STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, April 24, 2014

Yohan Cabaye ajiandaa kutwaa taji la pili la Ligi Ufaransa

http://i.dailymail.co.uk/i/pix/2014/01/31/article-2549777-1B1CA23300000578-208_634x471.jpgKIUNGO Yohan Cabaye nyota wa mabingwa watetezi wa Ligi Kuu ya Ufaransa PSG, Yohan Cabaye anajiandaa kunyakua taji lake la pili la ligi hiyo iwapo timu yake hiyo itapata ushindi katika pambano lao dhidi ya Sochaux litakalochezwa Jumapili.
PSG imebakisha pointi tatu tu kutetea taji hilo baada ya jana kupata ushindi mwembamba dhidi ya Evian TG na kuzidi kuikimbia Monaco, wapinzani wao wa karibu waliopo nafasi ya pili na waliowaacha kwa pointi 10 huku ligi ikisaliwa na mechi nne kabla msimu haujafungwa.
Cabaye aliyesajiliwa kwenye usajili wa majira ya baridi akitokea Newcastle United ya Uingereza anasema atakuwa mwenye furaha iwapo PSG itatwaa taji hilo ambalo kwake itakuwa ni mara ya pili baada ya kunyakua mara ya kwanza mwaka 2011 akiwa na Lille.
Mkali huyo anayeichezea pia timu ya taifa ya Ufaransa, anasema angependa kuongeza medali nyingine ya dhahabu katika chumba chake kupitia PSG.
"Tuna hamu kubwa ya kupata mafanikio ya kunyakua taji hilo na kitu hicho ni muhimu sana kwangu," alisema Cabaye, 28 na kuongeza; "Itakuwa vyema kama nitanyakua ubingwa huo nikiwa na PSG."
Mwishoni mwa wiki Cabaye alifanikiwa kunyakua Kombe la Ligi wakati PSG ilipoicharaza Olympique Lyon mabao 2-1 kwa mabao la Edinson Cavani na kudai ingawa hajawahi kunyakua Kombe la Ligi au Kombe la Mfalme mara mbili, lakini katika ligi anaamini itafanikiwa na anajiandaa kushangilia furaha ya ushindi huo anaousubiri kwa hamu.

Sturridge arejea,, Chelsea ikipanga kupumzisha nyota wake

http://www3.pictures.zimbio.com/gi/Daniel+Sturridge+Liverpool+v+Fulham+Premier+HI6EojIbLKll.jpg
Daniel Sturridge
http://i.dailymail.co.uk/i/pix/2013/03/06/article-2288964-09591184000005DC-339_306x423.jpg
Kocha wa Chelsea Jose Mourinho
 WAKATI kocha Jose Mourinho akidaiwa kutaka kuwapumzisha wachezaji wake nyota wake katika pambano lao la Ligi Kuu dhidi ya Chelsea ili kuitafutia kasi Atletico Madrid katika mechi ya nusu fainali ya marudiano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, wapinzani wao Liverpool wanachekelea kurejea kwa Daniel Sturridge.
Sturridge anategemewa kurejea kutoka katika majeruhi katika mchezo huo wa Jumapili ambao watakwaana na Chelsea.
Nyota huyo wa kimataifa wa Uingereza mwenye miaka 24 alikuwa akilalamika maumivu ya msuli katika ushindi wa mabao 3-2 waliopata dhidi ya Manchester City Aprili 13 hivyo kupelekea kutolewa nje. 
Toka apate majeruhi hayo alikosa mechi moja lakini sasa anategemewa kurejea tena uwanjani kuisaidia Liverpool katika mchezo huo muhimu ambao kama wakishinda utawafanya kuendelea kujikita kileleni hivyo kuweka hai matumaini yao ya ubingwa wa Ligi Kuu. 
Sturridge amesema kwa sasa anajisikia vyema na ni mategemeo yake atakuwepo katika mchezo huo wa Jumapili lakini itategemea kama kocha Brendan Rodgers atamchagua.
Katika hatua nyingine, Kocha wa Chelsea, Jose Mourinho amesema anataka kuwapumzisha nyota wake kwa ajili ya safari kwenda Anfield kwa ajili ya mchezo wa Ligi Kuu dhidi ya Liverpool Jumapili ijayo. 
Chelsea bado wako katika kinyang’anyiro cha taji la ligi wakiwa wamebakiwa na michezo mitatu lakini Mourinho anataka kuhamishia nguvu zake katika mchezo wa marudiano wa nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Atletico Madrid. 
Katika mechi yao ya kwanza iliyochezwa juzi, Chelsea iling'ang'aniwa na wenyeji wao Atletico kwa kutoka suluhu.
Hata hivyo, kocha huyo amesema uamuzi huyo wa kuwapumzisha baadhi ya nyota wake unaweza usiwe wa kwake kuufanya kwa sababu anataka kusikiliza na mawazo ya wengine. 
Kipigo cha mabao 2-1 walichopata Chelsea kutoka kwa Sunderland mwishoni mwa wiki iliyopita kinamaanisha hata kama wakishinda mchezo wa Anfield inaweza isitoshe kuizuia Liverpool kushinda taji la ligi baada ya kupita miaka 24.
Liverpool inaoongoza msimamo wa ligi hiyo ikiwa na pointi 80, huku wapinzani wao waliopo nafasi ya pili wana pointi 75 moja zaidi ya ilizonazo Manchester City iliyo na mchezo mmoja zaidi ya timu hizo mbili za juu zilizocheza mechi 35.

