shinyanga

KAGERA Sugar ambayo tangu ihame dimba lake la Kaitaba ilikuwa haijaonja ushindi zaidi ya kupokea vip[igo katika uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza na kuamua kukimbilia Kambarage, Shinyanga.
Katika pambano lao la kwanza kwenye uwanja huo mpya Kagera iliondoa gundu kwa kuichakaza Mgambo JKT kwa kuilaza bao 1-0.
Bao pekee la pambano hilo liliwekwa kimiani na Atupele Green dakika ya 50 kwa kichwa akiunganisha krosi pasi ya Daud Jumanne na kuwapa ushindi wa kwanza unaowapeleka hadi kwenye nafasi ya nane wakiizidi Simba wanaokamata nafasi ya 9, huku kipigi cha Mgambo kimewashusha hadi nafasi 12.
Maafande wa Prisons bado wapo mkiani wakiwa na pointi 11 baada ya mechi 13.

MSIMAMO LIGI KUU TANZANIA BARA:
                            P   W    D    L    F   A   GD  Pts
01. Azam             12  06   04   02  17  10  07   22
02. Yanga            12  06   04   02  13   07  06  22
03. Polisi Moro     14  04   07   03  12   11  01  19
04. JKT Ruvu       14  05   04   05  14   14  00  19
05. Ruvu Sh'ting  14  05   04   05  10   11   -1  19
06. Mtibwa Sugar 11  04   06   01  13   07  06  18
07. Coastal Union 14  04   06   04  11   10  01  18
08.
Kagera Sugar 14  04   06   04  11   11  00  18 
09. Simba            13  03   08   02  13   11  02  17
10. Mbeya City     13  04   04   05  09   11  -2   16
11.
Ndanda Fc      14  04  03   07  13    18  -5  15
12. Mgambo JKT   12  04  02  06   06    11  -5  14
13. Stand Utd       14  02  06   06   09   17  -8  12
14. Prisons           13  01  08   04   10   12  -2   11
Wafungaji:

7- Didier Kavumbagu(Azam)
6- Samuel Kamuntu (JKT Ruvu), Rashida Mandawa (Kagera Sugar)
5- Ame Ali (Mtibwa), Danny Mrwanda (Yanga)
4-
Rama Salim (Coastal),  Simon Msuva (Yanga),  Emmanuel Okwi (Simba),Nassor Kapama (Ndanda)
3- Ally Shomari (Mtibwa),  Jacob Massawe (Ndanda), Kipre tchetche (Azam)

Real Madrid na Ronaldo wao wazamishwa 4-0

Saul Niguez doubles Atletico's lead with a superb overhead kick just four minuted after the first goal 
Saul Niguez akifunga bao la pili la Atletico kwa tiktak
Mario Mandzukic akifunga bao la nne la Atletico Madrid
Cristiano Ronaldo looks dejected after Real Madrid concede two goals inside the opening 20 minutes of the game 
Kachokaaa! Ronaldo akiwa hoi timu yake ikitunguliwa ugenini
Former Bayern Munich midfielder Toni Kroos controls the ball while his old team-mate Mario Mandzukic closes him down 
Licha ya juhudi Real Madrid haikufua dafu kwa wapinzani wao wa jadi
MABINGWA wa Ulaya, Real Madrid licha ya kuwa na nahodha wake Cristiano Ronaldo wamepokea kipigo cha aibu cha mabao 4-0 toka kwa wapinzani wao wa jadi, Atletico Madrid katika pambano la La Liga lililochezwa kwenye uwanja wa Vincente Calderon.
Atletico ambao ndiyo watetezi la La Liga walianza kuwaadabisha wapinzani wao kwa kuandika bao la kwanza katika dakika ya 14 kupitia kwa Tiago kabla ya Saul Niguez kuongeza la pili dakika nne baadaye.
Mabao mengine yaliyendeleza ubabe wa Atletico Madrid dhidi ya wapinzani wao yalifungwa na Antoine Griezmann kwa shuti kali dakika ya 67kabla ya Mario Mandzukic kumalizia udhia kwa kufunga kwa kichwa dakika ya 89.Ligi hiyo itaendelea tena kwa michezo mingine mitatu ambapo hivi punde Villarreal ikiwa nyumbani imepata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Granada.


Arsenal yafa kwa Spurs, Man City yabanwa Itihad

Tottenham striker Harry Kane
Harry Kane aliyewaangamiza Arsenal leo
Harry Kane scores his first goal against Arsenal
Harry Kane akifunga bao la pili na la ushindi la  Spurs
Chelsea
Hazard na wachezaji wenzake wakishangilia bao la kwanza la Chelsea
Aston Villa
Jores Okore wa Aston Villa akishangilia bao la kufutia machozi la timu yake
James Milner scores Man City's equaliser against Hull
James Milner akiisawazishia Manchester CIty waliokuwa wakielekea kuzama nyumbani mbele ya Hull City leo
WAKATI Arsenal wakiduwazwa ugenini kwa kucharazwa mabao 2-1 na wapinzani wao wa jadi wa London ya Kaskazini, Tottenham Hotspur, mabingwa watetezi Manchester City imeng'ang'aniwa nyumbani  na Hull City na kutpoka sare ya 1-1, huku Chelsea ikizidi kujichimbia kileleni kwa kuilaza Asron Villa mabao 2-1.
Arsenal ikienda kwenye uwanja wa White Hart Lane wakiwa na kumbukumbu ya kupata ushindi mnono wa mabao 5-0 dhidi ya Aston Villa walitangulia kupata bao dakika ya 11 kupitia Mesut Ozil bao lililodumu hadi wakati wa mapumziko.
Wenyeji walirejea kipindi cha pili na hasira na kufanikiwa kuyarejesha mabao hayo kupitia kwa kinda linalotisha kwa sasa England, Harry Kane aliyefunga katika dakika ya 56 na 86 na kuipa ushindi muhimu Vijogoo vya London na kufikisha pointu 43 na kuingia kwenye Nne Bora wakiishusha Arsenal.
Katika mechi nyingine za ligi hiyo Mabingwa watetezi walilazimishwa sare ya 1-1 na Hull City, huku Chelsea wakishinda mabao 2-1 ugenini dhidi ya timu isiyofunga mabao ya Aston Villa,.
Mechi nyingine Southampton ikiwa ugenini ilipata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya QPR,  Swansea City ililazimishwa sare ya 1-1 na Sunderland, huku Leicester City ilikubali kipigo cha bao 1-0 nyumbani dhidi ya Crystal Palace.
Hivi sasa Everton na wapinzani wao wa jadi wa Merseyside, Liverpool zinajiandaa kupepetana kwenye uwanja wa Goodson Park.