Bomu jingine lalipuka Kenya

MATUKIO  ya kigaidi yamekua yakichukua vichwa vya habari mara nyingi nchini Kenya hasa baada ya nchi hiyo kupeleka wanajeshi wake nchini Somalia kupambana na wanamgambo wa kikundi cha kigaidi cha Al Shabaab.
Saa tatu na nusu usiku wa April 23 2014  bomu jingine limelipuka ndani ya gari karibu na kituo cha Polisi Nairobi.
Waziri wa mambo ya ndani amethibitisha kwa kusema Polisi wawili wamepoteza maisha kati ya watu wanne ambao wameuwawa huku hao wengine wawili wakihofiwa kuwa ni Mahabusu waliokuwemo kwenye gari hilo na Polisi.

Mhe Temba, Chegge Waueni sasa!

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj0xQoDnodEV9YYagUy0z9ZP5UpB52s4xbJjVzKwckA9t_5NJAr8AiEwl5VLg4SNI0Eai2GGsmoYGrWg7xq_-dy-LFWWRWtAzTTh_YVzi9J0tS628PHayncwU1-X7JWpIpqp6zF5OQ5/s1600/Temba+and+Chege.jpgNYOTA wa muziki wa kizazi kipya wanaotoka kundi la TMK Wanaume Family, Chegge na Mhe Temba wanatarajia kuachia hewani wimbo wao mpya uitwao 'Waue' waliowashirikisha 'membaz' wa Mkubwa wa Wanawe.
Wasanii walioshirikishwa na wakali hao ni Maromboso na YP ambao nao wanatokea 'ukoo' wa TMK Wanaume Family na Mkubwa na Wanae.
Mkurugenzi wa Mkubwa na Wanawe na Meneja wa wasanii hao, Said Fella 'Mkubwa' aliiambia MICHARAZO kuwa, wimbo huo utaachiwa 'audio' na video wiki mbili zijazo baada ya kukamilisha baadhi ya mambo.
Mkubwa, alisema wimbo huo umerekodiwa katika studio zao za Mkubwa na Wanae chini na mtayarishaji, Shirko na video imefanywa na Adam Juma kupitia kampuni yake ya Visual Lab.
"Wasanii Temba na Chegge wamekamilisha kurekodi 'audio' na video ya wimbo wao uitwao 'Waue' wallioimba na Maromboso na YP, na tunapanga kuachia kazi hizo kwa pamoja wiki ijayo," alisema.
Chegge na Mhe Temba wamekuwa wakitoa kazi za pamoja mbali na zile za binafsi za kila mmoja nje ya nyimbo za kundi lao la TMK Wanaume Family.

Mashauzi, Sikinde kuwasindikiza Talent Band

http://4.bp.blogspot.com/-O6fGijIG-Xg/TpazwGlqCXI/AAAAAAAAAIQ/RB1Z12Ke5k8/s320/Hussin+Jumbe
Hussein Jumbe 'Mtumishi'

http://api.ning.com/files/QB639EYNFoD4efIjz*tu6A-tokrUhXrM*zilTmqFjwPaPBf8MRFVKag*kDP98VUlJn2dEoatnVAzlwDEnsygi3UIFRYdWmh1/MITIKISIKOYAPWANIDARLIVE16.JPG?width=650
Ishi Mashauzi atakayemsindikiza Hussein Jumbe na Talent Band
KUNDI maarufu la muziki asilia la Ngoma Afrika na kundi la muziki wa taarab la Mashauzi Classic, yanatarajiwa kupamba uzinduzi wa albamu mpya ya Talent Band utakaofanyika wiki ijayo jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na MICHARAZO, Mkurugenzi wa Talent Band, Hussein Jumbe alisema kuwa uzinduzi huo utafanyika Aprili 30 kwenye ukumbi maarufu Kisuma Night Park lililopo eneo la Temeke Mwembeyanga na watasindikizwa na makundi hayo mawili.
Jumbe alisema pia bendi yake ya zamani ya Mlimani Park 'Wana Sikinde' watakuwepo ukumbini kumpiga tafu kwenye uzinduzi huo wa aina yake.
"Natarajia kufanya uzinduzi wa albamu ya bendi yetu ya Talent iitwayo 'Kiapo Mara Tatu' na makundi ya Mlimani Park, Mashauzi Classic na Ngoma Afrika watanisindikiza siku hiyo pale Mwembeyanga," alisema.
Jumbe alisema kuwa, maandalizi ya uzinduzi huo unaendelea vyema na kuwataka mashabiki wa muziki wa dansi kujitokeza kupata burudani ambayo wameikosa kwa muda mrefu jijini Dar es Salaam.

Arsenal yaingia mbio za kumwinda van Gaal

http://www.101greatgoals.com/wp-content/uploads/2014/04/Louis-Van-Gaal-Bayern-Mun-001.jpg
Kocha van Gaal
 KLABU ya Arsenal imedaiwa kufanya mawasiliano na kocha Louis van Gaal, anayetajwa kuchukua mikoba ya David Moyes aliyetimuliwa na klabu ya Manchester United juzi.
Duru za kispoti zinasema kuwa, Arsenal imelazimika kuwasiliana na Mholanzi huyo kutokana na kutokuwa na uhakika na mustakabaliwa wa kocha wake Arsene Wenger. 
Hata hivyo Arsenal bado ina matumaini kuwa Wenger atasaini mkataba mpya wa miaka miwili waliokubaliana Octoba mwaka jana, lakini inajulikana anaweza kujiuzulu kama akishindwa kufikia malengo aliyojiwekea baada ya kumalizika kwa msimu. 
Imebainika kuwa Mfaransa huyo aliwaambia marafiki zake kuwa anafikiria kuacha kuinoa Arsenal kama awatashinda Kombe la FA na kumaliza katika nafasi nne za juu kwenye msimamo wa Ligi Kuu. 
Kutokana na hali hiyo kumekuwa na mipango ya muda mfupi inayofanywa na Arsenal, mojawapo ni kujaribu kufanya mazungumzo na Van Gaal ambaye mkataba wake na timu ya taifa ya Uholanzi unamalizika baada ya Kombe la Dunia.
Mbali na kuwindwa na Arsenal, kocha huyo pia amekuwa akitajwa kunyemelewa na klabu za Manchester United na Tottenham Hotspurs ambao nao wanataka achukue nafasi ya Tim Sherwood mwishoni mwa msimu huu.
Kocha huyo mwente rekodi za kuvutia amekuwa akiwania kutokana na uwezo wake wa kuwaongoza na kuwadhibiti wachezaji hata wale wakorofi. 

Januzaj aichagua Ubelgiji

http://i.huffpost.com/gen/1235023/thumbs/o-ADNAN-JANUZAJ-570.jpg?6
Januzaj
WINGA chipukizi wa klabu ya Manchester United, Adnan Januzaj ameamua kuiwakilisha Ubelgiji katika michuano ya soka ya kimataifa. 
Kocha wa timu ya taifa ya Ubelgiji, Marc Wilmots ametangaza katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa twitter amefurahishwa na uamuzi uliochukuliwa na mchezaji huyo. 
Januzaj amezaliwa jijini Brussels akiwa na wazazi wenye asili ya Kosovo na Albania na kujiunga na United mwaka 2011. 
Chipukizi huyo mwenye umri wa miaka 19 alikuwa na nafasi ya kuzichezea nchi za Kosovo, Albania, Turkey, Serbia na hata Uingereza lakini sasa anaweza kuwemo katika kikosi cha Ubelgiji kitakachoshiriki Kombe la Dunia. 
Kikosi kamili cha wachezaji 30 wa Ubelgiji kinatarajiwa kutajwa Mei 13 mwaka huu.

Kocha mpya Stars kutua nchini Jumamosi

http://www.clubofmozambique.com/pt/sectionnews/data/entretenimento/mart_nooij.jpg
Huyu ndiye kocha mpya wa Taifa Stars

 KOCHA Mkuu mpya wa Taifa Stars, Martinus Ignatius Maria maarufu kama Mart Nooij anatarajiwa kuwasili nchini Jumamosi alfajiri (Aprili 26 mwaka huu) tayari kwa ajili ya kuanza kazi ya kuinoa timu hiyo.
Nooij (59) atawasili saa 7.20 usiku kwa ndege ya Ethiopia Airlines ambapo anatarajia kukutana na waandishi wa habari Jumamosi mchana, saa chache kabla ya kuanza mechi ya kirafiki kati ya Taifa Stars na Burundi itakayochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Mkenya kuzihukumu Stars na Intamba Murugamba

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjbouke40Ajpgip-WYtuNcSkslDTj7_vx1cW1lSk8TTr-VrfSpd48or2vfOoU95GSaeEPAw2h5x4McRiOOgSk6nbUS6SUXQKo3lzFQl3LThJA16UJsJRVH5TDtfBRQTKxdCPu8d59WboTi_/s400/waamuzi.jpg
Mwamuzi Ogwayo atakayezichezesha Stars na Intamba Murugamba
MWAMUZI Anthony Ogwayo mwenye beji ya Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) kutoka Kenya ndiye atakayechezesha mechi kati ya Tanzania (Taifa Stars) na Burundi (Intamba Mu Rugamba) itakayochezwa keshokutwa (Aprili 26 mwaka huu)  Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Ogwayo katika mechi hiyo ya maadhimisho ya miaka 50 ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar, atasaidiwa na Gilbert Cheruiyot na Oliver Odhiambo wote pia kutoka Kenya. Mwamuzi wa mezani atakuwa Israel Mujuni wa Tanzania.
Burundi inatarajia kuwasili nchini leo (Aprili 24 mwaka huu) saa 12 jioni kwa ndege ya Kenya Airways na itafanya mazoezi kesho (Aprili 25 mwaka huu) saa 10 jioni kwenye Uwanja wa Taifa.
Nayo Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager ipo kambini jijini Dar es Salaam kujiandaa kwa mechi hiyo ambayo itakuwa ya kwanza tangu kuanza kwa mpango wa maboresho wa timu hiyo.
Makocha wa timu zote mbili pamoja na manahodha wao kesho (Aprili 25 mwaka huu) saa 5 asubuhi kwenye ofisi za Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) watakuwa na mkutano na waandishi wa habari kuzungumzia mechi hiyo.
Viingilio katika mechi hiyo vitakuwa sh. 5,000 kwa viti vya rangi ya chungwa, bluu na kijani. Kwa VIP A kiingilio kitakuwa sh. 20,000 wakati VIP B na C ni sh. 10,000.

Zawadi za washindi Ligi Kuu Tanzania Bara zatangazwa

* Amissi Tambwe kuzoa Mil 5.2
* Azam kama bingwa kunyakua Mil 75
Mabingwa wapya wa Ligi Kuu Azam watakaozoa Mil 75
Tambwe wa Simba kajihakikishia Sh Mil 5.2
MSHAMBULIAJI Amisi Tambwe wa Simba atalamba Sh. milioni 5.2 za zawadi ya mfungaji bora zitakazotpolewa na wadhamini wakuu wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, kampuni ya huduma ya simu ya Vodacom Tanzania baada ya kuibuka mfungaji bora wa msimu wa 2013/14 wa ligi hiyo.

Aidha, timu yenye nidhamu italamba Sh. milioni 16 ikiwa ni ongezekon la Sh. milioni moja ikilinganishwa na ilivyokuwa msimu uliopita.

Hayo yamebainishwa na Ofisa Uhusiano wa Nje wa Vodacom Tanzania, Salum Mwalim katika mkutano na waandishi wa habari muda mfupi uliopita kwenye ofisi za Makao Makuu ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) zilizopo katikati ya Jiji la Dar es Salaam.

ZAWADI ZA WASHINDI LIGI KUU BARA 2013/2014
Bingwa: Sh. Milioni 75
Mfungaji Bora: Sh. Milioni 5.2
Timu yenye Nidhamu; Sh. Milioni 16
Kipa Bora: Sh. Milioni 5.2
Refa Bora; Sh. milioni 5.2
  Mwalim amesema mabingwa Azam FC watazawadiwa Sh. milioni 75 ikiwa ni ongezeko la Sh. milioni 5 ikilinganishwa na ilivyokuwa msimu uliopita.   Kipa bora, mwamuzi bora watapata Sh. milioni 5.2 kila mmoja ikikwa ni ongezeko la Sh. 200,000.Timu yenye nidhamu italamba Sh. milioni 16, ikiongezeka kutoka Sh. 15 ya msimu uliopita zilizochukuliwa na Yanga.   Silas Mwakibinga, Ofisa Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi Kuu (TPLB), aliyekuwa amefuatana na Mwalim kwenye mkutano huo na waandishi wa habari, alisema tarehe ya kutolewa kwa tuzo hizo itatangazwa baada ya wiki moja.

Kivumbi Europa League kutimka leo Juve yaifuata Benfica

Juve itavuna nini leo Ureno
KIVUMBI cha Nusu Fainali  ya Ligi Ndogo ya Ulaya (UEFA Europa League) kinatarajiwa kutimka usiku wa leo wakati timu nne zilizotinga hatua hiyozitakapopepetana kwenye viwaja viwili tofauti.
Klabu za Sevilla na Valencia zote kutokea Hispania zilizopangwa kucheza pamoja zitakutana kwa mara ya kwanza katika hatua hiyo, wakati mabingwa wa Italia Juventus watakwaruzana na Benfica ya Ureno katika mechi zinazotarajia kuwa na msisimko wa aina yake.
Valencia na Sevilla ambazo zilipindua matokeo yao ya awali walipolazwa ugenini na kushinda nyumbani kwa idadi kubwa ya mabao dhidi ya Porto na Basel zinakutana kwa mara ya kwanza kwenye michuano ya Ulaya.Mechi za mkondo wa kwanza baina ya timu hizo mbili itaanziua nyumbani kwa Sevilla kabla ya wiki ijayo kuwafuata wapinzani wao hao.
Timu zote mbili zimewahi kunyakua taji hilo kwa vipindi tofauti, Sevilla mara mbili mfululizo mwaka 2006 na 2007 na wenzao walitangulia mwaka 2004.
Juventus itakayokuwa ugenini ilishawahi kunyakua taji hilo mara tatu mwaka 1977, 1990 na 1993 na ingependa kufanya kweli katia michuano ya mwaka huu baada ya ndoto zao na kutamba Ligi ya Mabingwa Ulaya kukwama na kutolewa kwenye hatua ya 16 Bora.
Waitalia hao wanaoelekea kutetea taji lao la Seria watakutana na Benfica ambao hawajawahi kunyakua taji hilo la Europa, ingawa mkononi tayari wana taji la ligi kuu ya nchi yao ya Ureno.
Ikitamba na nyota wake kama Carlos Tevez, Andre Pirlo, Paul Pogba na wengine Juventus itahitaji ushindi ugenini ili mchi yao ya marudiano wilki ijayo iwe nyepesi ingawa watarajie kupata upinzani mkali kwa mabingwa hao wa Ureno inayotambia wakali wake kama Lima kutoka Brazil., Rodrigo, Cordozo, na Andre Gomes

Real Madrid yaizima Bayern Munich, ila kazi wanayo ugenini

Benzema (9) akishangiulia bao lake pekee lililoizamisha Bayern Munich
MABINGWA watetezi wa Ligi ya Mabingwa Ulaya, Bayern Munich imekubali kichapo cha bao 1-0 toka kwa wenyeji wao Real Madrid katika mechi ya mkondo wa kwanza ya Nusu fainali ya pili ya michuano hiyo iliyochezwa usiku wa kuamkia leo mjini Madrid -Hispania.
Baoa pekee la dakika ya 19 ya mchezo lililotumbukizwa kimiani na Karim Benzema lililitosha kuwapa wenyeji ushindi huo mwembamba kwenye uwanja wa Santiago Bernabeu.
Katika mchezo huo ilishuhudiwa wachezaji ghali wa klabu ya Real Madrid wanaodaiwa kuwa wagonjwa kupishana katika kipindi cha pili na kuwapa faraja vijana wa Carlo Ancelotte kupumua kabla ya wiki ijayo kurudiana na Wajerumani hao waliopoteza bafasi kadhaa za kufunga katika mechi hiyo.
Real Madfrid itakabiliwa na kazi nzito katika mchezo wa marudiano ili kulinda ushindi huo na kuvuta unyonge wa kutolewa mara katika hatua hiyo na wapinzani wao hao.

Wednesday, April 23, 2014

PSG yabakisha pointi tatu kutetea taji Ufaransa

MABINGWA watetezi wa Ligi ya Ufaransa (Ligue 1) PSG usiku huu imeibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Evian TG na kujiweka katika nafasi nzuri ya kutetea taji hilo ikibakisha pointi tatu
Bao pekee lililowekwa kimiani na Blaise Mataudi dakika moja kabla ya pambano hilo kwisha lilitosha kuwa ushindi muhimu kaioka pambano hilo lililoshuhudia wageni wa PSG wakicheza pungufu.
Beki Kassim Abdallah wa Evian alilimwa kadi ya njano ya pili dakika ya 61 na kusindikizwa na nyekundu na kuacha pengo kwa timu yake iliyoelekea kuikomalia wenyeji wao kabnla ya Mataudi kufunga bao hilo na kuifanya PSG kufikisha jumla ya pointi 82, 10 zaidi ya Monaco yenye 72.
Timu zote zimecheza michezo 34 na kukasaliwa na mechi nne kila moja kufungia msimu ambapo ushindi wa mechi moja kati ya hizo tatu utaipa nafasi PSG kutete taji hilo kwa mara ya pili mfululizo.
Katika mechi nyingine ya ligi hiyo iliyochezwa pia leo, Toulouse ikiwa nyumbani ililazimishwa suluhu ya 0-0 dhidi ya wageni wao Olympique Lyon

Azam kuacha nane, Kocha kutimka zake kesho

Kakolaki atakayesomea ukocha
MABINGWA wapya wa Ligi Kuu Tanzania, Azam imetangaza kuwa mbioni kuwaacha wachezaji nane waliokuwa kwenye kikosi cha timu hiyo.
Kwa mujibu wa Meneja wa klabu hiyo, Jemedari Said akinukuliwa na kupitia kipindi cha michezo cha Magic FM, wachezaji hao wamependekezwa na kocha mkuu wa timu hiyo, Joseph Omog katika ripoti yake aliyowasilisha kwa uongozi akijiandaa kutimkia kwao kwenye mapumziko mafupi.
Jemedari alisema miongoni mwa wachezaji hao nane waliopendekezwa kutemwa, wawili kati yao akiwemo mkongwe Luckson Kakolaki na majeruhi wa muda mrefu Sameer Haji Nuhu wao watapewa ofa za kusomeshwa ukocha na kupewa majukumu mengine katika brand za SSB.
"Kakolaki ambaye ni mmoja wa wachezaji wakongwe wa klabu hii atapelewa kusomea ukocha ili aje kuinoa timu ya vijana na Sameer anayesumbuliwa na majeraha ya muda mrefu, atapangiwa kazi nyingine katika makampuni baada ya wenyewe kuridhia na kuomba iwe hivyo," alisema Jemedari.
Meneja huyo alidokeza kuwa kocha wao amependekeza pia timu ianze kambi kwa msimu mpya wa ligi asubuhi ya Juni 16.

Burundi kutua nchini kesho kuifuata Stars

Burundi
TIMU ya Taifa ya Burundi 'Intamba Murugamba' inatarajiwa kuwasili nchini kesho (Aprili 24 mwaka huu) saa 12 jioni kwa ndege ya Kenya Airways tayari kwa mechi dhidi ya Taifa Stars itakayochezwa Jumamosi (Aprili 26 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Intamba Mu Rugamba itakuwa na msafara wa watu 28 wakiwemo wachezaji, benchi la ufundi na viongozi, na itafikia hoteli ya Accomondia. Mechi hiyo itachezwa kuanzia saa 10 jioni.
Nayo Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager ipo kambini kwenye hoteli ya Kunduchi Beach ikijiandaa kwa mechi hiyo itakayochezeshwa na waamuzi kutoka Kenya.
Viingilio katika mechi hiyo vitakuwa sh. 5,000 kwa viti vya rangi ya chungwa, bluu na kijani. Kwa VIP A kiingilio kitakuwa sh. 20,000 wakati VIP B na C ni sh. 10,000. Mechi hiyo ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 50 ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar

Chelsea, Atletico ngoma droo, leo ni Real, Bayern

KLABU ya Chelsea imejiweka katika nafasi nzuri ya kufuzu fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya baada ya usiku wa jana kulazimishwa sare isiyo na magoli ugenini dhidi na vinara wa La Liga, Atletico Madrid katika pambano la nusu fainali mkondo wa kwanza wa ligi hiyo.
Chelsea ambayo ilimpoteza kipa wake nyota Petr Cech dakika ya 17 baada ya kuumia na baadaye nahodha wake, John Terry pia kwa majeraha, kwa kutoka suluhu hiyo kwenye uwanja wa Vincente Calderon, itahitaji ushindi wowote nyumbani dhidi ya Atletico.
Katika mfululizo wa ligi hiyo usiku huu timu za Real Madrid na mabaingwa watetezi Bayern Munich zitapepetana leo katika mchezo mwingine wa nusu fainali pambano litakalochezwa kwenye uwanja wa Santiago Bernabeu, mjini Madrid nchini Hispania.
Pambano hilo linarejesha kumbukumbu ya mechi ya nusu fainali ya Ligi ya mabingwa ya mwaka 2012 ambapo Bayern iliiondosha Madrid kwa mikwaju ya penati na kwenda kufa mikononi  mwa Chelsea kwenye mchezo wa fainali.

Tuesday, April 22, 2014

Linex, Prof Jay kuwasindikiza Kalapina, Q.Chilla Maisha Club

Kalapina
NYOTA wa muziki wa kizazi kipya, Linex, Mapacha na Q Chillah ni baadhi ya watakaoshiriki kumsindikiza mkali wa Hip Hop nchini, Karama Masoud 'Kalapina' katika onyesho lake maalum.
Onyesho hilo linatarajiwa kufanyika April 27 Maisha Club, kwa lengo la kuwaenzi wale wote walioshiriki kwa namna moja au nyingine kutoa mchango wa kuisimamisha miondoko ya Hip Hop nchini.
Akizungumza na MICHARAZO, Kalapina alisema katika onyesho hilo ataimba 'live' wimbo wake mpya wa 'Hip Hop is Alive' alioimba na Q Chillah na kusindikizwa na mastaa kibao wa hip hop nchini.
Kalapina aliwataja baadhi ya wasanii hao ni pamoja na Prof Jay, Kimbunga, Linex, Mapacha, Q Chilla mwenyewe na Masharikanz.
"Yaani itakuwa burudani ya kipekee kwa mashabiki wa Hip Hop na muziki wa kizazi kipya kwa ujumla kwa namna onyesho hilo maalum litakavyokuwa wakishuhudia Hip Hop is Alive ukiimbwa live," alisema.
Kalapina alisema katika onyesho hilo watapiga pia nyimbo zake zote pamoja na Kikosi cha Mizinga ambazo zilisaidia kuamsha harakati za kijamii kupitia miondoko hiyo ya hip hop nchini.

Nani kuwa Kocha Bora 2013-2014?

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi-AHHPDGwpXoAhDL-i8HpX-pmC25TiA9fSclAHxGXB-QwTZ7iStXtw5TEAKYh4wrnLyJ8qIBLxi7tf09ZT7Tqb3t4NobyKE3Y1BuC1-WGEcAantKaqoxNk_ch228N3RBjqU-REA4ub2iPI/s1600/mwambusi+coach.jpg
Juma Mwambusi
http://api.ning.com/files/VMB94olbxS1KUXphY0U47D4laBLxC*CFhUlgLRS9F0nyaxUKrUNPfsr0M0JTm2GFIFYUVc9GC7kbzapFvqrS-DcuQ0M-I6aJ/PLUIJMKITAMBI.jpg
Hans Van der Pluijm

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjVdaBN_kEz_QQkUQixFaRYBjt9IW0QALzf8-c3JFXG3iio0mTB9PuxA1BVX6QVwnBP7bfc6RwHwxEbyyAN-3ApLjYz5j6dH1S6EF5Eq6dbMIL7xZHOuC6jy_h4i5L1DuEFI9kBrHhLJHE/s1600/1482940_668051136568579_1302657830_n.jpg
Joseph Omog
PAZIA la  Ligi Kuu Tanzania Bara msimu wa 2013-2014 lilifungwa mwishoni mwa wiki huku Azam ikiwa imeshatangaza ubingwa tangu wiki iliyopita kabla ya ligi hiyo haijafikia tamati.
Azam imetwaa taji hilo kwa mara ya kwanza baada ya kufikisha pointi 62 na kuingia kwenye rekodi ya kuwa klabu ya tisa nchini kunyakua  ubingwa nchini.
Baada ya ligi hiyo kumalizika, mashabiki wa soka wana hamu kubwa ya kutaka kujua nani atakayeibuka kuwa Mfungaji Bora, Mchezaji Bora na Kipa Bora wa ligi ya msimu huu.
Makocha Juma Mwambusi wa Mbeya City, Hans van der Pluijm wa Yanga na kocha wa Azam Joseph Omog walioziongoza timu zao kushika nafasi tatu za juu wanapewa nafasi kubwa kutwaa tuzo hiyo.
Katika msimu uliopita, kocha Abdallah Kibadeni aliyekuwa akiinoa Kagera Sugar aliibuka kidedea na kunyakua tuzo hiyo baada ya kuiwezesha Kagera Sugar kushika nafasi ya nne, ingawa msimu huu nafasi ya kuitetea inaonekana kuwa ndogo kwa hali ilivyo.
Kocha huyo aliyekuwa akiifundisha Simba, alitimuliwa na kuhamia Ashanti United ambayo ameshindwa kuikoa isirejee Ligi Daraja la Kwanza.
Mwambusi anapewa nafasi zaidi kwa kuipandisha daraja Mbeya City na kuifanya iwe tishio katika ligi licha ya ugeni wake na kumaliza katika nafasi ya tatu ikizidiwa na klabu za Azam na Yanga tu.
Omog aliyechukua nafasi ya Stewart Hall aliyetimuliwa na Azam baada ya kumalizika kwa duru la kwanza naye anapigiwa chapuo kama ilivyo kwa Pluijm wa Yanga aliyeinoa pia duru la pili tu.
Kabla ya hapo Yanga ilikuwa chini ya Mholanzi mwingine, Ernie Brandts aliyetimuliwa baada ya Yanga kufungwa kwenye mechi ya 'bonanza' ya Nani Mtaji Jembe.
Kwa upande wa Mchezaji Bora msimu uliopita alikuwa Kelvin Yondani na kipa akiwa Burhan aliyekuwa Prisons, je msimu huu tuzo hizo zitaenda wapi miongoni mwa wachezaji waliong'ara katika ligi hiyo?
Bila shaka mashabiki wana hamu kubwa ya kuona wachezaji wanaoamini walifanya vyema msimu huu wakinyakua tuzo hizo kama ilivyo kwa makocha na wachezaji chipukizi waliong'ara msimu huu.
Kwenye tuzo ya Mfungaji Bora nafasi ilikuwa ikionekana wazi ikielekea mikononi mwa Mrundi, Amissi Tambwe wa Simba aliyemaliza na mabao 19.
Je, Joseph Kimwaga atatetea tuzo yake ya Mchezaji Bora chipukizi katika msimu huu?Tusubiri tuone baada ya Bodi ya Ligi Tanzania pamoja na wadhamini wake kampuni ya Vodacom watakapoweka bayana orodha katika tuzo hizo kwa msimu wa 2013-2014.

Wanaoibeza Azam wana wivu-Himid Mao

Himid Mao
BAADHI ya nyota wa klabu ya Azam wamesema wanaowaponda kwa kufanikiwa kutwaa taji la Ligi Kuu Tanzania ni wasiokubali kushindwa na wenye dhana kuwa nje ya Simba na Yanga hakuna bingwa.
Azam iliweka rekodi ya kunyakua taji hilo baada ya misimu miwili mfululizo ikiishia kuambulia nafasi ya pili nyuma ya Simba na Yanga na kuwa klabu ya tisa kunyakua ubingwa huo tangu mwaka 1965.
Hata hivyo kabla na hata baada ya kunyakua taji hilo kumekuwa na kauli za kejeli dhidi ya mafanikio ya klabu hiyo, kitu kilichowakera baadhi ya nyota wa Azam waliodai wanaoponda wanawaonea gere.
Nahodha msaidizi wa klabu hiyo, Himid Mao, alisema mashabiki wa soka walipaswa kuipongeza Azam kwa kuonyesha ushindani wa kweli na kuweza kuzisimamisha Simba na Yanga na kuleta mapinduzi.
Mao, alisema Azam imechangia kuzika 'ligi ya klabu mbili' na kuonyesha kuwa kumbe hata timu nyingine zinaweza kuwa mabingwa kama zikijipanga, hivyo kupondwa kwao ni kuwakatisha tamaa.
"Nadhani wanaofanya hivyo wanasumbuliwa na wivu wa mafanikio yetu na pia kushindwa kuamini kuwa nje ya Simba na Yanga bingwa anaweza kupatikana tena kwa kuweka rekodi kama wao," alisema.
Alisema anaamini kuwepo kwa Mbeya City na kuongezeka kwa timu kama Ndanda Fc na Stand United kunaweza kuongeza chachu iliyoanzishwa na Azam ili kuifanya ligi iwe na utamu wa kusisimua.
"Ligi ya timu chache haivutii, ndiyo maana leo ligi ya England inavutia na kufuatiliwa kwa sababu haitabiriki kwa ushindani uliopo bila hadhi ya klabu, tumeonyesha uwezo tuungwe mkono tusikatishwe tamaa," alisema Mao mmoja wa 'nguzo' ya Azam tangu ipande daraja.

Abou Diaby arejesha tumaini Arsenal

http://www.images99.com/i99/02/36120/36120.jpg
Abou Diaby
BAADA ya kuwa nje ya dimba kwa karibu mwaka mzima, hatimaye Abou Diaby anatarajiwa kuanza kuonekana kwenye kikosi cha Arsenal.
Mchezaji huyo kutoka Ufaransa alikuwa nje ya dimba baada ya kuumia goti Machi mwaka 2013 wakati wa mechi baina yao na Swansea City.
Kwa mujibu wa Kocha wa Arsenal, Arsene Wenger, Diaby 27, amerejea na kungana na wachezaji wenzake kwenye mazoezi ya timu hiyo na huenda akamtumia katika mechi zilizosalia za ligi hiyo.
"Amerejea jumla kwenye mazoezi na sasa ataonekana uwanjani kuitumia timu," Wenger alinukuliwa na mtandao wa klabu hiyo na kuonyesha furaha yake.

Babi azidi kutisha Malaysia atupia mbili kuiokoa UiTM

Babi (kati mbele) ameziodi kudhihirisha ukali wake na kwamba UiTM hawakukosea kumpa unahodha
KIUNGO wa kimataifa wa Tanzania anayecheza soka la kulipwa nchini Malaysia, Abdi Kassim 'Babi' mwishoni mwa wili aliibeba na kuinusuru timu yake ya UiTM kupata kipigo kwa kutoka nyuma ya mabao 2-0 na kumaliza kwa sare ya 2-2 na Johor katika mfululizo wa Ligi Kuu ya Malaysia.
Babi alifunga mabao hayo katika dakika ya 70 na 89 na kuifanya timu yake kuambulia pointi moja ugenini iliyochezwa kwenye uwanja wa Pasir Gugand Corporation mjini Pasir Gudang.
Sare hiyo imekuja siku chache baada ya kuisaidia UiTM kupata ushindi wake wa kwanza wa 2-1 dhidi ya Kuala Lumpur SPA baada ya vipigo mfululizo katika ligi ya nchi hiyo.
Mabao hayo mawili yamemfanya Babi aliyeingia mkataba wa mwaka mmoja na klabu hiyo kufikisha jumla ya mabao matano tangu ajiunge na UiTM.
Babi ( wa pili kulia) akiwa na wachezaji wenzake wa UiTMya Malaysia

Mchezaji gabon afa kwa kikanyagwa kichwani

Sylvain Azougoui enzi za uhai wake
GOLIKIPA wa timu ya AC Bongoville, Sylvain Azougoui amefariki dunia baada ya kukanyagwa kichwani wakati wa mchezo wa ligi huko nchini Gabon. 
Golikipa huyo alifariki wakati akikimbizwa hospitali baada ya tukio hilo wakati wa mechi dhidi ya timu ya Centre Mberi Sportif. 
Azougoui mwenye umri wa miaka 30 raia wa Togo, alikuwa amezuia shuti lililokwenda langoni mwake lakini mshambuliaji aliyepiga shuti hilo alipoteza mwelekeo katika nyasi zilizokuwa zimelowa na kumkanyaga golikipa huyo kichwani. 
Klabu hiyo ilithibitisha habari za kifo cha golikipa huyo katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa facebook na kueleza masikitiko yake kwa pengo aliloacha klabuni na kwa familia yake.

Kuziona Stars, Burundi buku 5 tu

 https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEin6-ldauS1zEkRBorpFJr1e1uN1dZ2C8nAmp_zpxhzZG_7-7xspqqK7he1tkYg_WVJ9fVRMilD9viNnG2ZJomXBaCfg5IVA0aVoP8tvxmegczkBPC-ueY8F9mfDphYGy4tXpVqeZHckHlx/s1600/FKB_1765.JPG
KIINGILIO cha chini katika mechi ya kirafiki ya kimataifa kati ya timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) na Burundi (Intamba Mu Rugamba) itakayochezwa Aprili 26 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ni sh. 5,000.
Mechi hiyo itakuwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 50 ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar, na kiingilio hicho ni kwa viti vya rangi ya chungwa, bluu na kijani. Kwa wa VIP A kiingilio kitakuwa sh. 20,000 wakati VIP B na C ni sh. 10,000.
Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager tayari ipo kambini kwenye hoteli ya Kunduchi Beach kujiandaa kwa ajili ya mechi hiyo itakayochezeshwa na waamuzi kutoka nchini Kenya.
Burundi inatarajia kuwasili nchini keshokutwa (Aprili 22 mwaka huu) tayari kwa ajili ya mechi hiyo inayotajiwa kuwa ya kusisimua. Mechi hiyo imepangwa kuanza saa 10 jioni.
Wachezaji wa Taifa Stars waliopo kambini ni Deogratias Munishi, Mwadini Ali, Aidan Michael, Aggrey Morris, Erasto Nyoni, Hassan Mwasapili, Kelvin Yondani, Said Morad, Amri Kiemba, Frank Domayo, Himid Mao, Jonas Mkude, Athanas Mdamu, Haruna Chanongo, Juma Liuzio, Khamis Mcha, Mrisho Ngassa, Ramadhan Singano na Simon Msuva.
Wengine ni Benedicto Mlekwa, Emma Simwanda, Joram Mgeveje, Omari Kindamba, Edward Mayunga, Shiraz Sozigwa, Yusuf Mlipili, Said Ally, Abubakar Mohamed, Hashim Magona, Omari Nyenje, Chunga Zito, Mohammed Saidi, Ayoub Lipati, Abdurahman Ally na Paul Bundara.

Msiba! Mahabusu wa4 askari Magereza wafa ajalini

MAHABUSU wanne na Askari Magereza mmoja wamefariki dunia papo hapo katika ajali iliyotokea eneo la Mkenge, Mkuranga, Pwani.
Taarifa zilizopatikana hivi punde zinasema kuwa dereva wa gari lililokuwa limewabeba marehemu hao yupo hospitalini katika hali mbaya.
Taarifa zinasema kuwa marehemu hao na dereva walikuwa wakitokea Mkuranga kuja jijini Dar es Salaam na kukutwa na ajali hiyo inayopelezwa ni mbaya.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka eneo la tukio ni kwamba pick up ya Magereza ilipasuka tairi la kushoto na dereva wake kupoteza muelekeo na kugongana na lori lililokuwa likitokea Kimazichana na gari hilo lililokuwa na mahabusu hao na askari aliyekuwa akiwasindikiza lilipinduka na kusababisha vifo vyao.
Endelea kusoma MICHARAZO MITUPU kupata taarifa kamili, ingawa inaelezwa kuwa majeruhi wamehamishiwa Muhimbili kwa matibabu zaidi.
 

Newz Alert! Moyes hatimaye atimuliwa Man Utd, Giggs apewa shavu

Giggs (kushoto) akiwa na Moyes

Moyes kando ya Giggs, wawili hao wamebadilishana nafasi ya ukocha ndani ya klabu ya Manchester City
HATIMAYE klabu ya Manchester United imetangaza kumfuta kazi kocha wake, David Moyes na mkongwe Ryan Giggs amepewa 'shavu' la kuinoa timu hiyo kuelekea mwisho wa msimu.
Kwa mujibu wa taarifa ya mtandao wa klabu hiyo, Moyes amefutwa kazi baada ya miezi 10 na tayari ameshapewa barua ya kufutwa kazi ikiwa ni baada ya timu yake kupoteza mechi 11.
Nafasi ya kocha huyo imechukuliwa na mchezaji mkongwe wa klabu hiyo aliyedumu nayo kwa muda mrefu, Ryan Giggs wakati mipango ya kocha mpya ikifanywa, japo Louis van Gaal anatajwa kuja kubeba kibarua hicho baadaye.